Mkurugenzi Mtendaji wa Jiji la Arusha, Juma Idd
Imeandikwa na Veronica Mheta, Arusha /Habari Leo
WANASIASA na viongozi wengine mkoani Arusha wameshauriwa kuhamasisha wawezekaji wa ndani kuwekeza katika maeneo yaliyobomolewa nyumba na Halmashauri ya Jiji la Arusha kwa ajili ya ujenzi wa vitega uchumi.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Arusha, Juma Idd wakati alipokuwa akizungumza katika kikao cha baraza la madiwani.
Alisema wanasiasa wana nafasi kubwa ya kuhamasisha wawekezaji katika maeneo hayo yakiwemo eneo la Kaloleni na Themi jijini hapa.
Alisema katika maeneo hayo kulikuwa na nyumba zilizobomolewa kupisha ujenzi wa vitega uchumi mbalimbali.
Alisisitiza kwamba maeneo hayo hayatatolewa kinyemela.
Aidha Mkurugenzi huyo aliwataka madiwani kwa kushirikiana na viongozi wa kata zao kusimamia kikamilifu na kuzuia maambukizi ya ugonjwa wa kipindupindu unaosababishwa na uchafu wa mazingira.
Meya wa Jiji la Arusha, Calist Lazaro alisema halmashauri hiyo imewaelekeza wataalamu wake kuja na miradi michache ambayo inatekelezeka kwa wakati. Alisema hivi sasa hawatakuwa na miradi mingi ambayo mwisho wa mwaka haimaliziki.
DED wa Arusha ahimiza uwekezaji vitega uchumi
Written By CCMdijitali on Tuesday, February 16, 2016 | February 16, 2016
Related Articles
- WAZIRI MKUU MHE. KASSIM MAJALIWA MAJALIWA ATUA MKOANI ARUSHA.
- RC MONGELLA AAGIZA VITUO VYOTE VYA AFYA KUTUMIA MFUMO GotHoMIS
- WANANCHI WA NGORONGORO WAHAMIA MAENEO WALIYOCHAGUA NJE YA HIFADHI.
- PPAA yawanoa wazabuni Kanda ya Kaskazini
- VIONGOZI WANALOJUKUMU LA KUZINGATIA MATUMIZI YA TAKWIMU ZA MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022.
- MFUMO UNGANISHI KUONDOA CHANGAMOTO SEKTA YA ARDHI- PINDA
Labels:
ARUSHA