NAIBU WAZIRI PINDA AELEKEZA UENDELEZAJI MIJI KUZINGATIA MIPANGO KABAMBE

Na Munir Shemweta, WANMM Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Geofrey Pinda amezielekeza Halmashauri zote nchini kuhakik...

Latest Post

Uhamiaji wasafishwa Dar na Kilimanjaro

Written By CCMdijitali on Wednesday, February 24, 2016 | February 24, 2016

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga

Na Habari Leo

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga ameagiza watumishi wa Idara ya Uhamiaji walioko katika viwanja vya ndege vya kimataifa vya Julius Nyerere (JNIA), Dar es Salaam na Kilimanjaro (KIA), wahamishwe na kupelekwa maeneo mengine nchini, wakiwemo wale wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano.

Katika maagizo ya waziri huyo, amesisitiza kuwa anataka kuwepo na mabadiliko makubwa katika vitengo mbalimbali vya idara ya uhamiaji ili kuboresha huduma na kuimarisha uadilifu katika vitengo hivyo.

Aidha, utafiti uliofanywa hivi karibuni, umeonesha kuwa matatizo ya rushwa katika idara ya uhamiaji, yanashika nafasi ya kwanza kwa kuwa na asilimia 30, asilimia 20 ni uongozi mbovu na asilimia 20 ni matumizi mabaya ya madaraka.

Kitwanga alitoa maagizo hayo Dar es Salaam jana, alipozungumza katika kikao cha ndani na viongozi wa idara ya uhamiaji na viongozi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, wakiwemo Wakuu wa Idara na Vitengo vya Wizara.

Pamoja na watumishi hao wa Idara ya Uhamiaji wa viwanja hivyo vya ndege kutakiwa kuhamishwa, wengine walioagizwa na waziri huyo kuhamishwa ni kutoka Kitengo cha Pasipoti, Uhasibu, Hati za Ukaazi na Kitengo cha Upelelezi, vyote vya Makao Makuu ya Uhamiaji jijini Dar es Salaam.

Aidha, ameagiza pia kuwa Wakuu wote wa Vitengo vya Upelelezi vya wilaya zilizopo jijini Dar es Salaam, Tunduma, Mtukula, Holili na Kasumulo, wahamishiwe maeneo mengine, wakiwemo watumishi wote waliokaa kwa zaidi ya miaka mitatu katika vituo hivyo.

“Hatua hii inayochukuliwa ni mwanzo tu wa mabadiliko makubwa yatakayofanywa katika Idara ya Uhamiaji ili kuboresha huduma zinazotolewa na Idara hii ambayo ni moja ya Idara muhimu za Serikali,” alisisitiza Kitwanga.

Alisema katika kuisafisha idara hiyo, uangalifu mkubwa utachukuliwa ili kuhakikisha kuwa hakuna mtumishi anayeonewa wala kupendelewa, lengo likiwa ni kuvunja mtandao wa wapokea rushwa na wasiowajibika.

Alisema kutokana na utafiti uliofanywa hivi karibuni, umeonesha kuwa matatizo ya rushwa katika Idara ya Uhamiaji yanashika nafasi ya kwanza kwa kuwa na asilimia 30, asilimia 20 ni uongozi mbovu na asilimia 20 ni matumizi mabaya ya madaraka.

Aidha, alisema asilimia 15 inahusisha vitendea kazi, mifumo hafifu ya kufanya kazi, asilimia 10 huduma mbovu na asilimia tano ukabila na upendeleo.

Aliwataka viongozi na watumishi wote katika idara hiyo kufanya kazi zao kwa kuzingatia sheria, kanuni na maadili ya kazi na kuepuka vitendo vya kupokea rushwa na kusaidia wahamiaji haramu na wauza dawa za kulevya.

Nape: Maslahi tasnia ya habari kulindwa

Written By CCMdijitali on Monday, February 22, 2016 | February 22, 2016

 
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye


Imeandikwa na Halima Mlacha -Habari Leo

WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye amesema Serikali ya Awamu ya Tano itahakikisha maslahi ya wanahabari na tasnia ya habari nchini vinalindwa na kupewa uhuru wa kutosha lakini kwa kutanguliza maslahi ya taifa.

Pia amebainisha kuwa Muswada wa Sheria ya Kusimamia Vyombo vya Habari uko katika hatua za mwisho baada ya kushirikisha na kujumuisha mapendekezo ya wadau wa habari na kusisitiza kuwa endapo sheria hiyo itapitishwa itakuwa ni sheria bora itakayoijenga tasnia hiyo na itadumu kwa muda mrefu.

Amevitaka vyombo vya habari nchini kutumia fursa iliyopo kuibua matatizo yaliyopo kwenye jamii na hivyo Serikali kuvitumia kama sehemu ya kupatia taarifa na kuzifanyia kazi kwa maslahi ya Watanzania na Taifa kwa ujumla.

Nape aliyasema hayo juzi usiku katika kipindi cha Siku 100 za Rais John Magufuli madarakani katika sekta ya habari, utamaduni, sanaa na michezo kilichorushwa na televisheni ya Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC).

Alisema tangu Rais John Magufuli aingie madarakani amekuwa akiishi yale anayoyazungumza na hivyo ndivyo Serikali yake itakavyokuwa kwani hata yeye tangu alipoteuliwa kuwa Waziri wa Habari aliahidi kuijenga na kuilinda tasnia hiyo jambo ambalo ameapa kulifanikisha.

“Nawahakikishia wanahabari kwamba wako salama chini ya Serikali ya Awamu ya Tano na uongozi wake,” alisisitiza.

Alisema alipoanza kazi ya uwaziri, alikutana na makundi mbalimbali ya wadau wa habari wakiwemo wanahabari na wahariri wa habari lengo likiwa ni kukusanya na kuangalia mambo ambayo hayako sawa katika tasnia hiyo na kupokea maoni yao yaingizwe kwenye Muswada wa Sheria ya Habari.

Alisema kupitia maoni aliyoyakusanya kutoka katika makundi hayo ya wadau wa habari, mapendekezo yao yamefanyiwa kazi kwa kutumika kwenye muswada wa sheria hiyo ya habari ambayo iko katika hatua za mwisho na inatarajiwa kuwasilishwa bungeni.

Alisema sheria hiyo ya habari kwa kuzingatia mapendekezo hayo, itakuwa ni sheria nzuri, bora na itakayoijenga tasnia ya habari, na ni sheria itakayochukua muda mrefu kufanyiwa marekebisho kutokana na ubora wake.

Akizungumzia uhuru wa vyombo vya habari, alisema uhuru huo ulianza kupanuliwa tangu Serikali zilizopita ikiwemo ya Awamu ya Nne na umekuwa ukitekelezwa kwa kuzingatia sheria zilizopo za habari na maslahi ya taifa.

Alisema ndani ya Serikali ya Awamu ya Nne, uhuru wa vyombo vya habari nchini ulipanuliwa kwa wigo mkubwa ikilinganishwa na nchi nyingine za Afrika.

“Najua kumekuwa na malalamiko mengi hasa ndani ya siku hizi 100 za Mheshimiwa Rais, pale nilipolifungia gazeti la Mawio. Nilichukua hatua ile baada ya kupitia kwa umakini mwenendo mzima wa gazeti lile na kwa kweli lilikuwa na makosa na ndio maana hata baada ya hatua kuchukuliwa, Mawio wenyewe hawapigi kelele wanaopiga kelele ni wengine,” alisisitiza.

Alisema gazeti lile mwenendo wake wa uandishi ulikuwa hauendani na maadili ya uandishi wa habari na kukiuka sheria ya vyombo vya habari kupitia taarifa zake mojawapo ikiwemo ya kumtangaza kinyume cha Sheria ya Uchaguzi mgombea wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad kuwa ndiye Rais mteule wa Zanzibar.

Aidha, alisema pia alifuatilia mwenendo wa namna gazeti hilo linavyojibu barua za kulionya na kuonekana kama linajibizana na Msajili wa Magazeti na hata lilipoandika habari ya kumtangaza Maalim Seif kuwa Rais wa Zanzibar, majibu yake ya kujieleza yalikuwa ni ya kejeli na kiburi.

