MAKAMU WA RAIS ASHIRIKI MKUTANO WA 45 WA SADC
RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN APONGEZWA KWA KUSIMAMIA AMANI NA UTULIVU SADC. Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Phi...

Latest Post
August 17, 2025
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amemwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Mkutano wa 45 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) uliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Ivato, Antananarivo nchini Madagascar.
Katika Mkutano huo Rais wa Jamhuri ya Zimbabwe Mhe. Emmerson Mnangagwa amekabidhi Uenyekiti wa SADC kwa Rais wa Jamhuri ya Madagascar Mhe. Andry Nirina Rajoelina utakaodumu kwa kipindi cha mwaka mmoja. Vilevile Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imekabidhi uenyekiti wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama (SADC Organ Troika) kwa Jamhuri ya Malawi mara baada ya kuhitimisha uongozi wa mwaka mmoja wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ulioanza Agosti 2024.
Akisoma hotuba ya ufunguzi Mwenyekiti wa SADC anayemaliza muda wake, Rais wa Jamhuri ya Zimbabwe Mhe. Emmerson Mnangagwa pamoja na mambo mengine amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuiongoza vema Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama na kuhakikisha amani na utulivu katika Jumuiya ya Maendeleo Kusini Mwa Afrika.
Mkutano huo umejadili hatua iliyofikiwa katika utekelezaji wa Mpango Mkakati Elekezi wa kanda, kuanisha mafanikio na changamoto za utekelezaji. Utekelezaji umejikita katika nguzo kuu nne zikiongozwa na nguzo kuu ya Amani, Usalama na Utawala wa Kidemokrasia. Nguzo nyingine ni maendeleo ya viwanda na utangamano wa masoko, Maendeleo ya miundombinu katika kuchagiza utangamano pamoja na maendeleo ya kijamii na rasilimali watu.
Miongoni mwa mafanikio yaliyojadiliwa ambayo yamepatikana ni pamoja na kupungua kwa matukio ya ugaidi, kuimarika kwa demokrasia katika Kanda kupitia chaguzi huru na haki, kuongezeka kwa huduma za kifedha, kuongezeka kwa thamani ya mauzo ya bidhaa za viwanda na kuongezeka kwa miamala iliyofanyika kupitia mfumo wa malipo wa kikanda (Real Time Gross Settlement – RTGS).
Katika Mkutano huo washindi mbalimbali wa Tuzo zinazotolewa na SADC wametangazwa ikiwemo Mwanafunzi wa Shule ya Sekondari kutoka nchini Tanzania Crispin Kamugisha aliyetangazwa mshindi katika uandishi wa insha na kuzawadiwa dola elfu moja mia tano.
Kauli mbiu ya Mkutano wa 45 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) ni “Kuendeleza Viwanda, Mageuzi ya Kilimo na Matumizi bora ya Nishati kwa ustahimilivu wa kanda ya SADC” (Advancing Industrialisation, Agricultural Transformation, and Energy Transition for a Resilient SADC).
Imetolewa na
Ofisi ya Makamu wa Rais
17 Agosti 2025
Madagascar.













MAKAMU WA RAIS ASHIRIKI MKUTANO WA 45 WA SADC
Written By CCMdijitali on Sunday, August 17, 2025 | August 17, 2025
RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN APONGEZWA KWA KUSIMAMIA AMANI NA UTULIVU SADC.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amemwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Mkutano wa 45 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) uliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Ivato, Antananarivo nchini Madagascar.
Katika Mkutano huo Rais wa Jamhuri ya Zimbabwe Mhe. Emmerson Mnangagwa amekabidhi Uenyekiti wa SADC kwa Rais wa Jamhuri ya Madagascar Mhe. Andry Nirina Rajoelina utakaodumu kwa kipindi cha mwaka mmoja. Vilevile Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imekabidhi uenyekiti wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama (SADC Organ Troika) kwa Jamhuri ya Malawi mara baada ya kuhitimisha uongozi wa mwaka mmoja wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ulioanza Agosti 2024.
Akisoma hotuba ya ufunguzi Mwenyekiti wa SADC anayemaliza muda wake, Rais wa Jamhuri ya Zimbabwe Mhe. Emmerson Mnangagwa pamoja na mambo mengine amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuiongoza vema Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama na kuhakikisha amani na utulivu katika Jumuiya ya Maendeleo Kusini Mwa Afrika.
Mkutano huo umejadili hatua iliyofikiwa katika utekelezaji wa Mpango Mkakati Elekezi wa kanda, kuanisha mafanikio na changamoto za utekelezaji. Utekelezaji umejikita katika nguzo kuu nne zikiongozwa na nguzo kuu ya Amani, Usalama na Utawala wa Kidemokrasia. Nguzo nyingine ni maendeleo ya viwanda na utangamano wa masoko, Maendeleo ya miundombinu katika kuchagiza utangamano pamoja na maendeleo ya kijamii na rasilimali watu.
Miongoni mwa mafanikio yaliyojadiliwa ambayo yamepatikana ni pamoja na kupungua kwa matukio ya ugaidi, kuimarika kwa demokrasia katika Kanda kupitia chaguzi huru na haki, kuongezeka kwa huduma za kifedha, kuongezeka kwa thamani ya mauzo ya bidhaa za viwanda na kuongezeka kwa miamala iliyofanyika kupitia mfumo wa malipo wa kikanda (Real Time Gross Settlement – RTGS).
Katika Mkutano huo washindi mbalimbali wa Tuzo zinazotolewa na SADC wametangazwa ikiwemo Mwanafunzi wa Shule ya Sekondari kutoka nchini Tanzania Crispin Kamugisha aliyetangazwa mshindi katika uandishi wa insha na kuzawadiwa dola elfu moja mia tano.
