MAKAMU WA RAIS ASHIRIKI MKUTANO WA 45 WA SADC
RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN APONGEZWA KWA KUSIMAMIA AMANI NA UTULIVU SADC. Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Phi...

Latest Post
July 28, 2025
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb.), amefanya ziara katika Makao Makuu ya Kituo cha Afrika cha Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa (Africa CDC) jijini Addis Ababa, Ethiopia ambapo amepongeza juhudi za taasisi hiyo katika kuboresha afya na ustawi wa watu wa Afrika.
Akiwa katika mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa Africa CDC, Dkt. Jean Kaseya, Waziri Kombo ameeleza kufurahishwa na kazi ya taasisi hiyo na kuitaja kuwa na heshima kubwa kimataifa, ingawa bado mataifa ya Afrika hayajaitumia ipasavyo. “Tunapaswa kuwa mabalozi wenu ili viongozi wetu waelewe kwa undani kazi mnayofanya,” alisema Mhe. Kombo.
Waziri Kombo amesisitiza kuwa kazi ya Africa CDC inagusa sekta za afya, elimu, michezo na utamaduni, na hivyo kuitaka taasisi hiyo kushirikiana zaidi na wizara mbalimbali za nchi wanachama huku akionesha utayari wa Serikali ya Tanzania kuimarisha uhusiano huo.
Aidha, Waziri Kombo amependekeza ushirikiano wa kiufundi kati ya Africa CDC na Tanzania kupitia Bohari ya Dawa (MSD), ambapo Tanzania imepanga kuanzisha vituo vya usambazaji wa dawa katika mipaka na wilaya zote. Pia amepongeza juhudi za Africa CDC katika kupambana na ugonjwa wa seli mundu, akieleza kuwa Tanzania iko tayari kushiriki kupitia mpango wa “Building a Better Tomorrow (BBT)” unaoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan.
Kwa upande wake, Dkt. Kaseya amempongeza Waziri Kombo kwa ziara hiyo na kusema kuwa Tanzania inaweza kuwa mshirika muhimu katika kusaidia Africa CDC kufikisha ujumbe wake kwa viongozi wa Afrika, hasa kwa kuzingatia nafasi ya Rais Samia kama Mwenyekiti wa sasa wa Chombo cha Usalama cha SADC.
Waziri Kombo pia ametembelea Kituo cha Dharura cha Uendeshaji kinachofuatilia zaidi ya matukio 140 ya kiafya barani Afrika, na kuelezwa jinsi taasisi hiyo inavyotumia teknolojia ya kisasa kulinda afya ya bara la Afrika.
Katika ziara hiyo, Mhe. Waziri Kombo aliambatana na Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia, Mhe. Innocent Shiyo, pamoja na Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Noel Kaganda.
WAZIRI KOMBO ASIFIA MCHANGO WA AFRICA CDC KATIKA KULINDA AFYA YA AFRIKA
Written By CCMdijitali on Monday, July 28, 2025 | July 28, 2025
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb.), amefanya ziara katika Makao Makuu ya Kituo cha Afrika cha Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa (Africa CDC) jijini Addis Ababa, Ethiopia ambapo amepongeza juhudi za taasisi hiyo katika kuboresha afya na ustawi wa watu wa Afrika.
Akiwa katika mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa Africa CDC, Dkt. Jean Kaseya, Waziri Kombo ameeleza kufurahishwa na kazi ya taasisi hiyo na kuitaja kuwa na heshima kubwa kimataifa, ingawa bado mataifa ya Afrika hayajaitumia ipasavyo. “Tunapaswa kuwa mabalozi wenu ili viongozi wetu waelewe kwa undani kazi mnayofanya,” alisema Mhe. Kombo.
Waziri Kombo amesisitiza kuwa kazi ya Africa CDC inagusa sekta za afya, elimu, michezo na utamaduni, na hivyo kuitaka taasisi hiyo kushirikiana zaidi na wizara mbalimbali za nchi wanachama huku akionesha utayari wa Serikali ya Tanzania kuimarisha uhusiano huo.
Aidha, Waziri Kombo amependekeza ushirikiano wa kiufundi kati ya Africa CDC na Tanzania kupitia Bohari ya Dawa (MSD), ambapo Tanzania imepanga kuanzisha vituo vya usambazaji wa dawa katika mipaka na wilaya zote. Pia amepongeza juhudi za Africa CDC katika kupambana na ugonjwa wa seli mundu, akieleza kuwa Tanzania iko tayari kushiriki kupitia mpango wa “Building a Better Tomorrow (BBT)” unaoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan.
Kwa upande wake, Dkt. Kaseya amempongeza Waziri Kombo kwa ziara hiyo na kusema kuwa Tanzania inaweza kuwa mshirika muhimu katika kusaidia Africa CDC kufikisha ujumbe wake kwa viongozi wa Afrika, hasa kwa kuzingatia nafasi ya Rais Samia kama Mwenyekiti wa sasa wa Chombo cha Usalama cha SADC.
Waziri Kombo pia ametembelea Kituo cha Dharura cha Uendeshaji kinachofuatilia zaidi ya matukio 140 ya kiafya barani Afrika, na kuelezwa jinsi taasisi hiyo inavyotumia teknolojia ya kisasa kulinda afya ya bara la Afrika.
Katika ziara hiyo, Mhe. Waziri Kombo aliambatana na Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia, Mhe. Innocent Shiyo, pamoja na Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Noel Kaganda.
Labels:
KIMATAIFA
July 28, 2025
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb.), amesisitiza umuhimu wa kuchukua hatua madhubuti na za pamoja katika kuimarisha mifumo ya chakula ili kuhakikisha ushiriki endelevu wa Tanzania katika ajenda za maendeleo ya kimataifa.
