NAIBU WAZIRI PINDA AELEKEZA UENDELEZAJI MIJI KUZINGATIA MIPANGO KABAMBE

Na Munir Shemweta, WANMM Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Geofrey Pinda amezielekeza Halmashauri zote nchini kuhakik...

Latest Post

MJUMBE WA NEC JUMAA NA MBUNGE WA KISARAWE JAFO WAZIPAMBA KAMPENI ZA UDIWANI KATA YA KURUI KISARAWE

Written By CCMdijitali on Wednesday, January 10, 2018 | January 10, 2018

 Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM(NEC) Taifa Hajji Abuu Jumaa akipokea mwanachama mpya kutoka upinzani kwenye kampeni za uchaguzi kata ya Kurui.

 Mbunge wa Kisarawe Selemani Jafo akimnadi mgombea udiwani kata ya Kurui Mussa Kunikuni

 Viongozi wa CCM mkoani Pwani wakimuombea kura mgombea udiwani kata ya Kurui Mussa Kunikuni

 Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Kisarawe Khalfan Sika akimuonesha jambo Mbunge wa Kisarawe Selemani Jafo


Wanachama wa CCM wakiserebuka kwenye kampeni za udiwani kata ya Kurui
...................................................................................................................................................................

Zikiwa zimesalia siku chache kabla uchaguzi mdogo wa Ubunge na Udiwani kufanyika kwenye maeneo mbalimbali nchini Januari 13, mwaka huu, Mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa (NEC) kutoka mkoa wa Pwani Hajji Abuu Jumaa ameongoza kampeni za Udiwani wa kata ya Kurui wilayani Kisarawe na kumnadi mgombea udiwani kupitia CCM Mussa Kunikuni.

Katika kampeni hizo, Jumaa amemwagia sifa za uzalendo na uchapakazi mgombea huyo na kuwaomba wananchi wa kata ya Kurui kutofanya makosa siku ya uchaguzi huo mdogo januari 13, 2018.

Akizungumza katika kampeni hizo zilizofanyika kijiji cha Zegero, Jumaa amewaeleza wananchi kuwa "Kisarawe mmepata bahati kwa kuwa na mbunge wa Jimbo mchapakazi na mzalendo sana kwa taifa letu ndugu yetu Selemani Jafo ambaye pia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tamisemi. 

"Mnapaswa kumchagulia Diwani mzuri wa kushirikiana naye katika kata hii ili Ilani ya CCM iweze kutekelezwa vyema. Diwani huyo si mwingine bali Mussa Kunikuni"

Kwa upande wake, Jafo amewaomba wananchi wa kata ya Kurui kumchagua ndugu Mussa Kunikuni ili aweze kushirikiana naye katika kuwaletea wananchi maendeleo.

Jafo ametumia nafasi hiyo kuwaeleza wananchi mafanikio yaliyopatikana na yanayoendeleo kupatikana kupitia sekta ya Afya, Elimu, Barabara, Umeme, maji na mambo mbalimbali ya kijamii. 

Kadhalika, Katibu wa CCM mkoa wa Pwani amewatahadharisha wananchi kutokukubali kukurubuniwa na kauli za wanasiasa wa upinzani kwani hawana jipya isipokuwa wanatafuta maneno ya kuwalaghai wananchi ili wawapigie kura.

Kampeni hizo zinaendelea katika vijiji mbalimbali na zinatarajiwa kuhitimishwa Januari 12 mwaka huu katika kijiji cha Kidugalo kata ya Kurui wilayani Kisarawe.

JAFO ATAKA UJENZI WA RUVU SEKONDARI UWE WA HARAKA NA WA VIWANGO

Written By CCMdijitali on Tuesday, January 9, 2018 | January 09, 2018

 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selamani Jafo akikagua mambweni ya Shule ya Sekondari ya Ruvu wakati alipotembelea shule hiyo.

 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selamani Jafo akizungumza na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Ruvu wakati alipotembelea shule hiyo.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selamani Jafo katika picha ya pamoja na walimu wa Shule ya Sekondari ya Ruvu wakati alipotembelea shule hiyo.                      ......................................................................................................
Nteghenjwa Hosseah,Kibaha.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Selemani Jafo amemtaka atakayepewa jukumu la ukarabati wa Sekondari ya Ruvu wafanye kazi kwa kasi na haraka ili kuboresha mazingira ya shule hiyo.