Kauli mbiu ya Mkutano wa 45 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) ni “Kuendeleza Viwanda, Mageuzi ya Kilimo na Matumizi bora ya Nishati kwa ustahimilivu wa kanda ya SADC” (Advancing Industrialisation, Agricultural Transformation, and Energy Transition for a Resilient SADC).
Imetolewa na
Ofisi ya Makamu wa Rais
17 Agosti 2025
Madagascar.














Labels:
KIMATAIFA
August 12, 2025
Na OR-TAMISEMI, TARIME
12/08/2025
Mkurugenzi wa Idara ya Elimu, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Dkt. Emmanuel Shindika, amewakabidhi bendera ya taifa wanamichezo wa Tanzania watakaoshiriki Mashindano ya Michezo ya Shule za Sekondari Afrika Mashariki (FEASSA) 2025, huku akiwaasa kudumisha nidhamu, utulivu na mshikamano kipindi chote cha mashindano hayo.
Akizungumza kabla ya kuwakabidhi bendera hiyo, Dkt. Shindika alisisitiza kuwa wanamichezo hao wanabeba taswira ya taifa, hivyo wanapaswa kuonesha sifa kuu za Tanzania ambazo ni heshima, amani na mshikamano.
“Niwasihi mrejee na vikombe vingi ili tumthibitishie Rais wetu, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kuwa tulistahili kushiriki mashindano haya,” alisema Dkt. Shindika.
Aidha, aliwataka kuongeza bidii katika michezo yao, akiwakumbusha kuwa kuibeba bendera ya taifa ni kuibeba nchi, na macho ya Watanzania yote yako kwao wakitarajia kuona wakifanya vizuri na kuibua heshima kwa taifa.
Kwa upande wao, wanamichezo hao walieleza kujiamini kuwa mwaka huu watafanya vizuri zaidi na kurejea na medali nyingi kuliko mwaka jana, ambapo walishiriki FEASSA nchini Uganda na kufanikwa kurejea na medali 58 pekee.
Wanamichezo hao wameondoka kupitia mpaka wa Sirari, mkoani Mara, baada ya kuweka kambi ya mazoezi kwa siku kadhaa katika Chuo cha Ualimu Tarime, wakijiandaa kushindana na wenzao kutoka nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, kituo chao cha mashindano kikiwa Kakamega, Kenya.
TANZANIA YAAPA KUNG’ARA FEASSA 2025 KAKAMEGA
Written By CCMdijitali on Tuesday, August 12, 2025 | August 12, 2025
Na OR-TAMISEMI, TARIME
12/08/2025
Mkurugenzi wa Idara ya Elimu, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Dkt. Emmanuel Shindika, amewakabidhi bendera ya taifa wanamichezo wa Tanzania watakaoshiriki Mashindano ya Michezo ya Shule za Sekondari Afrika Mashariki (FEASSA) 2025, huku akiwaasa kudumisha nidhamu, utulivu na mshikamano kipindi chote cha mashindano hayo.
Akizungumza kabla ya kuwakabidhi bendera hiyo, Dkt. Shindika alisisitiza kuwa wanamichezo hao wanabeba taswira ya taifa, hivyo wanapaswa kuonesha sifa kuu za Tanzania ambazo ni heshima, amani na mshikamano.
“Niwasihi mrejee na vikombe vingi ili tumthibitishie Rais wetu, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kuwa tulistahili kushiriki mashindano haya,” alisema Dkt. Shindika.
Aidha, aliwataka kuongeza bidii katika michezo yao, akiwakumbusha kuwa kuibeba bendera ya taifa ni kuibeba nchi, na macho ya Watanzania yote yako kwao wakitarajia kuona wakifanya vizuri na kuibua heshima kwa taifa.
Kwa upande wao, wanamichezo hao walieleza kujiamini kuwa mwaka huu watafanya vizuri zaidi na kurejea na medali nyingi kuliko mwaka jana, ambapo walishiriki FEASSA nchini Uganda na kufanikwa kurejea na medali 58 pekee.
Wanamichezo hao wameondoka kupitia mpaka wa Sirari, mkoani Mara, baada ya kuweka kambi ya mazoezi kwa siku kadhaa katika Chuo cha Ualimu Tarime, wakijiandaa kushindana na wenzao kutoka nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, kituo chao cha mashindano kikiwa Kakamega, Kenya.
Labels:
MICHEZO
August 11, 2025
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amesema ni muhimu Jeshi la Polisi kuimarisha ushirikiano wa karibu na wadau wote wa uchaguzi, hatua ambayo itasaidia kuhakikisha kila mdau anatendewa haki, na kuondoa tofauti zinazoweza kusababisha migongano.
Makamu wa Rais ametoa wito huo wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi unaofanyika katika ukumbi wa Chuo Cha Polisi (CCP) Moshi Mkoani Kilimanjaro. Amesema Baadhi ya maeneo muhimu ya ushirikiano ni pamoja na kuhakikisha mikutano ya kampeni inafanyika kwenye maeneo yaliyoruhusiwa na ndani ya muda uliopangwa, Kuzuia maandamano yasiyo na kibali, kuimarisha ulinzi wa wagombea na viongozi wa vyama vya kisiasa, bila kujali vyama vyao au itikadi zao pamoja na kudhibiti misongamano mikubwa ya watu ili kuhakikisha shughuli nyingine za kijamii na kiuchumi zinaendelea bila usumbufu.
Pia Makamu wa Rais amelitaka Jeshi la Polisi kushirikiana kwa karibu na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) pamoja na taasisi nyingine za Serikali ili kujiandaa vyema kutumia Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) katika kufuatilia taarifa mbalimbali zenye mlengo wa uchochezi, zinazotolewa kupitia mitandao ya kijamii na vyombo vingine vya habari. Amesema kwa kutumia teknolojia za akili bandia baadhi ya watu wanaweza kusambaza picha au video za uongo za wagombea wa vyama vya siasa, jambo linaloweza kuleta madhara makubwa kwa amani na utulivu wa jamii.