Waziri Kombo ameyasema hayo wakati wa kikao kilichofanyika katika Ubalozi wa Tanzania jijini Addis Ababa, Ethiopia, ambako anamwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Mkutano wa Pili wa Mfumo wa Chakula wa Umoja wa Mataifa (UNFSS+4), unaofanyika tarehe 27 hadi 29 Julai 2025.
Wakati wa kikao hicho, Waziri Kombo amepokea taarifa kuhusu maandalizi ya mkutano kutoka kwa Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia, Mhe. Innocent Shiyo ambaye ameeleza kuwa mkutano huo ni jukwaa la kipekee kwa Tanzania kushiriki katika kujenga ajenda ya kimataifa ya kilimo, kukuza usalama wa chakula, na kuimarisha ushirikiano wa kikanda na kimataifa.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Noel Kaganda, amewasilisha taarifa ya kiufundi akifafanua kuwa mkutano huo unalenga kutathmini utekelezaji wa mageuzi ya mifumo ya chakula kwa misingi ya haki za binadamu, usawa wa kijinsia, utawala bora, na ulinganifu wa sera za kitaifa na kimataifa.
Amesisitiza umuhimu wa kushirikisha wadau mbalimbali wakiwemo vijana, wanawake, sekta binafsi, watu wenye ulemavu na mashirika ya kiraia ili kujenga usimamizi shirikishi wa rasilimali za chakula.
Vilevile Balozi Kaganda amebainisha kuwa licha ya changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya kilimo nchini, zikiwemo mabadiliko ya tabianchi, upungufu wa teknolojia ya kisasa, na miundombinu duni ya usambazaji wa chakula, Tanzania imefanikiwa kufikia asilimia 128.3 ya kiwango cha uzalishaji wa chakula, ikionesha kuwa nchi imezalisha chakula zaidi ya mahitaji ya ndani, jambo linaloashiria mafanikio ya juhudi za serikali katika sekta ya kilimo.
Aidha, wajumbe wa kikao wamesisitiza kuwa Tanzania inapaswa kutumia mkutano huo kama fursa ya kujenga ushawishi wa kisera, kuvutia uwekezaji mpya na kuimarisha ushiriki wake katika programu za kikanda na kimataifa.
WAZIRI KOMBO ATAKA MIKAKATI ENDELEVU YA KISEKTA KUIMARISHA MIFUMO YA CHAKULA KIMATAIFA
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb.), amesisitiza umuhimu wa kuchukua hatua madhubuti na za pamoja katika kuimarisha mifumo ya chakula ili kuhakikisha ushiriki endelevu wa Tanzania katika ajenda za maendeleo ya kimataifa.
Waziri Kombo ameyasema hayo wakati wa kikao kilichofanyika katika Ubalozi wa Tanzania jijini Addis Ababa, Ethiopia, ambako anamwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Mkutano wa Pili wa Mfumo wa Chakula wa Umoja wa Mataifa (UNFSS+4), unaofanyika tarehe 27 hadi 29 Julai 2025.
Wakati wa kikao hicho, Waziri Kombo amepokea taarifa kuhusu maandalizi ya mkutano kutoka kwa Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia, Mhe. Innocent Shiyo ambaye ameeleza kuwa mkutano huo ni jukwaa la kipekee kwa Tanzania kushiriki katika kujenga ajenda ya kimataifa ya kilimo, kukuza usalama wa chakula, na kuimarisha ushirikiano wa kikanda na kimataifa.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Noel Kaganda, amewasilisha taarifa ya kiufundi akifafanua kuwa mkutano huo unalenga kutathmini utekelezaji wa mageuzi ya mifumo ya chakula kwa misingi ya haki za binadamu, usawa wa kijinsia, utawala bora, na ulinganifu wa sera za kitaifa na kimataifa.
Amesisitiza umuhimu wa kushirikisha wadau mbalimbali wakiwemo vijana, wanawake, sekta binafsi, watu wenye ulemavu na mashirika ya kiraia ili kujenga usimamizi shirikishi wa rasilimali za chakula.
Vilevile Balozi Kaganda amebainisha kuwa licha ya changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya kilimo nchini, zikiwemo mabadiliko ya tabianchi, upungufu wa teknolojia ya kisasa, na miundombinu duni ya usambazaji wa chakula, Tanzania imefanikiwa kufikia asilimia 128.3 ya kiwango cha uzalishaji wa chakula, ikionesha kuwa nchi imezalisha chakula zaidi ya mahitaji ya ndani, jambo linaloashiria mafanikio ya juhudi za serikali katika sekta ya kilimo.
Aidha, wajumbe wa kikao wamesisitiza kuwa Tanzania inapaswa kutumia mkutano huo kama fursa ya kujenga ushawishi wa kisera, kuvutia uwekezaji mpya na kuimarisha ushiriki wake katika programu za kikanda na kimataifa.
![]() |
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo akizungumza kwenye kikao na wajumbe wanaoshiriki Mkutano wa pili wa Mfumo wa chakula wa Umoja wa Mataifa |
![]() |
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo akizungumza kwenye kikao na wajumbe wanaoshiriki Mkutano wa pili wa Mfumo wa chakula wa Umoja wa Mataifa |
Labels:
KIMATAIFA
July 28, 2025
Tanzania imesisitiza dhamira yake ya kushiriki kikamilifu katika juhudi za kimataifa za mageuzi ya mifumo ya chakula duniani, ikilenga kujenga mifumo endelevu, jumuishi na yenye ustahimilivu kwa ajili ya ustawi wa watu, sayari na uchumi wa dunia.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo, ametoa kauli hiyo alipowasilisha tamko la Tanzania katika kikao cha Mkutano wa Pili wa Mfumo wa Chakula wa Umoja wa Mataifa (UNFSS+4), unaofanyika jijini Addis Ababa kuanzia tarehe 27 hadi 29 Julai 2025.
