NAIBU WAZIRI PINDA AELEKEZA UENDELEZAJI MIJI KUZINGATIA MIPANGO KABAMBE

Na Munir Shemweta, WANMM Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Geofrey Pinda amezielekeza Halmashauri zote nchini kuhakik...

Latest Post

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi atoa nasaha kwa Waandishi wa habari.

Written By CCMdijitali on Sunday, November 29, 2015 | November 29, 2015


Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akitoa ufafanuzi juu ya taarifa zilizotolewa na baadhi ya vyombo vya Habari kuhusu kurejewa kwa uchaguzi Mkuu wa Zanzibar.

Alichokirejena tena ni kwamba CCM imethibitisha kuwa iko tayari endapo uchaguzi huo utapangwa tena na si vyenginevyo.Picha na –OMPR – ZNZ.

 Press Release:-

Wanahabari wanapaswa kuwa makini zaidi katika utoaji wa Habari zao hasa kipindi hichi ambacho Zanzibar inaendelea kutafuta njia muwafaka ya hatma yake ya baadaye kufuatia Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar { ZEC } kufuta Uchaguzi Mkuu wa Mwezi Oktoba mwaka huu baada ya kubaini hitilafu kadhaa katika zoezi zima la uchaguzi.

Nasaha hizo zimetolewa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi hapo Ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar alipotoa ufafanuzi wa kina juu ya taarifa zilizotolewa na baadhi ya vyombo vya Habari vikieleza kuwa Viongozi wanaokutana kujadili suala hilo wamekubaliana kurudiwa kwa uchaguzi huo.

Alisema Kalamu za waandishi wa Habari kwa sasa ni vyema zikawaelekeza na kuwaongoza Wananchi kujihusisha na harakati zao za kimaisha badala ya kuwaendeleza katika wimbi la mizozano na mifarakano inayoweza kuamsha hamasa.

Balozi Seif akiongea na Redio ya Kiswahili ya Kimataifa ya Ufaransa { RFI } juzi alichokisema kuwaeleza wanahabari hao ni kwamba Chama cha Mapinduzi { CCM } pekee ndicho kilichotamka na kuthibitisha kuwa kiko tayari kurejea uchaguzi huo endapo utapangwa upya.

“ Nilichokieleza juzi ni kwamba CCM peeke ndio Tuliothibitisha na kukubali kurejea uchaguzi endepo utapangwa tena na hili tunaloendelea nalo la vikao na wenzetu bado tunajadiliana na maamuzi ya pamoja yatatolewa kwa Waandishi hapo baadaye “. Alisema Balozi Seif.

Alisema hadi sasa hakuna chombo chochote cha Habari ndani na nje ya Nchi kilichoitwa au kupewa Habari za mazungumzo yanayoendelea kati ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dr. Ali Mohammed Shein na Katibu Mkuu wa CUF ambae pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamadi kwa kuwashirikisha Marais wastaafu wa Zanzibar.

Balozi Seif alisema utaratibu maalum utaandaliwa wa kutolewa taarifa rasmi kwa vyombo vyote vya Habari ili ziwafikie Wananchi wote mara baada ya kukamilika kwa mazungumzo hayo na makubaliano yatakayofikiwa baina ya pande hizo mbili.

Aliwathibitishia Wananchi na wageni kwamba hali ya Zanzibar bado iko shwari na salama na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na ile ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia vyombo vyake vya Dola vitasiamia ipasavyo hali hiyo.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliwaomba Wananchi wabakie kuwa watulivu, wastahamilivu na kuendeleza Umoja na mshikamano utakaosaidia kulivua Taifa hili katika shari inayoweza kuepukwa.

Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zan

JOB NDUGAI NDIYE SPIKA MPYA WA BUNGE LA 11 LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

Written By CCMdijitali on Tuesday, November 17, 2015 | November 17, 2015


Hatimaye Job Yustino Ndugai CCM amechaguliwa kuwa Spika 
wa bunge la jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa 
kuchaguliwa kwa kura 254 sawa na asilimia 70% ya kura zilizopigwa akifuatiwa  na mgombea wa 
CHADEMA Goodluck Ole Medeye ambaye 
amepata kura 109.