Makamu wa Rais amesema Jeshi la Polisi linapaswa kujiandaa kikamilifu kufanya doria ya mtandao ili kubaini na kuchambua machapisho, picha, na video zenye viashiria vya uvunjifu wa sheria, na kuchukua hatua za kisheria kwa haraka.
Vilevile, Makamu wa Rais amesisitiza Jeshi la Polisi lishirikiane kwa karibu na wadau wengine wa uchaguzi, ikiwemo TAKUKURU na vyombo vingine vya usalama, ili kudhibiti vitendo vya Rushwa katika kipindi cha uchaguzi. Ameongeza kwamba ni muhimu Jeshi la Polisi likijumuisha Polisi Jamii lishirikiane kwa karibu na TAMISEMI katika kusimamia usalama, hasa katika ngazi za Kata, Shehia, Vijiji na Mitaa.
Makamu wa Rais amelitaka Jeshi la Polisi kusimamia vema utekelezaji wa sheria ya uchaguzi na sheria nyingine za nchi. Amesema ni wajibu wa Jeshi la Polisi na wadau wengine wa uchaguzi, kuielewa vizuri Sheria ya Uchaguzi na kusimamia utekelezaji wake, ili kuepuka kuonea watu na kuvuruga uchaguzi. Aidha ametoa wito kwa wananchi na viongozi wa vyama vya siasa kuepuka kujichukulia sheria mkononi pale wanapoona ukiukwaji wa sheria za uchaguzi, na badala yake watoe taarifa kwenye vyombo vya sheria kwa hatua stahiki.
Halikadhalika Makamu wa Rais amesema katika kuelekea Uchaguzi Mkuu ni muhimu kuendelea kuwajengea uwezo maafisa na askari kwa kuwapatia mafunzo ya utayari, uadilifu, na ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao. Amempongeza Mkuu wa Jeshi la Polisi kwa kuendelea kuhakikisha askari wa Jeshi la Polisi wanapata mafunzo ya kitaalam ya kuwajengea uwezo na utayari.
Kwa upande wake Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Daniel Sillo ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuiwezesha Wizara kibajeti,vifaa na vitendea kazi vya kisasa ambavyo vimesaidia kuimarisha na kuboresha utendaji wa Jeshi la Polisi na vyombo vya usalama vilivyopo chini ya Wizara hiyo.
Ameishukuru Serikali kwa kutoa vibali vya ajira na upandishaji vyeo hali inayosaidia katika udhibiti wa uhalifu nchini na kuongeza ari ya utendaji kazi kwa maafisa na askari ndani ya Wizara. Amesema Wizara na vyombo vyote vya usalama vilivyo chini yake itaendelea kufanya kazi kwa ushirikiano, nidhamu, weledi na uadilifu ili kuhakikisha nchi inaendelea kuwa salama yenye amani na utulivu na mazingira mazuri kwa ajili maendeleo na uchumi endelevu wa Taifa.
Awali akitoa taarifa ya Mkutano huo, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Camillus Wambura amesema Jeshi la Polisi limejipanga kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa amani na utulivu na kuwasihi Watanzania wawe na uhakika na utulivu wakiamini kipindi hicho chote kitapita katika hali ya usalama na utulivu wa hali ya juu pamoja na Serikali itakayochaguliwa itaingia madarakani bila kikwazo.
Amesema kauli mbiu inayoongoza mkutano huo inaweka msisitizo katika kusimamia amani na utulivu wakati wote wa mchakato wa uchaguzi ili kuhakikisha wananchi wanashiriki kwa utulivu, uhuru na amani bila kuwa na vikwazo vya aina yeyote. Pia amesema inasisitiza na kuweka jukumu kwa kila mwananchi kuhakikisha analinda amani usalama na utulivu kipindi cha kabla, wakati na baada ya uchaguzi.
Imetolewa na
Ofisi ya Makamu wa Rais
11 Agosti 2025
Moshi – Kilimanjaro.










Makamu wa Rais afungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi
Written By CCMdijitali on Monday, August 11, 2025 | August 11, 2025
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amesema ni muhimu Jeshi la Polisi kuimarisha ushirikiano wa karibu na wadau wote wa uchaguzi, hatua ambayo itasaidia kuhakikisha kila mdau anatendewa haki, na kuondoa tofauti zinazoweza kusababisha migongano.
Makamu wa Rais ametoa wito huo wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi unaofanyika katika ukumbi wa Chuo Cha Polisi (CCP) Moshi Mkoani Kilimanjaro. Amesema Baadhi ya maeneo muhimu ya ushirikiano ni pamoja na kuhakikisha mikutano ya kampeni inafanyika kwenye maeneo yaliyoruhusiwa na ndani ya muda uliopangwa, Kuzuia maandamano yasiyo na kibali, kuimarisha ulinzi wa wagombea na viongozi wa vyama vya kisiasa, bila kujali vyama vyao au itikadi zao pamoja na kudhibiti misongamano mikubwa ya watu ili kuhakikisha shughuli nyingine za kijamii na kiuchumi zinaendelea bila usumbufu.
Pia Makamu wa Rais amelitaka Jeshi la Polisi kushirikiana kwa karibu na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) pamoja na taasisi nyingine za Serikali ili kujiandaa vyema kutumia Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) katika kufuatilia taarifa mbalimbali zenye mlengo wa uchochezi, zinazotolewa kupitia mitandao ya kijamii na vyombo vingine vya habari. Amesema kwa kutumia teknolojia za akili bandia baadhi ya watu wanaweza kusambaza picha au video za uongo za wagombea wa vyama vya siasa, jambo linaloweza kuleta madhara makubwa kwa amani na utulivu wa jamii.
Makamu wa Rais amesema Jeshi la Polisi linapaswa kujiandaa kikamilifu kufanya doria ya mtandao ili kubaini na kuchambua machapisho, picha, na video zenye viashiria vya uvunjifu wa sheria, na kuchukua hatua za kisheria kwa haraka.
