DAY [3] WABUNGE WA JIMBO LA ARUSHA KATA YA OLASITI
Mkutano wa kujitambulisha Wagombea Ubunge na Udiwani wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Arusha, Kata ya OLASITI MKOA WA ARUSHA Jimbo la A...
Latest Post
June 30, 2025
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango ametoa wito wa kufanyika maboresho ya mfumo wa fedha na ufadhili wa maendeleo duniani ili kutoa nafuu ya riba, kuwa endelevu, unaotabirika na unaozingatia usawa na vipaumbele vya mataifa yanayoendelea.
Makamu wa Rais ametoa wito huo wakati akihutubia Mkutano wa Nne wa Kimataifa kuhusu Ufadhili wa Maendeleo (FfD4) unaofanyika Jijini Sevilla nchini Hispania. Amesisitiza umuhimu wa mbinu za kibunifu katika ufadhili ikiwemo kubadili madeni ya kifedha kwenda katika utekelezaji wa miradi mbalimbali kama vile uhifadhi wa mazingira.
Vilevile Makamu wa Rais amesema taratibu za upimaji wa uwezo wa serikali kifedha katika ulipaji madeni unapaswa kupitiwa upya ili kuongeza uwazi na kuwa wa haki. Ameongeza kwamba Mkutano huo unapaswa kutoa ufumbuzi wa namna ya kupunguza gharama za ukopaji na kuongeza fursa za mikopo nafuu na ya muda mrefu.
Makamu wa Rais amesema kutokana na biashara kuwa nguzo ya kiuchumi ni vema mataifa kuwezeshwa katika uzalishaji na uongezawaji thamani wa bidhaa ili kufikia viwango vya kimataifa. Amesisitiza uwepo wa usawa na haki katika taratibu na sheria za kibiashara za kimataifa ikiwemo masuala ya ushuru wa forodha na ukomo wa mauzo kwa mataifa yanayoendelea.
Aidha Makamu wa Rais amesema unahitajika ushirikiano baina ya Mataifa yaliyoendelea na yanayoendelea katika kuharakisha maendeleo ya sayansi, teknolojia na takwimu ili kuweza kusaidia katika utungaji sera na utekelezaji kwa kuzingatia tafiti na takwimu sahihi.
Halikadhalika, Makamu wa Rais amesisitiza umuhimu wa Mataifa tajiri kushirikiana na nchi zinazoendelea katika kupunguza viatarishi kwenye uwekezaji na ufadhili wa miradi mikubwa ya kimkakati ya maendeleo.
Kuhusu Mazingira, Makamu wa Rais ametoa wito wa kutoa kipaumbele katika ufadhili wa usimamizi na urejerezaji wa bioanuai pamoja na kuongeza wigo wa ufadhili katika miradi ya kujenga uhimilivu na miradi ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi. Amesisitiza umuhimu wa kuanza kazi kwa mfuko wa mazingira wa kukabiliana na hasara na uharibifu unaosababishwa na mabadiliko ya tabianchi (Loss and Demage Fund).
Makamu wa Rais amesema kufikia mwaka 2024, Tanzania imefikia asilimia 60 ya utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs) kwa kupiga hatua zaidi katika lengo namba 2 hadi namba 7 hususani katika maeneo ya afya, utoshelevu wa chakula, elimu, usawa wa kijinsia, upatikanaji wa maji safi na salama pamoja na upatikanaji wa nishati.
Ameongeza kwamba ili kuendeleza mafanikio hayo unahitajika ushirikiano na ufadhili wa gharama nafuu katika kuongezea mapato ya ndani ya nchi.
Mkutano wa Nne wa Kimataifa wa kuhusu Ufadhili wa Maendeleo unalenga kutafuta ufumbuzi wa changamoto zinazoikabili dunia katika kugharamia utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs), kujadili njia za kurekebisha mfumo wa fedha wa kimataifa ili kuwa jumuishi, wenye usawa na unaozingatia mahitaji ya nchi zinazoendelea.
Malengo mengine ya Mkutano huo ni pamoja na kupendekeza mbinu bora za kupunguza na kushughulikia mzigo wa madeni kwa nchi maskini na zenye kipato cha kati pamoja na kujenga mifumo madhubuti ya kifedha inayoweza kukabili athari za majanga ya kiuchumi, kijamii na kimazingira.
Mkutano kuhusu Ufadhili wa Maendeleo ulianzishwa rasmi mwaka 2002 kupitia Mkutano wa kwanza uliofanyika Monterrey, Mexico na kupelekea kuundwa kwa msingi wa ushirikiano wa kimataifa katika kufadhili maendeleo. Mkutano wa Pili ulifanyika mjini Doha, Qatar mwaka 2008 ambao ulianzisha Azimio la Doha kusisitiza haja ya kuimarisha mshikamano wa kimataifa katika kukabiliana na athari za mtikisiko wa kifedha duniani.
Mkutano wa Tatu ulifanyika Addis Ababa, Ethiopia, mwaka 2015, na matokeo yake yalikuwa ni Addis Ababa Action Agenda (AAAA), ambayo ilijikita katika uhamasishaji wa vyanzo vya ndani vya mapato, ushirikiano wa kimataifa, uwekezaji wa sekta binafsi, pamoja na kushughulikia changamoto za madeni na usawa wa kijinsia.
Mkutano huu wa Nne ambao umepitisha Azimio la Sevilla unalenga kuchambua maendeleo yaliyopatikana tangu Addis Ababa na kujadili njia bora za kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu katika muktadha wa changamoto mpya kama vile mabadiliko ya tabianchi, migogoro ya kimataifa na athari za kiuchumi za janga la Uviko -19.
Imetolewa na
Ofisi ya Makamu wa Rais
30 Juni 2025
Sevilla - Hispania.



Dkt. Philip Mpango ametoa wito wa kufanyika maboresho ya mfumo wa fedha na ufadhili wa maendeleo duniani.
Written By CCMdijitali on Monday, June 30, 2025 | June 30, 2025
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango ametoa wito wa kufanyika maboresho ya mfumo wa fedha na ufadhili wa maendeleo duniani ili kutoa nafuu ya riba, kuwa endelevu, unaotabirika na unaozingatia usawa na vipaumbele vya mataifa yanayoendelea.
Makamu wa Rais ametoa wito huo wakati akihutubia Mkutano wa Nne wa Kimataifa kuhusu Ufadhili wa Maendeleo (FfD4) unaofanyika Jijini Sevilla nchini Hispania. Amesisitiza umuhimu wa mbinu za kibunifu katika ufadhili ikiwemo kubadili madeni ya kifedha kwenda katika utekelezaji wa miradi mbalimbali kama vile uhifadhi wa mazingira.
Vilevile Makamu wa Rais amesema taratibu za upimaji wa uwezo wa serikali kifedha katika ulipaji madeni unapaswa kupitiwa upya ili kuongeza uwazi na kuwa wa haki. Ameongeza kwamba Mkutano huo unapaswa kutoa ufumbuzi wa namna ya kupunguza gharama za ukopaji na kuongeza fursa za mikopo nafuu na ya muda mrefu.
Makamu wa Rais amesema kutokana na biashara kuwa nguzo ya kiuchumi ni vema mataifa kuwezeshwa katika uzalishaji na uongezawaji thamani wa bidhaa ili kufikia viwango vya kimataifa. Amesisitiza uwepo wa usawa na haki katika taratibu na sheria za kibiashara za kimataifa ikiwemo masuala ya ushuru wa forodha na ukomo wa mauzo kwa mataifa yanayoendelea.
Aidha Makamu wa Rais amesema unahitajika ushirikiano baina ya Mataifa yaliyoendelea na yanayoendelea katika kuharakisha maendeleo ya sayansi, teknolojia na takwimu ili kuweza kusaidia katika utungaji sera na utekelezaji kwa kuzingatia tafiti na takwimu sahihi.
Halikadhalika, Makamu wa Rais amesisitiza umuhimu wa Mataifa tajiri kushirikiana na nchi zinazoendelea katika kupunguza viatarishi kwenye uwekezaji na ufadhili wa miradi mikubwa ya kimkakati ya maendeleo.
Kuhusu Mazingira, Makamu wa Rais ametoa wito wa kutoa kipaumbele katika ufadhili wa usimamizi na urejerezaji wa bioanuai pamoja na kuongeza wigo wa ufadhili katika miradi ya kujenga uhimilivu na miradi ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi. Amesisitiza umuhimu wa kuanza kazi kwa mfuko wa mazingira wa kukabiliana na hasara na uharibifu unaosababishwa na mabadiliko ya tabianchi (Loss and Demage Fund).