Akizungumza kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Waziri Kombo ameeleza kuwa licha ya changamoto nyingi za kimataifa ikiwemo mabadiliko ya tabianchi, migogoro ya kiuchumi na ukosefu wa usawa, Tanzania inaendelea kutekeleza mkakati wake wa mageuzi ya mifumo ya chakula kwa kuzingatia misingi ya usawa wa kijinsia, utawala bora na maendeleo shirikishi.
“Chakula lazima kisiishie kutulisha tu, bali kiwe sehemu ya kuimarisha uchumi wetu, kurejesha mazingira yetu na kulinda heshima ya kila mwanadamu,” alisema Waziri Kombo, akisisitiza kwamba Tanzania inajielekeza katika kilimo rafiki kwa mazingira, uwezeshaji wa wakulima wadogo, wanawake na vijana, pamoja na kuunganisha lishe bora katika sera na mipango ya kitaifa.
Katika hotuba hiyo, Tanzania pia imetoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kuimarisha mshikamano, kuongeza uwekezaji katika kilimo endelevu, na kutoa teknolojia na rasilimali ili kuongeza ushiriki wao katika mifumo ya chakula ya dunia.
Mkutano wa UNFSS+4 ni jukwaa muhimu la kutathmini mafanikio na changamoto zilizojitokeza tangu mkutano wa awali wa mwaka 2021, huku ukilenga kuimarisha ushirikiano wa kimataifa katika kupatikana kwa mifumo ya chakula salama, shirikishi na inayojali mazingira
TANZANIA YATHIBITISHA DIRA YAKE YA KIMATAIFA KUHUSU MAGEUZI YA MIFUMO YA CHAKULA DUNIANI
Tanzania imesisitiza dhamira yake ya kushiriki kikamilifu katika juhudi za kimataifa za mageuzi ya mifumo ya chakula duniani, ikilenga kujenga mifumo endelevu, jumuishi na yenye ustahimilivu kwa ajili ya ustawi wa watu, sayari na uchumi wa dunia.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo, ametoa kauli hiyo alipowasilisha tamko la Tanzania katika kikao cha Mkutano wa Pili wa Mfumo wa Chakula wa Umoja wa Mataifa (UNFSS+4), unaofanyika jijini Addis Ababa kuanzia tarehe 27 hadi 29 Julai 2025.
Akizungumza kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Waziri Kombo ameeleza kuwa licha ya changamoto nyingi za kimataifa ikiwemo mabadiliko ya tabianchi, migogoro ya kiuchumi na ukosefu wa usawa, Tanzania inaendelea kutekeleza mkakati wake wa mageuzi ya mifumo ya chakula kwa kuzingatia misingi ya usawa wa kijinsia, utawala bora na maendeleo shirikishi.
“Chakula lazima kisiishie kutulisha tu, bali kiwe sehemu ya kuimarisha uchumi wetu, kurejesha mazingira yetu na kulinda heshima ya kila mwanadamu,” alisema Waziri Kombo, akisisitiza kwamba Tanzania inajielekeza katika kilimo rafiki kwa mazingira, uwezeshaji wa wakulima wadogo, wanawake na vijana, pamoja na kuunganisha lishe bora katika sera na mipango ya kitaifa.
Katika hotuba hiyo, Tanzania pia imetoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kuimarisha mshikamano, kuongeza uwekezaji katika kilimo endelevu, na kutoa teknolojia na rasilimali ili kuongeza ushiriki wao katika mifumo ya chakula ya dunia.
Mkutano wa UNFSS+4 ni jukwaa muhimu la kutathmini mafanikio na changamoto zilizojitokeza tangu mkutano wa awali wa mwaka 2021, huku ukilenga kuimarisha ushirikiano wa kimataifa katika kupatikana kwa mifumo ya chakula salama, shirikishi na inayojali mazingira
Labels:
KIMATAIFA
July 28, 2025
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
Tanzania inauhitaji mkubwa wa nyumba kutokana na kasi ya ukuaji wa miji nchini ambapo inakadiriwa kuwa na mahitaji ya nyumba 26,840,909 ifikapo 2050 ili kukidhi mahitaji wa watu milioni 118.1.
Akizungumza na waandishi wa Habari mara baada ya kufungua semina kuhusu makazi, ujenzi na maendeleo ya miji kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Wawekezaji wa sekta ya Milki kutoka Japan Julai 28, jijini Dar es Salaam, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Deogratius Ndejembi amesema kuna uhitaji mkubwa wa nyumba nchini ili kukidhi mahitaji watu katika maeneo mbalimbali nchini.
Akitolea mfano wa miji inayokuwa kwa kasi, Waziri Ndejembi amesema awali hali ya ukuaji wa miji nchini ilikuwa kwenye majiji ya Dar es salaam na Mbeya, kwa sasa hali ni tofauti ambapo miji Geita, Katavi na Mpanda inakua kwa kasi.
Kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022, mahitaji ya nyumba nchini yalikuwa 14,724,164 ambayo ni idadi ya nyumba zilizokuwepo na ambao zinahudumia wakazi 61.7 million kwa mwaka 2022, mwaka 2025 mahitaji ya nyumba ni 15,500,000 huku idadi ya watu ikiwa ni milioni 68.2 na mahitaji ya nyumba ifikapo 2030 yanatarajiwa kuwa 17,659,090 na idadi ya watu inatarajiwa kuwa milioni 77.7 huku mahitaji ya nyumba yanatarajiwa kuwa 26,840,909 ili kukidhi mahitaji ya nyumba kwa watu wanatarajiwa kufikia milioni 118.1 ifikapo mwaka 2050.
