NAIBU WAZIRI PINDA AELEKEZA UENDELEZAJI MIJI KUZINGATIA MIPANGO KABAMBE

Na Munir Shemweta, WANMM Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Geofrey Pinda amezielekeza Halmashauri zote nchini kuhakik...

Latest Post

Mhe Gambo awahakikishia Wananchi wa Mkoa wa Arusha kuwepo kwa amani na utulivu 01Sept 2016

Written By CCMdijitali on Wednesday, August 31, 2016 | August 31, 2016

 Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe Mrisho Mashaka Gambo na Mwenyekiti wa  Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa akisistiza jambo wakati akizungumza na waandishi wa habari leo 31 August 2016.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe Mrisho Mashaka Gambo na Mwenyekiti wa  Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa akizungumza na waandishi wa habari leo 31 August 2016.

Na Mwandishi Wetu - Arusha.
 
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Mashaka Gambo ambaye pia ni mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa amesema kesho hapatakua na maandamo yeyote katika Mkoa huu na kuwataka wananchi kuendelea na shughuli zao kama kawaida.

Mhe. Gambo ameyasema hayo mapema leo alipokua akizungumza na waandishi wa habari na kusisitiza kwamba Kamati ya Ulinzi na Usalama imejipanga kikamilifu kuhakikisha amani ya Mkoa huu inaendelea kuwepo na kudhibiti viashiria vyote vya uvunjifu wa amani vitakavyojitokeza.

Amewatoa hofu wananchi na kuwataka kuendelea na shughuli zao kama kawaida pia amewahakikishia amani na utulivu na kuwataka  kuendelea kumuunga Mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kujituma na kufanya kazi kwa maendeleo ya Nchi yetu.

Pia ameelezea dhana ya wanajeshi wa JWTZ kuadhimisha miaka 52 ya Jeshi  kwa kufanya usafi siku ya kesho kwamba ni utaratibu wa kawaida na wanaunga mkono agizo la Rais wetu la kuwataka watu wote kufanya usafi katika maeneo yao ili kujikinga na maradhi.


North Korea has executed a deputy premier, Seoul reports



 North Korean leader Kim Jong-un. / Internet photo

Kim Yong Jin, second from left, vice premier on education affairs in North Korea's cabinet.

Kim Yong Jin, a vice premier in North Korea’s cabinet, has been executed for being “an anti-party, anti-revolutionary agitator,” South Korean officials said Wednesday. Two other senior officials have been banished to rural areas for reeducation, the officials added.

According to the officials in Seoul, these are the latest executions and demotions of top North Korean officials since Kim Jong Un assumed power in 2011.

“Kim Yong Jin was denounced for his bad sitting posture when he was sitting below the rostrum” during a session of the reclusive country’s parliament, according to a South Korean official, who declined to be named. The vice premier was then interrogated during which his other crimes were revealed, the official told reporters. He was allegedly executed by a firing squad.


South Korean daily JoongAng Ilbo reported Tuesday that the official, who served as vice premier for education, was executed but the newspaper identified him as Ri Yong Jin, and not as Kim Yong Jin. It reported that another official, former agriculture minister Hwang Min, was also executed because his policy proposals were viewed as a challenge to the North Korean leader.

Meanwhile, Kim Yong Chol, the head of the North’s United Front Department that looks over inter-Korean relations, was ordered to carry out “revolutionary reeducation,” Seoul’s Unification Ministry spokesman Jeong Joon Hee said. Another top official dealing with propaganda affairs, Choe Hwi, was also reportedly put on “revolutionary reeducation” program.

The Associated Press, however, noted that South Korea that has several intelligence organizations mostly spying on North Korea has a mixed track record for news from the secretive country. In May, a former North Korean military official, who South Korea had said was executed, was found to be alive and holding several senior-level positions.

The latest alleged execution comes after North Korea’s deputy ambassador in London reportedly defected and arrived in South Korea with his family. Last year, Seoul’s spy agency said that a former North Korean defense minister, Hyon Yong Chol, was executed for treason.

TANAPA kuongeza watalii Hifadhi ya Ruaha


SHIRIKA la Hifadhi za Taifa (TANAPA) limetangaza kutumia tukio la kupatwa kwa jua linalotarajia kuonekana Septemba mosi mwaka huu kufungua lango la Ikoga katika wilaya ya Mbarari mkoani Mbeya ili kuongeza watalii katika HIFADHI ya Taifa ya Ruaha 


Kufuguliwa kwa lango hilo kunafanya idadi ya milango ya kuingilia katika hifadhi hiyo kufikia miwili ukiacha lango kuu la Way Junction ambalo limekuwa likitumika kwa muda mrefu sasa

Meneja Uhusiano wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Pascal Shelutete anasema kuongezeka kwa geti la Ikoga ni fursa kubwa ya kuhamasisha utalii wa ndani kwa kuwa eneo la Ihefu linakivutio kikubwa cha wanyama wa aina mbalimbali .

Mkuu wa Wilaya ya Mbarali, Reuben Ndiza Mfune, anasema Wilaya hiyo ina vivutio vingi, hivyo amewataka wananchi watakaofika kuangalia kupatwa kwa jua hiyo Septemba Mosi , kutumia fursa hiyo kutembelea vivutio vilivyopo Wilayani humo.

Tukio la kupatwa kwa jua linategemea kutokea Septeba mosi majira ya nne asubuhi hadi saa nane mchana katika kata ya Rujewa eneo la Mpunga Relini Kiometa 3.5 kutoka barabara kuu ya kutoka Dar es Salaam kueleka Mbeya.

 Mkuu wa Wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya ,Reuben Fune akiangalia jua kwa kutumia kifaa maalum ambacho kinachuja mwanga ili usiweze kuathiri macho kifaa hicho kitatumika katika tukio la kupatwa kwa jua linalotarajia kutokea Septemba mosi .Kushoto ni mnajimu Dkt Noorali Jiwaji akimuelekeza namna ya kukitumia. 

 Meneja Mawasiliano wa Shirika la Hifadhi za Taifa (Tanapa) Pascal Shelutete akizungumza na wanahabari wilayani Mbarali (hawapo pichani) namna ambavyo Tanapa ilivyo jipanga na tukio la kupatwa kwa jua litakalotokea Septemba mosi. Kulia ni Mkuu wa wilaya ya Mbarali , Reuben Fune 
 Mtaalam wa masuala ya anga (Mnajimu) Dkt Noorali Jiwaji akizungumza na waandishi wa habari wilayani Mbarali mkoani Mbeya kuhusu maandalizi na uwepo wa vifaa vya kuangalizia jua wakati wa tukio la kupatwa litakalotokea Septemba Mosi.
 Mahema yakiwa yameanza kuwekwa katika eneo la Mpunga Relini ,Rujewa wilayani Mbarali,eneo lililotengwa maalum kwa ajili ya kutizamia tukio la kupatwa kwa jua linalotarajia kutokea Septemba mosi . 
 Eneo la Mpunga Relini ,Rujewa wilayani Mbarali,eneo lililotengwa maalum kwa ajili ya kutizamia tukio la kupatwa kwa jua linalotarajia kutokea Septemba mosi . 
Na Dixon Busagaga wa Michuzi Blog, Mbarali, Mbeya . 


