Maonyesho ya 12 ya Kimataifa ya Biashara ya Zanzibar yafunguliwa
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar afungua Maonyesho ya 12 ya Kimataifa ya Biashara ya Zanzibar Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapi...
Latest Post
January 07, 2026

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar afungua Maonyesho ya 12 ya Kimataifa ya Biashara ya Zanzibar
Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mheshimiwa Hemed Suleiman Abdulla,amefungua rasmi Maonyesho ya Biashara ya Kimataifa ya 62 ya Zanzibar yanayiendelea katika viunga vya maonyesho vya Nyamanzi, Fumba mjini Unguja.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa maonesho hayo Makamu wa Pili wa Rais Mheshimiwa Abdulla amesisitiza umuhimu wa maonesho hayo kama chombo cha kukuza biashara, kuongeza fursa za uwekezaji na kuinua sekta ya uzalishaji hasa kwa wajasiriamali wa ndani.
Alieleza kuwa serikali itaendelea kuwa miongoni mwa waungaji mkono wakuu wa biashara ndogo ndogo, za kati na kubwa ili kuhakikisha ukuaji endelevu wa uchumi wa visiwa vya Zanzibar na Pemba.
Mheshimiwa Abdulla ametembelea mabanda mbalimbali yanayoshiriki katika maonesho hayo ikiwa ni pamoja na banda la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Taasisi zake za AICC,APRM na Kituo cha Uhusiano wa Kimataifa cha Dkt .Salim Ahmed Salim.
Katika banda la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mheshimiwa Abdullah Abdullah alipokelewa na Kaimu Mkurugenzi wa Afisi ya Mambo ya Nje Zanzibar Bw. Ally Ally na wafanyakazi wa Wizara walioko katika afisi hiyo.
Mheshimiwa Abdulla amewapongeza watumishi wa Wizara na taasisi zake kwa kazi kubwa na nzuri wanayoifanya katika kutekeleza majukumu yao.
Naye Mkurugenzi wa Maonyesho hayo amewataka wadau walioshiriki maonesho hayo kutumia fursa hiyo ya kipekee kuuza bidhaa, kutafuta washirika wa kibiashara na kupanua mitandao ya uwekezaji kwa kuwa maonyesho hayo ni jukwaa muhimu la kukuza soko la ndani na nje ya nchi.
Maonesho hayo yanashirikisha zaidi ya taasisi 316 kutoka serikalini, kampuni binafsi na washirika wa kimataifa yatamalizika Januari 16,2026.












Maonyesho ya 12 ya Kimataifa ya Biashara ya Zanzibar yafunguliwa
Written By CCMdijitali on Wednesday, January 7, 2026 | January 07, 2026

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar afungua Maonyesho ya 12 ya Kimataifa ya Biashara ya Zanzibar
Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mheshimiwa Hemed Suleiman Abdulla,amefungua rasmi Maonyesho ya Biashara ya Kimataifa ya 62 ya Zanzibar yanayiendelea katika viunga vya maonyesho vya Nyamanzi, Fumba mjini Unguja.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa maonesho hayo Makamu wa Pili wa Rais Mheshimiwa Abdulla amesisitiza umuhimu wa maonesho hayo kama chombo cha kukuza biashara, kuongeza fursa za uwekezaji na kuinua sekta ya uzalishaji hasa kwa wajasiriamali wa ndani.
Alieleza kuwa serikali itaendelea kuwa miongoni mwa waungaji mkono wakuu wa biashara ndogo ndogo, za kati na kubwa ili kuhakikisha ukuaji endelevu wa uchumi wa visiwa vya Zanzibar na Pemba.
Mheshimiwa Abdulla ametembelea mabanda mbalimbali yanayoshiriki katika maonesho hayo ikiwa ni pamoja na banda la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Taasisi zake za AICC,APRM na Kituo cha Uhusiano wa Kimataifa cha Dkt .Salim Ahmed Salim.
Katika banda la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mheshimiwa Abdullah Abdullah alipokelewa na Kaimu Mkurugenzi wa Afisi ya Mambo ya Nje Zanzibar Bw. Ally Ally na wafanyakazi wa Wizara walioko katika afisi hiyo.
Mheshimiwa Abdulla amewapongeza watumishi wa Wizara na taasisi zake kwa kazi kubwa na nzuri wanayoifanya katika kutekeleza majukumu yao.
Naye Mkurugenzi wa Maonyesho hayo amewataka wadau walioshiriki maonesho hayo kutumia fursa hiyo ya kipekee kuuza bidhaa, kutafuta washirika wa kibiashara na kupanua mitandao ya uwekezaji kwa kuwa maonyesho hayo ni jukwaa muhimu la kukuza soko la ndani na nje ya nchi.
Maonesho hayo yanashirikisha zaidi ya taasisi 316 kutoka serikalini, kampuni binafsi na washirika wa kimataifa yatamalizika Januari 16,2026.













