MIUNDOMBINU YA ELIMU ZANZIBAR SASA YALINGANA NA MAHITAJI YA KARNE YA 21
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Zanzibar imepiga hatua kubwa katika kuimarisha mazin...
Latest Post
December 31, 2025
RAIS MWINYI AFUNGUA NYUMBA ZA WAFANYAKAZI HOSPITALI YA KITOGANI
Written By CCMdijitali on Wednesday, December 31, 2025 | December 31, 2025
RAIS MWINYI AFUNGUA NYUMBA ZA WAFANYAKAZI HOSPITALI YA KITOGANI, AAGIZA ZHC KUSIMAMIA UJENZI WA MAKAAZI YA WATUMISHI

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema lengo la Serikali ni kuimarisha na kuongeza ubora wa huduma za afya kwa wananchi katika maeneo yote ya Zanzibar, sambamba na kuwapunguzia wafanyakazi wa sekta ya afya masafa ya kusafiri kwa kuhakikisha wanakuwa karibu na jamii wanayoihudumia.
Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo tarehe 31 Disemba 2025 alipofungua nyumba za makaazi ya wafanyakazi wa Hospitali ya Kitogani, Mkoa wa Kusini Unguja.
Aidha, Rais Dkt. Mwinyi ameagiza miradi yote ya ujenzi wa nyumba za makaazi ya wafanyakazi wa Serikali isimamiwe na Shirika la Nyumba la Zanzibar (ZHC), ili kuongeza ufanisi, kasi ya utekelezaji na kupunguza gharama za ujenzi. Ameielekeza Wizara ya Afya kujikita zaidi katika ujenzi wa hospitali na utoaji wa huduma za afya, badala ya kujenga nyumba za wafanyakazi, jukumu ambalo amesema ni mahsusi kwa Shirika la Nyumba la Zanzibar.
Ameeleza kuwa ZHC lina dhamana na uwezo wa kitaalamu wa kushughulikia masuala ya makaazi, kusimamia miradi ya ujenzi kwa ufanisi na kuhakikisha inatekelezwa kwa viwango vinavyotakiwa.
Rais Dkt. Mwinyi amebainisha kuwa baada ya Serikali kufanikisha ujenzi wa vituo vya afya na hospitali za wilaya katika wilaya zote 11 za Zanzibar, sasa inaelekeza nguvu katika kukamilisha ujenzi wa hospitali za mikoa katika mikoa yote mitano.
Vilevile, amefahamisha kuwa Serikali inaendelea na ujenzi wa hospitali tatu kubwa za rufaa, ambazo ni ujenzi mpya wa Hospitali ya Mnazi Mmoja, Hospitali ya Matibabu ya Saratani ya Binguni, pamoja na Hospitali ya Kujifunzia (Teaching Hospital) itakayojengwa Binguni. Amesisitiza kuwa hospitali hizo zote zitaambatana na nyumba za makaazi ya wafanyakazi.
Akizungumzia nyumba za makaazi za Kitogani alizozifungua, Rais Dkt. Mwinyi amesema ni utekelezaji wa ahadi ya Serikali ya kuwapatia wafanyakazi wa hospitali, hususan wataalamu wabobezi, makaazi bora yaliyo karibu na maeneo yao ya kazi. Amesema hatua hiyo itahamasisha watumishi, kuboresha utoaji wa huduma za afya, na kupunguza upungufu wa nyumba za makaazi kwa watumishi wa umma.
Rais amefafanua kuwa Serikali tayari imejenga nyumba za wafanyakazi katika hospitali nyingine za wilaya, ikiwemo Hospitali ya Abdalla Mzee, Mkoani Pemba, kupitia Wizara ya Afya.
Ameeleza kuwa hatua hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa ahadi kwa wananchi wa Zanzibar iliyotolewa wakati wa kampeni za uchaguzi, kwa kushirikiana nao katika kutatua changamoto mbalimbali, ikiwemo sekta ya afya. Amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kutekeleza miradi ya maendeleo ili kufikia maendeleo endelevu ifikapo mwaka 2030.
Rais Dkt. Mwinyi ameipongeza Wizara ya Afya kwa kufanikisha ujenzi wa nyumba hizo, na amemuagiza mkandarasi kukamilisha maeneo yote yaliyosalia kwa muda mfupi ujao.
Akitoa taarifa ya kitaalamu, Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Ndg. Mngereza Miraji Mzee, amesema jengo hilo la ghorofa tatu limejengwa na Kampuni ya Quality Building Contractor kwa gharama ya Shilingi bilioni 5.5 kutoka Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, na lina uwezo wa kuhudumia familia 16 za wafanyakazi wa Hospitali ya Kitogani.














Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema lengo la Serikali ni kuimarisha na kuongeza ubora wa huduma za afya kwa wananchi katika maeneo yote ya Zanzibar, sambamba na kuwapunguzia wafanyakazi wa sekta ya afya masafa ya kusafiri kwa kuhakikisha wanakuwa karibu na jamii wanayoihudumia.
Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo tarehe 31 Disemba 2025 alipofungua nyumba za makaazi ya wafanyakazi wa Hospitali ya Kitogani, Mkoa wa Kusini Unguja.
Aidha, Rais Dkt. Mwinyi ameagiza miradi yote ya ujenzi wa nyumba za makaazi ya wafanyakazi wa Serikali isimamiwe na Shirika la Nyumba la Zanzibar (ZHC), ili kuongeza ufanisi, kasi ya utekelezaji na kupunguza gharama za ujenzi. Ameielekeza Wizara ya Afya kujikita zaidi katika ujenzi wa hospitali na utoaji wa huduma za afya, badala ya kujenga nyumba za wafanyakazi, jukumu ambalo amesema ni mahsusi kwa Shirika la Nyumba la Zanzibar.
Ameeleza kuwa ZHC lina dhamana na uwezo wa kitaalamu wa kushughulikia masuala ya makaazi, kusimamia miradi ya ujenzi kwa ufanisi na kuhakikisha inatekelezwa kwa viwango vinavyotakiwa.
Rais Dkt. Mwinyi amebainisha kuwa baada ya Serikali kufanikisha ujenzi wa vituo vya afya na hospitali za wilaya katika wilaya zote 11 za Zanzibar, sasa inaelekeza nguvu katika kukamilisha ujenzi wa hospitali za mikoa katika mikoa yote mitano.
Vilevile, amefahamisha kuwa Serikali inaendelea na ujenzi wa hospitali tatu kubwa za rufaa, ambazo ni ujenzi mpya wa Hospitali ya Mnazi Mmoja, Hospitali ya Matibabu ya Saratani ya Binguni, pamoja na Hospitali ya Kujifunzia (Teaching Hospital) itakayojengwa Binguni. Amesisitiza kuwa hospitali hizo zote zitaambatana na nyumba za makaazi ya wafanyakazi.
Akizungumzia nyumba za makaazi za Kitogani alizozifungua, Rais Dkt. Mwinyi amesema ni utekelezaji wa ahadi ya Serikali ya kuwapatia wafanyakazi wa hospitali, hususan wataalamu wabobezi, makaazi bora yaliyo karibu na maeneo yao ya kazi. Amesema hatua hiyo itahamasisha watumishi, kuboresha utoaji wa huduma za afya, na kupunguza upungufu wa nyumba za makaazi kwa watumishi wa umma.
Rais amefafanua kuwa Serikali tayari imejenga nyumba za wafanyakazi katika hospitali nyingine za wilaya, ikiwemo Hospitali ya Abdalla Mzee, Mkoani Pemba, kupitia Wizara ya Afya.
Ameeleza kuwa hatua hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa ahadi kwa wananchi wa Zanzibar iliyotolewa wakati wa kampeni za uchaguzi, kwa kushirikiana nao katika kutatua changamoto mbalimbali, ikiwemo sekta ya afya. Amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kutekeleza miradi ya maendeleo ili kufikia maendeleo endelevu ifikapo mwaka 2030.
Rais Dkt. Mwinyi ameipongeza Wizara ya Afya kwa kufanikisha ujenzi wa nyumba hizo, na amemuagiza mkandarasi kukamilisha maeneo yote yaliyosalia kwa muda mfupi ujao.
Akitoa taarifa ya kitaalamu, Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Ndg. Mngereza Miraji Mzee, amesema jengo hilo la ghorofa tatu limejengwa na Kampuni ya Quality Building Contractor kwa gharama ya Shilingi bilioni 5.5 kutoka Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, na lina uwezo wa kuhudumia familia 16 za wafanyakazi wa Hospitali ya Kitogani.













