NAIBU WAZIRI PINDA AELEKEZA UENDELEZAJI MIJI KUZINGATIA MIPANGO KABAMBE

Na Munir Shemweta, WANMM Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Geofrey Pinda amezielekeza Halmashauri zote nchini kuhakik...

Latest Post

Mwanademokrasia wa kweli hahitaji vurugu

Written By CCMdijitali on Friday, October 11, 2013 | October 11, 2013

http://www.nationsonline.org/maps/political_world_map3000.jpg

KATIKA jamii yeyote iliyostaarabika, kutofautiana kimawazo ni jambo lililo la afya katika maendeleo yake ;na ndio msingi wa kupata wazo bora na linaloweza kuboreshwa katika ushindani wa hoja.

Ni tofauti hizo za mawazo kwa wastaarabu, hujenga maslahi na vikundi maslahi katika jamii na hata katika mifumo ya siasa na vyama vya siasa duniani kote.

Ndio maana katika nchi yenye demokrasia, ikiwemo Tanzania, uongozi hauna budi kusikiliza sauti na mawazo mbadala, ili kupata wazo bora linalokubalika la lenye maslahi kwa wote.

Kwa hili, hatuna budi kuipongeza Serikali na hasa Rais Jakaya Kikwete binafsi kwa kuwa kiongozi mwanademokrasia, aliye tayari kusikiliza mawazo ya pande zote, hata kwa wanaomzushia.

Mwishoni mwa wiki iliyopita katika hotuba ya kila mwisho wa mwezi, Rais Kikwete aliendelea kuonesha alivyo mwanademokrasia wa kweli, pale alipowaambia Kambi ya Upinzani, kuwa maoni yao kuhusu Muswada wa Sheria ya Katiba, yanazungumzika.

Aliwaambia kwamba hata baadhi ya maoni hayo, yangeweza kukubalika kama wabunge wake wangekuwepo bungeni, ambako ndio chombo cha kuwasilisha mawazo mbadala na kujenga wazo bora.

Alisema bahati mbaya hawakuwepo, hivyo hapakuwepo mtu wa kusema mawazo yao na baada ya kupoteza fursa yao halali, kutaka kupata ufumbuzi nje ya Bunge ni jambo lisilowezekana. Alisisitiza kuwa masuala yanayohusu Bunge, hujadiliwa na kuamuliwa bungeni na si vinginevyo.

Pamoja na kambi hiyo iliyoundwa na NCCR-Mageuzi, CUF na Chadema, kupoteza fursa halali ya kutoa maoni yao bungeni, ambayo hutumiwa na nchi zote zilizokomaa kidemokrasia, Rais Kikwete amewapa fursa nyingine ya kukutana nao kati ya Jumapili ya Oktoba 13 mwaka huu, ama Jumanne ya Oktoba 15.

Uungwana huu wa Rais Kikwete kwa kweli ni wa kuungwa mkono, lakini pia unapaswa kuigwa na wanasiasa na vyama vyote vya siasa, kama kweli vinataka kushika dola na kuongoza taifa ambalo msingi na uimara wake ni umoja, mshikamano na undugu unaostawi katika jamii yenye utii wa sheria.

Tunasema hivyo kwa kuwa kila mmoja ni shahidi kuwa vyama hivyo havijakomaa kisiasa, kiasi cha kupewa dola, ambayo kuiongoza lazima watu wake wawe na umoja, mshikamano na udugu utakaostawishwa na uongozi unaoamini katika utii wa sheria.

Hakuna ambaye hakusikia viongozi hao, ambao baadhi yao wamewahi kuomba kura ili waongoze taifa hili, wakitamka hadharani kuwa watahamasisha Watanzania wasitii sheria na kubatiza Oktoba 10 mwaka huu kuwa siku ya kutotii sheria.

Tumejiuliza hivi kweli kiongozi anayetaka kuongoza taifa hili, kama ameiva na kukomaa kisiasa, anaweza kutangaza siku ya kutotii sheria?

Siku ambayo haina tofauti na kuhamisha watu kuvunja na kuiba mali za walipa kodi wanaowapa viongozi hao ruzuku kila mwezi kupitia vyama vyao?

Tumesikitika kuona viongozi hao wa vyama vinavyoungwa mkono na wananchi, wakihamasisha wananchi hao hao wasitii sheria, lakini tumefarijika, kusikia wamekubali busara za Rais Kikwete za kukaa meza moja na kumaliza tofauti zao.

Tunashauri kukitokea tofauti tena, ambazo tuna hakika zitatokea katika mambo mbalimbali tu kwa kuwa ndivyo jamii iliyostaarabika ilivyo, basi tuepuke kutoa kauli za namna hiyo, za kushawishi wananchi wasitii sheria, kwa kuwa ni kauli za jabu ambazo hakuna mwanademokrasia makini anayeweza kuziunga mkono.

Diwani wa Chadema mbaroni



WATU tisa akiwemo Diwani wa Kata ya Old Moshi Magharibi, Elisaria Mosha (Chadema) wametiwa mbaroni wakituhumiwa kupokea fedha kwa njia ya udanganyifu kupitia mradi wa umeme mkoani Kilimanjaro.