Hata hivyo wagombea hao ambao walikuwa 7 kati ya 8 
wameweza kutoa shukrani na pongezi kwa Ndugai 
wakisema anastahili na ndio maana akachaguliwa na 
kumtaka aongoze vyema bunge hilo.

 Job Ndugai ameibuka mshindi wa kiti cha Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kupata kura 254 sawa na asilimia 70 ya kura zote ambapo jumla ya kura zilizopigwa ni 365

Matokeo ya kura za Spika.

A: Job Ndugai (CCM)- 254

B: Goodluck Ole Medeye (CHADEMA) - 109

C: Hashimu Rungwe (CHAUMA)- 0

D: Peter Sarungi (AFP) -0

E: Dkt Godfrey Malisa (CCK)- 0

F: Richard Lymo (T.L.P) -0

G: Robert Kisinini (DP) -0

Kura zilizoharibika ni 2

Magufuli afuta safari zote nje

Written By CCMdijitali on Sunday, November 8, 2015 | November 08, 2015

Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akizungumza na Makatibu Wakuu, Manaibu Katibu Wakuu, Watendaji Wakuu serikalini leo Ikulu jijini Dar es salaam kupanga mikakati ya kuendesha serikali kwa weledi, nidhamu na moyo wa kupenda kazi.

 Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli katika picha ya pamoja Makatibu Wakuu, Manaibu Katibu Wakuu, Watendaji Wakuu serikalini leo Ikulu jijini Dar es salaam baada ya kukutana nao na kupanga mikakati ya kuendesha serikali kwa weledi, nidhamu na moyo wa kupenda kazi.
PICHA NA IKULU

WATENDAJI wote wa Serikali, wamepigwa marufuku kufanya safari za nje ya nchi na badala yake majukumu yanayowapeleka katika nchi hizo, wametakiwa wayakabidhi kwa mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania katika nchi husika.

Rais John Magufuli ametoa agizo hilo jana katika siku yake ya tatu Ikulu, alipokutana na makatibu wakuu, naibu makatibu wakuu, Gavana wa Benki Kuu (BoT), Profesa Benno Ndulu na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Rished Bade.

“Nataka Serikali iendelee kwa nguvu zote na katika kutekeleza dhana ya ‘Hapa Kazi Tu’ na viongozi wazingatie na kukumbuka ahadi nilizotoa, ili zianze kuonekana na kufanyiwa kazi mara moja,” amesema Rais Magufuli katika taarifa iliyotumwa na Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu.

Katika kusisitiza katazo hilo la ziara za nje ya nchi, Rais Magufuli amesema pakitokea jambo la dharura sana, pamoja na udharura wake kabla ya mtendaji yeyote kwenda nje ya nchi, atalazimika kupata kibali kutoka kwa Rais au Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue.

*Vijijini, shule bure

Badala ya kufanya ziara katika nchi ambako Tanzania ina mabalozi, Rais amewataka watendaji hao kufanya zaidi ziara za kwenda vijijini ili kuzijua na kutatua kero za wananchi wa Tanzania.

Katika hilo, amesisitiza kwamba kuanzia Januari mwaka 2016, wanafunzi wote wanaoanza shule watasoma bure bila kulipa ada, ambapo Rais amewataka watendaji kuliwekea mikakati agizo hilo tayari kwa utekelezaji.

Agizo hilo ni utekelezaji wa ahadi aliyotoa wakati wa kampeni za uchaguzi zilizoisha Oktoba 24 mwaka huu, kwamba kuanzia mwakani wanafunzi wote wanaosoma shule za Serikali kuanzia darasa la awali mpaka kidato cha nne, watasoma bure.

Kuhusu elimu ya juu, Rais Magufuli katika kikao hicho, ameagiza suala la mikopo ya wanafunzi lifanyiwe kazi na mipango yake ikamilike kwa ajili ya utekelezaji mzuri zaidi. Rais ameelekeza watendaji hao wasimamie maagizo hayo, yawekewe mikakati na kuyapanga vizuri, ili atakapoteua Baraza la Mawaziri, watakaoteuliwa wakayasimamie bila kukosa.

*Mapato

Kuhusu ukusanyaji mapato, Rais Magufuli alitoa maagizo mahususi, alipomtaka Kamishna wa TRA, Bade kusimamia kwa makini ukusanyaji wa mapato nchini na kuhakikisha kero ndogo ndogo kwa wananchi, zinaanza kutatuliwa kama alivyoahidi.

