Home » » MKUU WA WILAYA YA KASKAZINI B AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZIA

MKUU WA WILAYA YA KASKAZINI B AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZIA

Written By CCMdijitali on Tuesday, February 8, 2022 | February 08, 2022

 

Mkuu wa Wilaya ya Kaskazini B Hamid Seif Said

Wilaya ya Kaskazini B


Mkuu wa wilaya ya kaskazini B Hamid Seif Said ameiagiza idara ya misitu Zanzibar kumchukulia hatua za kisheria msimamizi wa shamba liliopo miulani shehiya ya matetema bwana Saleh Salum Haji kwa kosa la kukata miti zaidi ya 60 bila ya
 kibali chochote kutoka serikalini

Amesema idadi  ya miti iliyokatwa ni kubwa hivyo ni vyema Kwa idara hiyo kumchukulia hatua za kisheria mtu huyo  Ili iwe fundisho kwake na Kwa wananchi wengine

Akizungumza mara baada ya kulikagua shamba Hilo na kukuta vigogo vya miti ambayo tayari vimeandaliwa Kwa ajili ya kuchomwa mkaa akiwa na kamati ya ulinzi na usalama ,watendaji wa wilaya ,watendaji wa idara ya misitu pamoja na uongozi wa shehiya
 
Amesema kumiliki shamba au kulisimamia Bado haijawa kigezo Cha mtu kukata miti bila ya kuwa na kibali Cha misitu hivyo ameahidi kufanya Ziara za mara Kwa mara katika mashamba yote ya wilaya ya kaskazini B Ili kubaini waharibifu wa mazingira na kuwachikulia hatua za kisheria

Amesema licha ya kuikosesha serikali mapato yake lakini pia kitendo hicho kinarudisha nyuma juhudi za serikali za kutunza mazingira kutokana na kutumia gharama kubwa katika kuzalisha miti na kuigawa Kwa wananchi wake bila ya malipo

Hata hivyo bwana Hamid amewataka wananchi kuacha kujichukulia maamuzi mikononi mwao na badala yake wazingatie sheria zilizowekwa na serikali Ili kuepuka usumbufu 

Kaimu mkurugenzi kutoka idara ya misitu said juma Ali Amesema utaratibu wa serikali unaelekeza kuwa mmiliki wa shamba anapotaka kusafisha shamba lake Kwa kukata miti anatakiwa  kufika idara ya misitu Ili aweze kutembelewa  na kubainishiwa miti inayotakiwa kukatwa Kwa mujibu wa  sheria

Hata hivyo amepongeza uongozi wa wilaya Kwa mashirikiano unayoyatoa Kwa idara hiyo na kusema kuwa ushirikiano huo utasaidia Kwa kiasi kikubwa kidhibiti vitendo Kama visiendelee kutokea na kuathiri mazingiza.

Akitoa ufafaunuzi wa sheria kuhusu ukataji wa miti katika shamba Hilo mwana sheria kutoka idara ya misitu Asha Muhammed Ahmed Amesema kitendo hicho ni kinyume na sheria  namba 10 ya mwaka 1996 ambayo inakataza mwananchi yoyote kukata mti bila ya kibali kutoka serikalini

Ziara hiyo ya kushtukiza imekuja baada ya hivi karibuni mkuu wa wilaya ya kaskazini B kufika katika eneo Hilo Kwa ajili ya kusikiliza mgogoro wa shamba ndipo alipokuta uharibifu huo na kuwasiliana na watendaji wa idara ya misitu Kwa ajili ya kupata muongozo wa serikali kuhusu ukataji wa miti Kwa mujibu wa sheria ya misitu.
Share this article :
 
Support : #BegaKwaBegaNaMamaSamia | JAK | CCM Arusha
Copyright © 2011. CCM Dijitali - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Jasper K
Proudly powered by Blogger
Link