NAIBU WAZIRI PINDA AELEKEZA UENDELEZAJI MIJI KUZINGATIA MIPANGO KABAMBE

Na Munir Shemweta, WANMM Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Geofrey Pinda amezielekeza Halmashauri zote nchini kuhakik...

Latest Post

PROF. MAKUBI AWATAKA WATUMISHI WA WIZARA AFYA KUFUATA MIONGOZO YA UNUNUZI

Written By CCMdijitali on Thursday, March 31, 2022 | March 31, 2022

  











PROF. MAKUBI AWATAKA WATUMISHI WA WIZARA 

AFYA KUFUATA MIONGOZO YA UNUNUZI


Wakurugenzi wa taasisi na wa Hospitali za rufaa za mikoa wametakiwa kufuata miongozo na sheria za manunuzi ili kuondoa hati chafu na zenye mashaka kwenye taasisi zao.

Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya afya Prof. Abel Makubi wakati akiendesha mkutano wa baraza kuu la wafanyakazi wa Wizara ya afya, taasisi pamoja waganga wakuu wa Hospitali za rufaa za mikoa lililofanyika jijini Dodoma.

Prof. Makubi amesema ni viongozi wanatakiwa kuwa mfano katika utekelezaji wa majukumu yao mahali pa kazi kwa kufuata miongozo na sheria ya manunuzi ya bidhaa kwa ajili ya mahitaji ya ofisi au ujenzi pamoja na maboresho ya miundombinu ya hospitali zao ili kuondokana na hati chafu au zenye mashaka.

Aidha, Prof. Makubi aliwataka waganga wafawidhi wa hospitali za Rufaa za Mikoa kuhakikisha wanasimamia upatikanaji wa dawa, vifaa na vifaa tiba kwenye hospitali zao.

"Ifike muda kila mgonjwa anayefika kwenye hospitali yako uhakikishe anapata dawa zilizopo kwenye mwongozo wa dawa (STG). Tunataka malalamiko yanayotolewa na wananchi yapungue ikiwemo ukosefu wa dawa pamoja na kutopata huduma kwa wakati". Alisisitiza Prof. Makubi.


Hata hivyo, Katibu Mkuu huyo aliwakumbusha viongozi hao pindi wanaporudi kwenye vituo vyao vya kazi kuwakumbusha madaktari walio chini yao kuandika dawa zilizopo kwenye muongozo huo na wahakikishe dawa wanazoziagiza ni zile ambazo zipo kwenye muongozo.

Prof. Makubi amewataka watumishi hao kutofanya kazi kwa mazoea na wanatakiwa kufanya kazi kulingana na kasi ya utendaji wa viongozi waliopo na kutekeleza majukumu wanayopangiwa kwa weledi.

📍OPERESHENI ANWANI ZA MAKAZI SASA NI ASILIMIA 67📍

  








📍OPERESHENI ANWANI ZA MAKAZI 

SASA NI ASILIMIA 67📍


Operesheni ya uwekaji wa Anwani za Makazi nchini iliyotangazwa tarehe 8 Februari mwaka huu wa 2022 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan sasa utekelezaji wake umefikia asilimia 67 kulingana na takwimu za mfumo unaopokea taarifa za utekelezaji wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Taarifa hiyo imetolewa na Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye wakati wa mkutano na Wakuu wa Mikoa yote nchini uliofanyika jijini Dodoma uliolenga kutoa taarifa ya utekelezaji wa operesheni hiyo

“Tathimini iliyofanyika ya kupata asilimia 67 imezingatia kazi zilizotekelezwa ikiwa ni kazi ya kutambua maeneo; kujenga uwezo kwa maafisa na watendaji wanaofanya kazi hii; kutoa elimu ya zoezi husika; kukusanya taarifa; kutengeneza mfumo utakaopokea taarifa na kuingiza taarifa kwenye mfumo ili ziweze kutumika na kuweka muundombinu (physical) katika maeneo mbalimbali nchini”, amezungumza Mhe. Nape