Makamu wa Rais amesema kufikia mwaka 2024, Tanzania imefikia asilimia 60 ya utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs) kwa kupiga hatua zaidi katika lengo namba 2 hadi namba 7 hususani katika maeneo ya afya, utoshelevu wa chakula, elimu, usawa wa kijinsia, upatikanaji wa maji safi na salama pamoja na upatikanaji wa nishati.
Ameongeza kwamba ili kuendeleza mafanikio hayo unahitajika ushirikiano na ufadhili wa gharama nafuu katika kuongezea mapato ya ndani ya nchi.
Mkutano wa Nne wa Kimataifa wa kuhusu Ufadhili wa Maendeleo unalenga kutafuta ufumbuzi wa changamoto zinazoikabili dunia katika kugharamia utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs), kujadili njia za kurekebisha mfumo wa fedha wa kimataifa ili kuwa jumuishi, wenye usawa na unaozingatia mahitaji ya nchi zinazoendelea.
Malengo mengine ya Mkutano huo ni pamoja na kupendekeza mbinu bora za kupunguza na kushughulikia mzigo wa madeni kwa nchi maskini na zenye kipato cha kati pamoja na kujenga mifumo madhubuti ya kifedha inayoweza kukabili athari za majanga ya kiuchumi, kijamii na kimazingira.
Mkutano kuhusu Ufadhili wa Maendeleo ulianzishwa rasmi mwaka 2002 kupitia Mkutano wa kwanza uliofanyika Monterrey, Mexico na kupelekea kuundwa kwa msingi wa ushirikiano wa kimataifa katika kufadhili maendeleo. Mkutano wa Pili ulifanyika mjini Doha, Qatar mwaka 2008 ambao ulianzisha Azimio la Doha kusisitiza haja ya kuimarisha mshikamano wa kimataifa katika kukabiliana na athari za mtikisiko wa kifedha duniani.
Mkutano wa Tatu ulifanyika Addis Ababa, Ethiopia, mwaka 2015, na matokeo yake yalikuwa ni Addis Ababa Action Agenda (AAAA), ambayo ilijikita katika uhamasishaji wa vyanzo vya ndani vya mapato, ushirikiano wa kimataifa, uwekezaji wa sekta binafsi, pamoja na kushughulikia changamoto za madeni na usawa wa kijinsia.
Mkutano huu wa Nne ambao umepitisha Azimio la Sevilla unalenga kuchambua maendeleo yaliyopatikana tangu Addis Ababa na kujadili njia bora za kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu katika muktadha wa changamoto mpya kama vile mabadiliko ya tabianchi, migogoro ya kimataifa na athari za kiuchumi za janga la Uviko -19.
Imetolewa na
Ofisi ya Makamu wa Rais
30 Juni 2025
Sevilla - Hispania.




Labels:
KIMATAIFA
June 29, 2025
Dar es Salaam
Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) mkoa wa Dar es Salaam wamefanya ukaguzi wa ujenzi na matengenezo ya barabara katika mkoa huo unaolenga kuhakikisha miradi inakamilika kwa viwango na kwa wakati.
Meneja wa TARURA mkoa wa Dar es Salaam, Mhandisi Geofrey Mkinga amesema kuwa, wametembelea wilaya ya Temeke ambapo walikagua barabara mbalimbali ikiwemo barabara ya kwa Diwani na zile zinazotekelezwa chini ya mradi wa Uendelezaji Jiji la Dar es Salaam awamu ya pili (DMDP).
“Tumeona maendeleo mazuri kwenye utekelezaji, Mkandarasi yupo kazini na tunatarajia kujenga zaidi ya Km 7.2 katika eneo la makazi na biashara, ambapo magari makubwa na malori hupita mara kwa mara. Barabara zinajengwa kwa kiwango cha zege ili kukidhi mahitaji ya shughuli za kiuchumi zinazofanyika", amesema Mkinga.
Pia alitembelea barabara ya Yombo yenye urefu wa Km 1.6, ambapo ujenzi unaendelea kwa kiwango cha zege katika maeneo ya wazi pamoja na kipande cha mita 600 kinachojengwa kwa kushirikiana na Manispaa ya Temeke.
“Ninamshukuru Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke kwa kuwezesha upatikanaji wa fedha za matengenezo. Hii imerahisisha utekelezaji wa barabara ya Yombo na ile ya Dkt. Omar. Kipande cha mita 600 kinachojengwa chote kwa zege”, ameongeza.
Meneja Mkinga pia alitembelea barabara ya Tuangoma–Masaki yenye urefu wa Km 3.9, eneo ambalo awali lilikuwa na changamoto kubwa ya mvua na udongo laini uliokuwa ukisababisha kukatika kwa mawasiliano.
“Hili ni eneo la mchanga, mvua ikinyesha tu hakuna mawasiliano kabisa. Mkandarasi anayetekeleza mradi huu anafanya kazi chini ya mkataba wenye thamani ya Shilingi bilioni 27. Mradi unahusisha pia ujenzi wa vivuko vya Chaulembo ambavyo vimepangwa kwa mujibu wa maelekezo ya viongozi wa mkoa”, amesema.
Akiwa eneo la Chamaruba, ameeleza namna mvua kubwa za Aprili na Mei zilivyoharibu miundombinu na kufunga kabisa mawasiliano kati ya pande mbili za mtaa huo. Hata hivyo, kwa ushirikiano na viongozi wa Serikali ya Mtaa na Serikali Kuu, fedha za dharura zilitolewa ili kujenga makalavati matano na kurudisha mawasiliano.
Kwa upande wao, wananchi wa maeneo hayo walitoa shukrani zao kwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan kwa kufanikisha miradi hiyo ambayo imeleta unafuu mkubwa kwa wananchi.
“Awali ilikuwa tunapata shida kuwavusha watoto kwenda shule, hadi mzazi umpeleke mtoto na umrudishe. Wakati mwingine wagonjwa walihitaji kubebwa hadi upande wa pili. Lakini sasa hivi, tuna daraja, tuna barabara, tuna amani, tunaishukuru serikali", amesema mmoja wa wakazi wa eneo la Chamaruba.






TARURA YAENDELEA NA UKAGUZI WA BARABARA TEMEKE, YAELEZA MAFANIKIO YA MIRADI YA DMDP II
Written By CCMdijitali on Sunday, June 29, 2025 | June 29, 2025
Dar es Salaam
Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) mkoa wa Dar es Salaam wamefanya ukaguzi wa ujenzi na matengenezo ya barabara katika mkoa huo unaolenga kuhakikisha miradi inakamilika kwa viwango na kwa wakati.
Meneja wa TARURA mkoa wa Dar es Salaam, Mhandisi Geofrey Mkinga amesema kuwa, wametembelea wilaya ya Temeke ambapo walikagua barabara mbalimbali ikiwemo barabara ya kwa Diwani na zile zinazotekelezwa chini ya mradi wa Uendelezaji Jiji la Dar es Salaam awamu ya pili (DMDP).
“Tumeona maendeleo mazuri kwenye utekelezaji, Mkandarasi yupo kazini na tunatarajia kujenga zaidi ya Km 7.2 katika eneo la makazi na biashara, ambapo magari makubwa na malori hupita mara kwa mara. Barabara zinajengwa kwa kiwango cha zege ili kukidhi mahitaji ya shughuli za kiuchumi zinazofanyika", amesema Mkinga.
Pia alitembelea barabara ya Yombo yenye urefu wa Km 1.6, ambapo ujenzi unaendelea kwa kiwango cha zege katika maeneo ya wazi pamoja na kipande cha mita 600 kinachojengwa kwa kushirikiana na Manispaa ya Temeke.
“Ninamshukuru Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke kwa kuwezesha upatikanaji wa fedha za matengenezo. Hii imerahisisha utekelezaji wa barabara ya Yombo na ile ya Dkt. Omar. Kipande cha mita 600 kinachojengwa chote kwa zege”, ameongeza.
Meneja Mkinga pia alitembelea barabara ya Tuangoma–Masaki yenye urefu wa Km 3.9, eneo ambalo awali lilikuwa na changamoto kubwa ya mvua na udongo laini uliokuwa ukisababisha kukatika kwa mawasiliano.
“Hili ni eneo la mchanga, mvua ikinyesha tu hakuna mawasiliano kabisa. Mkandarasi anayetekeleza mradi huu anafanya kazi chini ya mkataba wenye thamani ya Shilingi bilioni 27. Mradi unahusisha pia ujenzi wa vivuko vya Chaulembo ambavyo vimepangwa kwa mujibu wa maelekezo ya viongozi wa mkoa”, amesema.
