HUDUMA ZA FIDIA KWA WAFANYAKAZI SI SUALA LA HIARI-MAJALIWA.
Asema Serikali itaendelea kuhakikisha kunakuwa na ulinzi wa haki na ustawi wa wafanyakazi. Atoa wito kwa waajiri kuzingatia matakwa ya Sh...

Latest Post
July 04, 2025
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema kuwa huduma za fidia kwa wafanyakazi si suala la hiari bali ni haki ya msingi ya mfanyakazi, inayopaswa kulindwa, kuendelezwa na kusimamiwa kwa weledi na uwajibikaji wa hali ya juu.
Amesema kuwa dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuendelea kuhakikisha kuwa maendeleo ya nchi yanakwenda sambamba na ulinzi wa haki na ustawi wa wafanyakazi wake.
Amesema hayo leo (Ijumaa, Julai 05, 2025) alipomwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika ufunguzi wa maadhimisho ya miaka kumi ya Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), katika kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
“Waajiri, wafanyakazi na Serikali tunapaswa kuendelea kushirikiana kwa dhati katika kuhakikisha kuwa kazi inaendelea kwa tija, na wakati huo huo, wafanyakazi wanalindwa dhidi ya madhila yanayotokana na kazi wanazozifanya kila siku.”
Aidha, Mheshimiwa Majaliwa ametoa wito kwa waajiri wote nchini kuhakikisha wanazingatia kikamilifu matakwa ya Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi ikiwa ni pamoja na kujisajili katika Mfuko, kuwasilisha michango kwa wakati, na kutoa taarifa mapema pale wafanyakazi wanapopata madhila yanayotokana na kazi. ” Kutotimiza wajibu huu ni kutotendea haki ustawi wa wafanyakazi na kulemaza ufanisi wa Mfuko.”
Kadhalika, Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa Rais Dkt. Samia wakati wote ametoa miongozo ya kuhakikisha Serikali inaboresha maslahi ya watumishi wa umma, kuboresha mazingira yakufanyia kazi na Utumishi wa umma kuendeshwa kwa kuzingatia misingi ya utawala bora.
Kwa Upande wake Waziri wa Nchi- Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Ridhiwani Kikwete amesema kuwa katika jitihada za Serikali ya Awamu ya Sita kuendelea kuboresha ustawi wa Wafanyakazi walioumia kazini, Serikali imekwishatangaza kwenye Gazeti la Serikali Ongezeko la malipo ya fidia ya kila mwezi kwa wanufaika wa Mfuko wa WCF kwa kati ya asilimia 3 hadi asilimia 31 kutegemea mnufaika alistahili kulipwa kuanzia lini.
Ameongeza kuwa WCF imeishi falsafa ya 4R ya Rais Samia Suluhu Hassan ambapo utendaji mzuri wa mfuko huo umeleta mageuzi chanya ya kiuchumi kwa wafanyakazi na kuleta maelewano kati ya wafanyakazi na waajiri. “Kwa kiasi kikubwa hii imewajengea ari ya kufanya kazi kwa bidii na kuongeza uzalishaji hasa tunapoendelea kujenga uchumi wa viwanda”.
Kwa Upande wake Mkurugenzi Mkuu wa WCF, Dkt. John Mduma ameipongeza Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kupunguza kiwango cha uchangiaji kwa waajiri wa sekta binafsi kutoka asilimia moja wakati Mfuko unaanzishwa hadi asilimia sifuri nukta tano (0.5%) hivi sasa. Hiki kilikuwa ni kilio cha waajiri cha muda mrefu
“Tunaipongeza Serikali pia kwa kuwezesha kupunguza kiwango cha riba ya ucheleweshaji wa michango kwa waajiri kutoka asilimia kumi hadi asilimia mbili kwa mwezi. Hatua hii imeongeza imani ya wawekezaji kwa WCF na Serikali kwa ujumla”.
Naye Mwakilishi mkazi wa Kanda ya Afrika Mashariki wa Shirika la Kazi (ILO) Bi. Caroline Mugalla amesema kuwa katika maadhimisho ya miaka 10 ya WCF, jamii inapaswa kukumbuka kuwa kinga ya jamii sio matumizi yasiyo na tija bali ni uwekezaji katika haki, uzalishaji wenye tija unaolifanya Taifa kuwa thabiti. “Tuendelee kujenga Tanzania ambayo kila mfanyakazi anapata huduma stahiki”
Kwa upande wake Afisa Mtendaji Mkuu wa Chama cha Waajiri Tanzania (ATE) Suzanne Ndomba-Doran amesema kuwa Chama hicho kwa kushirikiana na WCF wamekuwa wakitoa mafunzo na kuhamasisha waajiri kuhusu fidia kwa wafanyakazi.
“Mafunzo haya yameongeza uelewa na kuchangia kupunguza ajali na magonjwa au vifo vinavyotokana nakazi. Tangu mwaka 2016-2024, ATE kwa kushirikiana na WCF tumefanikiwa kutoa mafunzo mara 21 katika Maudhui Kuhusu Sheria ya Fidia kwa Wafanyakaziya mwaka 2008 na kanuni zake, Fidia Mahali pa Kazi, Ajali na Magonjwa.“
Naye, Naibu Katibu Mkuu wa TUCTA Rehema Ludanga ameipongeza WCF kwa kuimarisha matumizi ya mifumo ya teknolojia ya habari na Mawasiliano ambayo imeweza kuongeza ufanisi na kuhudumia wanachama wake.
“Tunaipongeza sana Serikali kwa kuendelea kuipa nguvu WCF sisi TUCTA tunaahi
di kuendelea kushiriana nao ili mafanikio yazidi kwenda mbele na tunaipongeza kwa kufikia miaka 10 ya faida”
Katika hafla hiyo Mheshimiwa Majaliwa alizindua fao la utengamao ambalo litamuwezesha mfanyakazi aliyepata madhara kazini kurejeshwa ofisini na kupatiwa kazi mbadala inayoendana na hali yake.






HUDUMA ZA FIDIA KWA WAFANYAKAZI SI SUALA LA HIARI-MAJALIWA.
Written By CCMdijitali on Friday, July 4, 2025 | July 04, 2025
- Asema Serikali itaendelea kuhakikisha kunakuwa na ulinzi wa haki na ustawi wa wafanyakazi.
- Atoa wito kwa waajiri kuzingatia matakwa ya Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi.
- Aitaka WCF iendelee kushirikiana na wadau katika sekta ya ajira.
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema kuwa huduma za fidia kwa wafanyakazi si suala la hiari bali ni haki ya msingi ya mfanyakazi, inayopaswa kulindwa, kuendelezwa na kusimamiwa kwa weledi na uwajibikaji wa hali ya juu.
Amesema kuwa dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuendelea kuhakikisha kuwa maendeleo ya nchi yanakwenda sambamba na ulinzi wa haki na ustawi wa wafanyakazi wake.
Amesema hayo leo (Ijumaa, Julai 05, 2025) alipomwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika ufunguzi wa maadhimisho ya miaka kumi ya Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), katika kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
“Waajiri, wafanyakazi na Serikali tunapaswa kuendelea kushirikiana kwa dhati katika kuhakikisha kuwa kazi inaendelea kwa tija, na wakati huo huo, wafanyakazi wanalindwa dhidi ya madhila yanayotokana na kazi wanazozifanya kila siku.”
Aidha, Mheshimiwa Majaliwa ametoa wito kwa waajiri wote nchini kuhakikisha wanazingatia kikamilifu matakwa ya Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi ikiwa ni pamoja na kujisajili katika Mfuko, kuwasilisha michango kwa wakati, na kutoa taarifa mapema pale wafanyakazi wanapopata madhila yanayotokana na kazi. ” Kutotimiza wajibu huu ni kutotendea haki ustawi wa wafanyakazi na kulemaza ufanisi wa Mfuko.”
Kadhalika, Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa Rais Dkt. Samia wakati wote ametoa miongozo ya kuhakikisha Serikali inaboresha maslahi ya watumishi wa umma, kuboresha mazingira yakufanyia kazi na Utumishi wa umma kuendeshwa kwa kuzingatia misingi ya utawala bora.
Kwa Upande wake Waziri wa Nchi- Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Ridhiwani Kikwete amesema kuwa katika jitihada za Serikali ya Awamu ya Sita kuendelea kuboresha ustawi wa Wafanyakazi walioumia kazini, Serikali imekwishatangaza kwenye Gazeti la Serikali Ongezeko la malipo ya fidia ya kila mwezi kwa wanufaika wa Mfuko wa WCF kwa kati ya asilimia 3 hadi asilimia 31 kutegemea mnufaika alistahili kulipwa kuanzia lini.
Ameongeza kuwa WCF imeishi falsafa ya 4R ya Rais Samia Suluhu Hassan ambapo utendaji mzuri wa mfuko huo umeleta mageuzi chanya ya kiuchumi kwa wafanyakazi na kuleta maelewano kati ya wafanyakazi na waajiri. “Kwa kiasi kikubwa hii imewajengea ari ya kufanya kazi kwa bidii na kuongeza uzalishaji hasa tunapoendelea kujenga uchumi wa viwanda”.
Kwa Upande wake Mkurugenzi Mkuu wa WCF, Dkt. John Mduma ameipongeza Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kupunguza kiwango cha uchangiaji kwa waajiri wa sekta binafsi kutoka asilimia moja wakati Mfuko unaanzishwa hadi asilimia sifuri nukta tano (0.5%) hivi sasa. Hiki kilikuwa ni kilio cha waajiri cha muda mrefu
“Tunaipongeza Serikali pia kwa kuwezesha kupunguza kiwango cha riba ya ucheleweshaji wa michango kwa waajiri kutoka asilimia kumi hadi asilimia mbili kwa mwezi. Hatua hii imeongeza imani ya wawekezaji kwa WCF na Serikali kwa ujumla”.
Naye Mwakilishi mkazi wa Kanda ya Afrika Mashariki wa Shirika la Kazi (ILO) Bi. Caroline Mugalla amesema kuwa katika maadhimisho ya miaka 10 ya WCF, jamii inapaswa kukumbuka kuwa kinga ya jamii sio matumizi yasiyo na tija bali ni uwekezaji katika haki, uzalishaji wenye tija unaolifanya Taifa kuwa thabiti. “Tuendelee kujenga Tanzania ambayo kila mfanyakazi anapata huduma stahiki”
Kwa upande wake Afisa Mtendaji Mkuu wa Chama cha Waajiri Tanzania (ATE) Suzanne Ndomba-Doran amesema kuwa Chama hicho kwa kushirikiana na WCF wamekuwa wakitoa mafunzo na kuhamasisha waajiri kuhusu fidia kwa wafanyakazi.
“Mafunzo haya yameongeza uelewa na kuchangia kupunguza ajali na magonjwa au vifo vinavyotokana nakazi. Tangu mwaka 2016-2024, ATE kwa kushirikiana na WCF tumefanikiwa kutoa mafunzo mara 21 katika Maudhui Kuhusu Sheria ya Fidia kwa Wafanyakaziya mwaka 2008 na kanuni zake, Fidia Mahali pa Kazi, Ajali na Magonjwa.“
Naye, Naibu Katibu Mkuu wa TUCTA Rehema Ludanga ameipongeza WCF kwa kuimarisha matumizi ya mifumo ya teknolojia ya habari na Mawasiliano ambayo imeweza kuongeza ufanisi na kuhudumia wanachama wake.
“Tunaipongeza sana Serikali kwa kuendelea kuipa nguvu WCF sisi TUCTA tunaahi
di kuendelea kushiriana nao ili mafanikio yazidi kwenda mbele na tunaipongeza kwa kufikia miaka 10 ya faida”
Katika hafla hiyo Mheshimiwa Majaliwa alizindua fao la utengamao ambalo litamuwezesha mfanyakazi aliyepata madhara kazini kurejeshwa ofisini na kupatiwa kazi mbadala inayoendana na hali yake.







