Home » » WAZIRI DKT.PINDI CHANA ATEMBELEA ONESHO LA KIMATAIFA LA UTALII LA SWAHILI.

WAZIRI DKT.PINDI CHANA ATEMBELEA ONESHO LA KIMATAIFA LA UTALII LA SWAHILI.

Written By CCMdijitali on Saturday, October 22, 2022 | October 22, 2022

Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana (Mb) ametembelea Onesho la Kimataifa la Utalii la Swahili lililoanza leo jijini Dar es Salaam akiwa ameambatana na Naibu Waziri wake ,Mhe. Mary Masanja(Mb).

Lengo kuu la Onesho hilo ni kutangaza vivutio vya utalii vilivyoko nchini Tanzania, na kukutanisha wanunuzi na wauzaji wa bidhaa za utalii wa Kitaifa na Kimataifa.

Onesho hilo litahudhuriwa na waoneshaji zaidi 200, wanunuzi wa Kimataifa takribani 100 kutoka masoko ya Kimakakati hususan nchi za Marekani, Uholanzi, Afrika Kusini, India, Urusi, Hispania, UAE, Poland, Finland, Japan, Oman na nyinginezo.

Onesho hilo litamalizika tarehe 23 Oktoba 2022.









Share this article :
 
Support : #BegaKwaBegaNaMamaSamia | JAK | CCM Arusha
Copyright © 2011. CCM Dijitali - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Jasper K
Proudly powered by Blogger
Link