Vilevile, Makamu wa Rais amesisitiza Jeshi la Polisi lishirikiane kwa karibu na wadau wengine wa uchaguzi, ikiwemo TAKUKURU na vyombo vingine vya usalama, ili kudhibiti vitendo vya Rushwa katika kipindi cha uchaguzi. Ameongeza kwamba ni muhimu Jeshi la Polisi likijumuisha Polisi Jamii lishirikiane kwa karibu na TAMISEMI katika kusimamia usalama, hasa katika ngazi za Kata, Shehia, Vijiji na Mitaa.
Makamu wa Rais amelitaka Jeshi la Polisi kusimamia vema utekelezaji wa sheria ya uchaguzi na sheria nyingine za nchi. Amesema ni wajibu wa Jeshi la Polisi na wadau wengine wa uchaguzi, kuielewa vizuri Sheria ya Uchaguzi na kusimamia utekelezaji wake, ili kuepuka kuonea watu na kuvuruga uchaguzi. Aidha ametoa wito kwa wananchi na viongozi wa vyama vya siasa kuepuka kujichukulia sheria mkononi pale wanapoona ukiukwaji wa sheria za uchaguzi, na badala yake watoe taarifa kwenye vyombo vya sheria kwa hatua stahiki.
Halikadhalika Makamu wa Rais amesema katika kuelekea Uchaguzi Mkuu ni muhimu kuendelea kuwajengea uwezo maafisa na askari kwa kuwapatia mafunzo ya utayari, uadilifu, na ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao. Amempongeza Mkuu wa Jeshi la Polisi kwa kuendelea kuhakikisha askari wa Jeshi la Polisi wanapata mafunzo ya kitaalam ya kuwajengea uwezo na utayari.
Kwa upande wake Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Daniel Sillo ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuiwezesha Wizara kibajeti,vifaa na vitendea kazi vya kisasa ambavyo vimesaidia kuimarisha na kuboresha utendaji wa Jeshi la Polisi na vyombo vya usalama vilivyopo chini ya Wizara hiyo.
Ameishukuru Serikali kwa kutoa vibali vya ajira na upandishaji vyeo hali inayosaidia katika udhibiti wa uhalifu nchini na kuongeza ari ya utendaji kazi kwa maafisa na askari ndani ya Wizara. Amesema Wizara na vyombo vyote vya usalama vilivyo chini yake itaendelea kufanya kazi kwa ushirikiano, nidhamu, weledi na uadilifu ili kuhakikisha nchi inaendelea kuwa salama yenye amani na utulivu na mazingira mazuri kwa ajili maendeleo na uchumi endelevu wa Taifa.
Awali akitoa taarifa ya Mkutano huo, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Camillus Wambura amesema Jeshi la Polisi limejipanga kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa amani na utulivu na kuwasihi Watanzania wawe na uhakika na utulivu wakiamini kipindi hicho chote kitapita katika hali ya usalama na utulivu wa hali ya juu pamoja na Serikali itakayochaguliwa itaingia madarakani bila kikwazo.
Amesema kauli mbiu inayoongoza mkutano huo inaweka msisitizo katika kusimamia amani na utulivu wakati wote wa mchakato wa uchaguzi ili kuhakikisha wananchi wanashiriki kwa utulivu, uhuru na amani bila kuwa na vikwazo vya aina yeyote. Pia amesema inasisitiza na kuweka jukumu kwa kila mwananchi kuhakikisha analinda amani usalama na utulivu kipindi cha kabla, wakati na baada ya uchaguzi.
Mkutano huo wa siku tano kuanzia tarehe 11-15 Agosti 2025 unaongozwa na kauli mbiu isemayo “Amani, Utulivu na Usalama kabla, wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu 2025 ni jukumu letu sote”
Imetolewa na
Ofisi ya Makamu wa Rais
11 Agosti 2025
Moshi – Kilimanjaro.










Labels:
KITAIFA
August 11, 2025
Akizungumza katika ibada ya mazishi, Waziri Mkuu amewataka Watanzania kuenzi mema yote yaliyofanywa na Hayati Ndugai enzi za uhai wake, akisema mchango wake katika uongozi wa Bunge na Taifa kwa ujumla utabaki kuwa kumbukumbu muhimu kwa vizazi vijavyo.
Aidha, Waziri Mkuu ameeleza kuwa hayati Ndugai alikuwa mlinzi wa taratibu za Bunge na mshirika wa karibu katika kuimarisha ushirikiano kati ya Bunge na Serikali kwa maslahi mapana ya Taifa, akisisitiza mawasiliano ya uwazi, mshikamano na mwelekeo wa pamoja wa utekelezaji wa ajenda za kitaifa.
Vilevile, Mheshimiwa Majaliwa amemtaja hayati Ndugai kama kiongozi mwenye weledi, uadilifu, unyenyekevu, na mchapakazi ambaye alibeba heshima ya mkoa wa Dodoma na jimbo la Kongwa kupitia uongozi na siasa za uwajibikaji.
Kwa upande wake, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko, ametoa salamu za pole kwa familia ya marehemu, wananchi wa Kongwa na Watanzania wote kwa ujumla kutokana na msiba wa hayati Ndugai.
Naye, Spika wa Bunge Dkt. Tulia Ackson amesema kuwa wanaamini katika kumuenzi hayati Ndugai na watamkumbuka daima kwa kuendeleza misingi pamoja na mambo mema yote aliyoyatenda wakati wa uhai wake.
Mazishi ya Hayati Ndugai yamehudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Katibu Mkuu Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhandisi Zena Saidi, Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara, John Mongela, Waziri Mkuu Mstaafu Mizengo Pinda, viongozi wengine kitaifa, ndugu, jamaa na wananchi kutoka maeneo mbalimbali.
Hayati Job Ndugai alifariki agosti 06, 2025 jijini Dodoma kwa Shinikizo la damu lililoshuka sana.