Akiwa eneo la Chamaruba, ameeleza namna mvua kubwa za Aprili na Mei zilivyoharibu miundombinu na kufunga kabisa mawasiliano kati ya pande mbili za mtaa huo. Hata hivyo, kwa ushirikiano na viongozi wa Serikali ya Mtaa na Serikali Kuu, fedha za dharura zilitolewa ili kujenga makalavati matano na kurudisha mawasiliano.
Kwa upande wao, wananchi wa maeneo hayo walitoa shukrani zao kwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan kwa kufanikisha miradi hiyo ambayo imeleta unafuu mkubwa kwa wananchi.
“Awali ilikuwa tunapata shida kuwavusha watoto kwenda shule, hadi mzazi umpeleke mtoto na umrudishe. Wakati mwingine wagonjwa walihitaji kubebwa hadi upande wa pili. Lakini sasa hivi, tuna daraja, tuna barabara, tuna amani, tunaishukuru serikali", amesema mmoja wa wakazi wa eneo la Chamaruba.







Labels:
MKOANI
June 29, 2025
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema kuwa Serikali itaendelea kuweka mkazo katika kulinda na kudumisha amani nchini ili kuhamasisha maendeleo na kuziba mianya ya kuibuka kwa migogoro miongoni mwa wanajamii.
Ametoa kauli hiyo leo (Jumapili Juni 29, 2025) wakati alipomwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kufunga kongamano la Afrika Mashariki la Amani lililoandaliwa na The Islamic Foundation, katika viwanja vya shule ya msingi Mirongo jijini Mwanza
“Nataka niwaambie bila amani hatuwezi kupata mafanikio yoyote, kupitia kongamano hili mmepata nafasi ya kujadili kuhusu tunu hii ya amani, ambayo wakati wote tumeshuhudia viongozi wa dini mkiwa kwenye majukwaa yenu mkihimiza amani miongoni mwa wanajamii, tuishike tunu hii”.
Kadhalika, amewataka Watanzania kuangalia kwa upana wake suala la mmomonyoko wa maadili katika jamii hasa kwa vijana. “Ni muhimu sana suala hili mkaliweka kama agenda katika mikutano na vikao vyenu, kila kiongozi wa dini anapozungumza, suala la maadili na mmomonyoko wa liwe ni ajenga ya kudumu”
Amesema kuwa mabadiliko ya teknolojia na kuiga tamaduni za mataifa ya nje imekuwa miongoni mwa chanzo kikubwa cha mmomonyoko wa maadili. “Siku hizi vijana kuwaita wazee kwa majina yasiyo na heshima ni kitu cha kawaida, viongozi ndio wenye jukumu la kusimamia eneo la maadili, mkifanya hivyo tupata vijana wenye maadili mema”
Pia Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa falsafa ya 4R ya Resilience (Ustahimilivu), Reconciliation (Maridhiano) and Reforms (Mageuzi), Rebulding (Kujenga upya) iliyoasisiwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imejikita katika misingi imara ya kulinda amani. “Falsafa hii imeifanya Tanzania kuwa tulivu na salama”
Wakati huo huo Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa jamii inapaswa kuona umuhimu wa kukuza utamaduni wa majadiliano na maridhiano katika kushughulikia tofauti zilizopo mingoni mwa jamii.
“Tunapaswa kujenga jamii inayoheshimu maoni tofauti, na kuhimiza mijadala kwenye majukwaa na kwa nafasi hii viongozi, taasisi na wanajamii mnapaswa kuwa daraja la maridhiano badala ya kuwa vyanzo vya migawanyiko”
Naye Mwenyekiti wa Islamic Foundation Aref Nahdi amesema kuwa taasisi zao zitaendelea kushirikiana na Serikali katika kuijenga Tanzania yenye haki, Amani, usawa, maendeleo na heshima kwa wote.
Aidha, amesema kuwa taasisi hizo zitaendelea kukemea vikali kauli zenye viashiria vya uvunjifu wa amani, upendo na kuvunja heshima za viongozi wa kitaifa. “Kwa kufanya hivyo inakuwa ni sehemu ya mafundisho ya dini”.





TUTAENDELEA KUILINDA NA KUIDUMISHA AMANI NCHINI-MAJALIWA
- Asema falsafa ya 4R ya Rais Dkt. Samia imekuwa msingi imara wa kulinda amani.
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema kuwa Serikali itaendelea kuweka mkazo katika kulinda na kudumisha amani nchini ili kuhamasisha maendeleo na kuziba mianya ya kuibuka kwa migogoro miongoni mwa wanajamii.
Ametoa kauli hiyo leo (Jumapili Juni 29, 2025) wakati alipomwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kufunga kongamano la Afrika Mashariki la Amani lililoandaliwa na The Islamic Foundation, katika viwanja vya shule ya msingi Mirongo jijini Mwanza
“Nataka niwaambie bila amani hatuwezi kupata mafanikio yoyote, kupitia kongamano hili mmepata nafasi ya kujadili kuhusu tunu hii ya amani, ambayo wakati wote tumeshuhudia viongozi wa dini mkiwa kwenye majukwaa yenu mkihimiza amani miongoni mwa wanajamii, tuishike tunu hii”.
Kadhalika, amewataka Watanzania kuangalia kwa upana wake suala la mmomonyoko wa maadili katika jamii hasa kwa vijana. “Ni muhimu sana suala hili mkaliweka kama agenda katika mikutano na vikao vyenu, kila kiongozi wa dini anapozungumza, suala la maadili na mmomonyoko wa liwe ni ajenga ya kudumu”
Amesema kuwa mabadiliko ya teknolojia na kuiga tamaduni za mataifa ya nje imekuwa miongoni mwa chanzo kikubwa cha mmomonyoko wa maadili. “Siku hizi vijana kuwaita wazee kwa majina yasiyo na heshima ni kitu cha kawaida, viongozi ndio wenye jukumu la kusimamia eneo la maadili, mkifanya hivyo tupata vijana wenye maadili mema”
Pia Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa falsafa ya 4R ya Resilience (Ustahimilivu), Reconciliation (Maridhiano) and Reforms (Mageuzi), Rebulding (Kujenga upya) iliyoasisiwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imejikita katika misingi imara ya kulinda amani. “Falsafa hii imeifanya Tanzania kuwa tulivu na salama”
Wakati huo huo Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa jamii inapaswa kuona umuhimu wa kukuza utamaduni wa majadiliano na maridhiano katika kushughulikia tofauti zilizopo mingoni mwa jamii.
“Tunapaswa kujenga jamii inayoheshimu maoni tofauti, na kuhimiza mijadala kwenye majukwaa na kwa nafasi hii viongozi, taasisi na wanajamii mnapaswa kuwa daraja la maridhiano badala ya kuwa vyanzo vya migawanyiko”
Naye Mwenyekiti wa Islamic Foundation Aref Nahdi amesema kuwa taasisi zao zitaendelea kushirikiana na Serikali katika kuijenga Tanzania yenye haki, Amani, usawa, maendeleo na heshima kwa wote.
Aidha, amesema kuwa taasisi hizo zitaendelea kukemea vikali kauli zenye viashiria vya uvunjifu wa amani, upendo na kuvunja heshima za viongozi wa kitaifa. “Kwa kufanya hivyo inakuwa ni sehemu ya mafundisho ya dini”.






Labels:
KITAIFA
June 23, 2025
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa ameziagiza taasisi za Serikali ambazo hazijajiunga na mfumo wa kielektroni utakaowezesha mifumo ya Serikali kuwasiliana (GovESB) kujiunga na mfumo huo ifikapo Julai 30 mwaka huu ili kuendana na mabadiliko ya teknolojia katika kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa wananchi.
Ametoa maagizo hayo leo Jumatatu (Juni 23, 2025) alipomwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Utumishi wa Umma yaliyofanyika katika viwanja vya Chinangali Park Jijini Dodoma.
“Taasisi zote za umma ambazo hazijajiunga na mfumo huu mwisho ni Julai 30 mwaka huu, wote muwe mmeshaingia pale GovESB, huu ni msisitizo ambao ulitolewa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia pindi eGA watakapokamilisha kila taasisi ipeleke mfumo wake, idadi ya taasisi zilizounganishwa ni chache, hakuna gharama na hutakiwi kupanga bajeti”
Ameongeza kuwa mfumo huo unafaida kubwa katika utumishi wa umma kwani utasaidia kurahisisha utendaji, kutoa taarifa kwa wakati, kuondoa makosa ya kibinadamu katika kuwahudumia wananchi pamoja na kuwabana wala rushwa. “Nimefurahi kujulishwa kwamba jumla ya mifumo 223 kutoka kwenye taasisi 185 imeunganishwa na kusomana”.
