Na Mwantanga Juma MaelezoWaziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Katiba, Sheria Utumishi  na Utawala Bora Dkt. Harouna Ali Suleiman ameviomba vyombo vya Sheria kuhakikisha wanatenda haki ili suluhu ...

Read more »

Asema Rais Dkt. Samia ametoa shilingi bilioni 130 kwa ajili ya ukarabati madaraja mkoa wa Lindi. Awatoa hofu wakazi na watumiaji wa barabara ya Dar, Lindi. WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amet ...

Read more »

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amesema Serikali ya Awamu ya Sita itaendelea kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji nchini ikiwemo kuimarisha hali ya u ...

Read more »

 Na Mwandishi wetu, ArushaMamlaka ya Rufani ya Zabuni za Umma (PPAA) imeendelea na zoezi la kuwajengea uwezo wazabuni kuhusu matumizi ya Moduli ya kuwasilisha na kushughulikia malalamiko na rufa ...

Read more »

 Kaimu Naibu Wakili Mkuu wa Serikali, Bi. Vivin Method akizungumza na watumishi wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali wakati akifungua Mafunzo kuhusu Upimaji wa Afya yaliyofanyika jijini Dar es Sa ...

Read more »

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Ukraine zimekubaliana kuongeza ushirikiano katika sekta mbalimbali za kiuchumi na kijamii ikiwemo kilimo, biashara na uwekezaji, viwanda, utalii, elimu n ...

Read more »

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb), amewasili jijini Antalya, Uturiki kwa ziara ya kikazi anayotarajia kuifanya nchini humo kuanzia Aprili ...

Read more »

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt, Hussein Ali Mwinyi ameeleza kuwa Ziara yake Uingereza imekuwa na Manufaa Makubwa kwa Zanzibar kwani Wawekezaji wengi wameonesha dhamira ya k ...

Read more »

WAZIRI HAROUNA KUZINDUA KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA YA MAMA SAMIA KASKAZINI UNGUJA

  Na Mwantanga Juma Maelezo Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Katiba, Sheria Utumishi  na Utawala Bora Dkt. Harouna Ali Suleiman ameviomba vyomb...

Latest Post

WAZIRI HAROUNA KUZINDUA KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA YA MAMA SAMIA KASKAZINI UNGUJA

Written By CCMdijitali on Wednesday, April 23, 2025 | April 23, 2025

 Na Mwantanga Juma Maelezo


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Katiba, Sheria Utumishi  na Utawala Bora Dkt. Harouna Ali Suleiman ameviomba vyombo vya Sheria kuhakikisha wanatenda haki ili suluhu zipatikane hasa Kwa migogoro ya ardhi.

Akizindua kampeni ya Msaada wa kisheria ya mama Samia mkoa wa kaskazini unguja katika uwanja wa Tumaini Mkwajuni amesema kutokana na kilio Cha muda mrefu Kwa wananchi kunyimwa haki zao hivyo Kwa kampeni hii timu za wataalamu zitaweza kuwasikiliza katika masuala mbalimbali yakiwemo ya jinsia na migogoro ya ardhi.

Amesema Matarajio baada ya  kukamilika Kwa utekelezaji wa kampeni hiyo ni kupata uelewa zaidi Kwa wananchi kuhusu upatikanaji wa haki, mifumo ya kisheria iliopo, haki za binaadam na makundi maalumu.

Dkt. Mw. Harouna amefahamisha kwamba kampeni  hiyo inatarajiwa kufikia asilimia 75 katika utoaji wa huduma za wananchi  hadi Sasa kampeni imewafikia wananchi takriban 1246 Kwa mikoa iliozinduliwa.