“Walipoandikiwa barua ya kujieleza kuhusu habari hiyo yenye uchochezi, walijibu eti wanaishangaa Serikali kwa nini inahoji wao kumtangaza mshindi Zanzibar, na kusisitiza kuwa walipaswa kupongezwa. Huu ni uhaini kutangaza Rais bila kuwa na mamlaka. Huu ni uchochezi na ndio maana tulichukua hatua,” alisema Nape.

Alisema pamoja na kwamba sheria iliyotumika kulifungua gazeti hilo inalalamikiwa akiwemo yeye mwenyewe kutoridhika nayo, ni vyema vyombo vya habari vitakatambua kuwa sheria hiyo bado ipo hadi pale utakapopitishwa Muswada wa Sheria ya Habari.

Alivitaka vyombo vya habari kuitekeleza kwa vitendo changamoto aliyoitoa Rais Magufuli wakati akizungumza na wazee hivi karibuni, kwa kuandika habari za utafiti zinazoibua masuala nyeti yanayohitaji kufanyiwa kazi na Serikali kwa maslahi ya wananchi na taifa kwa ujumla.

“Hata mheshimiwa Rais Magufuli alisema tutumie vyombo vya habari kupata taarifa muhimu za kufanyia kazi. Ili Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Dk Magufuli ifanikiwe, ni lazima itoe uhuru wa kutosha kwa vyombo vya habari kufanya kazi zake,” alisema Nape.

Katika hatua nyingine, Nape amesema Serikali imejipanga kuhakikisha Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) linakuwa chombo cha kuaminika na linafanya kazi zake kuendana na kasi ya utendaji wa Serikali hiyo.

Aidha, amesema imepanga kuanza kulipa madeni yote ambayo shirika hilo na Shirika la Magazeti ya Serikali, Tanzania Standard Newspapers (TSN) wachapishaji wa magazeti ya Daily News, SpotiLeo na HabariLeo, inaidai Serikali ili mashirika hayo yajiendeshe kwa ufanisi.

Nape alisema katika kufanikisha azma hiyo tayari akiwa Waziri mwenye dhamana ameunda Bodi mpya ya TBC na Rais Magufuli ameshamteua Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Balozi Herbert Mrango baada ya Bodi iliyopita kumaliza muda wake kwa mujibu wa sheria.

“Tunataka TBC kuwa chombo cha umma kinachoaminika nchini kuanzia kwenye vipindi na taarifa za habari na matukio. Kila Mtanzania anaona kasi ya Serikali ya Awamu ya Tano. Ni kasi kubwa hata taasisi zilizo chini ya wizara zetu ikiwemo TBC, tunataka ziende na kasi hiyo,” alisisitiza Nape.

Pamoja na hayo, Waziri Nape alisema Serikali inatambua kuwa shirika hilo linakabiliwa na tatizo la uchakavu wa mitambo na kukabiliwa na madeni makubwa ambayo taasisi za Serikali zinadaiwa na kuahidi kulifanyia kazi.

“Tayari Rais Magufuli ameagiza madeni yote ambayo TBC inadai taasisi za Serikali yaanze kulipwa pamoja na madeni ambayo Shirika la Magazeti la Serikali (TSN) linazidai taasisi hizo. Mashirika haya yanaidai Serikali fedha nyingi inabidi yalipwe ili yafanye kazi zake kwa ufanisi,” alisisitiza.

Jecha: Tunamtambua Maalim Seif mgombea


Mwenyekiti wa ZEC, Jecha Salim Jecha


Imeandikwa na Mwandishi Wetu, Zanzibar na Habari Leo

LICHA ya Chama cha Wananchi (CUF) na vyama vingine sita vya siasa kuandika barua ya kueleza kutoshiriki Uchaguzi Mkuu wa marudio uliopangwa kufanyika Machi 20, mwaka huu, Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha amesema ofisi yake bado inawatambua wagombea wa vyama hivyo.

“Mgombea Urais wa CUF na wagombea wake wa Baraza la Wawakilishi na Madiwani, na vyama vingine sita waliandika barua kwa ZEC wakisema hawatashiriki uchaguzi huo. Kwa bahati mbaya, wagombea wote na vyama vyao vya siasa vinavyodai kususia, wameshindwa kufuata taratibu.

“Inaelezwa wazi katika Kifungu cha 31 na 37A na Sura ya 46 na 50 ya Sheria ya Uchaguzi ya Zanzibar, kuhusu taratibu za uteuzi wa wagombea na jinsi gani wagombea wanaweza kujitoa katika uchaguzi. Hakuna hata mgombea mmoja aliyefuata sheria hiyo,” alisema Jecha katika taarifa yake kwa vyombo vya habari jana.

Jecha alisema kulingana na kanuni, ni jukumu la chama cha siasa kuandika kwa ZEC kuhusu kuondoa udhamini wake kwa mgombea. Alisema hata CUF ambayo mgombea wake ni Maalim Seif Shariff Hamad, imeshindwa kufuata kanuni hizo.

“Ni muhimu sana kuelewa na kufuata sheria za uchaguzi. Tumekuwa tukiwasiliana na vyama vyote 14 vya siasa, sambamba na kusambaza vifaa vya uchaguzi kwa wilaya zote kumi na moja kabla ya kuvitawanya baadaye kwenye vituo 1,580 vya kupigia kura,” alisema Jecha.

Alisema wagombea wote 14 wa urais, watu wanaowania Uwakilishi kutoka katika majimbo 54 na wagombea 111 katika ngazi ya Udiwani, bado wanaendelea kutambulika kama wagombea halali kwa uchaguzi wa mwezi ujao.

Jecha amekiri kupokea barua kutoka CUF na vyama vingine sita wakisema hawatashiriki uchaguzi huo, wakati vyama vingine vinane kikiwamo CCM, ACT, ADC CCK AFP, SAU, TLP na ADA-TADEA vimethibitisha kushiriki.

“Tunakamilisha taratibu ili kuwapatia wagombea wote wa urais ulinzi kwa saa 24 hadi wakati matokeo ya uchaguzi yatakapokuwa yametangazwa,” alisema Jecha na kuongeza kuwa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura litawekwa katika sehemu mbalimbali ili wapiga kura waone vituo vyao vya kupigia kura.

Alisema kuwa maandalizi kwa ajili ya marudio ya uchaguzi huo yanaendelea vizuri na tayari uteuzi na kuajiri maofisa wa uchaguzi na wafanyakazi wengine umefanyika na kufuatiwa na mafunzo kuhusu jinsi gani ya kusimamia vizuri uchaguzi.

Alisema mafunzo kwa ajili ya wasimamizi wa uchaguzi (ngazi ya majimbo) yanatarajiwa kuanza leo hadi Februari 28, wakati mafunzo kwa maofisa wa vituo vya kupigia kura yataanza Machi 11 hadi 13, mwaka huu.

Mafunzo kwa ajili ya mawakala wa vyama vya siasa na maofisa wa kusimamia usalama yatafanyika Machi 14 na 15, mwaka huu, kwa mujibu wa Mwenyekiti huyo wa ZEC.

Mwenyekiti huyo wa ZEC alisema maandalizi ya awali ya kuchapisha karatasi za kura yamekamilika, na mchapaji ambaye hakutaka kumtaja anaendelea na kazi ya kuchapa karatasi hizo ambazo zinatarajiwa kuletwa Zanzibar mapema mwezi ujao.

“Tunawaomba wananchi wajiandae kwa uchaguzi wa marudio na wagombea wote kutoka vyama tofauti vya siasa kufuata kanuni na sheria za uchaguzi,” alisema Jecha.

Uchaguzi huo wa marudio wa Machi 20, mwaka huu utafanyika baada ya ule wa Oktoba 25, mwaka jana, kufutwa kutokana na kasoro mbalimbali zilizoufanya usiwe huru na wa haki. Juhudi za kuwapata wasemaji wa CUF jana hadi tunaenda mitamboni hazikufanikiwa.

Wabunge na Maseneta wa Bunge la Marekani wamuombea Rais Magufuli

Written By CCMdijitali on Saturday, February 20, 2016 | February 20, 2016


Wabunge na Maseneta wa Bunge la Marekani wakimuombea Rais Magufuli, ili aweze kufanya kazi zake vizuri walipotembelea ofisi za Spika wa Bunge kwa mazungumzo mafupi jana. Rais Magufuli siku zote amekuwa akisisitiza na kuomba wananchi wamuombee.

