Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) |
Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) |
Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara Dkt. Ashatu Kijaji (Mb)
amewataka wazalishaji wa vifaa vya ujenzi, wasambazaji na
wafanyabiashara kushusha mara moja Bei ya bidhaa hizo walizopandisha
kiholela bila sababu za msingi ambayo imepelekea kumuumiza mlaji wa
chini.
Agizo hilo ni matokeo ya tathimini iliyofanyika ambayo
ilibaini kuwa ongezeko holela la bei ya vifaa vya ujenzi hususani
saruji na nondo ambalo linasabishwa na wazalishaji wa bidhaa husika
kutokuwa na mfumo wa wazi.
Waziri Kijaji ameyasema hayo tarehe 7
Februari, 2022 Jijini Dodoma wakati alipokuwa akiongea na vyombo vya
Habari ambapo pia alisema agizo hilo pia linawahusu wazalishaji na
wasambazaji wa vinywaji baridi.
Alisema kuwa tathimini
iliyofanyika imeonesha kuwa gharama halisi za uzalishaji wa saruji
haiakisiwi katika bei ya saruji iliyopo sokoni ikilinganisha na uwiano
huo Katika Nchi jirani, na kwamba ongezeko la Bei ya saruji na nondo
halina uwiano halisi na gharama za usafirishaji na usambazaji.
"Utafiti
wetu umegundua kuwa Kuna ucheleweshaji wa makusudi wa utoaji saruji
kutoka viwandani kwenda kwa wasambazaji na wanunuzi wa ndani hususani
wale wasambazaji na wanunuzi wadogo ambao tayari wanakuwa wamekwisha
lipia saruji husika na kuweza kusababisha wao kupandisha bei " Alisema
Dkt. Kijaji.
Aidha kupitia utafiti huo ametoa maagizo kwa mamlaka
zote za udhibiti kuchukua hatua kali dhidi ya walimbikizaji na wauzaji
kupitia mlango wa nyuma (black market) wanaosababisha bei za bidhaa
sokoni kupanda ili kuhakikisha bidhaa zinafika sokoni Kwa wakati na kwa
bei shindani ambayo haina maumivu kwa wananchi.
"Kwa kuwa kitendo cha kupanga bei kati ya washindani ni uhujumu uchumi nawaagiza mamlaka husika kuchukua hatua kali dhidi ya wote watakaobainika kukaa na kupanga bei kwa bidhaa kwa mujibu wa sheria za Nchi yetu"
"Ninawaelekeza wazalishaji kuzalisha bidhaa hizo kulingana na uwezo uliosimikwa kwenye viwanda vyenu ili kukidhi mahitaji ya soko ndani ya Taifa letu na kuwa na uwezo wa kuuza nje ya mipaka yetu ." Alisema Dkt. Kijaji.