Na Mwandishi WetuMAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Stephen Wasira amesema Chama cha Demokrasia na Maendeleo hakina hoja ya msingi ya kuzuia Uchaguzi Mkuu mwaka huu kwani kama ni mabadilik ...

Read more »

HOTUBA YA MHESHIMIWA WAZIRI WA AFYA, JENISTA MHAGAMA KWA WAANDISHI WA HABARI WAKATI WA KUMTAMBULISHA PROF. MOHAMED YAKUB JANABI KAMA MGOMBEA MTEULE WA NAFASI YA UKURUGENZI WA SHIRIKA LA AFYA DUNIAN ...

Read more »

Serikali imewakumbusha wakopaji kusoma kwa kina masharti yote ya mikataba kabla ya kuchukua mikopo kutoka kwa Taasisi za kifedha ili kujiepusha na matatizo yanayoweza kutokea kutokana na masharti mag ...

Read more »

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa Mahmoud Thabit Kombo (Mb.) wamekutana kwa mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje, Uhamiaji na Wamisri Waishio Nje wa Jamhuri ya Kia ...

Read more »

 WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametoa wito kwa wadau wa elimu na mafunzo ya ufundi stadi nchini watoe mafunzo yanayozingatia mahitaji halisi ya soko la ajira. “Mahitaji ya soko la ajira tutay ...

Read more »

Na Mwandishi Wetu,MbeyaMAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Tanzania Bara amesema Rais Dk.Samia Suluhu Hassan kupitia kauli mbiu yake ya kazi iendelee ametekeleza miradi mikubwa ya kimkakati ...

Read more »

 Waziri wa Mambo ya Nje na Biashara wa Ireland anayeshughulikia Ushirikiano wa Kimataifa, Maendeleo, na Diaspora, Mhe. Neale Richmond Waziri wa Mambo ya Nje na Biashara wa Ireland anayeshug ...

Read more »

 Waziri wa Mambo ya Nje na Biashara wa Ireland anayeshughulikia ushirikiano wa kimataifa, maendeleo, na diaspora, Mhe. Neale Richmond, amefanya ziara rasmi mkoani Tanga kwa lengo la kukagua mira ...

Read more »

WASIRA : TUMESHAFANYA MABADILIKO YA SHERIA ZA UCHAGUZI, CHADEMA HAWAWEZI ZUIA UCHAGUZI.

Na Mwandishi Wetu MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Stephen Wasira amesema Chama cha Demokrasia na Maendeleo hakina hoja ya msin...

Latest Post

WASIRA : TUMESHAFANYA MABADILIKO YA SHERIA ZA UCHAGUZI, CHADEMA HAWAWEZI ZUIA UCHAGUZI.

Written By CCMdijitali on Friday, March 28, 2025 | March 28, 2025




Na Mwandishi Wetu

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Stephen Wasira amesema Chama cha Demokrasia na Maendeleo hakina hoja ya msingi ya kuzuia Uchaguzi Mkuu mwaka huu kwani kama ni mabadiliko wanayoyazungumza yameshafika tayari.

Amesema CHADEMA wao wanasema hawataki uchaguzi mpaka yafanyike mabadiliko ya uchaguzi, lakini ukweli wameshafanya marekebisho, na kusisitiza marekebisho yaliyofanyika yanahusisha sheria tatu ambazo zimefanyiwa mabadiliko.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika leo Machi 27,2025 katika Halmashauri ya Wilaya ya Kahama,Wasira aliyekuwa akihutubia wananchi hao amesema sheria zilizofanyiwa mabadiliko ni Sheria ya Uchaguzi wa Rais,Wabunge na madiwani.

Amesema nyingine ni sheria nyingine ni ya Tume ya uchaguzi pamoja na sheria ya vyama vya siasa vinavyosimamiwa na msajili wa vyama vya siasa na kuongeza mambo hayo ndiyo waliyokuwa wanalalamikia.

“Moja wanasema wao hawataki uchaguzi wanasema tume ile inateuliwa na Rais moja kwa moja kwahiyo sio huru, tukasema hamna tabu sheria mpya wabunge wako hapa, wakaunda kwamba tuweke kamati maalumu ili mtu anayetaka ukamishna wa tume ya uchaguzi waombe na ipo hiyo inaongozwa na Jaji Mkuu wa Zanzibar na watu kutoka Tume ya Haki za Binafamu na Utawala Bora.

“Kwahiyo ukifika wakati atakayetaka ukamishna anaomba na huyo anayeomba anatazamwa kwa vigezo vilivyowekwa kulingana na kazi anayoomba ,hiyo kamati ipo na maana yake ni kwamba mamlaka ya Rais yamepunguzwa…zamani alikuwa anaweza kuteua sasa hawezi, mpaka kamati ya usaili halafu imuambie Rais umehitaji watu watano tunakupa wanane chagua watano.”

Wasira amesema hayo ni mabadiliko makubwa na kuongeza wapinzani walisema Wakurugenzi watendaji wa halmashauri wanaiba kura hivyo hawataki wasimamie uchaguzi na walienda mpaka Mahakama ya Afrika Mashariki kupinga wakurugenzi hao ,hivyo sheria mpya imewaondoa.

“Sasa tume itakuwa inateua watumishi wa umma waandamizi na watumishi waandamizi wa umma sio wote wanateuliwa na Rais hata ukienda vyuo vikuu utawakuta watumishi wa umma waandamizi ni watu wasomi lakini hawateuliwi na Rais bali wanateuliwa na bodi za vyuo vyao na wanakuwepo kwa ajili ya usomi wao.