Labels:
ZANZIBAR
January 06, 2026

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe.Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Serikali inaendelea kujipanga kuimarisha matumizi ya mifumo ya kidigitali ili kudhibiti vifo vinavyotokana na ajali pamoja na makosa ya barabarani.
Rais Dkt. Mwinyi ametoa kauli hiyo leo tarehe 6 Januari, 2026 alipokutana na Waziri wa Mambo ya Ndani wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.George Simbachawene, aliyefika Ikulu Zanzibar kwa mazungumzo ya kikazi.
Amesema kukamilika kwa mfumo huo wa kidigitali pamoja na matumizi ya taa za usalama barabarani (Traffic Lights) na uwekaji wa rada za kudhibiti kasi, kutasaidia kwa kiasi kikubwa kudhibiti makosa yanayofanyika barabarani, kupunguza vifo vinavyotokana na ajali pamoja na kupunguza gharama za huduma za afya zinazobebwa na Serikali baada ya ajali kutokea.
Akizungumzia suala la unyanyasaji na ukatili wa kijinsia, ikiwemo vitendo vya ubakaji, Rais Dkt. Mwinyi amesema Serikali imechukua hatua madhubuti kudhibiti vitendo hivyo, ikiwemo kuondoa dhamana kwa watuhumiwa wa makosa hayo, pamoja na kuendelea kutoa elimu kwa umma dhidi ya udhalilishaji.
Halikadhalika, akizungumzia matukio ya uhalifu na makosa katika maeneo ya utalii, Rais Dkt. Mwinyi amesema Serikali inaendelea kuchukua juhudi kubwa za kuimarisha usalama katika maeneo hayo, ikiwemo kuwataka wamiliki wa hoteli kuweka kamera za CCTV ili kusaidia kukabiliana na vitendo vya uhalifu.
Rais Dkt. Mwinyi amepongeza ushirikiano uliopo kati ya Wizara ya Mambo ya Ndani na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, hususan katika kuimarisha utendaji wa pamoja wa sekta za Uhamiaji, Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) na Jeshi la Polisi, na kusisitiza kuendelezwa kwa ushirikiano huo.
Kwa upande wake, Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhe.George Simbachawene, ameonesha kuridhishwa na mchango na ushirikiano unaotolewa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuimarisha utendaji wa taasisi zilizo chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani, ikiwemo Uhamiaji, NIDA na Polisi.






SMZ KUIMARISHA MFUMO WA KIDIGITALI KATIKA KUDHIBITI AJALI NA MAKOSA YA BARABARANI | RAIS MWINYI
Written By CCMdijitali on Tuesday, January 6, 2026 | January 06, 2026

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe.Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Serikali inaendelea kujipanga kuimarisha matumizi ya mifumo ya kidigitali ili kudhibiti vifo vinavyotokana na ajali pamoja na makosa ya barabarani.
Rais Dkt. Mwinyi ametoa kauli hiyo leo tarehe 6 Januari, 2026 alipokutana na Waziri wa Mambo ya Ndani wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.George Simbachawene, aliyefika Ikulu Zanzibar kwa mazungumzo ya kikazi.
Amesema kukamilika kwa mfumo huo wa kidigitali pamoja na matumizi ya taa za usalama barabarani (Traffic Lights) na uwekaji wa rada za kudhibiti kasi, kutasaidia kwa kiasi kikubwa kudhibiti makosa yanayofanyika barabarani, kupunguza vifo vinavyotokana na ajali pamoja na kupunguza gharama za huduma za afya zinazobebwa na Serikali baada ya ajali kutokea.
Akizungumzia suala la unyanyasaji na ukatili wa kijinsia, ikiwemo vitendo vya ubakaji, Rais Dkt. Mwinyi amesema Serikali imechukua hatua madhubuti kudhibiti vitendo hivyo, ikiwemo kuondoa dhamana kwa watuhumiwa wa makosa hayo, pamoja na kuendelea kutoa elimu kwa umma dhidi ya udhalilishaji.
Halikadhalika, akizungumzia matukio ya uhalifu na makosa katika maeneo ya utalii, Rais Dkt. Mwinyi amesema Serikali inaendelea kuchukua juhudi kubwa za kuimarisha usalama katika maeneo hayo, ikiwemo kuwataka wamiliki wa hoteli kuweka kamera za CCTV ili kusaidia kukabiliana na vitendo vya uhalifu.
Rais Dkt. Mwinyi amepongeza ushirikiano uliopo kati ya Wizara ya Mambo ya Ndani na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, hususan katika kuimarisha utendaji wa pamoja wa sekta za Uhamiaji, Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) na Jeshi la Polisi, na kusisitiza kuendelezwa kwa ushirikiano huo.
Kwa upande wake, Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhe.George Simbachawene, ameonesha kuridhishwa na mchango na ushirikiano unaotolewa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuimarisha utendaji wa taasisi zilizo chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani, ikiwemo Uhamiaji, NIDA na Polisi.