MAAJABU YA MTI WA MLONGE KUPITIA HAPA


KAMA kuna mti wenye faida nyingi za kiafya, basi Mlonge/mlongo/ mronge, mrongo/mkimbo au mzunze (kwa Kiingereza unaitwa Moringa Oleifera ) unaweza kuwa unaongoza. 

Kila eneo la mti huu, kuanzia majani, maua, mbegu, magamba hadi mizizi yake ina virutubisho vya kipekee vyenye faida nyingi za kiafya kwa binadamu ingawa kwa bahati mbaya sana huenda wengi hatuujui ima tunaujua na kuupuzia. Kwa mujibu wa tafiti mbalimbali, mti wa Mlonge unatibu karibu magonjwa 300 ya aina mbalimbali, yakiwemo yale magonjwa sugu.
Profesa Mmoja wa Chuo Kikuu cha Kilimo (SUA) amenukuliwa akisema   “imethibitishwa na kufanyiwa utafiti  kupitia Idara ya Sayansi na Chakula iliyopo SUA na kugundua kuwa mti wa mlonge ni mti muhimu sana katika jamii na una faida nyingi.”....

Mlonge unaweza kutibu Pumu, Kikohozi na Kifua Kikuu. Aidha, magonjwa mengine kama Kisukari, Shinikizo la damu, magonjwa ya ngozi, magonjwa ya kwenye njia ya mkojo (UTI) kuongeza kinga ya mwili (CD4) na kuongeza nguvu za kiume.

Mbegu za Mlonge hutibu maradhi pia kama Malaria, Saratani ya tumbo, hupunguza sonona stress, huleta hamu ya kunywa maji, jambo amabalo ni adimu kwa watu wengi

Faida nyingine  itokanayo na unga wa majani ya mti wa mlonge ni kusafishia maji ambayo ni machafu na kuweza kuwa safi na salama na kuwa tayari kwa matumizi yoyote ya nyumbani kama vile kupikia na kunywa,  hii inaweza kuwa ni mbadala ya madawa mengine yanayoweza kutibu maji kama vile watergard na mengineyo.

Majani ya Mlonge yamepachikwa jina la chakula chenye viwango kwasababu wanasayansi waligundua yana kiasi cha madini ya Kalisium yanayoweza kupatiakana katika glasi nne za maziwa, kiasi cha vitamini c inayopatikana kwenye machungwa saba, Potasium ya kwenye ndizi mbivu tatu. Pia unapata kiasi cha madini ya chuma mara nne zaidi.

Majani ya Mlonge yana Vitamin A nyingi kuliko karoti, vitamin C nyingi kuliko machungwa na madini ya Potassium nyingi kuliko ndizi mbivu, halikadhalika ubora wa protini yake ni bora kushinda maziwa na mayai.

Kutokana na kuwa na kiasi kingi cha madini ya chuma (Iron), kasiamu (Calcium) na vitamin nyingi za aina mbalimbali, majani ya mmea huu yamekuwa yakitumika kama ‘tonic’ kwa watoto wadogo na vijana ili kuimarisha mifupa na kusafisha mfumo wa damu mwilini.
Majani mabichi ya Moringa ni mazuri kwa kina mama wajawazito na wenye kunyonyesha, huongeza wingi wa maziwa na hushauriwa kwa kutibu Anaemia.
-Juisi ya majani ya Moringa hutumika kusafisha tumbo na hutibu magonjwa ya zinaa. Juisi ikichanganywa na asali inatibu kuharisha.
Pia juisi ina uwezo wa kusawazisha presha (BP) na kudhibiti viwango vya sukari kwa wagonjwa wenye kisukari.

-Majani pia huweza kupakwa mwilini katika kutibu majipu na maambukizi ya ngozi.

-Waweza kutumia majani kama unavyotumia mchaichai na hapo unatibu MALARIA bila kujua.......Majani ya Mlonge yanaweza kutafunwa mabichi, yaliyochemshwa kama mboga au yaliyokaushwa na kusagwa kuwa unga. Unga wake unaweza kuhifadhiwa kwa miezi kadhaa bila kupoteza ubora na faida zake za kiafya huku ukitumia kama kiungo kwenye mboga na mchuzi (zingatia usikaushe kwenye JUA)
​Mafuta kutoka kwenye mbegu za mti wa Moringa huweza kutumika katika kupikia na kuwasha katika nyumba. Pia hutumika sana kwenye viwanda katika utengenazaji wa sabuni na bidhaa za urembo. Mafuta hukamuliwa kutoka kwenye mbegu kama ambavyo alizeti hukamuliwa.

Licha ya kuwa dawa nzuri sana ya kusafisha tumbo (Jaribu kutafuna mbegu zake tatu baada ya kumenya huku ukinywa maji mengi sana na kuhakikisha upo jirani na choo) Mbegu za mti wa Moringa ni kinga dhidi ya vijidudu (bacteria) wasababishao magonjwa na kuathiri ngozi.

Pia mbegu hutuminka katika kusafisha au kuchuja maji ambapo zikipondwa na kuwekwa kwenye maji yenye tope au machafu husababisha uchafu kujikusanya na kuzama chini kisha kuacha maji yakiwa safi na salama kwa kupikia au kunywa baada ya kuchemsha.

Magome

Magome ya mti wa Moringa hupondwa na kuwa rojorojo kisha hutumika kutibu majipu pia hupakwa ili kupunguza maumivu yatokanayo na kung'atwa na wadudu kama nyoka na nge. mmea huu pia ni MBOLEA 

...........HIZI NI BAADHI TU LAKINI WAWEZA JISOMEA ZAIDI KUPITIA VYANZO MBALIMBALI ..............

Ndugu tuna tabibu mbalimbali, za asili na zisizo na madhara kama ya vidonge vya makemikali na bado tunapuuza.
Nimekuwa nikiusikia huu mmea leo umepata undani matumizi yake.

ni zao zao rahisi kupanda unapanda umbali wa mita 3 unapanda punje mbili kila shimo ikiota vizuri unang'oa moja baada ya miezi 9 inaanzakuzaa unavuna x2 kwa mwaka mlonge unazaa sana ila kung'oa mlonge sio kazi rahisi una kiazi ambacho hakifi

imeandikwa na Geofrey Chambua kutoka vyanzo mbalimbali​


Kodi ya simu yazaa matunda

Imeandikwa na Stella Nyemenohi, Dodoma | Habari Leo



SHERIA ya Fedha ya Mwaka 2016 iliyopitishwa kuhusu utozaji ushuru kwenye ada ya kutuma na kupokea fedha kwenye miamala ya benki na simu, imeanza kuzaa matunda kutokana na ongezeko la mapato lililoanza kushuhudiwa kutoka kampuni za simu.