Labels:
KITAIFA
July 03, 2025
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema kuwa Serikali itaendelea kuimarisha mazingira ya ufanyaji biashara za huduma za kifedha ili kuvutia uwekezaji wa ndani na nje kwa kuwa maendeleo endelevu ya taifa hayawezi kufikiwa bila ushiriki thabiti wa sekta binafsi.
Amesema kuwa sekta ya fedha ni kichocheo kikubwa katika ukuaji wa Uchumi na ustawi wa wananchi kwa ujumla na ni moja ya sababu inyowezesha maendeleo ya Taifa kwenda kwa kasi.
Amesema hayo leo Alhamisi (Julai 03, 2025) wakati wa uzinduzi wa Benki ya Maendeleo PLC, kuwa Benki kamili ya kibiashara, kwenye ukumbi wa mikutano wa hotel ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam.
“Endeleeni kuimarisha ushirikiano miongoni mwenu, serikali kwa kutambua umuhimu wa sekta ya fedha katika kuchagiza maendeleo, imeendelea kuhamasisha matumizi ya teknolojia bunifu”.
Katika hatua nyingine, Mheshimiwa Majaliwa ametoa wito kwa taasisi zote za kifedha zikiwemo benki kuongeza juhudi katika kutoa elimu ya kifedha kwa wananchi ili kuwajengea uwezo wa kuelewa, kutumia na kunufaika na huduma za kifedha kwa maendeleo yao binafsi na kwa ustawi wa taifa kwa ujumla.
“Tukifanya haya tutapunguza wizi, upotevu wa fedha kiholela kwa sababu kila mmoja atakuwa anaweza kujua fedha yake ataipataje, ataihifadhi wapi na namna ya kutoa lakini pia wapeni wateja wenu namna ya utunzaji wa fedha”
Pia, Mheshimiwa Majaliwa ameongeza kuwa kwa mujibu wa takwimu za utafiti wa Finscope huduma jumuishi za fedha zimeweza kukua kutoka asilimia 65 mwaka 2017 hadi kufikia asilimia 76 mwaka 2023. “kwa mujibu wa utafiti huo, matumizi ya huduma za benki yameongezeka na kufikia asilimia 22 mwaka 2023 kutoka asilimia 17 mwaka 2017”.
Kadhalika, Mheshimiwa ametoa wito kwa taasisi zote za fedha zijenge mifumo rahisi na rafiki kwa makundi yote ya watumiaji wa huduma za kifedha.
Awali, Akizungumza kwa niaba ya Askofu Mkuu wa Kanisa la KKKT na Mkuu wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani Dkt. Alex Malasusa, Muwakilishi wa Askofu Dean Chadiel Lwiza ameishukuru Benki Kuu ya Tanzania (BOT) kwa kuisimamia benki hiyo na kuwa mfano wa benki iliyoanzishwa na wazawa kwa mtaji mdogo hadi kufikia kuwa benki kitaifa. “Tunaiomba benki kuu jicho lenu liwe kali kuliko letu, itazameni hii benki”
Kadhalika, ameongeza kuwa sera nzuri na mazingira mazuri ya uwekezaji katika biashara na usimamizi mzuri za biashara. “Tunaishukuru Serikali ya awamu ya Sita inayoomgizwa na Rais Dkt. Samia kwa kuendelea kuweka mazingira haya mazuri ya ufanyaji biashara”
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Maendeleo Bank PLC Lomnyaki Saitabau amesema kuwa benki hiyo imejiweka katika nafasi bora zaidi ya kuwa benki ya kisasa, shindani na jumuishi kwa Watanzania wote hasa kipindi dunia inapoelekea kwenye zama mpya zenye msukumo wa kiteknolojia, ubunifu, na uwajibikaji wa hali ya juu.
“Kwa kufanya hivyo, tunaunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya sita inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassani, yenye dhamira ya kuwafikia watanzania wengi zaidi nchi nzima kupitia dira ya taifa ya ujumuishaji wa kifedha (financial inclusion) na kuchochea maendeleo ya kiuchumi kupitia sekta binafsi, tutaendelea kushirikiana na Serikali, katika ujenzi wa Uchumi wa nchi”.
Naye, Naibu Waziri wa Fedha Hamad Hassan Chande ameipongeza benki hiyo kwa hatua kuwa iliyofikiwa na benki hiyo katika utoaji huduma kwa watanzania hasa kwa kutumia fursa zilizowekwa na Serikali “Sisi Wizara ya Fedha tumeendelea kuweka mazingira mazuri na rafiki ya ufanyaji wa shughuli za kifedha, sasa wekeni mkakati wa kuifikisha benki hii maeneo mengi zaidi”.




SERIKALI ITAENDELEA KUIMARISHA MAZINGIRA YA UFANYAJI BIASHARA-MAJALIWA
Written By CCMdijitali on Thursday, July 3, 2025 | July 03, 2025
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema kuwa Serikali itaendelea kuimarisha mazingira ya ufanyaji biashara za huduma za kifedha ili kuvutia uwekezaji wa ndani na nje kwa kuwa maendeleo endelevu ya taifa hayawezi kufikiwa bila ushiriki thabiti wa sekta binafsi.
Amesema kuwa sekta ya fedha ni kichocheo kikubwa katika ukuaji wa Uchumi na ustawi wa wananchi kwa ujumla na ni moja ya sababu inyowezesha maendeleo ya Taifa kwenda kwa kasi.
Amesema hayo leo Alhamisi (Julai 03, 2025) wakati wa uzinduzi wa Benki ya Maendeleo PLC, kuwa Benki kamili ya kibiashara, kwenye ukumbi wa mikutano wa hotel ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam.
“Endeleeni kuimarisha ushirikiano miongoni mwenu, serikali kwa kutambua umuhimu wa sekta ya fedha katika kuchagiza maendeleo, imeendelea kuhamasisha matumizi ya teknolojia bunifu”.
Katika hatua nyingine, Mheshimiwa Majaliwa ametoa wito kwa taasisi zote za kifedha zikiwemo benki kuongeza juhudi katika kutoa elimu ya kifedha kwa wananchi ili kuwajengea uwezo wa kuelewa, kutumia na kunufaika na huduma za kifedha kwa maendeleo yao binafsi na kwa ustawi wa taifa kwa ujumla.
“Tukifanya haya tutapunguza wizi, upotevu wa fedha kiholela kwa sababu kila mmoja atakuwa anaweza kujua fedha yake ataipataje, ataihifadhi wapi na namna ya kutoa lakini pia wapeni wateja wenu namna ya utunzaji wa fedha”
Pia, Mheshimiwa Majaliwa ameongeza kuwa kwa mujibu wa takwimu za utafiti wa Finscope huduma jumuishi za fedha zimeweza kukua kutoka asilimia 65 mwaka 2017 hadi kufikia asilimia 76 mwaka 2023. “kwa mujibu wa utafiti huo, matumizi ya huduma za benki yameongezeka na kufikia asilimia 22 mwaka 2023 kutoka asilimia 17 mwaka 2017”.
Kadhalika, Mheshimiwa ametoa wito kwa taasisi zote za fedha zijenge mifumo rahisi na rafiki kwa makundi yote ya watumiaji wa huduma za kifedha.
Awali, Akizungumza kwa niaba ya Askofu Mkuu wa Kanisa la KKKT na Mkuu wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani Dkt. Alex Malasusa, Muwakilishi wa Askofu Dean Chadiel Lwiza ameishukuru Benki Kuu ya Tanzania (BOT) kwa kuisimamia benki hiyo na kuwa mfano wa benki iliyoanzishwa na wazawa kwa mtaji mdogo hadi kufikia kuwa benki kitaifa. “Tunaiomba benki kuu jicho lenu liwe kali kuliko letu, itazameni hii benki”
Kadhalika, ameongeza kuwa sera nzuri na mazingira mazuri ya uwekezaji katika biashara na usimamizi mzuri za biashara. “Tunaishukuru Serikali ya awamu ya Sita inayoomgizwa na Rais Dkt. Samia kwa kuendelea kuweka mazingira haya mazuri ya ufanyaji biashara”
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Maendeleo Bank PLC Lomnyaki Saitabau amesema kuwa benki hiyo imejiweka katika nafasi bora zaidi ya kuwa benki ya kisasa, shindani na jumuishi kwa Watanzania wote hasa kipindi dunia inapoelekea kwenye zama mpya zenye msukumo wa kiteknolojia, ubunifu, na uwajibikaji wa hali ya juu.
“Kwa kufanya hivyo, tunaunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya sita inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassani, yenye dhamira ya kuwafikia watanzania wengi zaidi nchi nzima kupitia dira ya taifa ya ujumuishaji wa kifedha (financial inclusion) na kuchochea maendeleo ya kiuchumi kupitia sekta binafsi, tutaendelea kushirikiana na Serikali, katika ujenzi wa Uchumi wa nchi”.
Naye, Naibu Waziri wa Fedha Hamad Hassan Chande ameipongeza benki hiyo kwa hatua kuwa iliyofikiwa na benki hiyo katika utoaji huduma kwa watanzania hasa kwa kutumia fursa zilizowekwa na Serikali “Sisi Wizara ya Fedha tumeendelea kuweka mazingira mazuri na rafiki ya ufanyaji wa shughuli za kifedha, sasa wekeni mkakati wa kuifikisha benki hii maeneo mengi zaidi”.