“Wakiteuliwa watu wa namna hiyo na hasa watumishi wengine wa serikali waaminifu kwa ajili ya kusimamia uchaguzi na wakurugenzi waliokuwa wametamkwa kwenye ile sheria ya zamani wakaondolewa.Sasa hayo ndio mabadiliko makubwa ambayo yamefanywa,sasa imekuja hii hoja mpya mmeisikia na nyinyi ila inasemwa kwa kiingereza 

“Inasema No Reform No election eti wanataka mabadiliko zaidi ya yale yaliyofanyika sasa tunawauliza wabunge ndio wenye kazi ya kufanya mabadiliko ya kisheria na Bunge linavunjwa Juni 27 na wabunge wanarudi kwetu wanakuwa raia kama sisi sasa uwalazimishe wafanye mabadiliko tena na presha ya ubunge iko juu,”amesema.

Ameongesa kuwa eti wabunge wabaki bungeni kwa ajili ya reform watakimbia hiyo reform kwani hawapo wamemaliza muda wao kwahiyo CHADEMA wanasema mambo ambayo hayawezekani.Unajua unaweza ukaeleza mambo hayatekelezeki hata wenye akili wakasema huyu anasema nini naye huyu

“Sasa hilo wametoka wanasema wanataka reform ipi wakati reform tumefanya kumbe ile ni danganya toto kwasababu wanaogopa uchaguzi wanakuja wakijua mtawapiga chini,walizoea kudanganya sasa udanganyifu mwisho ,wamekuwa kama timu ya mpira inayoweka mpira kwapani.

“Siunajua timu ya mpira ikiweka mpira kwapani ujue wanaogopa,nazungumzia mpira wa siasa sio wa uwanjani.Sasa nawaambia haya ndio mambo ,kwahiyo badala ya kusema tunaogopa uchaguzi wanasema mpaka yafanyike mabadiliko ,tutazuia uchaguzi,”

Wasira amewaambia wananchi wa Kahama wajue CHADEMA hawana uwezo wa kuzuia uchaguzi ,na waeleze watazuia kwa kufanyaje maana Katiba inasema katika ibara ya 41 hakuna mtu mwenye uwezo wa kuzuia uchaguzi wa Tanzania 

Amefafanua Uchaguzi utahairishwa kama kuna vita ,na nchi haina vita sasa anahairisha kwasababu ipi au vita iko ndani ya vichwa vyao maana inawezekana anatembea halafu ndani ya vichwa kuna vita inapiganwa.

“Uchaguzi unaanza kwa kujiandikisha na wakati wao wanaendelea na kelele za No Reform wenzao wanajiandikisha na Dar es Salaam maelfu ya watu wamejiandikisha mpaka siku zimeongezwa maana wanakwambia achana na no reform achana na maneno yao ,watu wanataka kupiga kura.”

Published from Blogger Prime Android App
Published from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android App
====

WAZIRI WA AFYA MHE MHAGAMA AMTAMBULISHA MGOMBEA MTEULE WA SHIRIKA LA AFYA DUNIANI KWA WAANDISHI WA HABARI

Written By CCMdijitali on Saturday, March 22, 2025 | March 22, 2025

HOTUBA YA MHESHIMIWA WAZIRI WA AFYA, JENISTA MHAGAMA KWA WAANDISHI WA HABARI WAKATI WA KUMTAMBULISHA PROF. MOHAMED YAKUB JANABI KAMA MGOMBEA MTEULE WA NAFASI YA UKURUGENZI WA SHIRIKA LA AFYA DUNIANI (WHO) KANDA YA AFRIKA UTAKAOFANYIKA TAREHE 18 MEI 2025, GENEVA, USWISI.

Katibu Mkuu Wizara ya Afya – Dkt. Seif Shekalaghe

Kaimu Mganga Mkuu wa Serikali –

Mshauri wa Rais wa Masuala ya Afya na Lishe na Mkurugenzi Mtendaji Hospitali ya Taifa Muhimbili – Prof. Mohamed Janabi.

Mkurugenzi Huduma za Kinga na Mkurugenzi Mkuu wa Jumuiya ya Afya ya Afrika Mashariki, Kati na Kusini (ECSA – HC) – Dkt. Ntuli A. Kapologwe

Wageni Waalikwa mliopo hapa

Ndugu Wanahabari:

Nawasalimu kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania…

Mnamo tarehe 14 Januari 2025 Shirika la Afya Duniani Kanda ya Afrika liliitisha kikao maalum na nchi wanachama wake 47 kwa ajili ya kujadili uchaguzi wa Mkurugenzi wa Shirika hilo kwa Kanda ya Afrika.

Ikumbukwe mnamo mwezi Agosti 2024, Tanzania iliwania nafasi hii kupitia Marehemu Dkt. Faustine E.Ndugulile aliyekuwa pia alikuwa Mbunge wa Jimbo la Kigamboni. Dkt. Ndugulile alishinda nafasi hiyo katika uchaguzi uliofanyika mnamo tarehe 26 Agosti 2024 wakati wa Mkutano wa 74 wa Shirika la Afya Duniani Kanda ya Afrika uliofanyika Brazaville, Jamhuri ya Kongo.

Dkt. Faustine alishinda nafasi hiyo baada ya kuwashinda wagombea wengine watatu ambao ni Dkt. Socce Fall (Senegal), Dkt. Richard Mihigo (Rwanda) na Dkt. Boureima Hama Sambo (Niger).



Ndugu Wanahabari;

 

Tarehe 27 Novemba 2024, Tanzania na Jumuiya ya Kimataifa tulipokea kwa mshutko mkubwa taarifa za kifo cha mpendwa wetu Dkt. Faustine Ndugulile ambaye alifariki kabla ya kuanza kuitumikia nafasi hiyo Mwezi Februari 2025. Naomba tusimame kwa dakika moja kumuombea Marehemu Dkt.Faustine Ndugulile apumzike kwa amani.