Rwanda wampongeza Magufuli

Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Dk Agustine Mahiga


Imeandikwa na Katuma Masamba - Habari Leo

 WAFANYABIASHARA wa Rwanda wamepongeza hatua zinazochukuliwa na Rais John Magufuli katika Bandari ya Dar es Salaam, kwa kuimarisha ufanisi wa bandari, kukuza biashara baina ya Tanzania na nchi jirani.

Aidha wamesema tangu Rais Magufuli aanze kuchukua hatua hizo, mizigo yao imekuwa salama zaidi na wamefanikiwa kuipata kwa urahisi tofauti na zamani ambapo mingi ilikuwa ikipotea.

Hayo yalielezwa jana na Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Augustine Mahiga wakati akizungumza na waandishi wa habari katika Ukumbi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA).

Akizungumza baada ya kutua nchini akitokea Kigali, Rwanda, Balozi Mahiga alisema pia Rais wa nchi hiyo, Paul Kagame amemhakikishia kuwa ataendelea kushawishi wafanyabiashara wake kutumia Bandari ya Dar es Salaam, ili kukuza uhusiano wa kibiashara uliopo.

“Nilipata bahati ya kuzungumza na wafanyabiashara wa kule... wamepongeza sana hatua zinazochukuliwa na Rais Magufuli pale bandarini kwa sababu wanasema sasa hivi itawasaidia sana kuhakikisha usalama wa mizigo yao,” alisema Blozi Mahiga.

Alisema wafanyabiashara hao pia wameomba mkutano wa pamoja na wenzao wa Tanzania, ili kujadili masuala mbalimbali, ikiwemo fursa za uwekezaji ndani ya Rwanda na Tanzania.

Alisema Rais Kagame anaunga mkono ujenzi wa reli itakayotumika kusafarisha mizigo kwa kuwa ni njia mojawapo ya kukuza uchumi wa nchi hizo mbili rafiki.

Akizungumzia safari yake hiyo, Balozi Mahiga alisema, alienda nchini humo kujadiliana masuala mbalimbali aliyoagizwa na Rais Magufuli kwa Rais wa nchi hiyo, ambapo walijadili masuala matatu, ikiwemo machafuko yanayoendelea Burundi.

Alisema kuhusu machafuko ya Burundi, Rais Kagame alikanusha tuhuma zinazotolewa na nchi hiyo pamoja na jumuiya za kimataifa kuwa anahusika katika kuchochea machafuko hayo.

Kwa mujibu wa Balozi Mahiga, maandamano ya nchi nzima yaliyofanyika wiki iliyopita nchini Burundi ya kuishutumu Rwanda kuhusika na machafuko nchini mwao, yalishitua nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), kutokana na baadhi ya maneno ya chuki yaliyokuwa yakitolewa na wananchi hao dhidi ya nchi hiyo.

Alisema hali hiyo, ilihofiwa kwamba ingeweza kuvunja mazungumzo ya kutafuta suluhu yanayoendelea.

“Nilimuuliza Rais Kagame kuhusu hili suala, akasema hatachukua hatua yoyote licha ya kwamba wananchi wake wamemlazimisha kufanya kitu. Lakini alisema atashiriki katika majadiliano ya kutafuta suluhu ya Burundi. “Sisi tulikuwa tunahofia kuwa huenda akachukua hatua ambazo zingeweza kuleta matatizo na hata mazungumzo yanayoendelea kuvunjika, lakini ameniambia hatachukua hatua yoyote inayoweza kusababisha kuvunjika kwa uhusiano,” alisema Balozi Mahiga.

Hata hivyo, alisema Rais Kagame alilalamikia nchi yake kushutumiwa kwa kutoa mafunzo ya kijeshi kwa wakimbizi wa Burundi, ili kuipindua Serikali ya nchi hiyo na kutaka Jumuiya za Kimataifa, kuwaondoa wakimbizi zaidi ya 70,000 na kuwahamishia nchi nyingine za jirani.

“Aliniambia kuwa kuendelea kuwa na hawa wakimbizi katika nchi yake, kunaweza kumletea matatizo makubwa, kwa sababu amekuwa akilaumiwa sana. Hivyo kuliko lawama, ni bora hizi Jumuiya za Kimataifa zikawaondoa wakimbizi,” alisema.

Alisema kwa mujibu wa Rais Kagame, Rwanda itaendelea kushiriki katika mijadala mbalimbali ya kutafuta suluhu ya Burundi na itahakikisha Burundi inakuwa salama.

Jambo lingine walilozungumza na Rais Kagame ni mkutano wa marais wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki, unaotarajiwa kufanyika mwisho wa mwezi nchini Tanzania, ambapo pia alikuwa katika hatua ya mwisho katika kukamilisha ajenda na watakaoshiriki mkutano huo.

Waziri Mkuu Majaliwa aibukia bandari ya Tanga

 Matishari matatu ambayo Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ametaka apewe maelezo kwa maandishi kuwa ni nani aliyeidhinisha mchakato wa manunuzi yake bila kuzingatia viwango na ubora uliokusudiwa na serikali.. (Picha na ofisi ya Waziri Mkuu)

Na Habari Leo

WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amefanya ziara ya kushitukiza ya kukagua Bandari ya Tanga na kumtaka Mkuu wa Bandari hiyo (Port Master), Henry Arika ampelekee maelezo kuhusu ukiukwaji wa ununuzi wa tishari ifikapo leo saa 6 mchana.

Waziri Mkuu ambaye aliwasili Tanga jana mchana kushiriki maziko ya Mzee Ally Mwalimu Makwaya, ambaye ni baba mzazi wa Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, aliamua kuzuru bandari hiyo kabla ya kuelekea uwanja wa ndege akiwa njiani kurejea Dar es Salaam.
Katika ziara hiyo fupi, Waziri Mkuu alikataa kuingia ofisini (bandarini) na akataka apelekwe mahali tishari tatu za bandari hiyo zilipo.

Katika maswali aliyoulizwa na Waziri Mkuu, Arika alikiri kuwa matishari hayo hayafanyi kazi kama inavyotakiwa kwa sababu yanasubiri kusukumwa na tugboat (meli ndogo).

“Nataka kesho saa 6 mchana uniletee barua yenye maelezo ni kwa nini mlinunua tishari tatu ndogo badala ya mbili kubwa, wakati mnajua Serikali ilitenga Dola za Marekani milioni 10.113, kwa ajili ya kununua tishari mbili zenye uwezo wa kujiendesha zenyewe. “Nataka maelezo ni kwa nini mlizinunua tangu mwaka 2011 lakini zimekaa bila kufanya kazi hadi Novemba mwaka jana? 

Na kwa nini mnaendelea kutumia fedha za Serikali kwa kukodisha tishari kutoka Mombasa, badala ya kutengeneza za kwenu au kufundisha vijana wa Kitanzania? Kwani tunao wahitimu wangapi wa fani hii?” Alihoji Waziri Mkuu.

Waziri Mkuu Majaliwa alisema anazo taarifa kwamba moja ya tishari lilidondoka baharini, wakaenda kutafuta huko na kulivuta hadi pwani ndiyo maana yameshindwa kufanya kazi inavyotakiwa.

Katika majibu yake, Arika alisema wao waliagiza tishari hizo kupitia ofisi ya Bandari Makao Makuu ambayo iko Dar es Salaam.

“Pia wakati zinaagizwa sikuwepo hapa Tanga. Nimekuja mwishoni mwa mwaka jana,” alisema Mkuu huyo wa Bandari ambaye inaelezwa alitokea Mamlaka ya Bandari Dar es Salaam.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu alimtaka Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mwantumu Mahiza awaite watu wa Mamlaka ya Mapato (TRA), Mamlaka ya Bandari na Jeshi la Polisi wakae na kutafuta mbinu za kudhibiti njia za panya zinazotumika kupitisha sukari ya magendo.

“Mkuu wa Mkoa simamia hawa watu, msaidiane kudhibiti uingizaji wa sukari kwa njia za panya. Kuna majahazi yanaleta sukari kutoka Brazil. “Mheshimiwa Rais amepiga marufuku uingizaji wa sukari kutoka nje ili viwanda vyetu vya ndani viongeze uzalishaji. Dhibitini bandari zote ndogondogo hadi Pangani,” aliagiza Waziri Mkuu.

