MIUNDOMBINU YA ELIMU ZANZIBAR SASA YALINGANA NA MAHITAJI YA KARNE YA 21
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Zanzibar imepiga hatua kubwa katika kuimarisha mazin...
Latest Post
Showing posts with label KITAIFA. Show all posts
Showing posts with label KITAIFA. Show all posts
January 08, 2026

Naibu Waziri Millya akutana na Uongozi wa Jumuiya ya Waislamu wa Ahmadiyya
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. James Kinyasi Millya (Mb), amekutana na Amiri na Mbashiri Mkuu wa Jumuiya ya Waislamu wa Ahmadiyya Tanzania, Shekh Khawaja Muzaffar Ahmad, aliyetembelea Ofisi ndogo za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki jijini Dar Es Salaam kwa lengo la kujitambulisha na kuwasilisha salamu za pongezi kwa Uongozi wa Wizara kwa utekelezaji uliotukuka wa majukumu yake.
Mhe. Millya, akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabiti Kombo (Mb), aliishukuru Jumuiya ya Ahmadiyya kwa juhudi zake katika kutoa huduma mbalimbali za kijamii na kibinadamu maeneo mbalimbali nchini. Aliendelea kueleza kuwa Jumuiya ya Waislamu wa Ahmadiyya Tanzania imekuwa mshirika muhimu katika maendeleo ya taifa na kwamba Serikali inatambua na kuthamini mchango wa taasisi hiyo katika kuleta maendeleo endelevu nchini katika sekta mbalimbali.
Ameongeza kuwa Wizara ipo tayari kutoa ushirikiano wowote utakaohitajika ili kuwezesha utekelezaji wa shughuli mbalimbali za jumuiya hiyo, ikiwemo utekelezaji wa programu za kurejesha kwa jamii na mikutano, ikiwa ni pamoja na Mkutano Mkuu wa Mwaka (Jalsa Salana) unaotarajiwa kufanyika Septemba 2026, na Mkutano Mkuu wa Kimataifa wa Jumuiya ya Ahmadiya Duniani unaopangwa kufanyika mwezi July 2026 nchini Uingereza.
Mazungumzo hayo yalihudhuriwa na, Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Abdalah Kilima pamoja na maafisa waandamizi wa Wizara.
Kwa upande wake, Amiri na Mbashiri Mkuu wa Jumuiya ya Waislamu wa Ahmadiyya Tanzania, Shekh Khawaja Muzaffar Ahmad, amesema kuwa tangu jumuiya hiyo ilipoanzishwa mwaka 1934, imefanikiwa kuanzisha matawi 450 nchini na kueneza mafundisho ya Dini ya Kiislam kwa misingi ya Qur’an Tukufu, huku ikikuza amani, upendo, udugu, uvumilivu, heshima, na kusaidia watu wote bila kujali kabila, imani au itikadi zao.
Sheikh Ahmad ametaja miradi na programu za kurejesha kwa jamii inayotekelezwa na jumuiya hiyo kuwa ni mradi wa hospitali, shule za msingi na sekondari mkoani Morogoro, chuo cha mafunzo cha ufundishaji dini kwa wazawa, uchimbaji wa visima kuunga mkono juhudi za serikali katika kampeni yake ya Kumtua ndoo mama, ambapo hadi sasa wamechimba visima 500 katika maeneo mbalimbali nchini na mradi wa kuendeleza Kijiji cha Kisasa katika Mkoa wa Geita.
Shekh Ahmad aliambatana na viongozi wakuu wa Jumuiya hiyo, wakiwemo Naibu Amiri-1Shekh Abid Mahmood Bhatti, Naibu Amiri-2 Shekh Abdurahman M. Ame, Katibu wa Mambo ya Ndani Bw. Yahya A. Kambaulaya, Katibu wa Mambo ya Nje Bw. Abdallah Kombo na Katibu wa Sauti na Video Shekh Asif M. Butt.





Millya akutana na Uongozi wa Jumuiya ya Waislamu wa Ahmadiyya
Written By CCMdijitali on Thursday, January 8, 2026 | January 08, 2026

Naibu Waziri Millya akutana na Uongozi wa Jumuiya ya Waislamu wa Ahmadiyya
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. James Kinyasi Millya (Mb), amekutana na Amiri na Mbashiri Mkuu wa Jumuiya ya Waislamu wa Ahmadiyya Tanzania, Shekh Khawaja Muzaffar Ahmad, aliyetembelea Ofisi ndogo za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki jijini Dar Es Salaam kwa lengo la kujitambulisha na kuwasilisha salamu za pongezi kwa Uongozi wa Wizara kwa utekelezaji uliotukuka wa majukumu yake.
Mhe. Millya, akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabiti Kombo (Mb), aliishukuru Jumuiya ya Ahmadiyya kwa juhudi zake katika kutoa huduma mbalimbali za kijamii na kibinadamu maeneo mbalimbali nchini. Aliendelea kueleza kuwa Jumuiya ya Waislamu wa Ahmadiyya Tanzania imekuwa mshirika muhimu katika maendeleo ya taifa na kwamba Serikali inatambua na kuthamini mchango wa taasisi hiyo katika kuleta maendeleo endelevu nchini katika sekta mbalimbali.
Ameongeza kuwa Wizara ipo tayari kutoa ushirikiano wowote utakaohitajika ili kuwezesha utekelezaji wa shughuli mbalimbali za jumuiya hiyo, ikiwemo utekelezaji wa programu za kurejesha kwa jamii na mikutano, ikiwa ni pamoja na Mkutano Mkuu wa Mwaka (Jalsa Salana) unaotarajiwa kufanyika Septemba 2026, na Mkutano Mkuu wa Kimataifa wa Jumuiya ya Ahmadiya Duniani unaopangwa kufanyika mwezi July 2026 nchini Uingereza.
Mazungumzo hayo yalihudhuriwa na, Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Abdalah Kilima pamoja na maafisa waandamizi wa Wizara.
Kwa upande wake, Amiri na Mbashiri Mkuu wa Jumuiya ya Waislamu wa Ahmadiyya Tanzania, Shekh Khawaja Muzaffar Ahmad, amesema kuwa tangu jumuiya hiyo ilipoanzishwa mwaka 1934, imefanikiwa kuanzisha matawi 450 nchini na kueneza mafundisho ya Dini ya Kiislam kwa misingi ya Qur’an Tukufu, huku ikikuza amani, upendo, udugu, uvumilivu, heshima, na kusaidia watu wote bila kujali kabila, imani au itikadi zao.
Sheikh Ahmad ametaja miradi na programu za kurejesha kwa jamii inayotekelezwa na jumuiya hiyo kuwa ni mradi wa hospitali, shule za msingi na sekondari mkoani Morogoro, chuo cha mafunzo cha ufundishaji dini kwa wazawa, uchimbaji wa visima kuunga mkono juhudi za serikali katika kampeni yake ya Kumtua ndoo mama, ambapo hadi sasa wamechimba visima 500 katika maeneo mbalimbali nchini na mradi wa kuendeleza Kijiji cha Kisasa katika Mkoa wa Geita.
Shekh Ahmad aliambatana na viongozi wakuu wa Jumuiya hiyo, wakiwemo Naibu Amiri-1Shekh Abid Mahmood Bhatti, Naibu Amiri-2 Shekh Abdurahman M. Ame, Katibu wa Mambo ya Ndani Bw. Yahya A. Kambaulaya, Katibu wa Mambo ya Nje Bw. Abdallah Kombo na Katibu wa Sauti na Video Shekh Asif M. Butt.






Labels:
KITAIFA
December 20, 2025

Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Laurent Degratius Luswetula (Mb), amerejea wito wake kwa vijana kutumia teknolojia hususani Akili Mnemba (AI) na mitandao ya kijamii ili kubuni fursa za kiuchumi na kuongeza kipato.
Mhe. Luswetula amesema hayo wakati wa Mahafali ya 23 ya Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) -Kampasi ya Dar es Salaam, Zanzibar na Tanga yaliyofanyika katika viwanja vya Chuo hicho, Kurasini jijini Dar es Salaam.
Mhe. Luswetula alisema kuwa matumizi ya teknolojia yakitumika vizuri itawajengea vijana kujiamini, kufikiri kwa ubunifu na kuwa wazalishaji wa fursa badala ya kuwa watafuta ajira pekee.
Aidha Mhe. Luswetula aliwaasa vijana kuwa watengeneza maudhui (content creator) wenye tija na wanaozalisha maudhui yenye thamani, yanayongeza kipato, kuzingatia maadili na kufuata sheria na taratibu za nchi.
‘’Katika dunia ya sasa, tumieni teknolojia, hususan Akili Mnemba (AI) na mitandao ya kijamii, kubuni fursa za kiuchumi na kuongeza kipato. Vijana wa leo wanaita hii kuwa ‘content creator’ nawasihi muwe content creator wenye tija, wanaozalisha maudhui yenye thamani, yanayoongeza kipato kwa njia halali, kuzingatia maadili na kufuata sheria na taratibu za nchi yetu’’. Alisisitiza Mhe. Luswetula.
Katika mahafali hayo Mhe. Luswetula aliwataka wahitimu kutumia elimu na maarifa waliyoyapata chuoni kama mtaji wa maisha yao kwa kuwa Serikali inawategemea kuwa vijana wabunifu, waadilifu na watumiaji mahiri wa teknolojia katika kuleta mabadiliko Chanya katika jamii.
Mhe. Luswetula aliipongeza Taasisi ya Uhasibu Tanzania kwa kujumuisha Kampasi tatu za Dar es Salaam, Zanzibar na Tanga katika Mahafali ya 23 ya Taasisi hiyo na kuongeza kuwa mwelekeo wa maendeleo na faida za kijiografia, Dar es Salaam, Zanzibar na Tanga ni miongoni mwa maeneo muhimu yanayoendelea kukua kwa kasi na kuwa nguzo ya uchumi wa Taifa na hayo yanachangia kutoa fursa nyingi kwa wahitimu kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi na kuchangia maendeleo ya Taifa.
‘’Dar es Salaam inaendelea kuwa kitovu cha biashara, bandari na huduma za kifedha, Zanzibar ni lango muhimu la utalii, uchumi wa buluu na biashara ya bandari, huku Tanga ikiwa na nafasi ya kimkakati, viwanda na utalii wa fukwe. Maeneo haya yanatoa fursa nyingi kwa wahitimu wetu kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi na kuchangia maendeleo ya Taifa’’ Aliongeza Mhe. Luswetula.
Akiongea kwenye mahafali hayo, Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) Prof. William Pallangyo alisema kuwa Taasisi imeendelea kuboresha miundombinu ya kujifunzia na kufundishia katika Kampasi za Mtwara, Mbeya, Mwanza na Kigoma, huku shughuli za ujenzi zikiendelea katika Kampasi za Singida, Mwanza na Zanzibar ambapo Jumla ya shilingi za Kitanzania bilioni 59 zimetumika kupitia Mradi wa HEET na mapato ya ndani ya Taasisi katika ujenzi wa Kampasi hizo.
Prof. Pallangyo aliongeza kuwa Taasisi ya Uhasibu Tanzania imeanzisha kozi mpya za shahada ya Uzamili zinazolenga kukuza ujasiriamali, ubunifu na usimamizi wa miradi ili kuwaandaa wahitimu wenye ujuzi unaoendana na mahitaji ya soko.
‘’Katika Mwaka wa Masomo 2025/2056 TIA imeanzisha kozi mpya za Shahada ya Uzamili zinazolenga kukuza ujasiriamali, ubunifu na usimamizi wa miradi ya maendeleo. Lengo letu ni kuandaa wahitimu wenye ujuzi unaoendana na mahitaji ya soko la ajira, teknolojia na mwelekeo na Mpango wa Maendeleo ya Taifa (2050)’’ Alisema Prof.Pallangyo.
Prof. Pallangyo aliongeza kuwa Katika kuendeleza taaluma na ujuzi wa vitendo kwa wanafunzi, Taasisi imehimiza mafunzo ya vitendo na ubunifu kupitia mashindano ya Mawazo Bunifu (Business Ideas Competitions) katika kampasi zote nane ambapo kupitia mpango huu umewezesha wanafunzi kushiriki katika ziara za kielemu katika vyuo mbalimbali barani Afrika.
‘’ Kupitia mpango huu, mwaka 2023/24 wanafunzi walishiriki ziara za kielimu katika Chuo Kikuu cha Mount Kenya (Kenya). Mwaka 2024/25 walipelekwa Chuo Kikuu cha Makerere (Uganda). Mwaka huu maandalizi yanaendelea ya kuwapeleka washindi wa kampasi zote Chuo Kikuu cha Pretoria, Afrika Kusini’’ aliongeza Prof. Pallangyo.
Awali akimkaribisha mgeni rasmi, Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Laurent Degratius Luswetula (Mb), Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Wizara Profesa Jehovaness Aikael alisema bodi inaweka mkazo mkubwa katika ubora wa elimu, maadili, uwajibikaji na uadilifu ikitambua kwamba elimu bora haipimwi kwa maarifa pekee bali kwa uwezo wa Taasisi kulea wahitimu wenye tabia njema, weledi na uwezo wa kuaminika katika jamii na za kazi.
Profesa Aikael alisema kuwa Bodi ya ushauri ya Wizara imeendelea kusimamia muelekeo wa kimkakati wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania kwa lengo la kuifanya TIA kuwa Taasisi shindani kitaifa na kikanda, kwa kuhakikisha mitaala, mbinu za ufundishaji na mazingira ya kujifunzia vinaendana na mahitaji ya sasa na baadae kiuchumi, kwenye soko la ajira na maendeleo ya sayansi na teknolojia.
‘’Katika kusimamia mwelekeo huo, Bodi ya ushauri ya Wizara inaendelea kusisitiza umuhimu wa kuandaa wahitimu wanaoendana na mabadiliko ya sayansi na teknolojia, ikiwemo matumizi yenye weledi na uwajibikaji ya Akili Bandia (Artificial Intelligence) ili kuongeza ubora, ufanisi na ushindani wa rasilimali watu’’ alisema Prof. Aikael
Katika mahafali ya 23 ya Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) imejumuisha wahitimu 6,334 kati yao wanawake ni 3,589 na wanaume 2,745 ambao wametunikiwa vyeti katika ngazi mbalimbali kuanzia cheti cha Awali hadi shahada ya Uzamili.






