RAIS MWINYI AISHUKURU INDIA KWA MCHANGO MKUBWA KATIKA MAENDELEO YA ZANZIBAR

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ameishukuru Serikali ya India kwa misaada ambayo imeku...

Latest Post

RAIS MWINYI AISHUKURU INDIA KWA MCHANGO MKUBWA KATIKA MAENDELEO YA ZANZIBAR

Written By CCMdijitali on Monday, December 1, 2025 | December 01, 2025


Published from Blogger Prime Android App

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ameishukuru Serikali ya India kwa misaada ambayo imekuwa ikichangia maendeleo ya kiuchumi na kijamii nchini. 

Dkt. Mwinyi ameyasema hayo alipokutana na Balozi wa India nchini, Balozi Bishwadip Dey, aliyefika Ikulu Zanzibar leo tarehe 01 Desemba 2025 kuwasilisha salamu maalumu za pongezi kufuatia ushindi alioupata katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 29 Oktoba 2025.

Rais Dkt. Mwinyi ameihakikishia India kuwa Zanzibar itaendelea kuimarisha uhusiano wa karibu na wa muda mrefu baina ya nchi hizo mbili kwa manufaa ya wananchi wa pande zote mbili.

Ameeleza kuwa misaada inayotolewa na India kwa Zanzibar katika sekta za miundombinu, mradi wa maji mjini, nafasi za mafunzo kwa vijana wa Zanzibar, afya na teknolojia ya mawasiliano imekuwa kichocheo muhimu cha kuimarisha uhusiano wa mataifa hayo mawili na kuchangia maendeleo katika nyanja tofauti.

Aidha, Dkt. Mwinyi amesema Zanzibar inafarijika na ushirikiano inaoupata kutoka Serikali ya India na ipo tayari kwa ushirikiano zaidi hususan katika sekta za biashara, elimu na afya. 

Ameipongeza India kwa kuendelea kutoa nafasi za mafunzo kwa vijana wa Zanzibar katika nyanja mbalimbali.

Rais Dkt. Mwinyi amemueleza Balozi Bishwadip kuwa zipo fursa zaidi za uwekezaji ambazo wawekezaji na wafanyabiashara wa India wanaweza kuwekeza hapa nchini, na amewakaribisha kuwekeza hususan katika sekta za utalii na uchumi wa buluu ambazo ndizo sekta kuu za uchumi wa Zanzibar.

Akizungumzia teknolojia ya habari na mawasiliano, Rais Dkt. Mwinyi amesema mafunzo na maendeleo ya teknolojia yanayotolewa katika Taasisi ya IIT Madras hapa nchini yamekuwa chombo muhimu katika kuiwezesha Zanzibar kufikia dhamira ya kuwa na huduma za kidijitali katika sekta zote za utoaji huduma, na ameahidi kuwa Serikali itaendelea kutoa ushirikiano zaidi kwa ajili ya maendeleo ya taasisi hiyo.

Naye Balozi Bishwadip Dey amesema India itaendelea kushirikiana na Zanzibar katika nyanja mbalimbali za maendeleo kwani uhusiano huo ni nguzo muhimu ya kudumisha na kuimarisha mahusiano ya muda mrefu baina ya mataifa hayo.


Amempongeza Rais Dkt. Mwinyi kwa uongozi wake unaoleta mabadiliko makubwa ya maendeleo na kuihakikishia Zanzibar misaada zaidi, nafasi za mafunzo nchini India na ongezeko la bajeti ya miradi ya maendeleo.

Published from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android App

RAIS SAMIA: POLISI WAACHE KUMTAFUTA DKT. GWAJIMA

Written By CCMdijitali on Sunday, November 30, 2025 | November 30, 2025

Published from Blogger Prime Android App

WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameliagiza Jeshi la Polisi liache kumtafuta Askofu Dkt. Josephat Gwajima kama walivyokuwa wametangaza awali ili aweze kuendelea shughuli zake.

