Home » » Viwanda vya vileo vyashauriwa kutumia mazao yanayozalishwa nchini

Viwanda vya vileo vyashauriwa kutumia mazao yanayozalishwa nchini

Written By CCMdijitali on Saturday, January 10, 2015 | January 10, 2015

Naibu waziri wa Viwanda na Biashara JANET MBENE

Naibu waziri wa Viwanda na Biashara JANET MBENE amevishauri viwanda vya vileo kutumia mazao yanayozalishwa nchini ili kuwawezesha wakulima kuwa na soko la uhakika la mazo yao. 

Akizungumza baada ya kutembelea kiwanda cha bia cha Serengeti cha mjini MOSHI mkoani KILIMANJARO, MBENE amesema malighafi kama shayiri, mtama na mahindi yanazalishwa kwa wingi hapa nchini na hivyo hakuna sababu ya viwanda kuagiza mazao hayo nje. 

Naye Meneja wa kiwanda hicho, GIDEON KABUTHI amesema kiwanda chake kinakabiliwa na changamoto za kukatika kwa umeme mara kwa mara, jambo ambalo linaathiri shughuli za uzalishaji kiwandani hapo. 

Katika hatua nyingine Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, JANET MBENE, amevitaka viwanda vinavyozalisha vyakula nchini kuzingatia usalama na ubora wa vyakula kwa kutumia vipimo sahihi vinavyobaini uhakika wa chakula kwa walaji.
Share this article :
 
Support : #BegaKwaBegaNaMamaSamia | JAK | CCM Arusha
Copyright © 2011. CCM Dijitali - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Jasper K
Proudly powered by Blogger
Link