Alisema changamoto inayoikabili Serikali ni kwamba hata Shirika la Viwango Tanzania (TBS) au Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) hawawezi kukagua sukari hizo na hazijulikani ubora wake licha ya kuwa zinafika kwa walaji.

 Waziri Mkuu Kassim Majliwa akizungumza na Mkuu wa bandari ya Tanga, Henry Arika (kulia kwake ) na Mhandisi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania Felix Mahangwa ( kulia wakati alipotembelea bandari ya Tanga Februari 19, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Waziri Mkuu, Kssim Majaliwa akiongozwa na Mkuu wa Bandari ya Tanga , Henry Arika (kulia kwake) kukagua bandari hiyo Februari 19, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Mama Magufuli amwaga chozi

Written By CCMdijitali on Thursday, February 18, 2016 | February 18, 2016


Mke wa Rais, Mama Janeth Magufuli akifuta machozi baada ya kuwaaga rasmi walimu wenzake na wanafunzi aliokuwa akiwafundisha katika Shule ya Msingi Mbuyuni, Dar es Salaam jana. Kulia kwake ni Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Dorothy Malecela na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda (wa pili kushoto). (Picha na Fadhili Akida).


Imeandikwa na Ikunda Erick - Habari Leo

HAIKUWA kazi rahisi kwa Mama Janet Magufuli kuaga walimu na wanafunzi wa Shule ya Msingi Mbuyuni jijini Dar es Salaam aliyoitumikia kwa miaka 18 ya ualimu na miaka mingine saba ya kusoma shule hiyo aliyosisitiza ina historia ya maisha yake, pale alipoaga na kudondosha machozi.

Hafla ya kuagwa kwa Mama Magufuli ilifanywa jana katika shule hiyo iliyopo Oysterbay katika Manispaa ya Kinondoni.

“Nimeona niwaage rasmi, nimekuwa nanyi kwa miaka 18 ya ualimu lakini pia nina historia na shule hii, nimesoma hapa shule ya msingi na watoto wangu wote wamesoma hapa pia,” alisema mke huyo wa Rais John Magufuli, maarufu akiwa shuleni kama Mwalimu Pombe.
Alisema anawaaga jumuiya ya shule hiyo kutokana na nafasi yake hivi sasa katika kumsaidia Rais Magufuli katika kuwatumikia Watanzania, lakini bado ataendelea kuwa mwanajumuiya wa Shule ya Mbuyuni.

Akizungumzia historia ya maisha yake na shule hiyo, Mama Magufuli alisema baba yake mzazi (sasa marehemu) askari Mbizo wa Kituo cha Oysterbay (sio mbali kutoka shuleni) kwa wakati huo, alimuandikisha kuanza elimu ya msingi hapo.

Na wakati huo, mwalimu aliyempokea na kumuandikisha, hivi sasa marehemu, Mwalimu Hatibu, alimwandikisha darasa la kwanza na kuanza kusoma, na kwamba muda wa masomo ulipoisha, baba yake alimfuata na kumrudisha nyumbani.

“Hii shule siwezi kuaga, niliandikishwa darasa la kwanza hapa na baba yangu aliyekuwa askari wa Kituo cha Oysterbay, baada ya kumaliza masomo nilirudi tena kufundisha mwaka 1997, na watoto wangu wote wamesoma hapa, ni vigumu kuaga,” alisema Mama Magufuli kwa majonzi huku akitoa machozi.
Alisema akiwa hapo, alikuwa mwalimu wa somo la Uraia na Historia kwa darasa la tatu na la tano, kazi aliyoifanya kwa miaka 18 hadi mwaka jana katikati alipoomba ruhusa ya kwenda kumsaidia kampeni mumewe, Dk Magufuli.

Akizungumzia changamoto zinazoikabili shule hiyo ambayo imeingia katika historia kwa kutoa wake wa marais wawili akitangulia Mama Salma Kikwete, Mama Magufuli alisema atazifikisha kwa Rais ili aangalie jinsi ya kusaidia kuzitatua zikiwemo pia changamoto za walimu wa nchi nzima.

Awali, akisoma risala ya walimu, Mwalimu Mkuu Doroth Malecela alisema pamoja na kuongezeka kwa idadi ya wanafunzi walioandikishwa kuanza elimu ya msingi na upatikanaji wa ruzuku kwa wakati, changamoto kubwa ni uhaba wa madarasa, matundu ya vyoo na madawati.

Pia fedha za likizo za walimu kutopatikana kwa wakati na tatizo la kutopanda madaraja kwa walimu kwa wakati mara wajiendelezapo kielimu na pia walimu wastaafu kucheleweshewa stahiki zao kwa wakati.

Awali, wakati Mama Magufuli alipoingia shuleni hapo, alipokewa na alikwenda moja kwa moja kwenye Ofisi ya Mwalimu Mkuu kusaini kitabu cha wageni na kisha kwenda ofisi za walimu na kuketi kwenye kiti alichokuwa akitumia wakati akifundisha, kisha akaelekea kwenye jukwaa lililoandaliwa kwa ajili ya hafla ya kuagwa.

Wakimzungumzia Mwalimu Pombe, wanafunzi wa shule hiyo katika risala yao iliyosomwa na Jane Andrew ambaye ni mwanafunzi wa darasa la saba, walisema tangu aondoke hawajala tena makande wala chakula kingine; wakimaanisha kuwa sasa hakuna utaratibu wa chakula bure chini ya elimu bure.

Aidha, walimu waliomzungumzia Mwalimu Pombe, walisema wamesikitika kuondoka kwake kwa sababu ni mwalimu mzuri na mwenye huruma, ukarimu na asiyejikweza.

“Yaani tunasikitika kweli, tutammisi mwalimu mwenzetu, alikuwa hana makundi ni rafiki wa walimu wote, hakuchagua rafiki, wote aliwaona ni marafiki, huwezi sema nani ni rafiki yake zaidi ya mwingine, sote alituona tu wamoja”, alisema Mwalimu Amina Kisenge.
Naye wajina wake, Mwalimu Janet Salakana alisema Mwalimu Pombe alikuwa mmoja wa walimu wenye huruma na alijitoa kusaidia wanafunzi wasiojiweza na mfano mzuri ni kununua baiskeli ya mwanafunzi asiyeweza kutembea mwenyewe kutokana na miguu kukosa nguvu.

Katika wosia kwao, Mama Magufuli aliwasisitiza wanafunzi shuleni hapo kusoma kwa bidii na kuacha tabia ya kuangalia video za usiku zinazooneshwa kwenye vibanda ambazo haziwajengi kimaadili.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda aliyemkaribisha Mama Magufuli shuleni hapo, alisema ili kusaidia sekta ya elimu kuendelea zaidi na kuwapunguzia mzigo walimu, amezungumza na baadhi ya wamiliki ya mabasi ya abiria ya jijini ili kutowatoza nauli walimu na kuwapa kipaumbele kuwahi kazini.

Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akiweka saini kitabu cha wageni alipowasili katika shule ya Msingi ya Mbuyuni, Oysterbay, jijini Dar es salaam kwa sherehe fupi ya kuwaaga rasmi walimu wenzake na wanafunzi wa shule hiyo ambayo ana historia nayo ndefu sana kwani ndipo yeye mwenyewe aliposomea elimu ya msingi toka darasa la kwanza hadi la saba kabla hajarudi tena hapo kama mwalimu na kufanya kazi kwa miaka 17 mfululizo.
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akiongozana na mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi ya Mbuyuni, Mwalimu Dorothy Mwalecela , Oysterbay, jijini Dar es salaam kabla ya kuanza kwa sherehe fupi ya kuwaaga rasmi walimu wenzake na wanafunzi wa shule hiyo ambayo ana historia nayo ndefu sana kwani ndipo yeye mwenyewe aliposomea elimu ya msingi toka darasa la kwanza hadi la saba kabla hajarudi tena hapo kama mwalimu na kufanya kazi kwa miaka 17 mfululizo.
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akiwa ameketi kwenye meza yake katika ofisi ya waalimu katika shule ya Msingi ya Mbuyuni, Oysterbay, jijini Dar es salaam wakati wa sherehe fupi ya kuwaaga rasmi walimu wenzake na wanafunzi wa shule hiyo ambayo ana historia nayo ndefu sana kwani ndipo yeye mwenyewe aliposomea elimu ya msingi toka darasa la kwanza hadi la saba kabla hajarudi tena hapo kama mwalimu na kufanya kazi kwa miaka 17 mfululizo.