Jafo aliyasema hayo leo asubuhi katika shule ya sekondari Ruvu iliyopo mkoani pwani ambapo ni siku ya pili tokea shule zianze kufunguliwa kwa mwaka huu 2018. 


Ikumbukwe kwamba Waziri Jafo alitumia siku ya kwanza ya tarehe 08 January ya kufunguliwa shule hapa nchini kwa kuongea na wanafunzi wa mkoa wa mbeya kupitia shule ya sekondari Ilomba iliyopo jiji la Mbeya.


Jafo amesisitiza kwamba Serikali imeamua kufanya ukarabati wa Shule zote kongwe hapa nchini kupitia TEA ili kutengeneza mazingira bora ya kujifunzia na kufundishia. 


Amesisitiza kwamba Serikali inayo ongozwa na Rais Dkt. John Magufuli imedhamiria kuleta mapinduzi makubwa katika elimu hapa nchini.


Jafo amewaeleza wanafunzi na walimu wa Ruvu sekondari kwamba wakati wa zoezi la ukarabati atatumia muda mwingi kukagua ujenzi wa shule hiyo akiwa pamoja na mbunge wa Jimbo hilo Mhe. Hamood Abuu Jumaa ili thamani ya fedha ipatikane. 


Wanafunzi wa Ruvu sekondari walionyesha furaha kubwa kwa mipango ya Serikali juu ya shule yao kwani uchakavu wa miundombinu umekuwa ukiwaletea shida kubwa kutokana na maeneo mengi ya majengo yao kuvuja wakati wa Mvua.


Pia walimu na wanafunzi wa Shle hiyo wameahidi matokea mazuri zaidi katika mitihani inayokuja kwa kuzingatia mangira bora ya kujifunzia na kujisomea watakayokuwa wameyapata baada ya Ukarabati huo.


MAVUNDE AWAASA ASKARI WA JESHI LA POLISI KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI DODOMA


 Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Anthony Mavunde akizungumza katika semina fupi ya Chama cha Polisi Wanawake.

 washiriki wa semina

 


washiriki wa semina

 
Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Anthony Mavunde amewataka askari wa kike wa Jeshi la Polisi mkoani Dodoma kuchangamkia fursa za kiuchumi zilizopo mkoani hapo kwa kushiriki katika shughuli mbalimbali za uzalishaji mali na uchumi wa viwanda.

Mavunde ameyasema hayo leo wakati akizungumza na Chama cha Polisi Wanawake katika semina fupi aliyoiandaa katika Bwalo la Polisi-Dodoma kwa lengo la kuwapa Askari Polisi elimu juu ya masuala ya UJASIRIAMALI na UWEKEZAJI.


“Najua jukumu lenu la msingi ni Ulinzi wa Mali na Raia,lakini si vibaya pia mkautumia muda wenu wa ziada kufanya shughuli za uzalishaji mali kwa lengo la kuwaongezea kipato”amesema Mavunde

Naye,Kiongozi wa mtandao wa Askari Polisi wanawake Mkoa wa Dodoma SP Hiki amemshukuru Mbunge Mavunde kwa kuona haja na umuhimu wa kukutana na Askari hao na kufanikisha semina hiyo ambayo imehusisha wataalamu kutoka SIDO,Mifuko ya Uwezeshwaji na Wataalamu kutoka Manispaa ya Dodoma.


JAFO AWAPONGEZA TAFOPA KWA KUUNGA MKONO KAMPENI YA MKOA WANGU VIWANDA VYANGU.

 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.Selemani Jafo akizungumza na viongozi wa Umoja wa wasindikaji wa vyakula (TAFOPA) waliotembelea Ofisini kwake mapema leo.

 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.Selemani Jafo na baadhi ya viongozi wa TAFOPA ofisini kwake mapema leo.

 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.Selemani Jafo katika Picha ya pamoja na viongozi wa TAFOPA.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.Selemani Jafo(kushoto) akiagana na Mwenyekiti wa TAFOPA Suzy Laiser mara baada ya kikao chao mapema leo.
 
Nteghenjwa Hosseah,Dar es Salaam

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa amepongeza Umoja wa Washindaji wa Vyakula(Tafopa) kwa jitihada zao za kuunga mkojo kampeni ya ujenzi wa viwanda 100 kila Mkoa inayojulikana kama Mkoa wangu Viwanda vyetu.