Labels:
ZANZIBAR
January 04, 2026

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Serikali itaendelea na ujenzi wa masoko ya kisasa katika maeneo mbalimbali ya Zanzibar kwa lengo la kuwawezesha wafanyabiashara kufanya shughuli zao katika mazingira bora, salama na yenye hadhi.
Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo tarehe 4 Januari 2026 alipolizindua Soko la Kisasa la Mbogamboga la Mombasa, lililopo Mkoa wa Mjini Magharibi.
Ameeleza kuwa Serikali inapowahamisha wafanyabiashara kutoka maeneo yao ya awali, hufanya hivyo kwa nia njema ya kujenga masoko yenye viwango na hadhi, pamoja na kuwaandalia mazingira mazuri yatakayochangia ukuaji wa biashara zao na ustawi wa maisha yao.
Rais Dkt. Mwinyi amewahakikishia wananchi kuwa Serikali ipo katika maandalizi ya kujenga soko kubwa na la kisasa katika eneo la Kibanda Maiti, pamoja na uanzishaji wa Bazaar katika Mtaa wa Kwa Hajitumbo, Wilaya ya Mjini, hatua itakayosaidia kudhibiti biashara holela, kuondoa mazingira duni katika masoko na kuzuia ufanyaji wa biashara pembezoni mwa barabara.
Aidha, amesema Serikali itaendelea kutoa mikopo isiyo na riba kwa wafanyabiashara ili kuwawezesha kukuza mitaji yao, huku akitoa wito kwa watakaopewa fursa ya kuliendesha soko hilo jipya kuhakikisha wanalinda miundombinu na kuimarisha usafi wakati wote.
Rais Dkt. Mwinyi ametoa maelekezo maalum kwamba wafanyabiashara wa mwanzo waliopisha ujenzi wa Soko la Mombasa wapewe kipaumbele wakati wa ugawaji wa vizimba vya kufanyia biashara sokoni hapo.
Vilevile, ameushauri Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (ZSSF) kujikita zaidi katika uwekezaji wa miradi mikubwa yenye tija, ikiwemo nishati ya umeme, teksi za baharini na mabasi ya umeme, kufuatia mafanikio yaliyopatikana katika miradi ya nyumba za Makaazi na Masoko.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF), Ndugu Nassor Shaaban, ameishukuru Serikali kwa kuendelea kuiamini taasisi hiyo katika utekelezaji wa miradi ya uwekezaji inayochangia ukuaji wa uchumi na maendeleo ya Zanzibar, ikiwemo ujenzi wa nyumba za Makaazi na Masoko ya kisasa.
Ujenzi wa Soko la Kisasa la Mbogamboga la Mombasa umegharimu jumla ya Shilingi Bilioni 16.6, na umetekelezwa na Kampuni ya RANS.





RAIS MWINYI:SMZ KUENDELEA KUJENGA MASOKO YA KISASA KATIKA KUIMARISHA BIASHARA ZANZIBAR.
Written By CCMdijitali on Sunday, January 4, 2026 | January 04, 2026