Wanafunzi wa shule ya Msingi ya Mbuyuni, Oysterbay, jijini Dar es salaam katika sherehe hiyo fupi ya Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli kuwaaga rasmi walimu wenzake na wanafunzi wa shule hiyo ambayo ana historia nayo ndefu sana kwani ndipo yeye mwenyewe aliposomea elimu ya msingi toka darasa la kwanza hadi la saba kabla hajarudi tena hapo kama mwalimu na kufanya kazi kwa miaka 17 mfululizo.
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akisikiliza maelezo ya utangulizi ya mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi ya Mbuyuni, Mwalimu Dorothy Mwalecela , Oysterbay, jijini Dar es salaam wakati wa sherehe fupi ya kuwaaga rasmi walimu wenzake na wanafunzi wa shule hiyo ambayo ana historia nayo ndefu sana kwani ndipo yeye mwenyewe aliposomea elimu ya msingi toka darasa la kwanza hadi la saba kabla hajarudi tena hapo kama mwalimu na kufanya kazi kwa miaka 17 mfululizo.
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akisikiliza maelezo ya utangulizi ya mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi ya Mbuyuni, Mwalimu Dorothy Mwalecela , Oysterbay, jijini Dar es salaam wakati wa sherehe fupi ya kuwaaga rasmi walimu wenzake na wanafunzi wa shule hiyo ambayo ana historia nayo ndefu sana kwani ndipo yeye mwenyewe aliposomea elimu ya msingi toka darasa la kwanza hadi la saba kabla hajarudi tena hapo kama mwalimu na kufanya kazi kwa miaka 17 mfululizo.

Waalimu wa Shule ya msingi ya Mbuyuni Oysterbay, jijini Dar es salaam wakati wa sherehe fupi ya Mama janeth Magufuli kuwaaga rasmi walimu wenzake na wanafunzi wa shule hiyo ambayo ana historia nayo ndefu sana kwani ndipo yeye mwenyewe aliposomea elimu ya msingi toka darasa la kwanza hadi la saba kabla hajarudi tena hapo kama mwalimu na kufanya kazi kwa miaka 17 mfululizo.
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akipokea zawadi toka kwa Afisa Elimu wa Wilaya ya Kinondoni katika Shule ya msingi ya Mbuyuni Oysterbay, jijini Dar es salaam wakati wa sherehe fupi ya kuwaaga rasmi walimu wenzake na wanafunzi wa shule hiyo ambayo ana historia nayo ndefu sana kwani ndipo yeye mwenyewe aliposomea elimu ya msingi toka darasa la kwanza hadi la saba kabla hajarudi tena hapo kama mwalimu na kufanya kazi kwa miaka 17 mfululizo.
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akisikiliza risala toka kwa mwanafunzi wa shule ya Msingi ya Mbuyuni Oysterbay, jijini Dar es salaam wakati wa sherehe fupi ya kuwaaga rasmi walimu wenzake na wanafunzi wa shule hiyo ambayo ana historia nayo ndefu sana kwani ndipo yeye mwenyewe aliposomea elimu ya msingi toka darasa la kwanza hadi la saba kabla hajarudi tena hapo kama mwalimu na kufanya kazi kwa miaka 17 mfululizo.
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akipokea risala toka kwa mwanafunzi wa shule ya Msingi ya Mbuyuni Oysterbay, jijini Dar es salaam wakati wa sherehe fupi ya kuwaaga rasmi walimu wenzake na wanafunzi wa shule hiyo ambayo ana historia nayo ndefu sana kwani ndipo yeye mwenyewe aliposomea elimu ya msingi toka darasa la kwanza hadi la saba kabla hajarudi tena hapo kama mwalimu na kufanya kazi kwa miaka 17 mfululizo.
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akisikiliza maelezo ya utangulizi ya mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi ya Mbuyuni, Mwalimu Dorothy Mwalecela , Oysterbay, jijini Dar es salaam wakati wa sherehe fupi ya kuwaaga rasmi walimu wenzake na wanafunzi wa shule hiyo ambayo ana historia nayo ndefu sana kwani ndipo yeye mwenyewe aliposomea elimu ya msingi toka darasa la kwanza hadi la saba kabla hajarudi tena hapo kama mwalimu na kufanya kazi kwa miaka 17 mfululizo.
Wanafunzi wakitumia simu za walimu wao katika Shule ya msingi ya Mbuyuni Oysterbay, jijini Dar es salaam kurekodia wa sherehe fupi ya Mama janeth Magufuli kuwaaga rasmi walimu wenzake na wanafunzi wa shule hiyo ambayo ana historia nayo ndefu sana kwani ndipo yeye mwenyewe aliposomea elimu ya msingi toka darasa la kwanza hadi la saba kabla hajarudi tena hapo kama mwalimu na kufanya kazi kwa miaka 17 mfululizo.
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akipokea zawadi ya saa toka kwa mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi ya Mbuyuni, Mwalimu Dorothy Mwalecela , Oysterbay, jijini Dar es salaam wakati wa sherehe fupi ya kuwaaga rasmi walimu wenzake na wanafunzi wa shule hiyo ambayo ana historia nayo ndefu sana kwani ndipo yeye mwenyewe aliposomea elimu ya msingi toka darasa la kwanza hadi la saba kabla hajarudi tena hapo kama mwalimu na kufanya kazi kwa miaka 17 mfululizo.


Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akitoa msaada wa vifaa vya shule kwa wanafunzi wasiojiweza katika shule ya Msingi ya Mbuyuni, Mwalimu Dorothy Mwalecela , Oysterbay, jijini Dar es salaam wakati wa sherehe fupi ya kuwaaga rasmi walimu wenzake na wanafunzi wa shule hiyo ambayo ana historia nayo ndefu sana kwani ndipo yeye mwenyewe aliposomea elimu ya msingi toka darasa la kwanza hadi la saba kabla hajarudi tena hapo kama mwalimu na kufanya kazi kwa miaka 17 mfululizo.
Mkuu wa wilaya ya Kinondoni Mhe Paul Makonda akimkaribisha Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli kutoa nasaha zake katika shule ya msingi ya Mbuyuni, Oysterbay, jijini Dar es salaam wakati wa sherehe fupi ya kuwaaga rasmi walimu wenzake na wanafunzi wa shule hiyo ambayo ana historia nayo ndefu sana kwani ndipo yeye mwenyewe aliposomea elimu ya msingi toka darasa la kwanza hadi la saba kabla hajarudi tena hapo kama mwalimu na kufanya kazi kwa miaka 17 mfululizo leo February 17, 2016.
Kabla ya kuanza kuhutubia Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli na meza kuu aliimbisha wimbo maalumu wa shule ya msingi ya Mbuyuni, Oysterbay, jijini Dar es salaam wakati wa sherehe fupi ya kuwaaga rasmi walimu wenzake na wanafunzi wa shule hiyo ambayo ana historia nayo ndefu sana kwani ndipo yeye mwenyewe aliposomea elimu ya msingi toka darasa la kwanza hadi la saba kabla hajarudi tena hapo kama mwalimu na kufanya kazi kwa miaka 17 mfululizo leo February 17, 2016.






Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akiwaaga walimu na wanafunzi wa shule ya msingi ya Mbuyuni, Oysterbay, jijini Dar es salaam baada ya sherehe fupi ya kuwaaga rasmi walimu wenzake na wanafunzi wa shule hiyo ambayo ana historia nayo ndefu sana kwani ndipo yeye mwenyewe aliposomea elimu ya msingi toka darasa la kwanza hadi la saba kabla hajarudi tena hapo kama mwalimu na kufanya kazi kwa miaka 17 mfululizo leo February 17, 2016.
PICHA NA IKULU

Bodi ya Mikopo yatumbuliwa

Written By CCMdijitali on Wednesday, February 17, 2016 | February 17, 2016

Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako akisisitiza jambo wakati akitoa uamuzi wa Serikali wa kusitisha mkataba wa Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo, George Nyatega pamoja na kuwasimamisha kazi Wakurugenzi watatu Dar es Salaam jana. Mwingine ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Maimuna Tarishi. (Picha na Raymond Mushumbusi, Maelezo).