Waziri Jafo ametoa pongezi hizo kwa wanachama wa Umoja huo waliotembelea Ofisini kwake kwa lengo la kuelezea namna wanavyoshiriki katika kukuza Viwanda kupitia chama hicho cha Usindikaji wa Vyakula.


"Tafopa mnafanya kazi nzuri ambayo moja kwa inaisaidia Tanzania ya Viwanda; kuunganisha watu katika maeneo ya kuwapa elimu ya namna ya kusindika Vyakula kwa namna moja mnatoa ajira kwa watanzania na mnaongeza thamani ya mazao ambayo bila kusindikwa yangeweza kuharibika na kusabisha hasara kwa Wakulima" Alisema Jafo.

Serikali itaendelea kuwashirikisha katika fursa mbalimbali zinazoendelea kutokea na kuwakutanisha na wadau wa maendeleo ili muweze kuwa na Uhakika wa masoko, Mpate maeneo ya kujengea viwanda vya kusindika vyakula na kutatua changamoto zingine zinazowakabili, alimalizia Jafo.


Alizungumza katika kikao hicho Mwenyekiti ya TAFOPA Suzy Laiser amesema mpaka sasa hivi umoja huo una jumla ya wanachama zaidi ya 600 ambao wote wanajishighulisha na usindikaji vyakula na wamekua wakoshiriki na maonyesho ya Taifa ya biashara lakini bado wanakabiliwa na uhaba wa maeneo ya kujenga viwanda kwa ajili ya kazi hiyo.


Aliongeza kuwa wanaishkuru Shirika la Viwanda Vidogo Vidogo (Sido) kwa kuendelea kutoa mafunzo kwa Wanachama ambao wamepata ujuzi zaidi wa kusindika vyakula vya aina mbalimbali lakino changamoto ni ukosefu wa maeneo ya kufanyia kazi zao. Hivyo wengi hufanyia nyumbani ambapo hawawezi kupata Nembo ya Ubora kutoka Tbs nk.


Waziri Jafo alifunga kikao kwa kusema kuwa Suala la Maeneo liko katika Mamlaka za Serikali za Mitaa hivyo atawakutanisha wanachama hao na Viongozi wa Wilaya na Mkoa ili waweze kuangalia suala hilo kwa mapana yake.


Shamra shamra za maadhimisho ya sherehe za kutimia Miaka 54 ya Mapinduzi ya Zanzibar zaendelea.

 Wanafunzi wa Skuli za Msingi na Sekondari wa Wizaya Chake Chake Pemba wakishuhudia hafla ya uzinduzi wa Jengo Jipya la Baraza la Mji Chake Chake Pemba.

 Baadhi ya Wananchi waliohudhuria Uzinduzi wa Jengo Jipya la Baraza la Maji Chake chake Pemba katika shamra shamra za maadhimisho ya kutimia Miaka 54 ya Mapinduzi ya Zanzibar.

 Balozi Seif akizungumza na Wananchi na Watumishi wa Baraza la Mji Chake Cheka wakati wa hafla ya kulizindua Jengo Jipya la Baraza hilo ikiwa ni shamra shamra za Miaka 54 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.
Kushoto ya Balozi Seif ni Waziri wa Fedha na Mipango wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dr. Khalid Salum Mohamed.
 
 Haiba ya Jengo Jipya la Baraza la Mji wa Chake Chake linavyoonekana katika maeneo ya kando ya Bara bara ya Mji wa Chake kuelekea Macho Mane.


Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akizindua rasmi Jengo Jipya la Baraza la Maji Chake chake Pemba ikiwa ni shamra shamra za maadhimisho ya sherehe za kutimia Miaka 54 ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Picha na – OMPR – ZNZ.

                                        Press Release:-

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar haitamuonea haya  kwa kumfukuza kazi mara moja Mtumishi yeyote wa Serikali au Taasisi za Umma atakayegundulika anatoa huduma  kwa Umma katika misingi ya Kibaguzi.

Akizindua rasmi Jengo Jipya la Ofisi ya Baraza la Mji la Chake chake Pemba ikiwa miongoni mwa shamra shamra za sherehe za Maadhimisho ya kutimia Miaka 54 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar  Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alisema Serikali Kuu inataka kuona mabadiliko makubwa katika maeneo ya Utawala.

Balozi Seif alisema Serikali imefanya mageuzi makubwa katika mfumo uitwayo Ugatuzi na kuhamisha majukumu yake katika Serikali za Mitaa kwa lengo la kuimarisha utoaji bora wa huduma mbali mbali kwa Wananchi.