 

Ndugu Wanahabari:

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ikiwa ni miongoni mwa nchi wanachama wa Shirika la Afya Duniani Kanda ya Afya ilimpendekeza Prof. Mohamed Yakub Janabi, Mshauri wa Rais kwenye Masuala ya Afya na Lishe ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kuwania nafasi ya Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani Kanda ya Afrika.

Kama mnavyofahamu, Shirika la Afya Duniani ni chombo yenye mchango mkubwa katika kuboresha mifumo ya afya ulimwenguni. Nafasi hii ya Ukurugenzi wa Kanda ya Afrika ni muhimu sana kwa sababu inatoa mwelekeo wa kisera, kisayansi, na kimkakati katika kutatua changamoto za afya zinazolikabili bara letu, hivyo tunaamini Tanzania kuwa na mwakilishi katika Shirika hili itaweza kuongeza mchango wake katika maendeleo ya Sekta ya Afya barani Afrika.

Ndugu Wanahabari;

Prof. Mohamed Janabi ni mtaalamu mwenye uzoefu mkubwa katika sekta ya afya. Amehudumu katika nyadhifa mbalimbali za uongozi, ikiwa ni pamoja na kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili ambapo ameshiriki katika kuleta mageuzi makubwa ya utoaji wa huduma bora za afya na kuimarisha mifumo ya rufaa kutoka vituo vya kutolea huduma za afya ngazi ya msingi mpaka Taifa.

Akiwa Mkurugenzi Mtendaji wa kwanza na mwanzilishi wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Janabi aliongoza mageuzi makubwa katika huduma za matibabu ya moyo nchini Tanzania na Barani Afrika na hivyo kupekelea kupunguza rufaa za nje ya nchi kwa asilimia 95.

Pamoja na sifa hizo mbili, Prof. Janabi amekuwa akishiriki kwenye masuala ya utekelezaji wa afua za afya ya jamii kwa kutoa elimu ya afya na kushiriki kwenye shughuli mbalimbali za uimarishaji huduma za afya ngazi ya jamii. Prof. Janabi ameshiriki kwenye tafiti mbalimbali zilizolenga kuboresha utoaji wa huduma za afya pia ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Tiba na Afya Shirikishi Muhimbili (MUHAS) na Mhadhiri wa kualikwa katika Vyuo mbalimbali Duniani.

Prof. Janabi amefanya kazi kwa ukaribu na Mashirika ya Kikanda, Kimataifa, Serikali mbalimbali pamoja na Wadau wa Sekta ya Afya ili kuboresha upatikanaji wa huduma bora na endelevu za afya kwa wananchi. Uzoefu wake wa kitaaluma na kiutendaji unampa sifa zinazohitajika kuongoza Shirika la Afya Duniani (WHO) Kanda ya Afrika kwa ufanisi.

Ndugu Wanahabari;

Baadhi ya vigezo vilivyopelekea Prof.Janabi kugombea nafasi hii ni pamoja na;

v Uongozi Thabiti,

Prof. Janabi, ameonesha uwezo mkubwa wa kuleta mageuzi katika Sekta ya afya kupitia uongozi wake kwenye taasisi alizoziongoza lakini pia kuwa Mshauri Mkuu wa Masuala ya Afya na Lishe kwa Waheshimiwa Marais wawili (Mhe. Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na Mhe. Dkt. Samia Suluh Hassan).

 

v Uwezo wa Kitaalamu,

Prof. Janabi kupitia tafiti alizozifanya ndani na nje ya Nchi zimemjengea uelewa mpana wa masuala ya Afya ya Jamii na Lishe na kufanikiwa kuleta mabadiliko ya Sekta ya Afya nchini.

 

v Mtazamo wa Kikanda na Kimataifa,

Prof. Janabi ana mtazamo na maono ya maendeleo ya Sekta ya Afya yanayozingatia afya kwa wote na hii inatokana na uzoefu wake wa kufanya kazi katika maeneo tofauti ndani na nje ya nchi.

 

v Ushirikiano na Wadau wa Sekta ya Afya na Lishe,

Prof. Janabi ameendelea kuwa na uhusiano mzuri na mashirika ya Kikanda na Kimataifa, Taasisi za utafiti, na wahisani wa Afya ambayo kwa ujumla yanalenga kuimarisha mifumo ya Afya.

Ndugu Wanahabari;

Prof. Janabi anaingia katika uchaguzi huu akishindana na wagombea wengine wanne ambao ni: Profesa Moustafa Mijiyawa (Togo), Dkt. Michael Yao (Ivory Coast), Dkt. Boureima Hama Sambo (Niger) na Dr. Mohamed Lamine Drame (Guinea Conakry).

Wagombea hawa wanaowania nafasi hii pamoja na Prof. Janabi wote wanatokea nchi za Afrika ya Magharibi na wawili kati yao Dkt. Michael Yao (Ivory Coast) na Dkt. Boureima Hama Sambo (Niger) walishiriki katika uchaguzi uliopita ambao Marehemu Dkt. Ndugulile alishinda.

Ndugu Wanahabari;

Tanzania kupitia mgombea wetu Prof. Janabi tunaimani kubwa ya kushinda tena kwenye uchaguzi wa Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani Kanda ya Afrika kutokana na sababu zifuatazo:-

v Historia, Diplomasia pamoja na Ushirikiano ambao Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameendelea kuuimirisha baina ya nchi yetu na mataifa mengine, zinaipaisha Taifa letu kwenye majukwaa ya Kikanda na Kimataifa.

 

v Taifa letu lina sifa ya kutoa viongozi wenye weledi katika nyanja mbalimbali, na tunajivunia kwamba Prof. Janabi yuko tayari kulihudumia Bara letu katika nafasi hii.