Ameongeza kuwa mwenendo wa utekelezaji unaonesha matumaini ya zoezi kukamilika kabla ya muda uliopangwa na kazi itakayofuata itakuwa ni kusafisha baadhi ya taarifa kwenye mfumo kwa hatua za kuukabidhi mfumo kwa mujibu wa maelekezo ya kuukabidhi ifikapo tarehe 22 Mei, mwaka 2022.
@samia_suluhu_hassan @ikulu_mawasiliano @ikulu_habari @kassim_m_majaliwa @napennauye @innocentbash @drjimyonazi @ortamisemi @wizara_ya_ardhi @tcra_tanzania @ucsaftz @ttcl_corporation @posta_tz

ZOEZI LA ANWANI ZA MAKAZI KUKAMILIKA IFIKAPO MEI 2022


 Zoezi la Anwani za Makazi linatakiwa kukamilika ifikapo mwezi Mei 2022 , ewe mwananchi hakikisha unashiriki kikamilifu katika zoezi hili. 

Anwani za Makazi kwa maendeleo ya kijamii na kiuchumi.




HATUTAWASHUSHA VYEO TU BALI MTAONDOLEWA KWENYE UTUMISHI WA UMMA’ BASHUNGWA


  

HATUTAWASHUSHA VYEO TU BALI

 MTAONDOLEWA KWENYE 

UTUMISHI WA UMMA’ BASHUNGWA


OR-TAMISEMI

Waziri Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe. Innocent Bashungwa
amesema hatawafumbia macho watumishi ambao hawatoshi na kuwa wataondolewa kwenye utumishi wa umma na si kuwashusha vyeo au kuwahamisha

Pia Mhe. Bashungwa amewataka watumishi katika Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kufanya kazi kwa bidii, kujituma na uadilifu mkubwa na kwa wachache wanaoenda kinyume na taratibu hizo watachukuliwa hatua kwa kutolewa kwenye utumishi wa umma.

Amesema kumekuwepo na utaratibu wa kuwashusha vyeo watumishi wachache ambao wanafanya kazi kwa mazoea na kutozingatia taratibu za kiutumishi lakini chini ya usimamizi wangu hilo jambo halivumiliki watatolewa kwenye utumishi wa umma maana wanadhohofisha mchakato mzima wa kuleta maendeleo kwa Watanzania.

Mhe. Bashungwa ametoa wito huo 29, Machi 2022 alipozungumza na waandishi wa habari Jijini Dodoma muda mfupi baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan kuiagiza Ofisi ya Rais TAMISEMI kuzisimamia Halmashauri ipasavyo na kuchukua hatua kwa watumishi wenye matumizi mabaya ya fedha za Serikali.

“Nimuhakikishie Mheshimiwa Rais kwa maagizo aliyoyatoa leo kuhusu weledi na uadilifu wa Watumishi wa umma, nitaanzia hapa Ofisi ya Rais TAMISEMI kuhakikisha tunajenga taswira na mwelekeo unaoendana na ofisi ya Mheshimiwa Rais” amaesema Bashungwa


Amesema matarajio yake ni kuona wale wachache waliokuwa wanaenda kinyume wanabadilika na kujirekebisha maana kuna Watanzania wasomi na wazalendo wapo mtaani ambao wakipewa nafasi wataweza kutumikia Watanzania kwa uaminifu.

Aidha, Waziri Bashungwa amemwagiza Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI ndani ya siku tatu kuhakikisha anamaliza uchambuzi wa Wakahazina wa Halmashauri ambao hawafanyi kazi kikamilifu ili waweze kuchukuliwa hatua.

Pia, Waziri Bashungwa amewataka Wakuu wa Mikoa na Wilaya kuhakikisha wanasimamia nidhamu ya Utumishi katika maeneo yao hasa katika usimamizi wa fedha za utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuchukua hatua mapema kabla ya Wizara haijalazimika kufanya hivyo.