Labels:
ZANZIBAR
December 20, 2025
"INGIENI KATIKA DUNIA YA KAZI KWA MOYO WA UADILIFU"- DKT AKWILAPO
Written By CCMdijitali on Saturday, December 20, 2025 | December 20, 2025
Na Munir Shemweta, WANMM TABORA
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo amewataka wahitimu wa chuo cha ardhi Tabora (ARITA) kuingia kwenye dunia ya kazi kwa moyo wa uadilifu, uzalendo na ubunifu.
Amesema, Taifa linawategemea wahitimu hao sambamba na kuhitaji wataalamu wanaoweza kutumia elimu kwa manufaa ya wote na si kwa maslahi binafsi.
"Tumieni utaalamu wenu kwa weledi, uadilifu na kufuata sheria. Epukeni kabisa mambo ya rushwa na ufisadi". Amesema.
Mhe. Dkt Akwilapo ametoa kauli hiyo leo tarehe 19 Desemba 2025 katika Mahafali ya 43 Chuo cha Ardhi Tabora (ARITA) yaliyofanyika chuoni hapo mkoani Tabora.
Aidha, amewataka wahitimu hao wa chuo cha ARITA kuendelea kujifunza kwa kuwa elimu haina mwisho na kusisitiza kuwa anataka kuona elimu waliyoipata inakuwa na manufaa kwa Taifa na sio machungu kwa Taifa.
"Muwe mabalozi wema wa Chuo. Msidanganyike na yanayoandikwa kwenye mitandao kwamba nyie ni kundi la wanajamii wenye ukaidi, wasio na utii, wala heshima kwa wazazi, viongozi na Serikali, Nyinyi ni hazina ya Taifa". Amesema
Mkuu wa wilaya ya Tabora Bi. Upendo Wella amewataka wahitimu wa chuo hicho kutumia vizuri utaalamu na ujuzi walioupata kwa kushirikiana na jamii katika kutatua changamoto za sekta ya ardhi.
"Wahitimu kama hamna ajira mkajiunge katika vikundi na muanzishe shughuli,elimu mliyopata mkaitumie vyema". Amesema
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Chuo cha Ardhi Tabora Dkt Lucy Shule amesema, chuo hicho kinaendelea kufanya maboresho mbalimbali yatakayokiwezesha chuo kuwa na miundombinu ya kisasa ya kufundishia na kujifunza.
Kwa mujibu wa Dkt Shule, maboresho hayo yatakiwezesha chuo cha Ardhi Tabora kuwa na uwezo wa kuongeza udahili na kozi mpya.
Mkuu wa chuo cha Ardhi Tabora Bw. Jeremiah Minja amesema, chuo chake ni miongoni mwa vyuo vichache nchini vinavyotoa mafunzo ya uchapishaji wa nyaraka nchini.
"Kutokana na kuongezeka kwa mahitaji ya kazi za uchapishaji katika ngazi ya Wizara na wateja wengine na kutokana na Wizara kukipa Chuo mtambo mkubwa wa uchapishaji uliopo Dar es Salaam chuo kina nia ya kuanzisha karakana nyingine ya uchapishaji katika Jiji la Dar es Salaam".Amesema Bw. Minja.
Katika risala yao iliyosomwa na Yohana Mhendi wahitimu wa chuo hicho wameishukuru Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa kuboresha mazingira ya chuo ikiwemo miundombinu ya kujifunzia kama vile kumbi za Mihadhara na Maktaba.
Katika mahafali hayo ya 43 ya chuo cha Ardhi Tabora, jumla ya wanafunzi 688 walihitimu ambapo kati ya hao kozi za Sanaa, Ubunifu na Uchapishaji ni 28, Kozi za Urasimu Ramani ni 126, Kozi za Usimamizi wa Ardhi, Uthamini na Usajili ni 483, Kozi za Usimamizi wa Mazingira ni 22 na Kozi za Mfumo wa Taarifa za Kijiografia ni 29.









Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo amewataka wahitimu wa chuo cha ardhi Tabora (ARITA) kuingia kwenye dunia ya kazi kwa moyo wa uadilifu, uzalendo na ubunifu.
Amesema, Taifa linawategemea wahitimu hao sambamba na kuhitaji wataalamu wanaoweza kutumia elimu kwa manufaa ya wote na si kwa maslahi binafsi.
"Tumieni utaalamu wenu kwa weledi, uadilifu na kufuata sheria. Epukeni kabisa mambo ya rushwa na ufisadi". Amesema.
Mhe. Dkt Akwilapo ametoa kauli hiyo leo tarehe 19 Desemba 2025 katika Mahafali ya 43 Chuo cha Ardhi Tabora (ARITA) yaliyofanyika chuoni hapo mkoani Tabora.
Aidha, amewataka wahitimu hao wa chuo cha ARITA kuendelea kujifunza kwa kuwa elimu haina mwisho na kusisitiza kuwa anataka kuona elimu waliyoipata inakuwa na manufaa kwa Taifa na sio machungu kwa Taifa.
"Muwe mabalozi wema wa Chuo. Msidanganyike na yanayoandikwa kwenye mitandao kwamba nyie ni kundi la wanajamii wenye ukaidi, wasio na utii, wala heshima kwa wazazi, viongozi na Serikali, Nyinyi ni hazina ya Taifa". Amesema
Mkuu wa wilaya ya Tabora Bi. Upendo Wella amewataka wahitimu wa chuo hicho kutumia vizuri utaalamu na ujuzi walioupata kwa kushirikiana na jamii katika kutatua changamoto za sekta ya ardhi.
"Wahitimu kama hamna ajira mkajiunge katika vikundi na muanzishe shughuli,elimu mliyopata mkaitumie vyema". Amesema
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Chuo cha Ardhi Tabora Dkt Lucy Shule amesema, chuo hicho kinaendelea kufanya maboresho mbalimbali yatakayokiwezesha chuo kuwa na miundombinu ya kisasa ya kufundishia na kujifunza.
Kwa mujibu wa Dkt Shule, maboresho hayo yatakiwezesha chuo cha Ardhi Tabora kuwa na uwezo wa kuongeza udahili na kozi mpya.
Mkuu wa chuo cha Ardhi Tabora Bw. Jeremiah Minja amesema, chuo chake ni miongoni mwa vyuo vichache nchini vinavyotoa mafunzo ya uchapishaji wa nyaraka nchini.
"Kutokana na kuongezeka kwa mahitaji ya kazi za uchapishaji katika ngazi ya Wizara na wateja wengine na kutokana na Wizara kukipa Chuo mtambo mkubwa wa uchapishaji uliopo Dar es Salaam chuo kina nia ya kuanzisha karakana nyingine ya uchapishaji katika Jiji la Dar es Salaam".Amesema Bw. Minja.
Katika risala yao iliyosomwa na Yohana Mhendi wahitimu wa chuo hicho wameishukuru Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa kuboresha mazingira ya chuo ikiwemo miundombinu ya kujifunzia kama vile kumbi za Mihadhara na Maktaba.
Katika mahafali hayo ya 43 ya chuo cha Ardhi Tabora, jumla ya wanafunzi 688 walihitimu ambapo kati ya hao kozi za Sanaa, Ubunifu na Uchapishaji ni 28, Kozi za Urasimu Ramani ni 126, Kozi za Usimamizi wa Ardhi, Uthamini na Usajili ni 483, Kozi za Usimamizi wa Mazingira ni 22 na Kozi za Mfumo wa Taarifa za Kijiografia ni 29.









December 20, 2025

Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Laurent Degratius Luswetula (Mb), amerejea wito wake kwa vijana kutumia teknolojia hususani Akili Mnemba (AI) na mitandao ya kijamii ili kubuni fursa za kiuchumi na kuongeza kipato.
Mhe. Luswetula amesema hayo wakati wa Mahafali ya 23 ya Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) -Kampasi ya Dar es Salaam, Zanzibar na Tanga yaliyofanyika katika viwanja vya Chuo hicho, Kurasini jijini Dar es Salaam.
Mhe. Luswetula alisema kuwa matumizi ya teknolojia yakitumika vizuri itawajengea vijana kujiamini, kufikiri kwa ubunifu na kuwa wazalishaji wa fursa badala ya kuwa watafuta ajira pekee.
Aidha Mhe. Luswetula aliwaasa vijana kuwa watengeneza maudhui (content creator) wenye tija na wanaozalisha maudhui yenye thamani, yanayongeza kipato, kuzingatia maadili na kufuata sheria na taratibu za nchi.
‘’Katika dunia ya sasa, tumieni teknolojia, hususan Akili Mnemba (AI) na mitandao ya kijamii, kubuni fursa za kiuchumi na kuongeza kipato. Vijana wa leo wanaita hii kuwa ‘content creator’ nawasihi muwe content creator wenye tija, wanaozalisha maudhui yenye thamani, yanayoongeza kipato kwa njia halali, kuzingatia maadili na kufuata sheria na taratibu za nchi yetu’’. Alisisitiza Mhe. Luswetula.
Katika mahafali hayo Mhe. Luswetula aliwataka wahitimu kutumia elimu na maarifa waliyoyapata chuoni kama mtaji wa maisha yao kwa kuwa Serikali inawategemea kuwa vijana wabunifu, waadilifu na watumiaji mahiri wa teknolojia katika kuleta mabadiliko Chanya katika jamii.
Mhe. Luswetula aliipongeza Taasisi ya Uhasibu Tanzania kwa kujumuisha Kampasi tatu za Dar es Salaam, Zanzibar na Tanga katika Mahafali ya 23 ya Taasisi hiyo na kuongeza kuwa mwelekeo wa maendeleo na faida za kijiografia, Dar es Salaam, Zanzibar na Tanga ni miongoni mwa maeneo muhimu yanayoendelea kukua kwa kasi na kuwa nguzo ya uchumi wa Taifa na hayo yanachangia kutoa fursa nyingi kwa wahitimu kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi na kuchangia maendeleo ya Taifa.
‘’Dar es Salaam inaendelea kuwa kitovu cha biashara, bandari na huduma za kifedha, Zanzibar ni lango muhimu la utalii, uchumi wa buluu na biashara ya bandari, huku Tanga ikiwa na nafasi ya kimkakati, viwanda na utalii wa fukwe. Maeneo haya yanatoa fursa nyingi kwa wahitimu wetu kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi na kuchangia maendeleo ya Taifa’’ Aliongeza Mhe. Luswetula.
Akiongea kwenye mahafali hayo, Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) Prof. William Pallangyo alisema kuwa Taasisi imeendelea kuboresha miundombinu ya kujifunzia na kufundishia katika Kampasi za Mtwara, Mbeya, Mwanza na Kigoma, huku shughuli za ujenzi zikiendelea katika Kampasi za Singida, Mwanza na Zanzibar ambapo Jumla ya shilingi za Kitanzania bilioni 59 zimetumika kupitia Mradi wa HEET na mapato ya ndani ya Taasisi katika ujenzi wa Kampasi hizo.
Prof. Pallangyo aliongeza kuwa Taasisi ya Uhasibu Tanzania imeanzisha kozi mpya za shahada ya Uzamili zinazolenga kukuza ujasiriamali, ubunifu na usimamizi wa miradi ili kuwaandaa wahitimu wenye ujuzi unaoendana na mahitaji ya soko.
‘’Katika Mwaka wa Masomo 2025/2056 TIA imeanzisha kozi mpya za Shahada ya Uzamili zinazolenga kukuza ujasiriamali, ubunifu na usimamizi wa miradi ya maendeleo. Lengo letu ni kuandaa wahitimu wenye ujuzi unaoendana na mahitaji ya soko la ajira, teknolojia na mwelekeo na Mpango wa Maendeleo ya Taifa (2050)’’ Alisema Prof.Pallangyo.
Prof. Pallangyo aliongeza kuwa Katika kuendeleza taaluma na ujuzi wa vitendo kwa wanafunzi, Taasisi imehimiza mafunzo ya vitendo na ubunifu kupitia mashindano ya Mawazo Bunifu (Business Ideas Competitions) katika kampasi zote nane ambapo kupitia mpango huu umewezesha wanafunzi kushiriki katika ziara za kielemu katika vyuo mbalimbali barani Afrika.
‘’ Kupitia mpango huu, mwaka 2023/24 wanafunzi walishiriki ziara za kielimu katika Chuo Kikuu cha Mount Kenya (Kenya). Mwaka 2024/25 walipelekwa Chuo Kikuu cha Makerere (Uganda). Mwaka huu maandalizi yanaendelea ya kuwapeleka washindi wa kampasi zote Chuo Kikuu cha Pretoria, Afrika Kusini’’ aliongeza Prof. Pallangyo.
Awali akimkaribisha mgeni rasmi, Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Laurent Degratius Luswetula (Mb), Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Wizara Profesa Jehovaness Aikael alisema bodi inaweka mkazo mkubwa katika ubora wa elimu, maadili, uwajibikaji na uadilifu ikitambua kwamba elimu bora haipimwi kwa maarifa pekee bali kwa uwezo wa Taasisi kulea wahitimu wenye tabia njema, weledi na uwezo wa kuaminika katika jamii na za kazi.
Profesa Aikael alisema kuwa Bodi ya ushauri ya Wizara imeendelea kusimamia muelekeo wa kimkakati wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania kwa lengo la kuifanya TIA kuwa Taasisi shindani kitaifa na kikanda, kwa kuhakikisha mitaala, mbinu za ufundishaji na mazingira ya kujifunzia vinaendana na mahitaji ya sasa na baadae kiuchumi, kwenye soko la ajira na maendeleo ya sayansi na teknolojia.
‘’Katika kusimamia mwelekeo huo, Bodi ya ushauri ya Wizara inaendelea kusisitiza umuhimu wa kuandaa wahitimu wanaoendana na mabadiliko ya sayansi na teknolojia, ikiwemo matumizi yenye weledi na uwajibikaji ya Akili Bandia (Artificial Intelligence) ili kuongeza ubora, ufanisi na ushindani wa rasilimali watu’’ alisema Prof. Aikael
Katika mahafali ya 23 ya Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) imejumuisha wahitimu 6,334 kati yao wanawake ni 3,589 na wanaume 2,745 ambao wametunikiwa vyeti katika ngazi mbalimbali kuanzia cheti cha Awali hadi shahada ya Uzamili.






