Home » » PROF. MAKUBI AWATAKA WATUMISHI WA WIZARA AFYA KUFUATA MIONGOZO YA UNUNUZI

PROF. MAKUBI AWATAKA WATUMISHI WA WIZARA AFYA KUFUATA MIONGOZO YA UNUNUZI

Written By CCMdijitali on Thursday, March 31, 2022 | March 31, 2022

  











PROF. MAKUBI AWATAKA WATUMISHI WA WIZARA 

AFYA KUFUATA MIONGOZO YA UNUNUZI


Wakurugenzi wa taasisi na wa Hospitali za rufaa za mikoa wametakiwa kufuata miongozo na sheria za manunuzi ili kuondoa hati chafu na zenye mashaka kwenye taasisi zao.

Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya afya Prof. Abel Makubi wakati akiendesha mkutano wa baraza kuu la wafanyakazi wa Wizara ya afya, taasisi pamoja waganga wakuu wa Hospitali za rufaa za mikoa lililofanyika jijini Dodoma.

Prof. Makubi amesema ni viongozi wanatakiwa kuwa mfano katika utekelezaji wa majukumu yao mahali pa kazi kwa kufuata miongozo na sheria ya manunuzi ya bidhaa kwa ajili ya mahitaji ya ofisi au ujenzi pamoja na maboresho ya miundombinu ya hospitali zao ili kuondokana na hati chafu au zenye mashaka.

Aidha, Prof. Makubi aliwataka waganga wafawidhi wa hospitali za Rufaa za Mikoa kuhakikisha wanasimamia upatikanaji wa dawa, vifaa na vifaa tiba kwenye hospitali zao.

"Ifike muda kila mgonjwa anayefika kwenye hospitali yako uhakikishe anapata dawa zilizopo kwenye mwongozo wa dawa (STG). Tunataka malalamiko yanayotolewa na wananchi yapungue ikiwemo ukosefu wa dawa pamoja na kutopata huduma kwa wakati". Alisisitiza Prof. Makubi.


Hata hivyo, Katibu Mkuu huyo aliwakumbusha viongozi hao pindi wanaporudi kwenye vituo vyao vya kazi kuwakumbusha madaktari walio chini yao kuandika dawa zilizopo kwenye muongozo huo na wahakikishe dawa wanazoziagiza ni zile ambazo zipo kwenye muongozo.

Prof. Makubi amewataka watumishi hao kutofanya kazi kwa mazoea na wanatakiwa kufanya kazi kulingana na kasi ya utendaji wa viongozi waliopo na kutekeleza majukumu wanayopangiwa kwa weledi.

Share this article :
 
Support : #BegaKwaBegaNaMamaSamia | JAK | CCM Arusha
Copyright © 2011. CCM Dijitali - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Jasper K
Proudly powered by Blogger
Link