Labels:
KITAIFA/ BIASHARA
July 03, 2025
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amesema Serikali ya Tanzania ipo tayari kufanya kazi kwa karibu na jumuiya ya wafanyabiashara wa Uhispania kwa kuwa Tanzania na Uhispania zinaweza kuunda ushirikiano wa kiuchumi wenye nguvu ili kuimarisha diplomasia ya kiuchumi.
Makamu wa Rais amesema hayo wakati akifungua Jukwaa la Biashara la Tanzania na Wafanyabiashara wa Uhispania lililofanyika Jijini Sevilla nchini Uhispania leo tarehe 02 Julai 2025. Amesema Tanzania bado inaitambua Uhispania kama mshirika muhimu katika sekta za kimkakati kama vile nishati mbadala, miundombinu, teknolojia ya kilimo, utalii, viwanda vya rasilimali za baharini na biashara.
Makamu wa Rais amesema Tanzania inatambua sekta ya binafsi kama mshirika mkuu katika juhudi za maendeleo inayoongoza katika mabadiliko ya kijamii na kiuchumi. Amewakaribisha wawekezaji hao kuwekeza Tanzania katika fursa mbalimbali zilizopo.
Aidha Makamu wa Rais ameongeza kwamba Tanzania ni Taifa lenye utulivu wa kisiasa, eneo la kimkakati la kijiografia, maliasili nyingi, idadi kubwa ya vijana pamoja na uchumi unaokua kwa kasi. Ameeleza utekelezaji wa mageuzi unaofanywa na serikali ili kuboresha mazingira ya uwekezaji kwa kutambua nafasi muhimu ya sekta binafsi katika maendeleo endelevu.
Makamu wa Rais amesema chini ya uongozi wa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan, Serikali imeimarisha mifumo ya sheria, miundombinu ya kisasa na kuweka dhamira thabiti ya uwazi na utawala bora. Ameongeza kwamba kwa sasa Tanzania ni kivutio cha uwekezaji katika Afrika Mashariki na Kusini mwa Afrika huku ikitoa fursa katika sekta muhimu kama vile biashara ya kilimo, utalii, nishati, madini, viwanda, uchumi wa bluu, na miundombinu.
Makamu wa Rais amewakaribisha kuwekeza katika maeneo ya kimkakati ikiwemo teknolojia ya nishati safi ya kupikia ili kukabiliana na uharibifu wa mazingira unaotokana na matumizi ya mkaa na kuni. Amesema eneo lingine la uwekezaji ni uvunaji wa rasilimali za uchumi wa bluu katika Bahari ya Hindi pamoja na Maziwa Makuu.
Ametaja maeneo mengine ni pamoja na uvuvi na usindikaji, uchunguzi wa madini, utalii wa pwani na baharini, usafirishaji pamoja na uwekezaji katika kuendeleza maeneo ya pwani ya Tanzania na visiwa ili kunufaika na rasilimali za uchumi wa bluu na uhifadhi wa mazingira.
Katika Mkutano huo Viongozi wa Sekta ya Uwekezaji wamewasilisha maeneo mbalimbali ya kuwekeza nchini Tanzania pamoja na kuonesha mageuzi mbalimbali yaliyofanyika nchini ili kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji. Pia wameeleza fursa za uwepo wa soko la uhakika wa bidhaa kutokana idadi ya watu, eneo la kijiographia la Tanzania ambalo linahudumia nchi mbalimbali, uboreshaji wa miundombinu ya msingi pamoja na maendeleo makubwa katika sekta ya TEHAMA.
Jumla ya Makampuni 31 yameshiriki katika Mkutano huo ambayo yamejikita katika uwekezaji kwenye sekta mbalimbali ikiwemo chakula na kilimo, ujenzi wa miundombinu, viwanda, sekta maji, sekta ya madini, nishati, TEHAMA, utalii pamoja na sekta ya fedha.
Mkutano huo umehudhuriwa na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Fedha na Mipango Zanzibar Aboud Mwinyi, Balozi wa Tanzania nchini Hispania mwenye Makazi yake nchini Ufaransa Mhe. Ali Mwadini, Mkurugenzi wa Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalumu ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA) Gilead Teri, Meneja wa Uwekezaji wa Mamlaka ya Kukuza Uwekezaji Zanzibar (ZIPA) Omary Omary, Mkurugenzi Mtendaji wa Sekta Binafsi Raphael Maganga, Katibu wa Baraza la Biashara Tanzania Dr. Godwill Wanga pamoja na Kamishna wa Fedha za Nje Wizara ya Fedha Rished Bade.
Imetolewa na
Ofisi ya Makamu wa Rais
02 Julai 2025
Sevilla – Uhispania.








TANZANIA INAITAMBUA UHISPANIA KAMA MSHIRIKA MUHIMU - DKT MPANGO
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amesema Serikali ya Tanzania ipo tayari kufanya kazi kwa karibu na jumuiya ya wafanyabiashara wa Uhispania kwa kuwa Tanzania na Uhispania zinaweza kuunda ushirikiano wa kiuchumi wenye nguvu ili kuimarisha diplomasia ya kiuchumi.
Makamu wa Rais amesema hayo wakati akifungua Jukwaa la Biashara la Tanzania na Wafanyabiashara wa Uhispania lililofanyika Jijini Sevilla nchini Uhispania leo tarehe 02 Julai 2025. Amesema Tanzania bado inaitambua Uhispania kama mshirika muhimu katika sekta za kimkakati kama vile nishati mbadala, miundombinu, teknolojia ya kilimo, utalii, viwanda vya rasilimali za baharini na biashara.
Makamu wa Rais amesema Tanzania inatambua sekta ya binafsi kama mshirika mkuu katika juhudi za maendeleo inayoongoza katika mabadiliko ya kijamii na kiuchumi. Amewakaribisha wawekezaji hao kuwekeza Tanzania katika fursa mbalimbali zilizopo.
Aidha Makamu wa Rais ameongeza kwamba Tanzania ni Taifa lenye utulivu wa kisiasa, eneo la kimkakati la kijiografia, maliasili nyingi, idadi kubwa ya vijana pamoja na uchumi unaokua kwa kasi. Ameeleza utekelezaji wa mageuzi unaofanywa na serikali ili kuboresha mazingira ya uwekezaji kwa kutambua nafasi muhimu ya sekta binafsi katika maendeleo endelevu.
Makamu wa Rais amesema chini ya uongozi wa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan, Serikali imeimarisha mifumo ya sheria, miundombinu ya kisasa na kuweka dhamira thabiti ya uwazi na utawala bora. Ameongeza kwamba kwa sasa Tanzania ni kivutio cha uwekezaji katika Afrika Mashariki na Kusini mwa Afrika huku ikitoa fursa katika sekta muhimu kama vile biashara ya kilimo, utalii, nishati, madini, viwanda, uchumi wa bluu, na miundombinu.
Makamu wa Rais amewakaribisha kuwekeza katika maeneo ya kimkakati ikiwemo teknolojia ya nishati safi ya kupikia ili kukabiliana na uharibifu wa mazingira unaotokana na matumizi ya mkaa na kuni. Amesema eneo lingine la uwekezaji ni uvunaji wa rasilimali za uchumi wa bluu katika Bahari ya Hindi pamoja na Maziwa Makuu.
Ametaja maeneo mengine ni pamoja na uvuvi na usindikaji, uchunguzi wa madini, utalii wa pwani na baharini, usafirishaji pamoja na uwekezaji katika kuendeleza maeneo ya pwani ya Tanzania na visiwa ili kunufaika na rasilimali za uchumi wa bluu na uhifadhi wa mazingira.
Katika Mkutano huo Viongozi wa Sekta ya Uwekezaji wamewasilisha maeneo mbalimbali ya kuwekeza nchini Tanzania pamoja na kuonesha mageuzi mbalimbali yaliyofanyika nchini ili kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji. Pia wameeleza fursa za uwepo wa soko la uhakika wa bidhaa kutokana idadi ya watu, eneo la kijiographia la Tanzania ambalo linahudumia nchi mbalimbali, uboreshaji wa miundombinu ya msingi pamoja na maendeleo makubwa katika sekta ya TEHAMA.
Jumla ya Makampuni 31 yameshiriki katika Mkutano huo ambayo yamejikita katika uwekezaji kwenye sekta mbalimbali ikiwemo chakula na kilimo, ujenzi wa miundombinu, viwanda, sekta maji, sekta ya madini, nishati, TEHAMA, utalii pamoja na sekta ya fedha.
Mkutano huo umehudhuriwa na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Fedha na Mipango Zanzibar Aboud Mwinyi, Balozi wa Tanzania nchini Hispania mwenye Makazi yake nchini Ufaransa Mhe. Ali Mwadini, Mkurugenzi wa Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalumu ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA) Gilead Teri, Meneja wa Uwekezaji wa Mamlaka ya Kukuza Uwekezaji Zanzibar (ZIPA) Omary Omary, Mkurugenzi Mtendaji wa Sekta Binafsi Raphael Maganga, Katibu wa Baraza la Biashara Tanzania Dr. Godwill Wanga pamoja na Kamishna wa Fedha za Nje Wizara ya Fedha Rished Bade.
Imetolewa na
Ofisi ya Makamu wa Rais
02 Julai 2025
Sevilla – Uhispania.









