Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro Mhe.Raymond Mwangwala Leo tarehe 13 Octoba 2023 ametembelea Maendeleo ya Ujenzi wa Shule mpya ya Sekondari PINYINYI
Mhe.Mwangwala amesema Serikali inayoongozwa na Mhe.Rais Dkt Samia Suluhu Hassan Mwezi June 2023 kupitia mpango wa kuboresha elimu ya sekondari yaani SEQUIP ilileta sh. 584,280,028 kwaajili ya ujenzi wa shule mpya ya SEQUIP kata ya Pinyinyi.
"Majengo yatakayojengwa ni ,Vyumba 8 vya madarasa,Jengo la utawala,Maabara 3 za sayansi,Jengo la TEHAMA ,Maktaba , Matundu 20 ya choo cha wanafunzi,Matanki ya kukusanyia maji" amesema Mwangwala
"Aidha Mwangalwa ameridhishwa na Ujenzi baadhi ya majengo na kuwataka mafundi na wasimamizi Ujenzi Shule Hiyo kuongeza Kasi ya Ujenzi ili kukabuliana na Hali ya mvua ya EL NINO inayotarajia kuanzia hivi Karibuni ili Ujenzi usisimame na majengo yawe yamekamilika kabla ya tarehe 25 Octoba 2023