PROF. MBARAWA ATOA MIEZI MITATU UKARABATI MV. KAZI

 






 PROF. MBARAWA ATOA MIEZI MITATU

 UKARABATI MV. KAZI


WAZIRI wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa
amemtaka mkandarasi Songoro Marine anayefanya ukarabati mkubwa wa Kivuko cha MV. Kazi kuhakikisha kivuko hicho kinakamilika ndani ya kipindi cha miezi mitatu kuanzia sasa.
 
Akizungumza alipokagua ukarabati wa kivuko hicho leo jijini Dar es Salaam, Prof. Mbarawa amesema Serikali imeshapata fedha kwa ajili ya ukarabati huo, hivyo ni wajibu wa Wakala wa Ufundi na Umeme nchini (TEMESA) na Mkandarasi Songoro Marine kuhakikisha taratibu za manunuzi na mikataba ya kazi hiyo inakamilika kwa haraka.
 

"Hakikisheni ifikapo Ijumaa ya Aprili Mosi taratibu za mikataba ziwe zimekamilika na kasi ya ujenzi na uagizaji vifaa nje ya nchi kwa ajili ya kazi hiyo iongezeke ili kufikia lengo," amesisitiza Prof. Mbarawa.

 
Prof. Mbarawa amesema idadi ya wakazi wa Kigamboni wanaohitaji huduma ya kivuko imekuwa ikiongezeka siku hadi siku hivyo kuwataka TEMESA kutengeneza ratiba maalum ya ukarabati wa vivuko vyake ili kuondoa usumbufu pindi vinapokwenda matengenezo.
 
"Serikali imetenga fedha katika bajeti ijayo ya ujenzi wa kivuko kipya kikubwa kitakachokuwa na uwezo wa kubeba abiria elfu tatu kwa wakati mmoja hivyo TEMESA jipangeni kuendana na kasi ya Serikali," amesisitiza Prof. Mbarawa.


Naye Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni, Bi. Fatma Almas Nyangasa amemshukuru Prof. Mbarawa kwa mikakati inayofanywa na Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi kuboresha huduma za usafiri kwa wakazi wa Kigamboni, na kumuomba aangalie upya viwango vya gharama zinazotozwa kwa mabasi ya abiria yanayotumia Daraja la Nyerere.
 
"Kupungua kwa gharama za mabasi ya abiria katika Daraja la Nyerere kutapunguza msongamano wa magari katika kivuko cha Magogoni na hivyo kupunguza msongamano kwa kuwa magari mengi yatapita darajani," amesema Bi. Nyangasa.

 
Naye Meneja wa Ujenzi wa Vivuko TEMESA, Eng. Lukombe Kingo'mbe amemhakikishia Prof. Mbarawa kuwa TEMESA imejipanga kusimamia vizuri ukarabati wa Kivuko cha MV. Kazi na Kivuko kipya kitakachoanza kujengwa baadaye mwaka huu.
 
Zaidi ya abiria laki moja hadi laki moja na elfu hamsini kwa sasa wanakadiriwa kutumia huduma za vivuko kati ya Kigamboni na Feri kwa siku.


@temesatanzania

WIZARA YA ARDHI YASHIRIKIANA NA KOREA KUBADILISHA MIFUMO YAKE KUWA YA KIDIGITALI

 

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula (Kushoto) akipokea zawadi kutoka kwa Mtendaji Mkuu na Rais wa Kampuni ya Hojung Solutions Co Ltd ya Korea Kusini baada yeye na ujumbe wake kumtembelea ofisini kwake eneo la Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma tarehe 30 Machi 2022.

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akizungumza na ujumbe kutoka Korea Kusini ulioongozwa na Mtendaji Mkuu na Rais wa Kampuni ya Hojung Solutions Co Ltd Munseok Lee baada ya kumtembelea ofisini kwake eneo la Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma tarehe 30 Machi 2022.