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu iliyokutana jana na Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA), iliambiwa kutokana na sheria hiyo iliyopitishwa Bunge baada ya kupitisha bajeti ya mwaka huu, mwezi uliopita serikali imeshuhudia ongezeko kubwa la mapato, yaliyotolewa na kampuni za simu.

Taarifa hiyo ilitolewa jana kwenye Kamati ya Kudumu ya Miundombinu, imeonesha Kampuni ya Vodacom ilikuwa ikitoa kodi ya ushuru wa bidhaa kwa fedha zinazotumwa kwa wastani wa Sh milioni 360 kwa mwezi, lakini baada ya mabadiliko ya sheria, Julai pekee mwaka huu imelipa Sh bilioni 1.9.

Mwakilishi wa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato (TRA), Godwin Barongo aliiambia kamati hiyo kuwa kwa upande wa Kampuni ya Tigo, walikuwa wanatoa wastani wa Sh milioni 250 kwa mwezi, lakini sasa wametoa Sh bilioni 1.48.

Barongo ambaye ni Meneja Msaidizi, Kitengo cha Walipa Kodi Wakubwa TRA alikuwa akizungumzia namna Mtambo Maalumu wa Kusimamia Mawasiliano na Udhibiti wa Mapato yatokanayo na Simu (TTMS) unaosimamiwa na Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA) ulivyowezesha kufanikisha ukusanyaji mapato.

“Pamoja na mabadiliko ya sheria yaliyoanza mwezi Julai mwaka huu, kampuni za simu zilikuwa zikitoza transfer, lakini sheria ilikuwa haigusi kwenye kutoa, Baada ya hiyo, tuligundua kuwa sasa kamisheni nyingi zilipelekwa kwenye kutoa kwa sababu hakuna tozo na kwenye transfer zinapungua,” alisema Barongo.

Aliendelea kusema, “Kwa hiyo mabadiliko haya ya sheria ya sasa hivi ambayo tunatoza kwenye kuweka na kutoa, yametusaidia.” Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, Selemani Kakoso alisisitiza kuwa wabunge wanategemea Wizara ya Miundombinu kupitia sekta ya mawasiliano, ichangie mapato mengi kwa serikali.

Baada ya Bunge kupitisha mabadiliko ya sheria ya fedha yaliyopitisha utozaji kodi ya ushuru wa bidhaa katika miamala ya benki na simu za mkononi, ulijitokeza mjadala ambao baadhi ya watu walidai ushuru huo utaathiri wateja wa kampuni za simu na benki.

Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango alifafanua kwamba serikali imeamua kutoza ushuru kwenye ada ya kutuma na kupokea fedha au vyote kwa kadri itakavyotozwa akisisitiza kwamba utalipwa na benki na kampuni na si mtumiaji au mpokeaji wa fedha katika miamala itakayofanyika.

Wakati huo huo akielezea Mtambo Maalumu wa Kusimamia Mawasiliano na Udhibiti wa Mapato yatokanayo na Simu (TTMS), Barongo alisema pia umesaidia kwa kiwango kikubwa katika mapato kutoka kampuni za simu. Barongo alisema kabla ya mwaka 2013, mtambo ulipokuwa haujapatikana, walishindwa kujua kiwango cha kodi kutoka kwenye kampuni za simu.

Aliwaambia wabunge kuwa awali kulikuwa na tatizo kubwa la kufahamu ni kwa kiwango gani kampuni za simu zinazalisha ikizingatiwa kwamba, mfumo wa sasa wa ulipaji kodi ni wa kujitathmini.

“Kwa hiyo tunasema huu mfumo unasaidia, unaonesha sasa ni namna gani sasa wanaweza (kampuni za simu) kutambua kuwa wanafuatiliwa kwa nyuma,” alisema.

Awali, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, James Kilaba alisema mtambo huo wa TTMS una kazi nyingi ikiwemo kutambua mawasiliano ya udanganyifu katika mitandao na namba za ulaghai zinazotumika kwenye mawasiliano ya kimataifa kinyume cha sheria.

Akizungumzia hoja za baadhi ya wabunge waliotaka kufahamu ni kwa nini kampuni za simu haziko kwenye walipa kodi wakubwa 10 wa mwanzo , Barongo alisema hivi sasa zinapangwa kulingana na sekta. Hata hivyo alisema, itakapokuja kwenye sekta ya mawasiliano, anaamini angalau kampuni tatu za simu zitaonekana kwenye nafasi ya juu.

Aliisifu kampuni mpya ya Halotel akisema inafanya vizuri. Kwa upande wa TTCL, alisema bado haijatoa mchango wa kutosha katika mapato ya serikali, jambo aliloshauri kuwa inahitaji kusaidiwa hatimaye iwe miongoni mwa vyanzo vya mapato ya serikali.

‘Maandamano ya Ukuta ni ndoto ya mchana’

Imeandika na Lucy Lyatuu, Halima Mlacha na Jonas Kamaleki, Maelezo.


MSOMI maarufu nchini, Profesa Benson Bana na mwanasiasa aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa chama cha NCCR-Mageuzi, Leticia Mosore wamesema maandamano yaliyopewa jina la Umoja wa Kupinga Udikteta Tanzania (Ukuta), hayawezekani kwani ni ndoto ya mchana na hayana msingi wowote wala tija kwa wahusika hata kwa Taifa.

Aidha, maandamano hayo ya nchi nzima imeelezwa kuwa ndio kifo cha Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), kwani kila chama kimekuwa kikihangaika kivyake.

“Wanaotaka kuandamana wanajidanganya na kuwalaghai wenzao kwani kufanya operesheni ni suala la dola na si la mtu au kikundi cha watu, hivyo maandamano hayo hayawezekani kabisa,” alisema Profesa Bana katika mahojiano maalumu na Idara ya Habari (MAELEZO).

Mhadhiri huyo Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, aliongeza kuwa wanaojiita Ukuta ni kwamba Rais John Magufuli amewanyima ajenda, kwani utendaji wake umezidi fahamu zao na kuwafanya waanze kutapatapa wasijue nini cha kufanya.

Alisema kama viongozi wa Ukuta ni waungwana, inabidi watamke wazi kuwa wametafakari na kuona kuwa maandamano hayana maana hivyo wameamua kuyasitisha nchi nzima.