MHE. LUSWETULA: VIJANA TUMIENI MITANDAO YA KIJAMII KUBUNI FURSA ZA KUJIKWAMUA KIUCHUMI.
Written By CCMdijitali on Saturday, December 20, 2025 | December 20, 2025

Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Laurent Degratius Luswetula (Mb), amerejea wito wake kwa vijana kutumia teknolojia hususani Akili Mnemba (AI) na mitandao ya kijamii ili kubuni fursa za kiuchumi na kuongeza kipato.
Mhe. Luswetula amesema hayo wakati wa Mahafali ya 23 ya Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) -Kampasi ya Dar es Salaam, Zanzibar na Tanga yaliyofanyika katika viwanja vya Chuo hicho, Kurasini jijini Dar es Salaam.
Mhe. Luswetula alisema kuwa matumizi ya teknolojia yakitumika vizuri itawajengea vijana kujiamini, kufikiri kwa ubunifu na kuwa wazalishaji wa fursa badala ya kuwa watafuta ajira pekee.
Aidha Mhe. Luswetula aliwaasa vijana kuwa watengeneza maudhui (content creator) wenye tija na wanaozalisha maudhui yenye thamani, yanayongeza kipato, kuzingatia maadili na kufuata sheria na taratibu za nchi.
‘’Katika dunia ya sasa, tumieni teknolojia, hususan Akili Mnemba (AI) na mitandao ya kijamii, kubuni fursa za kiuchumi na kuongeza kipato. Vijana wa leo wanaita hii kuwa ‘content creator’ nawasihi muwe content creator wenye tija, wanaozalisha maudhui yenye thamani, yanayoongeza kipato kwa njia halali, kuzingatia maadili na kufuata sheria na taratibu za nchi yetu’’. Alisisitiza Mhe. Luswetula.
Katika mahafali hayo Mhe. Luswetula aliwataka wahitimu kutumia elimu na maarifa waliyoyapata chuoni kama mtaji wa maisha yao kwa kuwa Serikali inawategemea kuwa vijana wabunifu, waadilifu na watumiaji mahiri wa teknolojia katika kuleta mabadiliko Chanya katika jamii.
Mhe. Luswetula aliipongeza Taasisi ya Uhasibu Tanzania kwa kujumuisha Kampasi tatu za Dar es Salaam, Zanzibar na Tanga katika Mahafali ya 23 ya Taasisi hiyo na kuongeza kuwa mwelekeo wa maendeleo na faida za kijiografia, Dar es Salaam, Zanzibar na Tanga ni miongoni mwa maeneo muhimu yanayoendelea kukua kwa kasi na kuwa nguzo ya uchumi wa Taifa na hayo yanachangia kutoa fursa nyingi kwa wahitimu kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi na kuchangia maendeleo ya Taifa.
‘’Dar es Salaam inaendelea kuwa kitovu cha biashara, bandari na huduma za kifedha, Zanzibar ni lango muhimu la utalii, uchumi wa buluu na biashara ya bandari, huku Tanga ikiwa na nafasi ya kimkakati, viwanda na utalii wa fukwe. Maeneo haya yanatoa fursa nyingi kwa wahitimu wetu kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi na kuchangia maendeleo ya Taifa’’ Aliongeza Mhe. Luswetula.
Akiongea kwenye mahafali hayo, Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) Prof. William Pallangyo alisema kuwa Taasisi imeendelea kuboresha miundombinu ya kujifunzia na kufundishia katika Kampasi za Mtwara, Mbeya, Mwanza na Kigoma, huku shughuli za ujenzi zikiendelea katika Kampasi za Singida, Mwanza na Zanzibar ambapo Jumla ya shilingi za Kitanzania bilioni 59 zimetumika kupitia Mradi wa HEET na mapato ya ndani ya Taasisi katika ujenzi wa Kampasi hizo.
Prof. Pallangyo aliongeza kuwa Taasisi ya Uhasibu Tanzania imeanzisha kozi mpya za shahada ya Uzamili zinazolenga kukuza ujasiriamali, ubunifu na usimamizi wa miradi ili kuwaandaa wahitimu wenye ujuzi unaoendana na mahitaji ya soko.
‘’Katika Mwaka wa Masomo 2025/2056 TIA imeanzisha kozi mpya za Shahada ya Uzamili zinazolenga kukuza ujasiriamali, ubunifu na usimamizi wa miradi ya maendeleo. Lengo letu ni kuandaa wahitimu wenye ujuzi unaoendana na mahitaji ya soko la ajira, teknolojia na mwelekeo na Mpango wa Maendeleo ya Taifa (2050)’’ Alisema Prof.Pallangyo.
Prof. Pallangyo aliongeza kuwa Katika kuendeleza taaluma na ujuzi wa vitendo kwa wanafunzi, Taasisi imehimiza mafunzo ya vitendo na ubunifu kupitia mashindano ya Mawazo Bunifu (Business Ideas Competitions) katika kampasi zote nane ambapo kupitia mpango huu umewezesha wanafunzi kushiriki katika ziara za kielemu katika vyuo mbalimbali barani Afrika.
‘’ Kupitia mpango huu, mwaka 2023/24 wanafunzi walishiriki ziara za kielimu katika Chuo Kikuu cha Mount Kenya (Kenya). Mwaka 2024/25 walipelekwa Chuo Kikuu cha Makerere (Uganda). Mwaka huu maandalizi yanaendelea ya kuwapeleka washindi wa kampasi zote Chuo Kikuu cha Pretoria, Afrika Kusini’’ aliongeza Prof. Pallangyo.
Awali akimkaribisha mgeni rasmi, Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Laurent Degratius Luswetula (Mb), Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Wizara Profesa Jehovaness Aikael alisema bodi inaweka mkazo mkubwa katika ubora wa elimu, maadili, uwajibikaji na uadilifu ikitambua kwamba elimu bora haipimwi kwa maarifa pekee bali kwa uwezo wa Taasisi kulea wahitimu wenye tabia njema, weledi na uwezo wa kuaminika katika jamii na za kazi.
Profesa Aikael alisema kuwa Bodi ya ushauri ya Wizara imeendelea kusimamia muelekeo wa kimkakati wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania kwa lengo la kuifanya TIA kuwa Taasisi shindani kitaifa na kikanda, kwa kuhakikisha mitaala, mbinu za ufundishaji na mazingira ya kujifunzia vinaendana na mahitaji ya sasa na baadae kiuchumi, kwenye soko la ajira na maendeleo ya sayansi na teknolojia.
‘’Katika kusimamia mwelekeo huo, Bodi ya ushauri ya Wizara inaendelea kusisitiza umuhimu wa kuandaa wahitimu wanaoendana na mabadiliko ya sayansi na teknolojia, ikiwemo matumizi yenye weledi na uwajibikaji ya Akili Bandia (Artificial Intelligence) ili kuongeza ubora, ufanisi na ushindani wa rasilimali watu’’ alisema Prof. Aikael
Katika mahafali ya 23 ya Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) imejumuisha wahitimu 6,334 kati yao wanawake ni 3,589 na wanaume 2,745 ambao wametunikiwa vyeti katika ngazi mbalimbali kuanzia cheti cha Awali hadi shahada ya Uzamili.







Labels:
KITAIFA
December 17, 2025

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amewaagiza Watendaji Wakuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) na Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) kufanya tathmini ya miradi yote ambayo malipo ya awali yameshafanyika na hatua za ujenzi zilizofikiwa katika miradi hiyo.
Pia amewaagiza kuangalia kama utekelezaji wa miradi hiyo unaendana na kiwango cha fedha ambacho kimeshatolewa. “Na ikiwa itapatikana miradi ambayo imefanyika chini ya fedha iliyopatikana itakuwa ni hujuma dhidi ya uchumi wa nchi yetu, hawa ni lazima wafike kwenye mkono wa sheria”
Ametoa maagizo hayo leo, Jumatano, Desemba 17, 2025 wakati akizungumza na wananchi baada ya kukagua uharibifu wa miundombinu mbalimbali ikiwemo mzani wa. Magari (Mpemba), Mahakama ya Mwanzo Tunduma, soko la Machinga akiwa katika ziara ya kikazi mkoani Songwe.
“Nimefuatilia, yupo mkandarasi ambaye mlimtoa kule Mbinga, asipate kazi nyingine yeyote hapa nchini, wapatieni wazawa, haiwezekani tumpatie mtu pesa halafu aje atuchezeechezee hapa, wale wote mnaowalipa fedha halafu wanatumia kwenye miradi na madeni yao hawawalipi wazawa wasipate kazi tena”
Amesema kuwa wapo baadhi ya wakandarasi wanaolazimisha fedha za utekelezaji wa miradi inayofanyika nchini Tanzania zilipwe katika benki za nchi zao badala yake katika mikataba itakayoanza kuingiwa waelekezwe kufungua akaunti hapa nchini.
“Haiwezekani mradi unafanyika hapa nchini yeye anataka fedha zilipwe kwenye akaunti za nchi zao, zikifika huko wanalipa madeni, huku miradi inasimama, hapana, kwenye mikataba hakikisheni mnaweka kipengele cha wao kufungua akaunti hapa hapa nchini ili malipo yafanyike hapahapa”
Kadhalika, Mheshimiwa Waziri Mkuu amewataka viongozi katika maeneo yote nchini kutopuuza changamoto zinazowakabili wananchi na badala yake wafike kwenye maeneo yao na kushirikiana nao katika kuzitatua.
Amesema Serikali ipo kazini na amewahakikishia wananchi kwamba ahadi zote zilizotolewa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, zilizopo kwenye ilani ya uchaguzi pamoja na yaliyopo katika dira yatatekelezwa kwa vitendo.
Akizungumzia kuhusu usaili wa watumishi wa sekta za afya na elimu, Waziri Mkuu amewataka wahusika wote wa zoezi hilo wazingatie vigezo vilivyowekwa na wasitumie fursa hiyo kuwaweka watu wao. “Msidhulumu watu zingatieni vigezo.”
Pia, Waziri Mkuu amewasihi Watanzania wakiwemo wakazi wa Songwe waendelee kushirikiana kudumisha amani na wakatae kutumika na watu wanaotaka kuivuruga. “Sisi ndio wanufaika wa kwanza wa amani, tuwe na wivu na nchi yetu na haiwezi kuendeshwa kwa rimoti wala vikundi vya wahuni.”
Wakati huo huo, Waziri Mkuu amemuagiza Naibu Waziri wa Ujenzi Mhandisi, Godfrey Kasekenya ahakikishe wakati wa utiaji saini mikataba yote ya miradi ya ukandarasi malipo yake yafanyike kupitia benki na ndani ya nchi.
Mheshimiwa Dkt. Mwigulu pia amemuagiza Naibu Waziri huyo ahakikishe wakandarasi wanasimamiwa vizuri ili fedha zote wanazolipwa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali zitumike katika ujenzi wa miradi husika na si vinginevyo.

