Home » » THBUB YATEMBELEA VYUO VYA MAFUNZO YA AMALI, PEMBA

THBUB YATEMBELEA VYUO VYA MAFUNZO YA AMALI, PEMBA

Written By CCMdijitali on Saturday, February 1, 2025 | February 01, 2025

 THBUB YATEMBELEA VYUO VYA MAFUNZO YA AMALI, PEMBA


TUME ya Haki za Binaadamu na Utawala Bora (THBUB) imefanya ziara ya kuvitembelea vyuo

viwili vya Mafunzo ya Amali vya Vitongoji, Wilaya ya Chake Mkoa wa Kusini Pemba na cha

Daya Mtambwe, Wilaya ya Wete, Mkoa wa Kaskazini Pemba, kwa lengo la kutoa elimu na

kujenga uelewa mpana kwa jamii juu ya dhana nzima ya Haki za Binadamu na Misingi ya

Utawala Bora.


Maafisa wa Tume hiyo, Ofisi ya Pemba wakiongozwa na Afisa Uchunguzi Ndg. Ramadhani Slaa

wameifunza jamii juu ya umuhimu wa kutambua Haki za Binaadamu na Utawala Bora pamoja

ushiriki na kuanzisha klabu za Haki za Binaadamu katika vyuo na kuwashauri wanafunzi wa vyuo

hivyo kujiunga na klabu hizo.


Akizungumza kwenye ziara hiyo, ofisi za chuo cha Vitongoji, Bw. Slaa alieleza nia ya ziara yao

chuoni hapo mbali na kutoa elimu ya Haki za Binaadamu na Utawala Bora lakini kushirikiana na

vyuo hivyo kuanzisha Klabu za Haki za Binadamu na Utawala Bora ili kukuza ushirikiano na nguvu

ya pamoja kwa kuongeza uelewa kwa jamii juu dhana ya Haki za Binaadamu na misingi ya Utawala

Bora.


Aidha, Bw. Ramadhan Slaa awasihi wanafunzi vyuoni humo kuendelea kuwa mabalozi wazuri wa

jamii zao katika kueneza dhana halisi ya Haki za Binaadamu na misingi ya Utawala Bora ili kukuza

jamii yenye uelewa mpana kwa maeneo hayo.


Katika hatua nyengine, THBUB ilimshauri, Mkuu wa chuo cha Daya cha Mtambwe, Mwl. Saada Ali

Hamad, kuanzisha Klabu ya Haki za Binadamu na Utawala Bora chuoni hapo ili kuongeza hamasa

na uelewa zaidi kwa jamii.


Naye, Mwalimu dhamana wa Chuo cha Mafunzo ya Amali cha Vitongoji na Mkuu wa Idara ya

Masomo Mtambukwa chuoni hapo, Mwl. Khamis Abdalla Khamis alitoa shukrani kwa THBUB kwa

kuwatembelea chuoni hapo sambamba na kuishauri Tume kuwa karibu na Klabu hizo ili kuzijengea

uimara na ziwe endelevu pamoja na kuahidi kuzisimamia vyema katika kuendeleza shughuli za

kutoa elimu kupitia klabu hizo.


Halikadhalika,kwa nyakati tofauti wanafunzi wa vyuo viwili hivyo, walipata nafasi ya kuuliza maswali

kuhusu dhana na uelewa wa Haki za Binaadamu na Utawala Bora pia kutaka kujua umuhimu na

faida za kujiunga na Klabu za Haki za Binadamu na Utawala Bora vyuoni humo.


Kwaupande mwengine, wanafunzi hao wameiomba THBUB kurudi tena kwenye vyuo vyao na

kujenga utamaduni wa kuwatembelea mara kwa mara ili wajifunze zaidi. Hata hivyo, waliiahidi Tume

kuongeza ushiriki wao mpana katika kusimamia na kuendeleza klabu hizo ndani ya vyuo vyao.


Kiasi cha wanafunzi wasiopungua 600 wakiwemo 400 kutoka Chuo Cha mafunzo ya Amali cha

Vitongoji na 200 kutoka chuo cha Daya, Mtambile kwa nyakati tofauti walihudhuria hafla hiyo

iliyowajenga kitaaluma na kuelezwa juu ya umuhimu wa kushiriki klabu kama hizo na umuhimu wake

wa kuanzishwa kwenye vyuo vyao.

MAOFISA kutoka Tume ya Haki za Binaadamu na Utawala Bora (THBUB) wakiwapa elimu ya uelewa mapana juu ya dhana ya Haki za binaadamu na misingi ya Utawala Bora katika vyuo vya Mafunzo ya Amali vya Vitongoji na Daya, Pemba.



WANAFUNZI wa Chuo Cha Mafunzo ya Amali wa chuo cha Daya, mtambile,Wilaya ya Wete, Mkoa wa Kaskazini Pemba wakiwasikiliza Maofisa kutoka Tume ya Haki za Binaadamu na Utawala Bora (THBUB) juu ya uelewa mpana wa dhana ya Haki za binaadamu na misingi ya Utawala Bora.


WANAFUNZI wa Chuo Cha Mafunzo ya Amali wa chuo cha Daya, mtambile,Wilaya ya Wete, Mkoa wa Kaskazini Pemba wakiwasikiliza Maofisa kutoka Tume ya Haki za Binaadamu na Utawala Bora (THBUB) juu ya uelewa mpana wa dhana ya Haki za binaadamu na misingi ya Utawala Bora.


MAOFISA kutoka Tume ya Haki za Binaadamu na Utawala Bora (THBUB) wakiwapa elimu ya uelewa mapana juu ya dhana ya Haki za binaadamu na misingi ya Utawala Bora katika vyuo vya Mafunzo ya Amali vya Vitongoji na Daya, Pemba.



MWISHO.

Share this article :
 
Support : #BegaKwaBegaNaMamaSamia | JAK | CCM Arusha
Copyright © 2011. CCM Dijitali - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Jasper K
Proudly powered by Blogger
Link