Kuhusu utendaji wa Serikali ya Awamu ya Tano, Profesa Bana alisema ni serikali yenye maamuzi ya uhakika na inayowajali watu wote bila kujali itikadi zao za vyama, dini wala makabila hivyo inabidi Watanzania waipende na kuiheshimu.

“Rais Magufuli utendaji wake ni wa kuigwa na viongozi wengi duniani kwani anafanya maamuzi ya uhakika ikiwemo kukuza uchumi kwa kukusanya kodi na kuziba mianya ya ubadhirifu wa mali ya umma,” alisema Profesa Bana.

“Pamoja na kuwa Rais Magufuli amekuwa madarakani kwa kipindi kifupi, viashiria vyote vinaonesha kuwa ni kiongozi imara na shupavu kutokana na mambo makubwa ambayo ameyafanya kwa kipindi hiki kifupi. Katika kipindi hiki kumekuwepo na nidhamu katika utumishi wa umma, kodi inakusanywa kwa kiwango kikubwa na elimu ya msingi inatolewa bure kama Ilani ya Uchaguzi ya Chama Tawala inavyosema,” alisema Profesa Bana.

Aidha, Profesa Bana alisema kuwa wanaomlaumu Rais Magufuli ni wale ambao hawajitambui na labda wanaona mianya ya ubadhirifu anayoendelea kuiziba, wao wanakosa mapato, vinginevyo Rais anafanya vizuri katika kuliongoza Taifa.

“Rais Magufuli yuko sahihi kwa jinsi anavyosimamia vipaumbele vya serikali ikiwemo elimu bure, kukusanya kodi na kuzuia mianya ya rushwa pia dhamira ya kuifanya Tanzania kuwa na uchumi wa viwanda,” alifafanua Profesa Bana.

Aliitofautisha Serikali ya Awamu ya Tano na awamu nyingine zilizopita kwa kutokuwa na kigugumizi katika kufanya maamuzi ikiwemo ya kuhamia Dodoma, kuondoa wabadhirifu katika utumishi wa umma na kupunguza matumizi yasiyo ya lazima na fedha hizo kutumika kwa miradi ya maendeleo kama miundombinu, afya na elimu.

Kwa upande wake, aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha NCCR Mageuzi, Leticia Mosore amesema vyama vilivyoko katika Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), vimepoteza mwelekeo na vinashindwa kwenda na kasi ya Serikali ya Awamu ya Tano.

Mosore alisema ujio wa maandamano ya nchi nzima yaliyopewa jina la Ukuta, ndio kifo cha Ukawa kwani kila chama kimekuwa kikihangaika kivyake.

Kuhusu Ukawa kupoteza mwelekeo, alisema Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Dk Magufuli inayafanyia kazi kivitendo yale yote ambayo yalikuwa ni kero na matatizo yaliyokuwa yakipigiwa kelele na upinzani, na hivyo ingewapasa sasa kufurahia na kumpongeza kwa dhati kwa hatua hizo.

Alisema Ukawa hivi sasa imekuwa ikitoa matamko ya ajabu, imekuwa kama umoja wa kufanya vituko bungeni kila siku wanatoka na kususa, kufunga midomo, mara wavae nguo nyeusi, na hata kuwatimua wale wanaotofautiana nao.

Katika hatua nyingine, Mosore alisisitiza kwamba hatambui kusimamishwa uanachama na uongozi katika chama hicho na ataendelea kufanya majukumu yake kama kawaida kwa kuwa barua aliyopewa haijatoa sababu za hatua hiyo. Alisema hakupewa haki ya kujitetea kwa mujibu wa Katiba ya chama hicho ya mwaka 1992.

“Ninachoweza kusema kwa ufupi, sitambui kusimamishwa uanachama kwa sababu sijaelezwa sababu za kusimamishwa kwangu wala barua haielezi vifungu vya kikatiba au kanuni zilizotumika kufikia maamuzi,” alisema Mosore.

Uongozi wa wafanyabiashara ndogo maarufu kama ‘wamachinga’ wa soko la Mwenge jijini Dar es Salaam, umesema hauungi mkono maandamano ya Ukuta kwa kuwa maandamano hayo si halali kisheria. Uongozi huo, umesema maandamano hayo hayana uhalali wa kisheria kwa kuwa tayari Jeshi la Polisi nchini limeyazuia.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa Wafanyabiashara wa soko hilo, Omari Hamisi alisema hawapo tayari kuumizwa na askari Polisi kwa sababu ya maandamano hayo ya Ukuta.

Alisema wafanyabiashara hao wanamuunga mkono Rais John Magufuli kwa kutojihusisha na maandamano hayo na badala yake wataendelea na kazi yao ya kufanya biashara ikiwa ni njia ya kutekeleza kaulimbiu ya rais huyo ya ‘Hapa Kazi Tu’.

Kiongozi huyo, alibainisha kuwa Dk Magufuli tangu aingie madarakani, amekuwa akiwatetea wanyonge hasa wafanyabiashara ndogo hivyo kujihusisha na maandamano hayo ni sawa na kumsaliti. Alisema rais huyo alionesha wazi nia yake ya kutetea wanyonge alivyozungumza hivi karibuni na wananchi wa Mwanza na baadaye Dar es Salaam ambako alielezea mikakati na mipango ya Serikali ya Awamu ya Tano katika kuwasaidia na kuwakomboa wanyonge.

“Dk Magufuli ameonesha nia ya dhati kutetea wanyonge sasa leo hii tukiandamana na kuunga mkono maandamano yaliyozuiwa na Polisi ni sawa na kumsaliti,” alisema.

“Ukuta ina maana gani na faida gani kwetu? Nchi yetu ni moja, taifa letu ni moja, sisi ni wamoja hivyo hatukubali kufanya maandamano yasiyo na tija kwetu na taifa pia,” alisisitiza na kueleza kuwa wafanyabiashara hao wameshtuka na kuchoshwa na kitendo cha wanasiasa kuwatumia vijana wachache kwa faida yao binafsi.

Maandamano ya Ukuta yaliyoratibiwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) yakilenga kupinga kile wanachokiita udikteta wa Serikali ya Rais Magufuli yanatarajiwa kufanyika kesho nchi nzima. Polisi na vyombo vingine nchini vimetangaza kuwa maandamano hayo si halali.

 

MHE. SAMIA SULUHU AHUDHURIA UFUNGUZI WA MKUTANO WA 36 WA SADC MJINI MBABANE SWAZILAND

Written By CCMdijitali on Tuesday, August 30, 2016 | August 30, 2016

Mwenyekiti anayemaliza muda wake wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika -SADC-
ambaye pia ni Rais wa Botswana Luteni Jenerali Dkt. Seretse Khama Ian
Khama amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John
Pombe Magufuli kwa kuchaguliwa kwake kwa kishindo katika uchaguzi mkuu
uliofanyika mwaka jana.