Rais ameitaka TRA kukusanya mapato hayo kutoka kwa wafanyabiashara wakubwa zaidi na wale wanaokwepa kodi bila kuogopa mtu wala taasisi yoyote hapa Tanzania.

Katika kuweka msisitizo, Rais Magufuli alisema katika Serikali hii wa kutoa uamuzi vinginevyo zaidi ya huo, ni yeye Rais ama Makamu wake, Samia Suluhu Hassan.

*Ahadi zingine

Ahadi zingine zilizotolewa na Rais Magufuli wakati wa kampeni zake ambazo ametaka watendaji hao kuzizingatia ni pamoja na kushusha bei ya vifaa vya ujenzi hasa saruji, mabati na misumari, ili wananchi waweze kujenga nyumba bora.

Katika kuongeza idadi ya Watanzania wanaofanya kazi, alisema katika kila mtaa na kijiji, Serikali yake itatoa Sh milioni 50 kwa ajili ya kuanzisha na kukuza biashara ndogo za wanawake na vijana.

Alisema atataka kila anayefanya kazi apate kipato kizuri kitakachomsaidia kukabiliana na mahitaji ya maisha yake, ikiwemo kujenga nyumba bora kutokana na kushushwa kwa bei za bidhaa za ujenzi.

Mbali na kutoa mikopo hiyo izunguke katika ngazi ya kijiji na mtaa, Dk Magufuli pia aliahidi kwamba Serikali yake itazuia kila aina ya usumbufu unaofanywa kwa wafanyabiashara hao, ikiwemo kukamatwa kwa bodaboda na mama ntilie.

Kwa wakulima, alisema atahakikisha pembejeo sahihi zinatolewa kwa wakati na mazao yatakayovunwa, itakuwa marufuku kwa Serikali kukopa mazao yao. Aidha aliahidi kuondoa ushuru unaosumbua wafanyabiashara wadogo na hasa wakulima, ili wafanye biashara kwa uhuru wajipatie kipato halali.

Rais Magufuli pia alisema baada ya kusambaza umeme, atahakikisha viwanda vidogo na vya kati vinajengwa vijijini kusindika mazao ya kilimo, ili kutoka shambani bidhaa za viwandani zikauzwe kwenye masoko ya ndani na nje ya nchi.

Kuhusu migogoro ya ardhi kati ya wakulima na wafugaji, Rais Magufuli alisema atatoa ardhi zaidi kwa ajili ya wakulima na wafugaji, ili kuondoa uhaba wa ardhi uliosababisha ugomvi wa maeneo ya kulishia mifugo na kulima.

Lakini pia aliahidi kunyang’anya mashamba ambayo yamehodhiwa na watu bila kutumiwa kwa ufugaji wala kilimo, na kuyagawa kwa wakulima na wafugaji wasio na maeneo ya kilimo wala eneo la kufugia.

Katika sekta ya afya, mbali na kuahidi kuendelea kujenga zahanati kwa kila kijiji na mtaa, kituo cha afya kwa kila kata na hospitali ya rufaa katika kila mkoa, aliahidi kukomesha kero ya kukosekana dawa katika hospitali za Serikali.

Katika kero ya maji, alisema kama amefanikiwa kujenga zaidi ya kilometa 17,000 za barabara, hatashindwa kuchimba mabwawa na kujenga mtandao wa mabomba kwenda kwa wananchi.

Maagizo hayo ya Rais Magufuli yamekuja siku ya tatu tu ya kuingia Ikulu, ambapo siku ya kwanza Alhamisi iliyopita, alianza kwa kumteua Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju na siku ya pili, juzi alimuapisha na kufanya ziara ya ghafla katika ofisi za Wizara ya Fedha, Hazina, akakagua ofisi za watumishi wa ngazi za chini.

Baada ya kukagua ofisi hizo, ambako alikuta baadhi ya watendaji wamefika ofisini na kuondoka, alifanya mazungumzo na watendaji wakuu wa wizara hiyo na kusisitiza umuhimu wa kukusanya kodi.

Na Habari Leo.

