NAIBU WAZIRI PINDA AELEKEZA UENDELEZAJI MIJI KUZINGATIA MIPANGO KABAMBE

Na Munir Shemweta, WANMM Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Geofrey Pinda amezielekeza Halmashauri zote nchini kuhakik...

Latest Post

Gavana: Pato la taifa limeongezeka

Written By CCMdijitali on Friday, September 30, 2016 | September 30, 2016

Gavana wa Benki Kuu (BoT), Profesa Benno Ndulu

Imeandikwa na Sophia Mwambe | Habari Leo

UKUAJI wa pato la taifa katika nusu ya kwanza ya mwaka ya Januari mpaka Juni, umeongezeka na kufikia asilimia 6.7 kutoka asilimia 5.7 kwa nusu ya kwanza ya mwaka 2015.

Hayo yamesemwa Dar es Salaam na Gavana wa Benki Kuu (BoT), Profesa Benno Ndulu wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu ukuaji wa pato la taifa kwa robo na nusu mwaka 2016.

Alisema shughuli zilizochangia ukuaji huo wa uchumi kwa kiasi kikubwa kwa nusu ya kwanza ya mwaka 2016 ni uchukuzi na uhifadhi wa mizigo asilimia 16.0, ujenzi asilimia 10.7, na kilimo asilimia 10.3.

”Kilimo kimepiga hatua kubwa kwa nusu ya kwanza ya mwaka huu, ambapo kimekua kwa asilimia 10.3 wakati kilishuka kwa asilimia 8.4 kwa nusu ya kwanza ya mwaka jana,” alisema Ndulu.

Aliongeza kuwa sekta zilizoonekana kukua zaidi katika nusu ya kwanza ya mwaka 2016 ni uchukuzi na uhifadhi wa mizigo ambao umekuwa kwa asilimia 17.4, uchimbaji wa madini na gesi umekuwa kwa asilimia 13.7, mawasiliano umekuwa kwa asilimia 13.0 na sekta ya fedha na bima ambayo imekuwa kwa asilimia 13.0.

“Sisi tunaamini kwa kuangalia hali ya ukuaji wa pato la Taifa kwa nusu ya kwanza ya mwaka pamoja na viashiria ya uchumi mpaka sasa, ni mategemeo yetu kwamba lengo la ukuaji wa pato la taifa kwa asilimia 7.2 kwa mwaka 2016 litafikiwa,” aliongeza.

Akizungumzia mauzo ya nje, alisema utalii unachangia kuongezeka kwa pato la taifa. Alisema idadi ya watalii imeongezeka kutoka watalii 1,075,541 na kufikia milioni 1.1 mwaka huu ambayo imechangia pato kuongezeka kwa asilimia 5.8.

Aliongeza kuwa usafirishaji wa mizigo nje ya nchi umeongezeka, ambapo Uganda umeongezeka kwa asilimia 22.3, Rwanda 7.5, Malawi 14, Burundi 5.8 na Zambia 3.7 huku Kongo ikionekana kushuka kutokana na kushuka kwa thamani ya fedha ya Afrika Kusini.

Ndulu alisema uuzwaji wa bidhaa za viwandani nje ya nchi, umeendelea kukua kwa kasi na mauzo yameongezeka kwa asilimia 12.6, jambo ambalo limechangia kuongezeka kwa fedha za kigeni.

Akizungumzia ukuaji wa pato la taifa katika robo ya pili ya mwaka, alisema kwa mujibu wa takwimu kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), hali ya ukuaji wa uchumi wa Tanzania imeendelea kuwa ya kuridhisha.

Katika robo ya pili ya mwaka 2016, ukuaji wa Pato la Taifa unakadiriwa kuongezeka kwa asilimia 7.9 ikilinganishwa na ongezeko la asilimia 5.8kwa kipindi kama hicho mwaka 2015.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Mashaka Gambo afungua Kongamano la 49 la Chama cha Wafamasia Tanzania

Rais wa Chama cha Wafamasia Tanzania (PST) Ndg. Michael Kishiwa (aliyesimama)akitoa taarifa ya Chama kwa kifupi kwa  Mgeni Rasmi Mhe. Mrisho Gambo katika Kongamano la 49 la wafamasia Tanzania linalofanyika Jijini Arusha.

Wanachama wa PST wakifuatilia ufunguzi wa Kongamano

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Mashaka Gambo akitoa hotuba katika ufunguzi wa kongamano la 49 la Chama cha     Wafamasia Tanzania

Wajumbe wa kongamano wakiendelea kufuatilia Hotuba ya Ufunguzi.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe Mrisho Gambo(Kushoto) akiwa pamoja na Mkurugenzi wa Mamlaka ya Chakula na dawa Hiti Silo katika Kongamano la wafamasia linalofanyika katika Jiji la Arusha.

Na Nteghenjwa Hosseah, ARUSHA

SERIKALI imesema kuwa inaanza kufanya maboresho kwa kuandaa na kuhakikisha  Sera ya Uboreshaji wa Viwanda vya Dawa vilivyopo nchini  kwa kuwawezesha na kuwajengea uwezo  wenye viwanda nchini ili waweze kuzalisha dawa na kupunguza uagizaji wa dawa kutoka nje ya nchi.


Kauli hiyo ilitolewa jana na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Mashaka Gambo kwa niaba ya Waziri  wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Jenista Mhagama alipokuwa akizungumza katika Kongamano la  49 la Chama Cha Wafamasia Tanzania (PST),linalofanyika jijini hapa kwa siku mbili.


Akizungumza kwa niaba ya Mhagama, Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo,alisema kuwa kutokana na umuhimu wa sekta hiyo ya dawa, Serikali inaangalia taaluma hiyo kwa macho mawili kwa lengo la kuiboresha ili iweze kutoa huduma bora.


