MWENYEKITI WA CCM NA RAIS MSTAAFU DKT. KIKWETE AHITIMISHA KAMPENI ZA UCHAGUZI KATIKA MAJIMBO MATANO YA ZANZIBAR
Na Mwandishi Wetu, Zanzibar Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, leo amehit...
MWENYEKITI WA CCM NA RAIS MSTAAFU DKT. KIKWETE AHITIMISHA KAMPENI ZA UCHAGUZI KATIKA MAJIMBO MATANO YA ZANZIBAR
Written By CCMdijitali on Thursday, October 23, 2025 | October 23, 2025
Na Mwandishi Wetu, Zanzibar
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, leo amehitimisha rasmi kampeni za uchaguzi kwa majimbo matano ya Zanzibar, akiwataka wananchi wa pande zote mbili za Muungano kujitokeza kwa wingi ifikapo Oktoba 29 kupiga kura kwa amani, umoja na utulivu.
Dkt. Kikwete alihitimisha kampeni hizo katika mkutano mkubwa wa wa hadhara uliofanyikia katika uwanja wa Skuli ya Ghana jimbo la Uzini Wilaya ya Kati, Mkoa wa Kusini na Shehia ya Kiboje, na kuhitimisha kampeni za majimbo ya Tunguu, Chwaka na Uzini katika Wilaya ya Kati, pamoja na majimbo ya Paje na Makunduchi, Wilaya ya Kusini Unguja.
Akihutubia mkutano huo, Dkt Kikwete amesisitiza kuwa wananchi hawana sababu ya kuwa na wasiwasi, kwani Tanzania inasifika kwa utamaduni wa uchaguzi wa amani, uliosimama katika misingi ya demokrasia, uadilifu na umoja wa kitaifa.
Dkt. Kikwete amesema ana imani kubwa kuwa wagombea wa CCM wataibuka na ushindi kutokana na utekelezaji wa Ilani wa chama hicho kwa kiwango cha zaidi ya asilimia 85.
“Asilimia 15 zilizosalia ni miradi ambayo utekelezaji wake unaendelea. Yaani kazi imeshaanza. Hii inathibitisha msemo wetu kwamba ‘CCM ikiahidi, inatekeleza,’” alisema kwa msisitizo, akipigiwa makofi na wananchi.
Amesema Ilani ya CCM imeendelea kudumisha misingi ya uhuru, umoja, amani na utulivu wa nchi, huku akiwataka wananchi kuendelea kuilinda amani hiyo ambayo ni tunu ya taifa.
“Tanzania ni nchi yenye utulivu na usalama. Wapo waliowahi kujaribu kuivuruga amani hiyo, lakini hawakufaulu, na hawatafaulu sasa. Rais na Amieri Jeshi Mkuu Dkt. Samia Suluhu Hassan mwenyewe amewahakikishia Watanzania kuwa hakutakuwa na vurugu wala maandamano katika kipindi hiki cha uchaguzi,” aliongeza.
Dkt. Kikwete alieleza kuwa kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Katiba ya Zanzibar, uchaguzi wa viongozi hufanyika kila baada ya miaka mitano, na mwaka huu, Oktoba 29, Watanzania watapiga kura kuchagua Rais wa Muungano, Rais wa Zanzibar, Wabunge, Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi na Madiwani.
“CCM ina wagombea katika ngazi zote – kuanzia Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa Jamhuri ya Muungano, Dkt. Hussein Ali Mwinyi kwa Zanzibar, pamoja na wagombea wote wa ubunge, uwakilishi na udiwani katika kila jimbo, kata na wadi. Hii ndiyo nguvu ya chama chetu,” alisema Kikwete.
Akiendelea kueleza falsafa ya chama hicho, alisema CCM imekuwa na utamaduni wa kutoa Ilani ya Uchaguzi kila baada ya miaka mitano, ikieleza ahadi na vipaumbele vya chama vitakavyotekelezwa na serikali zake endapo kitapewa ridhaa.
“Ilani ndiyo mkataba kati ya CCM na wananchi. Huo ndio mwongozo wa viongozi wetu wanapotekeleza majukumu yao. Hata hivyo, wagombea hawazuiliwi kuongeza mambo mapya kulingana na mahitaji ya wananchi,” alifafanua.
Akitolea mifano, Dkt. Kikwete alisema viongozi mbalimbali wa CCM akiwemo Hayati Rais Benjamin Mkapa, Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, na hata yeye mwenyewe, waliwahi kutoa ahadi nje ya Ilani kutokana na maoni ya wananchi waliokutana nao wakati wa kampeni.
“Ahadi ni deni, na wananchi hawasahau. Ni kama msemo ule wa ‘mla kunde husahau, lakini mtupa maganda hasahau,’” alisema kwa tabasamu.