Amesema baada ya kutoa msamaha kwa Kanisa la Ufufuo na Uzima, waumini wanahitaji wamuone kiongozi wao, hivyo anatakiwa ajitokeze hadharani aendelee na kazi yake. “Mwacheni ajitokekeze tujenge umoja wa kitaifa, tushikamane kurudisha umoja wa kitaifa. Tumekutana na TEC, viongozi wa dini, wa mila na viongozi mbalimbali; twendeni sote kwenye jambo hili, tujitokeze tuhamasishe Tanzania yenye amani, huu ndio wito wa kiongozi wetu wa nchi”

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumapili, Novemba 30, 2025) wakati akizungumza na mamia ya wakazi wa Arumeru katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Magufuli Leganga, kata ya Usa River, wilayani Arumeru mkoani Arusha.

Waziri Mkuu amewataka Watanzania wakatae kushawishiwa na wanaharakati wanaochochea vurugu kwani zinarudisha nyuma maendeleo ya nchi. "Nimekuja kuwapa pole wananchi wenzangu, kwa niaba ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan. Anatambua mambo yanayoendelea. Anatambua kazi kubwa ya kujenga Taifa mnayoifanya," amesema.

Kabla ya mkutano huo, Waziri Mkuu alikagua uharibifu uliofanywa wakati wa vurugu za Oktoba 29, mwaka huu kwenye kituo cha polisi cha Kikatiti (mita 500 kutoka barabara kuu ya Arusha - Moshi); Mahakama ya Mwanzo ya Maji ya Chai (km. 3 kutoka barabara hiyo kuu); kituo cha mafuta Total Energies kilichopo Maji ya Chai (kipo barabarani) ambavyo vyote vilichomwa moto ikiwemo kuiba mali kwenye supermarket na kubomoa sefu ya kutunzia fedha.

Waziri Mkuu amesema masuala ya maendeleo ya wilaya ya hiyo kama vile maji na barabara yamo kwenye Ilani ya CCM na kwenye ahadi za Mheshimiwa Rais lakini yatafanyika endapo tu nchi itakuwa na amani. “Tukichagua vurugu tutakuwa tumechagua kufukuza maendeleo, tukichagua vurugu tutakuwa tumechagua kuongeza umaskini kwa mtu mmoja mmoja," ameonya.

"Kila Mtanzania akatae haya yaliyotokea juzijuzi. Tumechochewa, tumechonganishwa lakini wao wako nje, wanalipwa ili kutuvuruga tu. Wengi wanaochochea vurugu ni wanaharakati, wako nje ya nchi. Hakuna kiongozi wa chama cha siasa anasema wananchi wafanye vurugu. Au mmemuona?" alihoji.

Amesema baadhi ya vijana walioko nje ya nchi wamebainika kupokea dola za Marekani milioni mbili (sawa na sh. bilioni 4.5) ili wachochee vurugu. “Hawa wanaowalipa, wana maslahi gani na nchi yetu? Wana ajenda gani na nchi yetu? Tunajua watazirudishaje hizo fedha?”

“Hawa watu wanalenga tugombane ili wachukue madini adimu (rare earth minerals). Sasa hivi Tanzania imegundua uranium ambapo inakuwa nchi ya tisa duniani na ya kwanza barani Afrika. Ina tani za ujazo 890,000. Hii ni karibu tani milioni moja."
 
Waziri Mkuu ameonya dhidi ya mchezo unaotumika kuanzisha chokochoko ili kusambaratisha nchi pindi inapobainika kuwa na rasilimali. Amesema ziko baadhi ya nchi barani Afrika ziliathirika kutoka na chokochoko hizo. “Wanaanzisha chokochoko, wanaacha mnavurugana, rasilmali zikiisha, wao wanaondoka,” amesisitiza.

"Watanzania tuamkeni, tuchukue tahadhari. Kuna kamchezo kanachezwa. Wanajua Tanzania ina gesi asilia nyingi na inakaribia kuanza. Wanajua ikianza miradi hii, Tanzania itakuwa ya kwanza katika Afrika Mashariki na wala hatutahitaji kutoa mikopo ya wanafunzi."

Amewataka Watanzania waamke na kukataa kurudishwa tena kwenye hali ya vurugu. "Watanzania tuamke, tukatae kurejeshwa kule nyuma. Umaskini utaondolewa nchi ikiwa kwenye amani. Ajira za vijana zitaweza kupatikana nchi ikiwa kwenye amani."

Amesisitiza kuwa vurugu zikiwepo, hata wakulima wa karoti na nyanya wa Ngarenanyuki hazitauzwa na hivyo kuathiri uchumi wa mtu binafsi.

