Home » » Majaji wajinoa mahakama ya ufisadi

Majaji wajinoa mahakama ya ufisadi

Written By CCMdijitali on Monday, July 4, 2016 | July 04, 2016


Kwa ufupi                       

Kesi hizo zitakuwa zinaendeshwa katika Mahakama Kuu, Kitengo cha Uhujumu Uchumi na tayari majaji 14 wa wataanza kozi maalumu ya siku tano katika Chuo cha Sheria kilichopo Lushoto, Tanga. 

By Kalunde Jamal, Mwananchi kjamal@mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Jaji Mkuu, Mohamed Chande amesema jopo la majaji linatarajiwa kuingia darasani ili kujifunza sheria mpya ya kuendesha kesi za ufisadi.

Kesi hizo zitakuwa zinaendeshwa katika Mahakama Kuu, Kitengo cha Uhujumu Uchumi na tayari majaji 14 wa wataanza kozi maalumu ya siku tano katika Chuo cha Sheria kilichopo Lushoto, Tanga.

Amesema hatua hiyo inakuja baada ya wiki iliyopita, Bunge kupitisha sheria ya uhujumu uchumi ya mwaka 2002 ikiwa na maboresho mbalimbali.

“Maeneo yapo tayari na tumeshapeleka wasajili na watendaji wameanza kufanya kazi, baada ya michakato mingine kukamilika kila kitu kitakuwa sawa na majaji wataanza kazi,” amesema Jaji Chande.

Share this article :
 
Support : #BegaKwaBegaNaMamaSamia | JAK | CCM Arusha
Copyright © 2011. CCM Dijitali - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Jasper K
Proudly powered by Blogger
Link