Dkt. Kikwete pia alitoa pongezi maalumu kwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa namna anavyoendesha kampeni kwa uwazi, ukweli na ufasaha.
“Wananchi wanapenda kiongozi anayesema ukweli.
Anayeonyesha mafanikio yaliyopatikana na kukiri changamoto zilizopo huku akieleza mipango ya kuzitatua. Huyo ndiye Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan, mwanamke jasiri, mkweli na mwenye dira ya maendeleo,” alisisisitiza
Aidha, alimpongeza Rais wa Zanzibar, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, kwa kazi kubwa aliyoifanya katika kipindi chake cha uongozi, akisema kuwa ametekeleza miradi mingi mipya ambayo haikuwa hata kwenye Ilani ya CCM.
“Dkt. Mwinyi ameleta mapinduzi makubwa ya kiuchumi, kijamii na kiutawala Zanzibar. Hii ni ishara ya kiongozi mwenye maono na anayejali wananchi wake,” alisema.
Dkt. Kikwete alimaliza kwa kuwataka wananchi wote wa Zanzibar na Tanzania Bara kujitokeza kwa wingi siku ya uchaguzi, kupiga kura mapema, na kuhakikisha kuwa amani inatawala katika kila hatua ya zoezi hilo.
Tanzania ni yetu sote, na amani yake ni jukumu letu sote. Tuwaheshimu viongozi, tuwapigie kura kwa utulivu, na tushiriki katika kuimarisha demokrasia yetu,” alihitimisha huku akishangiliwa kwa vifijo na nderemo.
Mwisho






DKT. SAMIA: NIWAHAKIKISHIE, MAANDAMANO PEKEE YA OKT. 29 NI KUPIGA KURA
Written By CCMdijitali on Tuesday, October 21, 2025 | October 21, 2025
𝙈𝙧𝙖𝙙𝙞 𝙬𝙖 𝘿𝙈𝘿𝙋 𝙠𝙪𝙢𝙖𝙡𝙞𝙯𝙖 𝙘𝙝𝙖𝙣𝙜𝙖𝙢𝙤𝙩𝙤 𝙮𝙖 𝙢𝙖𝙛𝙪𝙧𝙞𝙠𝙤 𝘿𝙨𝙢.
Mgombea nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Rais Dkt. 𝗦𝗮𝗺𝗶𝗮 𝗦𝘂𝗹𝘂𝗵𝘂 𝗛𝗮𝘀𝘀𝗮𝗻 amesema kuwa akipata ridhaa ya kuongoza tena nchi kwa miaka mitano ijayo, atahakikisha Serikali yake itajenga barabara za makutano (fly over) katika barabara za Morocco, Mwenge, Magomeni, barabara ya Ali Hassan Mwinyi na Umoja wa Mataifa.
Dkt. Samia amesema sababu ya ujenzi huo ni kupunguza msongamano na kukuza shughuli za biashara katika maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam ambapo zitaongeza tija katika ukuaji wa uchumi endelevu wenye kumgusa Mtanzania mmoja mmoja.
Akizungumza mbele ya kadamnasi ya wananchi wa Kinondoni na Ubungo alipokuwa akinadi Ilani ya Uchaguzi ya CCM (2025/30), sera na Ahadi zake katika viwanja vya Leaders Club, amesema atayakamilisha hayo pale ambapo wananchi watakwenda sambamba na kuchagau mafiga matatu kwa maana ya Rais kutoka CCM, Wabunge na Madiwani ili kuondoa makandokando katika kutekeleza majukumu hayo.
Pia, Mgombea Urais Dkt. Samia, ameahidi kujenga barabara ya Kimara - Mavurunza - Bonyokwa inayopita kwenye majimbo matatu ya Segerea, Ubungo na Kibamba yenye urefu wa kilomita 7 kwa kiwango cha lami huku akiongeza kuwa Serikali yake itatenga bajeti ili kujenga barabara nyingine muhimu kwa maendeleo ya wilaya zote zilizipo ndani ya Jiji la Dar es salaam.
Aidha, Dkt. Samia ameahidi kufanya utanuzi wa barabara ya Mwaikibaki yenye kilomita 9 kutoka Morocco - Kawe hadi Garden road pamoja na barabara ya Tegeta hadi Bagamoyo yenye urefu wa kilomita 57, Kibamba hadi Mloganzila yenye urefu wa kilomita 8.