"Wizara yangu inaangalia taaluma hii kwa macho mawili katika kuhakikisha kuwa sekta ya dawa inaboreka na inakua na hatimaye kuweza kukuza uchumi wetu, kwa kuwawezesha na kuwajengea uwezo wenye viwanda nchini ili waweze kuzalisha zaidi ikiwa ni pamoja na kuwahakikishia soko ndani ya nchi na kupunguza uagizaji wa dawa kutoka nje ya nchi na hivyo kuwa na dawa bora, salama na zenye ufanisi"


"Endapo tutazalisha dawa zetu wenyewe hii itatupunguzia gharama zisizo za lazima kuagiza dawa nje ya nchi, sambamba na hili pia tunaboresha vyuo vya Wafamasia ili waweze kutoka wataalamu bora wa masuala haya ya madawa,”alisema Gambo


Akizungumzia suala la wizi wa dawa katika hospitali za serikali,alisema kuwa Serikali haina mchezo na yoyote atakayokiuka maadili ya taaluma hiyo na kuwa watawachukulia hatua kali za kisheria ili wananchi wapate huduma bora za dawa.


"Mbali na changamoto ya upungufu wa dawa, wafanyakazi wasio waadilifu ambao wanatumia nafasi zao vibaya wanashirikiana na baadhi ya wafanyabiashara na kuuza  dawa, hili ni suala muhimu PST jadilianeni suala la maadili kwani hatua za kisheria dhidi yao zitachukuliwa"alisema


Awali Rais wa PST, Michael Kishiwa, aliiomba Serikali kuongeza udahili wa wanafunzi wa famasia wakiwemo mafamasia wasaidizi ili kutoa dawa sahihi kwa wagonjwa.


Alisema hivi sasa idadi ya watanzania ni kubwa, lakini wataalamu wa dawa Wafamasia ni 1,200, hali inayochangia kuwepo kwa watoa huduma hiyo wasio na sifa.


Alisema kutokana na kukosekana wanataaluma kumekuwepo na changamoto kubwa ya baadhi yao kukiuka maadili na wengine kufanya kazi ya utoaji dawa pasipokuwa na uelewa nayo, hali ambayo hatari kwa afya za binadamu.


Kishiwa alisema kazi kubwa ya chama chao kuhakikisha inasimamia ubora wa utoaji huduma ya dawa na kusimamia maadili, ili wananchi wapate dawa sahihi na kuzitumia ipasavyo.


“Tunashirikiana na baraza la usajili la wafamasia katika kukemea vitendo hivyo vya ukiukwaji wa maadili na ndiyo maana tunaiomba serikali iongeze udahili na vyuo vinavyotoa taaluma hii"alisema


Naye Msajili wa Baraza la Wafamasia, Elizabeth Shekalage alisema kwa sasa wananchi wengi wamechukulia huduma ya dawa ni biashara na kuwa baraza limejipanga kupambana na watu wanaofanya huduma hiyo ni biashara huku wakikiuka  maadili.


"Uchache wa wanataaluma unasababisha kika mtu aone hii ni biashara huria na yeyote anaweza kuifanya,kuna uhaba mkubwa wa fundi dawa sanifu,mafundi dawa wasaidizi,dawa ni sumu hivyo tunasimamia hili ili kuepusha madhara kwa watumiaji"alisema Elizabeth


Kongamano la Mwaka huu linaenda na kauli mbiu isemayo kuelezea ubora,usalama,ufanisi na upatikanaji wa huduma bora za kifamasia.


Mwisho



WADAU WA SEKTA YA MIUNDOMBINU YA BARABARA NA RELI WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA.

Written By CCMdijitali on Thursday, September 29, 2016 | September 29, 2016

 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akiongea na wadau wa miundombinu ya  barabara na reli wakati wa  mkutano wa  Saba wa wadau hao, uliofanyika jijini Dar es salaam.

 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa(Wa pili kutoka kulia) akijadiliana na wadau wa miundombinu ya  barabara na reli mara baada ya kufungua mkutano huo.Kulia kwake ni  Katibu Mkuu Wizara wa Wizara hiyo (Sekta ya Ujenzi) Eng .Joseph Nyamhanga.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akikagua ramani inayonyesha miundombinu ya barabara nchini wakati wa uzinduzi wa mkutano wa saba wa sekta ya Miundombinu ya barabara na reli, jijini Dar es salaam.

Picha na Benjamin Sawe-Maelezo


Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa amewataka wadau wa sekta ya miundombinu ya Reli na Barabara kushirikiana na Serikali katika kuchangamkia fursa za utekelezaji wa miradi mbalimbali ya sekta hiyo hapa nchini.

Akizungumza jijini Dar es Salaam wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Kimataifa wa Saba wa wadau wa Sekta hiyo, Prof. Mbarawa amesema kwa sasa Serikali kupitia Rais wa Awamu ya Tano inatekeleza miradi mbalimbali ikiwemo ujenzi wa bomba la mafuta kutoka Tanga hadi nchini Uganda, ujenzi wa barabara ya kulipia wa Dar es Salaam-Chalinze KM 144 (Dar-Chalinze Express way) na ujenzi wa reli ya kati hivyo ni muhimu kwa wadau hao kutumia mkutano huo katika kuijadili miradi hiyo.

“Ni matumaini yangu katika mkutano huu mtajadili kwa pamoja namna ya kushirikiana na Serikali katika kutekeleza fursa za ujenzi wa miundombinu hapa nchini ikiwemo kuungana na Serikali (Public Private Partnership) au kwa njia nyingine yoyote”, amesema Waziri Mbarawa.

Amesisitiza wadau hao kuja kwa wingi nchini na kuwekeza katika sekta hiyo ili kupanua ushindani wa kibiashara katika soko la kitaifa na kimataifa.


Waziri Mbarawa amebainisha kuwa Serikali inaendelea kutafuta pesa kutoka kwa wadau mbalimbali na kushirikisha taasisi binafsi kupitia mpango wa kushirikiana baina ya Serikali na Taasisi hizo (Public Private Partnership) ili kutekeleza miradi ya miundombinu ya reli na barabara nchini.

Kwa Upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA) Eng. Bruno Ching’andu amesema kuwa licha ya TAZARA kuwa na treni za umma zinazotoa huduma za usafiri nchini bado inakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo uhaba wa fedha katika uendeshaji wa shirika hilo ikiwemo gharama za ujenzi na ukararabati wa mabehewa.


Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, 

Uchukuzi na Mawasiliano.


