Home » » PINDA ATAKA MRADI UJENZI CHUO CHA ARDHI MOROGORO KUWEKEWA NGUVU

PINDA ATAKA MRADI UJENZI CHUO CHA ARDHI MOROGORO KUWEKEWA NGUVU

Written By CCMdijitali on Saturday, June 29, 2024 | June 29, 2024


Published from Blogger Prime Android App
Na Munir Shemweta, MOROGORO

Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Geophrey Pinda ametaka mradi wa ujenzi wa Chuo cha Ardhi Morogoro unaojumuisha eneo mahali chuo kilipo na eneo la mlima Kola kuwekewa nguvu ili uweze kukamilika kabla ya muda uliopangwa.

Mhe. Pinda ametoa kauli hiyo leo tarehe 29 Juni 2024 wakati alipokwenda kukagua eneo la ujenzi wa mradi huo katika eneo la mlima Kola mkoani Morogoro.

Mradi wa ujenzi wa Chuo cha Ardhi Morogoro unaojumisha mahali chuo kilipo pamoja na eneo la Mlima Kola umeelezwa kuchukua miaka 20 mpaka kukamilika kwake mwaka 2043 na utagharimu kiasi cga shilingi bilioni 70 ambapo bilioni 64 zitawekezwa eneo la mlima Kola na bil 6 kwenye kampasi ya chuo Kilakala.

Mradi huo unajumuisha Jengo la Utawala, Madarasa, Maktaba, Hosteli za Wanafunzi, Kumbi kubwa za kufundishia, Zahanati, Migahawa pamoja na maeneo ya kuabudia.

Kwa mujibu wa Kaimu Mkuu wa Idara ya Taaluma Pius Kafefa, vyanzo vya mapato kwa ajili ya ujenzi wa mradi huo wa chuo cha ARIMO ni ada za wanafunzi, miradi mbalimbali ya chuo kama vile ushauri wa kitaaluma, fedha kutoka serikalini pamoja na maombi kutoka kwa wafadhili.

 Naibu Waziri wa Ardhi Mhe. Pinda amesema, ni vyema mradi huo ukawekewa nguvu ili uende kwa haraka kwa kuwa kuchukua muda mrefu kutafifisha uharaka wa maendeleo ya chuo.

"Kujipa muda mrefu kukamilisha mradi wa chuo chenu hakuko sawa kabisa na sisi tunataka mradi uishe haraka ili tuwe na matokeo ya muda mfupi sambamba na waanzishaji mradi kuushuhudia". amesema Mhe. Pinda.

Ameutaka uongozi wa chuo cha ARIMO kuandika mapendekezo ya namna ya kukamilisha ujenzi wa mradi huo kwa haraka ili wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi ione namna ya kusaidia ili uishe kabla ya muda wa miaka 20 uliopangwa.

Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo cha Ardhi Morogoro Profesa Ernest Kahanga ameeleza kuwa, changamoto kubwa inayokikabili chuo ni upungufu wa walimu pamoja na miundombinu ambapo ameweka wazi kuwa, kama chuo hicho kingetatua changamoto hizo kingefanikiwa kudahili takriban wanafunzi 3000 na kukifanya chuo kusonga mbele kwa kasi na kuondokana na utegemezi.

Published from Blogger Prime Android App

Published from Blogger Prime Android App

Published from Blogger Prime Android App
 Published from Blogger Prime Android App
Share this article :
 
Support : #BegaKwaBegaNaMamaSamia | JAK | CCM Arusha
Copyright © 2011. CCM Dijitali - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Jasper K
Proudly powered by Blogger
Link