Home » » WAZIRI JAFO ASHIRIKI ZOEZI LA KUPANDA MITI KATIKA WILAYA YA BAGAMOYO.

WAZIRI JAFO ASHIRIKI ZOEZI LA KUPANDA MITI KATIKA WILAYA YA BAGAMOYO.

Written By CCMdijitali on Saturday, October 22, 2022 | October 22, 2022

Waziri wa Nchi ofisi ya Makamu wa Rais( Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt Selemani Jafo ameshiriki katika zoezi la upandaji miti lililofanyika katika  shule ya Msingi Mtoni iliyopo katika Wilaya ya Bagamoyo.

Akiwa shuleni hapo amepongeza Benki ya Standard Chattered ambao ndiyo waandaaji na wasimamizi wakubwa wa tukio hilo la upandaji miti katika shule hiyo.

“Nawapongeza sana benki ya Standard Chattered kwa kunialika kuwa Mgeni Rasmi katika shughuli hii ya upandaji miti ambayo ni mwendellezo wa juhudi katika kuendelea kutunza na kuhifadhi mazingira kwa kupanda miti”. Mhe Dkt Jafo

Aidha  ameziagiza Halmashauri zote Nchini ambazo hazijafikia malengo ya upandaji miti kama ilivyokua imeelekezwa awali  kuhakikisha wanapanda miti na kufanikisha azma hiyo ya Serikali ya ukupanda miti kwa wingi katika kila Halmashauri Nchini ili kuweza kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

“Naagiza Halmashauri zote kuhakikisha zinafikia malengo ya kupanda miti ili kuweza kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi. Mabadiliko ya tabianchi ni changamoto kubwa  inayoikabili dunia kwani husababisha, ukame, kuongezeka kwa kina cha bahari na maziwa”. Mhe Dkt Jafo

Naye Mkurugenzi wa Standard Chattered Bwana Herman Kasekende  amesema watendelea kuunga mkono juhudi za Serikali  kwa kusimamia zoezi la upandaji miti katika mashule mbalimbali  ili kusaidia kutunza na kuhifadhi mazingira.

#Kaziiendelee
#MheDktJafo
#Zoeziendelevulaupandajimiti 
#MitiRafikikwaMazingira 
#VivulinaMatundaMengineyo 
#KupambanaMabadilikoyaTabianchi 
#DktJafoktkMazingira 1
#Endeleakuupigamwingi 
#SSH2025🇹🇿
#MunguIbariki🇹🇿







Share this article :
 
Support : #BegaKwaBegaNaMamaSamia | JAK | CCM Arusha
Copyright © 2011. CCM Dijitali - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Jasper K
Proudly powered by Blogger
Link