Kigwangalla afanya ziara Hospitali za Wilaya ya Mlele na Mpanda Mkoani Katavi

 Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, 
Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla amefanya ziara ya kikazi katika Wilaya ya Mlele na 
kutembelea Hospitali ya Mlele ya Wilaya hiyo pamoja na Hospitali ya Mpanda iliyopo Wilaya ya Mpanda Mkoani Katavi huku akitoa maagizo mbalimbali ya kiutendaji.


Katika ziara yake katika Hospitali ya Mlele, Dk.Kigwangalla amewaagiza viongozi wa Serikali wa Wilaya na ule wa Hospitali hiyo kuhakikisha wanakamilisha mambo muhimu ikiwemo ujenzi wa chumba cha upasuaji, jengo la kuhifadhia mahiti na vitu 
vingine huku akitaka ndani ya miezi mitatu view vimekamilika.


Akiwa katika Hospitali hiyo ya Mlele, Dk.Kigwangalla ameweza kutembelea sehemu mbalimbali za hospitali pamoja na kukagua ujenzi wa majengo ya Chumba cha upasuaji, chumba cha kuhifadhia maiti na majengo mengine ambapo amemtaka Mkuu wa Wilaya kuhakikisha wanafanya juhudi wanakamilisha kwa wakati majengo
 hayo ili wananchi wapate huduma bora.


Kwa upande wa ziara yake hiyo katika Wilaya ya Tanganyika yaliyopo makao makuu ya Mkoa wa Katavi, Dk. Kigwangalla ameweza kutembelea Hospitali ya Mpanda ambayo
 kwa sasa inahudumia kama Hospitali ya Mkoa ambapo napo ameagiza kufanyiwa 
marekebisho mbalimbali ikiwemo kuzingatia masuala usafi.


Aidha, ametoa maagizo kuhakikisha wanafunga mfumo wa malipo wa kisasa katika
 vyanzo vyote vya mapato ili kukusanya pesa nyingi zaidi zitakazoweza kuendesha
 huduma  za Afya ndani ya Hospitali hiyo.

 Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla akisalimiana na Chifu Kayamba wa Pili wa Kabila la Wakonongo. Wakati wa kupokelewa alipowasili ofisi za Mkuu wa Wilaya ya Mlele,Mkoani Katavi.

 Mkuu wa Wilaya ya Mlele, Bi.Rachel Kasanda akisoma taarifa kwa Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla (katikati).

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla akikagua moja ya vifaa katika chumba cha Maabara ya hospitali ya Mlele.

Mgunduzi kutoka Veta kuileta dunia Tanzania

Written By CCMdijitali on Wednesday, September 28, 2016 | September 28, 2016

Mgunduzi wa kifaa kipya cha mitaala ya elimu ya anga, mfumo wa jua na sayari zake, Ernest Maranya akitoa maelezo kwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamiseni), Selemani Jafo, juu ya namna kifaa hicho kinavyofanya kazi.

Imeandikwa na Sifa Lubasi| Habari Leo


INGAWA ni kiziwi, Ernest Maranya (36), mkazi wa Dar es Salaam, ana kila sababu ya kuifanya dunia kuelekeza macho na masikio yao Tanzania kutokana na kugundua kifaa kipya cha kufundishia elimu ya anga, mfumo wa jua na sayari zake, huku akitoa makosa kwenye ugunduzi uliofanywa na wakongwe wa sayansi kama Newton.

Kwa ubunifu huo, sasa anaweza kufaidi matunda ya kazi yake mara tu kifaa hicho kitakapoanza kutumika shuleni na pengine wanasayansi wakaja kujifunza kitu Tanzania. Kifaa hicho cha kimaabara kwa ajili ya kufundishia kinatoa taarifa mpya zinazohusu mfumo wa jua baada ya kukifanyia utafiti kwa zaidi ya miaka 10. Kwa upande wake, serikali inasema kifaa hicho kitafungwa katika shule kadhaa za sekondari kwa kuanzia na shule 20 huku ikielekeza wahusika ‘kulinda’ haki miliki ya ugunduzi huo wa kijana wa Kitanzania.

“Tangu nimegundua kifaa hiki, naweza kusema sijapata manufaa kama ilivyotarajiwa, lakini sasa nashukuru kuona kuwa kilio changu kimesikika, nina matumaini makubwa kwamba sasa nitafaidika na ugunduzi huu,” anasema Maranya.

Anasema kwa sasa anafundisha katika Chuo cha Mafunzo ya Ufundi Stadi (Veta) jijini Dar es Salaam kama msaidizi wa mwalimu. Anasema taarifa alizonazo ni kwamba endapo serikali itaanza kununua vifaa hivyo kwa ajili ya kufundishia shuleni anaweza akawa anaiuzia serikali seti moja kwa Sh 600,000 na bei hiyo inaweza kupungua.

Elimu ya anga na tabia za sumaku

Anasema elimu ya anga imegawanyika katika madaraja ambayo yanahusu nishati ya mvutano kati ya jua na sayari inayoliwezesha jua kuzishikilia sayari angani na kuziwezesha kulizunguka jua. Anasema uvumbuzi wake hauna uhusiano kwa namna yoyote na nishati ambayo inaliwezesha jua na nyota kuwaka na kutoa joto na mwanga.

Anasema msingi wa ugunduzi wake ni matokeo ya kugunduliwa kwa kanuni au tabia mpya ya tatu ya usumaku, na kwamba tabia hiyo ya tatu ya usumaku ni matokeo ya kuunganishwa kwa kanuni au tabia kuu mbili za sumaku. Anafafanua kwamba ncha mbili mfanano za sumaku husukumana na ncha tofauti za sumaku huvutana.

Anasema matokeo ya kuunganishwa kwa kanuni hizo kuu mbili za sumaku hufanya masharti ya sumaku kubadilika kuwa nishati ya mvutano mithili ya mifumo ya jua. Anasema ugunduzi huo unaleta taarifa mpya za kisayansi kwamba asili ya nishati hiyo ya mvutano katika anga, kikanuni inatokana na muunganiko wa kanuni au sheria kuu mbili za sumaku (the nature of the universe gravitational potential energy is magnetic two laws combination).

“Hii ni kinyume na ilivyoelezwa na mwanasayansi Isaac Newton kwamba asili ya nishati hiyo ni uzito. (Universe gravitational potential energy is mass). “Kutokana na kugundua msingi huu wa muunganiko wa sheria hizo mbili za sumaku uliniwezesha kutumia sumaku za kawaida kubuni nyenzo hii sambamba na nishati ya mvutano katika anga, mahususi kwa matumizi ya kimaabara mashuleni katika shule za msingi na sekondari,” anasema Maranya.