Rais huyo wa Botswana ametoa kauli hiyo
ya pongezi katika hotuba yake kwenye ufunguzi wa Mkutano wa 36 wa Wakuu
wa Nchi na Serikali wa SADC unaofanyika Mbabane- Swaziland ambapo Katika
Mkutano huo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dakta JOHN POMBE
MAGUFULI anawakilishwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Rais huyo wa Botswana amesema ukuaji
wa demokrasia katika nchi wanachama wa jumuiya ya SADC unaendelea
kuimarika hivyo ni muhimu jitihada hizo zikaendelezwa zaidi.

Amesema ana Imani kubwa na Viongozi waliochaguliwa kwa njia ya
amani,uhuru na haki katika ukanda wa SADC akiwemo Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania na Rais wa Jamhuri ya Visiwa shelisheli kwamba
watafanya kazi kwa bidii ili kuharakisha maendeleo kwa wananchi wao.


Wakuu wa nchi na Serikali wa SADC katika mkutano huo wameshuhudia
utoaji wa zawadi mbalimbali kwa wanafunzi waliofanya vizuri katika
utunzi wa insha na kwa wanahabari ambao wameandika habari mbalimbali
kuhusu SADC ikiwemo masuala ya huduma ya maji.

Aidha katika Mkutano huo wa 36 wa SADC viongozi wanaohudhuria watafanya uchaguzi wa
Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa SADC na Uchaguzi wa Mwenyekiti na
Makamu Mwenyekiti wa Asasi ya SADC ya Siasa, 
Ulinzi na Usalama ( SADCTroika).

Katika mkutano huo Wakuu wa nchi na serikali pia
watapokea rasimu za maboresho ya mikataba mbalimbali kutoka kwenye
Baraza la Mawaziri kwa ajili ya kutia saini. Miongoni mwa rasimu hizo ni
mkataba wa kuboresha itifaki ya SADC dhidi ya rushwa, maboresho ya
itifaki ya ushirikiano wa siasa, ulinzi na usalama ya SADC na maboresho
ya itifaki ya biashara.

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisaini ubao wa kumbukumbu kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli wenye majina ya viongozi waliohudhuria mkutano wa 36 wa SADC uliofanyika Lozitha, Mbabane Swaziland.

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu  Hassan (katikati) akiwa kwenye mkutano wa 36 wa Wakuu wa Nchi na Serikali za Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) uliofunguliwa leo kwenye ukumbi wa Mandvulo uliopo Lozitha, Swaziland.

 Mfalme Mswati wa III (kushoto) akihutubia kwenye ufunguzi wa mkutano wa 36 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC kwenye ukumbi wa Mandvulo, Lozitha Swaziland.

 Binti akionyesha bendera ya Tanzania wakati wa kuimba shairi maalum ya ufunguzi wa mkutano wa 36 wa SADC

Wakuu wa nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa  Afrika (SADC) wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya ufunguzi wa mkutano wa 36, Lozitha Swaziland.

Dangote shakes Kenya’s cement market with Ethiopia imports

Nigeria’s Dangote Cement has started its shake-up of the Kenyan market with 

importation of the commodity from its plant in neighbouring Ethiopia 

as it prepares to establish a local manufacturing plant.

Mr Aliko Dangote, the president of Dangote Group. PHOTO | FILE  

In Summary
  • Ethiopia imports are expected to further drive retail prices downward in a market where they have remained static for nearly 10 years.
  • The cement exported to Kenya is priced at about Sh7,400 per tonne, making it up to 40 per cent cheaper than locally manufactured brands.

By VICTOR JUMA, vjuma@ke.nationmedia.com

Nigeria’s Dangote Cement has started its shake-up of the Kenyan market with imports of the commodity from its plant in neighbouring Ethiopia as it prepares to establish a local manufacturing plant.

Dangote’s targeting of the Kenyan consumer with low-cost cement from Ethiopia is expected to further drive retail prices downward in a market where they have remained static for nearly 10 years.

Importing cement into Kenya is seen as Dangote’s short-term market entry plan as it prepares to establish a local plant in 2019.

“In addition, we have begun exporting cement to neighbouring Kenya,” the company, which is owned by Africa’s richest man, Aliko Dangote, said in its latest trading update.

Dangote said the cement exported to Kenya is priced at about $74 (Sh7,400) per tonne, making it up to 40 per cent cheaper than locally manufactured brands.

The price is expected to incorporate the cost of transporting the cement to Kenya as well as taxes where applicable, while still leaving the company with a profit.

Dangote, which plans to topple LafargeHolcim as the largest producer of cement in Africa, rides on economies of scale to set lower prices that in turn grows its market share. Its plant in Ethiopia has an annual production capacity of 2.5 million tonnes.

However, cement industry sources said the exports mainly covered supplies to road construction projects in northern Kenya.

Dangote also started selling cement in Tanzania early this year after completing its factory in Mtwara about 400 kilometres from Dar es Salaam.

The company cut prices in Tanzania to rapidly gain market share at the expense of rivals, including Kenyan multinationals with a presence in that market.

ARM Cement said in a commentary accompanying its latest results that cement prices in Tanzania fell by a third in the half year ended June as a result of Dangote’s entry.

Dangote said in the trading update that it took market share from its competitors in Tanzania despite incurring higher transport costs since its factory is located relatively farther away from Dar es Salaam.

“We estimate that in June we achieved 23 per cent market share across Tanzania and were the leading supplier of cement in the key market of Dar es Salaam,” Dangote said.

The Nigerian firm’s price in Tanzania stood at about $80 (Sh8,000) per tonne in June, undercutting its competitors by more than 20 per cent.

The company is expected to replicate its lower-pricing strategy in Kenya when it starts to produce cement locally in 2019.

Dangote, which already has a licence to prospect for limestone in Kitui, says it has revised the upcoming factory’s annual production capacity to three million tonnes from the previous 1.5 million.

READ: Dangote to build Kenya cement plant in $1.48bn Africa deal

It has incorporated two majority-owned subsidiaries to house its local limestone mining and cement production operations. It has a 90 per cent stake in Dangote Cement Kenya Limited and a similar stake in Dangote Quarries Kenya Limited. The minority interests in the subsidiaries are not disclosed.

“We are still in the process of finalising agreements for the construction of a factory in Kenya, which we expect to be in operation in 2019,” Dangote said in an earlier trading update.

“Key factors will be good availability of limestone close to Kenya’s centres of demand.” The cost of the plant is yet to be confirmed, Dangote said.

The multinational’s entry comes at a time when cement prices in Kenya have dropped significantly on the effect of increased imports and expansion by established and new players.