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Serikali itaendelea na ujenzi wa masoko ya kisasa katika maeneo mbalimbali ya Zanzibar kwa lengo la kuwawezesha wafanyabiashara kufanya shughuli zao katika mazingira bora, salama na yenye hadhi.
Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo tarehe 4 Januari 2026 alipolizindua Soko la Kisasa la Mbogamboga la Mombasa, lililopo Mkoa wa Mjini Magharibi.
Ameeleza kuwa Serikali inapowahamisha wafanyabiashara kutoka maeneo yao ya awali, hufanya hivyo kwa nia njema ya kujenga masoko yenye viwango na hadhi, pamoja na kuwaandalia mazingira mazuri yatakayochangia ukuaji wa biashara zao na ustawi wa maisha yao.
Rais Dkt. Mwinyi amewahakikishia wananchi kuwa Serikali ipo katika maandalizi ya kujenga soko kubwa na la kisasa katika eneo la Kibanda Maiti, pamoja na uanzishaji wa Bazaar katika Mtaa wa Kwa Hajitumbo, Wilaya ya Mjini, hatua itakayosaidia kudhibiti biashara holela, kuondoa mazingira duni katika masoko na kuzuia ufanyaji wa biashara pembezoni mwa barabara.
Aidha, amesema Serikali itaendelea kutoa mikopo isiyo na riba kwa wafanyabiashara ili kuwawezesha kukuza mitaji yao, huku akitoa wito kwa watakaopewa fursa ya kuliendesha soko hilo jipya kuhakikisha wanalinda miundombinu na kuimarisha usafi wakati wote.
Rais Dkt. Mwinyi ametoa maelekezo maalum kwamba wafanyabiashara wa mwanzo waliopisha ujenzi wa Soko la Mombasa wapewe kipaumbele wakati wa ugawaji wa vizimba vya kufanyia biashara sokoni hapo.
Vilevile, ameushauri Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (ZSSF) kujikita zaidi katika uwekezaji wa miradi mikubwa yenye tija, ikiwemo nishati ya umeme, teksi za baharini na mabasi ya umeme, kufuatia mafanikio yaliyopatikana katika miradi ya nyumba za Makaazi na Masoko.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF), Ndugu Nassor Shaaban, ameishukuru Serikali kwa kuendelea kuiamini taasisi hiyo katika utekelezaji wa miradi ya uwekezaji inayochangia ukuaji wa uchumi na maendeleo ya Zanzibar, ikiwemo ujenzi wa nyumba za Makaazi na Masoko ya kisasa.
Ujenzi wa Soko la Kisasa la Mbogamboga la Mombasa umegharimu jumla ya Shilingi Bilioni 16.6, na umetekelezwa na Kampuni ya RANS.






Labels:
ZANZIBAR
January 01, 2026

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Serikali itaendelea kuwekeza katika ujenzi na uboreshaji wa miundombinu ya michezo kwa lengo la kuifanya Zanzibar kuwa kituo maalum cha utalii wa michezo kitaifa na kimataifa.
Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo tarehe 01 Januari 2026, aliposhiriki Bonanza la 16 la Mazoezi ya Viungo lililoandaliwa na Chama cha Mazoezi ya Viungo Zanzibar (ZABESA), lililofanyika katika Uwanja wa New Amaan Complex, Mkoa wa Mjini Magharibi. Bonanza hilo limehusisha vikundi 165 vya mazoezi kutoka vilabu 25 vya Pemba, 100 vya Unguja na 40 kutoka Tanzania Bara, likiwa na washiriki zaidi ya 500.
Amesema mazoezi ya viungo ni nguzo muhimu ya afya ya mwili na akili, na husaidia kuongeza kinga dhidi ya magonjwa yasiyoambukiza ikiwemo kisukari, shinikizo la damu na magonjwa ya moyo.
Aidha, amebainisha kuwa bonanza la kila mwaka ni jukwaa muhimu la kuwakumbusha wananchi umuhimu wa afya njema kwa maendeleo ya mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla.
Rais Dkt. Mwinyi amewahimiza wananchi kuendelea kushiriki michezo mbalimbali ikiwemo mpira wa miguu, volleyball, riadha pamoja na michezo ya asili ya kitamaduni ili kuimarisha afya zao. Ameeleza pia kuwa Serikali itaendelea kuhimiza mabonanza, matukio ya michezo, ligi na mashindano ya kitaifa na kimataifa ili kuongeza mvuto wa utalii wa michezo Zanzibar.
Amefafanua kuwa michezo ni sekta muhimu inayochangia maendeleo ya utalii na uchumi wa Taifa kwa kuvutia watalii na wawekezaji, kuongeza fursa za ajira kwa vijana na kukuza pato la Taifa. Serikali, kwa kushirikiana na wadau wa michezo, itaendelea kuimarisha miundombinu ili kufikia viwango vya kitaifa na kimataifa na kuendeleza vipaji kuanzia ngazi ya chini hadi ya juu.
Rais Dkt. Mwinyi amesema kupitia programu madhubuti za mafunzo, nidhamu na usimamizi bora, Zanzibar inaweza kuzalisha wanamichezo bora watakaoshindana kimataifa na kuinua hadhi ya Taifa pamoja na kuboresha maisha yao na familia zao. Ameongeza kuwa Serikali imeimarisha kwa kiwango kikubwa miundombinu ya michezo ikiwemo Uwanja wa Amaan Complex, Gombani na Mao Tse Tung, sambamba na ujenzi wa viwanja 17 unaoendelea katika mikoa yote, ambapo baadhi tayari vimekamilika.
Mapema, Rais Dkt. Mwinyi aliwaongoza mamia ya wana mazoezi katika matembezi maalum kutoka Michenzani kupitia Muembe Kisonge hadi Uwanja wa New Amaan Complex, kabla ya kushiriki mazoezi ya pamoja. Amewapongeza ZABESA na wadau wote kwa kufanikisha bonanza hilo na kuwakabidhi vyeti vya shukrani, huku akihimiza kuendelea kuliunga mkono. Aidha, alipata fursa ya kusalimiana na mwanariadha wa kimataifa wa Tanzania, mshindi wa medali ya dhahabu ya mbio za marathon, Alphonce Simbu, aliyeshiriki bonanza hilo.


