Aidha, Mheshimiwa Majaliwa ametoa wito kwa taasisi zote za umma zenye mifumo na zinazoendelea kubuni mifumo zihakikishe mifumo hiyo inasomana na inaweza kubadilishana taarifa kupitia mfumo huo wa GovESB ikiwa ni njia mojawapo ya kuendelea kuboresha huduma za Serikali.
Kadhalika Mheshimiwa Majaliwa ameitaka Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) kuhakikisha mifumo iliyounganishwa inaendelea kubadilishana taarifa. “Lakini pia kila anayeingia jiridhishe kuwa anaweza kuwasiliana na wengine wote waliomo ndani, mmenieleza na mmesema kwamba ndivyo ilivyo, nasisitiza kwamba hakikisheni hiyo mifumo inasomana na inabadilishana taarifa”
Katika hatua nyingine, Mheshimiwa Waziri Mkuu ametoa wito kwa watumishi wa umma kuzingatia miiko na maadili ya utumishi katika utekelezaji wa majukumu yao kwa kuzingitia Sera na Sheria kwa manufaa na maendeleo ya Taifa letu. “Nitumie nafasi hii kuwapongeza sana watumishi wote wa umma nchini, niwahikishie kuwa serikali ya awamu ya sita iko pamoja nanyi. “Fanyeni hivyo kwa ajili ya manufaa na maendeleo ya Taifa letu”.
Kwa upande wake, Waziri wa Nchi-Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora George Simbachawene amesema Tanzania imetambulika kimataifa ambapo mwaka 2022 Benki ya Dunia ilifanya utafiti kuhusu ukomavu wa matumizi ya teknolojia duniani katika utoaji wa huduma za Serikali na ushirikishwaji wa wananchi.
Amefafanua kuwa ripoti ya utafiti huo iliyotolewa Machi, 2023 ilibanisha kuwa Tanzania imefanikiwa kupanda daraja kutoka kundi B hadi kundi A na kushika nafasi ya 26 duniani, nafasi ya 2 Afrika na nafasi ya kwanza katika nchi za Afrika Mashariki.
Katika tukio hilo, Mheshimiwa Majaliwa alizindua mifumo miwili ambayo ni Mfumo wa kielektroni unaowezesha mifumo ya Serikali kuwasiliana na kubadilishana taarifa ujulikanao kama Government Enterprises Service Bus (GovESB) Pamoja na Mfumo wa e-Wekeza unaomuwezesha Mtumishi wa Umma kuwekeza katika Mfuko wa Faida (Faida Fund).
Siku ya Utumishi wa Umma husherehekewa Juni 23 kila mwaka na nchi wanachama wa Umoja wa Afrika kwa lengo la kutambua mchango wa Watumishi wa Umma katika maendeleo ya nchi zao na Bara la Afrika kwa ujumla.






MAJALIWA AZIPA WIKI TANO TAASISI ZA SERIKALI KUJIUNGA NA MFUMO UNAOWEZESHA SERIKALI KUWASILIANA
Written By CCMdijitali on Monday, June 23, 2025 | June 23, 2025
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa ameziagiza taasisi za Serikali ambazo hazijajiunga na mfumo wa kielektroni utakaowezesha mifumo ya Serikali kuwasiliana (GovESB) kujiunga na mfumo huo ifikapo Julai 30 mwaka huu ili kuendana na mabadiliko ya teknolojia katika kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa wananchi.
Ametoa maagizo hayo leo Jumatatu (Juni 23, 2025) alipomwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Utumishi wa Umma yaliyofanyika katika viwanja vya Chinangali Park Jijini Dodoma.
“Taasisi zote za umma ambazo hazijajiunga na mfumo huu mwisho ni Julai 30 mwaka huu, wote muwe mmeshaingia pale GovESB, huu ni msisitizo ambao ulitolewa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia pindi eGA watakapokamilisha kila taasisi ipeleke mfumo wake, idadi ya taasisi zilizounganishwa ni chache, hakuna gharama na hutakiwi kupanga bajeti”
Ameongeza kuwa mfumo huo unafaida kubwa katika utumishi wa umma kwani utasaidia kurahisisha utendaji, kutoa taarifa kwa wakati, kuondoa makosa ya kibinadamu katika kuwahudumia wananchi pamoja na kuwabana wala rushwa. “Nimefurahi kujulishwa kwamba jumla ya mifumo 223 kutoka kwenye taasisi 185 imeunganishwa na kusomana”.
Aidha, Mheshimiwa Majaliwa ametoa wito kwa taasisi zote za umma zenye mifumo na zinazoendelea kubuni mifumo zihakikishe mifumo hiyo inasomana na inaweza kubadilishana taarifa kupitia mfumo huo wa GovESB ikiwa ni njia mojawapo ya kuendelea kuboresha huduma za Serikali.
Kadhalika Mheshimiwa Majaliwa ameitaka Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) kuhakikisha mifumo iliyounganishwa inaendelea kubadilishana taarifa. “Lakini pia kila anayeingia jiridhishe kuwa anaweza kuwasiliana na wengine wote waliomo ndani, mmenieleza na mmesema kwamba ndivyo ilivyo, nasisitiza kwamba hakikisheni hiyo mifumo inasomana na inabadilishana taarifa”
Katika hatua nyingine, Mheshimiwa Waziri Mkuu ametoa wito kwa watumishi wa umma kuzingatia miiko na maadili ya utumishi katika utekelezaji wa majukumu yao kwa kuzingitia Sera na Sheria kwa manufaa na maendeleo ya Taifa letu. “Nitumie nafasi hii kuwapongeza sana watumishi wote wa umma nchini, niwahikishie kuwa serikali ya awamu ya sita iko pamoja nanyi. “Fanyeni hivyo kwa ajili ya manufaa na maendeleo ya Taifa letu”.
Kwa upande wake, Waziri wa Nchi-Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora George Simbachawene amesema Tanzania imetambulika kimataifa ambapo mwaka 2022 Benki ya Dunia ilifanya utafiti kuhusu ukomavu wa matumizi ya teknolojia duniani katika utoaji wa huduma za Serikali na ushirikishwaji wa wananchi.
Amefafanua kuwa ripoti ya utafiti huo iliyotolewa Machi, 2023 ilibanisha kuwa Tanzania imefanikiwa kupanda daraja kutoka kundi B hadi kundi A na kushika nafasi ya 26 duniani, nafasi ya 2 Afrika na nafasi ya kwanza katika nchi za Afrika Mashariki.
Katika tukio hilo, Mheshimiwa Majaliwa alizindua mifumo miwili ambayo ni Mfumo wa kielektroni unaowezesha mifumo ya Serikali kuwasiliana na kubadilishana taarifa ujulikanao kama Government Enterprises Service Bus (GovESB) Pamoja na Mfumo wa e-Wekeza unaomuwezesha Mtumishi wa Umma kuwekeza katika Mfuko wa Faida (Faida Fund).
Siku ya Utumishi wa Umma husherehekewa Juni 23 kila mwaka na nchi wanachama wa Umoja wa Afrika kwa lengo la kutambua mchango wa Watumishi wa Umma katika maendeleo ya nchi zao na Bara la Afrika kwa ujumla.







Labels:
KITAIFA
June 20, 2025
▪️Asema lengo ni kuendelea kutoa wahitimu wenye uwezo wa kukidhi vigezo vya kimataifa
▪️Rais Dkt. Samia atoa milioni 100 kuchangia maendeleo ya Chuo Kikuu cha Waislamu cha Morogoro
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa ameitaka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na TAMISEMI pamoja kusimamia na kudhibiti ubora wa elimu inayotolewa kuanzia elimu ya msingi mpaka elimu ya juu ili kuendelea kukidhi viwango vya kitaifa, kikanda na kimataifa.
Ametoa maagizo hayo leo (Ijumaa Juni 20, 2025) alipomwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye maadhimisho ya miaka 20 ya Chuo Kikuu cha Waislamu cha Morogoro (MUM), kwenye viwanja vya chuo hicho mkoani Morogoro.
