NAIBU WAZIRI PINDA AELEKEZA UENDELEZAJI MIJI KUZINGATIA MIPANGO KABAMBE

Na Munir Shemweta, WANMM Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Geofrey Pinda amezielekeza Halmashauri zote nchini kuhakik...

Latest Post

BALOZI KOMBO AKUTANA NA WADAU WA NGO’s JIJINI ROMA

Written By CCMdijitali on Monday, February 28, 2022 | February 28, 2022

Balozi wa Tanzania nchini Italia Mh. Mahmoud Thabit Kombo akipokea zawadi ya kitabu kutoka kwa mmoja wa wadau wa NGO's  mwishoni mwa wiki Jijini Roma, Italia

 
Balozi wa Tanzania nchini Italia Mhe. Mahmoud Thabit Kombo akipokea akiwa katika kikao na wadau wa NGO's mwishoni mwa wiki Jijini Roma, Italia


Na Mwandishi wetu, Roma

Balozi wa Tanzania nchini Italia Mhe. Mahmoud Thabit Kombo amekutana na kufanya mkutano na wadau wa NGO’s takribani sitini na nne zinazofanya shughuli zake nchini Tanzania mwishoni mwa wiki Jijini Roma, Italia.

Mkutano huo ulihudhuriwa pia na wadau mbalimbali wa Diaspora pamoja na wadau wa NGO walimpongeza Mhe. Balozi kwa kuwapa nafasi ya kujitambulisha na kutoa fursa ya kuwasikiliza mafanikio yao sambamba na changamoto wanazopitia katika kufanikisha shughulika zao nchini Tanzania.

Pamoja na kuwasikiliza lakini pia Balozi alitumia nafasi hiyo kuwashauri kuwa na ushirikiano wa pamoja ili kuleta ufanisi zaidi kwenye maeneo wanayo yafanyia kazi. Aidha, katika mkutano huo Balozi Kombo aliongea mubashara na Balozi wa Italia nchini Tanzania  Mhe. Marco Lombardi na kumpa fursa ya kutoa salaam zake moja kwa moja kwa njia ya mtandao.

Balozi wa Italia nchini Tanzania aliwahakikishia wadau hao kuwa wapo kwenye mikono salama ya Balozi wa Tanzania Rome na chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kuwa Tanzania ni nchi salama ya kufanya shughuli zao.

KATIBU MKKU WIZARA YA AFYA ATOA MAAGIZO MKOANI SINGIDA

Written By CCMdijitali on Sunday, February 27, 2022 | February 27, 2022



 

UJENZI WA HOSPITALI YA MKOA SINGIDA ULIOKWAMA UANZE BAADA YA SIKU 7 -KATIBU MKUU AFYA . 

Na.WAF-Singida

Katibu Mkuu Wizara ya Afya Prof. Abel Makubi ameagiza mradi wa ujenzi wa jengo la Magonjwa ya mlipuko la Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida uliokwama uendelee mapema baada ya siku saba. 

Ametoa maagizo hayo leo Mkoani hapa mara baada ya kutembelea ujenzi katika Hospital hiyo na kukutana na Katibu Tawala wa Mkoa, wajumbe wa Bodi ya ushauri ya Hospitali, uongozi wa Hospitali, mshauri elekezi na mkandarasi. 

Mradi wa ujenzi wa jengo hilo ambao ulianza mwaka 2014, umeshindwa kukamilika kwa wakati kutokana na changamoto mbalimbali.

Katika hatua nyingine Prof. Makubi ametoa muda wa siku saba kufungwa kwa mradi unaoendelea wa ujenzi wa ghorofa chini ya Mkandarasi ambaye muda wake pia umeisha na kukiagiza kitengo cha ununuzi na ugavi cha Wizara yake kuhakikisha kuwa mkandarasi wa kuendelea na kazi ya ujenzi anapatikana ndani ya siku saba hadi 14 ili kuendelea na 
ujenzi wa awamu ya pili ya kujenga ghorofa ya kwanza wa jengo hilo.

RAIS SAMIA AKUTANA NA MTENDAJI MKKU WA AIRTEL AFRIKA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa katika mazungumzo na Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Airtel Afrika Olusegun Ogunsanya pamoja na Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Airtel Afrika Mashariki Ian Ferrao leo tarehe 27 Februari, 2022, Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu UAE


 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa katika picha na Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Airtel Afrika Olusegun Ogunsanya pamoja na Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Airtel Afrika Mashariki Ian Ferrao mara baada ya mazungumzo na viongozi hao wa Kampuni ya Airtel Afrika leo tarehe 27 Februari, 2022 Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu UAE


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa katika picha na Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Airtel Afrika Olusegun Ogunsanya na Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Airtel Afrika Mashariki Ian Ferrao pamoja na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Kampuni ya Airtel Tanzania Beatrice Singano mara baada ya mazungumzo na viongozi hao wa Kampuni ya Airtel Afrika leo tarehe 27 Februari, 2022 Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu UAE


 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa katika picha na Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Airtel Afrika Olusegun Ogunsanya na Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Airtel Afrika Mashariki Ian Ferrao pamoja na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Kampuni ya Airtel Tanzania Beatrice Singano mara baada ya mazungumzo na viongozi hao wa Kampuni ya Airtel Afrika leo tarehe 27 Februari, 2022 Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu UAE.


 
Support : #BegaKwaBegaNaMamaSamia | JAK | CCM Arusha
Copyright © 2011. CCM Dijitali - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Jasper K
Proudly powered by Blogger
Link