Akigusia suala la changamoto ya mafuriko kwa baadhi ya maeno ya Jiji la Dar es salaam, Dkt. Samia amehaidi kuondoa changamoto hiyo katika kipindi cha mvua kwa maeneo mbalimbali ikiwemo yanayopakana na mto Gide, mto Mbezi na mto China akieleza kuwa changamoto hiyo itatatuliwa kupitia mradi wa pili wa uendelezaji wa Jiji la Dar es Salaam (DMDP)
𝗛𝗔𝗞𝗨𝗡𝗔 𝗧𝗜𝗦𝗛𝗜𝗢 𝗟𝗔 𝗨𝗦𝗔𝗟𝗔𝗠𝗔 𝗟𝗜𝗧𝗔𝗞𝗔𝗟𝗢𝗞𝗨𝗪𝗘𝗣𝗢, 𝗡𝗘𝗡𝗗𝗘𝗡𝗜 𝗠𝗞𝗔𝗣𝗜𝗚𝗘 𝗞𝗨𝗥𝗔 - 𝗗𝗞𝗧. 𝗦𝗔𝗠𝗜𝗔
𝙈𝙖𝙩𝙪𝙨𝙞 𝙣𝙞𝙖𝙘𝙝𝙞𝙚𝙣𝙞 𝙢𝙞𝙢𝙞, 𝙣𝙞𝙣𝙖𝙮𝙖𝙗𝙚𝙗𝙖 𝙠𝙬𝙖 𝙣𝙞𝙖𝙗𝙖 𝙮𝙚𝙣𝙪.
"..Niwahakikishie tarehe 29, kesho kutwa tu mwezi huu wa 10, niwaombe tokeni muende mkapige kura."
"Ninayeongea hapa ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa nchi hii, ninataka niwaambie, maandamano yatakayokuwepo ni ya watu kwenda vituoni kupiga kura, hakuna maandamano mengine yatakayokuwepo hapa.."
"..hakuna tishio la kiusalama litakalokuwepo, anayesemahapa ndiye Amiri Jeshi Mkuu wa Nchi hii."
"Niwaombe ndugu zangu, twendeni mkapige kura, twendeni mkapige kura... Ndugu zangu mengine niachieni mimi, matusi niachieni mimi, ninayabeba kwa niaba yenu"
"Niliapa kuwa Rais wa Tanzania, niliapa kuilinda Nchi hii kwa kudumisha Amani, Umoja na Mshikamano wetu"
Hayo yamesemwa na Mgombea wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. 𝗦𝗮𝗺𝗶𝗮 𝗦𝘂𝗹𝘂𝗵𝘂 𝗛𝗮𝘀𝘀𝗮𝗻 wakati akizungumza kwenye Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni Jijini Dar es Salaam katika mkutano wa hadhara wa kampeni za Uchaguzi Mkuu uliofanyika leo tarehe 21 Oktoba 2025.
𝘾𝙃𝘼𝙂𝙐𝘼 𝙎𝘼𝙈𝙄𝘼, 𝘾𝙃𝘼𝙂𝙐𝘼 𝘾𝘾𝙈
DKT. SAMIA: TUTAHAKIKISHA DAR INAONDOKANA NA ADHA YA MAJI KWA MIRADI MIPYA
"Katika miaka mitano inayokuja, tutaendelea kukamilisha utekelezaji wa miradi ya Bwawa la Kidunda lenye thamani ya Shilingi bilioni 336, na bwawa hili la Kidunda litakwenda kuhudumia mikoa ya Dar es Salaam, Pwani na Morogoro. Lakini mradi wa pili tunaokwenda kuufanya ili kuondoa uhaba wa maji Dar es Salaam hasa wakati wa kiangazi, ni mradi mkubwa wa kutoa maji mto Rufiji ambao kazi ya upembuzi yakinifu na utafiti wa kina tayari tumekwishaianza na awamu hii tunakwenda kufanya utekelezaji ili Dar es Salaam ipate maji kutoka Kidunda, Ruvu na Mto Rufiji kuondoa kabisa kadhia ya uhaba wa maji", - Dkt. Samia.
Mgombea wa nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza kwenye Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni Jijini Dar es Salaam katika mkutano wa hadhara wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 21, 2025.
"Niwahakikishie tarehe 29, kesho kutwa tu mwezi huu wa 10, niwaombe tokeni muende mkapige kura. Ninayeongea hapa ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa nchi hii, ninataka niwaambie, maandamano yatakayokuwepo ni ya watu kwenda vituoni kupiga kura, hakuna maandamano mengine yatakayokuwepo hapa, hakuna tishio la kiusalama litakalokuwepo, anayesema ni Amiri Jeshi Mkuu wa Nchi hii. Niwaombe ndugu zangu, twendeni mkapige kura, twendeni mkapige kura... Ndugu zangu mengine niachieni mimi, matusi niachieni mimi, ninayabeba kwa niaba yenu", - Dkt. Samia.
Mgombea wa nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza kwenye Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni Jijini Dar es Salaam katika mkutano wa hadhara wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 21, 2025.