Alisema uhamishaji huo wa majukumu umeanza rasmi Mwaka huu unaoendelea wa Fedha ambapo huduma za msingi kama vile elimu ya maandalizi na Msingi, afya ikiwemo huduma za msingi  za Kilimo sasa ziotakuwa chini ya dhamana ya Serikali za Mitaa za maeneo husika.

Alieleza kwamba Wananchi wanapaswa kutambua kuwa kitendo hicho cha kuwapelekea huduma karibu yao na huduma hizo zikatolewa katika mazingira mazuri mfano wa Jengo hilo zina lengo la kuimarisha  Utawala wa Demokrasia  hapa Nchini.

Balozi Seif alifahamisha kwamba wakati Serikali Kuu itabakia na mambo ya jumla kama vile uandaaji wa sera, kanuni na usimamizi wa jumla uimarishaji huo wa Serikali za Mitaa unatoa nafasi na fursa pana kwa Wananchi wajiongoze na kujitawala wenyewe katika maamuzi ya mambo yanayowakabili wenyewe.

Aliwakumbusha Wananchi kwamba Madiwani waliowachagua  wanawajibika kwao Wananchi, na pale watakapoona huduma wanazopaswa kupewa haziendi vyema wana haki ya kuwawajibisha, kuwahoji sambamba na kutaka maelezo yatakayowaridhiosha huku wakielewa kwamba hiyo ndio maana ya kuimarisha Demokrasia.

Hata Balozi Seif aliwaomba Wananchi waelewe kuwa kujitawala kuna gharama zake ambazo hazina budi kulipwa na Wananchi wenyewe wanaojitawala huku wakielewa kwamba Baraza la Mji ni lao linalotoa huduma kwao ambazo ni gharama zinazotokana na ada wanazotowa.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alielezea kutofurahishwa kwake na taarifa za Machinjio ya Wesha yasiyotumika vizuri na kuachwa bila ya matunzo jambo ambalo halikubaliki na wahusika wanapaswa kulishughulikia mara moja.

Balozi Seif  alionya kwamba wakati atalifuatilia suala hilo lazima Wananchi na watumishi wa Mabaraza la Miji  wathamini mali wanazopatiwa ambazo hugharimu fedha nyingi na kuwataka Wananchi wa Chake wakatae kuona mali zao zinatumika ovyo na hatimae kuharibika mapema.

Akitoa Taarifa za ujenzi wa Jengo hilo la Baraza la Mji wa Chake Chake Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Nd. Khamis Mussa Omar  alisema ujenzi huo ni sehemu ya Mradi Mkuu wa Huduma za Jamii  Zanzibar { ZUSP }.

Ndugu Mussa alisema changamoto ya ujenzi huo ilitokana na ubovu wa Nguzo za asili ambazo Mkandarasi wa Mradi huo alilazimika kujenga upya nguzo hizo na kuongezeka kwa gharama za ujenzi huo zilizofikia asilimia 36.4%.

Alisema mradi huo Mkuu wa huduma za Jamii hadi kukamilika kwake unatarajiwa kugharimu jumla ya shilingi Bilioni Moja ambapo tayari kwa awamu ya kwanza  zimeshajengwa Ngazi Nane za Kuvukia Wananchi kutoka sehemu moja kwenda nyengine katika maeneo ya Mabondeni.

Katibu Mkuu Mussa aliishukuru Benki ya Dunia { World Bank } kwa kuendelea kuipatia Mikopo  ya Fedha Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ili kutekeleza miradi mbali mbali ya Maendeleo.

Naye Waziri wa Fedha na Mipango Zanzibar Dr. Khalid Salum Mohamed  akimkaribisha Balozi Seif  kwenye Hafla hiyo alisema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inakusudia kuweka Taa za Bara barani katika Miji yote Mitatu ya Kisiwa cha Pemba. 

Dr. Khalid alisema jumla ya Dola za Kimarekani 55 Milioni zitakazotolewa Mkopo na Benki  ya Dunia zitaelekezwa katika mradi huo muhimu kwa kustawisha Miji hizo sambamba na kuweka haiba nzuri ya maeneo hayo.

Alisema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendelea kustawisha maisha ya Wananchi wake kadri ya hali ya uchumi inavyozidi kuongezeka mfano wa Mwaka 2016 uliopata mafanikio makubvwa kutokana na kuongezeka kwa Pato la Taifa na kufikia hadi asilimia 6.8%.

