Home » » 𝗠𝗔𝗩𝗨𝗡𝗗𝗘: 𝗨𝗧𝗘𝗞𝗘𝗟𝗘𝗭𝗔𝗝𝗜 𝗪𝗔 𝗠𝗜𝗥𝗔𝗗𝗜 𝗬𝗔 𝗨𝗝𝗘𝗡𝗭𝗜 𝗪𝗔 𝗠𝗔𝗕𝗪𝗔𝗪𝗔 𝗬𝗔 𝗨𝗠𝗪𝗔𝗚𝗜𝗟𝗜𝗔𝗝𝗜 𝗜𝗧𝗔𝗖𝗛𝗢𝗖𝗛𝗘𝗔 𝗞𝗨𝗞𝗨𝗔 𝗞𝗪𝗔 𝗦𝗘𝗞𝗧𝗔 𝗬𝗔 𝗞𝗜𝗟𝗜𝗠𝗢.

𝗠𝗔𝗩𝗨𝗡𝗗𝗘: 𝗨𝗧𝗘𝗞𝗘𝗟𝗘𝗭𝗔𝗝𝗜 𝗪𝗔 𝗠𝗜𝗥𝗔𝗗𝗜 𝗬𝗔 𝗨𝗝𝗘𝗡𝗭𝗜 𝗪𝗔 𝗠𝗔𝗕𝗪𝗔𝗪𝗔 𝗬𝗔 𝗨𝗠𝗪𝗔𝗚𝗜𝗟𝗜𝗔𝗝𝗜 𝗜𝗧𝗔𝗖𝗛𝗢𝗖𝗛𝗘𝗔 𝗞𝗨𝗞𝗨𝗔 𝗞𝗪𝗔 𝗦𝗘𝗞𝗧𝗔 𝗬𝗔 𝗞𝗜𝗟𝗜𝗠𝗢.

Written By CCMdijitali on Saturday, November 12, 2022 | November 12, 2022



𝗠𝗔𝗩𝗨𝗡𝗗𝗘: 𝗨𝗧𝗘𝗞𝗘𝗟𝗘𝗭𝗔𝗝𝗜 𝗪𝗔 𝗠𝗜𝗥𝗔𝗗𝗜 𝗬𝗔 𝗨𝗝𝗘𝗡𝗭𝗜 𝗪𝗔 𝗠𝗔𝗕𝗪𝗔𝗪𝗔 𝗬𝗔 𝗨𝗠𝗪𝗔𝗚𝗜𝗟𝗜𝗔𝗝𝗜 𝗜𝗧𝗔𝗖𝗛𝗢𝗖𝗛𝗘𝗔 𝗞𝗨𝗞𝗨𝗔 𝗞𝗪𝗔 𝗦𝗘𝗞𝗧𝗔 𝗬𝗔 𝗞𝗜𝗟𝗜𝗠𝗢.

Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Anthony Mavunde amesema utekelezaji wa miradi ya mabwawa unaoendelea nchini hivi sasa utasaidia sana kukuza sekta ya kilimo nchini Tanzania na kuongeza eneo kubwa zaidi linalofanya kilimo cha umwagiliaji.

Naibu Waziri Mavunde ameyasema hayo leo tarehe 12 Novemba, 2022 wakati wa ukaguzi wa ujenzi wa bwawa la Membe linalojengwa Wilayani Chamwino, Dodoma.

"Katika bajeti ya mwaka 2022/2023 Serikali kupitia Tume ya Umwagiliaji imepanga kujenga jumla ya mabwawa 14 nchi nzima, likiwemo bwawa hili la Membe litakalo kuwa na uwezo wa kuhifadhi maji lita Bilioni 12."

Pamoja na bwawa hili kutumika katika shughuli za umwagiliaji, pia litawekwa miundombinu ya kusaidia unyweshaji maji mifugo, kupeleka maji ya matumizi ya majumbani kwa vijiji vinavyozunguka na kuwa sehemu ya utalii kwa wananchi mbalimbali, hatua ambayo itaongeza mapato ya Halmashauri ya Chamwino.

"Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan ametuongezea bajeti Wizara ya Kilimo ambapo fedha nyingi zimeelekezwa katika miradi ya umwagiliaji ili kuhakikisha tunakuwa na vyanzo vya uhakika vya maji na kuwezesha wakulima kufanya kilimo zaidi ya mara moja ndani ya mwaka”Alisema Mavunde

Vilevile, Mhe Mavunde alimpongeza Bw. Raymond Mndolwa, Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji kwa kazi nzuri anayoifanyia ya usimamizi madhubuti wa mkakati wa Serikali wa kendeleza kilimi cha umwagiliaji, na kubainisha kuwa ni wazi kuwa ndoto ya Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan ya kufikia eneo la umwagiliaji la hekta 1,200,000 ifikapo 2025 linaenda kufikiwa.

Naye Diwani wa Kata ya Membe Wilayani Chamwino, Mheshimiwa Simon Petro Machengu alimshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwaletea mradi huo mkubwa kwenye Kata yake, na kubainisha kuwa wananchi wa Membe hawana cha kumlipa zaidi ya kumwombea kwa Mungu ili azidi kumpa afya njema na utashi wa kuwatumikia watanzania.
@bashehussein @anthonymavunde 
@nirc_tz

#SSH
#Agenda10/30 
#KilimoNiBiashara




Share this article :
 
Support : #BegaKwaBegaNaMamaSamia | JAK | CCM Arusha
Copyright © 2011. CCM Dijitali - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Jasper K
Proudly powered by Blogger
Link