 

v Uzoefu wa Prof. Janabi katika masuala ya ugharamiaji wa huduma za afya kwa kuzingatia kipindi hiki ambacho Dunia inapita katika changamoto ya kuwa na vyanzo vya uhakika wa ugharamiaji wa huduma za afya; uzoefu wake katika kudhibiti na kupambana na magonjwa ya mlipuko, uzalishaji wa bidhaa za afya nchini pamoja na usimamiaji wa mifumo ya utoaji wa huduma za afya zinatupa nafasi kubwa ya kushinda nafasi hii.

Ndugu Wanahabari;

Kampeni za wagombea wa nafasi hii tayari zimeshaanza kwa njia mbalimbali, nasi hatuna budi kushirikiana kumnadi mgombea wetu kwa nguvu, ari na morari kubwa. Nitoe rai kwa wananchi, mashirika na wadau wa Sekta wa ndani na nje kuungana pamoja katika kumnadi na kumuombea dua mgombea wetu.

Tuna imani kuwa kwa uongozi wake, Afrika itapiga hatua kubwa katika kuboresha mifumo ya afya, kupambana na magonjwa, na kuhakikisha kila mwananchi anapata huduma bora za afya.

Mungu ibariki Tanzania! Mungu ibariki Afrika! Asanteni kwa kunisikiliza.

 Published from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android App

WAKOPAJI WAKUMBUSHWA KUSOMA MIKATABA KABLA YA KUCHUKUA MIKOPO

Serikali imewakumbusha wakopaji kusoma kwa kina masharti yote ya mikataba kabla ya kuchukua mikopo kutoka kwa Taasisi za kifedha ili kujiepusha na matatizo yanayoweza kutokea kutokana na masharti magumu au riba kubwa ambazo huathiri urejeshaji wa mkopo.

Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza, Arch. Chagu Nghoma, aliyasema hayo  alipokutana na Timu ya Wataalamu kutoka Wizara ya Fedha pamoja  na Taasisi zake  ambayo imewasili mkoani humo kwa ajili ya kutoa elimu ya fedha  kwa Wananchi wa mkoa huo katika makundi mbalimbali.

“Tunaendelea kuwakumbusha wakopaji kuongeza umakini katika kusoma mikataba wanayoingia kutokana na kuongezeka kwa malalamiko kutoka kwa wakopaji ambao wanakabiliwa na riba kubwa, masharti magumu ya marejesho, na faini zisizoeleweka baada ya kushindwa kutimiza masharti ya mikopo.

Aliongeza kuwa ni muhimu kwa mkopaji ikiwa hajaelewa mkataba vizuri, atafute  ushauri wa kisheria au wa kifedha kabla ya kutia saini mkataba wowote wa mkopo ili kujiepusha na matatizo yanayoweza kujitokeza baadae.

Arch. Chagu Nghoma, aliwasisitiza wakopaji kuwa waangalifu na kuepuka kukopa kwenye Taasisi za Fedha zisizo rasmi ambazo zinaweza kuwa na masharti kandamizi iwapo watashindwa kulipa mkopo.

Naye mmoja wa washiriki wa mafunzo ya elimu ya fedha, mkazi wa Buhongwa, Mwanza, Bi. Julieth Siange, alishukuru kwa elimu waliyoipata ikiwemo msisitizo waliopewa wa kutojiunga na vikundi ambavyo havijasajiliwa bali wajiunge katika vikundi rasmi vilivyosajiliwa na vinavyotambulika na Serikali ili matatizo yanapotokea waweze kusaidiwa kisheria.

Kiongozi wa Timu ya Wataalamu wa utoaji wa elimu ya fedha kutoka Wizara ya Fedha, Bw. Salim Khalfan Kimaro, alisema kuwa, pamoja na juhudi mbalimbali zinazofanywa na Serikali kuweka sheria na kanuni mbalimbali kwa watoa huduma za fedha jinsi wanavyotakiwa kuendesha Taasisi hizo, bado kumekuwa na changamoto kwa baadhi ya watoa huduma kutofuata sheria na kanuni.

Bw. Kimaro, alifafanua kuwa kutokana na changamoto hizo kutoka kwa watoa huduma  kutokuwa waaminifu, Serikali itaendelea kufanya ufuatiliaji wa mara kwa mara na kuzichukulia hatua za kinidhamu ili kuhakikisha Taasisi hizo zinafanya kazi kwa kuzingatia taratibu, kanuni na sheria.

Wizara ya Fedha inaendelea na zoezi la utoaji elimu ya fedha kwa wananchi wa makundi yote ikiwa ni utekelezaji wa Mpango Mkuu wa Maendeleo ya Sekta ya Fedha kwa mwaka 2021/2022 hadi 2029/2030.








Tanzania na Misri kupanua wigo wa ushirikiano

Written By CCMdijitali on Wednesday, March 19, 2025 | March 19, 2025


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa Mahmoud Thabit Kombo (Mb.) wamekutana kwa mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje, Uhamiaji na Wamisri Waishio Nje wa Jamhuri ya Kiarabu ya Misri, Mheshimiwa Dkt. Badr Abdelatty, katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam baada ya mazungumzo yao, Waziri Kombo ameeleza kuwa Tanzania na Misri zimejidhatiti kuimarisha  ushirikiano wa uwili kwa manufaa ya kiuchumi ya pande zote mbili.

Waziri Kombo ameeleza kuwa Ujenzi wa Mradi wa Bwawa la Kufua Umeme la Julius Nyerere ni kielelezo cha uhusiano imara wa nchi hizi mbili. Pamoja na hayo, amesisitiza kuendeleza ushirikiano katika  utekelezaji wa miradi mingine ya kimkakati na kimaendeleo.

Waziri Kombo ameongeza kuwa lipo dirisha la kuongeza wigo wa ushirikiano kibiashara na uwekezaji katika sekta ya uvuvi, bidhaa za chakula na kilimo, utalii, huduma za bandari pamoja na sekta ya usafirishaji ambapo amelikaribisha Shirika la Ndege la Misri (Egypt Air) kuongeza safari zake nchini. 