KUANZIA 2026 MTAONA MAGEUZI MAKUBWA YA MWENDOKASI DAR - DKT. SAMIA
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema kuwa serikali yake itakwenda kusimamia na kukamilisha mradi wa miundombinu ya barabara ya mabasi yaendayo haraka maarufu kama mwendokasi, hiyo itafanyika ikiwa atachaguliwa kuiongoza nchi kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.
Dkt. Samia ameyasema hayo akizungumza kwenye Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni Jijini Dar es Salaam katika mkutano wa hadhara wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 21, 2025 ambapo amesisitiza kuwa utoaji wa huduma ya usafiri na usafirishaji kupitia miundombinu hizo zitakapokamilika, utajikita zaidi kwenye sekta binafsi.
"Tukapomaliza barabara zote, ni fursa muhimu kwa sekta binafsi kupata kazi ya kubeba abiria na kurudisha, kazi hiyo kwa kiasi hatutaki kuifanya sisi serikali bali sekta binafsi wataingiza mabasi yao na wafanye uendeshaji wa shughuli hizo", ameeleza Dkt. Samia.
Amewaahidi wakazi wa Dar es Salaam kuwa kuanzia Januari, 2026 kutakuwa na mageuzi makubwa ya utoaji wa huduma ya miundombinu ya mwendokasi.

Dkt. Kikwete Aunguruma Visiwani, Awataka Wazanzibari Walinde Amani na Maendeleo
Written By CCMdijitali on Sunday, October 12, 2025 | October 12, 2025
MAKAMU WA PILI WA RAIS ZANZIBAR- AKIZUNGUMZA NA WANAMICHEZO - JIMBONI KIWANI


Baraza la Vijana Zanzibar kuendelea kushirikiana na taasisi mbali mbali za Vijana ndani na nje ya Nchi kutunza Mazingira

RAIS DKT. SAMIA AMPONGEZA MWANARIADHA SIMBU
Written By CCMdijitali on Saturday, September 27, 2025 | September 27, 2025
- Amkabidhi Nyumba jijini Dodoma
- Mheshimiwa Majaliwa asema Simbu ameliheshimisha Taifa
- Atoa zawadi kwa Timu zilizofanya vizuri kimataifa
Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amempongeza Mwanariadha Alphonse Simbu kwa kuwa Bingwa wa Dunia wa mbio za marathon za Tokyo na kwamba ataendelea kutoa kipaumbele katika sekta ya michezo ili itoe mchango zaidi katika kukuza uchumi wa nchi na kuongeza wigo wa upatikanaji ajira kwa vijana
Pongezi hizo zimetolewa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Jumamosi (Septemba 27, 2025) alipomwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye hafla kuwapongeza wanamichezo na timu zilizofanya vizuri kwenye medani za kimataifa, hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa mikutano wa hotel jijini Dar es Salaam.
Katika tukio hilo Mheshimiwa Majaliwa alitangaza kuwa, Mheshimiwa Rais. Dkt. Samia amempatia Mwanariadha Simbu zawadi ya nyumba jijini Dodoma, sambamba na kikabidhiwa kitita cha shilingi milioni 20 ikiwa ni ishara ya kutambua ushindi huo ambao umeliletea Taifa heshima kwenye jukwaa la kimataifa"
"Mheshimiwa Rais Dkt. Samia ameandaa nyumba iliyopo mkoani Dodoma, ambayo itakabidhiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na zoezi hilo lisichukue muda mrefu kuanzia leo, tusiwe tunatamka ahadi za viongozi halafu zinakaa muda ambao mtu anajiuliza"
Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa Mwanariadha Simbu ameandika ukurasa wa upekee kwa kuwa mtanzania wa Kwanza kutwaa tuzo ya dhahabu katika marathoni ya Dunia ya mwaka 2025 "Haya ni Mashindano makubwa zaidi ya riadha duniani baada ya Michezo ya Olympic, yakihusisha wanariadha Bora kutoka Mataifa yote duniani"
Amesema kuwa Serikali mara zote umekuwa ikiweka jitihada za kutosha za kuhakikisha sekta ya Michezo inakuwa na mchango kwa Taifa "Matokeo tunayoyashuhudia hivi sasa ni matokeo ya uwekezaji mkubwa unaofanywa na Serikali ikiwemo ukarabati WA viwanja na kuongezwa kwa bajeti kutoka shilingi bilioni 38 mwaka 2022 Hadi bilioni 326 mwaka 2025/2026"
Katika hatua nyingine Mheshimiwa Majaliwa ametoa wito kwa wanamichezo nchini kuweka jitihada binafsi katika kushiriki katika michezo kwani ushindi unaweza kupatikana kwa kuweka nia "Wekeni mikakati ya ushindi ili muweze kuipeperusha bendera ya Taifa letu kimataifa".