Waziri Khalid alifahamisha kwamba nyongeza za Mishahara zilizotolewa na Serikali zikaenda sambamba na upandishwaji wa Pencheni kwa Wazee waliostaafu na wale waliofikia umri zaidi ya Miaka 70 ni miongoni mwa mafanikio ya ongezeko hilo la Mapato ya Taifa.


Othman Khamkis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
9/1/2018.

Who is the African of the year 2017?

Written By CCMdijitali on Wednesday, January 3, 2018 | January 03, 2018

CHANGE MAKERS, WEALTH CREATORS, MEET THE NOMINEES FOR ALM AFRICAN OF THE YEAR 2017

In a continent of over 1.2 Billion people, they have stood out. These group of individuals have elevated and redefined benchmarks for accessing performance in the continent. More importantly, they are committed to sustaining the “African Dream” – they are the nominees for African of the Year category in the African Leadership Magazine Persons of the Year award. The nominees are: Nana Addo Dankwa Akuffo Addo, President of Ghana; Tony Elumelu, Chairman, Heirs Holding; Paul Kagame, President of Rwanda; John Pombe Magufuli, President of Tanzania; Cyril Ramaphosa, Executive Chairman, Shanduka Group; Chief Oladipo Jadesimi, Chairman LADOL, Nigeria.

ABOUT AFRICAN LEADERSHIP MAGAZINE
The African Leadership magazine is published by African Leadership (UK) Limited, a company registered in the United Kingdom (Company No. 07435198). The magazine focuses on bringing the best of Africa to a global audience, telling the African story from an African perspective; while evolving solutions to peculiar challenges being faced by the continent today. Since its maiden edition, African Leadership Magazine has grown to become a leading pan-African flagship leadership-focused publication read by over 480, 000 targeted international investors, business executives, government policy makers and multilateral agencies across Africa, the Middle East and Asia, Europe, and the US. It is distributed at major international and African Leadership events around the world. The magazine has over 800,000 fans on Facebook and a virile readership on other social media platforms.

African of the Year 2017 (Previously Person of the Year)

  • African of the Year 2017 (Previously Person of the Year)
This recognition is open to an African whose actions have greatly impacted the continent positively in the year under review and helped shape his or her immediate society and continues to inspire globally.

This poll is closed! Poll activity: Start date 13-12-2017 11:47:38 End date 03-01-2018 14:29:29 Poll Results:
Who is the African of the year 2017?

NAIBU MEYA JIJI LA MBEYA (CHADEMA) AAHIDI USHIRIKIANO NA WATEULE WA RAIS MAGUFULI

  •  AMSIFU MHE MWANJELWA KWA KUSHIRIKIANA NA VYAMA VYA UPINZANI
 Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akizungumza na wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika Mtaa wa Kagwina Kata ya Sinde Jana Januari 2, 2018. Picha Zote Na Mathias Canal

 Naibu Meya wa Jiji la Mbeya Mhe Fanuel Kyanula ambaye ni Diwani wa Kata ya Sinde akizungumza na wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wa hadhara uliohudhuriwa na Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa katika Mtaa wa Kagwina Kata ya Sinde Jana Januari 2, 2018

 Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa akikagua hatua zilizofikiwa katika ujenzi wa Vyumba vya madarasa Shule ya Sekondari Sinde kabla ya kuzungumza na wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika Mtaa wa Kagwina Kata ya Sinde Jana Januari 2, 2018

 Baadhi ya wananchi wakimlaki Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa mara baada ya kuwasili kwa ajili ya Mkutano wa hadhara uliofanyika katika Mtaa wa Kagwina Kata ya Sinde Jana Januari 2, 2018.

Diwani wa Kata ya Manda Mkoani Mbeya Mhe Newton Mwakijobe akitoa salamu za wananchi wa Kata yake kwenye mkutano wa wananchi wa kata jirani ya Sinde kabla ya Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa kuzungumza na wananchi waliohudhuria kwenye mkutano huo Jana Januari 2, 2018

Na Mathias Canal, Mbeya


IMEBAINIKA kuwa tofauti za kiitikadi baina ya madiwani katika Halmashauri nyingi nchini, zimekuwa ni kikwazo kwenye utekelezaji wa miradi ya maendeleo yenye tija kubwa kwa wananchi.
 
