Home » » UBINAFSI WA MADIWANI WA CHADEMA WAENDELEA KUITIA HASARA HALMASHAURI YA JIJI LA ARUSHA

UBINAFSI WA MADIWANI WA CHADEMA WAENDELEA KUITIA HASARA HALMASHAURI YA JIJI LA ARUSHA

Written By CCMdijitali on Monday, August 29, 2016 | August 29, 2016

 Mstahiki Meya wa Jiji la Arusha Bukhay Kalisti

Na Mwandishi Wetu - Arusha 
 
Madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Arusha wamevunja kikao cha Baraza la Madiwani kilichokua kinafanyika leo asubuhi 29/08/2016 kwenye Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa maslahi ya chama chao (CHADEMA) na kutupilia mbali shida na kero za wananchi waliowachagua.

Walinukuliwa mara baada ya kuvunja kikao hicho,wakitoa  sababu ambazo,zilionekana kutokuwa na mashiko kwa maslahi ya Wananchi au wapiga kura wao.

Baadhi ya sababu walizozitoa ni :-
  • Kuna madiwani 8 wanaotafutwa na Jeshi la Polisi,hivyo kuhofia kukamatwa ,endapo wangefika kwenye kikao hicho.
  • Walihitaji kwenda kuwawekea dhamana baadhi ya Viongozi wa Chama chao
  • Kuhudhuria kesi inayomkabili Godbless Lema inayotarajiwa kusikilizwa leo machana
         Mahakamani

Hivi ninajiuliza ,sababu hizi zina umuhimu wowote wa mustakabali wa Wananchi wa Jiji la Arusha ? Jibu hapana ! Na sababu ziko wazi tu.

              i.        Je katika Jiji la Arusha,hakuna watu wenye sifa za kuweza kuwadhamini Viongozi hao ?

            ii.        Je Jeshi la Polisi limeshindwa kuwafikia mahali walipo, ikiwa Godbless Lema  (Mbunge ) amekamatwa, sembuse wao ?

           iii.        Hivi kweli kwa akili za kawaida, iwapo kikao kilikuwa ni asubuhi na Godbless Lema anapelekwa Mahakamani Mchana, je walishindwa kuendelea na kikao hicho kwa masaa waliyokuwa nayo?

           iv.        Hivi kweli dhamana iliyohitajiwa ni ya Madiwani wote 33 wanaotokana na Chama cha Demokrasia (Chadema) ?
Ili kikao kiendelee ,kilihitaji kiwe na angalau Madiwani wasiopungua 17,lakini pia walishindwa kuona umuhimu wa Baraza hilo,kwani mambo ya msingi na maendeleo yangeweza kujadiliwa na wengine wangeweza kwenda kushughulika na masuala ya kesi na dhamana za viongozi wao.

            v.        Hivi tujiulize Kikao cha robo ya tatu ambacho kinategemewa kutoa maazimio muhimu na kupitisha miradi mbalimbali ya maendeleo kwa ajili ya Utekelezaji ili kuleta  maendeleo kwa wananchi kinavunjika kwa sababu ya  kuhudhuria kesi ya mtu mmoja na  madai eti wanatafutwa na Polisi ? 

           vi.        Zaidi ya yote Halmashauri imetumia gharama kubwa na muda mwingi kwa watumishi wake kuandaa kikao hicho,pamoja na gharama za kupeleka Makabrasha kwa madiwani wote ambapo Magari yake yametumika kusambaza Makabrasha kwenye Kata zote na kutoa matangazo kwa ajili ya Kikao hicho, lakini yote hayo hawakuyathamini  na kuamua  kuvunja kikao hicho  kwa sababu zao binafsi.

MTAZAMO WA KIZALENDO

Ifike mahali busara na Uzalendo upewe kipaumbele katika masuala ya msingi na ya lazima yanayohusu Maendeleo na mustakabali wa  Jiji letu la Arusha.

Ni wazi Madiwani wa Arusha hawakuchaguliwa na kikundi cha watu wachache wanaonekana kuwa bora au muhimu zaidi ya Wananchi waliowachagua.

Haingii akilini kesi ya mtu mmoja ambaye ni ya kujitafutia mwenyewe iingizie hasara serikali na kusababisa shughuli na mipango ya maendeleo ya Jiji la Arusha kusimama.

Itakuwa haina maana Halmashauri ya Jiji la Arusha kufanya kazi kwa maslahi ya Chama cha siasa(CHADEMA) badala ya maslahi ya wananchi na wakazi wa Jiji la Arusha.

Ninukuu kauli ya Mh. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk John Pombe Magufuli,ambayo amekuwa akihimiza na kuirudiarudia kila alipopata fursa ya kuongea na Wananchi kuwa “MAENDELEO HAYANA CHAMA” 

Kila mwanachama wa Chama chochote cha Siasa na wale wasiokuwa na Chama,wanahitaji Maendeleo. Kwa sababu hiyo,kila mmoja napaswa kufanya kazi kwa kuweka maslahi ya Wananchi wote mbele.

Kwa hicho walichokifanya Madiwani wa Chadema chini Mstahiki Meya Lazaro , hakikubaliki na kinasthili kuchukuliwa hatua za kisheria na kikanuni na kukemewa kwa nguvu zote na Wanachi wote wapenda wa Jiji la Arusha.

ARUSHA BILA UBINAFSI INAWEZEKANA.
 

Share this article :
 
Support : #BegaKwaBegaNaMamaSamia | JAK | CCM Arusha
Copyright © 2011. CCM Dijitali - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Jasper K
Proudly powered by Blogger
Link