Naibu Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Dotto Biteko amesema ili kuwa na maendeleo ni vema kufanya siasa za kubadili maisha ya watu badala ya siasa za maneno.
Vilevile amesema Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wanatakiwa kuacha kujiingiza kwenye matusi na kejeli badala yake wa waelezee yale waliyofanyika kwenye maeneo.
Biteko ameyasema hayo leo mjini Lugoba alipokuwa akihutubia Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) pamoja na Wakazi wa Jimbo la Chalinze kwenye mkutano wa kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Ilani uliondaliwa na Mbunge wa jimbo hilo Ridhiwani Kikwete.