Anasema kifaa hicho alichokiita kwa jina la Kiingereza: A Teaching Aid Kit for Outer Space bodies ad/or Atomic part, kimelenga kuwa nyenzo ya majaribio ya awali ya kisayansi ili kusaidia zaidi utafiti wa mambo ya anga. Hii ni kwa sababu anasema kifaa hicho kinawezesha kuhakiki, mienendo tabia, matokeo na mahesabu ya utendaji wa vitu vyote vya anga kama vile vimondo, sayari, mwezi, nyota, sumaku za asili na zisizo za asili na tabia za nishati. Tofauti ya teknolojia yake na zilizopita.

Akizungumzia uhusiano na utofauti na vifaa au teknolojia zilizopita anasema vifaa mbalimbali vimetengenezwa ili kuhakiki namna ya mfumo wa jua na chembe za atomiki zinavyotenda kazi.

“Kwa bahati mbaya vifaa hivi hukosa sifa stahiki za mahusiano na tabia za utendaji wa mfumo wa jua au chembe za atomiki asilia kwa kuwa mara nyingi vifaa hivyo hujaribu kutumia njia za kimakenika kama matufe ya plastiki au shaba yaliyoshikiliwa kwa mifumo ya gia au vishikizo kama vile kamba na mpini na kuzungushwa kwa msaada wa mota za umeme,” anasema.

Anasema tofauti iliyopo kati ya teknolojia hizo na ugunduzi wake mpya ni kwamba vifaa hivyo havina uwezo wa kusanifu nguvu halisi ya mvutano ya mfumo wa jua katika anga inayotumiwa na mifumo halisi ya jua, nyota, sayari, vimondo, mwezi na mifumo ya chembe za atomiki.

“Kifaa hiki ndicho pekee chenye ufanisi wa asilimia 100 kwa kusanifu nguvu hiyo chenyewe kwa kutumia nguvu za sumaku pasipo kuhusisha umeme au nishati zingine. Hii ni kwa sababu, kiasilia na kisayansi, jua, sayari na nyota na chembe za atomiki ni sumaku,” anafafanua. Anasema ugunduzi huo pia unalenga kusaidia kubainisha na kusahihisha mapungufu ya baadhi ya taarifa za kisayansi zinazohusu mitaala ya elimu hiyo ya sayansi ya mfumo wa jua.

Anasema katika sayansi inayorasimishwa katika mitaala iliyopo, nadharia nyingi zimekuwa zikifundishwa kimakosa na mara nyingi hutolewa maelezo au majibu ya ubashiri tu pasipo uhakiki wa kimaabara.

“Ni vigumu kuthibitisha kwa sayansi iliyopo katika mitaala ya elimu kuhusu hisabati halisi ya kujipindua kwa mhimili wa dunia ili kuleta majira ya mwaka katika uso wa dunia kutokana na sayansi ya mitaala inafafanua na kutoa majibu ya kiimla tu. “Chanzo cha kujibetua (tilt) kwa mhimili wa dunia (axis) na kuleta majira ya mwaka ni mzunguko wa sayari kulizunguka jua yaani katika muda wa siku 365.24.

Anasema kimsingi matokeo haya ya kujibetua kwa mhimili wa dunia ndiyo elimu ya fizikia na wanasayansi walipaswa kuhakiki hisabati zake ili kubeba wazi chanzo halisi cha kujibetua kwa mhimili wa dunia na sio kutoa maelezo ya kiimla kuwa chanzo ni mzunguko (revolution), kwa sababu mbalimbali. Sababu mojawapo anasema ingewezekana kuwepo kwa majira ya mwaka katika uso wa dunia pasipo kuwepo kwa mzunguko wa dunia (revolution) endapo tu muhimili wa dunia utaweza kubadili vipimo vya egemeo lake la mtazamo wa jua.

“Pia pasingewezekana kuwepo kwa majira ya mwaka katika uso wa dunia endapo nishati ya usumaku wa jua lote, ungekuwa wa daraja moja tu la nishati hivyo uwepo wa mzunguko usingeweza kusaidia kubadili vipimo vya muhimili wa dunia bali muhimili huo ungebaki katika egemeo moja tu la nyuzi 23.5,” anasema.

Serikali kuanzia kutumia kifaa hicho

Akizungumza hivi karibuni wakati wa jopo la wataalamu kutoka Ofisi ya Rais, Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), walipokutana na mgunduzi huyo na kuona namna ya kifaa hicho kinavyofanya kazi, Naibu Waziri Tamisemi, Selemani Jafo anasema serikali itaanza kukitumia mashuleni kifaa hicho kilichobuniwa na Maranya.

Ametoa maagizo kwa wataalamu wa wizara yake na wale wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kuhakikisha kifaa hicho kinaanza kutumika shuleni pamoja na kumpatia mhusika hati miliki. Anasema wanaweza kuanza kwa kufunga kifaa hicho kwenye shule kongwe. Anawataka wataaluma wa Wizara ya Elimu na Tamisemi walinde ugunduzi huo kwani unaweza kuchukuliwa na wazungu na kuufanyia ukarabati kisha wakadai wamegundua wao.

“Angalau tuanze na shule 20 ili wanafunzi wafanye masomo kwa vitendo… Jambo hili ni kubwa sana hivyo ni wajibu wa wataalamu kuona ndani ya miaka mitano kitu kikubwa kikifanyika kutokana na ugunduzi huu,” anasema.

Tanzania kuna vipaji lukuki

Kwa upande wake, Mkuu wa Chuo cha Mafunzo na Ufundi Stadi (Veta) kanda ya kati, Ramadhani Mataka anasema Tanzania ina vipaji vingi lakini vinashindwa kuendelezwa kutokana na mfumo wa elimu uliopo nchini.