 "masheha kutokujiingiza katika migogoro ya kisheria ambayo hawana elimu nayo na badala yake kuwapeleka wananchi kwenye vyombo husika Kwa kupata ufafanuzi zaidi" alisisitiza Dkt. Harouna.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya katiba na sheria Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Franklin Rwezimula amesema kampeni hiyo imekuwa na muitikio mkubwa Kwa walengwa na kusaidia kutatua matatizo mbalimbali ya kisheria Kwa wananchi Kwa kupelekwa mashauri yao mahakamani Kwa wakati na kwa haraka zaidi.

Aidha Rwezimula amesema Wizara imepewa dhamana ya jukumu la kutoa msaada wa kisheria nchini Kwa wananchi kupata haki zao za kisheria.

Akimkaribisha mgeni rasmi mkuu wa mkoa wa kaskazini unguja mhe.  Mattar Zahor Masoud amesema kampeni hiyo Kwa kaskazini ni msaada mkubwa Kwa wananchi kupata msaada huo bure Kwa siku 9.

Amesema mkoa wa kaskazini umegubikwa na  changamoto nyingi hasa migogoro ya ardhi hivyo kampeni hiyo itakuwa ni msaada mkubwa kupunguza malalamiko ndani ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na Mkuu wa Wilaya

Amewataka uongozi wa Mkoa utahakikisha unasimamia katika kuwahamasisha wananchi kuyafikia maeneo hayo yanayotolewa huduma Kwa takriban siku zote 9 ndani ya Mkoa huo.

kampeni hiyo ya Kitaifa ya msaada wa kisheria ya mama Samia Leo imezinduliwa Katika Mkoa wa Kaskazini Unguja huku ikibakisha  Mikoa miwili Kwa Zanzibar ambayo ni kusini Unguja na Kusini Pemba imebeba kauli mbiu isemayo msaada wa kisheria Kwa haki, usawa, amani na maendeleo.












MAJALIWA AIPA MAAGIZO TANROADS UKARABATI WA BARABARA NA MADARAJA

Written By CCMdijitali on Wednesday, April 16, 2025 | April 16, 2025



Asema Rais Dkt. Samia ametoa shilingi bilioni 130 kwa ajili ya ukarabati madaraja mkoa wa Lindi.
 
Awatoa hofu wakazi na watumiaji wa barabara ya Dar, Lindi.
 
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa ametoa maagizo kwa Mameneja wa Wakala ya Barabara nchini (TANROADS) kufanya ukaguzi wa mara kwa mara kwenye madaraja na makalavati yote ya barabara kuu nchini ili kuepuka athari zinazoweza kusababishwa na maji ya mvua.
 
Ametoa agizo hilo leo Jumatano (Aprili 16, 2025) alipokagua maendeleo ya ukarabati wa madaraja katika maeneo ya Matandu na Somanga Mtama, Wilaya Kilwa Mkoani Lindi kwenye barabara kuu ya Dar es Salaam - Lindi yaliyokuwa yamekatika kufuatia mvua zinazonyesha nchini.
 
“Fedha ambayo tunatenga kwa ajili ya ukarabati itumike ipasavyo kila baada ya mvua kubwa kunyesha wakajiridhishe na kama kipenyo cha daraja na makavati yapo vilevile”
 
Pia amemuagiza Meneja wa Tanroads Mkoa wa Lindi kufanya kazi usiku na mchana ili kuhakikisha maeneo yote yaliyoathirika na maji ya mvua yanatengenezwa na kuyarudisha katika hali yake ya kawaida.
 
Amesema kuwa Serikali ina mpango wa muda mrefu wa kujenga upya barabara ya Dar es Salaam, Lindi na Mtwara kwa viwango, hivyo ujenzi wa madaraja ni hatua ya awali ya mpango mkakati huo. “Tumetenga fedha ya ujenzi wa kilomita 100, tumefanya hivi ili kuepuka kuweka viraka viraka badala yake tujenge upya eneo lote korofi.”
 