Labels:
KIMATAIFA
June 30, 2025
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango ametoa wito wa kufanyika maboresho ya mfumo wa fedha na ufadhili wa maendeleo duniani ili kutoa nafuu ya riba, kuwa endelevu, unaotabirika na unaozingatia usawa na vipaumbele vya mataifa yanayoendelea.
Makamu wa Rais ametoa wito huo wakati akihutubia Mkutano wa Nne wa Kimataifa kuhusu Ufadhili wa Maendeleo (FfD4) unaofanyika Jijini Sevilla nchini Hispania. Amesisitiza umuhimu wa mbinu za kibunifu katika ufadhili ikiwemo kubadili madeni ya kifedha kwenda katika utekelezaji wa miradi mbalimbali kama vile uhifadhi wa mazingira.
Vilevile Makamu wa Rais amesema taratibu za upimaji wa uwezo wa serikali kifedha katika ulipaji madeni unapaswa kupitiwa upya ili kuongeza uwazi na kuwa wa haki. Ameongeza kwamba Mkutano huo unapaswa kutoa ufumbuzi wa namna ya kupunguza gharama za ukopaji na kuongeza fursa za mikopo nafuu na ya muda mrefu.
Makamu wa Rais amesema kutokana na biashara kuwa nguzo ya kiuchumi ni vema mataifa kuwezeshwa katika uzalishaji na uongezawaji thamani wa bidhaa ili kufikia viwango vya kimataifa. Amesisitiza uwepo wa usawa na haki katika taratibu na sheria za kibiashara za kimataifa ikiwemo masuala ya ushuru wa forodha na ukomo wa mauzo kwa mataifa yanayoendelea.
Aidha Makamu wa Rais amesema unahitajika ushirikiano baina ya Mataifa yaliyoendelea na yanayoendelea katika kuharakisha maendeleo ya sayansi, teknolojia na takwimu ili kuweza kusaidia katika utungaji sera na utekelezaji kwa kuzingatia tafiti na takwimu sahihi.
Halikadhalika, Makamu wa Rais amesisitiza umuhimu wa Mataifa tajiri kushirikiana na nchi zinazoendelea katika kupunguza viatarishi kwenye uwekezaji na ufadhili wa miradi mikubwa ya kimkakati ya maendeleo.
Kuhusu Mazingira, Makamu wa Rais ametoa wito wa kutoa kipaumbele katika ufadhili wa usimamizi na urejerezaji wa bioanuai pamoja na kuongeza wigo wa ufadhili katika miradi ya kujenga uhimilivu na miradi ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi. Amesisitiza umuhimu wa kuanza kazi kwa mfuko wa mazingira wa kukabiliana na hasara na uharibifu unaosababishwa na mabadiliko ya tabianchi (Loss and Demage Fund).
Makamu wa Rais amesema kufikia mwaka 2024, Tanzania imefikia asilimia 60 ya utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs) kwa kupiga hatua zaidi katika lengo namba 2 hadi namba 7 hususani katika maeneo ya afya, utoshelevu wa chakula, elimu, usawa wa kijinsia, upatikanaji wa maji safi na salama pamoja na upatikanaji wa nishati.
Ameongeza kwamba ili kuendeleza mafanikio hayo unahitajika ushirikiano na ufadhili wa gharama nafuu katika kuongezea mapato ya ndani ya nchi.
Mkutano wa Nne wa Kimataifa wa kuhusu Ufadhili wa Maendeleo unalenga kutafuta ufumbuzi wa changamoto zinazoikabili dunia katika kugharamia utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs), kujadili njia za kurekebisha mfumo wa fedha wa kimataifa ili kuwa jumuishi, wenye usawa na unaozingatia mahitaji ya nchi zinazoendelea.
Malengo mengine ya Mkutano huo ni pamoja na kupendekeza mbinu bora za kupunguza na kushughulikia mzigo wa madeni kwa nchi maskini na zenye kipato cha kati pamoja na kujenga mifumo madhubuti ya kifedha inayoweza kukabili athari za majanga ya kiuchumi, kijamii na kimazingira.
Mkutano kuhusu Ufadhili wa Maendeleo ulianzishwa rasmi mwaka 2002 kupitia Mkutano wa kwanza uliofanyika Monterrey, Mexico na kupelekea kuundwa kwa msingi wa ushirikiano wa kimataifa katika kufadhili maendeleo. Mkutano wa Pili ulifanyika mjini Doha, Qatar mwaka 2008 ambao ulianzisha Azimio la Doha kusisitiza haja ya kuimarisha mshikamano wa kimataifa katika kukabiliana na athari za mtikisiko wa kifedha duniani.
Mkutano wa Tatu ulifanyika Addis Ababa, Ethiopia, mwaka 2015, na matokeo yake yalikuwa ni Addis Ababa Action Agenda (AAAA), ambayo ilijikita katika uhamasishaji wa vyanzo vya ndani vya mapato, ushirikiano wa kimataifa, uwekezaji wa sekta binafsi, pamoja na kushughulikia changamoto za madeni na usawa wa kijinsia.
Mkutano huu wa Nne ambao umepitisha Azimio la Sevilla unalenga kuchambua maendeleo yaliyopatikana tangu Addis Ababa na kujadili njia bora za kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu katika muktadha wa changamoto mpya kama vile mabadiliko ya tabianchi, migogoro ya kimataifa na athari za kiuchumi za janga la Uviko -19.
Imetolewa na
Ofisi ya Makamu wa Rais
30 Juni 2025
Sevilla - Hispania.



Dkt. Philip Mpango ametoa wito wa kufanyika maboresho ya mfumo wa fedha na ufadhili wa maendeleo duniani.
Written By CCMdijitali on Monday, June 30, 2025 | June 30, 2025
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango ametoa wito wa kufanyika maboresho ya mfumo wa fedha na ufadhili wa maendeleo duniani ili kutoa nafuu ya riba, kuwa endelevu, unaotabirika na unaozingatia usawa na vipaumbele vya mataifa yanayoendelea.
Makamu wa Rais ametoa wito huo wakati akihutubia Mkutano wa Nne wa Kimataifa kuhusu Ufadhili wa Maendeleo (FfD4) unaofanyika Jijini Sevilla nchini Hispania. Amesisitiza umuhimu wa mbinu za kibunifu katika ufadhili ikiwemo kubadili madeni ya kifedha kwenda katika utekelezaji wa miradi mbalimbali kama vile uhifadhi wa mazingira.
Vilevile Makamu wa Rais amesema taratibu za upimaji wa uwezo wa serikali kifedha katika ulipaji madeni unapaswa kupitiwa upya ili kuongeza uwazi na kuwa wa haki. Ameongeza kwamba Mkutano huo unapaswa kutoa ufumbuzi wa namna ya kupunguza gharama za ukopaji na kuongeza fursa za mikopo nafuu na ya muda mrefu.
Makamu wa Rais amesema kutokana na biashara kuwa nguzo ya kiuchumi ni vema mataifa kuwezeshwa katika uzalishaji na uongezawaji thamani wa bidhaa ili kufikia viwango vya kimataifa. Amesisitiza uwepo wa usawa na haki katika taratibu na sheria za kibiashara za kimataifa ikiwemo masuala ya ushuru wa forodha na ukomo wa mauzo kwa mataifa yanayoendelea.
Aidha Makamu wa Rais amesema unahitajika ushirikiano baina ya Mataifa yaliyoendelea na yanayoendelea katika kuharakisha maendeleo ya sayansi, teknolojia na takwimu ili kuweza kusaidia katika utungaji sera na utekelezaji kwa kuzingatia tafiti na takwimu sahihi.
Halikadhalika, Makamu wa Rais amesisitiza umuhimu wa Mataifa tajiri kushirikiana na nchi zinazoendelea katika kupunguza viatarishi kwenye uwekezaji na ufadhili wa miradi mikubwa ya kimkakati ya maendeleo.
Kuhusu Mazingira, Makamu wa Rais ametoa wito wa kutoa kipaumbele katika ufadhili wa usimamizi na urejerezaji wa bioanuai pamoja na kuongeza wigo wa ufadhili katika miradi ya kujenga uhimilivu na miradi ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi. Amesisitiza umuhimu wa kuanza kazi kwa mfuko wa mazingira wa kukabiliana na hasara na uharibifu unaosababishwa na mabadiliko ya tabianchi (Loss and Demage Fund).
Makamu wa Rais amesema kufikia mwaka 2024, Tanzania imefikia asilimia 60 ya utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs) kwa kupiga hatua zaidi katika lengo namba 2 hadi namba 7 hususani katika maeneo ya afya, utoshelevu wa chakula, elimu, usawa wa kijinsia, upatikanaji wa maji safi na salama pamoja na upatikanaji wa nishati.
Ameongeza kwamba ili kuendeleza mafanikio hayo unahitajika ushirikiano na ufadhili wa gharama nafuu katika kuongezea mapato ya ndani ya nchi.
Mkutano wa Nne wa Kimataifa wa kuhusu Ufadhili wa Maendeleo unalenga kutafuta ufumbuzi wa changamoto zinazoikabili dunia katika kugharamia utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs), kujadili njia za kurekebisha mfumo wa fedha wa kimataifa ili kuwa jumuishi, wenye usawa na unaozingatia mahitaji ya nchi zinazoendelea.
Malengo mengine ya Mkutano huo ni pamoja na kupendekeza mbinu bora za kupunguza na kushughulikia mzigo wa madeni kwa nchi maskini na zenye kipato cha kati pamoja na kujenga mifumo madhubuti ya kifedha inayoweza kukabili athari za majanga ya kiuchumi, kijamii na kimazingira.
Mkutano kuhusu Ufadhili wa Maendeleo ulianzishwa rasmi mwaka 2002 kupitia Mkutano wa kwanza uliofanyika Monterrey, Mexico na kupelekea kuundwa kwa msingi wa ushirikiano wa kimataifa katika kufadhili maendeleo. Mkutano wa Pili ulifanyika mjini Doha, Qatar mwaka 2008 ambao ulianzisha Azimio la Doha kusisitiza haja ya kuimarisha mshikamano wa kimataifa katika kukabiliana na athari za mtikisiko wa kifedha duniani.
Mkutano wa Tatu ulifanyika Addis Ababa, Ethiopia, mwaka 2015, na matokeo yake yalikuwa ni Addis Ababa Action Agenda (AAAA), ambayo ilijikita katika uhamasishaji wa vyanzo vya ndani vya mapato, ushirikiano wa kimataifa, uwekezaji wa sekta binafsi, pamoja na kushughulikia changamoto za madeni na usawa wa kijinsia.
Mkutano huu wa Nne ambao umepitisha Azimio la Sevilla unalenga kuchambua maendeleo yaliyopatikana tangu Addis Ababa na kujadili njia bora za kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu katika muktadha wa changamoto mpya kama vile mabadiliko ya tabianchi, migogoro ya kimataifa na athari za kiuchumi za janga la Uviko -19.
Imetolewa na
Ofisi ya Makamu wa Rais
30 Juni 2025
Sevilla - Hispania.