Kwa upande wake, Dk Jane Namseda ambaye ni mtaalamu wa lugha, Ofisi ya Rais Tamisemi, anasema mgunduzi huyo amekuja na kitu kizuri hajakipika wala hajaota ndoto na kwamba kinatokana na utafiti mmoja unaofuatia utafiti mwingine. “Hiki ni kitu kikubwa sana nina PhD, lakini sijagundua kitu kama hiki lakini mtu aliyeishia kidato cha nne anagundua mambo makubwa kama haya. Tusipofanya kitu cha kutangaza uvumbuzi wa Tanzania duniani Mungu atatuona,” anasema.

Mtaalamu wa Idara ya Elimu kutoka Tamisemi, Benjamin Oganga anasema kupingana katika utafiti sio dhambi na ndicho kitu kinachotakiwa kufanyika na kwamba ugunduzi huo umehakikiwa na kuthibitishwa na japo la wataalamu kutoka vyuo vikuu na taasisi mbalimbali za utafiti kupitia Wizara ya Sayansi na Teknolojia Chini ya uratibu wa Tume ya Sayansi na Teknolojia (Costech) na kusajiliwa na Wizara ya Viwanda, Biashara kwa hati namba TZ/P/14/00372.

Historia ya Maranya

Akizungumzia historia yake, Maranya anasema: “Nilizaliwa mwaka 1980 mkoani Mara na kukulia Jijini Dar es Salaam. Makuzi yangu ya utotoni hayakuwa na malezi maalumu. Nilipitia malezi ya kuhamahama kwa kupitia mazingira magumu ikiwemo kutumikishwa katika mifugo na kazi ngumu,” anasema. Anasema hali hiyo iliathiri maendeleo yake kielimu na kuwa chanzo cha ulemavu wake wa masikio.

Mwaka 1992 alijiunga na elimu ya msingi na kuhitimu mwaka 1998 katika Shule ya Msingi Ukonga na baadaye, mwaka 1999 alijiunga na shule ya sekondari na kuhitimu mwaka 2002 katika shule ya sekondari ya Benjamin Mkapa. “Matokeo yangu ya kidato cha nne hayakuwa mazuri na ndipo nikajiunga na elimu ya ufundi (Veta ) mwaka 2004. Hiyo ilikuwa ni baada ya Veta kugundua kipaji changu cha ugunduzi na kunichukua kwa nia ya kuniendeleza zaidi kielimu,” anasema.

Kadhalika, anasema Veta walimfadhili kwa masomo ambapo alisomea kozi ya Welding and Metal Fabrication katika mafunzo aliyoanza 2004 hadi 2005 na kutunukiwa cheti. Mwaka 2006 alipewa ufadhili na mamlaka ya Veta kupitia chuo cha Chang’ombe ili kuendeleza utafiti wa pampu ya maji, utafiti ulikamilika mwaka 2007 ukiwa na matokeo makubwa hali iliyomwezesha kutambuliwa ngazi ya taifa kuwa mwanasayansi, mtafiti na mvumbuzi wa sayansi na teknolojia.

Anasema mwaka 2008 alitunukiwa tuzo ya taifa ya sayansi na teknolojia (Tasta Award 2008) na kwamba tangu wakati huo amefanya tafiti mbalimbali akishirikiana na mamlaka ya Veta zilizoleta matokeo chanya. Miongoni mwa tafiti hizo ni ugunduzi wa kifaa hicho kipya cha elimu ya anga, mfumo wa jua na sayari zake.

Umeme wa gesi kuifikisha Tanzania uchumi wa viwanda

Imeandikwa na Fadhili Abdallah, Kigoma | Habari Leo

WAZIRI wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, amesema matumizi ya gesi asilia katika uzalishaji wa umeme nchini yataifikisha nchi kwenye uchumi wa kati kwa kuwa itakuwa ni ya viwanda.

Akizungumza katika kikao cha majumuisho ya ziara yake ya siku tano mkoani Kigoma, akiwa na viongozi wa Serikali na taasisi za Serikali zilizo chini ya wizara yake, Muhongo alisema kwa sasa uhakika wa kuwa na umeme wa uhakika kutokana na gesi asilia upo.

Alisema miradi mbalimbali ya umeme inayotekelezwa nchini ni kielelezo kwamba dhamira ya Serikali kuwa nchi ya viwanda na uchumi wa kati inatekelezeka. Aliwataka wananchi wajiandae kutumia fursa zitakazotokana na kuwepo kwa viwanda vingi nchini.

Akielezea hilo, Profesa Muhongo alisema tayari tafiti zimeonesha gesi asilia iliyopo Ruvu mkoani Pwani ina uwezo wa kuzalisha megawati 10,000, umeme ambao pamoja na matumizi ya nchi, unaweza kuuzwa nje na kuliingizia taifa fedha za kigeni.

Kuhusu utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini, alisema Serikali imeridhishwa na utekelezaji wa mradi huo na kwamba kazi kubwa ya kusafirisha umeme kwenda maeneo mbalimbali ya vijijini imekamilika.

"Natoa wito kwa wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya, wabunge na madiwani kuwahamasisha wananchi kutumia fursa hii kuunganisha umeme kwenye maeneo yao," alisema Profesa Muhongo.

Balozi Mpya wa India Zanzibar Bwana Tek Chand Barupal ajitambulisha rasmi Vuga Mjini Zanzibar

 Balozi  Mdogo Mpya wa India Bwana Tek Chand Barupal wa kwanza kutoka kushoto akizunghumza na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alipofika Ofisini kwake Vuga kujitambulisha rasmi.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akipokea zawadi ya ukumbusho kutoka kwa Mdogo Mpya wa India Bwana Tek Chand Barupal aliyefika ofisini kwake kujitambulisha rasmi.

Picha na – OMPR – ZNZ.



                                    Press Release:-


Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi ameiomba Serikali ya India pamoja na fursa za masomo ya juu inazotoa kwa vijana wa Zanzibar, ikatoa upendeleo maalum wa mafunzo ya uhandisi ili kusaidia kuziba pengo la fani hiyo katika Taasisi za Umma.

Alisema Wahandisi kadhaa wa Zanzibar waliopata mafunzo ya Muda mrefu na kufanyakazi katika idara na Mashirika mengi ya Umma hivi sasa tayari wengi wao wameshastaafu na wengine wako njiani kukamilisha muda wao wa utumishi Serikalini.