Tofauti hizo zimekuwa chanzo kikubwa katika utekelezaji wa miradi inayobuniwa na Halmashauri husika, au inayoletwa na Serikali Kuu na wafadhili. Mitazamo ya kisiasa, tofauti ya uwakilishi wa vyama na ubinafsi, ndio sababu kuu.

Katika Halmashauri ya Jiji la Mbeya inayoongozwa na Meya na Naibu Meya wanaotokana na vyama vya upinzania hali imekuwa tofauti kwani asilimia kubwa ya madiwani wanaunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli tofauti kabisa na Halmashauri zingine.


Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliohudhuriwa na Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa Jana 2 Januari 2018 uliofanyika katika Mtaa wa Kagwina, Kata ya Sinde Naibu Meya wa Jiji la Mbeya Mhe Fanuel Kyanula ambaye ni Diwani wa Kata ya Sinde alisema kuwa utendaji wa Rais Magufuli ni faida ya watanzania wote hivyo kuna kila sababu ya wananchi kuunga mkono juhudi za serikali yake.


Kyanula alisema kuwa pamoja na kuwa kiongozi anayetokana na chama cha upinzani lakini serikali ni moja hivyo anaungana na wateule wote wa Rais Magufuli katika kutekeleza dhamira ya serikali ya kuwaletea wananchi maendeleo huku akimtaja Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa kama kiongozi wa mfano katika Mkoa wa Mbeya hivyo kuahidi kushirikiana nae kwa karibu.


Naibu Meya huyo amempongeza Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa kwa kuchangia jumla ya mifuko 40 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule ya Sekondari Iyera (Mifuko 20) na Shule ya Sekondari Sinde (Mifuko 20) zilizopo Jijini Mbeya.


Alimtaja Mhe Mwanjelwa kwamba amekuwa mwalimu mzuri wa somo la Uraia Mkoani Mbeya akifundisha kuhusu umoja na mshikamano huku akisisitiza kuwa Maendeleo ni dhana pana kwa wananchi na hayapaswi kufanywa kwa mipaka ya vyama vya siasa.


Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Mary Mwanjelwa yupo ziarani Mkoani Mbeya ambapo amesifu Uongozi wa Wilaya ya Mbeya kwa kazi kubwa katika utendaji ikiwemo kuanza mchakato wa ujenzi wa vyumba vya madarsa ili kuikabili changamoto ya wingi wa wananfunzi waliofaulu kujiunga kidato cha kwanza Mwaka 2018.


JAFO,PROF.MAJI MAREFU WAUNGURUMA KAMPENI ZA UDIWANI KATA YA KWAGUNDA KOROGWE.

 Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais, TAMISEMI Selemani Jafo akimnadi Mgombea udiwani wa Kata ya Kwagunda(CCM) Saidi Athumani maarufu kwa jina la Moto.

 Mbunge wa Korogwe Vijijini Stephen Ngonyani akizungumza katika kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani kata ya Kwagunda

 Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais, TAMISEMI Selemani Jafo akiwa na viongozi mbalimbali katika kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani kata ya Kwagunda

 Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais, TAMISEMI Selemani Jafo akiwa na viongozi mbalimbali katika kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani kata ya Kwagunda

 Umati wa wananchi waliokuwepo kwenye kampeni za udiwani kata ya Kwagunda.

KAMPENI za uchaguzi mdogo wa udiwani kata ya Kwagunda wilayani Korogwe zimeendelea kushika kasi ambapo leo Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais, TAMISEMI Selemani Jafo na Mbunge wa Korogwe vijijini Stephen Ngonyani maarufu kwa jina la Prof. Maji marefu wameunguruma kumnadi mgombea wa CCM Saidi Athumani.

Uchaguzi umetokana na aliyekuwa diwani wa kata hiyo kufariki dunia miezi michache iliyopita.

Katika kampeni hizo, Jafo ambaye pia ni Mbunge wa Kisarawe ndiye aliyekuwa mgeni rasmi akiwa na mwenyeji wake Prof. Maji marefu wamewaeleza wananchi kwamba watumie fursa hiyo kuhakikisha januari 13 mwaka huu hawafanyi makosa wamemchague Saidi ili aweze kuwatumikia ipasavyo.

Wamewataka wananchi kukiamini chama cha Mapinduzi (CCM) kwa kuwa chini ya Rais John Magufuli kimejipambanua kuwatumikia wananchi wanyonge na maskini.

