Home » » Serikali ya awamu ya nane inayakaribisha mashirika ya bima kuja Zanzibar kuwekeza - Dr Mwinyi.

Serikali ya awamu ya nane inayakaribisha mashirika ya bima kuja Zanzibar kuwekeza - Dr Mwinyi.

Written By CCMdijitali on Monday, August 29, 2022 | August 29, 2022




Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi amesema
Serikali ya awamu ya nane inayakaribisha mashirika ya bima kuja Zanzibar kuwekeza kwenye miradi inayoipanga kuitekeleza.
Ameyasema hayo leo wakati akifungua mkutano wa 44 wa Umoja wa Wanabima Ukanda wa Mashariki na Kusini mwa Afrika (OESAI),uliofanyika katika ukumbi wa hoteli ya Madinat Al Bahr iliopo Mbweni jijini Zanzibar.
Rais Dk.Mwinyi amesema wakati Serikali inafanya mageuzi makubwa ya kiuchumi kuna haja ya sekta ya bima kuwepo kwenye eneo la uwekezaji ili kuwa na kinga katika fedha za miradi hiyo.

📆 29 Agosti, 2022


📍Madinat Al Bahr



Share this article :
 
Support : #BegaKwaBegaNaMamaSamia | JAK | CCM Arusha
Copyright © 2011. CCM Dijitali - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Jasper K
Proudly powered by Blogger
Link