Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo, amefanya mazungumzo na Makamu wa Rais wa Kampuni ya Viettel, ambayo ni kampuni tanzu ya Kampuni ya Mawasiliano ya Haotel Tanzania Kanali Dao Xuan Vu, katika makao makuu ya kampuni hiyo jijini Hanoi, Vietnam.
Mazungumzo hayo yalilenga kujadili kuhuhusu fursa mpya za uwekezaji zilizopo nchini na kuimarisha ushirikiano katika sekta za biashara na uwekezaji.
Waziri Kombo yuko nchini Vietnam kwa ziara ya kikazi, akiwa ameambatana na Balozi wa Tanzania nchini humo mwenye Makazi yake Jamhuri ya Watu wa China Mhe. Khamis Omar, Mkurugenzi wa Idara ya Diplomasia ya Uchumi na Biashara ya Kimataifa Balozi John Ulanga, Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia Bi. Felista Rugambwa wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania Bw. Gilead Teri na Viongozi wa Sekta Binafsi na Wafanyabiashara.
Mkurugenzi wa Idara ya Diplomasia ya Uchumi na Biashara ya Kimataifa Balozi John Ulanga akichangia jambo wakati wa mazungumzo na Kampuni Viettel ya Vietnam Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania Bw. Gilead Teri akifafanua jambo wakati wa mazungumzo na Kampuni Viettel ya Vietnam Mkurugenzi Mtendaji wa Nakiete Pharmacy na Rais wa Chemba ya Biashara, Viwanda na Kilimo Tanzania (TCCIA) Bw. Vicent Bruno Minja akichangia jambo wakati wa mazungumzo na Kampuni Viettel ya Vietnam PICHA YA PAMOJA Balozi wa Tanzania nchini Vietnam mwenye Makazi yake Jamhuri ya Watu wa China Mhe. Khamis Omar,akichangia jambo wakati wa mazungumzo na Kampuni Viettel ya Vietnam Balozi wa Tanzania nchini Vietnam mwenye Makazi yake Jamhuri ya Watu wa China Mhe. Khamis Omar,akichangia jambo wakati wa mazungumzo na Kampuni Viettel ya Vietnam