The excess capacity, contributed to by the setting up of new firms such as National Cement and Savannah Cement, has seen the average retail price of a 50kg bag of cement drop to Sh670 from the peak of Sh740 in 2008.

The resultant price wars have cut margins, leaving cost cutting and volume sales as the major profit drivers.

Despite the excess capacity, cement firms are planning more expansion in what will further heighten competition. ARM Cement, for instance, intends to build a new clinker and cement factory in Kitui in the medium term, backed by its new single-largest shareholder, CDC Group.

Viongozi Chaumma waungana na JPM kuhamia Dodoma


Kwa ufupi

Makamu Mwenyekiti wa chama hicho Kayumbo Katubali alisema ujio wa Serikali bado ni wa kusuasua kuliko kama Chaumma kingeingia madarakani kwani kilikuwa na mkakati thabiti wa kuanzia Serikali yao Dodoma tangu siku ya kiapo.


By Habel Chidawali, Mwananchi hchidawali@mwananchi.co.tz

Dodoma. Chama cha Ukombozi wa Umma (Chaumma) kimempongeza Rais John Magufuli kwa hatua yake ya kutekeleza azimio la kuhamishia makao makuu ya Serikali mkoani Dodoma, huku kikisema huo ndiyo ulikuwa mkakati wa chama hicho wa muda mrefu.

Makamu Mwenyekiti wa chama hicho Kayumbo Katubali alisema ujio wa Serikali bado ni wa kusuasua kuliko kama Chaumma kingeingia madarakani kwani kilikuwa na mkakati thabiti wa kuanzia Serikali yao Dodoma tangu siku ya kiapo.

“Nampongeza Magufuli, ametuonyesha kwa vitendo siyo maneno yaliyokuwa yakisemwa na wanachama wa chama chake kwa zaidi ya miaka 40. Sisi kwenye ilani yetu ya Uchaguzi Mkuu tulipanga kuanzia Dodoma na si vinginevyo,” alisema Kabutali.

Kabutali alisema kwenye ilani yao ya uchaguzi, ibara ya 18 walieleza Serikali yao itakuwa Dodoma baada ya kutangazwa washindi. Mwanasiasa huyo alimtaka Rais Magufuli kukamilisha mchakato wa kuhamia mjini hapa kwa kuutungia sheria ili wanasiasa wasitoe matamko yasiyo na tija.

Kuhusu wakazi wa Dodoma alisema kuwa huenda ikawa faraja kwao kwani kwa sasa Serikali itakuwa karibu nao hivyo watapumzika manyanyaso waliyokuwa wakiyaopata wanapotafuta ardhi.

Alisema wakazi wa Dodoma walishachoshwa na urasimu wa Mamlaka ya Uendelezaji Makao Makuu (CDA) na ndiyo maana migogoro ya ardhi ikawa haimaliziki. Aliwataka wana-Dodoma wawe makini na wasikubali kudanganywa na wajanja katika masuala ya ardhi.

Katibu Chadema Mwanza abwaga manyanga

Aliyekuwa Katibu wa Chadema Mkoa wa Mwanza, John Nzwalile (Kulia). Picha na mtandao


Kwa ufupi

  • Mbali na ukatibu wa mkoa, Nzwalile alikuwa mjumbe wa Baraza Kuu Taifa na mjumbe wa mkutano mkuu wa chama hicho taifa.



By Jesse Mikofu, Mwananchi mwananchipapares@mwananchi.co.tz



Mwanza. Katibu wa Chadema Mkoa wa Mwanza, John Nzwalile amejivua nyazifa zake tatu pamoja na uanachama wa chama hicho kwa madai kuwa chama hicho kimekuwa na ubabaishaji.


Mbali na ukatibu wa mkoa, Nzwalile alikuwa mjumbe wa Baraza Kuu Taifa na mjumbe wa mkutano mkuu wa chama hicho taifa.

Akizungumza na waandishi wa habari leo mkoani Mwanza, Nzwalile amesema Chadema kimekuwa kikiwachonganisha wananchi na Serikali, jambo ambalo amesema halikubaliki.


“Nimefikia uamuzi huu mgumu wa kujivua nyadhifa zangu zote na uanachama wa Chadema baada ya kuchoshwa na siasa za uchochezi, majungu na uchonganishi zinazofanywa na chama hiki kikubwa cha upinzani nchini,” amesema Nzwalile


Amesema imefika hatua viongozi wa Chadema wakijifungia ndani kwenye vikao vyake vinahusu maandamano na uchochezi pekee, kwanini “tusifanye shughuli za maendeleo badala ya kuhamasiha vurugu na uvunjifu wa amani,” amehoji Nzwalile.




Former President Mwai Kibaki discharged from hospital, says family

The former president will recuperate for a few more days before 

returning to Kenya.

Former President Mwai Kibaki acknowledges greetings during the 50th Jamhuri Day celebrations at Safaricom Stadium Kasarani in Nairobi on December 12, 2013. Mr Kibaki has been discharged from a Johannesburg hospital where he was admitted on August 21, 2016. PHOTO | MARTIN MUKANGU | NATION MEDIA GROUP

In Summary
  • Former President Mwai Kibaki discharged from a Johannesburg hospital where he was admitted, says his family.




By JOEL MUINDE
More by this Author

Former President Mwai Kibaki has been discharged from a Johannesburg hospital where he was admitted more than a week ago.

Mr Kibaki's family has said the former president is in "jovial and high spirits" and will continue to recuperate for a few more days before returning to Kenya.

The former leader underwent a surgery in the South African facility, Netcare Sunninghill Hospital, to remove a blood clot in a vein in his neck.

A South African source told Nation that doctors at the facility located the clot in good time while it was in a relatively safe part of the body.

A clot in the blood is generally dangerous especially if it gets into organs such as the brain, heart and the lungs.


USHIRIKIANO KATIKA SEKTA YA MAWASILIANO NA KAMPUNI YA ALARKO KUTOKA UTURUKI, NA SHIRIKA :LA MAENDELEO UJERUMANI (GIZ)

Written By CCMdijitali on Monday, August 29, 2016 | August 29, 2016

 Mkuu wa Wakurugenzi wa Kampuni ya Alarko kutoka nchini Uturuki Bw. Izzet Garih (wa kwanza kushoto) akizungumzia  kuhusu ushirikiano baina ya kampuni hiyo na sekta ya mawasiliano,  na (wa kwanza kulia) ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano anayesimamia  sekta ya Mawasiliano Prof. Faustin Kamuzora. 

 Picha ya pamoja baada ya mazungumzo.

 Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) Dkt. Kamugisha Kazaura akizungumza  wakati wa kikao  cha  Ushirikiano baina Sekta ya Mawasiliano na Kampuni ya Alarko.