CCM ilivyoongoza katika Majimbo ya Uchaguzi

Written By CCMdijitali on Wednesday, November 4, 2015 | November 04, 2015

  • CCM  majimbo - 159, 

  • Chadema majimbo - 35,

  • Chama cha Wananchi (CUF)  majimbo 17 ,

  • ACT-Maendeleo - 1 ,

  • Chama cha NCCR-Mageuzi - 1.



CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimeongoza kwa kunyakua majimbo ya uchaguzi 159, ambayo hadi jana yamethibitishwa na wasimamizi waliopewa mamlaka ya kutangaza matokeo hayo na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), huku Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kikifuatia kwa kupata majimbo 35.

Aidha, wanawake wengi wameonekana kufanya vizuri katika uchaguzi wa ubunge na hadi sasa waliotajwa na kuthibitishwa kushinda katika majimbo waliyogombea wamefikia wanawake 19 na idadi hiyo inaweza kuongezeka.

Hata hivyo, hayo si majimbo yote ambayo vyama hivyo vimefanikiwa kushinda, kutokana na baadhi ya majimbo bado matokeo yaliyoonesha utata, yanaendelea kuhesabiwa na kutangazwa pale inapoonekana inafaa.

Aidha, katika uchaguzi huo, Chama cha Wananchi (CUF) nacho kimefanikiwa kupata majimbo 17 huku Chama cha NCCR-Mageuzi na ACT-Maendeleo vyote vikipata jimbo moja moja. Jumla ya majimbo yote ya uchaguzi ni 264 na yaliyokwishatangazwa hadi sasa ni majimbo 207.

Katika upembuzi wa majimbo hayo uliofanywa na gazeti hili, baada ya kuthibitishwa, CCM imepata majimbo ya Busega (Raphael Chegeni), Nyamagana (Stanslaus Mabula), Msalala (Ezekiel Maige), Ngara (Alex Gashaza), Kigamboni (Faustine Ndugulile), Kishapu (Suleiman Nchambi) na Kisarawe (Suleiman Jaffo).

Majimbo mengine ni Bagamoyo (Dk Shukuru Kawamba), Ilemela (Angelina Mabula), Ilala (Mussa Azzan ‘Zungu’), Singida Mjini (Mussa Sima), Same Magharibi (Dk Mathayo David Mathayo), Rungwe (Saul Amon), Mbogwe (Augustino Masele), Chalinze (Ridhiwani Kikwete), Iramba Magharibi (Mwigulu Nchemba) na Hanang (Dk Mary Nagu).

Aidha, majimbo mengine ni Njombe Kaskazini (Joram Hongoli), Dodoma Mjini (Antony Mavunde), Mtama (Nape Nnauye), Babati Vijijini (Jitu Soni), Kahama Mjini (Jumanne Kishimba), Sikonge (George Kakunda), Nzega Mjini (Hussein Bashe), Urambo (Margaret Sitta), Mpanda Vijijini (Moshi Kakoso) na Geita Mjini (Constantine Kanyasu).

Chama hicho pia kilijipatia ushindi katika majimbo ya Mbeya Vijijini (Oran Njeza), Mafinga Mjini (Cosato Chumi), Kalenga (Godfrey Mgimwa), Isimani (William Lukuvi), Songea Mjini (Leonidas Gama), Mkalama (Allan Kiula), Newala (George Mkuchika), Kavuu (Dk Prudenciana Kikwembe) na Kwimba (Mansoor Shanif).

Mengine ni Bukoba Vijijini (Jason Rweikiza), Nyasa (Stella Manyanya), Kondoa Mjini (Edwin Sanda), Kondoa Vijijini (Dk Kashatu Kijaji), Chemba (Juma Nkamia), Chamwino (Joel Mwaka), Mtera (Livingstone Lusinde), Bahi (Omar Baduel), Mpwapwa (George Lubeleje), Kibakwe (George Simbachawene) na Kongwa (Job Ndugai).

CCM pia imepata Sengerema (William Ngeleja), Maswa Mashariki (Stanslaus Nyongo), Maswa Magharibi (Mshimba Ndaki), Itilima (Njalu Silanga), Bariadi (Andrew Chenge), Meatu (Salum Hamis), Muheza (Balozi Adadi Rajabu), Kasulu Mjini (Daniel Nsanzugwanko), Buhigwe (Albert Ntabaliba), Handeni Vijijini (Mboni Mhita) na Morogoro Mjini (Abdulaziz Abood).