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akiwa katika picha ya pamoja na ujumbe kutoka Korea Kusini ulioongozwa na Mtendaji Mkuu na Rais wa Kampuni ya Hojung Solutions Co Ltd Munseok Lee mara baada ya kumtembelea ofisini kwake eneo la Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma tarehe 30 Machi 2022.

Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Allan Kijazi akimvisha vazi la kimasai Mtendaji Mkuu na Rais wa Kampuni ya Hojung Solutions Co Ltd ya Korea Kusini baada ya kumtembelea ofisin ya Wizara ya Ardhi eneo la Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma tarehe 30 Machi 2022.

 

WIZARA YA ARDHI YASHIRIKIANA NA KOREA KUBADILISHA 

 

MIFUMO YAKE KUWA YA KIDIGITALI

 

Na Munir Shemweta, WANMM DODOMA

Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa ushirikiano wake na Korea Kusini imeanzisha mkakati wa kuhakikisha inabadilisha mifumo yake upangaji, utumiaji, upimaji na uwekaji kumbukumbu za sekta ya ardhi kutoka analogia kwenda digitali ili kuboresha sekta ya ardhi.

Hatua hiyo inafuatia mifumo mingi ya upangaji, utumiaji upimaji na uwekaji kumbukumbu za ardhi katika Wizara ya Ardhi kuendelea kutumia mifumo ya analogia katika upangaji, utumiaji, upimaji na uwekaji kumbukumbu za sekta ya ardhi.

Katika kufanikisha azma hiyo Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi pamoja na Serikali ya Korea Kusini zimeingia makubaliano ya ushirikiano wa utekelezaji mradi wa ujenzi wa kituo cha Kisasa cha Mafunzo pamoja na uboreshaji miundombinu ya sekta ya ardhi.

Hayo yamebainishwa tarehe 30 Machi 2022 jijini Dodoma na Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Allan Kijazi wakati akielezea ushirikiano baina ya serikali ya korea kusini na Wizara ya ardhi katika uanzishaji kituo cha kisasa cha kutolea mafunzo kwa wataalamu wa upimaji pamoja na uboreshaji miundombinu ya sekta ya ardhi.

Uanzishwaji Kituo cha kisasa utagharimu fedha za kitanzania Shilingi Bilioni 5.2 na ule wa ujenzi wa miundombinu utagharimu dola milioni 64.

Akielezea ujenzi wa kituo cha kisasa, Dkt Kijazi alisema uanzishwaji wa kituo hicho siyo tu kwa ajili ya kutumia teknolojia ya kisasa pekee bali ile itakayoendana na wakati ambapo kupitia mradi huo Wizara ya Ardhi itapokea msaada wa kiufundi sambamba na wataalamu wake kupatiwa mafunzo na kuwekewa vifaa vinavyohusu mifumo ya ardhi.

‘’Pamoja na kuwekwa vifaa kwenye kituo lakini pia watumishi watajengewa uwezo pamoja na kukusanya, kuchakata na kutumia takwimu za ardhi katika mipango ya kuendeleza sekta ya ardhi’’ alisema Dkt Kijazi.

Akigeukia sehemu ya pili ya mradi huo, Dkt Kijazi alisema, itakuwa ni ujenzi wa miundombinu itakayowezesha wizara ya Ardhi kutumia teknnolojia ya kisasa katika masuala mazima ya kupanga, kupima na kutumia takwimu za ardhi kwenye maeneo mbalimbali ya nchi..

Mradi mzima utahusisha uandaaji ramani za uwiano mdogo na zile za uwiano mkubwa kwa ile miji mikuu ya mikoa 26 ya Tanzania Bara sambamba na kuweka vituo vya kielektroniki vya upimaji ardhi na kuboresha miundombinu ya kusambaza taarifa za kijografia kwa idara za serikali na watumiaji wote nchini.