Labels:
KIMATAIFA
June 29, 2025
Dar es Salaam
Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) mkoa wa Dar es Salaam wamefanya ukaguzi wa ujenzi na matengenezo ya barabara katika mkoa huo unaolenga kuhakikisha miradi inakamilika kwa viwango na kwa wakati.
Meneja wa TARURA mkoa wa Dar es Salaam, Mhandisi Geofrey Mkinga amesema kuwa, wametembelea wilaya ya Temeke ambapo walikagua barabara mbalimbali ikiwemo barabara ya kwa Diwani na zile zinazotekelezwa chini ya mradi wa Uendelezaji Jiji la Dar es Salaam awamu ya pili (DMDP).
“Tumeona maendeleo mazuri kwenye utekelezaji, Mkandarasi yupo kazini na tunatarajia kujenga zaidi ya Km 7.2 katika eneo la makazi na biashara, ambapo magari makubwa na malori hupita mara kwa mara. Barabara zinajengwa kwa kiwango cha zege ili kukidhi mahitaji ya shughuli za kiuchumi zinazofanyika", amesema Mkinga.
Pia alitembelea barabara ya Yombo yenye urefu wa Km 1.6, ambapo ujenzi unaendelea kwa kiwango cha zege katika maeneo ya wazi pamoja na kipande cha mita 600 kinachojengwa kwa kushirikiana na Manispaa ya Temeke.
“Ninamshukuru Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke kwa kuwezesha upatikanaji wa fedha za matengenezo. Hii imerahisisha utekelezaji wa barabara ya Yombo na ile ya Dkt. Omar. Kipande cha mita 600 kinachojengwa chote kwa zege”, ameongeza.
Meneja Mkinga pia alitembelea barabara ya Tuangoma–Masaki yenye urefu wa Km 3.9, eneo ambalo awali lilikuwa na changamoto kubwa ya mvua na udongo laini uliokuwa ukisababisha kukatika kwa mawasiliano.
“Hili ni eneo la mchanga, mvua ikinyesha tu hakuna mawasiliano kabisa. Mkandarasi anayetekeleza mradi huu anafanya kazi chini ya mkataba wenye thamani ya Shilingi bilioni 27. Mradi unahusisha pia ujenzi wa vivuko vya Chaulembo ambavyo vimepangwa kwa mujibu wa maelekezo ya viongozi wa mkoa”, amesema.
Akiwa eneo la Chamaruba, ameeleza namna mvua kubwa za Aprili na Mei zilivyoharibu miundombinu na kufunga kabisa mawasiliano kati ya pande mbili za mtaa huo. Hata hivyo, kwa ushirikiano na viongozi wa Serikali ya Mtaa na Serikali Kuu, fedha za dharura zilitolewa ili kujenga makalavati matano na kurudisha mawasiliano.
Kwa upande wao, wananchi wa maeneo hayo walitoa shukrani zao kwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan kwa kufanikisha miradi hiyo ambayo imeleta unafuu mkubwa kwa wananchi.
“Awali ilikuwa tunapata shida kuwavusha watoto kwenda shule, hadi mzazi umpeleke mtoto na umrudishe. Wakati mwingine wagonjwa walihitaji kubebwa hadi upande wa pili. Lakini sasa hivi, tuna daraja, tuna barabara, tuna amani, tunaishukuru serikali", amesema mmoja wa wakazi wa eneo la Chamaruba.






TARURA YAENDELEA NA UKAGUZI WA BARABARA TEMEKE, YAELEZA MAFANIKIO YA MIRADI YA DMDP II
Written By CCMdijitali on Sunday, June 29, 2025 | June 29, 2025
Dar es Salaam
Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) mkoa wa Dar es Salaam wamefanya ukaguzi wa ujenzi na matengenezo ya barabara katika mkoa huo unaolenga kuhakikisha miradi inakamilika kwa viwango na kwa wakati.
Meneja wa TARURA mkoa wa Dar es Salaam, Mhandisi Geofrey Mkinga amesema kuwa, wametembelea wilaya ya Temeke ambapo walikagua barabara mbalimbali ikiwemo barabara ya kwa Diwani na zile zinazotekelezwa chini ya mradi wa Uendelezaji Jiji la Dar es Salaam awamu ya pili (DMDP).
“Tumeona maendeleo mazuri kwenye utekelezaji, Mkandarasi yupo kazini na tunatarajia kujenga zaidi ya Km 7.2 katika eneo la makazi na biashara, ambapo magari makubwa na malori hupita mara kwa mara. Barabara zinajengwa kwa kiwango cha zege ili kukidhi mahitaji ya shughuli za kiuchumi zinazofanyika", amesema Mkinga.
Pia alitembelea barabara ya Yombo yenye urefu wa Km 1.6, ambapo ujenzi unaendelea kwa kiwango cha zege katika maeneo ya wazi pamoja na kipande cha mita 600 kinachojengwa kwa kushirikiana na Manispaa ya Temeke.
“Ninamshukuru Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke kwa kuwezesha upatikanaji wa fedha za matengenezo. Hii imerahisisha utekelezaji wa barabara ya Yombo na ile ya Dkt. Omar. Kipande cha mita 600 kinachojengwa chote kwa zege”, ameongeza.
Meneja Mkinga pia alitembelea barabara ya Tuangoma–Masaki yenye urefu wa Km 3.9, eneo ambalo awali lilikuwa na changamoto kubwa ya mvua na udongo laini uliokuwa ukisababisha kukatika kwa mawasiliano.
“Hili ni eneo la mchanga, mvua ikinyesha tu hakuna mawasiliano kabisa. Mkandarasi anayetekeleza mradi huu anafanya kazi chini ya mkataba wenye thamani ya Shilingi bilioni 27. Mradi unahusisha pia ujenzi wa vivuko vya Chaulembo ambavyo vimepangwa kwa mujibu wa maelekezo ya viongozi wa mkoa”, amesema.
Akiwa eneo la Chamaruba, ameeleza namna mvua kubwa za Aprili na Mei zilivyoharibu miundombinu na kufunga kabisa mawasiliano kati ya pande mbili za mtaa huo. Hata hivyo, kwa ushirikiano na viongozi wa Serikali ya Mtaa na Serikali Kuu, fedha za dharura zilitolewa ili kujenga makalavati matano na kurudisha mawasiliano.
Kwa upande wao, wananchi wa maeneo hayo walitoa shukrani zao kwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan kwa kufanikisha miradi hiyo ambayo imeleta unafuu mkubwa kwa wananchi.
“Awali ilikuwa tunapata shida kuwavusha watoto kwenda shule, hadi mzazi umpeleke mtoto na umrudishe. Wakati mwingine wagonjwa walihitaji kubebwa hadi upande wa pili. Lakini sasa hivi, tuna daraja, tuna barabara, tuna amani, tunaishukuru serikali", amesema mmoja wa wakazi wa eneo la Chamaruba.