Naye RAIS wa Shirikisho la Riadha Tanzania (SRT) Rogath Stephen ameishukuru Serikali kwa namna inavyotoa mchango kubwa kwa vyama na namna anavyoendeleza Michezo. "Hatujawahi kufanyiwa mambo ambayo kwasasa yanafanyika, kupitia Serikali tumekuwa tunahudumiwa kwa namna ya kipekee"
Kwa Upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Gerson Msigwa amesema kuwa Medali ya dhahabu ya Alphose Simbu imefanikiwa kupata tiba ya kiu ya Watanzania ya kupata Medali za dhabau katika michezo ya kimataifa. "Hii imewezekana kutokana na na maamuzi ya viongozi wetu kuwa na maono ya kurudisha heshima kwa Taifa baada ya kufanya uwekezaji mkubwa mchezoni"
Ameongeza kuwa Kiu kubwa iliyobaki ni kuhakikisha watanzania wanapata medali kwenye Michezo ya Olympic pamoja na michezo ya jumuiya ya madola "Sisi kama Serikali tumejipanga kuhakikisha tunafanikiwa kuleta medali hizi hapa nyumbani, tunaweka mikakati imara ya usimamizi, kwa sasa kuwa wasindikizaji imetosha, Tunaamini mwakani tunaweza kupata media kwenye Michezo ya jumuiya ya madola na 2028 tutapata medali kwenye olympic"
Timu nyingine zilizopongezwa na kupewa zawadi ya shilingi milioni kumi ni Timu ya Taifa ya Futsal ya Wanawake ambayo imefuzu kushiriki kombe la dunia (Philippines 2025), Timu ya JKT Queens ambao ni mabingwa wa Mashindano ya CAF Woman's Championship League Cecafa Qualifiers 2025.
Timu nyingine ni timu ya Taifa ya Cricket U-19 ambayo itashiriki mashindano ya Dunia 2026 nchini Zimbabwe na timu ya wenye ulemavu (Tembo Worriers) ambao wamekuwa mshindi wa Pili wa Michezo ya Afrika Mashariki na Kati.










WANANCHI MAGU WAISHUKURU SERIKALI KUWAPATIA HATI ZA HAKIMILKI ZA KIMILA
Na Munir Shemweta, WANMM MAGU
Wananchi wa vijiji vitatu vya Chandulu, Salama, Mwabulenga vilivyopo kata ya Ng'haya wilaya ya Magu mkoa wa Mwanza wameishukuru serikali kwa uamuzi wake wa kuwapimia na kuwamilikisha maeneo yao kwa kuwapatia Hati za Hakimilki za Kimila.
Zoezi hilo la kuwapatia Hati za Hakimilki za Kimila limefanyika baada ya kufanyika mipango wa matumizi ya ardhi pamoja na upimaji ardhi katika vijiji hivyo vitatu.
Mipango ya Matumizi ya Ardhi huwekwa katika maeneo mbalimbali kwa lengo la kuboresha usalama wa umiliki wa ardhi, kukuza matumizi endelevu ya ardhi pamoja na kupunguza migogoro ya ardhi.
Wananchi wa vijiji hivyo wametoa kauli hiyo tarehe 26 Septemba 2025 katika kijiji cha Chandulu wilayani Magu wakati wa zoezi la kutoa hakimilki za kimila kwa wananchi waliomilikishwa maeneo yao.
Jumla ya Hati za Hakimilki za Kimila 1,415 zimeandaliwa huku takriban hatimilki 5000 ukamilishaji wake ukiendelea ambapo Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhandisi Anthony Sanga alikabidhi Hati za Hakimilki za kimila 50 kwa niaba ya wannachi wote waliomilikishwa.
Wananchi hao wamesema, wanajisikia furaha kubwa kumilikishwa maeneo yao waliyoyaelezea kuwa sasa umilikishaji wake umeongeza thamani ya maeneo hayo.
"Najisikia vizuri sana kwa sababu ardhi yangu nimemilikishwa kwa hati na sitokuwa tena na uharaka wa kuiuza, niipongeze sana serikali kwa uamuzi wake huu wa kutumilikisha" amesema mkazi wa Chadulu Bw. Mashiku Machunge.
Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhandisi Anthony Sanga amewataka wananchi waliokabidhiwa Hati za Hakimilki za kimila kuhakikisha wanazitunza na kuacha tabia ya kuuza ardhi hovyo ili ziweze kusaidia vizazi vijavyo.
"Ndugu wananchi hati hizi inatakiwa mzitunze kwa sababu huu ni urithi wenu, ardhi hii ni ya kwenu mzitunze na pili tusiwe na tabia ya kuuza ardhi, ardhi tuitunze itusiadie sisi, watoto wetu, wajukuu zetu na watakaotufutia katika vizazi vyetu" amesema.
