Home » » DR JAFO APOKEA TUZO YA MWANAFUNZI BORA ALIYELETA MANUFAA KWA CHUO NA TAIFA MIAKA 40 YA SUA

DR JAFO APOKEA TUZO YA MWANAFUNZI BORA ALIYELETA MANUFAA KWA CHUO NA TAIFA MIAKA 40 YA SUA

Written By CCMdijitali on Thursday, November 24, 2022 | November 24, 2022




DR JAFO APOKEA TUZO YA MWANAFUNZI BORA ALIYELETA MANUFAA KWA CHUO NA TAIFA MIAKA 40 YA SUA


Morogoro

Kuelekea miaka ya Arobaini tokea kuanzishwa na Chuo kikuu cha Kilimo cha Sokoine SUA kimetoa tuzo ya Kudhamini Mchango kwa Mwanafunzi Dr Selemani Said Jafo ambaye amefanya vizuri katika masomo na kuleta tija kwa Jamii hiyo Leo kwa miongoni mwa walisoma SUA,

Akizungumza wakati wa kupokea Tuzo hiyo Dr Jafo alisema kuwa ni heshima kwake binafsi na Taifa Kupokea Tuzo hiyo ya Udhamini Mchango mzuri kwa mwanafunzi aliyesoma SUA na kuleta tija kwa Jamii hasa katika Kilimo,Elimu na Mazingira ,

"Hii ni heshima Sana kwangu na taifa pia natoa Shukran za dhati kwa Uongozi Chuo kikuu cha Kilimo SUA Kwa kunipatia Tuzo maana nilipata kusoma hapa miaka iliyopita katika ngazi ya Shahada na Wanafunzi wapo wengi Sana ila waliona wanipatie mie hasa kwa Mchango mkubwa nilioutoa katika uhifadhi na utunzaji wa Mazingira alisema Dr Jafo"

Chuo kikuu cha Kilimo Sua leo 25.12.2022 kinahitisha Mahafali ya arobaini kwa kudahilisha wanafunzi katika kada mbalimbali ikiwemo ya Kilimo,Mifugo,Elimu na Afya.






Share this article :
 
Support : #BegaKwaBegaNaMamaSamia | JAK | CCM Arusha
Copyright © 2011. CCM Dijitali - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Jasper K
Proudly powered by Blogger
Link