Hatua hiyo imechukuliwa baada ya Makamu wa Rais Dk Mohamed Gharib Bilal, kufanya ziara mkoani Kilimanjaro na kuagiza watu waliofanya hivyo wakamatwe mara moja.

Akizungumza na waandishi wa habari jana ofisini kwake, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kilimanjaro, Robert Boaz alisema diwani huyo anatuhumiwa kujipatia Sh milioni 9.6 kwa njia ya udanganyifu.

Wengine wanaoshikiliwa ni Zakayo Kimathi (52) mkazi wa Mandaka, anayedaiwa kupokea Sh milioni 10.3, Oforo Kimambo (56) mkazi wa Mandaka anayedaiwa kupokea Sh milioni 29.

Wengine wanaotuhumiwa kupokea malipo hayo kwa njia ya udanganyifu ni Daud Mallya (69) mkazi wa Chekereni aliyepokea Sh milioni 8.6, Richard Mlaki (69) mkazi wa Kiboroloni alipokea Sh milioni 18.6 na Focus Herman (88) mkazi wa Kilototoni aliyepokea Sh milioni 36.

Boaz alisema kwa sasa watuhumiwa watatu hawajapatikana. Alieleza kuwa pamoja na watuhumiwa hao, polisi imemkamata Mwenyekiti wa Kijiji cha Mandaka Monono, Hassan Nduva (41) na Ofisa Mtendaji wa kijiji hicho, Vendelini Shayo (58) kwa kuhusika kufanikisha malipo hayo.

Dk Bilal alitoa agizo hilo mapema wiki hii wakati akizindua vituo vya kupozea na kusambaza umeme maeneo ya Kiyungi, YMCA na Makuyuni.

Alipokea taarifa kwa Mkuu wa Mkoa kuwapo kwa wananchi ambao hawakulipwa fidia zao, kutokana na kuwapo watu waliotumia ujanja wa kupokea fedha hizo, Sh milioni 169.2.

“Halmashauri ya Moshi Vijijini ndio ilikuwa wakala wa malipo hayo na ndio iliyofanya tathmini kwa kushirikiana na watendaji wa vijiji, ambapo wao walipeleka tathmini hiyo kwa Shirika la Umeme (Tanesco), ambalo lilitoa fedha hizo hivyo Tanesco hawahusiki,” alisema,” alisema Boaz.

Mangula: CCM toeni jasho msisubiri uchaguzi



MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) upande wa Bara, Phillip Mangula, amewataka viongozi wa chama hicho kuhakikisha wanafanya ziara za mara kwa mara ili kukiimarisha chama hicho.

“Hiki ndio kipindi cha kutoa jasho jingi na kukijenga chama na si kusubiri kipindi cha uchaguzi, ndio watu waanze kupita kwa wanachama kuanza kukijenga chama,” alisisitiza Mangula.

Alitoa agizo hilo Dar es Salaam jana katika siku ya pili ya ziara yake mkoani Dar es Salaam, ambapo alianza na wilaya za Kinondoni na Ilala.

Akizungumza na wajumbe wa Halmashauri ya CCM ya Wilaya ya Ilala, alisema viongozi wengi wa chama hicho, hawafanyi juhudi za kukutana na wananchi au kufanya ziara za mara kwa mara na hivyo kutoa mianya kwa vyama vya upinzani kupotosha jamii.

Alikemea tatizo la makundi ndani ya chama hicho na kutaka jitihada zifanyike ili yaweze kuvunjwa, kwani yakiachwa yanaweza kuathiri chama hicho katika uchaguzi ujao.

Akitoa taarifa ya chama, Katibu wa CCM Wilaya ya Ilala, Ernest Chale alisema hali ya kisiasa katika wilaya hiyo, inaridhisha, japo utekelezaji katika baadhi ya maeneo bado unasuasua.

Alitaja mambo yanayosababisha changamoto katika utekelezaji katika wilaya hiyo kuwa ni miundombinu ya barabara, upandaji wa ushuru wa uzoaji taka na maji taka.

MKUTANO WA SITA WA VYAMA VILIVYOKUWA VYA UKOMBOZI KUZINI MWA AFRIKA WAFANYIKA DAR

Written By CCMdijitali on Thursday, October 10, 2013 | October 10, 2013


 Katibu Mkuu wa sasa wa CCM, Abdulrahman Kinana, akisalimiana na Katibu Mkuu mstaafu Willson Mukama, walipokutana kwenye Mkutano wa sita wa Makatibu Wakuu wa vyama vilivyokuwa vya Ukombozi Kusini mwa Afrika, leo katika hoteli ya Kunduchi Beach, Dar es Salaam. Kushoto ni Katibu wa NEC, Oganaizesheni CCM, Mohamed Seif Khatib
 
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahmani Kinana akizungumza jambo na Katibu Mkuu wa Chama Cha FRELIMO cha Msumbiji, Philipe Paunde wakati wa mkutano huo
 
 Katibu wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro akishauriana jambo na Makatibu wenzake wa NEC, Zakia Meghji (Uchumi na Fedha) na Mohamed Seif Khatib (Oganaizesheni ) wakati wa mkutano huo. nyuma ni Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM, Sixtus Mapunda.
 