Kadhalika amewahakikishia watumiaji wa barabara hiyo kwamba hakuna shughuli itakayo simama wakati Serikali ipo na itaendelea kufuatilia mwenendo wa uimarishaji wa barabara hiyo. “Lengo ni kuhakikisha, Serikali ipo kazini, na imeshaleta wakandarasi hii ni kutokana na maelekezo ya Rais wetu, Dkt. Samia Suluhu Hassan.”
 
Aidha, Mheshimiwa Majaliwa amewahakikishia wakazi wa mikoa ya Lindi na Mtwara kuwa Rais Dkt. Samia ametoa fedha kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa vipande vilivyoharibiwa na mvua zinazoendelea kunyesha.
 
Naye, Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega amesema kuwa mpaka sasa mkandarasi ameshaweka nguzo 23 kati ya 43 kwa ajili ya ujenzi wa daraja la kudumu kwenye eneo la Somanga. “

Published from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android App

Makamu wa Rais afungua Kongamano la Kodi na Uwekezaji la Mwaka 2025




Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amesema Serikali ya Awamu ya Sita itaendelea kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji nchini ikiwemo kuimarisha hali ya ulinzi, amani na usalama na kuboresha mfumo wa viwango vya kodi.
 
Makamu wa Rais amesema hayo wakati akifungua Kongamano la Kodi na Uwekezaji la Mwaka 2025 linalofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam. Ametoa rai kwa washiriki wa Kongamano hilo kujielekeza katika kuibua mawazo na mikakati mipya itakayowezesha Taifa kuongeza makusanyo ya mapato ya ndani na hivyo kuiwezesha Serikali kutoa huduma bora kwa wananchi na kupunguza utegemezi kwa wahisani.
 
Aidha ametoa wito kwa wananchi kutumia vema fursa inayotolewa na Serikali kila mwaka kutoa maoni na kuwasilisha mapendekezo yao ya kuboresha sera za kodi na uwekezaji kwa kuchangia moja kwa moja katika jukwaa hilo au kupitia dirisha la kidigitali. Pia amewaagiza Mawaziri wa kila sekta kutoa maoni ya kuongeza mapato ya ndani katika sekta zao na kuhakikisha kuwa maoni na mapendekezo yatakayotolewa na wadau kwa njia mbalimbali yanafanyiwa kazi bila kudumaza ukuaji wa sekta husika.
 
Makamu wa Rais amesema zipo hatua mbalimbali zinazopaswa kutekelezwa zinazoweza kuongeza mapato ya ndani ikiwemo kuweka mkazo zaidi katika kuimarisha uwezo wa ukusanyaji na usimamizi wa mapato ya ndani, kuongeza jitihada katika kuboresha mfumo wa kodi ambao utahakikisha usawa na kuondokana na misamaha ya kodi isiyo na tija pamoja na kutoa vivutio vya kutosha kwa mawakala na taasisi za kukusanya kodi na kukabiliana na vitendo vya rushwa.
 
Makamu wa Rais ametaja hatua zingine za kutekelezwa ikiwemo kukuza matumizi ya TEHAMA katika ukusanyaji wa kodi na uwekaji wa akiba, kujenga kanzidata madhubuti ya taarifa za walipakodi na kufanya jitihada za kuongeza idadi ya walipa kodi kama njia ya kupunguza mzigo wa kodi, kubuni mbinu za kukabiliana na changamoto za kilojistiki na kisiasa katika utozaji wa kodi kutoka katika sekta isiyo rasmi, kuendelea kuboresha mazingira ya biashara ili kukuza uwekezaji pamoja na kuweka mfumo thabiti wa usimamizi, ufuatiliaji na upimaji kwa taasisi za kodi na zile za usimamizi.
Halikadhalika Makamu wa Rais amesema pamoja na jitihada kubwa zinazofanywa na Serikali ili kuongeza mapato, bado hali ya ulipaji kodi nchini inakabiliwa na changamoto mbalimbali hali inayopelekea ukuaji mdogo wa makusanyo ya ndani. Mathalan, uwiano wa mapato kwa Pato la Taifa umekuwa ukiongezeka kwa kasi ndogo katika kipindi cha zaidi ya miongo miwili kutoka 12.0% mwaka 2001/02 hadi 14.9% mwaka 2024/25.
 