WAZIRI MKUU AMWAKILISHA RAIS DKT. SAMIA MAZISHI YA HAYATI NDUGAI
- Asema aliimarisha ushirikiano kati ya Bunge na Serikali
- Atoa rai kwa Watanzania kuenzi mema yote aliyoyafanya enzi za uhai wake
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Agosti 11, 2025 amemwakilisha Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi ya Spika mstaafu wa Bunge la Tanzania, Job Yustino Ndugai, yaliyofanyika shambani kwake, kijiji cha Msunjulile, wilayani Kongwa mkoani Dodoma.
Akizungumza katika ibada ya mazishi, Waziri Mkuu amewataka Watanzania kuenzi mema yote yaliyofanywa na Hayati Ndugai enzi za uhai wake, akisema mchango wake katika uongozi wa Bunge na Taifa kwa ujumla utabaki kuwa kumbukumbu muhimu kwa vizazi vijavyo.
Amesema kuwa akiwa mwakilishi wa wananchi wa Kongwa, hayati Ndugai ametoa mchango mkubwa katika kipindi cha miaka 20 ya utumishi wake, na kwamba wote ni mashuhuda wa maendeleo makubwa yaliyopatikana katika sekta mbalimbali za maendeleo pamoja na huduma za kijamii. “Serikali itaendelea kumuenzi kwa yale yote aliyoyafanya kwa wanaKongwa”
Aidha, Waziri Mkuu ameeleza kuwa hayati Ndugai alikuwa mlinzi wa taratibu za Bunge na mshirika wa karibu katika kuimarisha ushirikiano kati ya Bunge na Serikali kwa maslahi mapana ya Taifa, akisisitiza mawasiliano ya uwazi, mshikamano na mwelekeo wa pamoja wa utekelezaji wa ajenda za kitaifa.
Vilevile, Mheshimiwa Majaliwa amemtaja hayati Ndugai kama kiongozi mwenye weledi, uadilifu, unyenyekevu, na mchapakazi ambaye alibeba heshima ya mkoa wa Dodoma na jimbo la Kongwa kupitia uongozi na siasa za uwajibikaji.
Pia, Waziri Mkuu amesema kuwa Serikali itasimamia utekelezaji wa maagizo yaliyotolewa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia ya kukamilishwa kwa masuala yote yaliyoanzishwa na Hayati Ndugai, pamoja na kuendeleza makumbusho ya Kongwa ikiwa ni kielelezo cha kupigania uhuru kwa nchi za kusini mwa afrika. “Tutasimamia agizo hili kwa ukamilifu.”
Kwa upande wake, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko, ametoa salamu za pole kwa familia ya marehemu, wananchi wa Kongwa na Watanzania wote kwa ujumla kutokana na msiba wa hayati Ndugai.
Naye, Spika wa Bunge Dkt. Tulia Ackson amesema kuwa wanaamini katika kumuenzi hayati Ndugai na watamkumbuka daima kwa kuendeleza misingi pamoja na mambo mema yote aliyoyatenda wakati wa uhai wake.
Mazishi ya Hayati Ndugai yamehudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Katibu Mkuu Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhandisi Zena Saidi, Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara, John Mongela, Waziri Mkuu Mstaafu Mizengo Pinda, viongozi wengine kitaifa, ndugu, jamaa na wananchi kutoka maeneo mbalimbali.
Hayati Job Ndugai alifariki agosti 06, 2025 jijini Dodoma kwa Shinikizo la damu lililoshuka sana.









Labels:
KITAIFA
August 07, 2025
Na Mwandishi Wetu – Dar es Salaam
Aliyewahi kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO), Assah Mwambene, pamoja na mpiga picha wa zamani wa Rais, Ikulu, Fredrick Maro, wamekabidhiwa rasmi Vitambulisho vyao vya Uandishi wa Habari (Presscard) leo tarehe 07 Agosti 2025, baada ya kukidhi vigezo vilivyowekwa kwa mujibu wa Sheria.
Zoezi hilo limefanyika katika Ofisi za Bodi zilizopo Mtaa wa Jamhuri, jijini Dar es Salaam na kuongozwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa JAB, Wakili Patrick Kipangula.
Akizungumza mara baada ya kuwakabidhi vitambulisho hivyo, Wakili Kipangula alibainisha kuwa Mwambene na Maro wamefuata utaratibu wa kisheria, ikiwa ni pamoja na kujisajili, kuthibitisha taaluma zao na kuwasilisha nyaraka zilizotakiwa.
“Hili ni zoezi endelevu. Waandishi wote wa habari nchini wanatakiwa kuwa na Presscard inayotolewa na Bodi ya Ithibati ili kuendesha shughuli zao za kihabari kihalali na kuzingatia maadili ya taaluma na Sheria,” alisema Kipangula.
Kwa mujibu wa Sheria ya Huduma za Habari ya Mwaka 2016, kifungu cha 19 (1), mtu yeyote anayetaka kufanya kazi za kihabari ni lazima awe amesajiliwa rasmi na Bodi, kuthibitishwa na kupewa kitambulisho kinachotambulika na Serikali. Vinginevyo, mtu anayejihusisha na shughuli za kihabari bila kuthibitishwa kisheria anakuwa anatenda kosa.
Assah Mwambene, ambaye pia amewahi kuhudumu kama Mkurugenzi wa Habari katika Ubalozi wa Tanzania nchini Ufaransa, ni mmoja wa Waandishi wa habari wenye uzoefu mpana katika sekta ya mawasiliano na diplomasia ya umma. Fredrick Maro pia ni mpiga picha maarufu aliyekuwa karibu na taasisi ya Urais kwa miaka kadhaa, na mchango wake umetambuliwa mara nyingi katika vyombo vya habari na kumbukumbu za taifa.