Ili kufikia mahitaji hayo, Serikali imeweka mazingira rafiki ya uwekezaji kwa kuwakaribisha wawekezaji mbalimbali katika sekta ya Milki nchini kurahisisha upatikanaji wa makazi ili Watanzania wapate nyumba za bei nafuu.
Hatua ambazo Tanzania imechukua ni pamoja na kuondoa kodi kwenye ujenzi wa nyumba za thamani ya chini ya Shilingi milioni 50 na kuzindua Sera ya Taifa ya Ardhi ya mwaka 1995 Toleo la mwaka 2023 ambayo iliyozinduliwa Machi 17, 2025 na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo inatoa fursa kwa wawekezaji katika sekta ya Milki ili Watanzania wapate nyumba za bei nafuu.
Kwa upande wake Balozi wa Japan nchini, Mhe. Yoichi Mikami amesema semina hiyo ni muhimu itasidia kuboresha mahusiano baina ya Tanzania na Japan ambapo makampuni na wataalam baina mataifa hayo watashirikiana kuhakikisha kunakuwa na makazi nchini kulingana na mahitaji.







TANZANIA INAUHITAJI WA ZAIDI YA NYUMBA MILIONI 26 IFIKAPO 2050
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
Tanzania inauhitaji mkubwa wa nyumba kutokana na kasi ya ukuaji wa miji nchini ambapo inakadiriwa kuwa na mahitaji ya nyumba 26,840,909 ifikapo 2050 ili kukidhi mahitaji wa watu milioni 118.1.
Akizungumza na waandishi wa Habari mara baada ya kufungua semina kuhusu makazi, ujenzi na maendeleo ya miji kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Wawekezaji wa sekta ya Milki kutoka Japan Julai 28, jijini Dar es Salaam, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Deogratius Ndejembi amesema kuna uhitaji mkubwa wa nyumba nchini ili kukidhi mahitaji watu katika maeneo mbalimbali nchini.
“Tanzania tuna uhitaji mkubwa wa nyumba kwa sababu ukiangalia miaka ya 1967, ukuaji wetu katika miji ulikuwa asilimia 6.2 tu, lakini katika sensa ya mwaka 2022 ukuaji katika miji yetu umekwenda asilimia 34.9 ambao ni ukuaji wa kasi kubwa sana na inatarajiwa kufikia asilimia 59 ifikapo mwaka 2050, hatua inayofanya nchi yetu kuwa moja ya nchi zenye miji inayokuwa kwa kasi katika nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara” amesema Waziri Ndejembi.
Akitolea mfano wa miji inayokuwa kwa kasi, Waziri Ndejembi amesema awali hali ya ukuaji wa miji nchini ilikuwa kwenye majiji ya Dar es salaam na Mbeya, kwa sasa hali ni tofauti ambapo miji Geita, Katavi na Mpanda inakua kwa kasi.
Kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022, mahitaji ya nyumba nchini yalikuwa 14,724,164 ambayo ni idadi ya nyumba zilizokuwepo na ambao zinahudumia wakazi 61.7 million kwa mwaka 2022, mwaka 2025 mahitaji ya nyumba ni 15,500,000 huku idadi ya watu ikiwa ni milioni 68.2 na mahitaji ya nyumba ifikapo 2030 yanatarajiwa kuwa 17,659,090 na idadi ya watu inatarajiwa kuwa milioni 77.7 huku mahitaji ya nyumba yanatarajiwa kuwa 26,840,909 ili kukidhi mahitaji ya nyumba kwa watu wanatarajiwa kufikia milioni 118.1 ifikapo mwaka 2050.
Ili kufikia mahitaji hayo, Serikali imeweka mazingira rafiki ya uwekezaji kwa kuwakaribisha wawekezaji mbalimbali katika sekta ya Milki nchini kurahisisha upatikanaji wa makazi ili Watanzania wapate nyumba za bei nafuu.
Hatua ambazo Tanzania imechukua ni pamoja na kuondoa kodi kwenye ujenzi wa nyumba za thamani ya chini ya Shilingi milioni 50 na kuzindua Sera ya Taifa ya Ardhi ya mwaka 1995 Toleo la mwaka 2023 ambayo iliyozinduliwa Machi 17, 2025 na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo inatoa fursa kwa wawekezaji katika sekta ya Milki ili Watanzania wapate nyumba za bei nafuu.
Kwa upande wake Balozi wa Japan nchini, Mhe. Yoichi Mikami amesema semina hiyo ni muhimu itasidia kuboresha mahusiano baina ya Tanzania na Japan ambapo makampuni na wataalam baina mataifa hayo watashirikiana kuhakikisha kunakuwa na makazi nchini kulingana na mahitaji.







Labels:
KITAIFA
July 27, 2025
Katika mkutano huo, Waziri Mkuu anatarajiwa kushiriki mjadala wa Mjadala wa Wakuu wa Nchi na Serikali, kukutana na viongozi wa mataifa mengine, pamoja na kushiriki katika mikutano ya uwili na wawekezaji wakubwa, ikiwa ni dhamira ya Tanzania ya kuendeleza juhudi zake za kuvutia wawekezaji wa kimataifa ili kusaidia katika kujenga uchumi wa kisasa na shindani duniani.