Gairo (Ahmed Shabiby), Rorya (Lameck Airo), Ngorongoro (William Ole Nasha), Mvomero (Suleiman Murad), Morogoro Kusini Mashariki (Mgumba Omary), Morogoro Kusini (Prosper Mbena), Nkasi Kusini (Deuderius Mipata), Nkasi Kaskazini (Ally Keissy), Singida Kaskazini (Lazaro Nyalandu), Singida Magharibi (Elibariki Kingu) na Igunga (Dk Dalaly Kafumu).

Mengine yaliyoenda CCM ni Solwa (Ahmed Salum), Katavi (Issac Kamwele), Mpanda Mjini (Sebastian Kapufi), Mpanda Vijijini (Moshi Kakoso), Nsimbo (Richard Mbogo), Ruangwa (Kassim Majaliwa), Sumbawanga Mjini (Aeshi Hilaly), Kyela (Dk Harrison Mwakyembe), Ileje (Janeth Mbene) na Mbarali (Pirmohamed Mulla).

Majimbo mengine yaliyochukuliwa na chama hicho ni Busokelo (Atupele Mwakibete), Vwawa (Japhet Hasunga), Lupa (Victor Mwambalaswa), Songwe (Philipo Mulugo), Madaba (Joseph Mhagama), Peramiho (Jenista Mhagama), Kilosa Kati (Mohamed Bawazir), Kiteto (Emanuel Papian), Mbulu (Paul Isaay) na Karagwe (Innocent Bashungwa).

Kyerwa (Innocent Bilakwate), Nkenge (Dk Diodorus Kamala), Muleba Kusini (Profesa Anna Tibaijuka), Muleba Kaskazini (Charles Mwijage), Biharamulo Magharibi (Mukasa Oscar), Mwibara (Kangi Lugola), Bunda Vijijini (Boniphace Getere), Makete (Dk Norman Sigala), Kibaha Vijijini (Hamoud Jumaa) na Sumve (Richard Ndassa).

Magu (Kiswaga Destery), Chato (Dk Merdad Kalemani), Nzega Vijijini (Dk Khamis Kigwangallah), Njombe Mjini (Edward Mwalongo), Mwanga (Profesa Jumanne Maghembe), Nyangh’wale (Hussein Kassu), Newala Vijijini (Rashid Akbal), Butiama (Nimrod Mkono), Korogwe Vijijini (Stephen Ngonyani) na Korogwe Mjini (Mary Chatanda).

Misungwi (Charles Kitwanga), Busanda (Lolensia Bukwimba), Manonga (Seif Gulamali), Tabora Mjini (Emmanuel Mwakasaka), Mlalo (Rashid Shangazi), Kisesa (Luhaga Mpina), Lindi Mjini (Selemani Kaunje), Mkinga (Dustan Kitandula), Mbinga Mjini (Sixtus Mapunda), Mbinga Vijijini (Martin Msuha) na Musoma Mjini (Vedastus Mathayo).

Mengine ni Geita Vijijini (Joseph Kasheku), Kibaha Mjini (Silvestry Koka), Bukombe (Dotto Biteko), Shinyanga Mjini (Steven Masele), Msalala (Ezekiel Maige), Pangani (Jumaa Aweso), Mufindi Kaskazini (Mahamoud Mgimwa), Mufindi Kusini (Mendrad Kigola), Kilolo (Venance Mwamoto) na Maswa Mashariki (Stanslaus Nyongo).

Maswa Magharibi (Mashimba Ndaki), Chilonwa (Joel Mwaka), Mtwara Vijijini (Hawa Ghasia), Nanyamba (Abdallah Chikota), Tunduru Kusini (Daimu Mpakate), Tunduru Kaskazini (Ramo Makani), Bunda Vijijini (Boniface Mgetere), Mkuranga (Abdallah Ulega) na Mbulu Vijijini (Gregory Massay) nayo yameenda CCM.