 “Takwimu za biashara kati ya Tanzania na Misri zimekuwa zikiongezeka, ambapo thamani ya biashara zimeongezeka kutoka Tsh bilioni 84.3 mwaka 2019 hadi Tsh bilioni 142 mwaka 2023. Hii ni hali ya kutia moyo, lakini wote tumekubaliana kuwa fursa za ukuaji ni kubwa zaidi, na tunahitaji kufanya zaidi ili ukuaji huo uendelee.” 

Aidha, Waziri Kombo amewasihi Watanzania kuchangamkia fursa za mafunzo katika kada mbalimbali zikiwemo  udaktari na kilimo ambazo zimekuwa zikitolewa na Serikali ya Misri.

Kwa upande wake, Mheshimiwa Dkt. Abdelatty amesema kuwa sasa ni wakati wa Tanzania na Misri kuongeza nguvu kukuza ushirikiano katika biashara na uwekezaji akieleza kuwa Misri iko tayari kushirikiana na Tanzania katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya miundombinu ikiwemo reli, barabara, na bandari.

Tanzania ni uti wa mgongo wa mazao ya chakula kwa nchi nyingi za Afrika na hivyo, Misri ingependa kuwa miongoni mwa nchi zinazoagiza mazao ya chakula kutoka Tanzania.

Aidha, Waziri Dkt. Abdelatty amesisitiza suala la matumizi mazuri ya maji ya Mto Nile pamoja na kushirikiana na Tanzania na nchi nyingine zote zenye vyanzo vya maji jumuishi katika kutunza vyanzo hivyo kwa faida ya vizazi vijavyo.

Misri inashika nafasi ya 8 katika uwekezaji hapa nchini, na uwekezaji wa Misri unafikia kiasi cha dola za Marekani bilioni 1.37, na kuchangia kutoa ajira kwa Watanzania wapatao 3,776.

Published from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android App

TOENI MAFUNZO YANAYOZINGATIA SOKO LA AJIRA-MAJALIWA

Written By CCMdijitali on Tuesday, March 18, 2025 | March 18, 2025


 
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametoa wito kwa wadau wa elimu na mafunzo ya ufundi stadi nchini watoe mafunzo yanayozingatia mahitaji halisi ya soko la ajira.
 
“Mahitaji ya soko la ajira tutayajua kwa kufanya tafiti za mara kwa mara kwa ushirikiano kati ya Serikali, sekta binafsi, na mashirika ya kimataifa.”
 
Ametoa wito huo leo (Jumanne, Machi 18, 2025) katika Maadhimisho ya miaka 30 ya Uanzishwaji wa Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) yaliyofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere, Dar es Salaam.
 
Amesema katika zama hizi zenye kasi ya maendeleo ya teknolojia, ni muhimu kwa VETA kuendelea kujiimarisha kukabiliana na mabadiliko ya teknolojia duniani.
 
“Toeni mafunzo ya ufundi stadi yanayoendana na mabadiliko ya teknolojia, mafunzo hayo yajumuishe ujuzi wa teknolojia za kisasa zinazochochea uzalishaji wenye tija.”
 
Akizungumza kuhusu umuhimu wa Elimu ya Ufundi Stadi, Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa takwimu za Shirika la Kazi Duniani (ILO) zinaonesha kuwa takribani asilimia 70 ya ajira zote ni ajira binafsi na kwa watu wenye elimu ya ufundi stadi hasa kwenye sekta za kilimo, ujenzi, usafirishaji, na huduma za kijamii.
 
“Kwa upande wa nchi yetu, takwimu za ajira zilizozalishwa kati ya mwaka 2020 na 2024 zinafikia Milioni 7 ambapo ajira binafsi katika sekta isiyo rasmi imeajiri watu milioni 6.1 sawa na asilimia 87.1 ambapo wengi wao wana elimu ya ufundi stadi, na sekta rasmi imeajiri watu 907,873 (asilimia 12.9) ambapo wengi wao ni wale wenye elimu ya juu”.
 
Pia, Waziri Mkuu ameiagiza Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais - TAMISEMI na Wizara ya Viwanda na Biashara wahakikishe ujenzi wa vyuo 65 vya ufundi unakamilika haraka.
 
Waziri Mkuu amesema ukamilishwaji wa vyuo hivyo vinavyojengwa na Serikali unalenga kutimiza dhamira ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuwawezesha Watanzania kiujuzi.
 
“Ujenzi wa vyuo hivi ukikamilika, VETA itakuwa na vyuo 145 katika ngazi ya Mikoa yote 26 na Wilaya zote nchini. Vilevile, katika vyuo 80 vilivyopo, vyuo 30 vilikamilishwa katika kipindi cha Serikali ya Awamu ya Sita (6). Tuna kila sababu ya kumpongeza Rais wetu kwa kazi kubwa anayowafanyia Watanzania.”
 
Kadhalika Waziri Mkuu ameitaka VETA ihakikishe inatangaza fursa za mafunzo zilizopo ili vijana haswa wa vijijini waweze kuzitumia. “Inawezekana kabisa kuwa, wapo vijana katika maeneo mbalimbali nchini haswa ya vijijini ambao hawana taarifa ya fursa za mafunzo zilizopo.”


Published from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android App

RAIS SAMIA AMEFANYA MAKUBWA KATIKA MIAKA MINNE YA UONGOZI WAKE-WASIRA



Na Mwandishi Wetu,Mbeya

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Tanzania Bara amesema Rais Dk.Samia Suluhu Hassan kupitia kauli mbiu yake ya kazi iendelee ametekeleza miradi mikubwa ya kimkakati ikiwemo iliyoachwa na mtangulizi wake Hayati Dk.John Magufuli aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano.