Ushiriki wa Mheshimiwa Majaliwa katika mkutano huo akimwakilisha Rais Dkt. Samia ni mwendelezo wa dhamira ya dhati ya kuimarisha diplomasia ya uchumi kwa kuifungua nchi kimataifa na kuimarisha ushirikiano, ili kuchochea maendeleo jumuishi kwa Watanzania wote.
Baadhi ya maeneo muhimu ambayo yatajadiliwa katika mkutano huo ni kuanzishwa kwa eneo la Biashara Huria kati ya Afrika na Karibiani, kuimarisha baraza la biashara la Afrika na Karibiani, kuchochea uchumi na ubunifu pamoja na Kukuza uhusiano wa usafiri wa anga na baharini kati ya Afrika na Karibiani.
Mkutano huo umeratibiwa na Jamhuri ya Granada pamoja na taasisi ya kifedha ya kimataifa yenye lengo la kukuza biashara ya bidhaa na huduma ndani na nje ya Afrika (Afreximbank).










WAZIRI MKUU KUMWAKILISHA RAIS DKT. SAMIA KATIKA MKUTANO WA ACTIF 2025 NCHINI GRENADA
Written By CCMdijitali on Sunday, July 27, 2025 | July 27, 2025
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa Julai 27, 2025 amewasili mjini St. George’s, nchini Grenada ambapo atamwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Jukwaa la nne wa Kibiashara na Uwekezaji kati ya Afrika na Karibiani (Afri-Caribbean Trade and Investment Forum - ACTIF 2025) unaotarajiwa kufanyika Julai 28–30, 2025 katika kituo cha mikutano cha Radisson.
Mkutano huo mkubwa unaolenga kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi kati ya mataifa ya Afrika na visiwa vya Karibiani una kaulimbiu inayosema: “Uhimilivu na Mabadiliko: Kuimarisha Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Afrika na Karibiani katika Kipindi cha Changamoto za Kidunia.”
Katika mkutano huo, Waziri Mkuu anatarajiwa kushiriki mjadala wa Mjadala wa Wakuu wa Nchi na Serikali, kukutana na viongozi wa mataifa mengine, pamoja na kushiriki katika mikutano ya uwili na wawekezaji wakubwa, ikiwa ni dhamira ya Tanzania ya kuendeleza juhudi zake za kuvutia wawekezaji wa kimataifa ili kusaidia katika kujenga uchumi wa kisasa na shindani duniani.
Ushiriki wa Mheshimiwa Majaliwa katika mkutano huo akimwakilisha Rais Dkt. Samia ni mwendelezo wa dhamira ya dhati ya kuimarisha diplomasia ya uchumi kwa kuifungua nchi kimataifa na kuimarisha ushirikiano, ili kuchochea maendeleo jumuishi kwa Watanzania wote.
Baadhi ya maeneo muhimu ambayo yatajadiliwa katika mkutano huo ni kuanzishwa kwa eneo la Biashara Huria kati ya Afrika na Karibiani, kuimarisha baraza la biashara la Afrika na Karibiani, kuchochea uchumi na ubunifu pamoja na Kukuza uhusiano wa usafiri wa anga na baharini kati ya Afrika na Karibiani.
Mkutano huo umeratibiwa na Jamhuri ya Granada pamoja na taasisi ya kifedha ya kimataifa yenye lengo la kukuza biashara ya bidhaa na huduma ndani na nje ya Afrika (Afreximbank).











July 27, 2025
Tanzania na Rwanda Zaimarisha Ushirikiano kwa Kusaini Hati Mbili za Makubaliano
Mkutano wa 16 wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano (JPC) kati ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Rwanda umefungwa rasmi jijini Kigali leo tarehe 26 Julai 2025, baada ya mawaziri wa pande zote mbili kusaini hati mbili za makubaliano ya ushirikiano ikiwemo ya kilimo na uanzishwaji wa Ofisi ya Mamlaka ya Bandari ya Tanzania (TPA) jijini Kigali, kama sehemu ya hatua za kuimarisha uhusiano wa karibu na kukuza maendeleo ya pamoja baina ya nchi hizo mbili.
Hati hizo zimesainiwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wa Tanzania, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb.), na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Olivier Nduhungirehe ikilenga kuimarisha ushirikiano wa kimkakati kati ya Tanzania na Rwanda kwa manufaa ya wananchi wa mataifa haya mawili. Kupitia makubaliano ya sekta ya kilimo, pande zote zimekusudia kubadilishana uzoefu, teknolojia, utaalamu na taarifa muhimu ili kuongeza uzalishaji, usalama wa chakula na fursa za biashara ya mazao ya kilimo.
Aidha, uanzishwaji wa Ofisi ya Mamlaka ya Bandari ya Tanzania (TPA) jijini Kigali unalenga Kurahisisha upatikanaji wa huduma za Bandari nchini Rwanda, kupunguza gharama za bidhaa, kuimarisha na kuongeza matumizi ya Bandari za Tanzania kama lango kuu ka kupitisha mizigo na shehena za Rwanda
Akizungumza wakati wa hafla ya kufunga mkutano, Waziri Kombo amesisitiza umuhimu wa utekelezaji wa makubaliano yote yaliyoafikiwa katika mkutano huo na kuwataka wataalamu na viongozi wa serikali kuhakikisha kuwa mipango na maazimio ya JPC yanatekelezwa kwa wakati.
