Home » » Rais Magufuli akubali Mkuu wa Magereza kusitisha mkataba

Rais Magufuli akubali Mkuu wa Magereza kusitisha mkataba

Written By CCMdijitali on Friday, December 2, 2016 | December 02, 2016

John Minja
Imeandikwa na Mwandishi Wetu - Habari Leo

Rais John Magufuli amekubali na kuridhia ombi la kusitisha mkataba na kustaafu kwa Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini Kamishna Jenerali wa Magereza (CGP) John Minja kuanzia leo.

Taarifa ya Ikulu jijini Dar es Salaam imesema Rais Magufuli amempongeza Kamishna Jenerali wa Magereza Mstaafu John Minja kwa utumishi wake na amemtakia maisha mema ya kustaafu.

Wakati huo huo, Rais Magufuli amemteua Kamishna wa Magereza (CP) Dkt. Juma Malewa kuwa Kaimu Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini hadi hapo uteuzi wa Kamishna Jenerali wa Magereza utakapofanyika.

Share this article :
 
Support : #BegaKwaBegaNaMamaSamia | JAK | CCM Arusha
Copyright © 2011. CCM Dijitali - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Jasper K
Proudly powered by Blogger
Link