Home » » Watumia jina la Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu kutapeli

Watumia jina la Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu kutapeli

Written By CCMdijitali on Saturday, September 17, 2016 | September 17, 2016

Mkurugenzi wa Mawasiliano wa  Ikulu, Gerson Msigwa
By Mwandishi Wetu, Mwananchi
mwananchipapers@mwananchi.co.tz

Kwa ufupi

Taarifa ya Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Ikulu, Gerson Msigwa iliyotolewa leo kwa vyombo vya habari, imeeleza kuwa matapeli hao huzisambaza barua hizo kwa kampuni binafsi na wakuruegnzi watendaji wakiwataka kuchangia fedha kwa ajili ya ‘Mkutano Mkuu wa Rekebisho la Bajeti za Miundombinu na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii utakaofanyika katika kumbi za Bunge Dodoma kuanzia Septemba 21 hadi 23, mwaka huu.



Dar es Salaam. Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu, imewatahadharisha Watanzania kuhusu kuwapo kwa matapeli wanaotumia nembo ya ofisi hiyo na jina la Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, kuchapisha na kusambaza barua kisha kuchangisha fedha.

Taarifa ya Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Ikulu, Gerson Msigwa iliyotolewa leo kwa vyombo vya habari, imeeleza kuwa matapeli hao huzisambaza barua hizo kwa kampuni binafsi na wakuruegnzi watendaji wakiwataka kuchangia fedha kwa ajili ya ‘Mkutano Mkuu wa Rekebisho la Bajeti za Miundombinu na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii utakaofanyika katika kumbi za Bunge Dodoma kuanzia Septemba 21 hadi 23, mwaka huu.

“Mnataarifiwa kuwa barua hizo zilizotiwa saini na zenye muhuri wa kughushi huku maelezo yake yakiwa hayaeleweki vizuri, hazijaandikwa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu, bali zimeandikwa na watu wenye nia mbaya na wanaolenga kujipatia fedha kwa njia ya utapeli,” ilimesema taarifa hiyo iliyotolewa sainiwa na Msigwa.


Share this article :
 
Support : #BegaKwaBegaNaMamaSamia | JAK | CCM Arusha
Copyright © 2011. CCM Dijitali - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Jasper K
Proudly powered by Blogger
Link