Kwa upande wake, Waziri Nduhungirehe ameipongeza Tanzania kwa ushirikiano mzuri na kusisitiza kuwa Rwanda itaendelea kushirikiana kwa karibu na nchi jirani ili kuhakikisha maridhiano ya kweli yanapatikana kupitia utekelezaji wa maazimio yaliyofikiwa. Ameeleza kuwa makubaliano kama hayo ni nyenzo muhimu ya kukuza uchumi, kuboresha usalama wa chakula, na kuimarisha mshikamano wa kidiplomasia na kijamii kati ya mataifa hayo mawili.
Mkutano wa 16 wa JPC umejadili masuala mbalimbali ya ushirikiano ikiwemo biashara, ulinzi na usalama, miundombinu, afya, elimu, nishati, na kilimo. Mazungumzo hayo yamekuwa na tija kubwa na kufanikisha hatua za pamoja za kuendeleza mahusiano ya kidiplomasia na kiuchumi baina ya Tanzania na Rwanda.
Labels:
KIMATAIFA
July 27, 2025
Mkutano wa 16 wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano (JPC) kati ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Rwanda umefungwa rasmi jijini Kigali leo tarehe 26 Julai 2025, baada ya mawaziri wa pande zote mbili kusaini hati mbili za makubaliano ya ushirikiano ikiwemo ya kilimo na uanzishwaji wa Ofisi ya Mamlaka ya Bandari ya Tanzania (TPA) jijini Kigali, kama sehemu ya hatua za kuimarisha uhusiano wa karibu na kukuza maendeleo ya pamoja baina ya nchi hizo mbili.
Hati hizo zimesainiwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wa Tanzania, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb.), na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Olivier Nduhungirehe ikilenga kuimarisha ushirikiano wa kimkakati kati ya Tanzania na Rwanda kwa manufaa ya wananchi wa mataifa haya mawili. Kupitia makubaliano ya sekta ya kilimo, pande zote zimekusudia kubadilishana uzoefu, teknolojia, utaalamu na taarifa muhimu ili kuongeza uzalishaji, usalama wa chakula na fursa za biashara ya mazao ya kilimo.
Aidha, uanzishwaji wa Ofisi ya Mamlaka ya Bandari ya Tanzania (TPA) jijini Kigali unalenga Kurahisisha upatikanaji wa huduma za Bandari nchini Rwanda, kupunguza gharama za bidhaa, kuimarisha na kuongeza matumizi ya Bandari za Tanzania kama lango kuu ka kupitisha mizigo na shehena za Rwanda
Akizungumza wakati wa hafla ya kufunga mkutano, Waziri Kombo amesisitiza umuhimu wa utekelezaji wa makubaliano yote yaliyoafikiwa katika mkutano huo na kuwataka wataalamu na viongozi wa serikali kuhakikisha kuwa mipango na maazimio ya JPC yanatekelezwa kwa wakati.
Kwa upande wake, Waziri Nduhungirehe ameipongeza Tanzania kwa ushirikiano mzuri na kusisitiza kuwa Rwanda itaendelea kushirikiana kwa karibu na nchi jirani ili kuhakikisha maridhiano ya kweli yanapatikana kupitia utekelezaji wa maazimio yaliyofikiwa. Ameeleza kuwa makubaliano kama hayo ni nyenzo muhimu ya kukuza uchumi, kuboresha usalama wa chakula, na kuimarisha mshikamano wa kidiplomasia na kijamii kati ya mataifa hayo mawili.
Mkutano wa 16 wa JPC umejadili masuala mbalimbali ya ushirikiano ikiwemo biashara, ulinzi na usalama, miundombinu, afya, elimu, nishati, na kilimo. Mazungumzo hayo yamekuwa na tija kubwa na kufanikisha hatua za pamoja za kuendeleza mahusiano ya kidiplomasia na kiuchumi baina ya Tanzania na Rwanda.
July 27, 2025
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb.), amefungua rasmi Mkutano wa 16 wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Rwanda, uliofanyika tarehe 26 Julai 2025 jijini Kigali, Rwanda.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano huo, Waziri Kombo ametoa salamu za kindugu kutoka kwa Serikali na Wananchi wa Tanzania kwa Serikali ya Jamhuri ya Rwanda, huku akitoa shukrani za dhati kwa mapokezi ya ukarimu na mazingira mazuri ya mkutano huo.
Waziri Kombo amebainisha kuwa miradi ya pamoja ya kimkakati inayotekelezwa na nchi hizo mbili, ikiwemo Mradi wa Umeme wa Rusumo, kituo cha pamoja cha forodha cha Rusumo (OSBP), pamoja na reli ya kisasa (Standard Gauge Railway – SGR), kuwa ni vielelezo vya mafanikio ya ushirikiano wa muda mrefu.
Licha ya mafanikio hayo, Mhe. Kombo amesisitiza kuwa bado kuna nafasi kubwa ya kuendeleza ushirikiano huo, hasa katika maeneo ya biashara, uwekezaji, kilimo, afya, teknolojia ya habari na mawasiliano (TEHAMA), nishati, utalii na miundombinu.
Kwa upande wake, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Rwanda, Mhe. Balozi Olivier Nduhungirehe , ameeleza kuwa uhusiano kati ya Rwanda na Tanzania una historia ya kina inayojengwa juu ya maadili ya pamoja, undugu wa karibu, na maono ya maendeleo ya pamoja.
Waziri Nduhungirehe pia amesisitiza mchango mkubwa wa Tanzania kama mshirika wa kimkakati wa biashara na maendeleo ya Rwanda, akieleza kuwa zaidi ya asilimia 70 ya mizigo ya Rwanda husafirishwa kupitia Bandari ya Dar es Salaam. Aidha, amepongeza hatua ya kufunguliwa kwa Ofisi ya Mamlaka ya Bandari ya Tanzania (TPA) mjini Kigali.
