Home » » DUA MAALUMU YA KUMUOMBEA DKT: SAMIA NA TAIFA LAFANYIKA MKOANI MBEYA

DUA MAALUMU YA KUMUOMBEA DKT: SAMIA NA TAIFA LAFANYIKA MKOANI MBEYA

Written By CCMdijitali on Sunday, October 29, 2023 | October 29, 2023




Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Comrade Juma Homera Leo Oktoba 29 2023 ameshiriki Kongamano la Jukwaa la Wanawake wa Kiislamu Tanzania Mkoa wa Mbeya (JUWAKITA) lililolenga kumuombea na kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt: Samia Suluhu Hassan kwa jitihada zake za kuyagusa Moja kwa Moja Maisha ya Makundi maalumu hasa Wanawake na Watoto (Walemavu,Yatima na Wajane) katika nyanja mbali mbali.


Katika Kongamano hilo imesomwa Dua maalumu ya Kumuombea Dkt: Samia na Taifa kwa Ujumla ambapo mbali na Dua hiyo Kiasi Cha zaidi ya Shilingi Milioni 31 zimechangwa kwaajiri ya kuyasiadia Makundi hayo maalumu ikiwa ni sehemu ya kutambua na kuunga Mkono Jitihada za Rais Dkt: Samia.

Ushiriki Wa RC Homera umewaibua pia Waziri wa Fedha pia Dkt: Mwigulu Nchemba ambaye ameshiriki kwa Njia ya Simu kadharika Naibu Waziri wa Maji Eng: Maryprisca Mahundi.

Katika hotuba yake fupi aliyoitoa baada ya Harambee RC Homera amewaasa Waislamu wote(Wanawake) kuendelea kudumisha Moyo wa kujitoa kwa kuwasaidia wasiojiweza na kuepuka Tabia ya kuyatenga na kuyanyanyapaa Makundi ya wasiojiweza na kuiga mfano kwa Rais wa Taifa hili.

Homera amesema mara zote Dkt: Samia amekuwa akiasa kuwa Kila binadamu anastahili kupendwa na kuthaminiwa hivyo jambo walililolifanya ni Ibada tosha na wamejitwalia thawabu Kutoka kwa Mwenyezi MUNGU kama ambavyo Mtume S.W.A anavyowaagiza katika Quran tukufu.






Share this article :
 
Support : #BegaKwaBegaNaMamaSamia | JAK | CCM Arusha
Copyright © 2011. CCM Dijitali - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Jasper K
Proudly powered by Blogger
Link