DKT. MWIGULU: TANROADS NA TARURA FANYENI TATHMINI YA MIRADI ILIYOLIPWA FEDHA ZA AWALI
Written By CCMdijitali on Wednesday, December 17, 2025 | December 17, 2025

Aagiza mikataba ya ujenzi wa miradi iwe na kipengele cha kufungua akaunti za malipo hapa nchini.
WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amewaagiza Watendaji Wakuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) na Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) kufanya tathmini ya miradi yote ambayo malipo ya awali yameshafanyika na hatua za ujenzi zilizofikiwa katika miradi hiyo.
Pia amewaagiza kuangalia kama utekelezaji wa miradi hiyo unaendana na kiwango cha fedha ambacho kimeshatolewa. “Na ikiwa itapatikana miradi ambayo imefanyika chini ya fedha iliyopatikana itakuwa ni hujuma dhidi ya uchumi wa nchi yetu, hawa ni lazima wafike kwenye mkono wa sheria”
Ametoa maagizo hayo leo, Jumatano, Desemba 17, 2025 wakati akizungumza na wananchi baada ya kukagua uharibifu wa miundombinu mbalimbali ikiwemo mzani wa. Magari (Mpemba), Mahakama ya Mwanzo Tunduma, soko la Machinga akiwa katika ziara ya kikazi mkoani Songwe.
“Nimefuatilia, yupo mkandarasi ambaye mlimtoa kule Mbinga, asipate kazi nyingine yeyote hapa nchini, wapatieni wazawa, haiwezekani tumpatie mtu pesa halafu aje atuchezeechezee hapa, wale wote mnaowalipa fedha halafu wanatumia kwenye miradi na madeni yao hawawalipi wazawa wasipate kazi tena”
Amesema kuwa wapo baadhi ya wakandarasi wanaolazimisha fedha za utekelezaji wa miradi inayofanyika nchini Tanzania zilipwe katika benki za nchi zao badala yake katika mikataba itakayoanza kuingiwa waelekezwe kufungua akaunti hapa nchini.
“Haiwezekani mradi unafanyika hapa nchini yeye anataka fedha zilipwe kwenye akaunti za nchi zao, zikifika huko wanalipa madeni, huku miradi inasimama, hapana, kwenye mikataba hakikisheni mnaweka kipengele cha wao kufungua akaunti hapa hapa nchini ili malipo yafanyike hapahapa”
Kadhalika, Mheshimiwa Waziri Mkuu amewataka viongozi katika maeneo yote nchini kutopuuza changamoto zinazowakabili wananchi na badala yake wafike kwenye maeneo yao na kushirikiana nao katika kuzitatua.
Amesema Serikali ipo kazini na amewahakikishia wananchi kwamba ahadi zote zilizotolewa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, zilizopo kwenye ilani ya uchaguzi pamoja na yaliyopo katika dira yatatekelezwa kwa vitendo.
Akizungumzia kuhusu usaili wa watumishi wa sekta za afya na elimu, Waziri Mkuu amewataka wahusika wote wa zoezi hilo wazingatie vigezo vilivyowekwa na wasitumie fursa hiyo kuwaweka watu wao. “Msidhulumu watu zingatieni vigezo.”
Pia, Waziri Mkuu amewasihi Watanzania wakiwemo wakazi wa Songwe waendelee kushirikiana kudumisha amani na wakatae kutumika na watu wanaotaka kuivuruga. “Sisi ndio wanufaika wa kwanza wa amani, tuwe na wivu na nchi yetu na haiwezi kuendeshwa kwa rimoti wala vikundi vya wahuni.”
Wakati huo huo, Waziri Mkuu amemuagiza Naibu Waziri wa Ujenzi Mhandisi, Godfrey Kasekenya ahakikishe wakati wa utiaji saini mikataba yote ya miradi ya ukandarasi malipo yake yafanyike kupitia benki na ndani ya nchi.
Mheshimiwa Dkt. Mwigulu pia amemuagiza Naibu Waziri huyo ahakikishe wakandarasi wanasimamiwa vizuri ili fedha zote wanazolipwa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali zitumike katika ujenzi wa miradi husika na si vinginevyo.


Labels:
KITAIFA
December 17, 2025

Na Munir Shemweta, WANMM
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo ameiagiza Tume ya Taifa ya Matumizi ya Ardhi kuongeza kasi ya kupanga na kupima ardhi katika maeneo mbalimbali nchini ikiwemo miradi ya kilimo, makazi na uwekezaji.
Mhe. Dkt Leonard Akwilapo amesema hayo leo tarehe 17 Desemba 2025 wakati akifungua Kikao Kazi cha Kamati ya Ufundi ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi kilichofanyika Makao Makuu ya Wizara jijini Dodoma.
Kupitia kikao hicho, Mhe. Dkt Akwilapo amehimiza kukuzwa kwa matumizi ya teknolojia katika ukusanyaji takwimu za kupanga ardhi, kulinda maeneo nyeti ya ikolojia, misitu, vyanzo vya maji, njia za wanyama pori pamoja na kujenga ustahimilivu wa mabadiliko ya tabia nchi kupitia mipango shirikishi na endelevu,
Amesema,Tanzania inakabiliwa na changamoto zinazohusiana na matumizi ya ardhi na kuzitaja kuwa ni pamoja na migongano kati ya shughuli za kilimo na ufugaji, malisho na uhifadhi na upungufu wa maeneo ya uwekezaji wa kimkakati kutokana na mabadiliko ya matumizi ya ardhi yasiyopangwa.
Changamoto nyingine ni uharibifu wa mazingira unaosababishwa na uvamizi wa vyanzo vya maji, ukataji miti hovyo, matumizi ya ardhi yasiyo rasmi, mabadiliko ya tabia nchi yanayoongeza shinikizo kwa ardhi na rasilimali zake na ukuaji wa haraka wa miji unaohitaji mipango bunifu na matumizi bora ya ardhi.
Katika kukabiliana na changamoto hizo, Mhe Dkt Akwilapo amesema, Serikali inategemea utaalamu na ushauri wa Kamati ya Ufundi ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi katika kuhakikisha ardhi inatumika kwa tija, usawa, usalama na uendelevu.
"Ninaamini ushauri wa Kamati utakuwa mhimili wa kuimarisha Sera, miongozi na taratibu zinazohusu matumizi ya ardhi nchini". Amesema Mhe. Dkt Akwilapo
"Niielekeze Tume kuwa makini kusaidia kamati kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi. Muwasidie ili waweze kutekeleza majukumu ili kusiwe na migongano mbele ya safari". Amesema.
Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhandisi Anthony Sanga Amesema, wizara yake ina imani kubwa na kazi za Tume ya Taifa ya Matumizi ya Ardhi kutokana na kuisaidia wizara na hasa katika maeneo ya migogoro ya vijijni ikiwemo ya wakulima na wafugaji.
"Nikiri kuwa migogoro ya wakulima na wafugaji imepungua sana tofauti na ilivyokuwa miaka ya zamani maana tulikuwa na kesi nyingi za hii migogoro lakini kwa kiasi kikubwa imepungua".Amesema.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi (NLUPC) Bw. Joseph Mafuru amesema,Tume yake itahakikisha kamati inatekeleza majukumu yake kwa weledi huku akiamini wajumbe walioteuliwa wataziwakilisha vyema taasisi walizotoka kwa kutekeleza kikamilifu majukumu ya Kamati.
"Katika kipindi chote ambacho Tume imekuwa bila Kamati, tumekosa mambo kadhaa muhimu kama vile fursa ya kupata ushauri wa kitaalamu unaotekelezwa kimfumo na kitaalamu katika sekta zote kuhusiana na matumizi ya ardhi kuanzia kilimo, mifugo, misitu, utalii, ujenzi, uwekezaji na nyinginezo ikiwemo tafiti". Amesema
Kwa mujibu wa Bw. Mafuru, mambo mengine ni kukosekana kwa mkakati wa pamoja wa utanzaji wa migogoro ya ardhi, upungufu wa takwimu za pamoja, pengo la uratibu wa taasisi pamoja na upungufu wa viwango vya kitaifa vya mipango.





WAZIRI AKWILAPO AAGIZA KUONGEZWA KWA KASI YA KUPANGA NA KUPIMA ARDHI NCHINI

Na Munir Shemweta, WANMM
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo ameiagiza Tume ya Taifa ya Matumizi ya Ardhi kuongeza kasi ya kupanga na kupima ardhi katika maeneo mbalimbali nchini ikiwemo miradi ya kilimo, makazi na uwekezaji.
Mhe. Dkt Leonard Akwilapo amesema hayo leo tarehe 17 Desemba 2025 wakati akifungua Kikao Kazi cha Kamati ya Ufundi ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi kilichofanyika Makao Makuu ya Wizara jijini Dodoma.
Kupitia kikao hicho, Mhe. Dkt Akwilapo amehimiza kukuzwa kwa matumizi ya teknolojia katika ukusanyaji takwimu za kupanga ardhi, kulinda maeneo nyeti ya ikolojia, misitu, vyanzo vya maji, njia za wanyama pori pamoja na kujenga ustahimilivu wa mabadiliko ya tabia nchi kupitia mipango shirikishi na endelevu,
Amesema,Tanzania inakabiliwa na changamoto zinazohusiana na matumizi ya ardhi na kuzitaja kuwa ni pamoja na migongano kati ya shughuli za kilimo na ufugaji, malisho na uhifadhi na upungufu wa maeneo ya uwekezaji wa kimkakati kutokana na mabadiliko ya matumizi ya ardhi yasiyopangwa.
Changamoto nyingine ni uharibifu wa mazingira unaosababishwa na uvamizi wa vyanzo vya maji, ukataji miti hovyo, matumizi ya ardhi yasiyo rasmi, mabadiliko ya tabia nchi yanayoongeza shinikizo kwa ardhi na rasilimali zake na ukuaji wa haraka wa miji unaohitaji mipango bunifu na matumizi bora ya ardhi.
Katika kukabiliana na changamoto hizo, Mhe Dkt Akwilapo amesema, Serikali inategemea utaalamu na ushauri wa Kamati ya Ufundi ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi katika kuhakikisha ardhi inatumika kwa tija, usawa, usalama na uendelevu.
"Ninaamini ushauri wa Kamati utakuwa mhimili wa kuimarisha Sera, miongozi na taratibu zinazohusu matumizi ya ardhi nchini". Amesema Mhe. Dkt Akwilapo
"Niielekeze Tume kuwa makini kusaidia kamati kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi. Muwasidie ili waweze kutekeleza majukumu ili kusiwe na migongano mbele ya safari". Amesema.
Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhandisi Anthony Sanga Amesema, wizara yake ina imani kubwa na kazi za Tume ya Taifa ya Matumizi ya Ardhi kutokana na kuisaidia wizara na hasa katika maeneo ya migogoro ya vijijni ikiwemo ya wakulima na wafugaji.
"Nikiri kuwa migogoro ya wakulima na wafugaji imepungua sana tofauti na ilivyokuwa miaka ya zamani maana tulikuwa na kesi nyingi za hii migogoro lakini kwa kiasi kikubwa imepungua".Amesema.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi (NLUPC) Bw. Joseph Mafuru amesema,Tume yake itahakikisha kamati inatekeleza majukumu yake kwa weledi huku akiamini wajumbe walioteuliwa wataziwakilisha vyema taasisi walizotoka kwa kutekeleza kikamilifu majukumu ya Kamati.
"Katika kipindi chote ambacho Tume imekuwa bila Kamati, tumekosa mambo kadhaa muhimu kama vile fursa ya kupata ushauri wa kitaalamu unaotekelezwa kimfumo na kitaalamu katika sekta zote kuhusiana na matumizi ya ardhi kuanzia kilimo, mifugo, misitu, utalii, ujenzi, uwekezaji na nyinginezo ikiwemo tafiti". Amesema
Kwa mujibu wa Bw. Mafuru, mambo mengine ni kukosekana kwa mkakati wa pamoja wa utanzaji wa migogoro ya ardhi, upungufu wa takwimu za pamoja, pengo la uratibu wa taasisi pamoja na upungufu wa viwango vya kitaifa vya mipango.






Labels:
KITAIFA
November 30, 2025

WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameliagiza Jeshi la Polisi liache kumtafuta Askofu Dkt. Josephat Gwajima kama walivyokuwa wametangaza awali ili aweze kuendelea shughuli zake.
Amesema baada ya kutoa msamaha kwa Kanisa la Ufufuo na Uzima, waumini wanahitaji wamuone kiongozi wao, hivyo anatakiwa ajitokeze hadharani aendelee na kazi yake. “Mwacheni ajitokekeze tujenge umoja wa kitaifa, tushikamane kurudisha umoja wa kitaifa. Tumekutana na TEC, viongozi wa dini, wa mila na viongozi mbalimbali; twendeni sote kwenye jambo hili, tujitokeze tuhamasishe Tanzania yenye amani, huu ndio wito wa kiongozi wetu wa nchi”
Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumapili, Novemba 30, 2025) wakati akizungumza na mamia ya wakazi wa Arumeru katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Magufuli Leganga, kata ya Usa River, wilayani Arumeru mkoani Arusha.
Waziri Mkuu amewataka Watanzania wakatae kushawishiwa na wanaharakati wanaochochea vurugu kwani zinarudisha nyuma maendeleo ya nchi. "Nimekuja kuwapa pole wananchi wenzangu, kwa niaba ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan. Anatambua mambo yanayoendelea. Anatambua kazi kubwa ya kujenga Taifa mnayoifanya," amesema.
Kabla ya mkutano huo, Waziri Mkuu alikagua uharibifu uliofanywa wakati wa vurugu za Oktoba 29, mwaka huu kwenye kituo cha polisi cha Kikatiti (mita 500 kutoka barabara kuu ya Arusha - Moshi); Mahakama ya Mwanzo ya Maji ya Chai (km. 3 kutoka barabara hiyo kuu); kituo cha mafuta Total Energies kilichopo Maji ya Chai (kipo barabarani) ambavyo vyote vilichomwa moto ikiwemo kuiba mali kwenye supermarket na kubomoa sefu ya kutunzia fedha.
Waziri Mkuu amesema masuala ya maendeleo ya wilaya ya hiyo kama vile maji na barabara yamo kwenye Ilani ya CCM na kwenye ahadi za Mheshimiwa Rais lakini yatafanyika endapo tu nchi itakuwa na amani. “Tukichagua vurugu tutakuwa tumechagua kufukuza maendeleo, tukichagua vurugu tutakuwa tumechagua kuongeza umaskini kwa mtu mmoja mmoja," ameonya.
"Kila Mtanzania akatae haya yaliyotokea juzijuzi. Tumechochewa, tumechonganishwa lakini wao wako nje, wanalipwa ili kutuvuruga tu. Wengi wanaochochea vurugu ni wanaharakati, wako nje ya nchi. Hakuna kiongozi wa chama cha siasa anasema wananchi wafanye vurugu. Au mmemuona?" alihoji.
Amesema baadhi ya vijana walioko nje ya nchi wamebainika kupokea dola za Marekani milioni mbili (sawa na sh. bilioni 4.5) ili wachochee vurugu. “Hawa wanaowalipa, wana maslahi gani na nchi yetu? Wana ajenda gani na nchi yetu? Tunajua watazirudishaje hizo fedha?”
“Hawa watu wanalenga tugombane ili wachukue madini adimu (rare earth minerals). Sasa hivi Tanzania imegundua uranium ambapo inakuwa nchi ya tisa duniani na ya kwanza barani Afrika. Ina tani za ujazo 890,000. Hii ni karibu tani milioni moja."
Waziri Mkuu ameonya dhidi ya mchezo unaotumika kuanzisha chokochoko ili kusambaratisha nchi pindi inapobainika kuwa na rasilimali. Amesema ziko baadhi ya nchi barani Afrika ziliathirika kutoka na chokochoko hizo. “Wanaanzisha chokochoko, wanaacha mnavurugana, rasilmali zikiisha, wao wanaondoka,” amesisitiza.
"Watanzania tuamkeni, tuchukue tahadhari. Kuna kamchezo kanachezwa. Wanajua Tanzania ina gesi asilia nyingi na inakaribia kuanza. Wanajua ikianza miradi hii, Tanzania itakuwa ya kwanza katika Afrika Mashariki na wala hatutahitaji kutoa mikopo ya wanafunzi."
Amewataka Watanzania waamke na kukataa kurudishwa tena kwenye hali ya vurugu. "Watanzania tuamke, tukatae kurejeshwa kule nyuma. Umaskini utaondolewa nchi ikiwa kwenye amani. Ajira za vijana zitaweza kupatikana nchi ikiwa kwenye amani."
Amesisitiza kuwa vurugu zikiwepo, hata wakulima wa karoti na nyanya wa Ngarenanyuki hazitauzwa na hivyo kuathiri uchumi wa mtu binafsi.