Published from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android App

DKT. MWIGULU AWAONYA WAVUNJIFU WA SHERIA

Written By CCMdijitali on Wednesday, November 26, 2025 | November 26, 2025



WAZIRI MKUU Dkt. Mwigulu Nchemba amevitaka vyombo vinavyosimamia usalama barabarani vitekeleze sheria hizo bila upendeleo kwani tabia ya kuogopana na kuoneana aibu imechangia baadhi ya watu kukwepa wajibu wakati wengine wakibebeshwa mzigo wa sheria. 

“Yeyote atakayevunja sheria akamatwe na hatua zichukuliwe kwa usawa. Huyu mmoja anavunja sheria anakamatwa, analipa. Huyu mwingine anavunja mbele yake anaachwa. Kama una haraka, toka mapema zaidi si kufidia kwa kuvunja sheria.”

Ametoa kauli hiyo leo (Jumatano, Novemba 26, 2025) wakati akifungua Maadhimisho ya Kimataifa ya Wiki ya Usafiri Endelevu Ardhini katika ukumbi wa Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.

Amesema kuwa haitakuwa uungwana kuona baadhi ya watu wakilipa adhabu papo hapo wanapokosea ilhali wengine wakiachwa kupita bila kuchukuliwa hatua.

Amewaonya baadhi ya viongozi na madereva wa Serikali ambao wanaelewa sheria vizuri lakini bado wanazikiuka kwa makusudi. “Ni muhimu kuwasaidia watumiaji wa vyombo vya usafiri kama bodaboda na bajaji ambao kwa sehemu kubwa wanaweza kuwa hawazielewi sheria kikamilifu, badala ya kuwaadhibu kwa upendeleo.” 

Dkt. Mwigulu amesisitiza umuhimu wa kuwapa Watanzania wote heshima na kuhakikisha sheria zilizowekwa zinatekelezwa kwa maslahi ya wote na kuongeza kuwa endapo zipo sheria ngumu kutekelezeka, basi zibadilishwe ili kila Mtanzania anufaike. 

Ameviagiza vyombo vya usimamizi wa sheria vihakikishe kuwa watumiaji wote wa vyombo vya usafiri wanazingatia usimamizi wa sheria na kuchukua hatua kwa yoyote anayevunja sheria akamatwe na kuchukuliwa hatua bila kuonewa aibu.

“Inaudhi mtu amebeba mgonjwa anafuata sheria, halafu mwingine anapita tu anavunja sheria, hapati adhabu. Mlalahoi akivunja sheria anapata adhabu, tunawapa kazi watekeleza sheria kuwaomba radhi watu waliovunja sheria. Naelekeza kila mtu afuate sheria, uwe wa serikalini ama uwe binafsi, tumeweka sheria, zifuatwe kama zilivyo.”

Mapema, akimkaribisha Waziri Mkuu kuzungumza na washiriki wa maadhimisho hayo, Waziri wa Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa alisema sekta ya uchukuzi ni mojawapo ya sekta wezeshi za uchumi duniani kota na kwamba watu wanahitaji njia za uchukuzi ili kusafiri kutoka sehemu moja kwenda nyingine. 

Alisema wizara yake itaendelea kushirikiana na wadau wa usafirishaji nchini ili kuhakikisha masuala ya nishati safi yanapewa kipaumbele. Akitoa mfano, Waziri Mbarawa alisema: “Uendeshaji wa reli ya kisasa (SGR) unatumia nishati ya umeme, mabasi ya mwendokasi njia ya Mbagala yanatumia gesi asili na baadhi ya taxi na bajaji zinatumia gesi asili.”

Published from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android App

RAIS MWINYI AAGIZA MAWAZIRI KUONGEZA KASI YA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU NA KUSHUKA HADI KWA WANANCHI

Written By CCMdijitali on Saturday, November 15, 2025 | November 15, 2025

Published from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android App


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ametoa agizo kwa Mawaziri na Manaibu Mawaziri kuongeza kasi ya utekelezaji wa majukumu yao na kushuka hadi ngazi za chini ili kuwahudumia wananchi kwa kutatua changamoto zinazowakabili badala ya kukaa maofisini.