Mkutano huo ulihudhuriwa na umati mkubwa wa wananchi huku CCM ikidhihirisha imejipanga kupata ushindi wa kishindo katika uchaguzi huo.

WAZIRI JAFO AKERWA HOSPITALI YA WILAYA YA HAI KUSHINDWA KUFUNGA MFUMO WA GoTHoMIS

 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.Selemani Jafo(katikati) akiwasili katika Hospital ya Wilaya ya Hai kukagua ujenzi wa miundombinu ya Afya.

 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.Selemani Jafo(kulia)akikagua ujenzi wa Duka la Dawa linaloendelea kujengwa katika Hospital ya Wilaya ya Hai.

Hii ndiyo Hospital ya Wilaya ya Hai ambayo mpaka sasa haijafunga mfumo wa Uendeshaji na Usimamizi wa Kutolea huduma za Afya - GoTHoMIS. .........................................................
Nteghenjwa Hosseah,Hai.

 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo amekasirishwa na uongozi wa hospital ya Wilaya ya Hai kwankushindwa kutumia mfumo wa Uendeshaji na Usimamizi wa Vituo vya kutolea huduma za Afya (GoTHoMIS).

Waziri Jafo akiwa ziarani Katika Wilaya hiyo kukagua ujenzi wa miundombinu ya Afya katika Hospital ya Wilaya alihoji endapo Hospital hiyo imeanza kutumia mfumo wa GoTHoMIS katika uendreshaji na usimamizi wa huduma za Afya ikiwa ni agizo alilolitoa miezi michache iliyopita wakati alipotembelea Hospital hiyo.

Majibu aliyoyapata katika Hospital hiyo hayakumridhisha ambapo Uongozi wa Hospital na Wilaya hiyo ulidai kutokua na mtaalam wa mifumo ya Tehama wa kusimamia usimikaji wa Mfumo ilihali vifaa vyote kama vile Computer kwa ajili ya matumizi ya mfumo vimekwishafika tayari kuanza kutumika.

“Haiwezekani Halmashauri za pembezoni watumie mfumo huu katika uendeshaji wa shughuli zao na nyie wa Mjini kabisa mpaka leo mnasingizia eti hamna mtaalamu, mlishindwa kutafuta hata kutoka katika Halmashauri za Jirani au mna vitu mnavifanya na mnaona mfumo ukianza kutumika hamtaweza kuendelea kufanya tena hayo mnayoyaficha ”

Aliongeza kuwa mapato mnayokusanya katika Hospital hii hayaridhishi ukilinganisha na Idadi ya wagonjwa wanaokuja kutibiwa kwa siku na mkianza kutumia Mfumo huu utaonyesha mapato sahihi ambayo mnakusanya na hili ndio ninaloona mnalikwepa, sasa ninawapa wiki mbili tu mfumo huu uwe umeanza kutumika.

 Akitoa Taarifa ya Hospital hiyo mganga Mkuu wa Wilaya hiyo alisema mapato yanayokusanywa kwa mwezi ni zaidi ya Mil. 50 na kwa kipindi cha Miaka 50 wamekusanya zaidi ya Mil 300 na baada ya kukamilisha ujenzi wa Duka la Dawa la Hospital hiyo watakusanya Fedha nyingi Zaidi.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Hai amemuahidi Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.Selemani Jafo kuwa mfumo huo utakamilika ndani ya wiki moja na utaanza kutumika katika kusimamia na kuendesha shughuli za utoaji wa huduma za Afya katika Hospital ya Wilaya ya Hai.

MAVUNDE AAHIDI KULIPATIA UFUMBUZI SUALA LA FIDIA KWA WANANCHI WA MAKOLE

 Mbunge wa Dodoma mjini Anthony Mavunde akizungumza na wananchi wa Kata ya Makole

 Mbunge wa Dodoma mjini Anthony Mavunde akizungumza na wananchi wa Kata ya Makole


Wananchi wakimsikiliza Mbunge wao

MBUNGE wa jimbo la Dodoma mjini Anthony Mavunde amefanya ziara katika kata ya Makole na kuahidi kulipatia ufumbuzi suala la ulipwaji fidia kwa wananchi wanaopisha upanuzi wa Kiwaja cha Ndege cha Dodoma.

Mavunde amefanya ziara hiyo kwa lengo la kusikiliza kero zinazowakabili wananchi wa maeneo mbalimbali.

Katika ziara yake kwenye kata hiyo,Mavunde amesema atafuatilia na kulipatia ufumbuzi suala la ulipwaji fidia kwa wananchi hao.