Imeandikwa na Anastazia Anyimike -Habari Leo

WAZIRI wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako amesitisha ajira ya Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), George Nyatega kwa tuhuma za udhaifu katika fedha za mikopo zaidi ya Sh bilioni 3.2.

Pia amewasimamisha kazi wakurugenzi watatu wa Fedha na Utawala, Urejeshaji Mikopo na Upangaji na Utoaji Mikopo katika HESLB kwa tuhuma za udhaifu huo wa mikopo ya Sh 3,234,452,259.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Profesa Ndalichako alisema hatua hiyo, imechukuliwa baada ya kuridhika na kuona utendaji usioridhisha kwenye taasisi hiyo, kiasi cha kuwapo matatizo mengi yanayojirudiarudia kwa wateja wao, ikiwamo ucheleweshaji wa mikopo bila sababu ya msingi.

Profesa Ndalichako alisema pia uongozi wa bodi hiyo, umeshindwa kutoa majibu ya Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali, alipoagizwa na Wizara Januari mwaka huu.

“Majibu yaliyowasilishwa na Bodi Februari 1, mwaka huu yanadai kuwa taarifa ya mkaguzi haikukidhi viwango na kwamba ilijikita katika ‘operational audit’, wakati kazi hiyo hufanywa na mkaguzi wao wa ndani.
Pia walikiri baadhi ya udhaifu kama kusajili mara mbili ambao ulitokana na kuwa wakati huo walikuwa hawajaanza kutumia mfumo wa kompyuta,” alieleza Waziri wa Elimu.

Aliongeza: “Kwa mamlaka niliyopewa kwa mujibu wa Kifungu D.5(3) cha Kanuni za Kudumu kinachohusu uteuzi wa maofisa wa juu wa taasisi za serikali na Kifungu D.12 kinachoruhusu utoaji wa taarifa za Mtendaji na Kifungu F.50(1) kinachohusu usitishaji wa mkataba na kile cha Bodi ya Mikopo Kifungu cha 11(3), nimesitisha mkataba wa ajira wa George Nyatega,” alieleza Profesa Ndalichako.

Alisema kutokana na kusitisha ajira ya kiongozi huyo, Bodi inatakiwa kumlipa mshahara wa mwezi mmoja kama notisi kulingana na Kifungu 50(3)(a) cha Kanuni za Kudumu. Nyatega alikuwa astaafu Agosti 31, mwaka huu baada ya kuwa aliongezewa mkataba wa miaka miwili baada ya kustaafu Machi 2014, na kuongezewa mkataba kuanzia Septemba 2014.

Alisema pia amewasimamisha kazi Mkurugenzi wa Fedha na Utawala, Yusufu Kisare, Mkurugenzi wa Urejeshaji Mikopo Juma Chagonja na Mkurugenzi wa Upangaji na Utoaji Mikopo, Onesmo Laizer na kuwa wizara itateua maofisa watakaoshika nafasi hizo hadi uchunguzi utakapokamilika na wakurugenzi hao kuchukuliwa hatua stahiki.

“Namwagiza Mkaguzi wa Ndani Mkuu wa Serikali ahakiki maelezo na nyaraka zilizowasilishwa na Bodi ya Mikopo pamoja na kufanya ukaguzi maalumu kwa kipindi cha kuanzia mwaka 2013 hadi sasa ukaguzi uanze mara moja,” alieleza Profesa Ndalichako.

Akifafanua zaidi kuhusu malipo yasiyo sahihi, alisema: “baadhi ya wanafunzi ambao walikwenda kusoma Algeria wamekuwa wakiendelea kulipwa fedha wakati mkataba wao wa mkopo wa miaka minne umekwisha, lakini wamelipwa hadi miaka saba kinyume cha utaratibu.”

Alisema ukaguzi huo wa mwaka 2013, umebainisha kuwa wanafunzi 23 walipata mikopo kupitia vyuo viwili tofauti na walilipwa jumla ya Sh 153,999,590 katika chuo kimoja na Sh 147,541,460 katika chuo cha pili ambazo zimelipwa miaka mitatu mfululizo.

Waziri alisema pia wanafunzi 169 walilipwa mikopo kupitia vyuo viwili tofauti ambapo Sh 658,047,570 zililipwa katika chuo cha kwanza na Sh 665,135,716 chuo cha pili zilizolipwa kwa miaka miwili mfululizo.

Alisema pia wanafunzi 343 wasiokuwa na usajili kwenye vyuo husika walilipwa Sh 342,468,500 huku wanafunzi 55 walioacha masomo walilipwa Sh 136,232,800.

“Jumla ya Sh 159,664,500 zililipwa kwa wanafunzi 306 zaidi ya kiwango kilichobainishwa kwenye vipengele namba 4.3 na 4.3.2 cha miongozo ya upangaji na ukopaji ya mwaka 2008/2009 na 2009/2010 na vipengele no 4.6 na 4.3.1 cha miongozo ya upangaji na ukopeshaji mikopo ya mwaka 2008.2009 na 2009/2010 hadi 2010/2011."

Alifafanua kuwa pia wanafunzi 77 walipatiwa mikopo kwenye vyuo vya ndani na nje ya nchi kwa wakati mmoja.

Wanafunzi hao walitumiwa Sh 467,620,654 kwa vyuo vya nje na Sh 123,047,119 ya vyuo vya ndani huku wanafunzi 19,348 walipatiwa mikopo bila kupitishwa na Kamati ya Mikopo wakati wanafunzi 54,299 walipangiwa mikopo wakati hawakuwa wameomba.

Alisema kuwa pia Bodi ilipeleka Sh 207,052,650 kwenye vituo sita vya elimu ya juu na kutochukuliwa na wanafunzi husika na fedha hizo hazikurejeshwa Bodi kinyume cha Hati ya Makubaliano (MOU) kifungu 3.3.4(b) na (c).

“Ukaguzi utakwenda mpaka kwenye vyuo, endapo tutabaini vyuo kiwe cha umma au binafsi wamehusika kushirikiana na watendaji wa Bodi kuhujumu fedha tutachukua hatua za kisheria dhidi yao. “Nazionya taasisi zilizo chini ya wizara, sitakuwa tayari kuona wanafunzi wanakaa chini, hawana madarasa halafu kuna taasisi zinahujumu hata senti tano, tutaendelea kuzifuatilia kwa karibu,” alionya Profesa Ndalichako.

Katika hatua nyingine, Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) limekanusha taarifa zilizosambazwa jana katika mitandao ya kijamii kuwa limezuia matokeo hadi yasahihishwe upya, kuwa si za kweli na kwamba mchakato wa kutunuku uko katika hatua nzuri; kwa mujibu wa Ofisa Habari wa Necta, John Nchimbi.

DED wa Arusha ahimiza uwekezaji vitega uchumi

Written By CCMdijitali on Tuesday, February 16, 2016 | February 16, 2016

Mkurugenzi Mtendaji wa Jiji la Arusha, Juma Idd

Imeandikwa na Veronica Mheta, Arusha /Habari Leo

WANASIASA na viongozi wengine mkoani Arusha wameshauriwa kuhamasisha wawezekaji wa ndani kuwekeza katika maeneo yaliyobomolewa nyumba na Halmashauri ya Jiji la Arusha kwa ajili ya ujenzi wa vitega uchumi.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Arusha, Juma Idd wakati alipokuwa akizungumza katika kikao cha baraza la madiwani.


Alisema wanasiasa wana nafasi kubwa ya kuhamasisha wawekezaji katika maeneo hayo yakiwemo eneo la Kaloleni na Themi jijini hapa.


Alisema katika maeneo hayo kulikuwa na nyumba zilizobomolewa kupisha ujenzi wa vitega uchumi mbalimbali.


Alisisitiza kwamba maeneo hayo hayatatolewa kinyemela.


Aidha Mkurugenzi huyo aliwataka madiwani kwa kushirikiana na viongozi wa kata zao kusimamia kikamilifu na kuzuia maambukizi ya ugonjwa wa kipindupindu unaosababishwa na uchafu wa mazingira.