Makamu wa Rais amelitaka Kongamano hilo kufanya tafakuri ya kina na kuainisha maboresho yanayohitajika kisera, kisheria, kikanuni na kiutaratibu ili kuwezesha uwekezaji na biashara na hivyo kuleta mageuzi makubwa katika mfumo wa kikodi na ukusanyaji wa mapato ya ndani.
 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Fedha na Mipango wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Saada Mkuya amesema Serikali ya Awamu ya Sita inatambua mchango wa Sekta Binafsi katika uwekezaji na hivyo imeendelea kuboresha mazingira ya uwekezaji na biashara nchini kupitia utekelezaji wa mpango wa kuboresha mazingira ya biashara nchini ili sekta binafsi iweze kushiriki kikamilifu katika kukuza uchumi wa Taifa.
 
Mhe. Mkuya ameongeza kwamba kupitia mpango huo, tozo na ada ambazo ni kero takribani 380 zimefutwa na baadhi zimepunguzwa. Amesema Serikali itaendelea kuhakikisha uhimilivu wa viashiria vya uchumi jumla, kuwa na sera za kodi ambazo zinatabirika na kuainisha tozo na ada mbalimbali zinazotozwa na Wizara na Mamlaka za udhibiti kwa lengo la kupunguza na kuimarisha usimamizi. Vilevile amesema mpango mwingine ni n matumizi ya TEHAMA ili kuweka urahisi wa kulipa kodi pamoja na kufanya biashara kwa ujumla.
 
Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi nchini Angelina Ngalula amesema ni vema elimu sahihi kuendelea kutolewa kwa wafanyabiashara ili waweze kurasimisha biashara zao hali itakayopelekea waweze kupata faida za mikopo na ufadhili na hivyo serikali kuongeza wigo wa ukasanyaji kodi.
 
Ameongeza kwamba, jitihada lazima zifanyike kupitia vitengo vya utafiti vya Wizara kuhakikisha elimu inapatikana kwa wafanyabiashara ili kuondokana na idadi ndogo ya walipa kodi ambao ni milioni mbili waliopo hivi sasa. 
 
Kongamano hilo linashirikisha viongozi wa Serikali, wadau mbalimbali wa sekta binafsi, wafanyabiashara na wawekezaji. Kauli mbiu ya Kongamano hilo ni “ Kuongeza ukuzaji wa rasilimali za ndani kupitia kustawisha fursa za wananchi”

Published from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android AppPublished from Blogger Prime Android App
 
Imetolewa na
Ofisi ya Makamu wa Rais
15 Aprili 2025
Dar es Salaam.

PPAA yawanoa wazabuni Kanda ya Kaskazini

Written By CCMdijitali on Friday, April 11, 2025 | April 11, 2025

 Na Mwandishi wetu, Arusha

Mamlaka ya Rufani ya Zabuni za Umma (PPAA) imeendelea na zoezi la kuwajengea uwezo wazabuni kuhusu matumizi ya Moduli ya kuwasilisha na kushughulikia malalamiko na rufaa kwa njia ya kielektroniki katika mfumo (NeST).

 

Akifungua mafunzo ya siku mbili (tarehe 10 – 11 Aprili, 2025) kwa wazabuni na wadau wa ununuzi wa Umma kutoka taasisi za Serikali kwa Kanda ya Kaskazini yaliyofanyika jijini Arusha, Katibu Mtendaji wa PPAA, Bw. James Sando amewasihi kujifunza matumizi ya moduli hiyo ili waweze kuitumia kwa ufasaha na kuisaidia Serikali kupata thamani halisi ya fedha.

