Home » » NDANI YA TAKUKURU KUNA ‘MAJIPU’ –KAIRUKI.

NDANI YA TAKUKURU KUNA ‘MAJIPU’ –KAIRUKI.

Written By CCMdijitali on Monday, February 15, 2016 | February 15, 2016

 Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Kamishna Valentino Mlowola akizungumza na viongozi wa TAKUKURU katika mkutano wa kazi na viongozi hao uliofanyika makuu ya ofisi hiyo mapema leo. Kushoto ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Utumishi na Utawala Bora Mhe. Angella Kairuki (Mb) akimsikiliza kwa umakini.
 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Utumishi na Utawala Bora Mhe. Angella Kairuki (Mb) akifungua mkutano wa kazi wa viongozi wa TAKUKURU uliofanyika makuu ya ofisi hiyo mapema leo.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Utumishi na Utawala Bora Mhe. Angella Kairuki (Mb) akiwa katika picha ya pamoja na wakaguzi wa kanda wa TAKUKURU mara baada ya kufungua mkutano wa kazi wa viongozi wa TAKUKURU uliofanyika makuu ya ofisi hiyo mapema leo.

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii


WAZIRI wa Nchi, Ofisi Rais Utumishi na Utawala Bora, Angela Kairuki amesema kuwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) ina baadhi ya watendaji wametumia nafasi zao vibaya na kufanya chombo hicho kukosa uaminifu hivyo na kufanya chombo hicho kuwa na ‘majipu’ ambayo yanatakiwa kupasuliwa.

Angela ameyasema hayo leo wakati akifungua mkutano wa mwaka wa utendaji kazi wa Takukuru uliofanyika leo jijini Dar es Salaam, amesema chombo hicho ni muhimu lakini kuna baadhi wametumia nafasi zao vibaya katika kufanya kazi na taarifa anazo hivyo atashughulikia ikiwemo na kuandika kiapo cha mali zao na kama walifanya warudie kujiridhisha.

 Amesema kuwa Takukuru inatakiwa kufika wilayani na mikoani kutokana na fedha nyingi za miradi ya serikali zinakwenda huko ambapo ameutaja mkoa wa Kilimanjaro unawatendaji ambao wametumia madaraka vibaya wa ubadhirifu wa fedha za serikali hivyo Takukuru lazima ichukue hatua dhidi yao.

Amesema kuwa ikitokea kuwepo na kutowajibika kwa chombo hicho serikali iamweza kuwandoa wote kutokana na kuwepo kwa watu wenye sifa wa kufanya kazi hiyo.

Aliongeza kuwa katika Takukuru inatakiwa kujiridhisha na uchunguzi na sio kuwa idadi nyingi za kesi ambazo mwisho wa siku kesi hizo wanashindwa kutokana kuushindwa kuwa na uchunguzi wenye ushahidi.

Aidha amesema kuwa baadhi ya mahakimu watakosa kazi kutokana na baadhi ya kesi wameendesha kwa kupindisha na kuwapa washitakiwa haki wasio kuwa nayo.

Waziri Angela amesemaTakukuru wafanye kazi kwa waadilifu kwa kuwalinda watoa taarifa ili waendelee kutoa taarifa kwa watu wanaojua kuwa wanahujumu nchi kwa kutumia madaraka yao.

Amesema watumishi wa Takukuru wana masilahi mazuri kuliko wa wafanye kazi wengine ikiwa ni kuwaondoa katika ushawishi wa kuwa na tama kutokana unyeti wa chombo hicho.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Kamishina (CP), Valentino Mlowola amesema wameokoa sh. Bilioni Saba (7) ambazo zilikuwa ziingie kwenye mifuko ya wabadhirifu wachache ambao wanatumia nafasi zao vibaya kwa masilahi yao.

Amesema walipokea malalamiko 4,675, uchunguzi uliokamilika wa majalada hayo ni 667, majalada yaliyokwenda kwa Mkurugenzi wa Mashitaka Nchini (DPP), ni 278, majarada yaliyorejeshwa na DPP, ni 172 kwa ajili ya vibali vya kufungua mashitaka na kesi mpya 314 nchini kote, na kesi zilizoshinda 132 ambao wamefungwa na wengine kulipa faini.
Share this article :
 
Support : #BegaKwaBegaNaMamaSamia | JAK | CCM Arusha
Copyright © 2011. CCM Dijitali - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Jasper K
Proudly powered by Blogger
Link