Home » » WAZIRI BASHUNGWA AMTEMBELEA RAIS MWINYI, IKULU ZANZIBAR

WAZIRI BASHUNGWA AMTEMBELEA RAIS MWINYI, IKULU ZANZIBAR

Written By CCMdijitali on Friday, November 11, 2022 | November 11, 2022

WAZIRI BASHUNGWA AMTEMBELEA RAIS MWINYI, IKULU ZANZIBAR 


Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mheshimiwa Innocent Lugha Bashungwa(Mb) leo tarehe 11 Novemba 2022, amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dk.Hussein Ali Mwinyi. Ikulu, Zanzibar. 

Hii ni ziara maalum ya Waziri Bashungwa kumtembelea na kufanya Mazungumzo na Rais wa Zanzibar, Mheshimiwa Hussein Ali Mwinyi ambaye pia aliwahi kuiongoza Wizara ya Ulinzi na JKT kabla ya nafasi ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi.

Kadhalika, Waziri Bashungwa amemshukuru na kumpongeza Rais Mwinyi kwa kuhudumu wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa miaka 11 huku akiahidi kuendelea kusimamia misingi aliyoianzisha kwa manufaa ya ustawi wa nchi na ustawi wa Muungano.

MWISHO



Share this article :
 
Support : #BegaKwaBegaNaMamaSamia | JAK | CCM Arusha
Copyright © 2011. CCM Dijitali - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Jasper K
Proudly powered by Blogger
Link