MHE. LUSWETULA: VIJANA TUMIENI MITANDAO YA KIJAMII KUBUNI FURSA ZA KUJIKWAMUA KIUCHUMI.

Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Laurent Degratius Luswetula (Mb), amerejea wito wake kwa vijana kutumia teknolojia hususani Akili Mnemba (AI) na mitandao ya kijamii ili kubuni fursa za kiuchumi na kuongeza kipato.
Mhe. Luswetula amesema hayo wakati wa Mahafali ya 23 ya Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) -Kampasi ya Dar es Salaam, Zanzibar na Tanga yaliyofanyika katika viwanja vya Chuo hicho, Kurasini jijini Dar es Salaam.
Mhe. Luswetula alisema kuwa matumizi ya teknolojia yakitumika vizuri itawajengea vijana kujiamini, kufikiri kwa ubunifu na kuwa wazalishaji wa fursa badala ya kuwa watafuta ajira pekee.
Aidha Mhe. Luswetula aliwaasa vijana kuwa watengeneza maudhui (content creator) wenye tija na wanaozalisha maudhui yenye thamani, yanayongeza kipato, kuzingatia maadili na kufuata sheria na taratibu za nchi.
‘’Katika dunia ya sasa, tumieni teknolojia, hususan Akili Mnemba (AI) na mitandao ya kijamii, kubuni fursa za kiuchumi na kuongeza kipato. Vijana wa leo wanaita hii kuwa ‘content creator’ nawasihi muwe content creator wenye tija, wanaozalisha maudhui yenye thamani, yanayoongeza kipato kwa njia halali, kuzingatia maadili na kufuata sheria na taratibu za nchi yetu’’. Alisisitiza Mhe. Luswetula.
Katika mahafali hayo Mhe. Luswetula aliwataka wahitimu kutumia elimu na maarifa waliyoyapata chuoni kama mtaji wa maisha yao kwa kuwa Serikali inawategemea kuwa vijana wabunifu, waadilifu na watumiaji mahiri wa teknolojia katika kuleta mabadiliko Chanya katika jamii.
Mhe. Luswetula aliipongeza Taasisi ya Uhasibu Tanzania kwa kujumuisha Kampasi tatu za Dar es Salaam, Zanzibar na Tanga katika Mahafali ya 23 ya Taasisi hiyo na kuongeza kuwa mwelekeo wa maendeleo na faida za kijiografia, Dar es Salaam, Zanzibar na Tanga ni miongoni mwa maeneo muhimu yanayoendelea kukua kwa kasi na kuwa nguzo ya uchumi wa Taifa na hayo yanachangia kutoa fursa nyingi kwa wahitimu kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi na kuchangia maendeleo ya Taifa.
‘’Dar es Salaam inaendelea kuwa kitovu cha biashara, bandari na huduma za kifedha, Zanzibar ni lango muhimu la utalii, uchumi wa buluu na biashara ya bandari, huku Tanga ikiwa na nafasi ya kimkakati, viwanda na utalii wa fukwe. Maeneo haya yanatoa fursa nyingi kwa wahitimu wetu kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi na kuchangia maendeleo ya Taifa’’ Aliongeza Mhe. Luswetula.
Akiongea kwenye mahafali hayo, Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) Prof. William Pallangyo alisema kuwa Taasisi imeendelea kuboresha miundombinu ya kujifunzia na kufundishia katika Kampasi za Mtwara, Mbeya, Mwanza na Kigoma, huku shughuli za ujenzi zikiendelea katika Kampasi za Singida, Mwanza na Zanzibar ambapo Jumla ya shilingi za Kitanzania bilioni 59 zimetumika kupitia Mradi wa HEET na mapato ya ndani ya Taasisi katika ujenzi wa Kampasi hizo.
Prof. Pallangyo aliongeza kuwa Taasisi ya Uhasibu Tanzania imeanzisha kozi mpya za shahada ya Uzamili zinazolenga kukuza ujasiriamali, ubunifu na usimamizi wa miradi ili kuwaandaa wahitimu wenye ujuzi unaoendana na mahitaji ya soko.
‘’Katika Mwaka wa Masomo 2025/2056 TIA imeanzisha kozi mpya za Shahada ya Uzamili zinazolenga kukuza ujasiriamali, ubunifu na usimamizi wa miradi ya maendeleo. Lengo letu ni kuandaa wahitimu wenye ujuzi unaoendana na mahitaji ya soko la ajira, teknolojia na mwelekeo na Mpango wa Maendeleo ya Taifa (2050)’’ Alisema Prof.Pallangyo.
Prof. Pallangyo aliongeza kuwa Katika kuendeleza taaluma na ujuzi wa vitendo kwa wanafunzi, Taasisi imehimiza mafunzo ya vitendo na ubunifu kupitia mashindano ya Mawazo Bunifu (Business Ideas Competitions) katika kampasi zote nane ambapo kupitia mpango huu umewezesha wanafunzi kushiriki katika ziara za kielemu katika vyuo mbalimbali barani Afrika.
‘’ Kupitia mpango huu, mwaka 2023/24 wanafunzi walishiriki ziara za kielimu katika Chuo Kikuu cha Mount Kenya (Kenya). Mwaka 2024/25 walipelekwa Chuo Kikuu cha Makerere (Uganda). Mwaka huu maandalizi yanaendelea ya kuwapeleka washindi wa kampasi zote Chuo Kikuu cha Pretoria, Afrika Kusini’’ aliongeza Prof. Pallangyo.