Meya wa Jiji la Arusha, Calist Lazaro alisema halmashauri hiyo imewaelekeza wataalamu wake kuja na miradi michache ambayo inatekelezeka kwa wakati. Alisema hivi sasa hawatakuwa na miradi mingi ambayo mwisho wa mwaka haimaliziki.


Muhongo: Fanyeni utafiti wa kutosha

 Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo


WAZIRI wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo amewataka wawekezaji katika sekta za nishati na madini kufanya utafiti wa kutosha katika maeneo husika kabla ya kuendelea na miradi yao.

Profesa Muhongo aliyasema hayo katika mkutano baina yake na wawakilishi kutoka Kampuni ya Lake Holdings ukiwa ni moja kati ya mikutano kadhaa inayoendelea wiki nzima baina ya Wizara na wawekezaji wa sekta hizo.

Kampuni hiyo iliyosajiliwa mwaka 2012 ina mpango ya kujenga kituo cha kuzalisha umeme chenye uwezo wa megawati 300 hadi megawati 450 wilayani Songea mkoani Ruvuma.

Huo ni mradi mkubwa zaidi ukilinganishwa na mradi wao wa awali katika Kata ya Kiwira wilayani Rungwe, Mbeya uliolenga megawati 200 za umeme.

Akizungumza katika mkutano huo, Mratibu wa mradi huo, Profesa Runyoro alieleza kuwa changamoto kuu waliyoipata katika kutekeleza mradi huo ni upatikanaji wa makaa ya mawe ambayo yanahitajika kwa kiasi kikubwa (tani milioni moja) ili kuwezesha mradi huo, huku maeneo mengi yameshachimbwa na watu wengine.

Akizungumzia suala hilo, Profesa Muhongo aliwataka wawekezaji waache ubahili na badala yake waende wenyewe katika maeneo hayo ili kujua kiasi cha makaa ya mawe yanayopatikana kwani mradi huo ni mkubwa na utahitaji uwekezaji mkubwa, hivyo kuwataka kufanya upimaji wa kijiografia na kisha kutoa majibu baada ya mwezi.

Aidha, alilitaka Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC) na Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) kufanya kazi kwa karibu na Lake Holdings ili waafikiane juu ya suala hilo na wawekezaji hao wapate maeneo ya kuchimbia makaa ya mawe.

Aliwataka wawekezaji kutochukua maeneo na kuyaacha na hivyo kupoteza muda wa Watanzania, badala yake wayafanyie kazi ili Watanzania wanufaike na rasilimali hiyo.

Ummy Mwalimu awasimamisha wakurugenzi Bohari ya Dawa ya Taifa (MSD) kwa ubadhilifu wa takribani Shillingi Billion 1.5.


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akiwa amebeba vifaa vilivyopelekwa na Bohari Kuu ya Dawa (MSD) Muhimbili jana. (Na Mpigapicha Wetu).
Waziri wa Afya ,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Watoto na Wazee Mhe. Ummy Mwalimu amewasimamisha wakurugenzi toka Bohari ya Dawa ya Taifa(MSD) kwa ubadhilifu wa fedha takribani Shillingi Billion 1.5.
 
Ameyasema hayo wakati akizungumza na Waandishi wa Habari katika Kitengo cha Afya ya Mama na Mtoto baada ya kupokea vifaa toka Bohari Kuu ya Dawa ya Taifa (MSD) amesema amepata taarifa ya uchunguzi ofisini kwake ya ubadhilifu wa kiasi hicho cha fedha na kuamua kuwasimamisha wakurugenzi wanne kupisha uchunguzi.

“ Nimeletewa taarifa ofisini kwangu na nimeamua kuchukua fursa hii kuwaambia na hili pia kwamba nimewasimamisha wakurugenzi wanne toka Bohari ya Kuu Dawa ya Taifa kwa ubadhilifu wa fedha na nisingeweza kusubiri nitumbuliwe mimi jipu na Mhe.Rais kwahiyo nimeamua kuwachukulia hatua kwa kuwasimamisha kazi ili kupisha uchunguzi”

“ Hizi ni zama za kufanya kazi na kuwajibika sasa inabidi tuwajibike kwa kufanya kazi na hatutowavumilia watendaji watakaoenda kinyume na utaratibu katika ofisi yoyote ile katika sekta ya afya na tutawachukulia hatua kwani tunataka uwajibikaji ili kuiendeleza sekta ya afya ambayo ni muhimu sana kwa kila mwanadamu” Alisema Ummy.

Amewataja aliowasimamisha kazi kuwa ni Joseph Tesha Mkurugenzi wa Fedha na Mipango, Misanga Muja Mkurugenzi wa Ugavi, Heri Mchunga Mkurugenzi wa Manunuzi na Cosmas Mwaifani Mkurugenzi Kanda na Huduma kwa Wateja ambapo amewataka Mkurugenzi na Mwenyekiti wa Bodi ya Bohari ya Dawa ya Taifa kuwaandikia barua mara moja ya kuwasimamisha kazi.

Katika kuboresha sekta ya afya nchini Wizara wa Afya ,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Watoto na Wazee imejipanga kufanya kazi kwa taratibu na misingi iliyopo ili kuhakikisha inapeleka mbele gurudumu la maendeleo ya hasa katika sekta ya afya kwa ujumla.

NDANI YA TAKUKURU KUNA ‘MAJIPU’ –KAIRUKI.

Written By CCMdijitali on Monday, February 15, 2016 | February 15, 2016

 Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Kamishna Valentino Mlowola akizungumza na viongozi wa TAKUKURU katika mkutano wa kazi na viongozi hao uliofanyika makuu ya ofisi hiyo mapema leo. Kushoto ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Utumishi na Utawala Bora Mhe. Angella Kairuki (Mb) akimsikiliza kwa umakini.
 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Utumishi na Utawala Bora Mhe. Angella Kairuki (Mb) akifungua mkutano wa kazi wa viongozi wa TAKUKURU uliofanyika makuu ya ofisi hiyo mapema leo.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Utumishi na Utawala Bora Mhe. Angella Kairuki (Mb) akiwa katika picha ya pamoja na wakaguzi wa kanda wa TAKUKURU mara baada ya kufungua mkutano wa kazi wa viongozi wa TAKUKURU uliofanyika makuu ya ofisi hiyo mapema leo.

Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii


WAZIRI wa Nchi, Ofisi Rais Utumishi na Utawala Bora, Angela Kairuki amesema kuwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) ina baadhi ya watendaji wametumia nafasi zao vibaya na kufanya chombo hicho kukosa uaminifu hivyo na kufanya chombo hicho kuwa na ‘majipu’ ambayo yanatakiwa kupasuliwa.

Angela ameyasema hayo leo wakati akifungua mkutano wa mwaka wa utendaji kazi wa Takukuru uliofanyika leo jijini Dar es Salaam, amesema chombo hicho ni muhimu lakini kuna baadhi wametumia nafasi zao vibaya katika kufanya kazi na taarifa anazo hivyo atashughulikia ikiwemo na kuandika kiapo cha mali zao na kama walifanya warudie kujiridhisha.

 Amesema kuwa Takukuru inatakiwa kufika wilayani na mikoani kutokana na fedha nyingi za miradi ya serikali zinakwenda huko ambapo ameutaja mkoa wa Kilimanjaro unawatendaji ambao wametumia madaraka vibaya wa ubadhirifu wa fedha za serikali hivyo Takukuru lazima ichukue hatua dhidi yao.

Amesema kuwa ikitokea kuwepo na kutowajibika kwa chombo hicho serikali iamweza kuwandoa wote kutokana na kuwepo kwa watu wenye sifa wa kufanya kazi hiyo.

Aliongeza kuwa katika Takukuru inatakiwa kujiridhisha na uchunguzi na sio kuwa idadi nyingi za kesi ambazo mwisho wa siku kesi hizo wanashindwa kutokana kuushindwa kuwa na uchunguzi wenye ushahidi.

Aidha amesema kuwa baadhi ya mahakimu watakosa kazi kutokana na baadhi ya kesi wameendesha kwa kupindisha na kuwapa washitakiwa haki wasio kuwa nayo.

Waziri Angela amesemaTakukuru wafanye kazi kwa waadilifu kwa kuwalinda watoa taarifa ili waendelee kutoa taarifa kwa watu wanaojua kuwa wanahujumu nchi kwa kutumia madaraka yao.