"Wananchi hawa wanapisha maeneo yao kwa ajili ya upanuzi wa Kiwanja cha Ndege,kurekebisha miundombinu ya barabara na kufungua barabara ambazo hazipitiki,kurekebisha mfumo wa majitaka eneo la Makole Kisiwani,Upatikanaji wa wodi ya wakina mama katika Kliniki ya Makole,"amesema

Aidha amewahakikishia wananchi juu ya upanuzi wa kituo cha Afya cha Makole kuwa kitakuwa cha kisasa kutokana na serikali kutoa ambapo kiasi cha Shilingi milioni mia tano (Tsh 500,000,000/=) kwa ajili ya kuboresha kituo hicho.

SIHA WAPATA NEEMA UKAMILISHAJI WA HOSPITALI YA WILAYA

 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo akisaini kitabu ha wageni wakati wa ziara yake katika Halmashauri ya Wilaya ya Siha, pembeni yake ni Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Anna Ngwira.

 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo(katikati) akikagua ukamilishaji wa Hospital ya Wilaya ya Hai alipofanya ziara yake katika Wilaya Hiyo.

 Hili ni kati ya majengo yanayoendelea kujengwa katika Hospital ya Wilaya ya Hai.

 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo akizuangumza na watumishi wa Idara ya Afya wakati alipotembelea Hospital ya Wilaya ya Hai.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Mkoa wa Kilimanjaro, Wilaya na Siha pamoja na watumishi wa Halmashauri hiyo.
 .................................................................
Nteghenjwa Hosseah, Siha.


 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo amesema atafanya kila liwezekanalo kupata Fedha zaidi kwa ajili ya ukamilishaji ya hospital ya Wilaya ya Siha.

Waziri Jafo amesema hayo alipokua akifuatilia Agizo lake alilolitoa miezi kadhaa iliyopita ya kuacha kutumia Mkandarasi na kutumia Mafundi wa jamii "Force Account" katika ujenzi wa hospital hiyo ambapo Halmashauri ya Siha ilishatoa kazi hiyo kwa Mkandarasi na gharama za ujenzi kuwa juu zaidi.

"Katika ziara yangu iliyopita Kazi ilikua haijaanza na bado mlikua mnajadiliana na Mkandarasi mlinieleza kuwa zinahitajika Fedha zaidi kwa ajili ya kukamilisha kazi hii kwa mujibu wa Mkandarasi ndipo niliposhauri mtumie Mafundi wa kijamii "Force Account" na sio Mkandarasi kama mlivyopanga hapo awali" alisema Jafo.

Aliongeza "nimefurahi kuwa mlinielewa na mkazingatia ushauri wangu na leo hii ninaona matunda ya matumizi ya mafundi wa kijamii ambao wamefanya kazi nzuri kwa ubora wa hali ya juu na gharama nafuu katika hili hongereni sana".

Alisisitiza kuwa Nimeona majengo ambayo yanakaribia kukamilika lakin pia nimeskia taarifa yenu kuwa bado kuna majengo zaidi yanahitajika ila kukamilisha hadhi ya hospital ya Wilaya ninaahidi kuwatafutia Fedha kwa ajili ya Ukamilishaji wa majengo hayo.

Akisoma taara ya Afya Mganga Mkuu wa Wilaya hiyo Dr Andrew Method amesema Wilaya hiyo unakabiliwa na changamoto kubwa ya Uhaba wa Hospital ya Wilaya na vituo vya Afya vilivyopo ni vitano tu ambavyo kati ya hivyo cha Serikali ni kimoja tu hivyo nguvu kubwa imewekwa katika kuhakikisha wanapata miundombinu bora ya hospital ya Wilaya.

" Fedha tulizopata ilikua ni Mil 200 na kwa kuzingatia maelekezo yako tulitumia Force Account na kama unavyoona Mhe. Waziri kazi iko katika hatua za mwishoni na tumebada majengo mengi zaidi ya ramani ya awali".

Ujenzi wa Hospital hii utakapokamilika utawezesha Wilaya ya Siha kuwa hospital nmoja ya Wilaya pamoja na ile ya Kibong'oto iliyoko chini ya Wizara ya Afya.

 
Support : #BegaKwaBegaNaMamaSamia | JAK | CCM Arusha
Copyright © 2011. CCM Dijitali - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Jasper K
Proudly powered by Blogger
Link