RAIS SAMIA: POLISI WAACHE KUMTAFUTA DKT. GWAJIMA
Written By CCMdijitali on Sunday, November 30, 2025 | November 30, 2025

WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameliagiza Jeshi la Polisi liache kumtafuta Askofu Dkt. Josephat Gwajima kama walivyokuwa wametangaza awali ili aweze kuendelea shughuli zake.
Amesema baada ya kutoa msamaha kwa Kanisa la Ufufuo na Uzima, waumini wanahitaji wamuone kiongozi wao, hivyo anatakiwa ajitokeze hadharani aendelee na kazi yake. “Mwacheni ajitokekeze tujenge umoja wa kitaifa, tushikamane kurudisha umoja wa kitaifa. Tumekutana na TEC, viongozi wa dini, wa mila na viongozi mbalimbali; twendeni sote kwenye jambo hili, tujitokeze tuhamasishe Tanzania yenye amani, huu ndio wito wa kiongozi wetu wa nchi”
Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumapili, Novemba 30, 2025) wakati akizungumza na mamia ya wakazi wa Arumeru katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Magufuli Leganga, kata ya Usa River, wilayani Arumeru mkoani Arusha.
Waziri Mkuu amewataka Watanzania wakatae kushawishiwa na wanaharakati wanaochochea vurugu kwani zinarudisha nyuma maendeleo ya nchi. "Nimekuja kuwapa pole wananchi wenzangu, kwa niaba ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan. Anatambua mambo yanayoendelea. Anatambua kazi kubwa ya kujenga Taifa mnayoifanya," amesema.
Kabla ya mkutano huo, Waziri Mkuu alikagua uharibifu uliofanywa wakati wa vurugu za Oktoba 29, mwaka huu kwenye kituo cha polisi cha Kikatiti (mita 500 kutoka barabara kuu ya Arusha - Moshi); Mahakama ya Mwanzo ya Maji ya Chai (km. 3 kutoka barabara hiyo kuu); kituo cha mafuta Total Energies kilichopo Maji ya Chai (kipo barabarani) ambavyo vyote vilichomwa moto ikiwemo kuiba mali kwenye supermarket na kubomoa sefu ya kutunzia fedha.
Waziri Mkuu amesema masuala ya maendeleo ya wilaya ya hiyo kama vile maji na barabara yamo kwenye Ilani ya CCM na kwenye ahadi za Mheshimiwa Rais lakini yatafanyika endapo tu nchi itakuwa na amani. “Tukichagua vurugu tutakuwa tumechagua kufukuza maendeleo, tukichagua vurugu tutakuwa tumechagua kuongeza umaskini kwa mtu mmoja mmoja," ameonya.
"Kila Mtanzania akatae haya yaliyotokea juzijuzi. Tumechochewa, tumechonganishwa lakini wao wako nje, wanalipwa ili kutuvuruga tu. Wengi wanaochochea vurugu ni wanaharakati, wako nje ya nchi. Hakuna kiongozi wa chama cha siasa anasema wananchi wafanye vurugu. Au mmemuona?" alihoji.
Amesema baadhi ya vijana walioko nje ya nchi wamebainika kupokea dola za Marekani milioni mbili (sawa na sh. bilioni 4.5) ili wachochee vurugu. “Hawa wanaowalipa, wana maslahi gani na nchi yetu? Wana ajenda gani na nchi yetu? Tunajua watazirudishaje hizo fedha?”
“Hawa watu wanalenga tugombane ili wachukue madini adimu (rare earth minerals). Sasa hivi Tanzania imegundua uranium ambapo inakuwa nchi ya tisa duniani na ya kwanza barani Afrika. Ina tani za ujazo 890,000. Hii ni karibu tani milioni moja."
Waziri Mkuu ameonya dhidi ya mchezo unaotumika kuanzisha chokochoko ili kusambaratisha nchi pindi inapobainika kuwa na rasilimali. Amesema ziko baadhi ya nchi barani Afrika ziliathirika kutoka na chokochoko hizo. “Wanaanzisha chokochoko, wanaacha mnavurugana, rasilmali zikiisha, wao wanaondoka,” amesisitiza.
"Watanzania tuamkeni, tuchukue tahadhari. Kuna kamchezo kanachezwa. Wanajua Tanzania ina gesi asilia nyingi na inakaribia kuanza. Wanajua ikianza miradi hii, Tanzania itakuwa ya kwanza katika Afrika Mashariki na wala hatutahitaji kutoa mikopo ya wanafunzi."
Amewataka Watanzania waamke na kukataa kurudishwa tena kwenye hali ya vurugu. "Watanzania tuamke, tukatae kurejeshwa kule nyuma. Umaskini utaondolewa nchi ikiwa kwenye amani. Ajira za vijana zitaweza kupatikana nchi ikiwa kwenye amani."
Amesisitiza kuwa vurugu zikiwepo, hata wakulima wa karoti na nyanya wa Ngarenanyuki hazitauzwa na hivyo kuathiri uchumi wa mtu binafsi.






Labels:
KITAIFA
November 26, 2025
“Yeyote atakayevunja sheria akamatwe na hatua zichukuliwe kwa usawa. Huyu mmoja anavunja sheria anakamatwa, analipa. Huyu mwingine anavunja mbele yake anaachwa. Kama una haraka, toka mapema zaidi si kufidia kwa kuvunja sheria.”
Ametoa kauli hiyo leo (Jumatano, Novemba 26, 2025) wakati akifungua Maadhimisho ya Kimataifa ya Wiki ya Usafiri Endelevu Ardhini katika ukumbi wa Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.
Amesema kuwa haitakuwa uungwana kuona baadhi ya watu wakilipa adhabu papo hapo wanapokosea ilhali wengine wakiachwa kupita bila kuchukuliwa hatua.
Amewaonya baadhi ya viongozi na madereva wa Serikali ambao wanaelewa sheria vizuri lakini bado wanazikiuka kwa makusudi. “Ni muhimu kuwasaidia watumiaji wa vyombo vya usafiri kama bodaboda na bajaji ambao kwa sehemu kubwa wanaweza kuwa hawazielewi sheria kikamilifu, badala ya kuwaadhibu kwa upendeleo.”
Dkt. Mwigulu amesisitiza umuhimu wa kuwapa Watanzania wote heshima na kuhakikisha sheria zilizowekwa zinatekelezwa kwa maslahi ya wote na kuongeza kuwa endapo zipo sheria ngumu kutekelezeka, basi zibadilishwe ili kila Mtanzania anufaike.
Ameviagiza vyombo vya usimamizi wa sheria vihakikishe kuwa watumiaji wote wa vyombo vya usafiri wanazingatia usimamizi wa sheria na kuchukua hatua kwa yoyote anayevunja sheria akamatwe na kuchukuliwa hatua bila kuonewa aibu.
“Inaudhi mtu amebeba mgonjwa anafuata sheria, halafu mwingine anapita tu anavunja sheria, hapati adhabu. Mlalahoi akivunja sheria anapata adhabu, tunawapa kazi watekeleza sheria kuwaomba radhi watu waliovunja sheria. Naelekeza kila mtu afuate sheria, uwe wa serikalini ama uwe binafsi, tumeweka sheria, zifuatwe kama zilivyo.”
Mapema, akimkaribisha Waziri Mkuu kuzungumza na washiriki wa maadhimisho hayo, Waziri wa Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa alisema sekta ya uchukuzi ni mojawapo ya sekta wezeshi za uchumi duniani kota na kwamba watu wanahitaji njia za uchukuzi ili kusafiri kutoka sehemu moja kwenda nyingine.
Alisema wizara yake itaendelea kushirikiana na wadau wa usafirishaji nchini ili kuhakikisha masuala ya nishati safi yanapewa kipaumbele. Akitoa mfano, Waziri Mbarawa alisema: “Uendeshaji wa reli ya kisasa (SGR) unatumia nishati ya umeme, mabasi ya mwendokasi njia ya Mbagala yanatumia gesi asili na baadhi ya taxi na bajaji zinatumia gesi asili.”

DKT. MWIGULU AWAONYA WAVUNJIFU WA SHERIA
Written By CCMdijitali on Wednesday, November 26, 2025 | November 26, 2025
WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amevitaka vyombo vinavyosimamia usalama barabarani vitekeleze sheria hizo bila upendeleo kwani tabia ya kuogopana na kuoneana aibu imechangia baadhi ya watu kukwepa wajibu wakati wengine wakibebeshwa mzigo wa sheria.
“Yeyote atakayevunja sheria akamatwe na hatua zichukuliwe kwa usawa. Huyu mmoja anavunja sheria anakamatwa, analipa. Huyu mwingine anavunja mbele yake anaachwa. Kama una haraka, toka mapema zaidi si kufidia kwa kuvunja sheria.”
Ametoa kauli hiyo leo (Jumatano, Novemba 26, 2025) wakati akifungua Maadhimisho ya Kimataifa ya Wiki ya Usafiri Endelevu Ardhini katika ukumbi wa Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.
Amesema kuwa haitakuwa uungwana kuona baadhi ya watu wakilipa adhabu papo hapo wanapokosea ilhali wengine wakiachwa kupita bila kuchukuliwa hatua.
Amewaonya baadhi ya viongozi na madereva wa Serikali ambao wanaelewa sheria vizuri lakini bado wanazikiuka kwa makusudi. “Ni muhimu kuwasaidia watumiaji wa vyombo vya usafiri kama bodaboda na bajaji ambao kwa sehemu kubwa wanaweza kuwa hawazielewi sheria kikamilifu, badala ya kuwaadhibu kwa upendeleo.”
Dkt. Mwigulu amesisitiza umuhimu wa kuwapa Watanzania wote heshima na kuhakikisha sheria zilizowekwa zinatekelezwa kwa maslahi ya wote na kuongeza kuwa endapo zipo sheria ngumu kutekelezeka, basi zibadilishwe ili kila Mtanzania anufaike.
Ameviagiza vyombo vya usimamizi wa sheria vihakikishe kuwa watumiaji wote wa vyombo vya usafiri wanazingatia usimamizi wa sheria na kuchukua hatua kwa yoyote anayevunja sheria akamatwe na kuchukuliwa hatua bila kuonewa aibu.
“Inaudhi mtu amebeba mgonjwa anafuata sheria, halafu mwingine anapita tu anavunja sheria, hapati adhabu. Mlalahoi akivunja sheria anapata adhabu, tunawapa kazi watekeleza sheria kuwaomba radhi watu waliovunja sheria. Naelekeza kila mtu afuate sheria, uwe wa serikalini ama uwe binafsi, tumeweka sheria, zifuatwe kama zilivyo.”
Mapema, akimkaribisha Waziri Mkuu kuzungumza na washiriki wa maadhimisho hayo, Waziri wa Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa alisema sekta ya uchukuzi ni mojawapo ya sekta wezeshi za uchumi duniani kota na kwamba watu wanahitaji njia za uchukuzi ili kusafiri kutoka sehemu moja kwenda nyingine.
Alisema wizara yake itaendelea kushirikiana na wadau wa usafirishaji nchini ili kuhakikisha masuala ya nishati safi yanapewa kipaumbele. Akitoa mfano, Waziri Mbarawa alisema: “Uendeshaji wa reli ya kisasa (SGR) unatumia nishati ya umeme, mabasi ya mwendokasi njia ya Mbagala yanatumia gesi asili na baadhi ya taxi na bajaji zinatumia gesi asili.”