“Mamlaka zetu ziendelee kusimamia hilo kwa kufanya hivyo sio tu kutaendelea kukuza ubora wa elimu yetu, bali pia kutawawezesha wasomi nchini kukidhi viwango na mahitaji ya soko la ajira”
Kadhalika, Mheshimiwa Majaliwa amezitaka Taasisi za Elimu nchini ziimarishe mahusiano na vyuo vyote nchini vinavyotoa maarifa kwa vijana wa kitanzania pamoja na kuzalisha wakufunzi ili kuwa sehemu ya mtandao wa utoaji maarifa na taalum hapa nchini.
Aidha, Mheshimiwa Majaliwa kuwa katika kuunga mkono jitihada za wadau mbalimbali katika kuchangia maendeleo ya chuo hicho kupitia mfumo maalum wa (MUM Community Fund), Rais Dkt. Samia ametoa kiasi cha Shilingi milioni 100 ili kiendelee kutoa huduma kwa watoto wa Kitanzania
Mheshimwa Waziri Mkuu ameongeza kuwa Serikali inaendelea na ujenzi wa Mfumo wa Takwimu wa Sekta ya Elimu utakaowezesha upatikanaji wa takwimu zote za sekta hiyo ambao utakuwa na uwezo wa kupokea takwimu mbalimbali zinazohusiana na elimu kutoka katika mifumo mingine ya Serikali ikiwemo NIDA, RITA na Wizara ya Mambo ya Nje.
Kwa Upande wake Naibu Waziri wa Elimu Qs Omar Kipanga amesema kuwa katika kipindi cha miaka 20, chuo hicho kimefanikiwa kuwa na progrma zaidi ya 32 kutoka program mbili wakati kinaanza na kimefanikiwa kutoa wahitimu zaidi ya 15,000.
“Wahitimu hawa wamekuwa wwamekuwa wa kupigiwa mfano katika kazi na maadili inayofanya waaminiwe katika nafasi mbalimbali kwenye jamii na Serikali kaa ujumla”
Kadhalika, ameongeza kuwa Chuo hicho kimeweka mipango inayozingatia dira ya maendeleo ya Taifa ya 2050 na mwelekeo mpya wa Elimu Nchini Tanzania unaolenga kutoa Elimu Ujuzi, Stadi na Maarifa kwa ajili ya kuwajengea wahitimu uwezo na sifa za kujiajiri na
kuajirika katika soko shindani la ajira duniani.
Naye Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania Sheikh Dkt. Abubakar Zubeir bin in Ali ametoa wito kwa Waislam na Watanzania kwa ujumla kuweka mikakati ya kukisaidia chuo ili kiendelee kufanya vizuri na kutoa elimu kwa watanzania nchini.
“Waislam na watanzania tukisaidie chuo hichi, hakuna uislam bila ualimu, uislam ulipokuja ulipiga sana vita ujinga, tuwaunge mkono viongozi wetu kwa kukisaidia chuo hiki”
Makamu Mkuu wa Chuo hicho Prof Juma Assad amesema kuwa moja ya changamoto kubwa katika chuo hicho ni kukosekana kwa hosteli za wanafunzi wa kike “Namna tunavyoingeza udahili ndivyo tunavyoibua changamoto nyingine, tunataka watoto wetu wa kike wote wake ndani ya chuo”
MAJALIWA AAGIZA USIMAMIAJI NA UDHIBITI WA UBORA WA ELIMU
Written By CCMdijitali on Friday, June 20, 2025 | June 20, 2025
▪️Asema lengo ni kuendelea kutoa wahitimu wenye uwezo wa kukidhi vigezo vya kimataifa
▪️Rais Dkt. Samia atoa milioni 100 kuchangia maendeleo ya Chuo Kikuu cha Waislamu cha Morogoro
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa ameitaka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na TAMISEMI pamoja kusimamia na kudhibiti ubora wa elimu inayotolewa kuanzia elimu ya msingi mpaka elimu ya juu ili kuendelea kukidhi viwango vya kitaifa, kikanda na kimataifa.
Ametoa maagizo hayo leo (Ijumaa Juni 20, 2025) alipomwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye maadhimisho ya miaka 20 ya Chuo Kikuu cha Waislamu cha Morogoro (MUM), kwenye viwanja vya chuo hicho mkoani Morogoro.
“Mamlaka zetu ziendelee kusimamia hilo kwa kufanya hivyo sio tu kutaendelea kukuza ubora wa elimu yetu, bali pia kutawawezesha wasomi nchini kukidhi viwango na mahitaji ya soko la ajira”
Kadhalika, Mheshimiwa Majaliwa amezitaka Taasisi za Elimu nchini ziimarishe mahusiano na vyuo vyote nchini vinavyotoa maarifa kwa vijana wa kitanzania pamoja na kuzalisha wakufunzi ili kuwa sehemu ya mtandao wa utoaji maarifa na taalum hapa nchini.
Aidha, Mheshimiwa Majaliwa kuwa katika kuunga mkono jitihada za wadau mbalimbali katika kuchangia maendeleo ya chuo hicho kupitia mfumo maalum wa (MUM Community Fund), Rais Dkt. Samia ametoa kiasi cha Shilingi milioni 100 ili kiendelee kutoa huduma kwa watoto wa Kitanzania
Mheshimwa Waziri Mkuu ameongeza kuwa Serikali inaendelea na ujenzi wa Mfumo wa Takwimu wa Sekta ya Elimu utakaowezesha upatikanaji wa takwimu zote za sekta hiyo ambao utakuwa na uwezo wa kupokea takwimu mbalimbali zinazohusiana na elimu kutoka katika mifumo mingine ya Serikali ikiwemo NIDA, RITA na Wizara ya Mambo ya Nje.
Kwa Upande wake Naibu Waziri wa Elimu Qs Omar Kipanga amesema kuwa katika kipindi cha miaka 20, chuo hicho kimefanikiwa kuwa na progrma zaidi ya 32 kutoka program mbili wakati kinaanza na kimefanikiwa kutoa wahitimu zaidi ya 15,000.
“Wahitimu hawa wamekuwa wwamekuwa wa kupigiwa mfano katika kazi na maadili inayofanya waaminiwe katika nafasi mbalimbali kwenye jamii na Serikali kaa ujumla”
Kadhalika, ameongeza kuwa Chuo hicho kimeweka mipango inayozingatia dira ya maendeleo ya Taifa ya 2050 na mwelekeo mpya wa Elimu Nchini Tanzania unaolenga kutoa Elimu Ujuzi, Stadi na Maarifa kwa ajili ya kuwajengea wahitimu uwezo na sifa za kujiajiri na
kuajirika katika soko shindani la ajira duniani.
Naye Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania Sheikh Dkt. Abubakar Zubeir bin in Ali ametoa wito kwa Waislam na Watanzania kwa ujumla kuweka mikakati ya kukisaidia chuo ili kiendelee kufanya vizuri na kutoa elimu kwa watanzania nchini.
“Waislam na watanzania tukisaidie chuo hichi, hakuna uislam bila ualimu, uislam ulipokuja ulipiga sana vita ujinga, tuwaunge mkono viongozi wetu kwa kukisaidia chuo hiki”
Makamu Mkuu wa Chuo hicho Prof Juma Assad amesema kuwa moja ya changamoto kubwa katika chuo hicho ni kukosekana kwa hosteli za wanafunzi wa kike “Namna tunavyoingeza udahili ndivyo tunavyoibua changamoto nyingine, tunataka watoto wetu wa kike wote wake ndani ya chuo”

Labels:
KITAIFA
June 20, 2025

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amesema Ubia wa Maendeleo baina ya Afrika na Italia kupitia mpango wa Mattei (Mattei Plan) na Mpango wa Ulaya (Global Gateway) utasaidia katika kuendeleza miundombinu, rasilimali watu, kilimo na maendeleo ya kidijitali barani Afrika.
Makamu wa Rais amesema hayo mara baada ya kushiriki Mkutano wa Ubia wa Maendeleo kati ya Bara la Afrika na Serikali ya Italia (Mattei Plan) pamoja na Mpango wa Ulaya (Global Gateway) unaofanyika katika Viwanja vya Villa Doria Pamphilj Jijini Roma nchini Italia akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Amesema mkutano huo umejadili zaidi vipaumbele vya nchi za Afrika na kudhamiria kutekeleza miradi kwa vitendo. Ameongeza kwamba majadiliano katika uongezaji thamani ya mazao hususani zao la kahawa yamelenga kuhakikisha Afrika inapata manufaa zaidi kutokana na kilimo hicho pamoja na kuongeza ajira kupitia zao hilo.
