Home » » DC LUSHOTO AKAGUA ZOEZI LA UPOKEAJI NA UANDIKISHWAJI WA WANAFUNZI DARASA LA KWANZA NA AWALI

DC LUSHOTO AKAGUA ZOEZI LA UPOKEAJI NA UANDIKISHWAJI WA WANAFUNZI DARASA LA KWANZA NA AWALI

Written By CCMdijitali on Wednesday, January 19, 2022 | January 19, 2022

 MKUU WA WILAYA YA LUSHOTO ATEMBELEA NA KUKAGUA ZOEZI LA UPOKEAJI NA UANDIKISHWAJI WA WANAFUNZI WA DARASA LA KWANZA NA AWALI KATIKA SHULE ZA MSINGI HALMASHAURI YA WILAYA YA LUSHOTO

Mkuu wa Wilaya ya Lushoto Ndugu Kalisti Lazaro ametembelea na Kukagua Zoezi la Upokeaji na Uandikishwaji wa Wanafunzi wa Darasa la Kwanza na Awali katika Shule za Msingi Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto.

Mkuu wa Wilaya ametoa Maagizo kwa Waalimu Wakuu kuwa Wawapokee na Kuwaandikisha Wanafunzi wa Darasa la Kwanza na Awali kama Utaratibu wa Serikali unavyoelekeza na bila Kuwarudisha Nyumbani kwa Kutokuwa na Sare za Shule na Kuwachangisha Wazazi Michango isiyo na Kibali. 
Alieleza "Mwalimu wapokeeni Wanafunzi na Kuwaandikisha bila Masharti, Serikali imeweka Utaratibu Mzuri msiuvuruge, Kama Mwanafunzi hana Sare za Shule apokelewe na Mzazi wake apewe muda wa Kulitekeleza hilo bila Mwanafunzi kuzuiwa kuingia Darasani na Michango inayoruhusiwa ni ile tuu ambayo Ofisi ya Mkuu wa Wilaya imeipitisha na kutoa Kibali cha Mchango"

 

Mkuu wa Wilaya ya Lushoto ndugu Kalisti Lazaro akiwa Shule ya Msingi Mbula katika Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto

Mkuu wa Wilaya ya Lushoto ndugu Kalisti Lazaro akiwa Shule ya Msingi Mbula katika Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto






Share this article :
 
Support : #BegaKwaBegaNaMamaSamia | JAK | CCM Arusha
Copyright © 2011. CCM Dijitali - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Jasper K
Proudly powered by Blogger
Link