"AWATULIZA WALIOMSIMAMISHA NA NDOO ZA MAJI"
Katibu mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Komredi Daniel Godfrey Chongolo ameonekana kutoridhishwa na hatua ya Ujenzi wa Hospitali ya Wilaya katika Halmashauri ya Sumbawanga Vijijini, ambapo ameagiza Serikali mkoani Rukwa pamoja na Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kutuma timu ya uchunguzi ili kubaini kinachokwamisha mradi huo kukamilika, huku ukionekana kutekelezwa chini ya kiwango cha ubora na thamani ya fedha kilichopelekewa hadi sasa.
Mbali na kutoridhishwa na ujenzi huo wa hospitali unavyotekelezwa, Komredi Chongolo pia alionekana kukerwa na mkandarasi wa Mradi wa Maji wa Ilemba, Jimbo la Kwela, ambaye pamoja na RUWASA Mkoa wa Rukwa kumwekea msukumo ili ajenge kwa kasi ya kukamilisha ndani ya muda wa mkataba, bado ameendelea kusuasua huku akitoa visingizio vingi vya kutomaliza kazi hiyo kwa wakati ili wananchi wa Kata ya Ilemba, Vijiji vya Ilemba A na B na Kata ya Kaswepa, wapate maji safi na salama ya kutumia.
#CCMImara
#Kaziinaendelea