Wakati huo huo, Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari imeendelea na kampeni ya kuwasisitiza waandishi wote wanaofanya kazi katika maeneo mbalimbali kuhakikisha wanajisajili, kuthibitishwa, na kufanya kazi kwa kufuata maadili ya taaluma yao.
“Tunapenda kuona taaluma ya habari ikiheshimika, na hilo linaanza na kila mwandishi kutekeleza wajibu wake kwa mujibu wa Sheria. Hii inalinda hadhi ya taaluma na maslahi mapana ya taifa,” aliongeza Wakili Kipangula.
Mpaka sasa ya waandishi wa habari 3,240 wameshajisajili, huku idadi hiyo ikitarajiwa kuongezeka kutokana na mabadiliko yanayoendelea ndani ya vyombo vya habari na utoaji wa elimu kuhusu umuhimu wa Ithibati.




MWAMBENE, MARO WAKABIDHIWA VITAMBULISHO RASMI VYA UANDISHI WA HABARI
Written By CCMdijitali on Thursday, August 7, 2025 | August 07, 2025
Na Mwandishi Wetu – Dar es Salaam
Aliyewahi kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO), Assah Mwambene, pamoja na mpiga picha wa zamani wa Rais, Ikulu, Fredrick Maro, wamekabidhiwa rasmi Vitambulisho vyao vya Uandishi wa Habari (Presscard) leo tarehe 07 Agosti 2025, baada ya kukidhi vigezo vilivyowekwa kwa mujibu wa Sheria.
Zoezi hilo limefanyika katika Ofisi za Bodi zilizopo Mtaa wa Jamhuri, jijini Dar es Salaam na kuongozwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa JAB, Wakili Patrick Kipangula.
Akizungumza mara baada ya kuwakabidhi vitambulisho hivyo, Wakili Kipangula alibainisha kuwa Mwambene na Maro wamefuata utaratibu wa kisheria, ikiwa ni pamoja na kujisajili, kuthibitisha taaluma zao na kuwasilisha nyaraka zilizotakiwa.
“Hili ni zoezi endelevu. Waandishi wote wa habari nchini wanatakiwa kuwa na Presscard inayotolewa na Bodi ya Ithibati ili kuendesha shughuli zao za kihabari kihalali na kuzingatia maadili ya taaluma na Sheria,” alisema Kipangula.
Kwa mujibu wa Sheria ya Huduma za Habari ya Mwaka 2016, kifungu cha 19 (1), mtu yeyote anayetaka kufanya kazi za kihabari ni lazima awe amesajiliwa rasmi na Bodi, kuthibitishwa na kupewa kitambulisho kinachotambulika na Serikali. Vinginevyo, mtu anayejihusisha na shughuli za kihabari bila kuthibitishwa kisheria anakuwa anatenda kosa.
Assah Mwambene, ambaye pia amewahi kuhudumu kama Mkurugenzi wa Habari katika Ubalozi wa Tanzania nchini Ufaransa, ni mmoja wa Waandishi wa habari wenye uzoefu mpana katika sekta ya mawasiliano na diplomasia ya umma. Fredrick Maro pia ni mpiga picha maarufu aliyekuwa karibu na taasisi ya Urais kwa miaka kadhaa, na mchango wake umetambuliwa mara nyingi katika vyombo vya habari na kumbukumbu za taifa.
Wakati huo huo, Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari imeendelea na kampeni ya kuwasisitiza waandishi wote wanaofanya kazi katika maeneo mbalimbali kuhakikisha wanajisajili, kuthibitishwa, na kufanya kazi kwa kufuata maadili ya taaluma yao.
“Tunapenda kuona taaluma ya habari ikiheshimika, na hilo linaanza na kila mwandishi kutekeleza wajibu wake kwa mujibu wa Sheria. Hii inalinda hadhi ya taaluma na maslahi mapana ya taifa,” aliongeza Wakili Kipangula.
Mpaka sasa ya waandishi wa habari 3,240 wameshajisajili, huku idadi hiyo ikitarajiwa kuongezeka kutokana na mabadiliko yanayoendelea ndani ya vyombo vya habari na utoaji wa elimu kuhusu umuhimu wa Ithibati.





Labels:
KITAIFA
August 07, 2025
Tanzania kuziunga mkono Nchi Zinazoendelea Zisizo na Mlango wa Bahari
Tanzania kuziunga mkono Nchi Zinazoendelea Zisizo na Mlango wa Bahari, Yatoa Wito kuutumia Mpango wa Awaza Kuwa Ramani ya Mageuzi
Tanzania imeeleza kuziunga mkono nchi zinazoendelea zisizo na mlango wa bahari kutimiza matarajio na kukabiliana na changamoto zinazozikabili na kutoa wito wa kuchukua hatua za pamoja na kuufanya Mpango wa Awaza kubadilisha ahadi kuwa matokeo halisi.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius Kahyarara, ametoa kauli hiyo alipozungumza tarehe 6 Agosti 2025 kwenye Mkutano wa Tatu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Nchi Zinazoendelea Zisizo na Bahari unaofanyika mjini Awaza, Turkmenistan.
Prof. Godius Kahyarara amesisitiza juu ya umuhimu wa kubadilisha Mpango wa Awaza kutoka kuwa tamko la Mkutano huo na kuufanya kuwa ramani ya kuelekea kwenya matokeo chanya ya maendeleo jumuishi.
“Tanzania si nchi isiyo na bahari, lakini nafasi yetu ya kimkakati kama nchi yenye Bahari na njia ya usafiri inatufanya kuwa kitovu cha muunganiko wa kikanda katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kusini mwa Afrika. Bandari zetu, njia za usafirishaji, na miundombinu ya usafirishaji hutumika kama mishipa muhimu kwa uchumi wa nchi kadhaa zisizo na mlango wa bahari, ikiwemo Zambia, Malawi, Uganda, Rwanda, Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo,” alieleza Prof. Kahyarara.