Ametaka hati milki walizokabidhiwa wananchi zilete mabadiliko ya kimaisha kwa kuwa mbali na kuwatambulisha kisheria lakini zinasaidia kupata mikopo na kueleza matarajio ya serikali ni kwamba pawepo matokeo chanya ya kimaendeleo na kusisitiza kuwa hati hizo zisiwe sehemu ya migogoro ya kudhulumiana.
Kwa upande wake Kamishna wa Ardhi Msaidizi mkoa wa Mwanza Bw. Wilson Luge ameeleza msingi mkubwa wa ofisi yake ni kuhakikisha wanawamilikisha wananchi maeneo yao kwa kuwapatia hati milki kwa kuwa ardhi ni rasimali itakayowawezesha kiuchumi.
"Ndani ya mkoa wa Mwanza katika halmashauri zote sita tutashirikiana na kampuni za upimaji kuhakikisha ardhi za wananchi wetu zinapimwa na kuwapatia hati zikiwemo hizi Hati za Hakimilki za kimila bila kuwacheleweshea" amesema Luge.
Zoezi la upimaji maeneo katika wilaya ya Magu limefanywa kwa ushirikiano na kampuni za upimaji za GMS Geo tech Consultancy Co.Ltd, GNT Property Ltd na CAIWAY Company Ltd ambazo zinatekeleza mazoezi katika vijiji 16 kati ya vijiji 82 vilivyoko ndani ya Wilaya ya Magu.







Tanzania yalaani kuibuka upya kwa ukiukwaji wa sheria za kimataifa
Written By CCMdijitali on Friday, September 26, 2025 | September 26, 2025
Makamu wa Rais amesema hayo wakati akihutubia Kikao cha 80 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kinachofanyika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa Jijini New York nchini Marekani. Amesema uwepo wa mitazamo ya kibeberu, ikiwa ni pamoja na ile ya kuichukulia Afrika kuwa sehemu ya uchukuaji rasilimali na uporaji wa ardhi, pamoja na uwepo wa makampuni ya kimataifa kuendelea kufanikiwa kutokana na unyonyaji wa mali asili za Afrika, huku wakisababisha au kuunga mkono migogoro inapaswa kumalizika sasa.
Makamu wa Rais amesema Tanzania inauchukulia msimamo wa upande mmoja na matumizi mabaya ya nguvu za kijeshi, pamoja na kushindwa kwa jumuiya ya kimataifa na mataifa yenye nguvu duniani katika kukomesha umwagaji damu na vita vya hatari vinavyoendelea katika maeneo mengi duniani, kuwa ni jambo lisilokubalika.
Pia ametoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kutambua kuwa ongezeko la matumizi ya fedha katika masuala ya kijeshi ikiwemo utafiti na utengenezaji wa silaha ni jambo la kusikitisha na ni kinyume cha maadili. Amesema hali hiyo inazuia jitihada za kutafuta amani duniani, na inachukua kiasi kikubwa cha rasilimali ambazo zingeweza kutumika kuendeleza maendeleo endelevu na ustawi kwa wanadamu wote.
Makamu wa Rais amesema dunia inapaswa kuendelea kutafuta amani bila kuchoka kwani ndio sharti la maendeleo ya kijamii na kiuchumi. Amepongeza juhudi za Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, viongozi wa dunia, na mashirika ambayo yanashiriki kikamilifu katika upatanishi na utatuzi wa migogoro katika nchi na maeneo kama vile Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Sudan, Urusi, Ukraine, na Mashariki ya Kati. Ametoa wito wa ushirikishwaji kamili wa wanawake katika kutafuta amani hususani katika kipindi hiki inaposherehekewa miaka 30 tangu azimio la Beijing na maendeleo yaliyopatikana katika kukuza usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa wanawake.
Amesema Rais wa kwanza mwanamke wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.Samia Suluhu Hassan ameonyesha njia katika kueleza sera na vitendo vinavyoimarisha nafasi ya mwanamke katika sekta zote za jamii. Amesema kikanda na kimataifa, amekuwa mtetezi wa amani, haki, usalama na matumizi ya nishati safi.
Amesema Tanzania kama mwanachama wa Baraza la Amani na Usalama la Umoja wa Afrika, pia nafasi iliyotumikia kama Mwenyekiti wa Asasi ya Siasa Ulinzi na Usalama Jumuiya ya SADC ilichangia kikamilifu katika mipango ya amani na kuunga mkono hatua za kuzuia na kutatua migogoro.
Tanzania imetangaza kugombea kiti kisicho cha kudumu katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa muhula wa 2029-2030, ili kuthibitisha dhamira iliyonayo ya amani na usalama duniani.
