Home » » MAKAMU WA PILI WA RAIS WA ZANZIBAR AFUNGUA MKUTANO WA BODI YA GPE

MAKAMU WA PILI WA RAIS WA ZANZIBAR AFUNGUA MKUTANO WA BODI YA GPE

Written By CCMdijitali on Tuesday, December 5, 2023 | December 05, 2023

  

MAKAMU WA PILI WA RAIS WA ZANZIBAR AFUNGUA MKUTANO WA BODI YA GPE MJINI UNGUJA LEO

 
Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdullah leo amefungua rasmi mkutano wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Ushirika wa Maendeleo ya Elimu Duniani (GPE) unaoongozwa na Mwenyekiti wa Bodi hio, Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, hoteli ya Zanzibar Hyatt, Unguja, leo.
 
Mkutano huo wa siku mbili, unafanyika kwa mara ya kwanza barani Afrika na nje ya Marekani na Ulaya, tangu Shirika hilo lianzishwe na mataifa tajiri duniani ya G7 miaka 20 iliyopita.
 
Kwa mujibu wa Dkt. Kikwete, ambaye ni Mwafrika wa kwanza kuongoza GPE, shirika hilo hadi sasa limeishaipatia Tanzania jumla ya Dola za Kimarekani Milioni 332 (takriban shilingi 834,980,332,000.00) ili kusaidia maendeleo ya sekta ya elimu Tanzania bara na Zanzibar.
 
Bodi ya Wakurugenzi ya GPE inaundwa na majimbo 20 yanayowakilisha washirika wote wa ushirikiano, ambapo katika mkutano wa bodi wanahudhuria Mjumbe wa Bodi na mjumbe mbadala wa Bodi wanawakilisha kila jimbo.
 
Bodi ya Wakurugenzi ya GPE huweka sera na mikakati ya ushirikiano, huku ikiakisi hali pana na tofauti ya ubia na inajumuisha wanachama kutoka serikali za nchi zenye mapato ya chini na washirika wote wa maendeleo: wakiwemo wafadhili, mashirika ya kiraia, sekta binafsi na wakfu, na mashirika ya kimataifa na benki za kikanda.
 
Nchi washirika wa GPE ni Afghanistan, Albania, Algeria, Angola, Bangladesh, Belize, Benin, Bhutan, Bolivia,  Burkina Faso, Burundi, Cabo Verde, Cambodia, Cameroon, Central African Republic, Chad, Comoros, Congo, Democratic Republic ofCongo, Republic of,  Côte d'Ivoire, Djibouti, Dominica, na  Egypt.
 
Nchi zingine ni El Salvador, Eritrea, Eswatini, Ethiopia, Fiji, The Gambia, Georgia, Ghana, Grenada, Guatemala, Guinea, Guinea-Bissau, Guyana, Haiti, Honduras, India, Indonesia, Kenya, Kiribati, Kyrgyz Republic, Lao PDR, Lesotho, Liberia, Madagascar, Malawi, Maldives, Mali, Marshall Islands, Mauritania, FS Micronesia, Moldova, Mongolia na Morocco.
 
Zingine ni Mozambique, Myanmar, Nepal, Nicaragua, Niger, Nigeria, Pacific region, Pakistan, Papua New Guinea, Philippines, Rwanda, Saint Lucia, Saint Vincent and the Grenadines, Samoa, São Tomé and Príncipe, Senegal, Sierra Leone, Solomon Islands, Somalia, South Sudan, Sri Lanka, Sudan, Tajikistan.
 
Tanzania, Timor-Leste, Togo, Tonga, Tunisia, Tuvalu, Uganda, Ukraine, Uzbekistan, Vanuatu, Viet Nam, West Bank and Gaza, Yemen, Zambia na Zimbabwe pia ni nchi washirika.  Syria si nchi mwanachama lakini imepokea ufadhili kwa idhini ya Bodi ya GPE.
 
 

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Ushirika wa Elimu Duniani (GPE) Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi kitabu Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdullah kabla hajafungua rasmi mkutano wa Bodi hio katika hoteli ya Zanzibar Hyatt, Unguja, leo.


 
 
 
 

Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdullah akiongea na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Ushirika wa Elimu Duniani (GPE) Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na Makamu Wake Bi Suzan Liautaud na Afisa Mtendaji Mkuu Laura Fringeti kabla hajafungua rasmi mkutano wa Bodi hio katika hoteli ya Zanzibar Hyatt, Unguja, leo.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Ushirika wa Elimu Duniani (GPE) Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akioingoza mkutano wa Bodi hio katika hoteli ya Zanzibar Hyatt, Unguja, leo.

 

 Na Ofisi ya Rais Mstaafu

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Ushirika wa Elimu Duniani (GPE) Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimsindikiza Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdullah baada ya kufungua  rasmi mkutano wa Bodi hio katika hoteli ya Zanzibar Hyatt, Unguja, leo.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Ushirika wa Elimu Duniani (GPE) Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimsindikiza Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdullah baada ya kufungua  rasmi mkutano wa Bodi hio katika hoteli ya Zanzibar Hyatt, Unguja, leo.

Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdullah akiwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Ushirika wa Elimu Duniani (GPE) Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na Makamu Wake Bi Suzan Liautaud na Afisa Mtendaji Mkuu Laura Fringeti  akifungua rasmi mkutano wa Bodi hio katika hoteli ya Zanzibar Hyatt, Unguja,

leo.

Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdullah akiwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Ushirika wa Elimu Duniani (GPE) Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na Makamu Wake Bi Suzan Liautaud na Afisa Mtendaji Mkuu Laura Fringeti  akifungua rasmi mkutano wa Bodi hio katika hoteli ya Zanzibar Hyatt, Unguja,

leo.

Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdullah akiwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Ushirika wa Elimu Duniani (GPE) Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na Makamu Wake Bi Suzan Liautaud na Afisa Mtendaji Mkuu Laura Fringeti  akifungua rasmi mkutano wa Bodi hio katika hoteli ya Zanzibar Hyatt, Unguja,

leo.

Share this article :
 
Support : #BegaKwaBegaNaMamaSamia | JAK | CCM Arusha
Copyright © 2011. CCM Dijitali - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Jasper K
Proudly powered by Blogger
Link