Akizungumza katika hafla ya kuwaapisha Mawaziri na Manaibu Mawaziri aliowateua hivi karibuni, iliyofanyika leo tarehe 15 Novemba 2025 katika Viwanja vya Ikulu, Mkoa wa Mjini Magharibi, Dkt. Mwinyi amesema Serikali katika Kipindi cha Pili cha Awamu ya Nane itaweka utaratibu maalum wa kutathmini utendaji wa kila wizara pamoja na watendaji wake.

Aidha, Dkt. Mwinyi ameeleza kuwa Serikali imeanzisha Wizara ya Mawasiliano, Teknolojia ya Habari na Ubunifu kwa lengo la kuhakikisha kuwa huduma na utekelezaji wa shughuli za Serikali vinafanyika kwa njia ya kidijitali, ikiwemo masuala ya kifedha na ukusanyaji wa mapato.

Pia ameongeza kuwa Serikali imeunda Wizara ya Vijana, Ajira na Uwezeshaji yenye jukumu la kushughulikia changamoto za ajira kwa vijana na kuwawezesha kujiajiri.

Katika mageuzi hayo ya kimuundo, Rais Mwinyi amesema amepunguza idadi ya wizara zilizokuwa chini ya Afisi ya Rais, ambapo sasa zimebaki wizara tatu pekee huku nyingine mbili zikihamishiwa katika maeneo mengine ili kuongeza ufanisi.

Akiwaagiza Mawaziri kuandaa mpango kazi maalum, Rais Mwinyi amesema mpango huo unatakiwa kuzingatia utekelezaji wa ahadi za kampeni, Dira ya Maendeleo ya Zanzibar, pamoja na Ilani ya Chama Cha Mapinduzi. Aidha, amesisitiza umuhimu wa Mawaziri kutembelea miradi iliyo chini ya wizara zao ili kufuatilia thamani ya fedha, ubora wa mradi, kiwango cha utekelezaji na kuhakikisha inakamilika kwa wakati.

Dkt. Mwinyi amehimiza nidhamu katika matumizi ya fedha za Serikali ikiwemo kupunguza safari za nje, matumizi makubwa ya mafuta, pamoja na kudhibiti udanganyifu na ubadhirifu serikalini. Amewataka viongozi hao kusimamia ipasavyo uwajibikaji wa watendaji walio chini yao, kulinda mali za umma na kupambana na rushwa na uzembe.

Halikadhalika, Rais Mwinyi ameagiza kila wizara kuanzisha utaratibu wa tathmini ya utekelezaji kila baada ya robo mwaka, na kutoa taarifa kwa vyombo vya habari ili wananchi wapate kuelewa hatua zinazochukuliwa katika kutatua changamoto zao.

Amesema Serikali itaandaa mkataba maalum wa kupima utendaji wa viongozi na taasisi zote zilizo chini ya wizara husika, huku akisisitiza kuwa utendaji wa mawaziri unapaswa kwenda sambamba na kasi inayohitajika na Serikali.



Kuhusu utatuzi wa changamoto za wananchi, Dkt. Mwinyi amesema Serikali itaweka mfumo maalum utakaosaidia katika kusikiliza na kutatua changamoto hizo sambamba na Mfumo wa Sema na Rais.

Akizungumzia Serikali ya Umoja wa Kitaifa (SUK), Rais Mwinyi amekitaka Chama cha ACT Wazalendo kutafakari upya umuhimu wa kuungana katika Serikali ya Umoja wa Kitaifa kwa maslahi ya Taifa, akibainisha kuwa matakwa ya Katiba bado yanatoa nafasi ya kuundwa kwa Serikali hiyo na kwamba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inasubiri ushiriki wao.


WAZIRI MKUU AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA MKOA WA DODOMA


  • Atoa maagizo kwa Wizara ya Afya, MSD na hospitali zote nchini.

  • Ataka wajawazito wasisubirishwe mapokezi wanapofika hospitali

  • Wagojwa waipongeza Srtikali kwa kuboresha huduma za afya
 
WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Novemba 15, 2025 amefanya ziara ya kushtukiza katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma na kuziagiza hospitali zote nchini zihakikishe wajawazito wanapofika hospitali wahudumiwe kwa haraka ili kuokoa maisha ya mama na mtoto.

