Home » , » Wanaobeza huduma ya umeme vijijini watakiwa kupuuzwa

Wanaobeza huduma ya umeme vijijini watakiwa kupuuzwa

Written By CCMdijitali on Tuesday, December 30, 2014 | December 30, 2014

Waziri wa Nishati na Madini Profesa SOSPETER MUHONGO

Waziri wa Nishati na Madini Profesa SOSPETER MUHONGO amewataka wananchi Wilayani SERENGETI mkoani MARA, kuwapuuza watu wanaohujumu mradi wa Umeme vijijini unaotekelezwa katika maeneo mbalimbali ndani na nje ya mkoa huo.

Akizungumza na baadhi ya wananchi wa kijiji cha GANTAMOME wilayani humo, Profesa MUHONGO amesema baadhi ya watu wamekuwa wakiwahadaa wananchi kuwa utekelezaji wa mradi huo hautafanikiwa kama ilivyokusudiwa na Serikali jambo ambalo linalenga kuwanyima fursa wananchi wa vijijini upatikanaji wa nishati ya umeme .

Nalo shirika la Umeme nchini TANESCO limewatahadharisha wananchi kutowapa fedha watu wasio waaaminifu ili kugharamia mradi huo wa nishati ya umeme vijijini.
Share this article :
 
Support : #BegaKwaBegaNaMamaSamia | JAK | CCM Arusha
Copyright © 2011. CCM Dijitali - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Jasper K
Proudly powered by Blogger
Link