Home » » KATIBU MKKU WIZARA YA AFYA ATOA MAAGIZO MKOANI SINGIDA

KATIBU MKKU WIZARA YA AFYA ATOA MAAGIZO MKOANI SINGIDA

Written By CCMdijitali on Sunday, February 27, 2022 | February 27, 2022



 

UJENZI WA HOSPITALI YA MKOA SINGIDA ULIOKWAMA UANZE BAADA YA SIKU 7 -KATIBU MKUU AFYA . 

Na.WAF-Singida

Katibu Mkuu Wizara ya Afya Prof. Abel Makubi ameagiza mradi wa ujenzi wa jengo la Magonjwa ya mlipuko la Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida uliokwama uendelee mapema baada ya siku saba. 

Ametoa maagizo hayo leo Mkoani hapa mara baada ya kutembelea ujenzi katika Hospital hiyo na kukutana na Katibu Tawala wa Mkoa, wajumbe wa Bodi ya ushauri ya Hospitali, uongozi wa Hospitali, mshauri elekezi na mkandarasi. 

Mradi wa ujenzi wa jengo hilo ambao ulianza mwaka 2014, umeshindwa kukamilika kwa wakati kutokana na changamoto mbalimbali.

Katika hatua nyingine Prof. Makubi ametoa muda wa siku saba kufungwa kwa mradi unaoendelea wa ujenzi wa ghorofa chini ya Mkandarasi ambaye muda wake pia umeisha na kukiagiza kitengo cha ununuzi na ugavi cha Wizara yake kuhakikisha kuwa mkandarasi wa kuendelea na kazi ya ujenzi anapatikana ndani ya siku saba hadi 14 ili kuendelea na 
ujenzi wa awamu ya pili ya kujenga ghorofa ya kwanza wa jengo hilo.
Share this article :
 
Support : #BegaKwaBegaNaMamaSamia | JAK | CCM Arusha
Copyright © 2011. CCM Dijitali - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Jasper K
Proudly powered by Blogger
Link