Mengine ni Mbulu Mjini (Zacharia Paul), Kilindi (Kigua Mohamed), Namtumbo (Edwin Ngonyani), Ushetu (Elias Kuandikwa), Bumbuli (January Makamba), Segerea (Bonnah Kaluwa), Kalambo (Josephat Kandege), Wanging’ombe (Gerson Lwenge), Kigoma Kaskazini (Peter Serukamba), Muhambwe (Justus Nditiye), Kasulu Vijijini (Agustie Vuma) na Kilolo (Venance Mwamoto).

Kwa upande wa Chadema, hadi sasa kimejinyakulia majimbo 35 ambayo ni Kibamba (John Mnyika), Mikumi (Joseph Haule), Bukoba Mjini (Wilfred Lwakatare), Same Mashariki (Nagenjwa Kayoboka), Rombo (Joseph Selasini), Bunda Mjini (Ester Bulaya), Hai (Freeman Mbowe) na Mbeya Mjini (Joseph Mbilinyi).

Majimbo mengine ni Kawe (Halima James Mdee), Longido (Onesmo Nangole), Ukonga (Waitara Mwita), Mlimba (Suzan Kiwanga), Singida Mashariki (Tundu Lissu), Ubungo (Said Kubenea), Mbozi (Paschal Haonga), Tunduma (Frank Mwakajoka), Momba (David Silinde), Kilombero (Peter Lijualikali) na Karatu (Willy Qambalo).

Aidha, chama hicho kilishinda katika majimbo ya Simanjiro (James ole Millya), Arumeru Magharibi (Gipson ole Meseyeki), Tarime Mjini (Ester Matiko), Siha (Godwin Mollel), Buyungu (Kasuku Bilago), Monduli (Julius Kalanga), Arumeru Mashariki (Joshua Nassari), Serengeti (Marwa Ryoba) na Babati Mjini (Pauline Gekul).

Mengine ni Moshi Mjini (Jaffar Michael), Tarime Vijijini (John Heche), Iringa Mjini (Peter Msigwa), Ndanda (Cecil Mwambe) na Moshi Vijijini (Anthony Komu). CUF yenyewe hadi sasa kina majimbo 17 ambayo ni Temeke (Abdallah Mtolea), Mchinga (Hamidu Bobali), Kilwa Kusini (Said Bungala), Kaliua (Magdalena Sakaya), Tandahimba (Ahmad Katani), Mtwara Mjini (Maftaha Nachuma), Kinondoni (Maulid Mtulia), Kilwa Kaskazini (Vedasto Ngombale) na Tanga Mjini (Musa Mbaruk).

Majimbo mengine ni Wawi, Chakechake, Ole, Ziwani, Kojani, Gando, Wete na Mgogono. Wanawake waliong’ara hadi sasa majimboni ni Kaliua (Magdalena Sakaya), Babati Mjini (Pauline Gekul), Hanang (Mary Nagu), Urambo (Margaret Sitta), Kavuu (Dk Prudenciana Kikwembe), Nyasa (Stella Manyanya), Handeni Vijijini (Mboni Mhita), Ileje (Janeth Mbene), Peramiho (Jenista Mhagama) na Muleba Kusini (Profesa Anna Tibaijuka).

Wengine ni Busanda (Lolensia Bukwimba), Mtwara Vijijini (Hawa Ghasia), Segerea (Bonnah Kaluwa), Same Mashariki (Nagenjwa Kayoboka), Bunda Mjini (Ester Bulaya), Kawe (Halima James Mdee), Mlimba (Suzan Kiwanga), Tarime Mjini (Ester Matiko) na Kaliua (Magdalena Sakaya).

Balozi Seif Ali Iddi wakati azungumza na Viongozi wa Dini mbali mbali - Zanzibar

Written By CCMdijitali on Tuesday, November 3, 2015 | November 03, 2015


 
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akiwa katika picha ya pamoja na Vongozi wa Dini mbali mbali Nchi mara baada ya kufanya mazungumzo nao
 Ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar.

Kushoto ya Balozi Seif ni Kiongozi wa Timu ya Waislamu Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Kabi na Kulia ya Balozi ni Kiongozi wa Wakristo Askofu Augustino Mweleli Shao.
Picha na – OMPR – ZNZ
.

 Press Release:-

 Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inakamilisha taratibu zilizobakia na tayari inajiandaa kuwachukulia hatua za Kisheria watu wote waliohusika kuharibu kwa makusudi zoezi zima la Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar uliofanyika Tarehe 25 Mwezi Oktoba mwaka huu.

