Home » » NAIBU WAZIRI WA MAJI AKAGUA MIRADI YA MAJI ROMBO

NAIBU WAZIRI WA MAJI AKAGUA MIRADI YA MAJI ROMBO

Written By CCMdijitali on Tuesday, July 30, 2013 | July 30, 2013


Naibu waziri wa maji Dk Binilith Mahenge akikagua miradi ya maji katika wilaya ya Rombo.

Mhandisi wa maji wilaya ya Rombo Andrew Tesha akitoa maelezo kwa naibu waziri wa maji Dk Binilith Mahenge alipotembelea miradi ya maji katika wilaya hiyo.

 Naibu waziri wa maji Dk Mahenge akikagua mradi wa maji wa kilichopo eneo la hifadhi ya Mlima Kilimanjaro (KINAPA)

Naibu waziri Dk Mahenge akizungumza na mhandisi wa maji wilaya ya Rombo Andrew Tesha alipotembelea kisima cha maji katika kijiji cha Ushiri.


WIZARA ya maji,imeelezea kutoridhishwa kwake na uendeshaji wa kampuni ya usambazaji maji wilayani Rombo ya Kiliwater kwamba haijajipanga kibiashara na ingeweza kupata faida kubwa kuliko hali waliyonayo sasa kama wangekuwa makini.

Naibu waziri wa maji Dk Binillith Mahenge alitoa kauli hiyo baada ya kupokea taarifa ya kampuni hiyo kuhusu usambazaji wa huduma za maji na mipango yao katika ununuzi wa mita kwa ajili ya kuwafungia wateja wao.

“Kwa mipango hii mliyonayo kama kampuni hii ingekuwa imekabidhiwa mfanyabiashara yeyote makini,angeshindwa kupata faida?” alihoji huku mwenyekiti wa bodi ya kampuni hiyo, Silayo akikiri kwamba faida ingepatikana.

Aliitaka kampuni hiyo kujipanga upya kwani wanayo fursa ya kupata faida kama wakijitahidi kupunguza maji yanayopotea lakini pia
kuhakikisha wanaondokana na mfumo wa ulipaji anka kwa ‘Flat rate’ bali wawafungie wateja mita za maji.

“Huu mfumo wenu wa watu wote kulipa maji kwa viwango sawa unawapotezea mapato, wapo wanaoyatumia kwa ajili kumwagilia migomba kasha watalipa sh 3,000 kwa mwezi, ninyi mnaona hilo ni sahihi,badilikeni”alisema.

Katika baarifa yake kwa naibu waziri meneja wa Kiliwater, Prosper Kessy alisema uzalishaji wanakabiliwa na uzalishaji mdogo wa maji usiokidhi mahitaji kwani upo upungufu wa mita za ujazo 13,000 sawa na lita 13,000,000 kwa siku.

Alisema pia wanakabiliwa nupungufu wa mita za ujazo 22,000 sawa na litaza ujazo 22,000,000 wakati wa kiangazi na hivyo kuongeza tatizo la maji kwa wateja wake.

“Kiwango kikubwa cha asilimia 78 ya maji yasiyouzwa kutokana na uchakavu wa miundombinu,wazi wa maji,wateja wasio na mita na wale wenye mita lakini hutumia maji kiholela”alisema. Hata hivyo alisema kampuni hiyo inahitaji zaidi y ash milioni 600 kwa ajili ya kuwafungia mita wateja wake kama njia moja wapo ya kuongeza mapato


Habari na Picha Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Moshi.

Share this article :
 
Support : #BegaKwaBegaNaMamaSamia | JAK | CCM Arusha
Copyright © 2011. CCM Dijitali - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Jasper K
Proudly powered by Blogger
Link