Pia, Waziri Mkuu ameiagiza Wizaya ya Afya, Bohari ya Dawa (MSD) na Hospitali zote nchini ziweke vipaumbele vya kuwa na dawa kulingana na mahitaji ya eneo husika. “ Haipendezi mwananchi kufika hospitali na kupatiwa vipimo vyote kisha anaambiwa dawa akanunue kwingine, kama duka binafsi linaweza kupata dawa hizo, inawezekanaje hospitali za serikali hapati? Naagiza Hospitali zote ziwe na dawa.”

Ametoa maagizo hayo wakati akizungumza na wananchi nje ya hospitali hiyo baada ya kutembelea wananchi waliofika hospitalini hapo kupata huduma mbalimbali za kitabibu ambapo amesisitiza wananchi waendelee kuhudumiwa vizuri kwa kuwa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa fedha nyingi kwa ajili ya kuboresha huduma za afya nchini vikiwemo vifaa tiba na dawa.

Kadhalika Mheshimiwa Waziri Mkuu ameziagiza hospitali zote nchini zihakikishe zinakuwa na vifaa vya usafi binafsi vya dharura vikiwemo ndoo na beseni katika wodi za wazazi ili viwasaidie akinamama wasiokuwa na vifaa hivyo. “Ujauzito sio suala la dharura vifaa kama ndoo tunapaswa kuwa navyo katika hospitali zetu za serikali.” 

Dkt. Mwigulu ametumia fursa hiyo kumpongeza Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayoifanya katika uboreshaji wa huduma za afya nchini. Waziri Mkuu akiwa hospitalini hapo, wananchi walimueleza kuwa wanahudumiwa vizuri na kwa uangalizi wa karibu.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu ameziagiza hospitali zote nchini zizingatie maelekezo ya kutumia mifumo sahihi ya malipo katika taratibu za kutoa huduma ili kuwezesha Serikali kuendelea kuhudumia wananchi. 

Dkt. Mwigulu ametoa agizo hilo kufuatia kuwepo kwa hospitali ambazo baadhi ya huduma wanapokea malipo kwa njia ya mtandao na nyingine malipo yanapokelewa malipo kwa njia zisizo rasmi.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wagonjwa na wananchi wanaoguza ndugu zao wamempongeza Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuhakikisha wananchi wanapatiwa huduma bora za afya. 

“Tunamshukuru Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwa tunapatiwa huduma nzuri kama tupo hospitali za private (binafsi).” Kauli hiyo imetolewa na Dinna Enock, mkazi wa Makulu jijini Dodoma ambaye amelazwa katika wodi ya wazazi.

Published from Blogger Prime Android App

RAIS MWINYI ATANGAZA MAWAZIRI WATEULE WA SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR

Written By CCMdijitali on Thursday, November 13, 2025 | November 13, 2025

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ametangaza uteuzi wa Mawaziri na Manaibu Mawaziri wateule, hatua inayolenga kuimarisha kasi ya maendeleo katika kipindi cha pili cha Awamu ya Nane ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Akizungumza leo, tarehe 13 Novemba 2025, Ikulu Zanzibar, Rais Dkt. Mwinyi amesema Serikali katika awamu hii itakuwa na wizara 20 badala ya 18 zilizokuwepo awali, ili kuongeza ufanisi wa utendaji Serikalini.

Katika uteuzi huo, Rais Dkt. Mwinyi amesisitiza weledi, uadilifu na uzingatiaji wa maslahi mapana ya Taifa, sambamba na kutoa huduma kwa wananchi kwa uwazi na ufanisi.

Ameeleza kuwa uteuzi huo umezingatia uwiano wa kijinsia, uwakilishi wa Unguja na Pemba, pamoja na uzoefu wa viongozi katika sekta zao husika.

Halikadhalika, Rais Dkt. Mwinyi amesema kuwa nafasi za Wizara nne zikiwemo Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais, Afya, Utalii na Mambo ya Kale, pamoja na Biashara na Maendeleo ya Viwanda , zitaachwa wazi kwa muda hadi Serikali ikamilishe makubaliano na Chama cha ACT Wazalendo katika kuunda Serikali ya Umoja wa Kitaifa.