WAZIRI KOMBO AFUNGUA MILANGO MIPYA YA USHIRIKIANO KATI YA TANZANIA NA RWANDA KUPITIA MKUTANO WA JPC KIGALI
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb.), amefungua rasmi Mkutano wa 16 wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Rwanda, uliofanyika tarehe 26 Julai 2025 jijini Kigali, Rwanda.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano huo, Waziri Kombo ametoa salamu za kindugu kutoka kwa Serikali na Wananchi wa Tanzania kwa Serikali ya Jamhuri ya Rwanda, huku akitoa shukrani za dhati kwa mapokezi ya ukarimu na mazingira mazuri ya mkutano huo.
Waziri Kombo amebainisha kuwa miradi ya pamoja ya kimkakati inayotekelezwa na nchi hizo mbili, ikiwemo Mradi wa Umeme wa Rusumo, kituo cha pamoja cha forodha cha Rusumo (OSBP), pamoja na reli ya kisasa (Standard Gauge Railway – SGR), kuwa ni vielelezo vya mafanikio ya ushirikiano wa muda mrefu.
Licha ya mafanikio hayo, Mhe. Kombo amesisitiza kuwa bado kuna nafasi kubwa ya kuendeleza ushirikiano huo, hasa katika maeneo ya biashara, uwekezaji, kilimo, afya, teknolojia ya habari na mawasiliano (TEHAMA), nishati, utalii na miundombinu.
Kwa upande wake, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Rwanda, Mhe. Balozi Olivier Nduhungirehe , ameeleza kuwa uhusiano kati ya Rwanda na Tanzania una historia ya kina inayojengwa juu ya maadili ya pamoja, undugu wa karibu, na maono ya maendeleo ya pamoja.
Waziri Nduhungirehe pia amesisitiza mchango mkubwa wa Tanzania kama mshirika wa kimkakati wa biashara na maendeleo ya Rwanda, akieleza kuwa zaidi ya asilimia 70 ya mizigo ya Rwanda husafirishwa kupitia Bandari ya Dar es Salaam. Aidha, amepongeza hatua ya kufunguliwa kwa Ofisi ya Mamlaka ya Bandari ya Tanzania (TPA) mjini Kigali.
Labels:
KIMATAIFA
July 26, 2025
Matukio mawili yaliyosisimua waumini na wageni waalikwa walioshiriki Harambee hiyo ni mnada wa mbuzi ambapo mbuzi wawili, mwenye rangi nyeusi akiwakilisha upande wa Yanga alinadiwa kwa shilingi milioni 31 na mbuzi mweupe (Simba) aliuzwa kwa bei kama hiyo ya shilingi milioni 31 na kufanya mbuzi hao wawili kunadiwa kwa jumla ya shilingi 61m.
Kama utani huo haukutosha, viliwekwa vikapu viwili bya sadaka ambapo waumini wanaoshabikia Yanga na Simba walipambanishwa na waumini mashabiki wa Yanga waliibuka kidedea kwa kuchangia shilingi 1,800,000 na Wekundu wa Msimbazi Simba walichangia shilingi 1,210,700.








UTANI WA JADI SIMBA NA YANGA WAPAMBA UZINDUZI WA HARAMBEE UJENZI KKKT DODOMA
Written By CCMdijitali on Saturday, July 26, 2025 | July 26, 2025
Utani wa jadi wa Klabu za Yanga na Simba umepamba uzinduzi wa Harambee ya Ujenzi wa Jengo la Ofisi Kuu ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Dodoma iliyofanyika katika eneo la Mradi la Nzuguni C, Jijini Dodoma, ambapo upande wa Wananchi (Yanga) uliongizwa na Waziri wa Fedha, Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, wakati upande wa Ubaya Ubwela (Simba) ulisimamiwa na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Alhaji Jabir Shekimweli.
Matukio mawili yaliyosisimua waumini na wageni waalikwa walioshiriki Harambee hiyo ni mnada wa mbuzi ambapo mbuzi wawili, mwenye rangi nyeusi akiwakilisha upande wa Yanga alinadiwa kwa shilingi milioni 31 na mbuzi mweupe (Simba) aliuzwa kwa bei kama hiyo ya shilingi milioni 31 na kufanya mbuzi hao wawili kunadiwa kwa jumla ya shilingi 61m.
Kama utani huo haukutosha, viliwekwa vikapu viwili bya sadaka ambapo waumini wanaoshabikia Yanga na Simba walipambanishwa na waumini mashabiki wa Yanga waliibuka kidedea kwa kuchangia shilingi 1,800,000 na Wekundu wa Msimbazi Simba walichangia shilingi 1,210,700.









Labels:
MIKOANI
July 26, 2025
WAZIRI KOMBO APONGEZA UJUMBE WA TANZANIA KATIKA MKUTANO WA JPC RWANDA, AHIMIZA KUCHANGAMKIA FURSA ZA USHIRIKIANO
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb.), amewapongeza wajumbe wa Tanzania waliowasili jijini Kigali, Rwanda kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa 16 wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano (JPC) kati ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Rwanda.
Akizungumza katika kikao kilichofanyika katika Ubalozi wa Tanzania jijini Kigali, Waziri Kombo ameeleza kuridhishwa na ushiriki wa ujumbe huo, akisema hatua yao ya kuwasili mapema ni uthibitisho wa uzalendo, uwajibikaji na dhamira ya dhati ya kulitumikia taifa.