Amesema watumishi wa Takukuru wana masilahi mazuri kuliko wa wafanye kazi wengine ikiwa ni kuwaondoa katika ushawishi wa kuwa na tama kutokana unyeti wa chombo hicho.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Kamishina (CP), Valentino Mlowola amesema wameokoa sh. Bilioni Saba (7) ambazo zilikuwa ziingie kwenye mifuko ya wabadhirifu wachache ambao wanatumia nafasi zao vibaya kwa masilahi yao.

Amesema walipokea malalamiko 4,675, uchunguzi uliokamilika wa majalada hayo ni 667, majalada yaliyokwenda kwa Mkurugenzi wa Mashitaka Nchini (DPP), ni 278, majarada yaliyorejeshwa na DPP, ni 172 kwa ajili ya vibali vya kufungua mashitaka na kesi mpya 314 nchini kote, na kesi zilizoshinda 132 ambao wamefungwa na wengine kulipa faini.

London underwater

Written By CCMdijitali on Sunday, February 14, 2016 | February 14, 2016

London underwater: Cars lie abandoned in upmarket areas of the capital as floods continue to wreak havoc after heavy rainfall - and there's an Arctic blast on the way
  •  Dramatic pictures from the capital showed roads and parks completely submerged under murky floodwater
  •  Flood warnings remain in place in areas alongside the River Thames, with more rain still due to fall
  •  The Met Office issued a weather warning for snow in north-east England and Scotland beginning tonight
  •  Wintry showers and freezing overnight temperatures expected for the rest of the UK falling as low as -11C
By Joseph Curtis For Mailonline

Dramatic pictures from London tonight showed more flooding in upmarket areas of the capital, with cars lying abandoned half-covered in murky water.

Residents were also seen wading through the high water to get to their homes in areas near the Thames, including Richmond.

The floods which has blighted large sections of the city over the past 24 hours has been caused by a combination of the after effects of the recent storms and a high Spring tide.

 A car is partly submerged in flood-water in Richmond, south-west London today after heavy rainfall caused heavy flooding
 The River Thames flooded this road near Richmond, west London at high tide
 Rain showers are expected to dry up by the end of the day, although the south west could see 10-20mm fall before the weather brightens up across the country by the end of Sunday and into Monday. Pictured: Another road in Richmond in London that is flooded
 South-west London, including Richmond (pictured) experienced localised flooding when the River Thames burst its banks as a result of heavy rain and high tides
 Rain showers are expected to dry up by the end of the day, although the south west could see 10-20mm fall before the weather brightens up across the country by the end of Sunday and into Monday

Yesterday, the water was seen overflowing in Charing Cross where the average property costs £4.7million, Kew where homes cost about £1m, in Putney where the average home is worth £693,000 and in Greenwich where the average three bedroom house costs around £1.6m

It comes after The Thames Barrier was shut for the first time this year 'to protect London from the threat of flooding due to the high level of rain combined with high tides from the sea'.

The action was taken after Storm Imogen lashed the country with heavy downpours earlier this week.

While some flood warnings still in effect around the River Thames, rain showers are expected to dry up by the end of the day, although the south west could see 10-20mm fall before the weather brightens up across the country by the end of Sunday and into Monday.

An Arctic blast is also set to hit Britain tonight with a fresh cold snap bringing up to six inches of snow with it.

Weather warnings have been issued for north-east England and Scotland overnight and into Sunday while temperatures will drop below freezing for much of the UK.

 The slow-moving cold front will begin in the Scottish Highlands today and move south gradually, with snow expected to start falling over England at midnight.

A Met Office spokesperson said there could even be some wintry showers in the south west with Exmoor and Dartmoor warned to expect sleet.

The spokesperson said: 'Snow warnings have been issued across Scotland and the borders and as the night goes on that will move down towards County Durham, with a warning issued for north England between midnight tonight and 12noon Sunday.'

Many in the north will then feel the full force of the cold snap on Sunday and Monday when the temperature will fall as low as -11C in some parts of Scotland.

 Flood warnings and alerts are still in place across many parts of the country, with Old Deer Park, Richmond, flooded today, pictured
 High tides and previous heavy rain are to blame for the rising water levels, but it didn't put off early morning joggers in Richmond, pictured
 The Thames burst its banks in Richmond, pictured, as well as Putney, Greenwich, Charing Cross and the Embankment

Met Office forecaster Alex Burkill added: ‘On Saturday, some of the snow settling in Scotland is likely to start falling in the North East. There could also be scatterings of wintry showers on higher ground in the South – such as the Cotswolds, the Chilterns, even Exmoor and Dartmoor.

‘As we go into Sunday, we’ll start to see colder air blowing from the North, which typically brings more showers to the East ...where these fall further inland, they are likely to fall as snow or sleet.

‘By Monday, these wintry showers could even start to move down as far as the Midlands – though they will be much more scattered.’

Mr Burkill said the start of next week is likely to see lower-than-average temperatures for this time of year.

 Snow, pictured in Glasgow, will continue to fall in Scotland today and start sprinkling over England from midnight tonight
 Pedestrians brave the snow in Glasgow, pictured . Up to 6in could fall in parts of Britain overnight say experts
 Pedestrians brave the snow in Glasgow, pictured . Up to 6in could fall in parts of Britain overnight say experts
 Hikers in the Brecon Beacons trudge through snow, pictured, while wintry showers could move as far south as Devon and Cornwall

 In a possible sign of what is to come, thousands of passengers travelling between Kent and London faced disruption due to ‘icy conditions’ on railway lines in the South yesterday, with some reporting delays of more than two hours.

The Met Office said a slow-moving cold front is expected to make its way southwards on Saturday, with weather warnings in place across Scotland for ice and up to 4in of snow.

The chill is expected to continue drifting down to northern England, meaning Valentine’s Day will start with widespread early frosts before temperatures drop as low as -5C (23F) as the evening draws in.

The North East is predicted to see around 2in of snow on lower ground inland, with up to 6in higher up. The South is likely to feel slightly milder throughout the weekend thanks to a wet weather front.

The wet forecast means that despite plummeting overnight temperatures, any scattering of snow across the Cotswolds and Dartmoor is unlikely to settle.

Suffolk is also forecast to see some of the coldest temperatures in the south, with lows of -4C (25F) in the village of Santon Downham.

Sharp frosts are then expected across Britain on Monday and Tuesday mornings.

 Rain will begin to ease off over the UK but although the weather will be dry, a cold snap will bring freezing temperatures to the country
 Drivers are battling blizzard-like conditions as they move through heavy snowfall on the M8 in West Lothian, Scotland, pictured
 A dog walker wraps up warm on the Pen y Fan mountain, Brecon Beacons, with temperatures around the country set to plummet from tomorrow onwards
 The conditions make the Brecon Beacons, pictured, look more like an Arctic wasteland than a Welsh national park
 Weather warnings for snow have been issued for Scotland and north-east England, including Glasgow, where snow is dusting Kelvin Bridge, pictured
But recent spells of wet weather mean this snow in Glasgow, pictured, is unlikely to settle for very long, if at al
 
SO MUCH FOR BRITISH GRIT? SCIENTISTS DEVELOPING HEATED CONCRETE TO TACKLE ICY ROADS 
 
Researchers in the US have come up with a new scheme to heat roads during cold weather rather using grit or salt to melt ice.

The plans are being developed in Lincoln, Nebraska, where scientists are developing a type of concrete complete with steel shavings and coal that will be able to carry an electric current, which can heat it up to 4C.

According to the Daily Telegraph, academics at the University of Nebraska say it would be cheaper to use this technology to heat a road during an expected cold snap than to spread de-icing chemicals across wide stretches of infrastructure.

It comes as the Met Office has issued weather warnings in Scotland and north England with ice expected to cover many roads over the next few days.

The Department of Transport is thought to have 286,000 tonnes of salt for local roads and another 102,000 tonnes for motorways and A-roads.

A 150ft bridge in Nebraska was the testing ground for the heated surface, with the current fed into the road using steel rods attached to electrodes.

The cost of using the technology across the bridge for three days would be around £173.
 
Support : #BegaKwaBegaNaMamaSamia | JAK | CCM Arusha
Copyright © 2011. CCM Dijitali - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Jasper K
Proudly powered by Blogger
Link