Akitangaza Mawaziri na Naibu Mawaziri hao wateule, Dkt. Mwinyi ameyataja majina yao pamoja na Wizara watakazoongoza kama ifuatavyo:

MAWAZIRI

1. DKT. HAROUN ALI SULEIMAN, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora
2. MHE. DKT. SAADA MKUYA SALUM, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Ikulu
3. MHE. DKT. JUMA MALIK AKIL, Waziri wa Fedha na Mipango
4. MHE. IDRISSA KITWANA MUSTAFA, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ
5. MHE. SHARIFF ALI SHARIFF, Waziri wa Kazi na Uwekezaji
6. MHE. HAMZA HASSAN JUMA, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Sera, Uratibu na Baraza la Wawakilishi
7. MHE. RAHMA KASSIM ALI, Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makaazi
8. MHE. LELA MUHAMED MUSSA, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali
9. MHE. SHAABAN ALI OTHMAN, Waziri wa Vijana, Ajira na Uwezeshaji
10. MHE. SULEIMAN MASOUD MAKAME, Waziri wa Kilimo, Umwagiliaji,Maliasili na Mifugo
11. MHE. NADIR ABDULLATIF ALWARDY, Waziri wa Maji, Nishati na Madini
12. MHE. MASOUD ALI MOHAMED, Waziri wa Uchumi wa Buluu na Uvuvi
13. MHE. DKT. KHALID SALUM MOHAMED, Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi
14. MHE. ANNA ATHANAS PAUL, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto
15. MHE. MUDRIK RAMADHAN SORAGA, Waziri wa Mawasiliano, Teknolojia ya Habari na Ubunifu
16. MHE. RIZIKI PEMBE JUMA, Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo


MANAIBU MAWAZIRI


1. MHE. BADRIA ATAI MASOUD, Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi

2. MHE. DKT. HAMAD OMAR BAKARI, Naibu Waziri wa Fedha na Mipango

3. MHE. ALI ABDULGULLAM HUSSEIN, Naibu Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo

4. MHE. ZAWADI AMOUR NASSOR, Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto

5. MHE. SALHA MOHAMED MWINJUMA, Naibu Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makaazi

6. MHE. SEIF KOMBO PANDU, Naibu Waziri wa Maji, Nishati na Madini

7. MHE.DKT.SALUM SOUD HAMID, Naibu Waziri wa Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo

8. MHE. MBOJA RAMADHAN MSHENGA, Naibu Waziri wa Uchumi wa Buluu na Uvuvi

9. MHE. MOHAMED SIJAMINI MOHAMED, Naibu Waziri wa Mawasiliano, Teknolojia ya Habari na Ubunifu

10. MHE. HASSAN KHAMIS HAFIDH, Naibu Waziri wa Vijana, Ajira na Uwezeshaji

11. MHE. KHADIJA SALUM ALI, Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali


RAIS MWINYI AZINDUA BARAZA LA 11 LA WAWAKILISHI, ATOA MWELEKEO WA SERIKALI KIPINDI CHA PILI CHA AWAMU YA NANE

Written By CCMdijitali on Monday, November 10, 2025 | November 10, 2025



Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amezindua rasmi Baraza la 11 la Wawakilishi Zanzibar na kutoa mwelekeo wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kipindi cha pili cha Awamu ya Nane, akisisitiza dhamira ya Serikali kuendeleza maendeleo ya kijamii na kiuchumi kwa msingi wa amani, umoja na mshikamano wa kitaifa.

Akizungumza leo tarehe 10 Novemba 2025, katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi Chukwani, Unguja, Rais Dkt. Mwinyi amesema Serikali itaendelea kutekeleza Ilani ya CCM 2025–2030, pamoja na ahadi za kampeni na kuendeleza mafanikio yaliyopatikana katika kipindi cha kwanza cha Awamu ya Nane.

Amesema Serikali itaendeleza mageuzi ya kiuchumi kwa kuimarisha sekta za uzalishaji, uwekezaji, sekta binafsi, na matumizi ya teknolojia za kisasa, ikiwa na lengo la kuongeza ukuaji wa uchumi kutoka asilimia 7 hadi 10 kwa mwaka, kudhibiti mfumko wa bei chini ya asilimia 5, kuzalisha ajira mpya 350,000, na kuongeza kipato cha mwananchi hadi Dola 1,880 kufikia mwaka 2030.

Aidha, Serikali itatekeleza ujenzi wa bandari jumuishi ya Mangapwani, bandari za abiria Mpigaduri, Kizimkazi, Shumba na Wete, pamoja na boti mbili za kisasa za mwendo kasi zitakazohudumia safari kati ya Unguja, Pemba, Tanga na Dar es Salaam.