Awali akimkaribisha mgeni rasmi, Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Laurent Degratius Luswetula (Mb), Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Wizara Profesa Jehovaness Aikael alisema bodi inaweka mkazo mkubwa katika ubora wa elimu, maadili, uwajibikaji na uadilifu ikitambua kwamba elimu bora haipimwi kwa maarifa pekee bali kwa uwezo wa Taasisi kulea wahitimu wenye tabia njema, weledi na uwezo wa kuaminika katika jamii na za kazi.
Profesa Aikael alisema kuwa Bodi ya ushauri ya Wizara imeendelea kusimamia muelekeo wa kimkakati wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania kwa lengo la kuifanya TIA kuwa Taasisi shindani kitaifa na kikanda, kwa kuhakikisha mitaala, mbinu za ufundishaji na mazingira ya kujifunzia vinaendana na mahitaji ya sasa na baadae kiuchumi, kwenye soko la ajira na maendeleo ya sayansi na teknolojia.
‘’Katika kusimamia mwelekeo huo, Bodi ya ushauri ya Wizara inaendelea kusisitiza umuhimu wa kuandaa wahitimu wanaoendana na mabadiliko ya sayansi na teknolojia, ikiwemo matumizi yenye weledi na uwajibikaji ya Akili Bandia (Artificial Intelligence) ili kuongeza ubora, ufanisi na ushindani wa rasilimali watu’’ alisema Prof. Aikael
Katika mahafali ya 23 ya Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) imejumuisha wahitimu 6,334 kati yao wanawake ni 3,589 na wanaume 2,745 ambao wametunikiwa vyeti katika ngazi mbalimbali kuanzia cheti cha Awali hadi shahada ya Uzamili.







Labels:
KITAIFA
December 17, 2025

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amewaagiza Watendaji Wakuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) na Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) kufanya tathmini ya miradi yote ambayo malipo ya awali yameshafanyika na hatua za ujenzi zilizofikiwa katika miradi hiyo.
Pia amewaagiza kuangalia kama utekelezaji wa miradi hiyo unaendana na kiwango cha fedha ambacho kimeshatolewa. “Na ikiwa itapatikana miradi ambayo imefanyika chini ya fedha iliyopatikana itakuwa ni hujuma dhidi ya uchumi wa nchi yetu, hawa ni lazima wafike kwenye mkono wa sheria”
Ametoa maagizo hayo leo, Jumatano, Desemba 17, 2025 wakati akizungumza na wananchi baada ya kukagua uharibifu wa miundombinu mbalimbali ikiwemo mzani wa. Magari (Mpemba), Mahakama ya Mwanzo Tunduma, soko la Machinga akiwa katika ziara ya kikazi mkoani Songwe.
“Nimefuatilia, yupo mkandarasi ambaye mlimtoa kule Mbinga, asipate kazi nyingine yeyote hapa nchini, wapatieni wazawa, haiwezekani tumpatie mtu pesa halafu aje atuchezeechezee hapa, wale wote mnaowalipa fedha halafu wanatumia kwenye miradi na madeni yao hawawalipi wazawa wasipate kazi tena”
Amesema kuwa wapo baadhi ya wakandarasi wanaolazimisha fedha za utekelezaji wa miradi inayofanyika nchini Tanzania zilipwe katika benki za nchi zao badala yake katika mikataba itakayoanza kuingiwa waelekezwe kufungua akaunti hapa nchini.
“Haiwezekani mradi unafanyika hapa nchini yeye anataka fedha zilipwe kwenye akaunti za nchi zao, zikifika huko wanalipa madeni, huku miradi inasimama, hapana, kwenye mikataba hakikisheni mnaweka kipengele cha wao kufungua akaunti hapa hapa nchini ili malipo yafanyike hapahapa”
Kadhalika, Mheshimiwa Waziri Mkuu amewataka viongozi katika maeneo yote nchini kutopuuza changamoto zinazowakabili wananchi na badala yake wafike kwenye maeneo yao na kushirikiana nao katika kuzitatua.
Amesema Serikali ipo kazini na amewahakikishia wananchi kwamba ahadi zote zilizotolewa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, zilizopo kwenye ilani ya uchaguzi pamoja na yaliyopo katika dira yatatekelezwa kwa vitendo.
Akizungumzia kuhusu usaili wa watumishi wa sekta za afya na elimu, Waziri Mkuu amewataka wahusika wote wa zoezi hilo wazingatie vigezo vilivyowekwa na wasitumie fursa hiyo kuwaweka watu wao. “Msidhulumu watu zingatieni vigezo.”
Pia, Waziri Mkuu amewasihi Watanzania wakiwemo wakazi wa Songwe waendelee kushirikiana kudumisha amani na wakatae kutumika na watu wanaotaka kuivuruga. “Sisi ndio wanufaika wa kwanza wa amani, tuwe na wivu na nchi yetu na haiwezi kuendeshwa kwa rimoti wala vikundi vya wahuni.”
Wakati huo huo, Waziri Mkuu amemuagiza Naibu Waziri wa Ujenzi Mhandisi, Godfrey Kasekenya ahakikishe wakati wa utiaji saini mikataba yote ya miradi ya ukandarasi malipo yake yafanyike kupitia benki na ndani ya nchi.
Mheshimiwa Dkt. Mwigulu pia amemuagiza Naibu Waziri huyo ahakikishe wakandarasi wanasimamiwa vizuri ili fedha zote wanazolipwa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali zitumike katika ujenzi wa miradi husika na si vinginevyo.