Akizungumza na Balozi Mpya wa India Zanzibar Bwana Tek Chand Barupal aliyefika kujitambulisha rasmi hapo Ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar Balozi Seif alisema upungufu huo wa watumishi wa umma wenye fani ya Uhandisi unaweza kuleta msuko msuko endapo hautachukuliwa hatua za haraka.

Balozi Seif  alisema Serikali kupitia baadhi ya Taasisi zake wakati mwengine hulazimika kuendelea kuwatumia wahandisi wenye ujuzi maalum wa muda mrefu licha ya wahandisi hao kufikia muda wao wa kustaafu kitendo ambacho kama hakikuandaliwa mpango maalum wahandisi wapya waliopo nchini wanaweza kukosa uwezo mkubwa wa  kushika nafasi hizo.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar kupitia Balozi Mdogo huyo wa India hapa Zanzibar ameipongeza India kwa jitihada zake za kuendelea kuiunga mkono Zanzibar katika miradi ya Maendeleo akiitaja baadhi yake kuwa ni pamoja na huduma za maji safi pamoja na Kiwanda cha Matrekta.

Alimuahidi balozi Tek kwamba Zanzibar pamoja na Tanzania kwa ujumla zitaendelea kuimarisha ushusiano wa muda mrefu uliopo kati ya pande hizo mbili hasa ikizingatiwa juhudi kubwa zilizochukuliwa na Viongozi waasisi pande hizo mbili katika kuuasisi uhusiano huo.

Hata hivyo balozi Seif alimuomba Balozi Tec Chand Barupal kutumia Diplomasia aliyonayo kuendelea kuyashawishi Makampuni na Taasisi za nchi yake kusaidia miradi mengine ya maendeleo kama kilimo cha umwagiliaji maji, Afya pamoja na Viwanda vidogo vidogo Visiwani Zanzibar.

Mapema Balozi Mpya mdogo wa India aliyepo Zanzibar Bwana Tel Chand Barupal alisema India katika mpango wake wa kuimarisha uhusiano na Mataifa ya Bara la Afrika imeongeza fursa ya masomo kwa Vijana wa Zanzibar  kutoka wanafunzi 60 mwaka 2014/2015 hadi  wanafunzi 75 mwaka 2016/2017.

Bwana Tek alisema utiaji saini mikaba mbali mbali umeshafanyika kati ya Viongozi wa India na Tanzania kwenye miradi tofauti ya Maendeleo na uchumi ikiwa na azma ya kuimarisha uhusiano uliopo wa miaka mingi kati ya pande hizo mbili rafiki.

Balozi mdogo Tek Chand  alimuhakikisha Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar kwamba katika kipindi chake cha utumishi hapa nchini ataongeza ushirikiano na viongozi wa Zanzibar ili kuona kundi kubwa la vijana linajengewa mazingira bora ya kujitegemea kimaisha katika mpango wa Serikali kuu wa kuimarisha mafunzo na miradi ya kazi za amali.





Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
28/09/2016.

Balozi Seif Ali achangia Milioni 13,078,000/- ujenzi wa Jengo la Kisasa la Maabara ya Skuli ya Sekondari ya Kitope

 Mwakilishi wa Jimbo la Mahonda Balozi Seif Ali Iddi pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Kaskazini  “B”  Nd. Issa Juma kushoto yake wakikaguwa maendeleo ya ujenzi wa Msikiti Mkuu wa Ijumaa wa Kijiji cha Fujoni.

 Haiba ya muonekano wa Jengo la Msikiti wa Ijumaa Fujoni  unavyoonekana nje ukiendelea ujenzi wake ambao unatarajiwa kuezeskwa mapema wiki ijayo.

 Balozi Seif kati kati akifafanua jambo wakati wa hafla ya kukabidhi Hundi kwa ajili ya kugharamia uendelezaji wa ujenzi wa jengo la Maabara la Skuli ya Sekondari ya Kitope.

Kushoto ya Balozi Seif ni Mkuu wa Wiaya ya Kaskazini B Nd. Issa Juma na Mkurugenzi wa Idara ya Elimu, Maandalizi na Msingi kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Bibi Safia Ali Rijali.


Kulia ya Balozi Seif ni Mwalimu Mkuu wa Skuli ya Sekondari ya Kitope Mwalimu Suleiman Juma Makame na Msimamizi wa Ujenzi wa Jengo la Maabara ya Skuli za Fujoni na Kitope Nd. Yasir De Costa.

Msimamizi wa Ujenzi wa Majengo ya Maabara ya Skuli za Fujoni na Kitope Nd. Yasir De Costa wa kwanza kushoto akitoa ufafanuzi wa ujenzi wa majengo ya Maabara ya skuli hizo.


Picha na – OMPR – ZNZ.



                                    Press Release:-


Mwakilishi wa Jimbo la Mahonda Balozi Seif Ali Iddi amewakumbusha Viongozi na washirika wa maendeleo katika Sekta ya Elimu kuzijengea uwezo zaidi wa miundombinu skuli mbali mbali Nchini ili ziwe na uwezo kamili wa kuhimili ushindani wa kitaaluma uliopo katika kiwango cha Kitaifa na Kimataifa.

Alisema wakati wa sasa ni ule wa sayansi uliobadilika kabisa Kiteknolojia tofauti na uliopita kiasi kwamba jamii inapaswa kuhakikisha wanafunzi wanasoma katika mazingira yanayokubalika kivifaa pamoja na walimu waliobobea.

Balozi Seif Ali Iddi ambae pia ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alitoa kumbusho hilo wakati akikabidhi Hundi ya shilingi Milioni 13,078,000/- kwa ajili ya ukamilishaji wa Jengo la Kisasa la Maabara ya Skuli ya Sekondari ya Kitope iliyomo ndani ya Jimbo la Mahonda.

Katika hafla hiyo fupi ambayo pia alikabidhi hundi ya shilingi Milioni  1.7 kukamilisha gharama za ujenzi wa Maabara ya Skuli ya Sekondari ya Fujoni kwa msimamizi wake Nd. Yasir De Costa Balozi Seif aliahidi kutoa vifaa vyote vya Maabara kwa Skuli ya Sekondari ya Kitope mara baada ya kukamilika kwa ujenzi huo.