ZANZIBAR KUWA KITOVU CHA UTALII WA MICHEZO | RAIS MWINYI
Written By CCMdijitali on Thursday, January 1, 2026 | January 01, 2026

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Serikali itaendelea kuwekeza katika ujenzi na uboreshaji wa miundombinu ya michezo kwa lengo la kuifanya Zanzibar kuwa kituo maalum cha utalii wa michezo kitaifa na kimataifa.
Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo tarehe 01 Januari 2026, aliposhiriki Bonanza la 16 la Mazoezi ya Viungo lililoandaliwa na Chama cha Mazoezi ya Viungo Zanzibar (ZABESA), lililofanyika katika Uwanja wa New Amaan Complex, Mkoa wa Mjini Magharibi. Bonanza hilo limehusisha vikundi 165 vya mazoezi kutoka vilabu 25 vya Pemba, 100 vya Unguja na 40 kutoka Tanzania Bara, likiwa na washiriki zaidi ya 500.
Amesema mazoezi ya viungo ni nguzo muhimu ya afya ya mwili na akili, na husaidia kuongeza kinga dhidi ya magonjwa yasiyoambukiza ikiwemo kisukari, shinikizo la damu na magonjwa ya moyo.
Aidha, amebainisha kuwa bonanza la kila mwaka ni jukwaa muhimu la kuwakumbusha wananchi umuhimu wa afya njema kwa maendeleo ya mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla.
Rais Dkt. Mwinyi amewahimiza wananchi kuendelea kushiriki michezo mbalimbali ikiwemo mpira wa miguu, volleyball, riadha pamoja na michezo ya asili ya kitamaduni ili kuimarisha afya zao. Ameeleza pia kuwa Serikali itaendelea kuhimiza mabonanza, matukio ya michezo, ligi na mashindano ya kitaifa na kimataifa ili kuongeza mvuto wa utalii wa michezo Zanzibar.
Amefafanua kuwa michezo ni sekta muhimu inayochangia maendeleo ya utalii na uchumi wa Taifa kwa kuvutia watalii na wawekezaji, kuongeza fursa za ajira kwa vijana na kukuza pato la Taifa. Serikali, kwa kushirikiana na wadau wa michezo, itaendelea kuimarisha miundombinu ili kufikia viwango vya kitaifa na kimataifa na kuendeleza vipaji kuanzia ngazi ya chini hadi ya juu.
Rais Dkt. Mwinyi amesema kupitia programu madhubuti za mafunzo, nidhamu na usimamizi bora, Zanzibar inaweza kuzalisha wanamichezo bora watakaoshindana kimataifa na kuinua hadhi ya Taifa pamoja na kuboresha maisha yao na familia zao. Ameongeza kuwa Serikali imeimarisha kwa kiwango kikubwa miundombinu ya michezo ikiwemo Uwanja wa Amaan Complex, Gombani na Mao Tse Tung, sambamba na ujenzi wa viwanja 17 unaoendelea katika mikoa yote, ambapo baadhi tayari vimekamilika.
Mapema, Rais Dkt. Mwinyi aliwaongoza mamia ya wana mazoezi katika matembezi maalum kutoka Michenzani kupitia Muembe Kisonge hadi Uwanja wa New Amaan Complex, kabla ya kushiriki mazoezi ya pamoja. Amewapongeza ZABESA na wadau wote kwa kufanikisha bonanza hilo na kuwakabidhi vyeti vya shukrani, huku akihimiza kuendelea kuliunga mkono. Aidha, alipata fursa ya kusalimiana na mwanariadha wa kimataifa wa Tanzania, mshindi wa medali ya dhahabu ya mbio za marathon, Alphonce Simbu, aliyeshiriki bonanza hilo.



























Labels:
ZANZIBAR