Labels:
KITAIFA
November 15, 2025
Pia, Waziri Mkuu ameiagiza Wizaya ya Afya, Bohari ya Dawa (MSD) na Hospitali zote nchini ziweke vipaumbele vya kuwa na dawa kulingana na mahitaji ya eneo husika. “ Haipendezi mwananchi kufika hospitali na kupatiwa vipimo vyote kisha anaambiwa dawa akanunue kwingine, kama duka binafsi linaweza kupata dawa hizo, inawezekanaje hospitali za serikali hapati? Naagiza Hospitali zote ziwe na dawa.”
Ametoa maagizo hayo wakati akizungumza na wananchi nje ya hospitali hiyo baada ya kutembelea wananchi waliofika hospitalini hapo kupata huduma mbalimbali za kitabibu ambapo amesisitiza wananchi waendelee kuhudumiwa vizuri kwa kuwa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa fedha nyingi kwa ajili ya kuboresha huduma za afya nchini vikiwemo vifaa tiba na dawa.
Kadhalika Mheshimiwa Waziri Mkuu ameziagiza hospitali zote nchini zihakikishe zinakuwa na vifaa vya usafi binafsi vya dharura vikiwemo ndoo na beseni katika wodi za wazazi ili viwasaidie akinamama wasiokuwa na vifaa hivyo. “Ujauzito sio suala la dharura vifaa kama ndoo tunapaswa kuwa navyo katika hospitali zetu za serikali.”
Dkt. Mwigulu ametumia fursa hiyo kumpongeza Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayoifanya katika uboreshaji wa huduma za afya nchini. Waziri Mkuu akiwa hospitalini hapo, wananchi walimueleza kuwa wanahudumiwa vizuri na kwa uangalizi wa karibu.
Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu ameziagiza hospitali zote nchini zizingatie maelekezo ya kutumia mifumo sahihi ya malipo katika taratibu za kutoa huduma ili kuwezesha Serikali kuendelea kuhudumia wananchi.
Dkt. Mwigulu ametoa agizo hilo kufuatia kuwepo kwa hospitali ambazo baadhi ya huduma wanapokea malipo kwa njia ya mtandao na nyingine malipo yanapokelewa malipo kwa njia zisizo rasmi.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti wagonjwa na wananchi wanaoguza ndugu zao wamempongeza Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuhakikisha wananchi wanapatiwa huduma bora za afya.
“Tunamshukuru Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwa tunapatiwa huduma nzuri kama tupo hospitali za private (binafsi).” Kauli hiyo imetolewa na Dinna Enock, mkazi wa Makulu jijini Dodoma ambaye amelazwa katika wodi ya wazazi.
WAZIRI MKUU AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA MKOA WA DODOMA
Written By CCMdijitali on Saturday, November 15, 2025 | November 15, 2025
- Atoa maagizo kwa Wizara ya Afya, MSD na hospitali zote nchini.
- Ataka wajawazito wasisubirishwe mapokezi wanapofika hospitali
- Wagojwa waipongeza Srtikali kwa kuboresha huduma za afya
WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Novemba 15, 2025 amefanya ziara ya kushtukiza katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma na kuziagiza hospitali zote nchini zihakikishe wajawazito wanapofika hospitali wahudumiwe kwa haraka ili kuokoa maisha ya mama na mtoto.
Pia, Waziri Mkuu ameiagiza Wizaya ya Afya, Bohari ya Dawa (MSD) na Hospitali zote nchini ziweke vipaumbele vya kuwa na dawa kulingana na mahitaji ya eneo husika. “ Haipendezi mwananchi kufika hospitali na kupatiwa vipimo vyote kisha anaambiwa dawa akanunue kwingine, kama duka binafsi linaweza kupata dawa hizo, inawezekanaje hospitali za serikali hapati? Naagiza Hospitali zote ziwe na dawa.”
Ametoa maagizo hayo wakati akizungumza na wananchi nje ya hospitali hiyo baada ya kutembelea wananchi waliofika hospitalini hapo kupata huduma mbalimbali za kitabibu ambapo amesisitiza wananchi waendelee kuhudumiwa vizuri kwa kuwa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa fedha nyingi kwa ajili ya kuboresha huduma za afya nchini vikiwemo vifaa tiba na dawa.
Kadhalika Mheshimiwa Waziri Mkuu ameziagiza hospitali zote nchini zihakikishe zinakuwa na vifaa vya usafi binafsi vya dharura vikiwemo ndoo na beseni katika wodi za wazazi ili viwasaidie akinamama wasiokuwa na vifaa hivyo. “Ujauzito sio suala la dharura vifaa kama ndoo tunapaswa kuwa navyo katika hospitali zetu za serikali.”
Dkt. Mwigulu ametumia fursa hiyo kumpongeza Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayoifanya katika uboreshaji wa huduma za afya nchini. Waziri Mkuu akiwa hospitalini hapo, wananchi walimueleza kuwa wanahudumiwa vizuri na kwa uangalizi wa karibu.
Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu ameziagiza hospitali zote nchini zizingatie maelekezo ya kutumia mifumo sahihi ya malipo katika taratibu za kutoa huduma ili kuwezesha Serikali kuendelea kuhudumia wananchi.
Dkt. Mwigulu ametoa agizo hilo kufuatia kuwepo kwa hospitali ambazo baadhi ya huduma wanapokea malipo kwa njia ya mtandao na nyingine malipo yanapokelewa malipo kwa njia zisizo rasmi.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti wagonjwa na wananchi wanaoguza ndugu zao wamempongeza Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuhakikisha wananchi wanapatiwa huduma bora za afya.
“Tunamshukuru Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwa tunapatiwa huduma nzuri kama tupo hospitali za private (binafsi).” Kauli hiyo imetolewa na Dinna Enock, mkazi wa Makulu jijini Dodoma ambaye amelazwa katika wodi ya wazazi.

Labels:
KITAIFA
October 21, 2025
DKT. SAMIA: NIWAHAKIKISHIE, MAANDAMANO PEKEE YA OKT. 29 NI KUPIGA KURA
Written By CCMdijitali on Tuesday, October 21, 2025 | October 21, 2025
𝗗𝗞𝗧. 𝗦𝗔𝗠𝗜𝗔 𝗞𝗨𝗘𝗡𝗗𝗘𝗟𝗘𝗔 𝗞𝗨𝗜𝗙𝗨𝗡𝗚𝗨𝗔 𝗗𝗔𝗥 𝗘𝗦 𝗦𝗔𝗟𝗔𝗔𝗠 𝗞𝗪𝗘𝗡𝗬𝗘 𝗠𝗜𝗨𝗡𝗗𝗢𝗠𝗕𝗜𝗡𝗨 𝗬𝗔 𝗕𝗔𝗥𝗔𝗕𝗔𝗥𝗔 𝗡𝗔 𝗠𝗔𝗗𝗔𝗥𝗔𝗝𝗔
𝙈𝙧𝙖𝙙𝙞 𝙬𝙖 𝘿𝙈𝘿𝙋 𝙠𝙪𝙢𝙖𝙡𝙞𝙯𝙖 𝙘𝙝𝙖𝙣𝙜𝙖𝙢𝙤𝙩𝙤 𝙮𝙖 𝙢𝙖𝙛𝙪𝙧𝙞𝙠𝙤 𝘿𝙨𝙢.
Mgombea nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Rais Dkt. 𝗦𝗮𝗺𝗶𝗮 𝗦𝘂𝗹𝘂𝗵𝘂 𝗛𝗮𝘀𝘀𝗮𝗻 amesema kuwa akipata ridhaa ya kuongoza tena nchi kwa miaka mitano ijayo, atahakikisha Serikali yake itajenga barabara za makutano (fly over) katika barabara za Morocco, Mwenge, Magomeni, barabara ya Ali Hassan Mwinyi na Umoja wa Mataifa.
Dkt. Samia amesema sababu ya ujenzi huo ni kupunguza msongamano na kukuza shughuli za biashara katika maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam ambapo zitaongeza tija katika ukuaji wa uchumi endelevu wenye kumgusa Mtanzania mmoja mmoja.
Akizungumza mbele ya kadamnasi ya wananchi wa Kinondoni na Ubungo alipokuwa akinadi Ilani ya Uchaguzi ya CCM (2025/30), sera na Ahadi zake katika viwanja vya Leaders Club, amesema atayakamilisha hayo pale ambapo wananchi watakwenda sambamba na kuchagau mafiga matatu kwa maana ya Rais kutoka CCM, Wabunge na Madiwani ili kuondoa makandokando katika kutekeleza majukumu hayo.
Pia, Mgombea Urais Dkt. Samia, ameahidi kujenga barabara ya Kimara - Mavurunza - Bonyokwa inayopita kwenye majimbo matatu ya Segerea, Ubungo na Kibamba yenye urefu wa kilomita 7 kwa kiwango cha lami huku akiongeza kuwa Serikali yake itatenga bajeti ili kujenga barabara nyingine muhimu kwa maendeleo ya wilaya zote zilizipo ndani ya Jiji la Dar es salaam.
Aidha, Dkt. Samia ameahidi kufanya utanuzi wa barabara ya Mwaikibaki yenye kilomita 9 kutoka Morocco - Kawe hadi Garden road pamoja na barabara ya Tegeta hadi Bagamoyo yenye urefu wa kilomita 57, Kibamba hadi Mloganzila yenye urefu wa kilomita 8.
Akigusia suala la changamoto ya mafuriko kwa baadhi ya maeno ya Jiji la Dar es salaam, Dkt. Samia amehaidi kuondoa changamoto hiyo katika kipindi cha mvua kwa maeneo mbalimbali ikiwemo yanayopakana na mto Gide, mto Mbezi na mto China akieleza kuwa changamoto hiyo itatatuliwa kupitia mradi wa pili wa uendelezaji wa Jiji la Dar es Salaam (DMDP)
𝗛𝗔𝗞𝗨𝗡𝗔 𝗧𝗜𝗦𝗛𝗜𝗢 𝗟𝗔 𝗨𝗦𝗔𝗟𝗔𝗠𝗔 𝗟𝗜𝗧𝗔𝗞𝗔𝗟𝗢𝗞𝗨𝗪𝗘𝗣𝗢, 𝗡𝗘𝗡𝗗𝗘𝗡𝗜 𝗠𝗞𝗔𝗣𝗜𝗚𝗘 𝗞𝗨𝗥𝗔 - 𝗗𝗞𝗧. 𝗦𝗔𝗠𝗜𝗔
𝙈𝙖𝙩𝙪𝙨𝙞 𝙣𝙞𝙖𝙘𝙝𝙞𝙚𝙣𝙞 𝙢𝙞𝙢𝙞, 𝙣𝙞𝙣𝙖𝙮𝙖𝙗𝙚𝙗𝙖 𝙠𝙬𝙖 𝙣𝙞𝙖𝙗𝙖 𝙮𝙚𝙣𝙪.
"Ninayeongea hapa ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa nchi hii, ninataka niwaambie, maandamano yatakayokuwepo ni ya watu kwenda vituoni kupiga kura, hakuna maandamano mengine yatakayokuwepo hapa.."
"Niwaombe ndugu zangu, twendeni mkapige kura, twendeni mkapige kura... Ndugu zangu mengine niachieni mimi, matusi niachieni mimi, ninayabeba kwa niaba yenu"
"Niliapa kuwa Rais wa Tanzania, niliapa kuilinda Nchi hii kwa kudumisha Amani, Umoja na Mshikamano wetu"
Hayo yamesemwa na Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. 𝗦𝗮𝗺𝗶𝗮 𝗦𝘂𝗹𝘂𝗵𝘂 𝗛𝗮𝘀𝘀𝗮𝗻 wakati akizungumza kwenye Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni Jijini Dar es Salaam katika mkutano wa hadhara wa kampeni za Uchaguzi Mkuu uliofanyika leo tarehe 21 Oktoba 2025.
𝘾𝙃𝘼𝙂𝙐𝘼 𝙎𝘼𝙈𝙄𝘼, 𝘾𝙃𝘼𝙂𝙐𝘼 𝘾𝘾𝙈
"Katika miaka mitano inayokuja, tutaendelea kukamilisha utekelezaji wa miradi ya Bwawa la Kidunda lenye thamani ya Shilingi bilioni 336, na bwawa hili la Kidunda litakwenda kuhudumia mikoa ya Dar es Salaam, Pwani na Morogoro. Lakini mradi wa pili tunaokwenda kuufanya ili kuondoa uhaba wa maji Dar es Salaam hasa wakati wa kiangazi, ni mradi mkubwa wa kutoa maji mto Rufiji ambao kazi ya upembuzi yakinifu na utafiti wa kina tayari tumekwishaianza na awamu hii tunakwenda kufanya utekelezaji ili Dar es Salaam ipate maji kutoka Kidunda, Ruvu na Mto Rufiji kuondoa kabisa kadhia ya uhaba wa maji", - Dkt. Samia.
Mgombea wa nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza kwenye Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni Jijini Dar es Salaam katika mkutano wa hadhara wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 21, 2025.
Mgombea wa nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza kwenye Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni Jijini Dar es Salaam katika mkutano wa hadhara wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 21, 2025.
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema kuwa serikali yake itakwenda kusimamia na kukamilisha mradi wa miundombinu ya barabara ya mabasi yaendayo haraka maarufu kama mwendokasi, hiyo itafanyika ikiwa atachaguliwa kuiongoza nchi kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.
Dkt. Samia ameyasema hayo akizungumza kwenye Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni Jijini Dar es Salaam katika mkutano wa hadhara wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 21, 2025 ambapo amesisitiza kuwa utoaji wa huduma ya usafiri na usafirishaji kupitia miundombinu hizo zitakapokamilika, utajikita zaidi kwenye sekta binafsi.
"Tukapomaliza barabara zote, ni fursa muhimu kwa sekta binafsi kupata kazi ya kubeba abiria na kurudisha, kazi hiyo kwa kiasi hatutaki kuifanya sisi serikali bali sekta binafsi wataingiza mabasi yao na wafanye uendeshaji wa shughuli hizo", ameeleza Dkt. Samia.
Amewaahidi wakazi wa Dar es Salaam kuwa kuanzia Januari, 2026 kutakuwa na mageuzi makubwa ya utoaji wa huduma ya miundombinu ya mwendokasi.