Labels:
MKOANI
June 29, 2025
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema kuwa Serikali itaendelea kuweka mkazo katika kulinda na kudumisha amani nchini ili kuhamasisha maendeleo na kuziba mianya ya kuibuka kwa migogoro miongoni mwa wanajamii.
Ametoa kauli hiyo leo (Jumapili Juni 29, 2025) wakati alipomwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kufunga kongamano la Afrika Mashariki la Amani lililoandaliwa na The Islamic Foundation, katika viwanja vya shule ya msingi Mirongo jijini Mwanza
“Nataka niwaambie bila amani hatuwezi kupata mafanikio yoyote, kupitia kongamano hili mmepata nafasi ya kujadili kuhusu tunu hii ya amani, ambayo wakati wote tumeshuhudia viongozi wa dini mkiwa kwenye majukwaa yenu mkihimiza amani miongoni mwa wanajamii, tuishike tunu hii”.
Kadhalika, amewataka Watanzania kuangalia kwa upana wake suala la mmomonyoko wa maadili katika jamii hasa kwa vijana. “Ni muhimu sana suala hili mkaliweka kama agenda katika mikutano na vikao vyenu, kila kiongozi wa dini anapozungumza, suala la maadili na mmomonyoko wa liwe ni ajenga ya kudumu”
Amesema kuwa mabadiliko ya teknolojia na kuiga tamaduni za mataifa ya nje imekuwa miongoni mwa chanzo kikubwa cha mmomonyoko wa maadili. “Siku hizi vijana kuwaita wazee kwa majina yasiyo na heshima ni kitu cha kawaida, viongozi ndio wenye jukumu la kusimamia eneo la maadili, mkifanya hivyo tupata vijana wenye maadili mema”
Pia Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa falsafa ya 4R ya Resilience (Ustahimilivu), Reconciliation (Maridhiano) and Reforms (Mageuzi), Rebulding (Kujenga upya) iliyoasisiwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imejikita katika misingi imara ya kulinda amani. “Falsafa hii imeifanya Tanzania kuwa tulivu na salama”
Wakati huo huo Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa jamii inapaswa kuona umuhimu wa kukuza utamaduni wa majadiliano na maridhiano katika kushughulikia tofauti zilizopo mingoni mwa jamii.
“Tunapaswa kujenga jamii inayoheshimu maoni tofauti, na kuhimiza mijadala kwenye majukwaa na kwa nafasi hii viongozi, taasisi na wanajamii mnapaswa kuwa daraja la maridhiano badala ya kuwa vyanzo vya migawanyiko”
Naye Mwenyekiti wa Islamic Foundation Aref Nahdi amesema kuwa taasisi zao zitaendelea kushirikiana na Serikali katika kuijenga Tanzania yenye haki, Amani, usawa, maendeleo na heshima kwa wote.
Aidha, amesema kuwa taasisi hizo zitaendelea kukemea vikali kauli zenye viashiria vya uvunjifu wa amani, upendo na kuvunja heshima za viongozi wa kitaifa. “Kwa kufanya hivyo inakuwa ni sehemu ya mafundisho ya dini”.





TUTAENDELEA KUILINDA NA KUIDUMISHA AMANI NCHINI-MAJALIWA
- Asema falsafa ya 4R ya Rais Dkt. Samia imekuwa msingi imara wa kulinda amani.
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema kuwa Serikali itaendelea kuweka mkazo katika kulinda na kudumisha amani nchini ili kuhamasisha maendeleo na kuziba mianya ya kuibuka kwa migogoro miongoni mwa wanajamii.
Ametoa kauli hiyo leo (Jumapili Juni 29, 2025) wakati alipomwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kufunga kongamano la Afrika Mashariki la Amani lililoandaliwa na The Islamic Foundation, katika viwanja vya shule ya msingi Mirongo jijini Mwanza
“Nataka niwaambie bila amani hatuwezi kupata mafanikio yoyote, kupitia kongamano hili mmepata nafasi ya kujadili kuhusu tunu hii ya amani, ambayo wakati wote tumeshuhudia viongozi wa dini mkiwa kwenye majukwaa yenu mkihimiza amani miongoni mwa wanajamii, tuishike tunu hii”.
Kadhalika, amewataka Watanzania kuangalia kwa upana wake suala la mmomonyoko wa maadili katika jamii hasa kwa vijana. “Ni muhimu sana suala hili mkaliweka kama agenda katika mikutano na vikao vyenu, kila kiongozi wa dini anapozungumza, suala la maadili na mmomonyoko wa liwe ni ajenga ya kudumu”
Amesema kuwa mabadiliko ya teknolojia na kuiga tamaduni za mataifa ya nje imekuwa miongoni mwa chanzo kikubwa cha mmomonyoko wa maadili. “Siku hizi vijana kuwaita wazee kwa majina yasiyo na heshima ni kitu cha kawaida, viongozi ndio wenye jukumu la kusimamia eneo la maadili, mkifanya hivyo tupata vijana wenye maadili mema”
Pia Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa falsafa ya 4R ya Resilience (Ustahimilivu), Reconciliation (Maridhiano) and Reforms (Mageuzi), Rebulding (Kujenga upya) iliyoasisiwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imejikita katika misingi imara ya kulinda amani. “Falsafa hii imeifanya Tanzania kuwa tulivu na salama”
Wakati huo huo Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa jamii inapaswa kuona umuhimu wa kukuza utamaduni wa majadiliano na maridhiano katika kushughulikia tofauti zilizopo mingoni mwa jamii.
“Tunapaswa kujenga jamii inayoheshimu maoni tofauti, na kuhimiza mijadala kwenye majukwaa na kwa nafasi hii viongozi, taasisi na wanajamii mnapaswa kuwa daraja la maridhiano badala ya kuwa vyanzo vya migawanyiko”
Naye Mwenyekiti wa Islamic Foundation Aref Nahdi amesema kuwa taasisi zao zitaendelea kushirikiana na Serikali katika kuijenga Tanzania yenye haki, Amani, usawa, maendeleo na heshima kwa wote.
Aidha, amesema kuwa taasisi hizo zitaendelea kukemea vikali kauli zenye viashiria vya uvunjifu wa amani, upendo na kuvunja heshima za viongozi wa kitaifa. “Kwa kufanya hivyo inakuwa ni sehemu ya mafundisho ya dini”.






Labels:
KITAIFA
June 23, 2025
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa ameziagiza taasisi za Serikali ambazo hazijajiunga na mfumo wa kielektroni utakaowezesha mifumo ya Serikali kuwasiliana (GovESB) kujiunga na mfumo huo ifikapo Julai 30 mwaka huu ili kuendana na mabadiliko ya teknolojia katika kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa wananchi.
Ametoa maagizo hayo leo Jumatatu (Juni 23, 2025) alipomwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Utumishi wa Umma yaliyofanyika katika viwanja vya Chinangali Park Jijini Dodoma.
“Taasisi zote za umma ambazo hazijajiunga na mfumo huu mwisho ni Julai 30 mwaka huu, wote muwe mmeshaingia pale GovESB, huu ni msisitizo ambao ulitolewa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia pindi eGA watakapokamilisha kila taasisi ipeleke mfumo wake, idadi ya taasisi zilizounganishwa ni chache, hakuna gharama na hutakiwi kupanga bajeti”
Ameongeza kuwa mfumo huo unafaida kubwa katika utumishi wa umma kwani utasaidia kurahisisha utendaji, kutoa taarifa kwa wakati, kuondoa makosa ya kibinadamu katika kuwahudumia wananchi pamoja na kuwabana wala rushwa. “Nimefurahi kujulishwa kwamba jumla ya mifumo 223 kutoka kwenye taasisi 185 imeunganishwa na kusomana”.
Aidha, Mheshimiwa Majaliwa ametoa wito kwa taasisi zote za umma zenye mifumo na zinazoendelea kubuni mifumo zihakikishe mifumo hiyo inasomana na inaweza kubadilishana taarifa kupitia mfumo huo wa GovESB ikiwa ni njia mojawapo ya kuendelea kuboresha huduma za Serikali.
Kadhalika Mheshimiwa Majaliwa ameitaka Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) kuhakikisha mifumo iliyounganishwa inaendelea kubadilishana taarifa. “Lakini pia kila anayeingia jiridhishe kuwa anaweza kuwasiliana na wengine wote waliomo ndani, mmenieleza na mmesema kwamba ndivyo ilivyo, nasisitiza kwamba hakikisheni hiyo mifumo inasomana na inabadilishana taarifa”
Katika hatua nyingine, Mheshimiwa Waziri Mkuu ametoa wito kwa watumishi wa umma kuzingatia miiko na maadili ya utumishi katika utekelezaji wa majukumu yao kwa kuzingitia Sera na Sheria kwa manufaa na maendeleo ya Taifa letu. “Nitumie nafasi hii kuwapongeza sana watumishi wote wa umma nchini, niwahikishie kuwa serikali ya awamu ya sita iko pamoja nanyi. “Fanyeni hivyo kwa ajili ya manufaa na maendeleo ya Taifa letu”.
Kwa upande wake, Waziri wa Nchi-Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora George Simbachawene amesema Tanzania imetambulika kimataifa ambapo mwaka 2022 Benki ya Dunia ilifanya utafiti kuhusu ukomavu wa matumizi ya teknolojia duniani katika utoaji wa huduma za Serikali na ushirikishwaji wa wananchi.
Amefafanua kuwa ripoti ya utafiti huo iliyotolewa Machi, 2023 ilibanisha kuwa Tanzania imefanikiwa kupanda daraja kutoka kundi B hadi kundi A na kushika nafasi ya 26 duniani, nafasi ya 2 Afrika na nafasi ya kwanza katika nchi za Afrika Mashariki.
Katika tukio hilo, Mheshimiwa Majaliwa alizindua mifumo miwili ambayo ni Mfumo wa kielektroni unaowezesha mifumo ya Serikali kuwasiliana na kubadilishana taarifa ujulikanao kama Government Enterprises Service Bus (GovESB) Pamoja na Mfumo wa e-Wekeza unaomuwezesha Mtumishi wa Umma kuwekeza katika Mfuko wa Faida (Faida Fund).
Siku ya Utumishi wa Umma husherehekewa Juni 23 kila mwaka na nchi wanachama wa Umoja wa Afrika kwa lengo la kutambua mchango wa Watumishi wa Umma katika maendeleo ya nchi zao na Bara la Afrika kwa ujumla.