 

Bw. Sando amesema kuwa moduli ya kupokea na kushughulikia malalamiko na rufaa kwa njia ya kielektroniki inafaida nyingi kwa wazabuni, taasisi nunuzi na PPAA kwa kuwa inarahisisha zoezi la uwasilishaji na ushughulikiwaji wa malalamiko na rufaa zinazotokana na michakato ya ununuzi wa umma.

 

“Moduli hii ina faida kadhaa zikiwemo kumsaidia mzabuni  kutolazimika kufika katika ofisi za taasisi nunuzi au za PPAA ili kuwasilisha lalamiko au rufaa yake na kupunguza gharama na muda kwa wazabuni kwa kuwa hawatatakiwa kusafiri ili kuweza kuwasilisha malalamiko au rufaa zao,” alisema Bw. Sando

 

Kadhalika, Bw. Sando ameainisha faida nyingine zinazotokana na matumizi ya moduli kuwa ni kuongeza uwazi katika mchakato wa ushughulikiwaji wa malalamiko na rufaa kwa kuwa mzabuni aliyewasilisha lalamiko au rufaa ataweza kuona hatua mbalimbali za ushughulikiaji wa lalamiko au rufaa yake.

 

Pamoja na mambo mengine, Bw. Sando amesema katika kipindi cha Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, PPAA imeweza kushughulikia mashauri 171 yaliyotokana na michakato mbalimbali ya Ununuzi wa Umma, ambapo katika mashauri hayo, PPAA ilizuia utoaji tuzo kwa zabuni 36 kwa wazabuni wasio na uwezo wa kifedha pamoja na wale waliokosa sifa za kitaalamu za kutekeleza zabuni husika.

 

“PPAA kwa kushirikiana na Wizara ya Fedha, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na taasisi zinazosimamia ununuzi wa Umma nchini, imeweza kushiriki katika kutungwa upya kwa Sheria ya Ununuzi wa Umma ya mwaka 2023 na Kanuni za Ununuzi wa Umma za Mwaka 2024 na Kanuni za Rufaa za Ununuzi wa Umma za Mwaka 2025,” aliongeza Bw. Sando.

 

Kwa upande wake Meneja wa Usimamizi wa Rufaa na Huduma za Sheria PPAA, Bi. Florida Mapunda amesema kuwa lengo la mafunzo hayo ni kuwaelimisha wadau wa ununuzi wa umma kuhusu matumizi ya moduli ya kuwasilisha na kushughulikia malalamiko na rufaa kwa njia ya kielektroniki katika mfumo wa NeST katika Kanda ya Kaskazini.

 

“Mtakumbuka kwa sasa Sheria ya Ununuzi wa Umma imeweka takwa la ulazima wa ununuzi wa umma kufanyika kwa njia ya Kieletroniki kupitia mfumo wa NeST. Kutokana na takwa hilo, PPAA imejenga moduli ya kupokea na kushughulikia malalamiko katika mfumo wa NeST ili kuwasaidia wadau wa ununuzi kuwasilisha malalamiko na rufaa kieletroniki pia,” alisema Bi. Mapunda.

 

Bi. Mapunda aliongeza kuwa, moduli imerahisisha zoezi la uwasilishaji wa malalamiko yatokanayo na michakato ya ununuzi wa umma pamoja na kusaidia utunzaji wa kumbukumbu za taarifa za malalamiko na rufaa ambazo zitakuwa zinawasilishwa katika michakato yote ya ununuzi wa umma.  

 

Naye Mkurugenzi wa Kampuni ya usambazaji wa vifaa mbalimbali kutoka Karatu ‘Gratian General Supplies’ Bi. Hilaria Joseph ameipongeza PPAA kwa kuandaa semina hiyo kwani imewasaidia kujua njia ya kuwasilisha malalamiko kwa wakati kupitia kwenye moduli ya kuwasilisha na kushughulikia malalamiko na rufaa kwa njia ya kielektroniki katika mfumo wa NeST.