DKT. MWIGULU: TANROADS NA TARURA FANYENI TATHMINI YA MIRADI ILIYOLIPWA FEDHA ZA AWALI
Written By CCMdijitali on Wednesday, December 17, 2025 | December 17, 2025

Aagiza mikataba ya ujenzi wa miradi iwe na kipengele cha kufungua akaunti za malipo hapa nchini.
WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amewaagiza Watendaji Wakuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) na Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) kufanya tathmini ya miradi yote ambayo malipo ya awali yameshafanyika na hatua za ujenzi zilizofikiwa katika miradi hiyo.
Pia amewaagiza kuangalia kama utekelezaji wa miradi hiyo unaendana na kiwango cha fedha ambacho kimeshatolewa. “Na ikiwa itapatikana miradi ambayo imefanyika chini ya fedha iliyopatikana itakuwa ni hujuma dhidi ya uchumi wa nchi yetu, hawa ni lazima wafike kwenye mkono wa sheria”
Ametoa maagizo hayo leo, Jumatano, Desemba 17, 2025 wakati akizungumza na wananchi baada ya kukagua uharibifu wa miundombinu mbalimbali ikiwemo mzani wa. Magari (Mpemba), Mahakama ya Mwanzo Tunduma, soko la Machinga akiwa katika ziara ya kikazi mkoani Songwe.
“Nimefuatilia, yupo mkandarasi ambaye mlimtoa kule Mbinga, asipate kazi nyingine yeyote hapa nchini, wapatieni wazawa, haiwezekani tumpatie mtu pesa halafu aje atuchezeechezee hapa, wale wote mnaowalipa fedha halafu wanatumia kwenye miradi na madeni yao hawawalipi wazawa wasipate kazi tena”
Amesema kuwa wapo baadhi ya wakandarasi wanaolazimisha fedha za utekelezaji wa miradi inayofanyika nchini Tanzania zilipwe katika benki za nchi zao badala yake katika mikataba itakayoanza kuingiwa waelekezwe kufungua akaunti hapa nchini.
“Haiwezekani mradi unafanyika hapa nchini yeye anataka fedha zilipwe kwenye akaunti za nchi zao, zikifika huko wanalipa madeni, huku miradi inasimama, hapana, kwenye mikataba hakikisheni mnaweka kipengele cha wao kufungua akaunti hapa hapa nchini ili malipo yafanyike hapahapa”
Kadhalika, Mheshimiwa Waziri Mkuu amewataka viongozi katika maeneo yote nchini kutopuuza changamoto zinazowakabili wananchi na badala yake wafike kwenye maeneo yao na kushirikiana nao katika kuzitatua.
Amesema Serikali ipo kazini na amewahakikishia wananchi kwamba ahadi zote zilizotolewa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, zilizopo kwenye ilani ya uchaguzi pamoja na yaliyopo katika dira yatatekelezwa kwa vitendo.
Akizungumzia kuhusu usaili wa watumishi wa sekta za afya na elimu, Waziri Mkuu amewataka wahusika wote wa zoezi hilo wazingatie vigezo vilivyowekwa na wasitumie fursa hiyo kuwaweka watu wao. “Msidhulumu watu zingatieni vigezo.”
Pia, Waziri Mkuu amewasihi Watanzania wakiwemo wakazi wa Songwe waendelee kushirikiana kudumisha amani na wakatae kutumika na watu wanaotaka kuivuruga. “Sisi ndio wanufaika wa kwanza wa amani, tuwe na wivu na nchi yetu na haiwezi kuendeshwa kwa rimoti wala vikundi vya wahuni.”
Wakati huo huo, Waziri Mkuu amemuagiza Naibu Waziri wa Ujenzi Mhandisi, Godfrey Kasekenya ahakikishe wakati wa utiaji saini mikataba yote ya miradi ya ukandarasi malipo yake yafanyike kupitia benki na ndani ya nchi.
Mheshimiwa Dkt. Mwigulu pia amemuagiza Naibu Waziri huyo ahakikishe wakandarasi wanasimamiwa vizuri ili fedha zote wanazolipwa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali zitumike katika ujenzi wa miradi husika na si vinginevyo.