MAJALIWA AZIPA WIKI TANO TAASISI ZA SERIKALI KUJIUNGA NA MFUMO UNAOWEZESHA SERIKALI KUWASILIANA
Written By CCMdijitali on Monday, June 23, 2025 | June 23, 2025
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa ameziagiza taasisi za Serikali ambazo hazijajiunga na mfumo wa kielektroni utakaowezesha mifumo ya Serikali kuwasiliana (GovESB) kujiunga na mfumo huo ifikapo Julai 30 mwaka huu ili kuendana na mabadiliko ya teknolojia katika kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa wananchi.
Ametoa maagizo hayo leo Jumatatu (Juni 23, 2025) alipomwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Utumishi wa Umma yaliyofanyika katika viwanja vya Chinangali Park Jijini Dodoma.
“Taasisi zote za umma ambazo hazijajiunga na mfumo huu mwisho ni Julai 30 mwaka huu, wote muwe mmeshaingia pale GovESB, huu ni msisitizo ambao ulitolewa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia pindi eGA watakapokamilisha kila taasisi ipeleke mfumo wake, idadi ya taasisi zilizounganishwa ni chache, hakuna gharama na hutakiwi kupanga bajeti”
Ameongeza kuwa mfumo huo unafaida kubwa katika utumishi wa umma kwani utasaidia kurahisisha utendaji, kutoa taarifa kwa wakati, kuondoa makosa ya kibinadamu katika kuwahudumia wananchi pamoja na kuwabana wala rushwa. “Nimefurahi kujulishwa kwamba jumla ya mifumo 223 kutoka kwenye taasisi 185 imeunganishwa na kusomana”.
Aidha, Mheshimiwa Majaliwa ametoa wito kwa taasisi zote za umma zenye mifumo na zinazoendelea kubuni mifumo zihakikishe mifumo hiyo inasomana na inaweza kubadilishana taarifa kupitia mfumo huo wa GovESB ikiwa ni njia mojawapo ya kuendelea kuboresha huduma za Serikali.
Kadhalika Mheshimiwa Majaliwa ameitaka Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) kuhakikisha mifumo iliyounganishwa inaendelea kubadilishana taarifa. “Lakini pia kila anayeingia jiridhishe kuwa anaweza kuwasiliana na wengine wote waliomo ndani, mmenieleza na mmesema kwamba ndivyo ilivyo, nasisitiza kwamba hakikisheni hiyo mifumo inasomana na inabadilishana taarifa”
Katika hatua nyingine, Mheshimiwa Waziri Mkuu ametoa wito kwa watumishi wa umma kuzingatia miiko na maadili ya utumishi katika utekelezaji wa majukumu yao kwa kuzingitia Sera na Sheria kwa manufaa na maendeleo ya Taifa letu. “Nitumie nafasi hii kuwapongeza sana watumishi wote wa umma nchini, niwahikishie kuwa serikali ya awamu ya sita iko pamoja nanyi. “Fanyeni hivyo kwa ajili ya manufaa na maendeleo ya Taifa letu”.
Kwa upande wake, Waziri wa Nchi-Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora George Simbachawene amesema Tanzania imetambulika kimataifa ambapo mwaka 2022 Benki ya Dunia ilifanya utafiti kuhusu ukomavu wa matumizi ya teknolojia duniani katika utoaji wa huduma za Serikali na ushirikishwaji wa wananchi.
Amefafanua kuwa ripoti ya utafiti huo iliyotolewa Machi, 2023 ilibanisha kuwa Tanzania imefanikiwa kupanda daraja kutoka kundi B hadi kundi A na kushika nafasi ya 26 duniani, nafasi ya 2 Afrika na nafasi ya kwanza katika nchi za Afrika Mashariki.
Katika tukio hilo, Mheshimiwa Majaliwa alizindua mifumo miwili ambayo ni Mfumo wa kielektroni unaowezesha mifumo ya Serikali kuwasiliana na kubadilishana taarifa ujulikanao kama Government Enterprises Service Bus (GovESB) Pamoja na Mfumo wa e-Wekeza unaomuwezesha Mtumishi wa Umma kuwekeza katika Mfuko wa Faida (Faida Fund).
Siku ya Utumishi wa Umma husherehekewa Juni 23 kila mwaka na nchi wanachama wa Umoja wa Afrika kwa lengo la kutambua mchango wa Watumishi wa Umma katika maendeleo ya nchi zao na Bara la Afrika kwa ujumla.







Labels:
KITAIFA
June 20, 2025
▪️Asema lengo ni kuendelea kutoa wahitimu wenye uwezo wa kukidhi vigezo vya kimataifa
▪️Rais Dkt. Samia atoa milioni 100 kuchangia maendeleo ya Chuo Kikuu cha Waislamu cha Morogoro
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa ameitaka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na TAMISEMI pamoja kusimamia na kudhibiti ubora wa elimu inayotolewa kuanzia elimu ya msingi mpaka elimu ya juu ili kuendelea kukidhi viwango vya kitaifa, kikanda na kimataifa.
Ametoa maagizo hayo leo (Ijumaa Juni 20, 2025) alipomwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye maadhimisho ya miaka 20 ya Chuo Kikuu cha Waislamu cha Morogoro (MUM), kwenye viwanja vya chuo hicho mkoani Morogoro.
“Mamlaka zetu ziendelee kusimamia hilo kwa kufanya hivyo sio tu kutaendelea kukuza ubora wa elimu yetu, bali pia kutawawezesha wasomi nchini kukidhi viwango na mahitaji ya soko la ajira”
Kadhalika, Mheshimiwa Majaliwa amezitaka Taasisi za Elimu nchini ziimarishe mahusiano na vyuo vyote nchini vinavyotoa maarifa kwa vijana wa kitanzania pamoja na kuzalisha wakufunzi ili kuwa sehemu ya mtandao wa utoaji maarifa na taalum hapa nchini.
Aidha, Mheshimiwa Majaliwa kuwa katika kuunga mkono jitihada za wadau mbalimbali katika kuchangia maendeleo ya chuo hicho kupitia mfumo maalum wa (MUM Community Fund), Rais Dkt. Samia ametoa kiasi cha Shilingi milioni 100 ili kiendelee kutoa huduma kwa watoto wa Kitanzania
Mheshimwa Waziri Mkuu ameongeza kuwa Serikali inaendelea na ujenzi wa Mfumo wa Takwimu wa Sekta ya Elimu utakaowezesha upatikanaji wa takwimu zote za sekta hiyo ambao utakuwa na uwezo wa kupokea takwimu mbalimbali zinazohusiana na elimu kutoka katika mifumo mingine ya Serikali ikiwemo NIDA, RITA na Wizara ya Mambo ya Nje.
Kwa Upande wake Naibu Waziri wa Elimu Qs Omar Kipanga amesema kuwa katika kipindi cha miaka 20, chuo hicho kimefanikiwa kuwa na progrma zaidi ya 32 kutoka program mbili wakati kinaanza na kimefanikiwa kutoa wahitimu zaidi ya 15,000.
“Wahitimu hawa wamekuwa wwamekuwa wa kupigiwa mfano katika kazi na maadili inayofanya waaminiwe katika nafasi mbalimbali kwenye jamii na Serikali kaa ujumla”
Kadhalika, ameongeza kuwa Chuo hicho kimeweka mipango inayozingatia dira ya maendeleo ya Taifa ya 2050 na mwelekeo mpya wa Elimu Nchini Tanzania unaolenga kutoa Elimu Ujuzi, Stadi na Maarifa kwa ajili ya kuwajengea wahitimu uwezo na sifa za kujiajiri na
kuajirika katika soko shindani la ajira duniani.
Naye Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania Sheikh Dkt. Abubakar Zubeir bin in Ali ametoa wito kwa Waislam na Watanzania kwa ujumla kuweka mikakati ya kukisaidia chuo ili kiendelee kufanya vizuri na kutoa elimu kwa watanzania nchini.
“Waislam na watanzania tukisaidie chuo hichi, hakuna uislam bila ualimu, uislam ulipokuja ulipiga sana vita ujinga, tuwaunge mkono viongozi wetu kwa kukisaidia chuo hiki”
Makamu Mkuu wa Chuo hicho Prof Juma Assad amesema kuwa moja ya changamoto kubwa katika chuo hicho ni kukosekana kwa hosteli za wanafunzi wa kike “Namna tunavyoingeza udahili ndivyo tunavyoibua changamoto nyingine, tunataka watoto wetu wa kike wote wake ndani ya chuo”
MAJALIWA AAGIZA USIMAMIAJI NA UDHIBITI WA UBORA WA ELIMU
Written By CCMdijitali on Friday, June 20, 2025 | June 20, 2025
▪️Asema lengo ni kuendelea kutoa wahitimu wenye uwezo wa kukidhi vigezo vya kimataifa
▪️Rais Dkt. Samia atoa milioni 100 kuchangia maendeleo ya Chuo Kikuu cha Waislamu cha Morogoro
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa ameitaka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na TAMISEMI pamoja kusimamia na kudhibiti ubora wa elimu inayotolewa kuanzia elimu ya msingi mpaka elimu ya juu ili kuendelea kukidhi viwango vya kitaifa, kikanda na kimataifa.
Ametoa maagizo hayo leo (Ijumaa Juni 20, 2025) alipomwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye maadhimisho ya miaka 20 ya Chuo Kikuu cha Waislamu cha Morogoro (MUM), kwenye viwanja vya chuo hicho mkoani Morogoro.
“Mamlaka zetu ziendelee kusimamia hilo kwa kufanya hivyo sio tu kutaendelea kukuza ubora wa elimu yetu, bali pia kutawawezesha wasomi nchini kukidhi viwango na mahitaji ya soko la ajira”
Kadhalika, Mheshimiwa Majaliwa amezitaka Taasisi za Elimu nchini ziimarishe mahusiano na vyuo vyote nchini vinavyotoa maarifa kwa vijana wa kitanzania pamoja na kuzalisha wakufunzi ili kuwa sehemu ya mtandao wa utoaji maarifa na taalum hapa nchini.
Aidha, Mheshimiwa Majaliwa kuwa katika kuunga mkono jitihada za wadau mbalimbali katika kuchangia maendeleo ya chuo hicho kupitia mfumo maalum wa (MUM Community Fund), Rais Dkt. Samia ametoa kiasi cha Shilingi milioni 100 ili kiendelee kutoa huduma kwa watoto wa Kitanzania
Mheshimwa Waziri Mkuu ameongeza kuwa Serikali inaendelea na ujenzi wa Mfumo wa Takwimu wa Sekta ya Elimu utakaowezesha upatikanaji wa takwimu zote za sekta hiyo ambao utakuwa na uwezo wa kupokea takwimu mbalimbali zinazohusiana na elimu kutoka katika mifumo mingine ya Serikali ikiwemo NIDA, RITA na Wizara ya Mambo ya Nje.
Kwa Upande wake Naibu Waziri wa Elimu Qs Omar Kipanga amesema kuwa katika kipindi cha miaka 20, chuo hicho kimefanikiwa kuwa na progrma zaidi ya 32 kutoka program mbili wakati kinaanza na kimefanikiwa kutoa wahitimu zaidi ya 15,000.
“Wahitimu hawa wamekuwa wwamekuwa wa kupigiwa mfano katika kazi na maadili inayofanya waaminiwe katika nafasi mbalimbali kwenye jamii na Serikali kaa ujumla”
Kadhalika, ameongeza kuwa Chuo hicho kimeweka mipango inayozingatia dira ya maendeleo ya Taifa ya 2050 na mwelekeo mpya wa Elimu Nchini Tanzania unaolenga kutoa Elimu Ujuzi, Stadi na Maarifa kwa ajili ya kuwajengea wahitimu uwezo na sifa za kujiajiri na
kuajirika katika soko shindani la ajira duniani.
Naye Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania Sheikh Dkt. Abubakar Zubeir bin in Ali ametoa wito kwa Waislam na Watanzania kwa ujumla kuweka mikakati ya kukisaidia chuo ili kiendelee kufanya vizuri na kutoa elimu kwa watanzania nchini.
“Waislam na watanzania tukisaidie chuo hichi, hakuna uislam bila ualimu, uislam ulipokuja ulipiga sana vita ujinga, tuwaunge mkono viongozi wetu kwa kukisaidia chuo hiki”
Makamu Mkuu wa Chuo hicho Prof Juma Assad amesema kuwa moja ya changamoto kubwa katika chuo hicho ni kukosekana kwa hosteli za wanafunzi wa kike “Namna tunavyoingeza udahili ndivyo tunavyoibua changamoto nyingine, tunataka watoto wetu wa kike wote wake ndani ya chuo”