 

Mafunzo hayo ya siku mbili kwa Kanda ya Kaskazini yamefanyika jijini Arusha kuanzia tarehe 10 – 11 Aprili, 2025 yanajumuisha mikioa ya Arusha, Manyara, Kilimanjaro na Tanga.

 

Awamu ya kwanza ya mafunzo kikanda yalifanyika Kanda ya Ziwa kwa siku tatu ambapo yalijumuisha washiriki zaidi ya 580 mkoani Mwanza kuanzia tarehe 4 – 6 Februari, 2025 yakijumuisha mikoa ya Mwanza, Geita, Mara, Kagera, Simiyu na Shinyanga.

Katibu Mtendaji wa PPAA, Bw. James Sando akifungua mafunzo ya siku mbili (tarehe 10 – 11 Aprili, 2025) kwa wazabuni na wadau wa ununuzi wa Umma kutoka taasisi za Serikali (hawapo pichani) kwa Kanda ya Kaskazini jijini Arusha


Katibu Mtendaji wa PPAA, Bw. James Sando (aliyekaa Katikati), Meneja wa Huduma za Utawala na Rasilimli watu PPAA, Bw.Paschal kajuna (kushoto), Meneja wa Usimamizi wa Rufaa na Huduma za Sheria PPAA, Bi. Florida Mapunda katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa mafunzo   ya siku kwa wazabuni na wadau wa ununuzi wa Umma kutoka taasisi za Serikali (hawapo pichani) kwa Kanda ya Kaskazini jijini Arusha



Sehemu ya washiriki wakifuatilia mada kuhusu matumizi ya moduli ya kuwasilisha na kushughulikia malalamiko na rufaa kwa njia ya kielektroniki katika mfumo wa NeST Jijini Arusha

Meneja wa Usimamizi wa Rufaa na Huduma za Sheria PPAA, Bi. Florida Mapunda akiwasilisha mada kuhusu matumizi ya moduli ya kuwasilisha na kushughulikia malalamiko na rufaa kwa njia ya kielektroniki katika mfumo wa NeST kwa wazabuni na wadau wa ununuzi wa Umma kutoka taasisi za Serikali kwa Kanda ya Kaskazini jijini Arusha

Katibu Mtendaji wa PPAA, Bw. James Sando akifungua mafunzo ya siku mbili (tarehe 10 – 11 Aprili, 2025) kwa wazabuni na wadau wa ununuzi wa Umma kutoka taasisi za Serikali kwa Kanda ya Kaskazini jijini Arusha

Katibu Mtendaji wa PPAA, Bw. James Sando akifungua mafunzo ya siku mbili (tarehe 10 – 11 Aprili, 2025) kwa wazabuni na wadau wa ununuzi wa Umma kutoka taasisi za Serikali kwa Kanda ya Kaskazini jijini Arusha

 

 

MAFUNZO NA KUPIMA AFYA KWA WATUMISHI WA OFISI YA WAKILI MKUU WA SERIKALI

 

Kaimu Naibu Wakili Mkuu wa Serikali, Bi. Vivin Method akizungumza na watumishi wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali wakati akifungua Mafunzo kuhusu Upimaji wa Afya yaliyofanyika jijini Dar es Salaam.


Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali, Bi.Asha Hayeshi akitoa neno la utangulizi kwa watumishi wa ofisi hiyo wakati wa Mafunzo kuhusu upimaji wa afya yaliyofanyika jijini Dar es Salaam.



Mratibu wa Kusimamia Magonjwa yanayoambukiza wa Ofisi ya Mganga Mkuu wa Halmashauri ya jiji la Dar es Salaam, Dkt. Aisha Zukheri akitoa maada kuhusu Magonjwa yanayoambukiza wakati wa mafunzo hayo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam.