Aidha, Waziri Kombo ameeleza kuwa hatua hiyo imewezesha wajumbe kufanya maandalizi ya kina kwa ajili ya majadiliano yenye tija, kwa kuzingatia masuala muhimu ya kipaumbele yatakayowasilishwa katika mkutano huo.
Katika hotuba yake, Waziri Kombo amesisitiza umuhimu wa kutumia kikamilifu fursa zinazojitokeza kupitia ushirikiano kati ya Tanzania na Rwanda. Ametoa wito kwa wajumbe kuwa na mikakati madhubuti ya kuzitumia ipasavyo fursa hizo kwa ajili ya maendeleo ya nchi na ustawi wa wananchi.
Vilevile, amewahimiza wajumbe kuendelea kusimamia maslahi ya taifa katika majadiliano yote, akisisitiza kuwa wao ni wawakilishi wa Watanzania na wanapaswa kuhakikisha kuwa Tanzania inanufaika kikamilifu na makubaliano yatakayofikiwa.
Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Said Shaib Mussa, ameeleza kuwa mkutano huo una ajenda mahsusi zilizoandaliwa na wataalamu kutoka pande zote mbili, zikilenga kuimarisha ushirikiano katika nyanja za uchumi, biashara, miundombinu, afya, elimu na usalama wa mipaka.
Mkutano wa 16 wa JPC unatarajiwa kuhitimishwa tarehe 26 Julai 2025 kwa ngazi ya Mawaziri, ambapo viongozi hao watapitisha maazimio ya pamoja na kuweka mikakati ya utekelezaji, ikiwa ni sehemu ya kuimarisha uhusiano wa kidugu kati ya Tanzania na Rwanda na kufungua kurasa mpya za ushirikiano wa kimkakati.
July 26, 2025
Naibu Waziri Londo Aishukuru Uswisi kwa kuboresha Maendeleo ya Jamii nchini.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki, Mhe. Dennis Londo (Mb.), ameishukuru Serikali ya Shirikisho la Uswisi kwa mchango wake katika maendeleo ya jamii kupitia utekelezaji wa miradi ya kisekta inayofadhiliwa na nchi hiyo katika maeneo mbalimbali hapa nchini.
Mhe. Londo amesema hayo tarehe 24 Juali, 2025 katika maadhimisho ya Siku ya Taifa ya Uswisi yaliyofanyika katika makazi ya Balozi wa Taifa hilo hapa nchini, jijini Dar Es Salaam.
Amesema historia ya uhusiano wa Tanzania na Uswisi ilianzia mwaka 1927 wakati ilipofungua konseli yake mjini Tanga, katika hatua zake za mwanzo za ushirikiano na Tanzania, na kuwezesha ushirikiano huo kuimarika zaidi miaka ya 1960, kupitia ufadhili wa miradi katika sekta mbalimbali.
Aidha, aliahidi kuwa Serikali ya Tanzania itaendelea kuimarisha uhusiano huo wa kirafiki kwa kuhakikisha kuwa misaada inayotolewa inaleta tija kwa wananchi na kuchangia katika kufikia malengo ya maendeleo endelevu.
Kwa upande wake, Balozi wa Tanzania nchini Uswisi, Mhe. Nicole Providoli, amesema kuwa Serikali ya nchi yake kupitia Chemba ya Biashara ya Uswisi na Tanzania (Swiss-Tanzania Chamber of Commerce - STCC), itaendelea kusaidia jitihada za pande zote mbili katika kuanzisha fursa za biashara na uwekezaji, kwa lengo la kukuza uchumi na ustawi wa wananchi wa pande zote.
Maadhimisho hayo yalihudhuriwa na mabalozi, wawakilishi wa mashirika ya kimataifa, viongozi wa serikali na wadau mbalimbali wa maendeleo.
Mhe. Londo amesema hayo tarehe 24 Juali, 2025 katika maadhimisho ya Siku ya Taifa ya Uswisi yaliyofanyika katika makazi ya Balozi wa Taifa hilo hapa nchini, jijini Dar Es Salaam.
Amesema historia ya uhusiano wa Tanzania na Uswisi ilianzia mwaka 1927 wakati ilipofungua konseli yake mjini Tanga, katika hatua zake za mwanzo za ushirikiano na Tanzania, na kuwezesha ushirikiano huo kuimarika zaidi miaka ya 1960, kupitia ufadhili wa miradi katika sekta mbalimbali.
“Tunatambua Uswisi imechangia maendeleo yetu katika sekta za afya, elimu, ajira kwa vijana, kuwawezesha wanawake na makundi maalum, pamoja na sekta ya kilimo. Ufadhili huu umechangia kuboresha maisha ya wananchi na kuwezesha kufikia malengo ya maendeleo endelevu,"Alifafanua Mhe. Londo.
Aidha, aliahidi kuwa Serikali ya Tanzania itaendelea kuimarisha uhusiano huo wa kirafiki kwa kuhakikisha kuwa misaada inayotolewa inaleta tija kwa wananchi na kuchangia katika kufikia malengo ya maendeleo endelevu.
Kwa upande wake, Balozi wa Tanzania nchini Uswisi, Mhe. Nicole Providoli, amesema kuwa Serikali ya nchi yake kupitia Chemba ya Biashara ya Uswisi na Tanzania (Swiss-Tanzania Chamber of Commerce - STCC), itaendelea kusaidia jitihada za pande zote mbili katika kuanzisha fursa za biashara na uwekezaji, kwa lengo la kukuza uchumi na ustawi wa wananchi wa pande zote.
Maadhimisho hayo yalihudhuriwa na mabalozi, wawakilishi wa mashirika ya kimataifa, viongozi wa serikali na wadau mbalimbali wa maendeleo.
Labels:
KITAIFA