Home » » MAONYESHO YA WAJASIRIAMALI NJOMBE KUELEKEA UZINDUZI WA MWENGE KITAIFA

MAONYESHO YA WAJASIRIAMALI NJOMBE KUELEKEA UZINDUZI WA MWENGE KITAIFA

Written By CCMdijitali on Wednesday, March 30, 2022 | March 30, 2022

 






 

 MAONYESHO YA WAJASIRIAMALI 

NJOMBE KUELEKEA UZINDUZI WA 

MWENGE KITAIFA


Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mhe. Waziri Kindamba . amezindua maonyesho ya kibiashara (Wajasiriamali) yaliyofanyika katika viwanja vya Sabasaba. kama amsha amsha kuelekea Uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa utakaofanyika katika Mkoa wa Njombe Tarehe 02 Aprili, 2022.

Mhe,Waziri ameipongeza Benki ya CRDB kwakudhamini Uzinduzi huu wa Mwenge wa Uhuru pamoja na kufanya maboresho ya uwanja ambao utatumika katika uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa .

Aidha Mhe.Waziri Kindamba amewasisitiza Wananchi kushiriki kikamilifu kwenye Sensa ya watu na Makazi ambayo itafanyika Mwezi wa Nane mwaka huu ili kuunga mkono Kaulimbiu ya Mbio za Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2022 isemayo-

"SENSA NI MSINGI WA MIPANGO YA MAENDELEO: SHIRIKI KUHESABIWA TUYAFIKIE MAENDELEO YA TAIFA".


Pamoja na mambo mengine Mhe.Kindamba amewaasa Wananchi kuendelea kujitokeza kupata chanjo ya UVIKO -19.


".. Chanjo ya UVIKO-19 ni muhimu kwajili ya Kujikinga na maambukizi ya Ugonjwa wa UVIKO ambalo ni gonjwa hatari sana linalo shambulia mataifa mengi, nawaomba Wananjombe mzidi kujitokeza kuchoma chanjo ya Uviko 19 na hapa kwenye maonyesho kuna Mabanda maalumu ya kutolea chanjo." Mhe.Kindamba.


Mwisho Mhe.Kindamba amewakaribisha Wananchi wote kushiriki katika Uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2022.

"..Napenda kuwaalika wananchi wote kwenye *Uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa utakaofanyika Katika viwanja vya Sabasaba Njombe..".
Mhe.Kindamba.


#Njombetupotayari
# VisitNjombe
#vijanawamamasamia🇹🇿

Share this article :
 
Support : #BegaKwaBegaNaMamaSamia | JAK | CCM Arusha
Copyright © 2011. CCM Dijitali - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Jasper K
Proudly powered by Blogger
Link