Home » » MKANDARASI WA MAJI, UJENZI HOSPITALI SUMBAWANGA DC 'WAMCHEFUA' CHONGOLO

MKANDARASI WA MAJI, UJENZI HOSPITALI SUMBAWANGA DC 'WAMCHEFUA' CHONGOLO

Written By CCMdijitali on Wednesday, October 11, 2023 | October 11, 2023

"AWATULIZA WALIOMSIMAMISHA NA NDOO ZA MAJI"


Katibu mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Komredi Daniel Godfrey Chongolo ameonekana kutoridhishwa na hatua ya Ujenzi wa Hospitali ya Wilaya katika Halmashauri ya Sumbawanga Vijijini, ambapo ameagiza Serikali mkoani Rukwa pamoja na Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kutuma timu ya uchunguzi ili kubaini kinachokwamisha mradi huo kukamilika, huku ukionekana kutekelezwa chini ya kiwango cha ubora na thamani ya fedha kilichopelekewa hadi sasa.

Mbali na kutoridhishwa na ujenzi huo wa hospitali unavyotekelezwa, Komredi Chongolo pia alionekana kukerwa na mkandarasi wa Mradi wa Maji wa Ilemba, Jimbo la Kwela, ambaye pamoja na RUWASA Mkoa wa Rukwa kumwekea msukumo ili ajenge kwa kasi ya kukamilisha ndani ya muda wa mkataba, bado ameendelea kusuasua huku akitoa visingizio vingi vya kutomaliza kazi hiyo kwa wakati ili wananchi wa Kata ya Ilemba, Vijiji vya Ilemba A na B na Kata ya Kaswepa, wapate maji safi na salama ya kutumia.

#CCMImara
#Kaziinaendelea
 

 









Share this article :
 
Support : #BegaKwaBegaNaMamaSamia | JAK | CCM Arusha
Copyright © 2011. CCM Dijitali - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Jasper K
Proudly powered by Blogger
Link