Makamu wa Rais amesema Tanzania ikiwa ni nchi ya nne barani Afrika kwa uuzaji wa kahawa nje ya bara hilo itanufaika zaidi na mpango wa uongezaji thamani wa zao hilo.
Pia amesema mkutano huo umejadili uwekezaji unaohitajika katika rasilimali watu ili kutengeneza mazingira mazuri zaidi kwa wananchi wa Afrika na kuwaepusha kukimbia nchi zao kuelekea mataifa ya Ulaya.
Makamu wa Rais amesema Mpango wa Mattei unabadili utoaji wa misaada ya maendeleo na kuleta mfumo mpya wa uwekezaji wa pamoja katika sekta za kimkakati ambao utatengeneza ajira na kuchochea mageuzi kwa maendeleo endelevu.
Katika Mkutano huo masuala yaliyopewa kipaumbele ni pamoja na uongezaji thamani katika zao la kahawa, nishati endelevu, uboreshaji miundombinu ikiwemo ushoroba wa Lobito pamoja na maendeleo ya kidijitali kama vile matumizi ya akili mnemba katika kukuza uchumi. Tanzania ni moja kati ya Mataifa 14 barani Afrika ambayo yanapewa kipaumbele na Italia kupitia mpango mpya wa kimkakati wa Mattei (Mattei Plan). Miradi ya kipaumbele katika Mpango huo ni pamoja na nishati, elimu na kilimo ambapo euro bilioni 5.5 zimetengwa kwaajili ya utekelezaji wa awamu ya kwanza ya miradi hiyo.
Mpango wa Umoja wa Ulaya (EU Global Gateway) ni wa kuboresha miundombinu katika sekta za kidijitali, nishati, usafirishaji, afya, elimu, na utafiti. Mpango huu unalenga uwekezaji wa Euro bilioni 300 ifikapo mwaka 2027, ambapo Euro bilioni 150 zimeelekezwa barani Afrika.
Umoja wa Ulaya wamedhamiria upanuzi wa mradi wa mawasiliano wa kidijiti (blue raman – submarine cable) unaopita chini ya bahari ambao unaunganisha Ulaya na India ili ufike nchini Tanzania na hivyo kuiunga Afrika Mashariki katika mradi huo.
Mkutano huo umeshirikisha Viongozi mbalimbali wa Afrika, Umoja wa Ulaya pamoja na Taasisi za Fedha za Kimataifa ikiwemo Benki ya Dunia, Shirika la Fedha Duniani (IMF) na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB).
Taasisi za fedha za kimataifa, Umoja wa Ulaya pamoja na Serikali ya Italia zimeahidi kutoa fedha kwaajili ya kugharamia miradi mbalimbali itakayotekelezwa katika Mpango huo.
Imetolewa na
Ofisi ya Makamu wa Rais
20 Juni 2025
Roma - Italia





MAKAMU WA RAIS DKT PHILIP MPANGO ASHIRIKI MKUTANO WA UBIA WA MAENDELEO NCHINI ITALIA

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amesema Ubia wa Maendeleo baina ya Afrika na Italia kupitia mpango wa Mattei (Mattei Plan) na Mpango wa Ulaya (Global Gateway) utasaidia katika kuendeleza miundombinu, rasilimali watu, kilimo na maendeleo ya kidijitali barani Afrika.
Makamu wa Rais amesema hayo mara baada ya kushiriki Mkutano wa Ubia wa Maendeleo kati ya Bara la Afrika na Serikali ya Italia (Mattei Plan) pamoja na Mpango wa Ulaya (Global Gateway) unaofanyika katika Viwanja vya Villa Doria Pamphilj Jijini Roma nchini Italia akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Amesema mkutano huo umejadili zaidi vipaumbele vya nchi za Afrika na kudhamiria kutekeleza miradi kwa vitendo. Ameongeza kwamba majadiliano katika uongezaji thamani ya mazao hususani zao la kahawa yamelenga kuhakikisha Afrika inapata manufaa zaidi kutokana na kilimo hicho pamoja na kuongeza ajira kupitia zao hilo.
Makamu wa Rais amesema Tanzania ikiwa ni nchi ya nne barani Afrika kwa uuzaji wa kahawa nje ya bara hilo itanufaika zaidi na mpango wa uongezaji thamani wa zao hilo.
Pia amesema mkutano huo umejadili uwekezaji unaohitajika katika rasilimali watu ili kutengeneza mazingira mazuri zaidi kwa wananchi wa Afrika na kuwaepusha kukimbia nchi zao kuelekea mataifa ya Ulaya.
Makamu wa Rais amesema Mpango wa Mattei unabadili utoaji wa misaada ya maendeleo na kuleta mfumo mpya wa uwekezaji wa pamoja katika sekta za kimkakati ambao utatengeneza ajira na kuchochea mageuzi kwa maendeleo endelevu.
Katika Mkutano huo masuala yaliyopewa kipaumbele ni pamoja na uongezaji thamani katika zao la kahawa, nishati endelevu, uboreshaji miundombinu ikiwemo ushoroba wa Lobito pamoja na maendeleo ya kidijitali kama vile matumizi ya akili mnemba katika kukuza uchumi. Tanzania ni moja kati ya Mataifa 14 barani Afrika ambayo yanapewa kipaumbele na Italia kupitia mpango mpya wa kimkakati wa Mattei (Mattei Plan). Miradi ya kipaumbele katika Mpango huo ni pamoja na nishati, elimu na kilimo ambapo euro bilioni 5.5 zimetengwa kwaajili ya utekelezaji wa awamu ya kwanza ya miradi hiyo.
Mpango wa Umoja wa Ulaya (EU Global Gateway) ni wa kuboresha miundombinu katika sekta za kidijitali, nishati, usafirishaji, afya, elimu, na utafiti. Mpango huu unalenga uwekezaji wa Euro bilioni 300 ifikapo mwaka 2027, ambapo Euro bilioni 150 zimeelekezwa barani Afrika.
Umoja wa Ulaya wamedhamiria upanuzi wa mradi wa mawasiliano wa kidijiti (blue raman – submarine cable) unaopita chini ya bahari ambao unaunganisha Ulaya na India ili ufike nchini Tanzania na hivyo kuiunga Afrika Mashariki katika mradi huo.
Mkutano huo umeshirikisha Viongozi mbalimbali wa Afrika, Umoja wa Ulaya pamoja na Taasisi za Fedha za Kimataifa ikiwemo Benki ya Dunia, Shirika la Fedha Duniani (IMF) na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB).
Taasisi za fedha za kimataifa, Umoja wa Ulaya pamoja na Serikali ya Italia zimeahidi kutoa fedha kwaajili ya kugharamia miradi mbalimbali itakayotekelezwa katika Mpango huo.
Imetolewa na
Ofisi ya Makamu wa Rais
20 Juni 2025
Roma - Italia






Labels:
KIMATAIFA
June 18, 2025
Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla amewataka wanachama wa CCM kuzidisha mshikamano ndani ya chama kwa kipindi chote cha maandalizi ya uchaguzi hadi utakapomalizia mwezi Oktoba.
Ameyasema hayo alipokutana na Viongozi wa Halmashauri Kuu ya Wilaya, Kamati za Siasa za Jimbo na wadi ikiwa ni muendelezo wa ziara yake ya kuimarisha chama ndani ya Wilaya ya Kaskazini "A", Mkoa wa kazkazini ungaja katika Tawi la CCM Chaani.
Amesema ili kuwa na nguvu kubwa ya ushindi katika uchaguzi wa mwezi oktoba, ni lazima wanachama kuwa na umoja na kuzungumza sauti moja ya kukisemea chama vizuri kwa wananchi jambo litakalorahisisha ushindi wa chama hicho.
Mhe. Hemed amesema katika kuelekea kwenye viakao vya uteuzi wa wagombea ni vyema viongozi na wajumbe wa kamati kufanya maamuzi kwa kufuata katiba ya chama inavyoelekeza ili kuweza kupata wagombea watakaweza kuwatetea wananchi majimboni mwao.
Amesema uaminifu, uadilifu, kuacha utashi binafsi, visasi na chuki ni jambo pekee litakalopelekea kupata wagombea wenye sifa na uwezo wa kukiletea ushindi wa kishindo chama cha mapinduzi.
Amewaasa viongozi wa CCM kutokubali kutumiwa vibaya kwa kukununuliwa ama kupokea rushwa katika kipindi chote cha harakati za uchaguzi Mkuu ili kiendelea kulinda heshima na hadhi zao pamoja na chama chao.