Halikadhalika, Makamu wa Rais amesema, Tanzania inasisitiza msimamo wa Afrika wa kurekebisha uwakilishi mdogo wa bara hilo katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, na kutoa wito wa kupitishwa kwa angalau viti viwili vya kudumu vya Afrika vyenye nguvu ya kura ya turufu.
Amesema Tanzania inaungana na nchi nyingine katika kudai mageuzi ya haraka na ya kina ya mfumo wa fedha wa kimataifa. Ametoa wito wa kuongeza ufadhili wa masharti nafuu wa muda mrefu, kurekebisha mifumo huru ya ukadiriaji wa mikopo, na kufikiria upya tathmini ya uhimilivu wa deni, ili kupatikana mtaji wa uwekezaji katika miundombinu, elimu, afya na kuhimili mabadiliko ya tabianchi. Amesisitiza nia ya kuongezeka kwa sauti na uwakilishi wa Afrika katika miundo ya utawala ya Shirika la Fedha Duniani (IMF) na Benki ya Dunia ambayo haijafanyiwa kazi kwa muda mrefu.
Makamu wa Rais amesema Tanzania imejitolea na imepiga hatua katika utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDG’s 2030) ikifikisha asilimia 60. Amesema kwa lengo namba 3, Tanzania imefanikiwa kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi kutoka vifo 750 kwa kila vizazi hai 1000 mwaka 2000 hadi 104 mwaka 2022. Kwa lengo namba 6, upatikanaji wa maji safi na salama uliongezeka katika maeneo ya vijijini na mijini kutoka asilimia 32 na 55 mwaka 2000 hadi asilimia 79.9 na 94 mwaka 2024. Kwa nishati safi ya bei nafuu ambayo ni lengo namba 7, Tanzania imefanikiwa kuunganisha nishati ya umeme kwa vijiji 8,587 mwaka (2000) hadi 12,318 mwaka 2024 ambapo ni vijiji 15 pekee vilivyobaki bila umeme.
Makamu wa Rais amehimiza jumuiya ya kimataifa kuimarisha mwitikio wa pamoja wa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi. Ametoa wito wa kutumia vyema fursa ya Mkutano wa wa COP30 nchini Brazil kuhakikisha ahadi zinatekelezwa ikiwemo uchangiaji wa Mfuko wa Hasara na Maafa kutokana na athari za mabadiliko ya tabianchi (Loss and Demage Fund) pamoja na kuongezwa kwa ufadhili wa masharti nafuu wa muda mrefu, uhamishaji wa teknolojia, na masharti ya kibiashara yanayozingatia haki ili kufanikisha ukusanyaji wa mapato ya ndani kwa mataifa na kutafuta ushirikiano wa manufaa kwa pande zote katika matumizi ya rasilimali.
Imetolewa na
Ofisi ya Makamu wa Rais
26 Septemba 2025
New York – Marekani.







MAKAMU WA PILI WA RAIS ZANZIBAR ASHIRIKI DUA YA KUIOMBEA NCHI
Written By CCMdijitali on Thursday, September 25, 2025 | September 25, 2025
Wazazi na walezi wametakiwa kuwahimiza vijana wao katika kuitunza amani iliyopo nchini hasa katika kipindi hichi cha kuelekea uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi ujao.
Hayo yamesemwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe.Hemed Suleiman Abdulla kwa niaba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dkt Hussein Ali Mwinyi katika dua ya kuiombea nchi iliyoandaliwa na ofisi ya mufti mkuu kanda ya Pemba na kufanyika katika Masjid Rahman uliopo Gombani Pemba.
Amesema kuwa ni lazima kukaa pamoja na kushirikiana kwa kila jambo ili kuhakikisha wanapiga vita viashiria vyote vya uvunjifu wa amani na kusisitiza kuwa bila ya amani hakuna chochote cha kimaendeleo kinachoweza kufanyika nchini.
Alhajj Hemed amefahamisha kuwa wazizi na walezi ndio wahusika wakuu katika kuwaandalia vijana mazingira wezeshi ili kuweza kuishi katika hali ya amani na utulivu sambamba na kuyafaidi matunda ya kimaendeleo yanayoendea kutekelezwa na serikali ya Awamu ya Nane.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amewataka waumini kutokukubali kushawishiwa kuingia katika uvunjifu wa amani kwa kisingizio cha siasa jambo ambalo sio sahihi.
Sambamba na hayo Alhajj Hemed amewashukuru waumini kwa kuendelea kuiombea dua nchi hasa katika kipindi hichi cha kuelekea uchaguzi mkuu wa nchi unaotarajiwa kufanyika mwezi ujao.