Balozi Seif  alisema Zanzibar kama Nchi nyengine yoyote Duniani inahitaji kuwa na wataalamu wa kutosha katika kusimamia majukumu ya Serikali na hilo litawezekana na kupatikana iwapo watoto wa Taifa hili watajengewa msingi imara wa Taaluma wawapo maskulini.

Mwakilishi huyo wa Jimbo la Mahonda alieleza kwamba Uongozi wa Jimbo hilo daima utakuwa kamini na imara katika kuhakikisha watoto wote wa Jimbo hilo wanapata elimu ya msingi hadi Sekondari kutegemea uwezo halisi wa mwanafunzi husika.

Akitoa shukrani kwa niaba ya Walimu, Wazazi na Wanafunzi wa Skuli ya Sekondari ya Kitope Mwalimu Mkuu wa Skuli hiyo Suleiman Juma Makame alisema msaada huo ni faraja kubwa itakayozaa mafanikio yanayotarajiwa kupatikana katika kipindi kifupi kijacho.

Mwalimu Suleiman alisema Skuli  hiyo ilikuwa ikipata changamoto kubwa la kupoteza fedha zaidi ya shilingi Laki sita hadi Saba kufanya  maandalizi ya vifaa kwa ajili ya matayarisho ya mitihani ya wanafunzi wa Darasa la Kumi na Mbili     { yaani Form IV}.

Kwa upande wake  Msimamizi wa ujenzi wa Majengo ya Maabara ya Skuli za Sekondari Fujoni na Kitope Ndugu Yasir De Costa alisema Jengo la Fujoni limeshakamilika ujenzi wake na tayari lina uwezo wa kutoa huduma ya Maabara kwa kiwango kinachokubalika.

Nd. De Costa aliahidi kwamba ukamilishaji wa jengo la Maabara la Skuli ya Sekondari ya Kitope unaotarajiwa wakati wowote kuanzia sasa utachukuwa takriban wiki Nne.

Naye Mkurugenzi wa Idara ya Elimu, Maandalizi na Msingi Bibi Safia Ali Rijali  kwa niaba ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar  alimpongeza Balozi Seif Ali Iddi kwa jitihada anazochukua katika kusaidia sekta ya Elimu hasa Vikalio, Kompyuta pamoja na vifaa vya Maabara.

Mkurugenzi Safia alisema jitihada zinazochukuliwa na Viongozi, wahisani pamoja na wananchi katika kuunga mkono mapambano dhidi ya kuzitafutia ufumbuzi changamoto zinazoikabili Sekta ya Elimu zinatoa mwanga wa kusaidia Watoto ambao ndio wasimamizi wa Taifa la sasa na lijalo.

Wakati huo huo Mwakilishi wa Jimbo la Mahonda Balozi Seif  alikagua maendeleo ya ujenzi wa Msikiti wa Ijumaa unaojengwa katika Kijiji cha Fujoni na kuridhika na hatua iliyofikiwa ya ujenzi huo.

Fundi Mkuu wa Ujenzi wa Msikiti huo Bwana Mbarouk Said alimueleza Balozi Seif  kwamba uchimbaji wa Kisima pamoja na usogezwaji wa huduma za Umeme zimekamilika na hatua za uwezekaji  zinatarajiwa kuanza wiki ijayo.

Msikiti wa Kisasa wa Ijumaa wa Fujoni utakuwa na uwezo wa kusaliwa na Waumini wa Dini ya Kiislamu  zaidi ya elfu moja kwa wakati mmoja wa sala kwa mujibu wa utafiti wa wataalamu wa masuala ya majengo ya Ibada.


Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
28/09/2016.


UZINDUZI WA WA NDEGE MPYA ATCL

RAIS DKT MAGUFULI AZINDUA RASMI NDEGE MBILI MPYA ZILIZONUNULIWA
NA SERIKALI KWA AJILI YA ATCL JIJINI DAR LEO
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiwa na maafisa na viongozi wengine mbalimbali akikata utepe kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.



 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimshukuru Balozi wa Canada nchini Mhe. Ian Myles baada ya kukata utepe kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli na mkewe Mama Janeth Magufuli wakiingia kwenye ndege mojawapo baada ya kukata utepe kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli na mkewe Mama Janeth Magufuli pamoja na maafisa wengine waandamizi wakiwa kwenye ndege mojawapo baada kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli na mkewe Mama Janeth Magufuli wakitoka kwenye ndege mojawapo na kuelekea ingine baada kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimpongeza mmoja wa wafanyakazi kwenye ndege mojawapo baada kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe akishuka kwenye ndege mojawapo baada kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es salaam Mhe Isaya Mwita akishuka kwenye ndege mojawapo baada ya Rais Magufuli kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es salaam Mhe Isaya Mwita (wa pili kulia) na Meya wa Halmashuri ya Manisapaa ya Temeke Mhe Abdallah Chaurmebo (wa pili kushoto)  pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe Sophia Mjema (kulia) wakijiandaa kupiga picha ya kumbukumbu mara baada ya Rais Magufuli kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli, Mama Janeth Magufuli pamoja na viongozi wengine waandamizi katika picha ya kumbukumbu na watumishi na viongozi wa ATCL mara baada ya Rais Magufuli kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli, Mama Janeth Magufuli pamoja na viongozi wengine waandamizi katika picha ya kumbukumbu na Brass band ya Polisi mara baada ya Rais Magufuli kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli, Mama Janeth Magufuli wakiagana na wafanyakazi wa ATCL baada ya uzinduzi rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.

 
Ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.

Sehemu ya wageni waliohudhuria sherehe za uzinduzi rasmi wa ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.

Sehemu ya wageni waliohudhuria sherehe za uzinduzi rasmi wa ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.

Sehemu ya wageni waliohudhuria sherehe za uzinduzi rasmi wa ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.