Mratibu wa Kusimamia Magonjwa yasiyoambukiza wa Ofisi ya Mganga Mkuu wa Halmashauri ya jiji la Dar es Salaam, Dkt. Milka Mathania akitoa mada kuhusu Magonjwa yasiyoambukiza wakati wa mafunzo hayo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam.



Kaimu Afisa Lishe wa Ofisi ya Mganga Mkuu wa Halmashauri ya jiji la Dar es Salaam,Bi. Neema Makasege akitoa mada kuhusu kuhusu Lishe na Afya wakati wa mafunzo hayo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam.


Baadhi ya Watumishi wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali wakichangia mada kuhusu Lishe na Afya wakati wa mafunzo hayo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam.


Baadhi ya Watumishi wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali wakichangia mada kuhusu Lishe na Afya wakati wa mafunzo hayo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam.


Baadhi ya Watumishi wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali wakichangia mada kuhusu Lishe na Afya wakati wa mafunzo hayo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam.


Baadhi ya Watumishi wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali wakichangia mada kuhusu Lishe na Afya wakati wa mafunzo hayo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam.

TANZANA – UKRAINE KUONGEZA USHIRIKIANO WA KIUCHUMI

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Ukraine zimekubaliana kuongeza ushirikiano katika sekta mbalimbali za kiuchumi na kijamii ikiwemo kilimo, biashara na uwekezaji, viwanda, utalii, elimu na afya kwa maslahi ya pande zote mbili.


Makubaliano hayo yamefikiwa kwenye mazungumzo baina ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Ukraine Mhe. Andrii Sybiha yaliyofanyika nchini Uturuki pembezoni mwa Mkutano wa 4 wa Diplomasia wa Antalya (The Antalya Diplomacy Forum – ADF2025).

Katika mazungumzo hayo Waziri Kombo amebainisha kuwa ni wakati muafaka kwa pande zote mbili kuimarisha mazingira yatakayonufaisha wananchi kiuchumi.

“Tanzania inafahamika na kusifika kote duniani kuwa ni rafiki wa wote, hivyo tutaendelea kudumisha na kufungua zaidi milango ya ushirikiano kwa Ukraine na washirika wengine wa maendeleo ili kuboresha maisha ya watanzania. Tuataendelea kuwavutia zaidi wawekezaji na watalii, kutafuta fursa za mafunzo na masomo nje ya nchi na soko la bidhaa zinazozalishwa na wananchi wetu ili kukuza uchumi wao na pato la taifa”. Alieleza Waziri Kombo.


Kwa upande wake Waziri wa Mambo ya Nje wa Ukraine ameeleza kuwa Tanzania ni mshirika muhimu kwa Ukraine kutokana msimamo wake thabiti na umahiri wake katika kusimamia agenda za msingi katika majukwaa ya kimataifa ikiwemo masuala ya amani na usalama.

Aliongeza kuwa Ukraine ipo tayari kuongeza maeneo ya ushirikiano wa kiuchumi na Tanzania ikiwemo sekta ya ujenzi wa miundombinu ya usafiri na usafirishaji kwa manufaa ya pande zote mbili.

Waziri Kombo yupo ziarani nchini Uturuki ambapo pamoja na masuala mengine anashiriki katika Mkutano wa 4 wa Diplomasia wa Antalya (The Antalya Diplomacy Forum – ADF2025) unaoendelea nchini humo.




Mazungumzo yakiendelea


Mazungumzo yakiendelea

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Mahmoud Thabit Kombo akijadili jambo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Ukraine Mhe.Andrii Sybiha walipokutana kwa mazungumzo pembezoni mwa Mkutano wa ADF2025 jijini Antalya, Uturuki.

1234567 Next

SPORTS

 
Support : #BegaKwaBegaNaMamaSamia | JAK | CCM Arusha
Copyright © 2011. CCM Dijitali - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Jasper K
Proudly powered by Blogger
Link