Labels:
KITAIFA
December 17, 2025

Na Munir Shemweta, WANMM
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo ameiagiza Tume ya Taifa ya Matumizi ya Ardhi kuongeza kasi ya kupanga na kupima ardhi katika maeneo mbalimbali nchini ikiwemo miradi ya kilimo, makazi na uwekezaji.
Mhe. Dkt Leonard Akwilapo amesema hayo leo tarehe 17 Desemba 2025 wakati akifungua Kikao Kazi cha Kamati ya Ufundi ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi kilichofanyika Makao Makuu ya Wizara jijini Dodoma.
Kupitia kikao hicho, Mhe. Dkt Akwilapo amehimiza kukuzwa kwa matumizi ya teknolojia katika ukusanyaji takwimu za kupanga ardhi, kulinda maeneo nyeti ya ikolojia, misitu, vyanzo vya maji, njia za wanyama pori pamoja na kujenga ustahimilivu wa mabadiliko ya tabia nchi kupitia mipango shirikishi na endelevu,
Amesema,Tanzania inakabiliwa na changamoto zinazohusiana na matumizi ya ardhi na kuzitaja kuwa ni pamoja na migongano kati ya shughuli za kilimo na ufugaji, malisho na uhifadhi na upungufu wa maeneo ya uwekezaji wa kimkakati kutokana na mabadiliko ya matumizi ya ardhi yasiyopangwa.
Changamoto nyingine ni uharibifu wa mazingira unaosababishwa na uvamizi wa vyanzo vya maji, ukataji miti hovyo, matumizi ya ardhi yasiyo rasmi, mabadiliko ya tabia nchi yanayoongeza shinikizo kwa ardhi na rasilimali zake na ukuaji wa haraka wa miji unaohitaji mipango bunifu na matumizi bora ya ardhi.
Katika kukabiliana na changamoto hizo, Mhe Dkt Akwilapo amesema, Serikali inategemea utaalamu na ushauri wa Kamati ya Ufundi ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi katika kuhakikisha ardhi inatumika kwa tija, usawa, usalama na uendelevu.
"Ninaamini ushauri wa Kamati utakuwa mhimili wa kuimarisha Sera, miongozi na taratibu zinazohusu matumizi ya ardhi nchini". Amesema Mhe. Dkt Akwilapo
"Niielekeze Tume kuwa makini kusaidia kamati kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi. Muwasidie ili waweze kutekeleza majukumu ili kusiwe na migongano mbele ya safari". Amesema.
Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhandisi Anthony Sanga Amesema, wizara yake ina imani kubwa na kazi za Tume ya Taifa ya Matumizi ya Ardhi kutokana na kuisaidia wizara na hasa katika maeneo ya migogoro ya vijijni ikiwemo ya wakulima na wafugaji.
"Nikiri kuwa migogoro ya wakulima na wafugaji imepungua sana tofauti na ilivyokuwa miaka ya zamani maana tulikuwa na kesi nyingi za hii migogoro lakini kwa kiasi kikubwa imepungua".Amesema.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi (NLUPC) Bw. Joseph Mafuru amesema,Tume yake itahakikisha kamati inatekeleza majukumu yake kwa weledi huku akiamini wajumbe walioteuliwa wataziwakilisha vyema taasisi walizotoka kwa kutekeleza kikamilifu majukumu ya Kamati.
"Katika kipindi chote ambacho Tume imekuwa bila Kamati, tumekosa mambo kadhaa muhimu kama vile fursa ya kupata ushauri wa kitaalamu unaotekelezwa kimfumo na kitaalamu katika sekta zote kuhusiana na matumizi ya ardhi kuanzia kilimo, mifugo, misitu, utalii, ujenzi, uwekezaji na nyinginezo ikiwemo tafiti". Amesema
Kwa mujibu wa Bw. Mafuru, mambo mengine ni kukosekana kwa mkakati wa pamoja wa utanzaji wa migogoro ya ardhi, upungufu wa takwimu za pamoja, pengo la uratibu wa taasisi pamoja na upungufu wa viwango vya kitaifa vya mipango.





WAZIRI AKWILAPO AAGIZA KUONGEZWA KWA KASI YA KUPANGA NA KUPIMA ARDHI NCHINI

Na Munir Shemweta, WANMM
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo ameiagiza Tume ya Taifa ya Matumizi ya Ardhi kuongeza kasi ya kupanga na kupima ardhi katika maeneo mbalimbali nchini ikiwemo miradi ya kilimo, makazi na uwekezaji.
Mhe. Dkt Leonard Akwilapo amesema hayo leo tarehe 17 Desemba 2025 wakati akifungua Kikao Kazi cha Kamati ya Ufundi ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi kilichofanyika Makao Makuu ya Wizara jijini Dodoma.
Kupitia kikao hicho, Mhe. Dkt Akwilapo amehimiza kukuzwa kwa matumizi ya teknolojia katika ukusanyaji takwimu za kupanga ardhi, kulinda maeneo nyeti ya ikolojia, misitu, vyanzo vya maji, njia za wanyama pori pamoja na kujenga ustahimilivu wa mabadiliko ya tabia nchi kupitia mipango shirikishi na endelevu,
Amesema,Tanzania inakabiliwa na changamoto zinazohusiana na matumizi ya ardhi na kuzitaja kuwa ni pamoja na migongano kati ya shughuli za kilimo na ufugaji, malisho na uhifadhi na upungufu wa maeneo ya uwekezaji wa kimkakati kutokana na mabadiliko ya matumizi ya ardhi yasiyopangwa.
Changamoto nyingine ni uharibifu wa mazingira unaosababishwa na uvamizi wa vyanzo vya maji, ukataji miti hovyo, matumizi ya ardhi yasiyo rasmi, mabadiliko ya tabia nchi yanayoongeza shinikizo kwa ardhi na rasilimali zake na ukuaji wa haraka wa miji unaohitaji mipango bunifu na matumizi bora ya ardhi.
Katika kukabiliana na changamoto hizo, Mhe Dkt Akwilapo amesema, Serikali inategemea utaalamu na ushauri wa Kamati ya Ufundi ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi katika kuhakikisha ardhi inatumika kwa tija, usawa, usalama na uendelevu.
"Ninaamini ushauri wa Kamati utakuwa mhimili wa kuimarisha Sera, miongozi na taratibu zinazohusu matumizi ya ardhi nchini". Amesema Mhe. Dkt Akwilapo
"Niielekeze Tume kuwa makini kusaidia kamati kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi. Muwasidie ili waweze kutekeleza majukumu ili kusiwe na migongano mbele ya safari". Amesema.
Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhandisi Anthony Sanga Amesema, wizara yake ina imani kubwa na kazi za Tume ya Taifa ya Matumizi ya Ardhi kutokana na kuisaidia wizara na hasa katika maeneo ya migogoro ya vijijni ikiwemo ya wakulima na wafugaji.
"Nikiri kuwa migogoro ya wakulima na wafugaji imepungua sana tofauti na ilivyokuwa miaka ya zamani maana tulikuwa na kesi nyingi za hii migogoro lakini kwa kiasi kikubwa imepungua".Amesema.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi (NLUPC) Bw. Joseph Mafuru amesema,Tume yake itahakikisha kamati inatekeleza majukumu yake kwa weledi huku akiamini wajumbe walioteuliwa wataziwakilisha vyema taasisi walizotoka kwa kutekeleza kikamilifu majukumu ya Kamati.
"Katika kipindi chote ambacho Tume imekuwa bila Kamati, tumekosa mambo kadhaa muhimu kama vile fursa ya kupata ushauri wa kitaalamu unaotekelezwa kimfumo na kitaalamu katika sekta zote kuhusiana na matumizi ya ardhi kuanzia kilimo, mifugo, misitu, utalii, ujenzi, uwekezaji na nyinginezo ikiwemo tafiti". Amesema
Kwa mujibu wa Bw. Mafuru, mambo mengine ni kukosekana kwa mkakati wa pamoja wa utanzaji wa migogoro ya ardhi, upungufu wa takwimu za pamoja, pengo la uratibu wa taasisi pamoja na upungufu wa viwango vya kitaifa vya mipango.