𝙈𝙧𝙖𝙙𝙞 𝙬𝙖 𝘿𝙈𝘿𝙋 𝙠𝙪𝙢𝙖𝙡𝙞𝙯𝙖 𝙘𝙝𝙖𝙣𝙜𝙖𝙢𝙤𝙩𝙤 𝙮𝙖 𝙢𝙖𝙛𝙪𝙧𝙞𝙠𝙤 𝘿𝙨𝙢.
Mgombea nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Rais Dkt. 𝗦𝗮𝗺𝗶𝗮 𝗦𝘂𝗹𝘂𝗵𝘂 𝗛𝗮𝘀𝘀𝗮𝗻 amesema kuwa akipata ridhaa ya kuongoza tena nchi kwa miaka mitano ijayo, atahakikisha Serikali yake itajenga barabara za makutano (fly over) katika barabara za Morocco, Mwenge, Magomeni, barabara ya Ali Hassan Mwinyi na Umoja wa Mataifa.
Dkt. Samia amesema sababu ya ujenzi huo ni kupunguza msongamano na kukuza shughuli za biashara katika maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam ambapo zitaongeza tija katika ukuaji wa uchumi endelevu wenye kumgusa Mtanzania mmoja mmoja.
Akizungumza mbele ya kadamnasi ya wananchi wa Kinondoni na Ubungo alipokuwa akinadi Ilani ya Uchaguzi ya CCM (2025/30), sera na Ahadi zake katika viwanja vya Leaders Club, amesema atayakamilisha hayo pale ambapo wananchi watakwenda sambamba na kuchagau mafiga matatu kwa maana ya Rais kutoka CCM, Wabunge na Madiwani ili kuondoa makandokando katika kutekeleza majukumu hayo.
Pia, Mgombea Urais Dkt. Samia, ameahidi kujenga barabara ya Kimara - Mavurunza - Bonyokwa inayopita kwenye majimbo matatu ya Segerea, Ubungo na Kibamba yenye urefu wa kilomita 7 kwa kiwango cha lami huku akiongeza kuwa Serikali yake itatenga bajeti ili kujenga barabara nyingine muhimu kwa maendeleo ya wilaya zote zilizipo ndani ya Jiji la Dar es salaam.
Aidha, Dkt. Samia ameahidi kufanya utanuzi wa barabara ya Mwaikibaki yenye kilomita 9 kutoka Morocco - Kawe hadi Garden road pamoja na barabara ya Tegeta hadi Bagamoyo yenye urefu wa kilomita 57, Kibamba hadi Mloganzila yenye urefu wa kilomita 8.
Akigusia suala la changamoto ya mafuriko kwa baadhi ya maeno ya Jiji la Dar es salaam, Dkt. Samia amehaidi kuondoa changamoto hiyo katika kipindi cha mvua kwa maeneo mbalimbali ikiwemo yanayopakana na mto Gide, mto Mbezi na mto China akieleza kuwa changamoto hiyo itatatuliwa kupitia mradi wa pili wa uendelezaji wa Jiji la Dar es Salaam (DMDP)
𝗛𝗔𝗞𝗨𝗡𝗔 𝗧𝗜𝗦𝗛𝗜𝗢 𝗟𝗔 𝗨𝗦𝗔𝗟𝗔𝗠𝗔 𝗟𝗜𝗧𝗔𝗞𝗔𝗟𝗢𝗞𝗨𝗪𝗘𝗣𝗢, 𝗡𝗘𝗡𝗗𝗘𝗡𝗜 𝗠𝗞𝗔𝗣𝗜𝗚𝗘 𝗞𝗨𝗥𝗔 - 𝗗𝗞𝗧. 𝗦𝗔𝗠𝗜𝗔
𝙈𝙖𝙩𝙪𝙨𝙞 𝙣𝙞𝙖𝙘𝙝𝙞𝙚𝙣𝙞 𝙢𝙞𝙢𝙞, 𝙣𝙞𝙣𝙖𝙮𝙖𝙗𝙚𝙗𝙖 𝙠𝙬𝙖 𝙣𝙞𝙖𝙗𝙖 𝙮𝙚𝙣𝙪.
"..Niwahakikishie tarehe 29, kesho kutwa tu mwezi huu wa 10, niwaombe tokeni muende mkapige kura."
"Ninayeongea hapa ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa nchi hii, ninataka niwaambie, maandamano yatakayokuwepo ni ya watu kwenda vituoni kupiga kura, hakuna maandamano mengine yatakayokuwepo hapa.."
"..hakuna tishio la kiusalama litakalokuwepo, anayesemahapa ndiye Amiri Jeshi Mkuu wa Nchi hii."
"Niwaombe ndugu zangu, twendeni mkapige kura, twendeni mkapige kura... Ndugu zangu mengine niachieni mimi, matusi niachieni mimi, ninayabeba kwa niaba yenu"
"Niliapa kuwa Rais wa Tanzania, niliapa kuilinda Nchi hii kwa kudumisha Amani, Umoja na Mshikamano wetu"
Hayo yamesemwa na Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. 𝗦𝗮𝗺𝗶𝗮 𝗦𝘂𝗹𝘂𝗵𝘂 𝗛𝗮𝘀𝘀𝗮𝗻 wakati akizungumza kwenye Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni Jijini Dar es Salaam katika mkutano wa hadhara wa kampeni za Uchaguzi Mkuu uliofanyika leo tarehe 21 Oktoba 2025.
𝘾𝙃𝘼𝙂𝙐𝘼 𝙎𝘼𝙈𝙄𝘼, 𝘾𝙃𝘼𝙂𝙐𝘼 𝘾𝘾𝙈
DKT. SAMIA: TUTAHAKIKISHA DAR INAONDOKANA NA ADHA YA MAJI KWA MIRADI MIPYA
"Katika miaka mitano inayokuja, tutaendelea kukamilisha utekelezaji wa miradi ya Bwawa la Kidunda lenye thamani ya Shilingi bilioni 336, na bwawa hili la Kidunda litakwenda kuhudumia mikoa ya Dar es Salaam, Pwani na Morogoro. Lakini mradi wa pili tunaokwenda kuufanya ili kuondoa uhaba wa maji Dar es Salaam hasa wakati wa kiangazi, ni mradi mkubwa wa kutoa maji mto Rufiji ambao kazi ya upembuzi yakinifu na utafiti wa kina tayari tumekwishaianza na awamu hii tunakwenda kufanya utekelezaji ili Dar es Salaam ipate maji kutoka Kidunda, Ruvu na Mto Rufiji kuondoa kabisa kadhia ya uhaba wa maji", - Dkt. Samia.
Mgombea wa nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza kwenye Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni Jijini Dar es Salaam katika mkutano wa hadhara wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 21, 2025.
"Niwahakikishie tarehe 29, kesho kutwa tu mwezi huu wa 10, niwaombe tokeni muende mkapige kura. Ninayeongea hapa ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa nchi hii, ninataka niwaambie, maandamano yatakayokuwepo ni ya watu kwenda vituoni kupiga kura, hakuna maandamano mengine yatakayokuwepo hapa, hakuna tishio la kiusalama litakalokuwepo, anayesema ni Amiri Jeshi Mkuu wa Nchi hii. Niwaombe ndugu zangu, twendeni mkapige kura, twendeni mkapige kura... Ndugu zangu mengine niachieni mimi, matusi niachieni mimi, ninayabeba kwa niaba yenu", - Dkt. Samia.
Mgombea wa nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza kwenye Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni Jijini Dar es Salaam katika mkutano wa hadhara wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 21, 2025.
KUANZIA 2026 MTAONA MAGEUZI MAKUBWA YA MWENDOKASI DAR - DKT. SAMIA
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema kuwa serikali yake itakwenda kusimamia na kukamilisha mradi wa miundombinu ya barabara ya mabasi yaendayo haraka maarufu kama mwendokasi, hiyo itafanyika ikiwa atachaguliwa kuiongoza nchi kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.
Dkt. Samia ameyasema hayo akizungumza kwenye Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni Jijini Dar es Salaam katika mkutano wa hadhara wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 21, 2025 ambapo amesisitiza kuwa utoaji wa huduma ya usafiri na usafirishaji kupitia miundombinu hizo zitakapokamilika, utajikita zaidi kwenye sekta binafsi.
"Tukapomaliza barabara zote, ni fursa muhimu kwa sekta binafsi kupata kazi ya kubeba abiria na kurudisha, kazi hiyo kwa kiasi hatutaki kuifanya sisi serikali bali sekta binafsi wataingiza mabasi yao na wafanye uendeshaji wa shughuli hizo", ameeleza Dkt. Samia.
Amewaahidi wakazi wa Dar es Salaam kuwa kuanzia Januari, 2026 kutakuwa na mageuzi makubwa ya utoaji wa huduma ya miundombinu ya mwendokasi.

Labels:
KITAIFA
September 18, 2025

WASIRA: DK. SAMIA, CCM WAMEDHARIA KULETA MABADILIKO KATIKA MAISHA YA WATANZANIA
Written By CCMdijitali on Thursday, September 18, 2025 | September 18, 2025
WASIRA: DK. SAMIA, CCM WAMEDHARIA KULETA MABADILIKO KATIKA MAISHA YA WATANZANIA
Na MWANDISHI WETU, MBEYA
MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wasira, amesema Chama kinafanya kazi kubwa ya kuleta mabadiliko ili kuwaletea maendeleo wananchi.
Aidha, amesisitiza wananchi wandelee kukiamini na kukipa nafasi Chama kiendelee kudumisha amani kwa kuwa maendeleo hayatapatikana iwapo itatoweka.
Wasira alieleza hayo alipokuwa akizungumza na viongozi na wanachama wa CCM kutoka Jimbo la Mbeya, akiwa katika ziara ya kumwombea kura mgombea urais wa CCM Dk. Samia Suluhu Hassan pamoja na wagombea wa ubunge na udiwani mkoani Mbeya, jana.
Alitumia mkutano huo kumwombea kura Dk. Samia, wagombea ubunge na udiwani waliosimamishwa kupeperusha bendera ya CCM katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, mwaka huu.
"Kazi yetu ni kuleta mabadiliko katika maisha ya watu, maendeleo ni mabadiliko katika maisha ya watu, ukitengeneza barabara unamwezesha huyu mtu aweze kufikisha bidhaa zake sokoni kwa hiyo ataongeza kilimo na uchumi wake utaongezeka kwa sababu ana mahali pakuuza.
"Ukimnyima barabara analima chakula chake cha kula na kufa, anakula ashibe angojee kifo maana hakuna maendeleo hapo," alisema.
Alisema kuwajengea wananchi miundombinu muhimu ikiwemo ya hospitali ni kuwapunguzia safari ya kwenda kutafuta dawa maeneo ya mbali kutoka katika makazi yao.
"Tumepiga hatua lakini maendeleo hayana kikomo na wala hayamalizi matatizo yote kwa mpigo kwa sababu hata ukifanya maendeleo makubwa zaidi unaweza ukazalisha matatizo mapya.
MIAKA MINNE YA MAFANIKIO
Alieleza kuwa, katika miaka CCM i.esimamiamaendeleo makubwa katika ngazi mbalimbali ambayo yamewagusa wananchi moja kwa moja.
"Tukisema Samia mitano tena ni kwa sababu kuna kazi amefanya na ameifanya kwa uzuri na ana uzoefu wa kuifanya, ametekeleza vema miradi mikubwa iliyoachwa na mtangulizi wake likiwemo bwawa la kufua umeme la Julius Nyerere.
"Amejenga lile bwawa limefikia asilimia 100, sasa tuna megawati 4000 badala ya 16,000 alizoachiwa na mtangulizi wake na sasa hakuna shida ya umeme labda matatizo ya miundombinu lakini hakuna shida ya mahitaji ya umeme," alisema.
Kwa miaka minne na nusu serikali imejenga shule tisa mpya za msingi hapa kwenye wilaya yenu na amejenga madarasa 280 mapya tena sio mapya tu bali mapya mazuri, amejenga sekondari mpya nane katika wilaya hii katika muda wa miaka minne na nusu, amejenga madarasa ya sekondari 218 na hamkuchangishwa kwa madarasa hayo.
KUHUSU AMANI
Alisisitiza Watanzania kulinda amani kwa kuwa ndiyo nyenzo muhimu ya kuleta maendeleo ya sekta zote.
Wasira alisema ukipoteza amani unapoteza maendeleo kwa sababu hata maendeleo yaliyofikiwa hayawezi kuwa na msaada kwa maisha ya watu.
"Amani ikipotea hata madaraja tuliyojenga hayana maana, hata barabara zinachimbika kwa sababu amani imetoweka kwa hiyo kqzi yetu kama chama cha Mapinduzi pamoja na kulinda u.oja wa taifa tunataka kuhakikisha amani amani inakuwepo kwa sababu ikitoweka hakuna maendeleo na haya yote mnayosema hapa hayatakuja," alieleza.
Kwa upande wake Kaimu Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mbeya, Ndele Mwaselela alisema Chama mkoani humo kimejipanga vema kuhakikisha uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, mwaka huu wagombea wake wote wanapata kura za kishindo.
Mwaselela alisema wamejipanga kumtafutia kura nyingi Dk. Samia zitakazomwezesha kuibuka mshindi aendelee kuiongoza nchi kwa mafanikio.
Mgombea ubunge katika Jimbo la Mbeya Vijijini, Patali Shida, alisema iwapo ataibuka mshindi ataendelea kusimamia vema kasi ya maendeleo kuendeleza iliyofanyika katika miaka mitano iliyopita.