Kauli hiyo imetolewa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi wakati akizungumza na Viongozi wa Dini mbali mbali Nchini aliokutana nao Ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar kutafakari na kutafuta mbinu za kuendelea kujaribu kudumisha amani ya Nchi iliyotetereka na kuleta mtafaruku katika kipindi hicho cha Uchaguzi.

Balozi Seif alisema ina uthibitisho kamili wa vielelezo vya ushahidi wa udanganyifu kwa maeneo yote ya Zanzibar hasa katika Majimbo ya Uchaguzi ya Kisiwa cha Pemba.

Alisema Afisa wa Tume ya Uchaguzi au Mtu yoyote aliyehusika na udanganyifu huo aelewe kwamba mkondo wa sheria utamkumba kwa vile vitendo walivyofanya wameisababishia hasara kubwa Serikali pamoja wa washirika wa maendeleo walioamua kusaidia uchaguzi huo.

Balozi Seif alibainisha kwamba wakati wahusika hao wanapandishwa katika vyombo vya kisheria kujibu shutuma zinazowakabili Serikali kwa upande wake itaweka hadharani uthibitisho kamili wa vielelezo vya ushahidi wa udanganyifu huo ili Wananchi wapate fursa ya kuelewa dhambi hiyo mbaya waliyofanyiwa na watu wachache kwa tamaa binafsi.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliwahakikishia Viongozi hao wa Dini kwamba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imejipanga vizuri kupitia vyombo vyake vya ulinzi kwa kupiga Doria maeneo yote katika kuona amani ya nchi inaendelea kudumu.

Aliwapongeza Viongozi hao wa Dini kwa jitihada zao wanazochukuwa za kutumia busara zao kwa kukutana na Viongozi wa pande mbali mbali za Kisiasa wakilenga kusaidia kutuliza mumkari na machungu ya waumini wao ambao takriban wote ni wafuasi wa vyama vya Kisiasa vilivyopo hapa Nchini.

Alivilaumu baadhi ya vyombo vya Habari hasa vile vya Nchi za Magharibi jinsi vilivyoonyesha wazi Taarifa zao nyingi wanazotowa za zoezi zima la uchaguzi Mkuu wa Zanzibar zikionyesha kuegemea upande mmoja tu.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alielezea masikitiko yake juu ya wangalizi wa Kimataifa walioamua kufuatilia uchaguzi Mkuu wa Zanzibar kwamba hawakwenda Kisiwani Pemba muda wote wa zoezi la kupiga kura kufuatilia changamoto zilizojitokeza katika majimbo ya Pemba.

" Nimesikitishwa na waangalizi wa Kimataifa waliokuwepo Zanzibar kwa karibu mwezi mmoja kufuatilia kampeni na uchaguzi wake wameshindwa kwenda Pemba wakati wa zoezi la kupiga kura na kuonekana zaidi katika majimbo ya Kisiwa cha Unguja.

Balozi Seif aliishauri Idara ya Habari Maelezo kuendelea kufuatilia Taarifa zinazotolewa na vyombo mbali mbali vya Habari ndani na nje ya Nchini na kukemea au kutoa Taarifa dhidi ya uchochezi unaotolewa na vyombo hivyo.

Nao Viongozi hao wa Dini mbali mbali Nchini wameishukuru na kuipongeza Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na ile ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa hatua iliyochukuwa katika kusimamia amani ya Nchi.

Wananchi wa Zanzibar wamerejea katika harakati zao za kawaida za kimaisha baada ya kutokea hitilafu tofauti ndani ya zoezi zima la upigaji kura kwenye uchaguzi Mkuu wa Tarehe 25 Mwezi uliopita na kupelekea kuibuka kwa mtafaruku uliotikisa amani ya Taifa.


Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
3/11/2015.

Balozi Seif Ali Iddi atoa taarifa ya Serikali kuhusu upotoshaji wa baadhi ya vifungu vya sheria

Written By CCMdijitali on Sunday, November 1, 2015 | November 01, 2015



Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akitoa taarifa rasmi ya Serikali kuhusu upotoshaji wa baadhi ya vifungu vya sheria unaendelea kufanywa na baadhi ya viongozi wa Kisiasa juu ya uhalali wa kuendelea kuwepo madarakani Rais wa Zanzibar.

