Home » » #SERIKALI YAMWAGA NEEMA KWA WATU WENYE ULEMAVU.

#SERIKALI YAMWAGA NEEMA KWA WATU WENYE ULEMAVU.

Written By CCMdijitali on Sunday, March 20, 2022 | March 20, 2022

 







#SERIKALI YAMWAGA NEEMA KWA WATU WENYE ULEMAVU.


Serikali ya Awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ikiwa inatimiza mwaka mmoja sasa wa uongozi, imefanikiwa kuwawezesha watu wenye Ulemavu kiuchumi, kielimu na kuboresha huduma.


Akifafanua masuala ambayo yametekelezwa kwa watu wenye Ulemavu kwa kipindi cha mwaka mmoja cha uongozi wa serikali hiyo, Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu), Mhe. Patrobas Katambi, amebainisha kuwa tayari watu wenye ulemavu wamejumuishwa kwenye Mpango wa Bima ya Afya kwa Wote kwa kipaumbele pekee cha kuwawezesha kupata Bima.

Ameyasema hayo wakati wa tamasha la TUPO PAMOJA liloandaliwa na Kundi la Mama Ongea na Mwanao walio washirikisha watu wenye Ulemavu, tarehe 19 Machi, 2022 jijini Dar es salaam.

Tamasha hilo lililoambatana na kumpongeza Mhe. Rais Samia kwa kutimiza mwaka mmoja wa uongozi wake, ambapo Mhe. Katambi ameeleza kuwa Mhe. Rais tayari ameelekeza mapitio ya sheria ili vifaa saidizi vya watu wenye Ulemavu vipunguzwe bei na vipatikane kwa wengi na kwa unafuu.

Mhe. Katambi ameendelea kubainisha kuwa katika kipindi cha mwaka mmoja cha uongozi wa Mhe.Rais Samia, ametoa ajira za moja kwa moja serikalini kwa watu wenye Ulemavu takribani 350.
Aidha, ameongeza kuwa Mhe. Rais amefanikiwa kuboresha miundo mbinu ya Elimu ambapo katika bajeti ya mwaka 2021/2022, ametenga bilioni 8 na tayari ametoa bilioni 3 kwa ajili ya kukarabati vyuo 6 vya watu wenye Ulemavu.

“Katika kipindi cha Mwaka mmoja, tumesharatibu kuandaa Alama maalum za barabarani na haki za watu wenye Ulemavu katika vyombo vya usafiri na Mhe. Rais ametoa maagizo kuandaliwa kwa Mpango wa kuwatambua mapema watoto wenye Ulemavu. Pia, Ameamua kutenga fedha kwa ajili ya mafuta yanayotumiwa na watu wenye Ulemavu yawe yanazalishwa hapa nchini “ Amesisitiza, Mhe. Katambi
Share this article :
 
Support : #BegaKwaBegaNaMamaSamia | JAK | CCM Arusha
Copyright © 2011. CCM Dijitali - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Jasper K
Proudly powered by Blogger
Link