Katika sekta ya afya, Serikali itajenga hospitali nne za mikoa, kuendeleza ujenzi wa Hospitali ya Saratani Binguni, na kuboresha Hospitali ya Mnazi Mmoja.
Katika elimu, Serikali itajenga madarasa mapya 2,000, shule tatu za sekondari za wasichana kwa kila mkoa, chuo cha kisasa cha ualimu, na kuajiri walimu 7,691.

Rais Dkt. Mwinyi amesema Serikali itaendelea kuimarisha utumishi wa umma kwa kuongeza mafunzo, maslahi na nidhamu ya kazi, huku taasisi za ZAECA na CAG zikiimarisha mifumo ya udhibiti wa rushwa na matumizi sahihi ya fedha za umma.
Ameongeza kuwa Afisi ya Usalama wa Shughuli za Serikali (GSO) itaongoza usimamizi wa nidhamu serikalini.

Vilevile, Serikali itajenga vituo viwili vya utamaduni Unguja na Pemba, kuendeleza michezo, na kukamilisha maandalizi ya AFCON 2027.

Akizungumzia Uchumi wa Buluu, Rais Dkt. Mwinyi amesema Serikali inalenga kuongeza idadi ya watalii wa kimataifa kutoka 800,000 hadi 1,500,000 kwa mwaka, na kwa Kisiwa cha Pemba watalii kuongezeka kutoka 200,000 hadi 300,000 kwa mwaka.

Ameeleza kuwa Serikali itaendeleza uvuvi na kilimo cha mwani kwa kuimarisha miundombinu ya uvuvi, ikiwemo madiko na masoko makubwa ya samaki, pamoja na kuwawezesha wafugaji wa mazao ya baharini kama samaki, matango bahari na kaa kwa njia za kibiashara.
Uzalishaji wa mwani mkavu unatarajiwa kuongezeka kutoka tani 19,715 mwaka 2024 hadi tani 40,000 mwaka 2030.

Serikali pia itaendelea kuwawezesha wananchi kiuchumi kwa kutoa mikopo yenye thamani ya shilingi bilioni 100, na mafunzo ya usimamizi wa fedha za ujasiriamali kwa wazalishaji na wafanyabiashara wadogo.
Aidha, Serikali itaandaa mpango maalum wa vijana wajasiriamali na wabunifu ili kukuza miradi yao na kuzalisha ajira mpya 350,000.

Dkt. Mwinyi amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kulinda ustawi wa watu wenye mahitaji maalum, wanawake, watoto na wazee, na kukamilisha ujenzi wa nyumba 4,715 katika maeneo ya Chumbuni, Nyamanzi na Kisakasaka Unguja, pamoja na maeneo mengine ya Pemba.

Katika sekta ya usafiri wa anga, Serikali imelenga kuongeza idadi ya abiria wa ndege kutoka 2,140,986 hadi 2,824,011 kwa mwaka, kujenga vituo viwili vya mafuta ya ndege, karakana ya matengenezo ya ndege, na eneo la maegesho kwa mita za mraba 106,000.

Serikali pia itaendeleza barabara ya kurukia ndege Pemba na kujenga jengo jipya la abiria.

Kwa upande wa sekta ya uzalishaji, Serikali itaanzisha sekta ya taifa ya chakula, kukarabati maghala manne na kujenga vihenge (silos) katika Dunga (Unguja) na Chamanangwe (Pemba) vyenye uwezo wa kuhifadhi tani 60,000 kwa wakati mmoja.

Serikali pia itajenga barabara kuu ikiwemo Tunguu–Makunduchi (km 48), Fumba–Kisauni (km 12), Mkoani–Chake Chake (km 43.5), na barabara za utalii Nungwi (km 12), sambamba na uwekaji wa taa za barabarani katika maeneo mbalimbali ya miji.

Baraza la Wawakilishi Zanzibar linatarajiwa kuanza rasmi shughuli zake tarehe 11 Februari 2025.




 
Support : #BegaKwaBegaNaMamaSamia | JAK | CCM Arusha
Copyright © 2011. CCM Dijitali - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Jasper K
Proudly powered by Blogger
Link