Wasira amesema kuwa Dk.Magufuli alikuwa na kauli mbiu ya Hapa Kazi Tu lakini Rais Samia alipochukua uongozi wa nchi hakuacha neno kazi na hivyo akaja na Kazi iendelee na hakika katika miaka minne ya uongozi wake amefanya mambo makubwa licha ya kwamba wapo baadhi ya watu hawakuamini kama ataweza.

Akingumza leo Machi 17,2025 katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Soko la Mwanjelwa jijini Mbeya, Wasira ambaye yupo katika ziara ya kukagua utekelezaji wa Ilani , kuzungumza na wana CCM pamoja na kusikiliza kero za wananchi amesema kwa mujibu wa Katiba baada ya kifo cha Rais , basi Makamu wa Rais ndio anaapishwa kuwa Rais.

“Katiba inasema Rais akifa Makamu wa Rais anaapishwa kuwa Rais, kwahiyo tarerehe 19 siku mbili zijazo Rais Samia alitangazwa kuwa Rais kuchukua nafasi ya Dk.John Pombe Magufuli na kama mnavyojua John Magufuli alikuwa na kauli mbiu anasema Hapa Kazi Tu…

“Sasa Rais Samia alipochukua hakutaka kuacha neno Kazi lakini akasema Kazi Iendelee, hiyo ndio historia ya miaka minne na yalipotokea hayo kama kawaida ya binadamu wanasitasita hivi inawezekana , nchi itakuwa salama?Miradi iliyoanzishwa itamalizwa? Lakini leo tulipo hapa unaweza kuuliza kazi imeendelea au haijaendelee?

“Kazi imendelee tena kuliko wengine tulivyodhani , nitawapa mifano michache, moja wakati Dk.Magufuli anaondoka duniani alianzisha ujenzi wa reli ilikuwa imefika Morogoro lakini ilikuwa haijakamilika ,Rais Samia ameendeleza reli ya SGR sasa imefika Makutupola mkoani Singida,leo Dar es Salaam na Morogoro mpaka Dodoma imekuwa karibu kwasababu ya reli hii,”amesema Wasira.

Ameongeza katika ujenzi wa reli hiyo kila kipande kuna mkandarasi na baada ya Uchaguzi Mkuu mwaka huu na miaka miwili ijayo reli itakuwa imefika Tabora, Kigoma lakini itakuwa inafika Mwanza .Kwahiyo kazi iliyokuwa imeachwa inafanyika.

Amesema kazi nyingine aliyoachiwa ni kujenga Bwawa la Mwalimu Nyerere ambalo limefikia asilimia 100 lakini wakati Rais Samia anachukua nchi ujenzi wake ulikuwa asilimia 30, hivyo kazi imendelee na kuongeza kulikuwa na tatizo la mgao lakini sasa hakuna.
 
“Kuna matatizo ya miundombinu ambapo umeme unaweza kukatika kwa muda lakini hakuna mgao , nchi yetu inaumeme wa kutosha na hay oni baadhi ya mambo ambayo utekelezaji wake umefanyika kwa asilimia 100 chini ya Rais Dk.Samia Suluhu Hassan na ndio maana tunasema Rais Samia mitano tena.

Amesema Rais Samia amefanya mambo makubwa katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wake na kutoa mfano kwa Mkoa wa Mbeya Mjini na Vijijni kwa upande wa elimu ya msingi madarasa mapya 156 yamejengwa lakini kwa upande wa sekondari yamejengwa madarasa 335 tena ya kisasa.

“Katika eneo la afya hapa Mbeya katika kipindi cha miaka minne zahanati 20 na vituo vya afya 14 vimejengwa na lengo kuu ni kusogeza huduma karibu na wananchi. Jana nilipokuwa Songwe niliambiwa jambo ambalo sikutarajia kuambiwa, nimeambiwa akina mama wakienda kujifungua wanadaiwa hadi Sh.300,000 .

“Sera ya CCM katika suala la tiba inasema kwanza wakina mama wajawazito hawatakiwi kutozwa hata sh.10 kwa ajili ya kujifungua.Sera yetu inasema watoto chini ya miaka mitano watibiwe bila masharti bila kudaiwa chochote,shabaha yetu watu watibiwe bure na ndio maana tunazungumza kuhusu bima kwa wote.

“Pia tunasema wazee wasiojiweza wakiorodheshwa na halmashauri wakienda na kadi walizopewa wanatakiwa kupewa matibabu bure. Jana usiku nimeongea na Waziri wa Afya naye amefikisha jambo hilo katika vituo vya afya na hospitali zote ambapo amepiga marufuku wajawazito wanaokwenda kujifungua kutozwa fedha.”

Kuhusu usambazaji maji katika Mkoa wa Mbeya, Wasira amesema usambazaji maji uko vizuri kwani umefikia asilimia 90 kutoka asilimia 80 na asilimia 10 iliyobakia itaingizwa katika Ilani inayokuja lengo likiwa kuhakikisha upatikanaji wa maji mijini unakuwa kwa asilimia 100 na vijijini asilimia 95.

Published from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android App
=====

WAZIRI WA IRELAND AZURU TANGA AKUTANA NA DKT. BURIANI.

Written By CCMdijitali on Sunday, March 16, 2025 | March 16, 2025

 Waziri wa Mambo ya Nje na Biashara wa Ireland anayeshughulikia Ushirikiano wa Kimataifa, Maendeleo, na Diaspora, Mhe. Neale Richmond

 

Waziri wa Mambo ya Nje na Biashara wa Ireland anayeshughulikia Ushirikiano wa Kimataifa, Maendeleo, na Diaspora, Mhe. Neale Richmond, amefanya ziara ya siku moja mkoani Tanga ambako amekutana na kuzungumza na Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Dkt. Batilda Buriani.

