Home » » Naibu Waziri Ofisi ya Makamo Muungano na asema elimu kubwa inahitajika kwa Wananchi kuacha matumizi ya Mkaa na Kuni

Naibu Waziri Ofisi ya Makamo Muungano na asema elimu kubwa inahitajika kwa Wananchi kuacha matumizi ya Mkaa na Kuni

Written By CCMdijitali on Wednesday, July 24, 2024 | July 24, 2024

Published from Blogger Prime Android App
Naibu Waziri Ofisi ya Makamo Muungano na Mazingira Khamis Hamza Chilo (wa tatu kushoto)Mwakilishi wa Jimbo la Uzini Haji Shaaban Waziri (wa kwanza kulia ) Mdau wa maendeleo ya Jimbo la Uzini Lucia Mwaipopo (wa pili kulia) na Katibu wa App skills Foundation Tinnah Didas Masaburi wakisikiliza maelezo mafupi yanahusu Mazingira, utumiaji wa nishati sahihi ya kupikia na ufahamu wa dhana ya uchumi wa buluu kwa Sister Agnes Paulo (wa pili kushoto)wa parokia ya Kanisa la Katoliki na Chuo cha Utalii cha Machui.

Na Bahati Habibu 

Naibu Waziri Ofisi ya Makamo wa Rais Muungano na Mazingira na Mbunge wa Jimbo la Uzini Khamis Hamza Chilo amesema elimu kubwa inahitajika kwa Wananchi kuacha matumizi ya Mkaa na Kuni kwa matumizi ya kupikia hali itakayopelelekea utunzaji wa Mazingira. 

Kauli hiyo ameitoa huko Machui wakati akizungumza na wananchi wa shehia ya machui mara baada ya kukamilika utafiti uliofanywa taasisi isiyo ya serekali ya up skills  foundation kutoka Tanzania  Bara unaohusisha matumizi ya nishati ya kupikia na ufahamu wa wananchi juu ya dhana ya uchumi wa buluuu.

Amesema  wananchi wengi hawana uelewa wa matumizi sahihi ya nishati ya kupikia  na dhana ya uchumi wa buluu   kwa  kuacha matumizi ya kuni na mkaa ambayo hupelekea uchafuzi  wa Mazingira na kusababisha maradhi kwa wananchi. 
 
Aidha ameeleza matumizi ya nishati ya gesi kwa kupikia majumbani itasadia kwa kiwango kikubwa utunzaji wa Mazingira  kwa nchi kavu na bahari. 


Nae Mwakilishi wa Jimbo la hilo Haji Shaaban Waziri amesema  kufanyika kwa utafiti  huo katika kijiji cha Machui itasaidia kwa Serekali kufahamu matumizi ya nishati ya kupikia  kwa wananchi wanaoishi vijijini  pamoja na dhana ya uchumi wa buluu. 

Aidha ameeleza Serekali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serekali ya Mapinduzi ya Zanzibar  imedhamiria kuondosha matumizi ya kuni na mkaa na badala yake wananchi watumie nishati ya gesi kwa matumizi ya kupikia .

Amesema matumizi ya nishati ya gesi ya kupikia ni salama  na huepusha maradhi yanayosababishwa na matumizi ya kuni na mkaa ikiwemo kifua kikuu na homa ya mapafu.

Nae katibu wa app skills foundation  Tinnah Didas Masaburi amesema utafiti huo wanaoufanya unalenga kujua ufahamu  wa jamii kuhusu dhana  ya uchumi wa buluu  na  matumizi ya nishati  ya kupikia. 

Pia utafiti huo utaonesha ni kwa namna gani jamii inatambua njia ya utunzaji wa Mazingira  na kutoa Elimu  ya matumizi sahihi  ya nishati isiyo na madhara kwa binaadamu.

Nao wananchi wa Shehia ya Machui  wameushukuru uongozi wa Jimbo la Uzini kwa kuiteua Shehia yao kuwa sehemu  ya utafiti  huo ambao umewasaidia kufahamu njia sahihi ya utunzaji wa Mazingira  na dhana nzima ya Uchumi wa buluu. 

Utafiti  huo umefanyika katika Shehia ua Machui  kwa Mkoa wa Kusini Unguja, Shehia ya Matemwe Kigomani, Shehia ya Mkokotoni kwa Mkoa wa Kaskazini Unguja na Shehia ya  Mndo kwa Mkoa wa Mjini Magharibi. 



Ujumbe wa App Skills foundation ukiongozwa na Mwakilishi wa Jimbo la Uzini Haji Shaaban Waziri akisalimiana na Mwakilishi wa Jimbo la Matemwe  na Mwenyekiti wa Kiwanda  Mungu ndie hakimu cha kuchakata takataka na kuwa mbolea  Sulubu Kidogo Amour huko Matemwe  ujumbe huo ulifika hapo kwa lengo la kufanya utafiti wa utunzaji wa Mazingira, matumizi sahihi ya nishati ya kupikia na ufahamu wa wananchi juu ya dhana ya uchumi wa buluu. 




Share this article :
 
Support : #BegaKwaBegaNaMamaSamia | JAK | CCM Arusha
Copyright © 2011. CCM Dijitali - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Jasper K
Proudly powered by Blogger
Link