Home » » WAZIRI BASHUNGWA AANZA ZIARA YA KIKAZI MKOA DODOMA

WAZIRI BASHUNGWA AANZA ZIARA YA KIKAZI MKOA DODOMA

Written By CCMdijitali on Thursday, January 18, 2024 | January 18, 2024

Published from Blogger Prime Android App
Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa (Mb) amewasili Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Dodoma na kupokelewa na Mkuu wa Mkoa, Rosemary Senyamule, kwa ajili ya kuanza ziara ya kikazi ya siku mbili mkoani humo, leo tarehe 19 Januari 2024

Katika ziara hiyo, Waziri Bashungwa atakagua miundombinu ya barabara katika wilaya za Mkoa wa Dodoma na miradi mingine inayotekelezwa katika Sekta ya Ujenzi mkoani humo.

Miradi atakayokagua na kutembelea ni pamoja ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Msalato na Majengo, ujenzi wa Barabara ya Mzunguko (Outer Ring Road), ujenzi wa Barabara ya Ntyuka-Mvumi- Kikombo, barabara ya Hogoro – Machenje - Kongwa, ujenzi wa barabara ya Kongwa - Mpwapwa sehemu ya Mpwapwa - Mwanakianga na Mpwapwa - Ving’awe pamoja na Ukaguzi wa eneo la Mtanana, Kongwa.

Published from Blogger Prime Android App

Published from Blogger Prime Android App
Published from Blogger Prime Android App

Published from Blogger Prime Android App


Share this article :
 
Support : #BegaKwaBegaNaMamaSamia | JAK | CCM Arusha
Copyright © 2011. CCM Dijitali - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Jasper K
Proudly powered by Blogger
Link