 

Katika mazungumzo yao, viongozi hao wameangazia namna ya kuendelea kushirikiana kupitia sekta za kimkakati, ikiwemo afya, ufugaji, uchumi wa bluu, uhifadhi wa mazingira ya pwani na baharini, uwezeshaji wa kijinsia, na maendeleo ya vijana.

 

Mhe. Dkt. Buriani ameishukuru Serikali ya Ireland kwa mchango wake katika miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani humo hasa katika sekta za afya, ufugaji, na uwezeshaji kiuchumi kwa wanawake na vijana.

 

Ameeleza dhamira ya mkoa wa Tanga kuendele kushirikiana na Ireland ili kuimarisha maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

 

Aidha, Mkuu wa Mkoa ametoa wito kwa Ireland kuangazia fursa za uwekezaji katika sekta za utafiti wa maziwa, uvuvi, na afya, huku akisisitiza umuhimu wa kuimarisha uchumi wa bluu kama nyenzo ya maendeleo endelevu katika mkoa huo.

 

Kwa upande wake, Mhe. Richmond ameahidi kuendeleza ushirikiano kati ya Ireland na Tanzania, akisisitiza kuwa nchi yake itaendelea kuunga mkono juhudi za Tanzania katika sekta za afya, usawa wa kijinsia, uwezeshaji wa wanawake na mifugo.

 

Katika ziara yake mkoani Tanga, Waziri Richmond ameambatana na Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, ambaye pia anawakilisha Ireland, Mhe. Mbelwa Kairuki, Balozi wa Ireland nchini Tanzania, Mhe. Nicola Brennan, Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Swahiba Mndeme, pamoja na maafisa wengine wa serikali kutoka Tanzania na Ireland.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Dkt Batilda Salha Buriani (kushoto) na Waziri wa Mambo ya Nje  Na Biashara Ireland anayeshughulikia masuala ya Ushirikiano wa Kimataifa, Maendeleo na Diaspora (Kulia)

Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Dkt Batilda Salha Buriani



Waziri wa Mambo ya Nje  Na Biashara Ireland anayeshughulikia masuala ya Ushirikiano wa Kimataifa, Maendeleo na Diaspora




WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA IRELAND ATEMBELEA MIRADI YA MAENDELEO MKOANI TANGA

 

Waziri wa Mambo ya Nje na Biashara wa Ireland anayeshughulikia ushirikiano wa kimataifa, maendeleo, na diaspora, Mhe. Neale Richmond, amefanya ziara rasmi mkoani Tanga kwa lengo la kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo inayofadhiliwa na Serikali ya Ireland.

 

Katika ziara yake, Mhe. Richmond alitembelea Mradi wa Faida Maziwa, unaotekelezwa na Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI). Mradi huo unalenga kuboresha uzalishaji wa maziwa, kuongeza thamani ya bidhaa za maziwa, na kuinua kipato cha wafugaji wa ng’ombe wa maziwa.

 

Aidha, ameweka mkazo katika matumizi ya mbegu bora za malisho, hatua inayosaidia kupunguza migogoro kati ya wafugaji na wakulima, na hivyo kuimarisha ustawi wa maisha ya jamii ya wakulima na wafugaji mkoani Tanga.

 

Pia, Mhe. Richmond alitembelea kituo cha afya kinachofadhiliwa na Benjamin Mkapa Foundation kwa kushirikiana na Shirika la Afya la Amref, ambacho ni miongoni mwa taasisi zinazopokea msaada kutoka Serikali ya Ireland.

 

Katika ziara hiyo, alishuhudia juhudi zinazofanywa katika kuboresha huduma za afya, hususan afya ya mama na mtoto, pamoja na uwekezaji katika miundombinu ya huduma za afya.

 

Aidha, Waziri Richmond alipata fursa ya kuzungumza na viongozi wa mashirika mbalimbali yakiwemo Amref, Benjamin Mkapa Foundation, Femina, na Uzikwasa, pamoja na vikundi vya kijamii vinavyotekeleza miradi ya maendeleo katika sekta tofauti.

 

Akihitimisha ziara yake mkoani humo Mhe. Richmond alisisitiza dhamira ya Serikali ya Ireland kuendelea kushirikiana na Tanzania katika kukuza maendeleo endelevu kupitia miradi yenye tija kwa wananchi.

 

Pia alitoa pongezi kwa wadau wote wanaoshiriki katika utekelezaji wa miradi hiyo na kusisitiza kuwa ni muhimu kuimarisha sekta za afya, kilimo, na biashara ili kukuza uchumi wa wananchi na Taifa kwa ujumla.













RAIS MSTAAFU DKT. KIKWETE ZIARANI JAPAN: KUKUTANA NA VIONGOZI, KUSUKUMA AJENDA YA ELIMU

Written By CCMdijitali on Thursday, March 13, 2025 | March 13, 2025

 

Rais mstaafu, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, akiwa  Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Elimu la Kimataifa (GPE), yupo Tokyo nchini Japan kwa ziara maalum yenye lengo la kuimarisha ushirikiano kati ya GPE na serikali ya Japan katika kutatua changamoto za elimu ya msingi katika nchi zinazoendelea.

 

Katika siku yake ya kwanza Tokyo, Dkt. Kikwete amefanya mazungumzo na Waziri wa Fedha wa Japan, Mhe. Shin-ichi Yokohama, pamoja na Naibu wake, Mhe. Atsushi Mimura. Mazungumzo hayo yalijikita katika ushirikiano wa kifedha ili kusaidia miradi ya elimu inayosimamiwa na GPE, ikiwemo upatikanaji wa rasilimali kwa ajili ya kuboresha mazingira ya kujifunzia kwa watoto wa nchi zinazoendelea.