Labels:
KITAIFA
June 20, 2025

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amesema Ubia wa Maendeleo baina ya Afrika na Italia kupitia mpango wa Mattei (Mattei Plan) na Mpango wa Ulaya (Global Gateway) utasaidia katika kuendeleza miundombinu, rasilimali watu, kilimo na maendeleo ya kidijitali barani Afrika.
Makamu wa Rais amesema hayo mara baada ya kushiriki Mkutano wa Ubia wa Maendeleo kati ya Bara la Afrika na Serikali ya Italia (Mattei Plan) pamoja na Mpango wa Ulaya (Global Gateway) unaofanyika katika Viwanja vya Villa Doria Pamphilj Jijini Roma nchini Italia akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Amesema mkutano huo umejadili zaidi vipaumbele vya nchi za Afrika na kudhamiria kutekeleza miradi kwa vitendo. Ameongeza kwamba majadiliano katika uongezaji thamani ya mazao hususani zao la kahawa yamelenga kuhakikisha Afrika inapata manufaa zaidi kutokana na kilimo hicho pamoja na kuongeza ajira kupitia zao hilo.
Makamu wa Rais amesema Tanzania ikiwa ni nchi ya nne barani Afrika kwa uuzaji wa kahawa nje ya bara hilo itanufaika zaidi na mpango wa uongezaji thamani wa zao hilo.
Pia amesema mkutano huo umejadili uwekezaji unaohitajika katika rasilimali watu ili kutengeneza mazingira mazuri zaidi kwa wananchi wa Afrika na kuwaepusha kukimbia nchi zao kuelekea mataifa ya Ulaya.
Makamu wa Rais amesema Mpango wa Mattei unabadili utoaji wa misaada ya maendeleo na kuleta mfumo mpya wa uwekezaji wa pamoja katika sekta za kimkakati ambao utatengeneza ajira na kuchochea mageuzi kwa maendeleo endelevu.
Katika Mkutano huo masuala yaliyopewa kipaumbele ni pamoja na uongezaji thamani katika zao la kahawa, nishati endelevu, uboreshaji miundombinu ikiwemo ushoroba wa Lobito pamoja na maendeleo ya kidijitali kama vile matumizi ya akili mnemba katika kukuza uchumi. Tanzania ni moja kati ya Mataifa 14 barani Afrika ambayo yanapewa kipaumbele na Italia kupitia mpango mpya wa kimkakati wa Mattei (Mattei Plan). Miradi ya kipaumbele katika Mpango huo ni pamoja na nishati, elimu na kilimo ambapo euro bilioni 5.5 zimetengwa kwaajili ya utekelezaji wa awamu ya kwanza ya miradi hiyo.
Mpango wa Umoja wa Ulaya (EU Global Gateway) ni wa kuboresha miundombinu katika sekta za kidijitali, nishati, usafirishaji, afya, elimu, na utafiti. Mpango huu unalenga uwekezaji wa Euro bilioni 300 ifikapo mwaka 2027, ambapo Euro bilioni 150 zimeelekezwa barani Afrika.
Umoja wa Ulaya wamedhamiria upanuzi wa mradi wa mawasiliano wa kidijiti (blue raman – submarine cable) unaopita chini ya bahari ambao unaunganisha Ulaya na India ili ufike nchini Tanzania na hivyo kuiunga Afrika Mashariki katika mradi huo.
Mkutano huo umeshirikisha Viongozi mbalimbali wa Afrika, Umoja wa Ulaya pamoja na Taasisi za Fedha za Kimataifa ikiwemo Benki ya Dunia, Shirika la Fedha Duniani (IMF) na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB).
Taasisi za fedha za kimataifa, Umoja wa Ulaya pamoja na Serikali ya Italia zimeahidi kutoa fedha kwaajili ya kugharamia miradi mbalimbali itakayotekelezwa katika Mpango huo.
Imetolewa na
Ofisi ya Makamu wa Rais
20 Juni 2025
Roma - Italia





MAKAMU WA RAIS DKT PHILIP MPANGO ASHIRIKI MKUTANO WA UBIA WA MAENDELEO NCHINI ITALIA

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amesema Ubia wa Maendeleo baina ya Afrika na Italia kupitia mpango wa Mattei (Mattei Plan) na Mpango wa Ulaya (Global Gateway) utasaidia katika kuendeleza miundombinu, rasilimali watu, kilimo na maendeleo ya kidijitali barani Afrika.
Makamu wa Rais amesema hayo mara baada ya kushiriki Mkutano wa Ubia wa Maendeleo kati ya Bara la Afrika na Serikali ya Italia (Mattei Plan) pamoja na Mpango wa Ulaya (Global Gateway) unaofanyika katika Viwanja vya Villa Doria Pamphilj Jijini Roma nchini Italia akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Amesema mkutano huo umejadili zaidi vipaumbele vya nchi za Afrika na kudhamiria kutekeleza miradi kwa vitendo. Ameongeza kwamba majadiliano katika uongezaji thamani ya mazao hususani zao la kahawa yamelenga kuhakikisha Afrika inapata manufaa zaidi kutokana na kilimo hicho pamoja na kuongeza ajira kupitia zao hilo.
Makamu wa Rais amesema Tanzania ikiwa ni nchi ya nne barani Afrika kwa uuzaji wa kahawa nje ya bara hilo itanufaika zaidi na mpango wa uongezaji thamani wa zao hilo.
Pia amesema mkutano huo umejadili uwekezaji unaohitajika katika rasilimali watu ili kutengeneza mazingira mazuri zaidi kwa wananchi wa Afrika na kuwaepusha kukimbia nchi zao kuelekea mataifa ya Ulaya.
Makamu wa Rais amesema Mpango wa Mattei unabadili utoaji wa misaada ya maendeleo na kuleta mfumo mpya wa uwekezaji wa pamoja katika sekta za kimkakati ambao utatengeneza ajira na kuchochea mageuzi kwa maendeleo endelevu.
Katika Mkutano huo masuala yaliyopewa kipaumbele ni pamoja na uongezaji thamani katika zao la kahawa, nishati endelevu, uboreshaji miundombinu ikiwemo ushoroba wa Lobito pamoja na maendeleo ya kidijitali kama vile matumizi ya akili mnemba katika kukuza uchumi. Tanzania ni moja kati ya Mataifa 14 barani Afrika ambayo yanapewa kipaumbele na Italia kupitia mpango mpya wa kimkakati wa Mattei (Mattei Plan). Miradi ya kipaumbele katika Mpango huo ni pamoja na nishati, elimu na kilimo ambapo euro bilioni 5.5 zimetengwa kwaajili ya utekelezaji wa awamu ya kwanza ya miradi hiyo.
Mpango wa Umoja wa Ulaya (EU Global Gateway) ni wa kuboresha miundombinu katika sekta za kidijitali, nishati, usafirishaji, afya, elimu, na utafiti. Mpango huu unalenga uwekezaji wa Euro bilioni 300 ifikapo mwaka 2027, ambapo Euro bilioni 150 zimeelekezwa barani Afrika.
Umoja wa Ulaya wamedhamiria upanuzi wa mradi wa mawasiliano wa kidijiti (blue raman – submarine cable) unaopita chini ya bahari ambao unaunganisha Ulaya na India ili ufike nchini Tanzania na hivyo kuiunga Afrika Mashariki katika mradi huo.
Mkutano huo umeshirikisha Viongozi mbalimbali wa Afrika, Umoja wa Ulaya pamoja na Taasisi za Fedha za Kimataifa ikiwemo Benki ya Dunia, Shirika la Fedha Duniani (IMF) na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB).
Taasisi za fedha za kimataifa, Umoja wa Ulaya pamoja na Serikali ya Italia zimeahidi kutoa fedha kwaajili ya kugharamia miradi mbalimbali itakayotekelezwa katika Mpango huo.
Imetolewa na
Ofisi ya Makamu wa Rais
20 Juni 2025
Roma - Italia






Labels:
KIMATAIFA