 Mwakilishi Mkazi wa shirika la Maendeleo la Ujerumani (GIZ) Dkt. Regine Qualmann (katikati) akizungumza jinsi wanavyoitumia TEHAMA  katika kufikisha huduma, (kushoto) ni Katibu
Mkuu wa Wizara  ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano anayesimamia sekta ya Mawasiliano Prof. Faustin Kamuzora na (Kulia) ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Mhandisi Dkt. Maria Sasabo.  


Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano anayesimamia sekta ya Mawasiliano Prof. Faustin Kamuzora (kushoto) akizungumza na Mwakilishi Mkazi wa shirika la maendeleo la Ujerumani (GIZ) Dkt. Regine Qualmann kuhusu ushirikiano baina ya Wizara  na  shirika hilo katika upande wa Tehama .


Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini,
Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

NDC yakopeshwa bil 4/- kukabili malaria

Imeandikwa na Anastazia Anyimike | Habari leo 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu ( Sera, Bunge,Vijana, Kazi, Ajira na Walemavu) Jenister Mhagama akikabidhi mfano wa hundi ya mkopo ambao Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) limeutoa kwa Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC) kwa ajili ya kuongeza uzalishaji kwenye kiwanda cha viuadudu cha Kibaha, Pwani. Katikati ni Mwenyekiti wa Bodi wa NDC, Dk Samuel Nyantahe, kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Azania Bank, Godfrey Dimaso na Kulia ni Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Assumpta Mshama.

SHIRIKA la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) limelikopesha Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC) dola za Marekani milioni 2.1 ambazo ni sawa na sh bilioni nne za Tanzania kuongeza uzalishaji katika kiwanda cha viuadudu kilichopo Kibaha, Pwani.

Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Profesa Godius Kahyarara amesema mkopo huo utakiwezesha kiwanda hicho kujiendesha kwa ufanisi na kuongeza usalishaji. Profesa Kahyarara amesema kiwandani hapo kuwa, mkopo huo utapitia na kusimamiwa na Benki ya Azania.

Amesema, NSSF ipo tayari kupokea maombi mengine ya mkopo kutoka NDC kwa kuwezesha masoko ya bidhaa hiyo.

“Huo ni mwanzo wa NSSF kuunga mkono katika uwekezaji kwani tunatarajia kuwekeza kuifufua shirika la usagishaji (National Millings), kiwanda kikubwa cha sukari ambacho tutakijenga kwa kushirikiana na PPF, kiwanda cha nguo, viatu na matairi,” amesema.

Profesa Lipumba, Sakaya wasimamishwa CUF

Imeandikwa na Mroki Mroki | Habari Leo
Profesa Ibrahimu Lipumba

BARAZA Kuu la Uongozi la Chama cha Wananchi CUF, limewasimamisha uanachama wanachama 11 akiwemo aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama hicho Taifa, Profesa Ibrahimu Lipumba na Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho Bara, Magdalena Sakaya.

Wanasiasa hao wamesimamishwa uanachama hadi watakapojieleza katika Baraza Kuu. Wanachama wawili Rukia Kassim Ahmed na Athumani Henku wamepewa karipio kali. Uamuzi wa Baraza Kuu la Uongozi la CUF umetolewa jana Jumapili wakati wa mkutano mkuu wa dharula.

Baraza hilo limemfuta uanachama aliyekuwa Kaimu Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Wazee wa CUF (JUWACUF), Shashu Lugeye.

“Baraza Kuu limechukua hatua mbili kubwa ambazo ni kutoa karipio kali, kusimamisha na kufukuza uanachama wahusika wote walioshiriki kuchochea vurugu zilizotokea wakati wa mkutano wa dharura Agosti 21, mwaka huu,”amesema Naibu Katibu Mkuu wa CUF, Nassor Ahmed Mazrui.

Mazrui imewataja wanachama 11 waliosimamishwa uanachama hadi watakapojieleza katika kamati ya uongozi ni Prof Ibrahim Haruna Lipumba, Magdalena Sakaya, Abdul Kambaya, Ashura Mustafa, Omar Mhina Masoud, Thomas Malima, Kapasha M. Kapasha, Maftaha Nachumu, Mohamed Habib Mnyaa, Haroub Shamis na Mussa Haji Kombo.

Inadaiwa kuwa walishiriki katika vurugu zilizosababisha kuvunjika Mkutano Mkuu wa dharura wa chama hicho Agosti 21 mwaka huu jijini Dar es Salaam.

“Baraza Kuu la Uongozi la Taifa limeridhika kwamba watu hao waliokuwa vinara wa vurugu na njama hizo ovu walipewa nafasi mara kadhaa kujirekebisha dhidi ya mwenendo wao huo dhidi ya chama lakini waliendelea na vurugu na hujuma zao hizo. Kwa hatua iliyofikia, Baraza Kuu limeona halina njia nyengine ya kukinusuru chama isipokuwa kuchukua hatua kali na madhubuti kukilinda chama ambao ni wajibu wake kikatiba,”amesema Mazrui.

Lema agoma, apambana na polisi

Imeandikwa na Veronica Mheta, Arusha


MBUNGE wa Arusha Mjini, Godbless Lema (Chadema) amezua tafrani kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha, baada ya askari polisi waliomleta awali kutaka apande gari kwenda mahabusu kwa sababu ya kutokidhi masharti ya dhamana.

Awali, Lema alisomewa makosa mawili yaliyokuwa yakimkabili mbele ya Hakimu Mkazi wa mahakama hiyo, Desdery Kamugisha na Wakili wa Serikali, Innocent Njau.

Katika mashtaka ya kwanza ni la kutuma ujumbe mfupi wa maneno kutoka kwake kwenda kwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo. Mashtaka ya pili, kutumia Whatsapp kwa ajili ya kuwashawishi wananchi wa Jiji la Arusha, kuandamana Septemba mosi.

Baada ya Lema kusomewa mashtaka hayo, Hakimu Kamugisha alimuuliza kama ni kweli au la; na Lema alikana. Baada ya kukana, wakili Njau aliomba Lema asipewe dhamana kwa sababu wana taarifa za kiintelijensia kuwa endapo atapewa dhamana, usalama wake utakuwa mashakani.

Hoja ya wakili huyo wa serikali, ilipingwa na wakili wa utetezi, John Mallya. Baada ya mabishano hayo, Hakimu Kamugisha alitupilia mbali pingamizi la wakili Njau la Lema kunyimwa dhamana.



Baada ya sharti la dhamana kutolewa, wadhamini wawili walijitokeza ambao ni madiwani wa Jiji la Arusha. Lakini, hali tofauti ilijitokeza baada ya wakili wa serikali, Njau kukagua barua ya kumdhamini Lema na kugundua kuna kasoro za matumizi ya majina.