Katika hatua nyingine, ujumbe wa wataalamu kutoka Korea kusini uliokuja kwa ajili ya hatua za awali za utekelezaji miradi hiyo ukiongozwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa Hojung Solution Co Ltd Munseok Lee umekutana na Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula kwa ajili ya kujitambulisha na kumuelezea maendeleo ya utekelezaji miradi hiyo.

Ujumbe huo ulimueleza Dkt Mabula uko tayari kuanza kazi ya utekelezaji mradi huo baada ya maandalizi ya awali ya kutoa mafunzo kwa baadhi ya watumishi nchini.

Kwa upande wake Dkt Mabula aliuambia ujumbe huo kuwa ana imani ujumbe huo ulishiriki vyema hatua zake za awali za maandalizi ya utekelezaji mradi huo na kueleza kuwa matarajio yake kila kitu kitaenda vizuri katika utekelezaji mradi huo.

 

WAZIRI UMMY ATAKA WATUMISHI WA AFYA KUBADILI FIKRA KATIKA UTENDAJI WA KAZI

Written By CCMdijitali on Wednesday, March 30, 2022 | March 30, 2022


WAZIRI UMMY ATAKA WATUMISHI WA 

AFYA KUBADILI FIKRA KATIKA 

UTENDAJI WA KAZI


Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu amewataka watumishi wa umma katika sekta ya afya kubadili fikra za utendaji kazi na kuwa wabunifu katika kutatua changamoto ili kuongeza chachu ya kufikia malengo na kutoa huduma bora kwa wananchi.

Waziri Ummy amesema hayo leo wakati akifungua mkutano wa baraza kuu la wafanyakazi wa Wizara ya afya,hospitali za rufaa za mikoa pamoja na taasisi zilizo chini yake uliofanyika jijini Dodoma.

“Nitoe rai kwa watumishi wote kubadili fikra zetu katika utendaji na tunatakiwa kufanya kazi kwa bidii tukilenga kufikia malengo na mafanikio tuliyojiwekea. Kila mmoja katika nafasi yake awe mbunifu katika kutatua changamoto zinazomkabili na hatimaye kutoa huduma bora”. Amesema Waziri Ummy.


Waziri Ummy amesema katika kipindi cha mwaka mmoja wa Rais Samia Suluhu Hassan akiwa madarakani ametoa Shilingi bilioni 891.5 kwa ajili ya kuboresha miundombinu pamoja na huduma za afya hivyo amewataka watumishi watumie fursa zinazopatikana zikawe chachu za kupata mafanikio makubwa Zaidi.

Akielezea mafanikio yaliyopatikana katika kipindi cha mwaka mmoja, Waziri Ummy ametaja kuwa ni pamoja na kuongezeka kwa wajawazito wanaohudhuria kniniki kwa mahudhurio manne na Zaidi, kuimarisha na kuboresha na kuboresha huduma za matibabu ya kibingwa na ubingwa bobezi, kuimarisha huduma katika Hospitali za rufaa za mikoa.

Kwa upande wa mahusiano na wawekezaji na sekta binafsi, Waziri Ummy amesema sekta binafsi zimesaidia kujenga viwanda vya kuzalisha dawa kupitia makubaliano ya pamoja na wawakilishi wa nchi, mashirika ya kimataifa pamoja na taasisi mbalimbali.

Aidha, mafanikio mengine yaliyopatikana ni pamoja na kuimarisha huduma za uchunguzi wa magonjwa ya milipuko ikiwemo UVIKO-19 kwa kuongeza vipimo vya haraka (Rapid Test) na nija ya vinasaba (RT-PCR). kuimarisha ubora wa takwimu za mifumo kielektroniki ya ugavi wa vifaa, vifaa tiba na vitendanishi kwa ngazi zote. Kuboreshwa kwa huduma za maabara na kupata ithibati ya kimataifa.

Kwa upande mwingine Waziri Ummy ameeleza changamoto ambazo bado zinaikabili sekta ya afya ikiwemo utoaji wa huduma bora kwa wananchi hasa wa kipato cha chini.