 

Baada ya mazungumzo hayo, Rais Mstaafu Kikwete alikutana na Bw. Akihiko Tanaka, Rais wa Shirika la Ushirikiano wa Kimataifa la Japan (JICA). Shirika hili limekuwa na mchango mkubwa katika miradi ya maendeleo barani Afrika, na mazungumzo yalihusu namna JICA inaweza kusaidia jitihada za GPE katika kukuza elimu bora.

 

Dkt. Kikwete pia alikutana na Bw. Yohei Sasakawa, Mwenyekiti wa Taasisi ya Nippon. Bw. Sasakawa, mwenye umri wa miaka 86, ni mtu mashuhuri wa kusaidia miradi ya kijamii duniani. Katika mazungumzo yao, waligusia nafasi ya sekta binafsi katika kusaidia elimu, hasa kupitia taasisi zisizo za kiserikali. Vilevile, Bw. Sasakawa alishangaza dunia baada ya kufanikisha kupanda Mlima Kilimanjaro tarehe 12 Februari 2024, kama sehemu ya maadhimisho ya miaka 85 ya kuzaliwa kwake – hatua inayothibitisha kuwa umri si kikwazo kwa ndoto kubwa.

 

Katika siku zinazofuata, Rais Mstaafu Kikwete anatarajiwa kukutana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Japan, Mhe. T. Miyaji, pamoja na wabunge wa Bunge la Japan, ambapo ajenda kuu itakuwa nafasi ya elimu na teknolojia katika maendeleo ya jamii. Pia, atashiriki mijadala maalum kuhusu elimu na teknolojia, kufanya mahojiano na vyombo vya habari, pamoja na kukutana na Mhe. Tetsuro Yano, Rais wa Taasisi ya AFRECO, ambayo inahusika na kukuza ushirikiano kati ya Japan na Afrika.

 

Ziara hii ni sehemu ya juhudi endelevu za Dkt. Kikwete katika kuboresha mifumo ya elimu duniani, hasa katika nchi zinazoendelea. Japan ni mshirika muhimu wa maendeleo ya elimu barani Afrika, na ushirikiano huu unaweza kuwa na mchango mkubwa katika kuhakikisha watoto wengi zaidi wanapata fursa ya elimu bora.


Rais Mstaafu Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Waziri wa Fedha wa Japan, Mhe. Shin-ichi Yokohama,jijini Tokyo




Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Bw. Yohei Sasakawa, Mwenyekiti wa Taasisi ya Nippon jijini Tokyo. Bw. Sasakawa, mwenye umri wa miaka 86, ni mtu mashuhuri wa kusaidia miradi ya kijamii duniani. Katika mazungumzo yao, waligusia nafasi ya sekta binafsi katika kusaidia elimu, hasa kupitia taasisi zisizo za kiserikali. Vilevile, Bw. Sasakawa alishangaza dunia baada ya kufanikisha kupanda Mlima Kilimanjaro tarehe 12 Februari 2024, kama sehemu ya maadhimisho ya miaka 85 ya kuzaliwa kwake – hatua inayothibitisha kuwa umri si kikwazo kwa ndoto kubwa.








Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika mazungumzo na Bw. Yohei Sasakawa, Mwenyekiti wa Taasisi ya Nippo, na maofisa wake waandamizi jijini Tokyo.




1234567 Next

SPORTS

BIASHARA

KIMATAIFA

See all posts

KITAIFA

WAZIRI WA IRELAND AZURU TANGA AKUTANA NA DKT. BURIANI.

 Waziri wa Mambo ya Nje na Biashara wa Ireland anayeshughulikia Ushirikiano wa Kimataifa, Maendeleo, na Diaspora, Mhe. Neale Richmond Waziri wa Mambo ya Nje na Biashara wa Ireland anayeshug...

Read More �
 Ausisitiza uongozi kuongeza wigo wa kuimarisha upatikanaji wa vitabuAmpon...
 Na. Mwandishi Wetu Uwepo wa mawakala wa vyama vya siasa wakati wa ubores...
Chama cha Mapinduzi (CCM), kimehamasisha wanachama wake kujitokeza kwa wingi kw...
 Na. Mwandishi Wetu  Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga K...

Wenye Umri wa Miaka 50-59 Wanogesha Riadha SHIMIWI

 Na Mwandishi Wetu, Tanga   Mchezo wa riadha watu wazima wenye umri...

Ligi ya timu za Vijana kwa ajili ya mashindano ya Neema Youth Cup kundi A,Jijini Arusha

Vijana katika kuendelea kuadhimisha sherehe za kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi...

Nigeria's Iwobi on target as Arsenal beat Stoke City at home

United Kingdom Nigerian forward Alex Iwobi was on target in the English Prem...

Manchester United 4-1 Fenerbahce

Manchester United 4-1 Fenerbahce: Paul Pogba nets brace as former Red Devil Ro...

See all posts

ARUSHA

VIONGOZI WANALOJUKUMU LA KUZINGATIA MATUMIZI YA TAKWIMU ZA MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022.

 MBUNGE WA JIMBO LA ARUMERU MASHARIKI MHE DKT D.JOHN PALLANGYOMbunge wa Arumeru Mashariki Mhe. Dkt. John Danielson Palangyo, amesema kuwa viongozi wa wananchi wanalojukumu la kuzingatia matumizi...

Read More �
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Geofrey Pinda akizungu...
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. John V.K. Mongella akifungua Mkutano Mkuu wa 6 mwak...
MWENYEKITI WA CCM MKOA WA ARUSHA ZELOTE STEPHEN AFARIKI DUNIA-Alhamisi, October...
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (M...
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. John V.K. Mongella Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. John...
See all videos

Video Category

 
Support : #BegaKwaBegaNaMamaSamia | JAK | CCM Arusha
Copyright © 2011. CCM Dijitali - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Jasper K
Proudly powered by Blogger
Link