Home » » 📍OPERESHENI ANWANI ZA MAKAZI SASA NI ASILIMIA 67📍

📍OPERESHENI ANWANI ZA MAKAZI SASA NI ASILIMIA 67📍

Written By CCMdijitali on Thursday, March 31, 2022 | March 31, 2022

  








📍OPERESHENI ANWANI ZA MAKAZI 

SASA NI ASILIMIA 67📍


Operesheni ya uwekaji wa Anwani za Makazi nchini iliyotangazwa tarehe 8 Februari mwaka huu wa 2022 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan sasa utekelezaji wake umefikia asilimia 67 kulingana na takwimu za mfumo unaopokea taarifa za utekelezaji wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Taarifa hiyo imetolewa na Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye wakati wa mkutano na Wakuu wa Mikoa yote nchini uliofanyika jijini Dodoma uliolenga kutoa taarifa ya utekelezaji wa operesheni hiyo

“Tathimini iliyofanyika ya kupata asilimia 67 imezingatia kazi zilizotekelezwa ikiwa ni kazi ya kutambua maeneo; kujenga uwezo kwa maafisa na watendaji wanaofanya kazi hii; kutoa elimu ya zoezi husika; kukusanya taarifa; kutengeneza mfumo utakaopokea taarifa na kuingiza taarifa kwenye mfumo ili ziweze kutumika na kuweka muundombinu (physical) katika maeneo mbalimbali nchini”, amezungumza Mhe. Nape


Ameongeza kuwa mwenendo wa utekelezaji unaonesha matumaini ya zoezi kukamilika kabla ya muda uliopangwa na kazi itakayofuata itakuwa ni kusafisha baadhi ya taarifa kwenye mfumo kwa hatua za kuukabidhi mfumo kwa mujibu wa maelekezo ya kuukabidhi ifikapo tarehe 22 Mei, mwaka 2022.
@samia_suluhu_hassan @ikulu_mawasiliano @ikulu_habari @kassim_m_majaliwa @napennauye @innocentbash @drjimyonazi @ortamisemi @wizara_ya_ardhi @tcra_tanzania @ucsaftz @ttcl_corporation @posta_tz

Share this article :
 
Support : #BegaKwaBegaNaMamaSamia | JAK | CCM Arusha
Copyright © 2011. CCM Dijitali - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Jasper K
Proudly powered by Blogger
Link