Kwa upande wake Naibu Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh. MAHMOUD MUSSA WADI amewataka waumini wa dini ya kiislamu na wananchi kwa ujumla kuiombea dua nchi na viongozi wake kila wakati ili Mwenyezi Mungu aweze kuiepusha nchi na machafuko hasa kipindi hichi cha kuelekea uchaguzi mkuu wan chi.
Sheikh Mahmoud amesema historia inaonesha kuwa nchi nyingi duniani kila ifikapo kipindi cha uchaguzu hupatwa na taharuki ya kutoweka k wa amani katika nchi zao hivyo ni wajibu wa kila mwananchi kuhakikisha anailinda amini kwa gharama yoyote kabla ya uchaguzi, wakati wa uchaguzi na baada ya uchaguzi.
Imetolewa na Kitengo cha Habari (OMPR)
25.09.2025
SEKTA YA MADINI IMEENDELEA KUWA NGUZO YA UKUAJI WA UCHUMI-MAJALIWA
Written By CCMdijitali on Monday, September 22, 2025 | September 22, 2025
WAZIRI MKUU,Kassim Majaliwa amesema kuwa Sekta ya madini imeendelea kuwa nguzo ya uchumi nchini ambapo katika mwaka 2022 sekta hiyo imekua kwa asilimia 10.9 na kufikia mchango wa asilimia 10.1 kwenye Pato la Taifa mwaka 2024, ikilinganishwa na asilimia 9.0 mwaka 2023.
Ametoa kauli hiyo Leo (Jumatatu, Septemba 22, 2025) wakati wa uzinduzi wa Maonesho ya Nane ya Teknolojia ya Madini Mkoa wa Geita, yaliyofanyika katika viwanja vya Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Amesema kuwa hatua hiyo imetokana na jitihada mbalimbali za Serikali ya awamu ya sita ikiwemo kuimarishwa kwa mifumo ya ukusanyaji wa mapato na udhibiti wa biashara ya madini, matumizi ya mifumo ya kielektroniki (online mining cadastre system), uwepo wa masoko ya madini na ufuatiliaji wa mikataba ya uwekezaji.
"Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuweka kipaumbele katika kuimarisha mazingira ya uwekezaji kwenye sekta ya madini ili rasilimali za madini zichangie kwa katika ukuaji wa uchumi na ustawi wa Watanzania wote".
Waziri Mkuu ametoa rai kwa wadau wa sekta ya madini kuendelea kuwekeza katika teknolojia kwani ndiyo daraja la mageuzi kuanzia utafiti na uchimbaji, usafishaji na biashara ya madini. "Bila teknolojia sahihi, haiwezekani kuongeza tija, kuhakikisha usalama wa wachimbaji, kulinda mazingira, wala kufanya uongezaji thamani wa madini yetu".
Ameongeza kuwa kupitia maonesho hayo, katika kiipindi cha mwaka 2021 hadi 2025 Wachimbaji wadogo wa Geita wamezalisha zaidi ya kilo 22,000 za dhahabu zenye thamani ya Shilingi Trilioni 3.44, huku Serikali ikipata zaidi ya Shilingi Bilioni 235.5 kama mrabaha. "
Aidha, makampuni makubwa kama Geita Gold Mine na Buckreef katika kipindi hicho wamezalisha kilo 76,530 za dhahabu zenye thamani ya Shilingi Trilioni 11.38, na Serikali kupata zaidi ya Shilingi Bilioni 793 kama mrabaha."
Kwa Upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Madini, Mhandisi Yahya Samamba amesema kuwa Tanzania sasa imepiga hatua kwa kuwa na viwanda vya kutengeneza zana mbalimbali za uchimbaji wa madini.
"Katika mwaka wa fedha 2024-2025 tumeweza kuzalisha tani 62 za dhahabu tofauti na nyuma tulikuwa tukizalisha tani 40-50 kila mwaka hii inatufanya Tanzania kuwa miongoni mwa nchi tano bora Afrika katika uzalishaji wa dhahabu."
Awali, Mkuu wa Mkoa wa Geita, Martine Shigela amesema huo umefanya kazi kubwa ya kusambaza umeme vijijini na kwa kuwa kazi ya uchimbaji unahitaji umeme tayari umeme umepelekwa katika maeneo mengi ya wachimbaji wadogo.
"Tumefanyia kazi maagizo ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kupeleka umeme katika maeneo ya wachimbaji wadogo ili wafanye kazi zao na kuwa na uzalishaji wa uhakika katika maeneo yao."



WASIRA: DK. SAMIA, CCM WAMEDHARIA KULETA MABADILIKO KATIKA MAISHA YA WATANZANIA
Written By CCMdijitali on Thursday, September 18, 2025 | September 18, 2025