Sehemu ya wageni waliohudhuria sherehe za uzinduzi rasmi wa ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Sehemu ya wageni waliohudhuria sherehe za uzinduzi rasmi wa ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Sehemu ya wageni waliohudhuria sherehe za uzinduzi rasmi wa ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Sehemu ya wageni waliohudhuria sherehe za uzinduzi rasmi wa ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Maafisa waandamizi wa  Kikosi cha Anga cha JWTZ  na sehemu ya wageni waliohudhuria sherehe za uzinduzi rasmi wa ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Sehemu ya marunani wa ATCL na wageni waliohudhuria sherehe za uzinduzi rasmi wa ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Burudani ya ngoma wakati  sherehe za uzinduzi rasmi wa ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Sehemu ya viongozi wa kada mbalimbali wakiwa katika sherehe za uzinduzi rasmi wa ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Sehemu ya viongozi wa kada mbalimbali wakiwa katika sherehe za uzinduzi rasmi wa ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Sehemu ya viongozi wa kada mbalimbali wakiwa katika sherehe za uzinduzi rasmi wa ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Burudani ya ngoma wakati  sherehe za uzinduzi rasmi wa ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Burudani ya ngoma wakati  sherehe za uzinduzi rasmi wa ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Bango la kampuni ya Bombadier
Burudani ya ngoma ya Gobogobo wakati  sherehe za uzinduzi rasmi wa ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Balozi wa Canada Mhe. Ian Myles akiongea machache wakati  wa sherehe za uzinduzi rasmi wa ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Balozi wa Canada Mhe. Ian Myles akipigiwa makofi baada ya kuongea  machache wakati  wa sherehe za uzinduzi rasmi wa ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Wanahabaari wakirekodi sherehe za uzinduzi rasmi wa ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Mhandisi John Kijazi akitoa muhtasari  wakati  wa sherehe za uzinduzi rasmi wa ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akiongea machahe na kumkaribisha Rais Dkt. Magufuli kuhutubia  wakati  wa sherehe za uzinduzi rasmi wa ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Spika Job Ndugai akiongea machache wakati  wa sherehe za uzinduzi rasmi wa ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akihutubua wakati wa sherehe za uzinduzi rasmi wa ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akihutubua wakati wa sherehe za uzinduzi rasmi wa ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Marubani wakifurahia wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akihutubua wakati wa sherehe za uzinduzi rasmi wa ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akihutubua wakati wa sherehe za uzinduzi rasmi wa ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Wananchi wakimsikiliza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akihutubua wakati wa sherehe za uzinduzi rasmi wa ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akisisitiza jambo wakati akihutubua wakati wa sherehe za uzinduzi rasmi wa ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Wafanyakazi wa Ndege za Serikali na wa ATCL wakiwa tayari kwa uzinduzi  wakati wa sherehe za uzinduzi rasmi wa ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Wafanyakazi wa ATCL tayari kuanza kazi
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Mhandisi John Kijazi na Katibu Mkuu Uchukuzi Dkt. Leonard Chamuriho wakisaini mikataba ya kukabidhiana  wakati wa sherehe za uzinduzi rasmi wa ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Mhandisi John Kijazi na Katibu Mkuu Uchukuzi Dkt. Leonard Chamuriho wakisaini mikataba ya kukabidhiana  wakati wa sherehe za uzinduzi rasmi wa ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiwa na meza kuu wakisalimia Marubani wakati wa  kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na Marubani wakati wa  kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na Marubani wakati wa  kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na Marubani wakati wa  kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimpongeza Katibu Mkuu Kiongozi kwa kusimamia vyema zoezi wakati wa  kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimpongeza Katibu Mkuu Uchukuzi Dkt leonard Chamuriho kwa kusimamia vyema zoezi wakati wa  kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiendelea kusalimiana na Marubani wakati wa  kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiendelea kusalimiana na Marubani wakati wa  kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiendelea kusalimiana na Marubani wakati wa  kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na Kepteni John Kuipers  wa aliyekuwa rubani wa ndege ya pili kuwasili nchini wakati wa  kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiendelea kusalimiana na Marubani wakati wa  kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiendelea kusalimiana na Marubani wakati wa  kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na wahandisi kutoka kampuni ya Bombadier  wakati wa  kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na wahandisi kutoka kampuni ya Bombadier  wakati wa  kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na mhandisi  Pavel Melicher  kutoka kampuni ya Bombadier  wakati wa  kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Marubani na wahandisi wa kampuni ya Bombadier na ATCL wakielekea kwenye ndege  wakati wa  kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.


Marubani, wahandisi na wafanyakazi wa wa kampuni ya Bombadier na ATCL wakiwa kwenye ndege  wakati wa  kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.



Marubani wa ndege ya pili wakiwa tayari kupaa
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli na mkewe Mama Janeth Magufuli wakitoka  kwenye ndege mojawapo baada ya kukata utepe kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli na mkewe Mama Janeth Magufuli wakisalimiana na wafanyakazi  wa ndege na Waziri wa  Viwanda na Biashara Mhe Charles Mwijage baada ya  kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli na mkewe Mama Janeth Magufuli wakiongozana na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa baada ya kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na Marubani wakati wa  kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na wafanyakazi wa ATCL wakati wa  kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na wafanyakazi wa ATCL wakati wa  kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiwa ameketi ndani ta ndege na mmoja wa wafanyakazi wa ATCL wakati wa  kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akipungia mkono kwa furaha baada ya  kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akipata picha ya kumbukumbu na wafanyakazi wa Wakala wa Ndege za Serikali bada ya  kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli na viongozi wengine akipata picha ya kumbukumbu viongozi wa Mkoa wa Dar es salaam baada ya  kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akipata picha ya kumbukumbu na marubani, wahandisi na wafanyakazi wa ATCL na wa Kampuni ya Bombadier baada ya  kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli na viongozi wengine akipata picha ya kumbukumbu na wafanyakazi wa  ATCL bada ya  kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akipata picha ya kumbukumbu na Brass Band ya Polisi baada ya  kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akipongezwa  na Brass Band ya Polisi baada ya  kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli  akiagana na wafanyakazi wa ATCL  baada ya  kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli  akiagana na wafanyakazi wa ATCL  na wananchi mara baada ya  kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli  akiagana na wafanyakazi wa ATCL  na wananchi mara baada ya  kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli  akiagana na wafanyakazi wa ATCL  na wananchi mara baada ya  kuzindua rasmi ndege mbili mpya aina ya Bombadier Q400 zilizonunuliwa na serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es salaam leo Jumatano Septemba 28, 2016.
PICHA NA IKULU

 
Support : #BegaKwaBegaNaMamaSamia | JAK | CCM Arusha
Copyright © 2011. CCM Dijitali - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Jasper K
Proudly powered by Blogger
Link