Taarifa hiyo aliitoa katika kituo cha matangazo ya Shirika la Habari Zanzibar {ZBC-TV } Karume House Mnazi Mmoja Mjini Zanzibar.
Picha na – OMPR – ZNZ.

 Press Release:-

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imewahakikishia Wananchi wa Zanzibar na Tanzania kwa ujumla kwamba Rais aliyepo madarakani hivi sasa ataendelea kushika madaraka ya Urais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi mpaka pale utaratibu wa Kikatiba na Kisheria wa kumpata Rais utakapokamilika.

Kauli hiyo imetolewa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi wakati akitoa Taarifa ya Serikali akisisitiza Taarifa ya awali ya Serikali iliyotolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar kuhusiana na kauli za kupotosha zinazotolewa na baadhi ya Viongozi wa vyama vya Kisiasa kuhusu uhalali wa kuendelea kuwepo kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi aliyopo madarakani pamoja na Serikali yake.

Balozi Seif aliwaomba Wananchi wazipuuze kauli za upotoshaji zinazotolewa zikiashira zaidi uvunjifu wa amani na kuwataka waendee kuwa watulivu na kudumisha amani iliyopo Nchini.

Alisema Kifungu cha 28 Mbili {a} cha Katiba ambacho kimekuwa kikitumika katika kutoa tafrisi potofu kwa Wananchi kwamba Rais aliyopo madarakani atamaliza muda wake wa miaka mitano kuanzia Tarehe ambayo alipokula kiapo cha uaminifu na kiapo cha kuwa Rais.

Balozi Seif alieleza kwamba ni dhahiri kwamba dhamira ya kifungu hicho cha Katiba ilikuwa kuweka bayana kuwa kama uchaguzi Mkuu utafanyika na msindi wa kiti chja Urais atatangazwa rasmi na Tumen ys Uchaguzi, hivyo muda wake wa kuendelea Mtu kuwa Rais ungemalizika kwa kufuatana na masharti ya Kifungu hicho.

Alifafanua kwa kuwa Tume ya Uchaguzi haikumtangaza mshindi wa kiti cha nafasi ya Urais ni dhahiri masharti ya kifungu hicho hayataweza kusimama na hivyo masharti ya Kifungu cha 28 {1} {a} cha Katiba kitakuwa na nguvu za Kikatiba kumpa uwezo wa Rais aliyopo madarakani kuendelea na madaraka ya Urais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi.

Alisema Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi anapatikana kwa mujibu wa masharti ya Kifungu cha 27 cha Katiba ambacho Rais anachaguliwa kufuatana na Katiba Hiyo na kwa mujibu wa Sheria yoyote itakayotungwa na Baraza la Wawakilishi hukusu Uchaguzi wa Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi.

Balozi Seif alifahamisha kuwa ili Rais wa Zanzibar apatikane kwa mujibu wa Katiba na sheria ya Uchaguzi nambari 11 ya Mwaka 1984, Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar inapaswa kuendesha uchaguzi na hatimae kumtangaza mshindi wa nafasi ya Urais ambae atashika madaraka hayo pale ambapo atakuwa ameapishwa rasmi kwa mujibu wa kifungu cha 31 cha Katiba ya Zanzibar.

Alisema Kifungu cha 28 {1} {a} cha Katiba kinaweka utaratibu kuhusu muda wa kuendelea kuwa kuwa Rais, na kwamba kwa kufuatana na kifungu hicho, mtu aliyechaguliwa kuwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi ataendelea na dhamana hiyo mpaka pale ambapo Rais anayefuata ale kiapo cha kuwa Rais.

Alieleza kwamba kwa msingi huo wa Kikatiba ni vyema Wananchi wakafahamu na kuelewa kuwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Braza la Mapinduzi ataendelea kuwepo madarakani mkapa pale Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar itakapomtangaza mshindi wa kiti cha Urais na Rais Mteule atashika madaraka hayo baada ya kuapishwa rasmi kwa mujibu wa kifungu cha 31 cha Katiba.

Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
1/11/2015.
 
Support : #BegaKwaBegaNaMamaSamia | JAK | CCM Arusha
Copyright © 2011. CCM Dijitali - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Jasper K
Proudly powered by Blogger
Link