Labels:
KITAIFA
December 15, 2025

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Serikali itachukua hatua kali za kisheria dhidi ya viongozi na watumishi wa umma watakaoshindwa kujaza na kuwasilisha kwa wakati fomu za tamko la maadili katika Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma.
Rais Dkt. Mwinyi ametoa kauli hiyo leo wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Maadili na Haki za Binadamu Zanzibar, yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Dimani, Mkoa wa Mjini Magharibi. Amesisitiza kuwa kwa mujibu wa sheria, kila kiongozi na mtumishi wa umma anatakiwa kuwasilisha fomu hizo kabla ya tarehe 30 Desemba 2025.
Akielezea taarifa ya Mwenyekiti wa Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Rais Dkt. Mwinyi amesema kuwa hadi sasa ni viongozi 530 pekee, sawa na asilimia 19, kati ya viongozi 2,750 wanaotakiwa kisheria, ndio waliokamilisha zoezi hilo. Ameeleza kuwa Serikali haitasita kuchukua hatua dhidi ya watakaokiuka matakwa hayo ya kisheria.
Katika hatua nyingine, Rais Dkt. Mwinyi amesema Serikali ipo katika maandalizi ya kuanzisha Mfumo wa Upimaji wa Utendaji Kazi kwa Viongozi, utakaolenga kuongeza uwajibikaji, ufanisi na tija katika utoaji wa huduma kwa wananchi pamoja na kuimarisha utendaji wa taasisi za umma.
Akizungumzia mapambano dhidi ya rushwa na uhujumu wa uchumi, Rais Dkt. Mwinyi amesema Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu wa Uchumi (ZAECA) imepokea na kufanyia kazi jumla ya taarifa 524. Amefafanua kuwa katika kipindi cha Januari hadi Oktoba 2025, ZAECA imefanikiwa kidhibiti na kuokoa Jumla ya Shilingi 6,426,282,551/= na dola za kimarekani (USD) 89,371 zilirejeshwa Serikalini na shilingi 1,143,487,556/= na dola za Kimaekani (USD) 4,999 zilirejeshwa kwa wananchi.
Rais Dkt. Mwinyi amesema Tanzania, ikiwemo Zanzibar, imeendelea kupiga hatua kubwa katika utekelezaji wa Malengo ya Umoja wa Mataifa yanayohusiana na haki za binadamu na mapambano dhidi ya rushwa, kupitia uridhiaji na utekelezaji wa mikataba na mikakati ya kimataifa.
Akihitimisha hotuba yake, Rais Dkt. Mwinyi ametoa wito kwa viongozi wa taasisi za Serikali kutumia vyombo vya habari kuwaelimisha wananchi kuhusu shughuli na maendeleo ya nchi, na pia kuhimiza wananchi, vyombo vya habari, asasi za kiraia na sekta ya umma kushirikiana na Serikali katika kuimarisha utawala bora, haki za binadamu na mapambano dhidi ya rushwa.
Vilevile, Rais Dkt. Mwinyi ameipongeza Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa kushughulikia malalamiko ya wananchi kuhusu uvunjaji wa maadili ya viongozi, ambapo jumla ya malalamiko 28 yalipokelewa na manane tayari yamefanyiwa kazi.















RAIS MWINYI:SMZ ITACHUKUA HATUA KALI KWA VIONGOZI WASIOWASILISHA FOMU ZA MAADILI KWA WAKATI.
Written By CCMdijitali on Monday, December 15, 2025 | December 15, 2025

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Serikali itachukua hatua kali za kisheria dhidi ya viongozi na watumishi wa umma watakaoshindwa kujaza na kuwasilisha kwa wakati fomu za tamko la maadili katika Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma.
Rais Dkt. Mwinyi ametoa kauli hiyo leo wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Maadili na Haki za Binadamu Zanzibar, yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Dimani, Mkoa wa Mjini Magharibi. Amesisitiza kuwa kwa mujibu wa sheria, kila kiongozi na mtumishi wa umma anatakiwa kuwasilisha fomu hizo kabla ya tarehe 30 Desemba 2025.
Akielezea taarifa ya Mwenyekiti wa Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Rais Dkt. Mwinyi amesema kuwa hadi sasa ni viongozi 530 pekee, sawa na asilimia 19, kati ya viongozi 2,750 wanaotakiwa kisheria, ndio waliokamilisha zoezi hilo. Ameeleza kuwa Serikali haitasita kuchukua hatua dhidi ya watakaokiuka matakwa hayo ya kisheria.
Katika hatua nyingine, Rais Dkt. Mwinyi amesema Serikali ipo katika maandalizi ya kuanzisha Mfumo wa Upimaji wa Utendaji Kazi kwa Viongozi, utakaolenga kuongeza uwajibikaji, ufanisi na tija katika utoaji wa huduma kwa wananchi pamoja na kuimarisha utendaji wa taasisi za umma.
Akizungumzia mapambano dhidi ya rushwa na uhujumu wa uchumi, Rais Dkt. Mwinyi amesema Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu wa Uchumi (ZAECA) imepokea na kufanyia kazi jumla ya taarifa 524. Amefafanua kuwa katika kipindi cha Januari hadi Oktoba 2025, ZAECA imefanikiwa kidhibiti na kuokoa Jumla ya Shilingi 6,426,282,551/= na dola za kimarekani (USD) 89,371 zilirejeshwa Serikalini na shilingi 1,143,487,556/= na dola za Kimaekani (USD) 4,999 zilirejeshwa kwa wananchi.
Rais Dkt. Mwinyi amesema Tanzania, ikiwemo Zanzibar, imeendelea kupiga hatua kubwa katika utekelezaji wa Malengo ya Umoja wa Mataifa yanayohusiana na haki za binadamu na mapambano dhidi ya rushwa, kupitia uridhiaji na utekelezaji wa mikataba na mikakati ya kimataifa.
Akihitimisha hotuba yake, Rais Dkt. Mwinyi ametoa wito kwa viongozi wa taasisi za Serikali kutumia vyombo vya habari kuwaelimisha wananchi kuhusu shughuli na maendeleo ya nchi, na pia kuhimiza wananchi, vyombo vya habari, asasi za kiraia na sekta ya umma kushirikiana na Serikali katika kuimarisha utawala bora, haki za binadamu na mapambano dhidi ya rushwa.
Vilevile, Rais Dkt. Mwinyi ameipongeza Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma kwa kushughulikia malalamiko ya wananchi kuhusu uvunjaji wa maadili ya viongozi, ambapo jumla ya malalamiko 28 yalipokelewa na manane tayari yamefanyiwa kazi.
















Labels:
ZANZIBAR