 Katibu Mkuu wa chama cha ZANU-PF cha Zimbabwe, Dydmus Mutasa akiwa kwenye mkutano huo.
 
Katibu Mkuu mstaafu wa CCM, Wilson Mukama akisalimiana na Dk. Asha-Rose Migiro wakati wa mkutano huo.
 
 Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akizungumza na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Uhusiano wa Kimataifa wa Chama Cha Kikomunisti cha Jamhuri ya Watu wa China, Ai Ping, wakati wa mkutano huo
 
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akizungumza na Ai Ping wa chama cha CPC cha china wakati wa mkutano huo. Katikati ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM (zanzibar), Vuai Ali Vuai
 
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiwaelekeza jambo, Katibu wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa CCM, Dk. Asha-Rose Migiro na Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, wakati wa mkutano huo.
 
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akizungumza kabla ya kuanza kwa kikao hicho
 
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akifungua mkutano wa sita wa Makatibu wakuu wa vyama vilivyokuwa vya ukombozi kusini mwa Afrika, leo kwenye hoteli ya Kunduchi Beach, Dar es Salaam. Kushoto ni Katibu wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa CCM, Dk. Asha-Rose Migiro na Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Zanzibar, Vuai Ali Vuai.
 
Mkutano huo ukiendelea katika hoteli ya Kunduchi Beach

Mwenyekiti wa Mkutano wa Sita wa Vyama vilivyokuwa vya Ukombozi Kusini mwa Afrika, Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiendesha mkutano huo, leo katika hoteli ya Kunduchi Beach, jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Zanzibar Vuai Ali Vuai na kulia ni Katibu wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa CCM, Dk. Asha-Rose Migiro.
 
Baadhi ya washiriki wakiwa kwenye mkutano huo
 
 VIONGOZI wa vyama vilivyokuwa vya Ukombozi Kusini mwa Afrika, walioshiriki kwenye mkutano wa sita wa vyama hivyo, leo kwenye hoteli ua Kunduchi Beach, jijini Dar es Salaam, Kutoka kushoto, Katibu Mkuu wa Chama Cha ANC cha Afrika Kusini, Gwede Mantash, Katibu Mkuu wa chama cha ZANU-PF cha Zimbabwe, Didy Mutasa, Naibu wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Chana Cha Kikomunisti cha China, Ai Ping,Katibu Mkuu wa MPLA cha Angola, Julio Paulo. Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, Katibu Mkuu wa chama cha FRELIMO cha Msumbiji, Philipe Paunde na Katibu Mkuu wa Chama cha SWAPO cha Namibia,Nangolo Mbumba
 
Makatibu wakuu wa vyama vilivyokuwa vya ukombozi kusini mwa Afrika, wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wengine waandamizi, baada ya ufunguzi wa mkutano huo.
 
Katibu Mkuu wa Chama Cha ZANU-PF, Didy Mutasa akionyesha alama ya hamasa ya chama chake, alipozungumza na waandishi wa habari, wakati wa mkutano wa makatibu wakuu wa vyama vilivyokuwa vya ukombozi mwa kusini mwa Afrika, kwenye hoteli ya Kunduchi Beach, Dar es Salaam. Kushoto ni Katibu Mkuu wa CCM, Andulrahman Kinana na Wanne kushoto ni Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye.

JK azindua Shule ya Sekondari ya Miono, Bagamoyo

http://4.bp.blogspot.com/-v-L_4CRpOLU/UlZhm9_XAoI/AAAAAAAE0BE/GGLTGF5M5lw/s1600/D92A6377.jpg
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akifunua kitambaa katika jiwe la msingi kuizindua rasmi shule ya sekondari ya Miono iliyopo Wilayani Bagamoyo, akishuhudiwa na  Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Mhe Philipo MulugoRais Kikwete yupo katika ziara ya kikazi Mkoa wa Pwani.
 http://3.bp.blogspot.com/-qnoN6yU6etc/UlZh3mFdW7I/AAAAAAAE0BQ/IpKFNokArfE/s1600/D92A6347.jpg
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akikagua maktaba ya Shule ya Sekondari ya Miono Muda mfupi baada ya kuizindua shule hiyo jana Wilayani Bagamoyo Mkoa wa Pwani
 http://2.bp.blogspot.com/-xKIoS-AAAgY/UlZhm3GGZ6I/AAAAAAAE0BA/kyGvp1OxBFI/s1600/D92A6311.jpg
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na  wanafunzi wa kidato cha tano wanaosoma Shule ya Sekondari ya Miono Wilayani Bagamoyo, Nyekwabi Jackline George,Penina Odara na Magret Machinyita wakitoa maelezo ya jaribio la sayani somo la biolojia wakati Rais alipofungua rasmi shule hiyo. Picha na mdau Freddy Maro wa Ikulu
 
Support : #BegaKwaBegaNaMamaSamia | JAK | CCM Arusha
Copyright © 2011. CCM Dijitali - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Jasper K
Proudly powered by Blogger
Link