== ==
VV1
Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara, Stephen Wasira akimnadi mgombea ubunge wa Jimbo la Mbeya Vijijini, Patali Shida katika mkutano wa viongozi wa CCM Jimbo la Mbeya Vijijini, Mbalizi mkoani Mbeya, jana. (Na Mpigapicha Wetu).
...
...
Viongozi wa CCM Jimbo la Mbeya Vijijini wakimsikiliza
Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara, Stephen Wasira alipozungumza nao katika mkutano uliofanyika Mbalizi, mkoani Mbeya, jana (Na Mpigapicha Wetu).
Labels:
KITAIFA
September 17, 2025
NA MWANDISHI WETU, MBEYA
MAKAMU MMwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wasira amesema Watanzania wataichagua CCM katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu kwa kuwa Ilani yake ya Uchaguzi inagusa maisha na maendeleo yao.
Amesema hakuna chama chochote cha siasa miongoni mwa vyama vinavyoshiriki uchaguzi huo ambacho kimejipanga kufanya mambo mazuri kama ilivyo CCM, hivyo wananchi hawataona sababu ya kuvichagua.
Wasira alieleza hayo jana mjini Mbeya alipozungumza na viongozi wa Chama kutoka majimbo ya Mbeya mjini na Uyole, alipokuwa akimwombea kura Mgombea Urais wa CCM, Dk. Samia Suluhu Hassan na kuweka mikakati ya ushindi katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, mwaka huu
"Yako mambo mengi tumedhamiria kuyafanya kupitia utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2020-2030 kwa manufaa ya wananchi.
"Elimu tumekubaliana tubadili mfumo wa elimu ili kijana akienda sekondari 'school' (shule ya sekondari) akitoka anajua ujuzi wa kazi. Tumeeneza umeme, tunapeleka maji, ukiwa na maji ya bomba endapo bomba likiharibika unafanyaje, lazima uwe na watu hapo mtaani kwako ambao wanaweza kurekebisha bomba na ndio kazi yao watakuwa wamesoma," alisema.
Alisema kutokana na kazi kubwa inayofanyika kutanua fursa mbalimbali ikiwemo ya kusambaza umeme, ni muhimu kuwa na mafundi wenye uwezo wa taaluma za umeme hadi vijijini na hiyo ni moja ya sababu za kubadili mfumo wa elimu uendane na mahitaji ya wakati.
"Tumesema katika Ilani hii vijana wasome, waanzishe kampuni zao zinazoendana na ujuzi wao na sisi tuwape mitaji waweze kufanya kazi ya kujiajiri na kuajiri wenzao na hii wamefanya Korea Kusini na wameweza, kwa nini sisi hatuwezi," alieleza.
Kwa mujibu wa Wasira, CCM inakusudia kuimarisha zaidi huduma za afya, kuwapa bima Watanzania wote wenye uwezo na wasiokuwa nao na kwamba sasa Bunge linatafuta vyanzo vya mapato kuona namna ya kugharimia bima kwa wasio lna uwezo.
Aliwataka viongozi hao kuhakikisha wanafikisha kwa wananchi elimu kuhusu ahadi za maendeleo zilizomo ndani ya Ilani ya Uchaguzi ya CCM.
"Sasa tukiyajua hayo tunaenda kwa wananchi maana mimi nawatuma nyie mwende kwa wananchi na elimu ninayowapa muipeleke kwa wananchi waelewe kumbe ndiyo mambo ya CCM haya, kumbe kuna bima, kumbe kuna elimu yenye ujuzi, kumbe maji yataongezeka," alisisitiza.
MBEYA MJINI KUNG'ARISHWA
Akizungumzia ahadi za Ilani ya Uchaguzi ya CCM kwa jiji la Mbeya, alisema kuhusu elimu ya msingi na sekondari inakusudia kujenga madarasa 1,600 kwa kuwa idadi ya watoto wanaozaliwa inaendelea kuongezeka.
Kwenye Afya alisema zahanati 10 na vituo vya afya vitano vipya vitajengwa pamoja na kuboresha huduma.
Ili kuzidi kuling'arisha jiji hilo alisema zitawekwa taa za barabarani, "taa zile kubwa takribani 100 kwa ajili ya kuleta mwanga na tutasimamia ujenzi wa barabara za mjini kwa ajili ya kuwa na mitaa inayovutia na kama nilivyosema tutaongeza huduma ya maji pamoja na yale ambayo niliyasema kuhusu uchumi.
HAKUNA WA KUSHINDANA NA CCM
Alisema kwa sasa hakuna chama cha siasa miongoni mwa vinavyowania nafasi katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu ambacho kina sera na ilani bora kama ya CCM.
"Sasa chama chenye sera na ilani ya kutushinda kiko wapi, maana tulipotoa hii ilani kiongozi mmoja wa chama cha siasa alitupigia simu akasema sasa CCM mmeandika mambo yote sisi tutaandika nini, nikasema hayo yetu muwe mnasoma halafu mnanukuu mnasema kama CCM ilivyosema.
Aliwahimiza wana CCM kuwauelimisha wananchi waielewe Ilani hiyo, pia kuweka mkakati wa kuhakikisha wananchi hususa wana CCM wanapiga kura.
WASIRA- ILANI YA UCHAGUZI CCM INAGUSA MAISHA YA WATU ,WATAICHAGUA
Written By CCMdijitali on Wednesday, September 17, 2025 | September 17, 2025
NA MWANDISHI WETU, MBEYA
MAKAMU MMwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wasira amesema Watanzania wataichagua CCM katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu kwa kuwa Ilani yake ya Uchaguzi inagusa maisha na maendeleo yao.
Amesema hakuna chama chochote cha siasa miongoni mwa vyama vinavyoshiriki uchaguzi huo ambacho kimejipanga kufanya mambo mazuri kama ilivyo CCM, hivyo wananchi hawataona sababu ya kuvichagua.
Wasira alieleza hayo jana mjini Mbeya alipozungumza na viongozi wa Chama kutoka majimbo ya Mbeya mjini na Uyole, alipokuwa akimwombea kura Mgombea Urais wa CCM, Dk. Samia Suluhu Hassan na kuweka mikakati ya ushindi katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, mwaka huu
"Yako mambo mengi tumedhamiria kuyafanya kupitia utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2020-2030 kwa manufaa ya wananchi.
"Elimu tumekubaliana tubadili mfumo wa elimu ili kijana akienda sekondari 'school' (shule ya sekondari) akitoka anajua ujuzi wa kazi. Tumeeneza umeme, tunapeleka maji, ukiwa na maji ya bomba endapo bomba likiharibika unafanyaje, lazima uwe na watu hapo mtaani kwako ambao wanaweza kurekebisha bomba na ndio kazi yao watakuwa wamesoma," alisema.
Alisema kutokana na kazi kubwa inayofanyika kutanua fursa mbalimbali ikiwemo ya kusambaza umeme, ni muhimu kuwa na mafundi wenye uwezo wa taaluma za umeme hadi vijijini na hiyo ni moja ya sababu za kubadili mfumo wa elimu uendane na mahitaji ya wakati.
"Tumesema katika Ilani hii vijana wasome, waanzishe kampuni zao zinazoendana na ujuzi wao na sisi tuwape mitaji waweze kufanya kazi ya kujiajiri na kuajiri wenzao na hii wamefanya Korea Kusini na wameweza, kwa nini sisi hatuwezi," alieleza.
Kwa mujibu wa Wasira, CCM inakusudia kuimarisha zaidi huduma za afya, kuwapa bima Watanzania wote wenye uwezo na wasiokuwa nao na kwamba sasa Bunge linatafuta vyanzo vya mapato kuona namna ya kugharimia bima kwa wasio lna uwezo.
Aliwataka viongozi hao kuhakikisha wanafikisha kwa wananchi elimu kuhusu ahadi za maendeleo zilizomo ndani ya Ilani ya Uchaguzi ya CCM.
"Sasa tukiyajua hayo tunaenda kwa wananchi maana mimi nawatuma nyie mwende kwa wananchi na elimu ninayowapa muipeleke kwa wananchi waelewe kumbe ndiyo mambo ya CCM haya, kumbe kuna bima, kumbe kuna elimu yenye ujuzi, kumbe maji yataongezeka," alisisitiza.
MBEYA MJINI KUNG'ARISHWA
Akizungumzia ahadi za Ilani ya Uchaguzi ya CCM kwa jiji la Mbeya, alisema kuhusu elimu ya msingi na sekondari inakusudia kujenga madarasa 1,600 kwa kuwa idadi ya watoto wanaozaliwa inaendelea kuongezeka.
Kwenye Afya alisema zahanati 10 na vituo vya afya vitano vipya vitajengwa pamoja na kuboresha huduma.
Ili kuzidi kuling'arisha jiji hilo alisema zitawekwa taa za barabarani, "taa zile kubwa takribani 100 kwa ajili ya kuleta mwanga na tutasimamia ujenzi wa barabara za mjini kwa ajili ya kuwa na mitaa inayovutia na kama nilivyosema tutaongeza huduma ya maji pamoja na yale ambayo niliyasema kuhusu uchumi.
HAKUNA WA KUSHINDANA NA CCM
Alisema kwa sasa hakuna chama cha siasa miongoni mwa vinavyowania nafasi katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu ambacho kina sera na ilani bora kama ya CCM.
"Sasa chama chenye sera na ilani ya kutushinda kiko wapi, maana tulipotoa hii ilani kiongozi mmoja wa chama cha siasa alitupigia simu akasema sasa CCM mmeandika mambo yote sisi tutaandika nini, nikasema hayo yetu muwe mnasoma halafu mnanukuu mnasema kama CCM ilivyosema.
Aliwahimiza wana CCM kuwauelimisha wananchi waielewe Ilani hiyo, pia kuweka mkakati wa kuhakikisha wananchi hususa wana CCM wanapiga kura.
Labels:
KITAIFA
August 11, 2025
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amesema ni muhimu Jeshi la Polisi kuimarisha ushirikiano wa karibu na wadau wote wa uchaguzi, hatua ambayo itasaidia kuhakikisha kila mdau anatendewa haki, na kuondoa tofauti zinazoweza kusababisha migongano.
Makamu wa Rais ametoa wito huo wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi unaofanyika katika ukumbi wa Chuo Cha Polisi (CCP) Moshi Mkoani Kilimanjaro. Amesema Baadhi ya maeneo muhimu ya ushirikiano ni pamoja na kuhakikisha mikutano ya kampeni inafanyika kwenye maeneo yaliyoruhusiwa na ndani ya muda uliopangwa, Kuzuia maandamano yasiyo na kibali, kuimarisha ulinzi wa wagombea na viongozi wa vyama vya kisiasa, bila kujali vyama vyao au itikadi zao pamoja na kudhibiti misongamano mikubwa ya watu ili kuhakikisha shughuli nyingine za kijamii na kiuchumi zinaendelea bila usumbufu.
Pia Makamu wa Rais amelitaka Jeshi la Polisi kushirikiana kwa karibu na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) pamoja na taasisi nyingine za Serikali ili kujiandaa vyema kutumia Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) katika kufuatilia taarifa mbalimbali zenye mlengo wa uchochezi, zinazotolewa kupitia mitandao ya kijamii na vyombo vingine vya habari. Amesema kwa kutumia teknolojia za akili bandia baadhi ya watu wanaweza kusambaza picha au video za uongo za wagombea wa vyama vya siasa, jambo linaloweza kuleta madhara makubwa kwa amani na utulivu wa jamii.
Makamu wa Rais amesema Jeshi la Polisi linapaswa kujiandaa kikamilifu kufanya doria ya mtandao ili kubaini na kuchambua machapisho, picha, na video zenye viashiria vya uvunjifu wa sheria, na kuchukua hatua za kisheria kwa haraka.
Vilevile, Makamu wa Rais amesisitiza Jeshi la Polisi lishirikiane kwa karibu na wadau wengine wa uchaguzi, ikiwemo TAKUKURU na vyombo vingine vya usalama, ili kudhibiti vitendo vya Rushwa katika kipindi cha uchaguzi. Ameongeza kwamba ni muhimu Jeshi la Polisi likijumuisha Polisi Jamii lishirikiane kwa karibu na TAMISEMI katika kusimamia usalama, hasa katika ngazi za Kata, Shehia, Vijiji na Mitaa.
Makamu wa Rais amelitaka Jeshi la Polisi kusimamia vema utekelezaji wa sheria ya uchaguzi na sheria nyingine za nchi. Amesema ni wajibu wa Jeshi la Polisi na wadau wengine wa uchaguzi, kuielewa vizuri Sheria ya Uchaguzi na kusimamia utekelezaji wake, ili kuepuka kuonea watu na kuvuruga uchaguzi. Aidha ametoa wito kwa wananchi na viongozi wa vyama vya siasa kuepuka kujichukulia sheria mkononi pale wanapoona ukiukwaji wa sheria za uchaguzi, na badala yake watoe taarifa kwenye vyombo vya sheria kwa hatua stahiki.
Halikadhalika Makamu wa Rais amesema katika kuelekea Uchaguzi Mkuu ni muhimu kuendelea kuwajengea uwezo maafisa na askari kwa kuwapatia mafunzo ya utayari, uadilifu, na ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao. Amempongeza Mkuu wa Jeshi la Polisi kwa kuendelea kuhakikisha askari wa Jeshi la Polisi wanapata mafunzo ya kitaalam ya kuwajengea uwezo na utayari.
Kwa upande wake Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Daniel Sillo ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuiwezesha Wizara kibajeti,vifaa na vitendea kazi vya kisasa ambavyo vimesaidia kuimarisha na kuboresha utendaji wa Jeshi la Polisi na vyombo vya usalama vilivyopo chini ya Wizara hiyo.
Ameishukuru Serikali kwa kutoa vibali vya ajira na upandishaji vyeo hali inayosaidia katika udhibiti wa uhalifu nchini na kuongeza ari ya utendaji kazi kwa maafisa na askari ndani ya Wizara. Amesema Wizara na vyombo vyote vya usalama vilivyo chini yake itaendelea kufanya kazi kwa ushirikiano, nidhamu, weledi na uadilifu ili kuhakikisha nchi inaendelea kuwa salama yenye amani na utulivu na mazingira mazuri kwa ajili maendeleo na uchumi endelevu wa Taifa.
Awali akitoa taarifa ya Mkutano huo, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Camillus Wambura amesema Jeshi la Polisi limejipanga kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa amani na utulivu na kuwasihi Watanzania wawe na uhakika na utulivu wakiamini kipindi hicho chote kitapita katika hali ya usalama na utulivu wa hali ya juu pamoja na Serikali itakayochaguliwa itaingia madarakani bila kikwazo.
Amesema kauli mbiu inayoongoza mkutano huo inaweka msisitizo katika kusimamia amani na utulivu wakati wote wa mchakato wa uchaguzi ili kuhakikisha wananchi wanashiriki kwa utulivu, uhuru na amani bila kuwa na vikwazo vya aina yeyote. Pia amesema inasisitiza na kuweka jukumu kwa kila mwananchi kuhakikisha analinda amani usalama na utulivu kipindi cha kabla, wakati na baada ya uchaguzi.
Imetolewa na
Ofisi ya Makamu wa Rais
11 Agosti 2025
Moshi – Kilimanjaro.