Alihimiza kuwa Tanzania itaendelea kujitolea kutoa suluhisho bora, salama na linalostahimili mabadiliko ya tabianchi kwa ajili ya kurahisisha biashara na maendeleo kwa majirani zake wasio na mlango wa bahari.
“Tunaendelea kutekeleza miradi mikubwa ya uwekezaji kupitia Ukanda wa Kati na TAZARA, kuboresha Bandari ya Dar es Salaam, kupanua miundombinu ya reli na barabara, pamoja na kurahisisha taratibu za forodha mipakani kwa mujibu wa Mkataba wa WTO wa Kurahisisha Biashara na soko la eneo huru la Afrika (AfCFTA). Tunaamini kuwa kubadilisha njia za usafirishaji kuwa kanda za kiuchumi ni hatua muhimu kwa mageuzi ya kiuchumi, ushirikiano wa kikanda, na ustawi wa pamoja,” alisisitiza.
Alieleza kuwa Tanzania imedhamiria kuendelea kushirikiana kwa njia za uwili, ushirikiano wa Kusini kwa Kusini, ushirikiano wa pembe tatu na majukwaa ya kikanda ili kusaidia nchi zisizo na mlango wa bahari kuvuka vizingiti vya kimfumo na kuwa nchi zenye uhusiano wa moja kwa moja na masoko.
Prof. Kahyarara alisema Tanzania inasisitiza haja ya kuchukua hatua za pamoja ili kuhakikisha Mpango wa Awaza unakuwa siyo tu tamko la nia, bali ni ramani ya kweli ya mageuzi.
“Mkutano huu uwe chombo cha mabadiliko ambacho kitaashiria mwanzo mpya—ambapo maendeleo ya nchi yoyote hayatekwi na jiografia yake, bali mshikamano na maendeleo ya pamoja ndiyo yanayoongoza safari yetu ya pamoja kuelekea 2030 na baada ya hapo,” alisisitiza.
Alisisitiza kuwa Mpango wa Awaza haupaswi kubaki kama hati isiyotenda kazi, bali uwe ramani hai ya mageuzi inayoungwa mkono kwa vitendo na washirika wa maendeleo, taasisi za kifedha, na nchi jirani za pwani kwa pamoja.
————————————————————————————————
Tanzania Reaffirms Strong Support for Landlocked Developing Countries.
Call the Awaza Programme of Action to be turned into a roadmap for change.
Tanzania has reaffirmed its commitment to the aspirations and challenges of landlocked developing countries (LLDCs), calling for collective action to turn promises into progress.
Permanent Secretary of the Ministry of Transport Prof. Godius Kahyarara told the General Debate during the third United Nations Conference on Landlocked Developing Countries (LLDC3) in Awaza, Turkmenistan, on 6th August, 2025.
He emphasised the need to transform the Awaza Programme of Action from a declaration of intent into a practical and impactful roadmap for inclusive development.
“Tanzania is not landlocked, but our strategic location as a coastal and transit country places us at the heart of regional connectivity in Eastern and Southern Africa. Our ports, transport corridors, and logistics infrastructure serve as vital arteries for the economies of several LLDCs, including Zambia, Malawi, Uganda, Rwanda, Burundi, and the Democratic Republic of Congo,” he emphasised.
Prof. Kyaharara reaffirmed Tanzania’s enduring commitment to facilitate efficient, secure, and climate-resilient transit solutions that unlock the trade and development potential of her landlocked neighbours.
“We are actively implementing flagship investments under the Central Corridor and TAZARA, modernising the Dar es Salaam Port, expanding rail and road networks, and simplifying border and customs procedures in line with the WTO Trade Facilitation Agreement and the AfCFTA. We believe that transforming transport corridors into economic corridors is essential for structural transformation, regional integration, and shared prosperity,” he added.
He said Tanzania also reaffirms its commitment to bilateral, South-South, triangular, and regional cooperation to help LLDCs overcome structural barriers and become “landlinked”. and supports the proposal to establish an International Day to raise awareness of the special needs and rights of LLDCs.
He finalised by saying that Tanzania reiterates its unwavering support for the aspirations of her landlocked brothers and sisters, emphasising the need for collective action to ensure that the Awaza Programme of Action becomes not merely a declaration of intent, but a true blueprint for transformation. “Let this conference mark a turning point where no country’s development is held hostage by its geography, and where solidarity and shared progress guide our collective journey to 2030 and beyond.
He said the Awaza Programme must not remain a static document; instead, it should serve as a living blueprint for transformation that is actively supported by development partners, financial institutions, and neighbouring coastal countries alike.
Tanzania imeeleza kuziunga mkono nchi zinazoendelea zisizo na mlango wa bahari kutimiza matarajio na kukabiliana na changamoto zinazozikabili na kutoa wito wa kuchukua hatua za pamoja na kuufanya Mpango wa Awaza kubadilisha ahadi kuwa matokeo halisi.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius Kahyarara, ametoa kauli hiyo alipozungumza tarehe 6 Agosti 2025 kwenye Mkutano wa Tatu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Nchi Zinazoendelea Zisizo na Bahari unaofanyika mjini Awaza, Turkmenistan.
Prof. Godius Kahyarara amesisitiza juu ya umuhimu wa kubadilisha Mpango wa Awaza kutoka kuwa tamko la Mkutano huo na kuufanya kuwa ramani ya kuelekea kwenya matokeo chanya ya maendeleo jumuishi.
“Tanzania si nchi isiyo na bahari, lakini nafasi yetu ya kimkakati kama nchi yenye Bahari na njia ya usafiri inatufanya kuwa kitovu cha muunganiko wa kikanda katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kusini mwa Afrika. Bandari zetu, njia za usafirishaji, na miundombinu ya usafirishaji hutumika kama mishipa muhimu kwa uchumi wa nchi kadhaa zisizo na mlango wa bahari, ikiwemo Zambia, Malawi, Uganda, Rwanda, Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo,” alieleza Prof. Kahyarara.