Kutokana na sintofahamu hiyo, hakimu alikubaliana na hoja ya wakili Njau na kusema kuwa Lema atafute wadhamini wengine na kuahirisha kesi hiyo kwa muda hadi Septemba 19 mwaka huu.

Baada ya kusomewa kesi hiyo, ikasomwa kesi ya pili ambayo inadaiwa ya kutoa lugha ya uchochezi kati ya Agosi mosi hadi 26 mwaka huu kwa njia ya kurekodi kwa sauti ‘audio clip’ na kurusha kwenye mitandao ya kijamii kwa ajili ya kuhamasisha maandamano Septemba mosi mwaka huu.

Saa 8:20 mchana askari polisi walimtoa chumba cha mahabusu na kutaka kumpandisha gari la Polisi kwa ajili ya kumpeleka mahabusu Kisongo. Kutokana na sintofahamu hiyo, Lema alibishana na polisi hao, huku akiwa na mawakili wake, Mallya na James Lyatuu, waliohoji kuwa wanampeleka wapi wakati muda wa mahakama haujafika.

“muda wa mahakama haujafika mnanipeleka wapi, nasema nitafia hapa mahakamani, saa hizi ni saa 8:00 muda wa mahakama haujaisha, mnanipeleka wapi, siendi, mniue, siendi popote, mniue hapa hapa, muda wa mahakama haujaisha, ‘broo’ mnanipeleka wapi na kwa nini mnanifanyia hivi, nasema siendi kokote, bora kufa, sikubali" alisema Lema.

UBINAFSI WA MADIWANI WA CHADEMA WAENDELEA KUITIA HASARA HALMASHAURI YA JIJI LA ARUSHA

 Mstahiki Meya wa Jiji la Arusha Bukhay Kalisti

Na Mwandishi Wetu - Arusha 
 
Madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Arusha wamevunja kikao cha Baraza la Madiwani kilichokua kinafanyika leo asubuhi 29/08/2016 kwenye Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa maslahi ya chama chao (CHADEMA) na kutupilia mbali shida na kero za wananchi waliowachagua.

Walinukuliwa mara baada ya kuvunja kikao hicho,wakitoa  sababu ambazo,zilionekana kutokuwa na mashiko kwa maslahi ya Wananchi au wapiga kura wao.

Baadhi ya sababu walizozitoa ni :-
  • Kuna madiwani 8 wanaotafutwa na Jeshi la Polisi,hivyo kuhofia kukamatwa ,endapo wangefika kwenye kikao hicho.
  • Walihitaji kwenda kuwawekea dhamana baadhi ya Viongozi wa Chama chao
  • Kuhudhuria kesi inayomkabili Godbless Lema inayotarajiwa kusikilizwa leo machana
         Mahakamani

Hivi ninajiuliza ,sababu hizi zina umuhimu wowote wa mustakabali wa Wananchi wa Jiji la Arusha ? Jibu hapana ! Na sababu ziko wazi tu.

              i.        Je katika Jiji la Arusha,hakuna watu wenye sifa za kuweza kuwadhamini Viongozi hao ?

            ii.        Je Jeshi la Polisi limeshindwa kuwafikia mahali walipo, ikiwa Godbless Lema  (Mbunge ) amekamatwa, sembuse wao ?

           iii.        Hivi kweli kwa akili za kawaida, iwapo kikao kilikuwa ni asubuhi na Godbless Lema anapelekwa Mahakamani Mchana, je walishindwa kuendelea na kikao hicho kwa masaa waliyokuwa nayo?

           iv.        Hivi kweli dhamana iliyohitajiwa ni ya Madiwani wote 33 wanaotokana na Chama cha Demokrasia (Chadema) ?
Ili kikao kiendelee ,kilihitaji kiwe na angalau Madiwani wasiopungua 17,lakini pia walishindwa kuona umuhimu wa Baraza hilo,kwani mambo ya msingi na maendeleo yangeweza kujadiliwa na wengine wangeweza kwenda kushughulika na masuala ya kesi na dhamana za viongozi wao.

            v.        Hivi tujiulize Kikao cha robo ya tatu ambacho kinategemewa kutoa maazimio muhimu na kupitisha miradi mbalimbali ya maendeleo kwa ajili ya Utekelezaji ili kuleta  maendeleo kwa wananchi kinavunjika kwa sababu ya  kuhudhuria kesi ya mtu mmoja na  madai eti wanatafutwa na Polisi ? 

           vi.        Zaidi ya yote Halmashauri imetumia gharama kubwa na muda mwingi kwa watumishi wake kuandaa kikao hicho,pamoja na gharama za kupeleka Makabrasha kwa madiwani wote ambapo Magari yake yametumika kusambaza Makabrasha kwenye Kata zote na kutoa matangazo kwa ajili ya Kikao hicho, lakini yote hayo hawakuyathamini  na kuamua  kuvunja kikao hicho  kwa sababu zao binafsi.

MTAZAMO WA KIZALENDO

Ifike mahali busara na Uzalendo upewe kipaumbele katika masuala ya msingi na ya lazima yanayohusu Maendeleo na mustakabali wa  Jiji letu la Arusha.

Ni wazi Madiwani wa Arusha hawakuchaguliwa na kikundi cha watu wachache wanaonekana kuwa bora au muhimu zaidi ya Wananchi waliowachagua.

Haingii akilini kesi ya mtu mmoja ambaye ni ya kujitafutia mwenyewe iingizie hasara serikali na kusababisa shughuli na mipango ya maendeleo ya Jiji la Arusha kusimama.

Itakuwa haina maana Halmashauri ya Jiji la Arusha kufanya kazi kwa maslahi ya Chama cha siasa(CHADEMA) badala ya maslahi ya wananchi na wakazi wa Jiji la Arusha.

Ninukuu kauli ya Mh. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk John Pombe Magufuli,ambayo amekuwa akihimiza na kuirudiarudia kila alipopata fursa ya kuongea na Wananchi kuwa “MAENDELEO HAYANA CHAMA” 

Kila mwanachama wa Chama chochote cha Siasa na wale wasiokuwa na Chama,wanahitaji Maendeleo. Kwa sababu hiyo,kila mmoja napaswa kufanya kazi kwa kuweka maslahi ya Wananchi wote mbele.

Kwa hicho walichokifanya Madiwani wa Chadema chini Mstahiki Meya Lazaro , hakikubaliki na kinasthili kuchukuliwa hatua za kisheria na kikanuni na kukemewa kwa nguvu zote na Wanachi wote wapenda wa Jiji la Arusha.

ARUSHA BILA UBINAFSI INAWEZEKANA.
 

 
Support : #BegaKwaBegaNaMamaSamia | JAK | CCM Arusha
Copyright © 2011. CCM Dijitali - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Jasper K
Proudly powered by Blogger
Link