Makamu wa Rais afungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi
Written By CCMdijitali on Monday, August 11, 2025 | August 11, 2025
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amesema ni muhimu Jeshi la Polisi kuimarisha ushirikiano wa karibu na wadau wote wa uchaguzi, hatua ambayo itasaidia kuhakikisha kila mdau anatendewa haki, na kuondoa tofauti zinazoweza kusababisha migongano.
Makamu wa Rais ametoa wito huo wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi unaofanyika katika ukumbi wa Chuo Cha Polisi (CCP) Moshi Mkoani Kilimanjaro. Amesema Baadhi ya maeneo muhimu ya ushirikiano ni pamoja na kuhakikisha mikutano ya kampeni inafanyika kwenye maeneo yaliyoruhusiwa na ndani ya muda uliopangwa, Kuzuia maandamano yasiyo na kibali, kuimarisha ulinzi wa wagombea na viongozi wa vyama vya kisiasa, bila kujali vyama vyao au itikadi zao pamoja na kudhibiti misongamano mikubwa ya watu ili kuhakikisha shughuli nyingine za kijamii na kiuchumi zinaendelea bila usumbufu.
Pia Makamu wa Rais amelitaka Jeshi la Polisi kushirikiana kwa karibu na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) pamoja na taasisi nyingine za Serikali ili kujiandaa vyema kutumia Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) katika kufuatilia taarifa mbalimbali zenye mlengo wa uchochezi, zinazotolewa kupitia mitandao ya kijamii na vyombo vingine vya habari. Amesema kwa kutumia teknolojia za akili bandia baadhi ya watu wanaweza kusambaza picha au video za uongo za wagombea wa vyama vya siasa, jambo linaloweza kuleta madhara makubwa kwa amani na utulivu wa jamii.
Makamu wa Rais amesema Jeshi la Polisi linapaswa kujiandaa kikamilifu kufanya doria ya mtandao ili kubaini na kuchambua machapisho, picha, na video zenye viashiria vya uvunjifu wa sheria, na kuchukua hatua za kisheria kwa haraka.
Vilevile, Makamu wa Rais amesisitiza Jeshi la Polisi lishirikiane kwa karibu na wadau wengine wa uchaguzi, ikiwemo TAKUKURU na vyombo vingine vya usalama, ili kudhibiti vitendo vya Rushwa katika kipindi cha uchaguzi. Ameongeza kwamba ni muhimu Jeshi la Polisi likijumuisha Polisi Jamii lishirikiane kwa karibu na TAMISEMI katika kusimamia usalama, hasa katika ngazi za Kata, Shehia, Vijiji na Mitaa.
Makamu wa Rais amelitaka Jeshi la Polisi kusimamia vema utekelezaji wa sheria ya uchaguzi na sheria nyingine za nchi. Amesema ni wajibu wa Jeshi la Polisi na wadau wengine wa uchaguzi, kuielewa vizuri Sheria ya Uchaguzi na kusimamia utekelezaji wake, ili kuepuka kuonea watu na kuvuruga uchaguzi. Aidha ametoa wito kwa wananchi na viongozi wa vyama vya siasa kuepuka kujichukulia sheria mkononi pale wanapoona ukiukwaji wa sheria za uchaguzi, na badala yake watoe taarifa kwenye vyombo vya sheria kwa hatua stahiki.
Halikadhalika Makamu wa Rais amesema katika kuelekea Uchaguzi Mkuu ni muhimu kuendelea kuwajengea uwezo maafisa na askari kwa kuwapatia mafunzo ya utayari, uadilifu, na ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao. Amempongeza Mkuu wa Jeshi la Polisi kwa kuendelea kuhakikisha askari wa Jeshi la Polisi wanapata mafunzo ya kitaalam ya kuwajengea uwezo na utayari.
Kwa upande wake Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Daniel Sillo ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuiwezesha Wizara kibajeti,vifaa na vitendea kazi vya kisasa ambavyo vimesaidia kuimarisha na kuboresha utendaji wa Jeshi la Polisi na vyombo vya usalama vilivyopo chini ya Wizara hiyo.
Ameishukuru Serikali kwa kutoa vibali vya ajira na upandishaji vyeo hali inayosaidia katika udhibiti wa uhalifu nchini na kuongeza ari ya utendaji kazi kwa maafisa na askari ndani ya Wizara. Amesema Wizara na vyombo vyote vya usalama vilivyo chini yake itaendelea kufanya kazi kwa ushirikiano, nidhamu, weledi na uadilifu ili kuhakikisha nchi inaendelea kuwa salama yenye amani na utulivu na mazingira mazuri kwa ajili maendeleo na uchumi endelevu wa Taifa.
Awali akitoa taarifa ya Mkutano huo, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Camillus Wambura amesema Jeshi la Polisi limejipanga kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa amani na utulivu na kuwasihi Watanzania wawe na uhakika na utulivu wakiamini kipindi hicho chote kitapita katika hali ya usalama na utulivu wa hali ya juu pamoja na Serikali itakayochaguliwa itaingia madarakani bila kikwazo.
Amesema kauli mbiu inayoongoza mkutano huo inaweka msisitizo katika kusimamia amani na utulivu wakati wote wa mchakato wa uchaguzi ili kuhakikisha wananchi wanashiriki kwa utulivu, uhuru na amani bila kuwa na vikwazo vya aina yeyote. Pia amesema inasisitiza na kuweka jukumu kwa kila mwananchi kuhakikisha analinda amani usalama na utulivu kipindi cha kabla, wakati na baada ya uchaguzi.
Mkutano huo wa siku tano kuanzia tarehe 11-15 Agosti 2025 unaongozwa na kauli mbiu isemayo “Amani, Utulivu na Usalama kabla, wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu 2025 ni jukumu letu sote”
Imetolewa na
Ofisi ya Makamu wa Rais
11 Agosti 2025
Moshi – Kilimanjaro.










Labels:
KITAIFA
August 11, 2025
Akizungumza katika ibada ya mazishi, Waziri Mkuu amewataka Watanzania kuenzi mema yote yaliyofanywa na Hayati Ndugai enzi za uhai wake, akisema mchango wake katika uongozi wa Bunge na Taifa kwa ujumla utabaki kuwa kumbukumbu muhimu kwa vizazi vijavyo.
Aidha, Waziri Mkuu ameeleza kuwa hayati Ndugai alikuwa mlinzi wa taratibu za Bunge na mshirika wa karibu katika kuimarisha ushirikiano kati ya Bunge na Serikali kwa maslahi mapana ya Taifa, akisisitiza mawasiliano ya uwazi, mshikamano na mwelekeo wa pamoja wa utekelezaji wa ajenda za kitaifa.
Vilevile, Mheshimiwa Majaliwa amemtaja hayati Ndugai kama kiongozi mwenye weledi, uadilifu, unyenyekevu, na mchapakazi ambaye alibeba heshima ya mkoa wa Dodoma na jimbo la Kongwa kupitia uongozi na siasa za uwajibikaji.
Kwa upande wake, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko, ametoa salamu za pole kwa familia ya marehemu, wananchi wa Kongwa na Watanzania wote kwa ujumla kutokana na msiba wa hayati Ndugai.
Naye, Spika wa Bunge Dkt. Tulia Ackson amesema kuwa wanaamini katika kumuenzi hayati Ndugai na watamkumbuka daima kwa kuendeleza misingi pamoja na mambo mema yote aliyoyatenda wakati wa uhai wake.
Mazishi ya Hayati Ndugai yamehudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Katibu Mkuu Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhandisi Zena Saidi, Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara, John Mongela, Waziri Mkuu Mstaafu Mizengo Pinda, viongozi wengine kitaifa, ndugu, jamaa na wananchi kutoka maeneo mbalimbali.
Hayati Job Ndugai alifariki agosti 06, 2025 jijini Dodoma kwa Shinikizo la damu lililoshuka sana.








WAZIRI MKUU AMWAKILISHA RAIS DKT. SAMIA MAZISHI YA HAYATI NDUGAI
- Asema aliimarisha ushirikiano kati ya Bunge na Serikali
- Atoa rai kwa Watanzania kuenzi mema yote aliyoyafanya enzi za uhai wake
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Agosti 11, 2025 amemwakilisha Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Spika mstaafu wa Bunge la Tanzania, Job Yustino Ndugai, yaliyofanyika shambani kwake, kijiji cha Msunjulile, wilayani Kongwa mkoani Dodoma.
Akizungumza katika ibada ya mazishi, Waziri Mkuu amewataka Watanzania kuenzi mema yote yaliyofanywa na Hayati Ndugai enzi za uhai wake, akisema mchango wake katika uongozi wa Bunge na Taifa kwa ujumla utabaki kuwa kumbukumbu muhimu kwa vizazi vijavyo.
Amesema kuwa akiwa mwakilishi wa wananchi wa Kongwa, hayati Ndugai ametoa mchango mkubwa katika kipindi cha miaka 20 ya utumishi wake, na kwamba wote ni mashuhuda wa maendeleo makubwa yaliyopatikana katika sekta mbalimbali za maendeleo pamoja na huduma za kijamii. “Serikali itaendelea kumuenzi kwa yale yote aliyoyafanya kwa wanaKongwa”
Aidha, Waziri Mkuu ameeleza kuwa hayati Ndugai alikuwa mlinzi wa taratibu za Bunge na mshirika wa karibu katika kuimarisha ushirikiano kati ya Bunge na Serikali kwa maslahi mapana ya Taifa, akisisitiza mawasiliano ya uwazi, mshikamano na mwelekeo wa pamoja wa utekelezaji wa ajenda za kitaifa.
Vilevile, Mheshimiwa Majaliwa amemtaja hayati Ndugai kama kiongozi mwenye weledi, uadilifu, unyenyekevu, na mchapakazi ambaye alibeba heshima ya mkoa wa Dodoma na jimbo la Kongwa kupitia uongozi na siasa za uwajibikaji.
Pia, Waziri Mkuu amesema kuwa Serikali itasimamia utekelezaji wa maagizo yaliyotolewa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia ya kukamilishwa kwa masuala yote yaliyoanzishwa na Hayati Ndugai, pamoja na kuendeleza makumbusho ya Kongwa ikiwa ni kielelezo cha kupigania uhuru kwa nchi za kusini mwa afrika. “Tutasimamia agizo hili kwa ukamilifu.”
Kwa upande wake, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko, ametoa salamu za pole kwa familia ya marehemu, wananchi wa Kongwa na Watanzania wote kwa ujumla kutokana na msiba wa hayati Ndugai.
Naye, Spika wa Bunge Dkt. Tulia Ackson amesema kuwa wanaamini katika kumuenzi hayati Ndugai na watamkumbuka daima kwa kuendeleza misingi pamoja na mambo mema yote aliyoyatenda wakati wa uhai wake.
Mazishi ya Hayati Ndugai yamehudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Katibu Mkuu Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhandisi Zena Saidi, Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara, John Mongela, Waziri Mkuu Mstaafu Mizengo Pinda, viongozi wengine kitaifa, ndugu, jamaa na wananchi kutoka maeneo mbalimbali.
Hayati Job Ndugai alifariki agosti 06, 2025 jijini Dodoma kwa Shinikizo la damu lililoshuka sana.









Labels:
KITAIFA