Alihimiza kuwa Tanzania itaendelea kujitolea kutoa suluhisho bora, salama na linalostahimili mabadiliko ya tabianchi kwa ajili ya kurahisisha biashara na maendeleo kwa majirani zake wasio na mlango wa bahari.
“Tunaendelea kutekeleza miradi mikubwa ya uwekezaji kupitia Ukanda wa Kati na TAZARA, kuboresha Bandari ya Dar es Salaam, kupanua miundombinu ya reli na barabara, pamoja na kurahisisha taratibu za forodha mipakani kwa mujibu wa Mkataba wa WTO wa Kurahisisha Biashara na soko la eneo huru la Afrika (AfCFTA). Tunaamini kuwa kubadilisha njia za usafirishaji kuwa kanda za kiuchumi ni hatua muhimu kwa mageuzi ya kiuchumi, ushirikiano wa kikanda, na ustawi wa pamoja,” alisisitiza.
Alieleza kuwa Tanzania imedhamiria kuendelea kushirikiana kwa njia za uwili, ushirikiano wa Kusini kwa Kusini, ushirikiano wa pembe tatu na majukwaa ya kikanda ili kusaidia nchi zisizo na mlango wa bahari kuvuka vizingiti vya kimfumo na kuwa nchi zenye uhusiano wa moja kwa moja na masoko.
Prof. Kahyarara alisema Tanzania inasisitiza haja ya kuchukua hatua za pamoja ili kuhakikisha Mpango wa Awaza unakuwa siyo tu tamko la nia, bali ni ramani ya kweli ya mageuzi.
“Mkutano huu uwe chombo cha mabadiliko ambacho kitaashiria mwanzo mpya—ambapo maendeleo ya nchi yoyote hayatekwi na jiografia yake, bali mshikamano na maendeleo ya pamoja ndiyo yanayoongoza safari yetu ya pamoja kuelekea 2030 na baada ya hapo,” alisisitiza.
Alisisitiza kuwa Mpango wa Awaza haupaswi kubaki kama hati isiyotenda kazi, bali uwe ramani hai ya mageuzi inayoungwa mkono kwa vitendo na washirika wa maendeleo, taasisi za kifedha, na nchi jirani za pwani kwa pamoja.
————————————————————————————————
Tanzania Reaffirms Strong Support for Landlocked Developing Countries.
Call the Awaza Programme of Action to be turned into a roadmap for change.
Tanzania has reaffirmed its commitment to the aspirations and challenges of landlocked developing countries (LLDCs), calling for collective action to turn promises into progress.
Permanent Secretary of the Ministry of Transport Prof. Godius Kahyarara told the General Debate during the third United Nations Conference on Landlocked Developing Countries (LLDC3) in Awaza, Turkmenistan, on 6th August, 2025.
He emphasised the need to transform the Awaza Programme of Action from a declaration of intent into a practical and impactful roadmap for inclusive development.
“Tanzania is not landlocked, but our strategic location as a coastal and transit country places us at the heart of regional connectivity in Eastern and Southern Africa. Our ports, transport corridors, and logistics infrastructure serve as vital arteries for the economies of several LLDCs, including Zambia, Malawi, Uganda, Rwanda, Burundi, and the Democratic Republic of Congo,” he emphasised.
Prof. Kyaharara reaffirmed Tanzania’s enduring commitment to facilitate efficient, secure, and climate-resilient transit solutions that unlock the trade and development potential of her landlocked neighbours.
“We are actively implementing flagship investments under the Central Corridor and TAZARA, modernising the Dar es Salaam Port, expanding rail and road networks, and simplifying border and customs procedures in line with the WTO Trade Facilitation Agreement and the AfCFTA. We believe that transforming transport corridors into economic corridors is essential for structural transformation, regional integration, and shared prosperity,” he added.
He said Tanzania also reaffirms its commitment to bilateral, South-South, triangular, and regional cooperation to help LLDCs overcome structural barriers and become “landlinked”. and supports the proposal to establish an International Day to raise awareness of the special needs and rights of LLDCs.
He finalised by saying that Tanzania reiterates its unwavering support for the aspirations of her landlocked brothers and sisters, emphasising the need for collective action to ensure that the Awaza Programme of Action becomes not merely a declaration of intent, but a true blueprint for transformation. “Let this conference mark a turning point where no country’s development is held hostage by its geography, and where solidarity and shared progress guide our collective journey to 2030 and beyond.
He said the Awaza Programme must not remain a static document; instead, it should serve as a living blueprint for transformation that is actively supported by development partners, financial institutions, and neighbouring coastal countries alike.
Labels:
KIMATAIFA
August 04, 2025
📆 August 31, 2025
📍OLASITI, ARUSHA
DAY [3] WABUNGE WA JIMBO LA ARUSHA KATA YA OLASITI
Written By CCMdijitali on Monday, August 4, 2025 | August 04, 2025
Mkutano wa kujitambulisha Wagombea Ubunge na Udiwani wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Arusha, Kata ya OLASITI
MKOA WA ARUSHA
Jimbo la Arusha Mjini
(1) Ndugu Ally Said BABU
(2) Ndugu Hussein Omarhajji GONGA
(3) Ndugu Aminatha Salash TOURE
(4) Ndugu Mustapha Said NASSORO
(5) Ndugu Paul Christian MAKONDA
(6) Ndugu Lwembo Mkwavi MGHWENO
(7) Ndugu Jasper Augustino KISHUMBUA
📆 August 31, 2025
📍OLASITI, ARUSHA
PICHA YA WABUNGE WATEULIWA |
Ndg Hussein Gonga akijitambulisha mbele ya Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Kata ya Olasiti. |
Ndg Hussein Gonga akijitambulisha mbele ya Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Kata ya Olasiti. |
Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Kata ya Olasiti. |
Cde Makonda akijitambulisha mbele ya Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Kata ya Olasiti. |
Labels:
MIKOANI