MAONYESHO YA WAJASIRIAMALI NJOMBE KUELEKEA UZINDUZI WA MWENGE KITAIFA

 






 

 MAONYESHO YA WAJASIRIAMALI 

NJOMBE KUELEKEA UZINDUZI WA 

MWENGE KITAIFA


Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mhe. Waziri Kindamba . amezindua maonyesho ya kibiashara (Wajasiriamali) yaliyofanyika katika viwanja vya Sabasaba. kama amsha amsha kuelekea Uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa utakaofanyika katika Mkoa wa Njombe Tarehe 02 Aprili, 2022.

Mhe,Waziri ameipongeza Benki ya CRDB kwakudhamini Uzinduzi huu wa Mwenge wa Uhuru pamoja na kufanya maboresho ya uwanja ambao utatumika katika uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa .

Aidha Mhe.Waziri Kindamba amewasisitiza Wananchi kushiriki kikamilifu kwenye Sensa ya watu na Makazi ambayo itafanyika Mwezi wa Nane mwaka huu ili kuunga mkono Kaulimbiu ya Mbio za Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2022 isemayo-

"SENSA NI MSINGI WA MIPANGO YA MAENDELEO: SHIRIKI KUHESABIWA TUYAFIKIE MAENDELEO YA TAIFA".


Pamoja na mambo mengine Mhe.Kindamba amewaasa Wananchi kuendelea kujitokeza kupata chanjo ya UVIKO -19.


".. Chanjo ya UVIKO-19 ni muhimu kwajili ya Kujikinga na maambukizi ya Ugonjwa wa UVIKO ambalo ni gonjwa hatari sana linalo shambulia mataifa mengi, nawaomba Wananjombe mzidi kujitokeza kuchoma chanjo ya Uviko 19 na hapa kwenye maonyesho kuna Mabanda maalumu ya kutolea chanjo." Mhe.Kindamba.


Mwisho Mhe.Kindamba amewakaribisha Wananchi wote kushiriki katika Uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2022.

"..Napenda kuwaalika wananchi wote kwenye *Uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa utakaofanyika Katika viwanja vya Sabasaba Njombe..".
Mhe.Kindamba.


#Njombetupotayari
# VisitNjombe
#vijanawamamasamia🇹🇿

SEMINA (MAFUNZO) YA ANUANI MAKAZI -NJOMBE

Written By CCMdijitali on Tuesday, March 29, 2022 | March 29, 2022

  









SEMINA (MAFUNZO) YA ANUANI MAKAZI


Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mhe Waziri Waziri Kindamba. Akiongozana pamoja na Katibu wa CCM Mkoa wa Njombe na Mkuu wa Wilaya ya Njombe, wameshiriki katika Ufunguzi wa semina ya Anuani ya Makazi kwa vijana 200 waliochaguliwa na Halmashauri ya Mji wa Njombe.

Mkuu wa Mkoa, amesisitiza vijana wafanye haraka kwenye zoezi la uandikishaji wa Anuani za Makazi na Ufanisi ili kuhakikisha tunakuwa namba moja kitaifa na kutoka katika nafasi zile za mwisho

Vijana kujitokeze kwenye chanjo za Uviko 19, kwawingi maana kinga ni bora kuliko tiba ambayo ghalama zake ninkubwa sana, kulingana na Chanjo za Bure zilizotoletwa na Serikali ya Awamu ya Sita, asema Mhe, Waziri Waziri.

Awasisitiza vijana hao wote kutokea kwenye Uzinduzi wa Mwenge wa Uhuru Mkoani Njombe utakao fanyika siku ya Jumamosi Tarehe 02/04/2022 katika viwanja vya Sabasaba Njombe, asema Mhe, Waziri Waziri.

#vijanawamamasamia🇹🇿
#VisitNjombe
#kaziendelee

 
Support : #BegaKwaBegaNaMamaSamia | JAK | CCM Arusha
Copyright © 2011. CCM Dijitali - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Jasper K
Proudly powered by Blogger
Link