Mhe.Hemed amewataka wanachama wa CCM kufanya kazi kwa umoja na mshikamano katika kukijenga na kukiimarisha chama cha Mapinduzi hasa kipindi hiki muhimu cha kukipambia chama kiweze kushinda katika uchaguzi wa mwezi oktoba na kuebelea kushikilia dola.
Amesisitiza kuwa kila mwanachama wa CCM ana haki ya kugombea akiwa na sifa zinazokubalika hivyo hakuna haja ya kutishana, kubezana na kudharauliana badala yake watiane mioyo na kusaidiana.
Amewahamasisha wanawake na vijana kujitokeza kwa wingi katika kitumia haki yao ya kikatiba kwa kugombea nafasi mbali mbali ili waweze kukitumikia chama chao na Taifa kwa ujumla.
Kwa upande wake Katibu wa Idara ya Siasa, Itikadi, Uwenezi na Mafunzo ya chama ndugu Khamis Mbeto amesema Bajeti ya Serikali ya mwaka 2025/2026 iliyosomwa jana Baraza la Wawakilishi inaenda kumaliza changamoto ndogo ndogo zilizobakia na kuendeleza utekelezaji wa miradi ya kimkati kwa lengo la kuwaletea wananchi maendeleo.
Mbeto amesema Rais Dkt Samia Suluhu na Rais Dkt Hussein Mwinyi hawana deni kwa wananchi kwani kupitia uongozi wao kero na changamoto nyingi za wananchi zimetatulia hivyo amewataka wana CCM kuendelea kuwaunga mkono viongozi hao ili wawndelee kuwatumikia Watanzania.
Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa kazi za Chama cha Mapinduzi kwa kipindi cha Januari hadi Mei, Katibu wa CCM Wilaya ya Kaskazini "A" ndugu Aboud Said Mpate amesema wamejipanga Kimikakati kukiletea ushindi chama chao katika uchaguzi Mkuu kwa kushinda kwenye Majimbo yote yaliyomo ndani ya Mkoa huo.
Mpate amesema Wilaya ya Kaskazini "A" haina shaka na kazi itakayofanywa na kamati ya uteuzi wa wagombea na kusema kuwa wanaamini watapatikana wagombea wenye sifa ya kukitumikia chama kwa uzalendo na kutatua kero na changamoto za wazanzibari.
MAKAMU WA PILI WA RAIS ZANZIBAR AFANYA ZIARA YA KICHAMA - KASKAZINI UNGUJA
Written By CCMdijitali on Wednesday, June 18, 2025 | June 18, 2025
Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla amewataka wanachama wa CCM kuzidisha mshikamano ndani ya chama kwa kipindi chote cha maandalizi ya uchaguzi hadi utakapomalizia mwezi Oktoba.
Ameyasema hayo alipokutana na Viongozi wa Halmashauri Kuu ya Wilaya, Kamati za Siasa za Jimbo na wadi ikiwa ni muendelezo wa ziara yake ya kuimarisha chama ndani ya Wilaya ya Kaskazini "A", Mkoa wa kazkazini ungaja katika Tawi la CCM Chaani.
Amesema ili kuwa na nguvu kubwa ya ushindi katika uchaguzi wa mwezi oktoba, ni lazima wanachama kuwa na umoja na kuzungumza sauti moja ya kukisemea chama vizuri kwa wananchi jambo litakalorahisisha ushindi wa chama hicho.
Mhe. Hemed amesema katika kuelekea kwenye viakao vya uteuzi wa wagombea ni vyema viongozi na wajumbe wa kamati kufanya maamuzi kwa kufuata katiba ya chama inavyoelekeza ili kuweza kupata wagombea watakaweza kuwatetea wananchi majimboni mwao.
Amesema uaminifu, uadilifu, kuacha utashi binafsi, visasi na chuki ni jambo pekee litakalopelekea kupata wagombea wenye sifa na uwezo wa kukiletea ushindi wa kishindo chama cha mapinduzi.
Amewaasa viongozi wa CCM kutokubali kutumiwa vibaya kwa kukununuliwa ama kupokea rushwa katika kipindi chote cha harakati za uchaguzi Mkuu ili kiendelea kulinda heshima na hadhi zao pamoja na chama chao.
Mhe.Hemed amewataka wanachama wa CCM kufanya kazi kwa umoja na mshikamano katika kukijenga na kukiimarisha chama cha Mapinduzi hasa kipindi hiki muhimu cha kukipambia chama kiweze kushinda katika uchaguzi wa mwezi oktoba na kuebelea kushikilia dola.
Amesisitiza kuwa kila mwanachama wa CCM ana haki ya kugombea akiwa na sifa zinazokubalika hivyo hakuna haja ya kutishana, kubezana na kudharauliana badala yake watiane mioyo na kusaidiana.
Amewahamasisha wanawake na vijana kujitokeza kwa wingi katika kitumia haki yao ya kikatiba kwa kugombea nafasi mbali mbali ili waweze kukitumikia chama chao na Taifa kwa ujumla.
Kwa upande wake Katibu wa Idara ya Siasa, Itikadi, Uwenezi na Mafunzo ya chama ndugu Khamis Mbeto amesema Bajeti ya Serikali ya mwaka 2025/2026 iliyosomwa jana Baraza la Wawakilishi inaenda kumaliza changamoto ndogo ndogo zilizobakia na kuendeleza utekelezaji wa miradi ya kimkati kwa lengo la kuwaletea wananchi maendeleo.
Mbeto amesema Rais Dkt Samia Suluhu na Rais Dkt Hussein Mwinyi hawana deni kwa wananchi kwani kupitia uongozi wao kero na changamoto nyingi za wananchi zimetatulia hivyo amewataka wana CCM kuendelea kuwaunga mkono viongozi hao ili wawndelee kuwatumikia Watanzania.
Akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa kazi za Chama cha Mapinduzi kwa kipindi cha Januari hadi Mei, Katibu wa CCM Wilaya ya Kaskazini "A" ndugu Aboud Said Mpate amesema wamejipanga Kimikakati kukiletea ushindi chama chao katika uchaguzi Mkuu kwa kushinda kwenye Majimbo yote yaliyomo ndani ya Mkoa huo.
Mpate amesema Wilaya ya Kaskazini "A" haina shaka na kazi itakayofanywa na kamati ya uteuzi wa wagombea na kusema kuwa wanaamini watapatikana wagombea wenye sifa ya kukitumikia chama kwa uzalendo na kutatua kero na changamoto za wazanzibari.
Imetolewa na Kitengo cha Habari(OMPR)
Tarehe 13.06.2025
June 18, 2025
Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa na Mhe. Hemed Suleiman Abdulla amewataka viongozi wa CCM kutokubali kutumika vibaya kwa kununuliwa na kupokea rushwa hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi Mkuu.
Ameyasema hayo alipokutana na Viongozi wa Halmashauri Kuu ya Wilaya, Kamati za Siasa za Jimbo na wadi ikiwa ni muendelezo wa ziara yake ya kuimarisha chama ndani ya Wilaya ya Kaskazini "B", Mkoa wa kaskazini ungaja katika Tawi la CCM Mahonda.
Amesema ni vyema kwa viongozi kuwa wazalendo kwa kuweka mbele maslahi ya chama na kuwa tayari kujitoa kwa hali na mali katika kukitumikia chama cha Mapinduzi.
Mhe. Hemed amesema kwa kipindi chote cha kuelekea uchaguzi Mkuu viongozi na wanchama wa CCM wanatakiwa kuwa wavumilivu na wastahmilivu na kuachana na mambo yote yanayokitia dosari chama ili kuwa mfano bora wa kuigwa na vyama vyengine.
Amesisitiza uminifu, uadilifu na kuacha utashi binafsi kwa viongozi na wajumbe watakaofanya kazi ya uteuzi wa wagombea jambo litakalopelekea kupata wagombea wenye sifa na uwezo wa kuwatetea majimboni mwao pamoja na kukiletea ushindi wa kishindo chama cha mapinduzi.
Mhe.Hemed amewataka wanachama wa CCM kufanya kazi kwa umoja na mshikamano katika kukijenga na kukiimarisha chama cha Mapinduzi hasa kipindi hiki muhimu cha kukipambia chama kiweze kushinda katika uchaguzi wa mwezi oktoba na kuebelea kushikilia dola.
Amesema cha Mapinduzi ni Chama cha wana CCM wote hivyo kila mmoja ana haki ya kugombea akiwa na sifa zinazokubalika ndani ya chama na kwa jamii iliyomzunguka.
Amewahamasisha wanawake na vijana kujitokeza kwa wingi katika kitumia haki yao ya kikatiba kwa kugombea nafasi mbali mbali ili waweze kukitumikia chama chao.
