Home » » SHIBUDA AMPONGEZA RAIS SAMIA KWA KUMTEUA MAKONDA KUWA MWENEZI WA CCM

SHIBUDA AMPONGEZA RAIS SAMIA KWA KUMTEUA MAKONDA KUWA MWENEZI WA CCM

Written By CCMdijitali on Monday, November 20, 2023 | November 20, 2023


MAGALLE SHIBUDA AMPONGEZA RAIS SAMIA KWA KUMTEUA MAKONDA KUWA MWENEZI WA CCM KWANI AMEONESHA JUHUDI NA SHABAHA ZA KUUNDA DARAJA RAFIKI KWA KAZI ZA RAIS SAMIA NA WATANZANIA


  • Asema Makonda amejenga uhusiano rafiki wa Kanda ya ziwa kwa kutoa Ahsante kwa uwajibikaji wa Serikali ya awamu ya 6 ya CCM chini ya Rais Samia Suluhu Hassan

  • Amejenga na kuleta wokovu wa mlango wa kutokea huzuni za ndani zilizounda ugumu wa mioyo katika kufumbua maono ya Ahsante_

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Baraza la Vyama Vya Siasa, MNEC Mstaafu na Mbunge wa (CCM 2005 & CHADEMA 2010) Mstaafu Magalle John Paul Shibuda ametoa barua aliyoandika Manufaa na Faida kwa Chama Cha Mapinduzi kutokana na Ziara ya Mikoa ya Kanda ya ziwa iliyofanywa na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Itikadi, Uenezi na Mafunzo Ndg. Paul Makonda.

Katika Barua hiyo, Mstaafu Shibuda ameandika kuwa Ziara ya Mwenezi Makonda imebainisha wazi kuwa kuna maisha ya Wajibu wa Uzalendo hitajika wa kufaidisha manufaa ya Maslahi mapana kwa Ujenzi wa kuunda Ustawi na Maendeleo ya Jamii, Uchumi na Taifa.

Mstaafu Shibuda amesema Rais wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan anastahili Tuzo za Utu kwa hali na sababu ni Kiongozi Mkwamuaji wa madhila yaundayo Huzuni.

Amesema kwa kuthibitishi hilo, Watanzania warejee kwa uundwaji wa Kamati kadhalika mfano ya Mhe. Jaji Mstaafu Othman Chande ya kuimairsha Haki za Raia.

Mstaafu Shibuda ameendelea kuandika kuwa Ziara ya Mwenezi Makonda imewadhiirishia Umma kuwa Serikali ya awamu ya 6 ina unyenyekevu wa kutumikia Maslahi ya Umma na kusema kuwa Simu zote kwa Mawaziri ni Fursa rafiki kwa Umma nao utambue kwa umakini na ukubali kuwa ni Uwazi na Ukweli pana mipango ya kazi za kutengua kasoro zinazounda sintofahamu kwa yao matumaini na matarajio ya Wananchi.

Pia, Mstaafu Shibuda amesema binafsi yake ameona Mwenezi Makonsa ameunda vema somo la kwamba Serikali ina wajibu wa kukithaminisha chama kinachoongoza Serikali hiyo ambacho ni CCM na vivyo hivyo CCM ina wajibu wa kuisadikisha Tija ya Serikali yake ndani ya Umma dhisi ya Propaganda Hasi za Vyama Kinzani.

Aidha, Mstaafu Shibda amemtaka Mwenezi Makonda kuendelea kusomesha kuhusu yeye anatenda uwajibikaji wake aminifu kwa Katiba ya Chama Cha Mapinduzi.

Kwa kumalizia, Mstaafu Shibuda ametoa rai kwa CCM kuwa macho na kupambanua akili zao dhidi ya mikakati ya wazuaji wa tafsiri ovu ambazo zinataka kuunda hali ya kuchafuana wenyewe kwa wenyewe na kuwataka kutokuwa malighafi au kitoweo cha Propaganda hasi za kujenga kuandika Uongo mtamu dhidi ya umoja na mshikamano wao.

MWISHO.



Share this article :
 
Support : #BegaKwaBegaNaMamaSamia | JAK | CCM Arusha
Copyright © 2011. CCM Dijitali - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Jasper K
Proudly powered by Blogger
Link