Katibu wa Idara ya Siasa, Itikadi, Uwenezi na Mafunzo ya chama ndugu Khamis Mbeto khamis amesema maendeleo makubwa yamefanywa na Serikali ya Awamu ya nane ikowemo ujezi wa miradi mbali mbali ya maendeleo ambayo inaendelea kuwanufaisha wanachi wa Mkoa wa Kaskazini.
Mbeto amesema kuna kila sababu ya kuendelea kuwarejesha madarakani ifikapo Oktoba Rais Dkt Mwinyi na Rais Dkt samia ili waedelee kuiimarisha na kuijenga vyema Tanzania.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kaskazini "B" ndugu Ali Khamis Ali amesema wakati utakapofika wa kupitisha wagombea kamati hazitakwenda kinyume na matakwa ya katiba ya chama na watafanya kazi kwa haki uwazi na hakuna mgombea atakae onewa kila mtu atapewa haki yake anayostahiki.
Katibu Ali amesema wanachama wa CCM wa Wilaya ya Kaskazini "B" wanaahidi ushindi wa kishindo katika uchaguzi mkuu na hawatopoteza jimbo hata moja ndani ya Mkoa huo.
Viongozi wa CCM waaswa kutokubali kutumika vibaya kwa kununuliwa na kupokea rushwa
Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa na Mhe. Hemed Suleiman Abdulla amewataka viongozi wa CCM kutokubali kutumika vibaya kwa kununuliwa na kupokea rushwa hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi Mkuu.
Ameyasema hayo alipokutana na Viongozi wa Halmashauri Kuu ya Wilaya, Kamati za Siasa za Jimbo na wadi ikiwa ni muendelezo wa ziara yake ya kuimarisha chama ndani ya Wilaya ya Kaskazini "B", Mkoa wa kaskazini ungaja katika Tawi la CCM Mahonda.
Amesema ni vyema kwa viongozi kuwa wazalendo kwa kuweka mbele maslahi ya chama na kuwa tayari kujitoa kwa hali na mali katika kukitumikia chama cha Mapinduzi.
Mhe. Hemed amesema kwa kipindi chote cha kuelekea uchaguzi Mkuu viongozi na wanchama wa CCM wanatakiwa kuwa wavumilivu na wastahmilivu na kuachana na mambo yote yanayokitia dosari chama ili kuwa mfano bora wa kuigwa na vyama vyengine.
Amesisitiza uminifu, uadilifu na kuacha utashi binafsi kwa viongozi na wajumbe watakaofanya kazi ya uteuzi wa wagombea jambo litakalopelekea kupata wagombea wenye sifa na uwezo wa kuwatetea majimboni mwao pamoja na kukiletea ushindi wa kishindo chama cha mapinduzi.
Mhe.Hemed amewataka wanachama wa CCM kufanya kazi kwa umoja na mshikamano katika kukijenga na kukiimarisha chama cha Mapinduzi hasa kipindi hiki muhimu cha kukipambia chama kiweze kushinda katika uchaguzi wa mwezi oktoba na kuebelea kushikilia dola.
Amesema cha Mapinduzi ni Chama cha wana CCM wote hivyo kila mmoja ana haki ya kugombea akiwa na sifa zinazokubalika ndani ya chama na kwa jamii iliyomzunguka.
Amewahamasisha wanawake na vijana kujitokeza kwa wingi katika kitumia haki yao ya kikatiba kwa kugombea nafasi mbali mbali ili waweze kukitumikia chama chao.
Katibu wa Idara ya Siasa, Itikadi, Uwenezi na Mafunzo ya chama ndugu Khamis Mbeto khamis amesema maendeleo makubwa yamefanywa na Serikali ya Awamu ya nane ikowemo ujezi wa miradi mbali mbali ya maendeleo ambayo inaendelea kuwanufaisha wanachi wa Mkoa wa Kaskazini.
Mbeto amesema kuna kila sababu ya kuendelea kuwarejesha madarakani ifikapo Oktoba Rais Dkt Mwinyi na Rais Dkt samia ili waedelee kuiimarisha na kuijenga vyema Tanzania.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kaskazini "B" ndugu Ali Khamis Ali amesema wakati utakapofika wa kupitisha wagombea kamati hazitakwenda kinyume na matakwa ya katiba ya chama na watafanya kazi kwa haki uwazi na hakuna mgombea atakae onewa kila mtu atapewa haki yake anayostahiki.
Katibu Ali amesema wanachama wa CCM wa Wilaya ya Kaskazini "B" wanaahidi ushindi wa kishindo katika uchaguzi mkuu na hawatopoteza jimbo hata moja ndani ya Mkoa huo.
Imetolewa na Kitengo cha Habari(OMPR)
Tarehe 14.06.2025
June 18, 2025
SIASA za kutakiana Heri kwenye majimbo zatawala katika Mkutano wa Chama cha Madaktari Arusha(M.A.T)
SIASA za kutakiana Heri kwenye majimbo zimetawala katika mkutano wa chama cha madaktari Arusha(M.A.T),ambapo Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda amemwomba waziri Mkuu Kasimu Majaliwa kumtakia kila la heri katika uchaguzi ujao.
Kauli hiyo ambayo ameitoa leo juni 18,2025 katika mkutano huo unaofanyika aicc Arusha,ni wazi kwamba Makonda ameingiza miguu yote kulinyakua jimbo hilo kutoka kwa mbunge wa Sasa Mrisho Gambo ambaye umaarufu wake umeendelea kuporomoka kutokana na mnyukano wa wawili hao unaoendelea.
Kadhalika Makonda amemtakia kila la heri waziri Mkuu Kasimu Majaliwa katika jimbo lake la Ruangwa huku akisisitiza kuwa isingekuwa uchaguzi alikuwa amepania jiji la Arusha kuwa kama dubai kutokana na mipango aliyokuwa nayo.
"Mhe. Waziri Mkuu katika mipango bora iliyopo ya kulifanya jiji la Arusha kuwa kitovu cha utalii na sasa katika usafiri wa anga kwa kipindi cha miaka mitano Arusha ingekuwa ni kitu kingine ni vile tu kuna uchaguzi na tumebakiza siku chache". Amesema Makonda.
"Nasema hivi ni uchaguzi tu naimani waziri Mkuu amenielewa na mimi nikutakie kila lenye kheri Ruangwa na mimi usiache kunitakia kheri ili baada ya uchaguzi utakapo malizika na tutakapo kutana tufurahie kwa pamoja kuwa tulitakiana kheri". Amesisitiza Makonda.
Naye naibu waziri wa Afya Dr Godwin Mollel alisema kuwa katika jimbo lake la SIHA amemaliza uchaguzi na kumtakia heri waziri Mkuu Majaliwa na kumuomba asiache kufika jimbo la Siha ili kuhakikisha kura zake zinaendelea kujaa.
"Mhe. Waziri Mkuu mimi ni kama M'bunge wa pili Ruangwa maana nimefika mara nyingi katika kuteleza majukumu katika sekta ya Afya nimejione kwamba umesha maliza na unasubilia kuongoza tena kwa miaka mitano na mimi pale Siha nimeshamaliza nasubilia kusheherekea na kuendelea kuchapa kazi". Amesema Mollel.
"Na kwa vile tunahitaji viongozi wanaochapa kazi na sio maneno nikutakie Mhe. Makonda kila la kheri pale ulipo panga kulitumikia taifa letu umefanya mengi katika uongozi wako kama Mkuu wa Mkoa na matunda yanaonekana". Ameongeza Mollel.
Kwa upande wake waziri Mkuu amewahamasisha wananchi kujitokeza kugombea nafasi yoyote ya uongozi kama haki yao ya msingi ya kila mwananchi.
Aliwataka wananchi kutafakari lugha za wagombea iwapo kama zinafaa kwa ushawishi .


Kauli hiyo ambayo ameitoa leo juni 18,2025 katika mkutano huo unaofanyika aicc Arusha,ni wazi kwamba Makonda ameingiza miguu yote kulinyakua jimbo hilo kutoka kwa mbunge wa Sasa Mrisho Gambo ambaye umaarufu wake umeendelea kuporomoka kutokana na mnyukano wa wawili hao unaoendelea.
Kadhalika Makonda amemtakia kila la heri waziri Mkuu Kasimu Majaliwa katika jimbo lake la Ruangwa huku akisisitiza kuwa isingekuwa uchaguzi alikuwa amepania jiji la Arusha kuwa kama dubai kutokana na mipango aliyokuwa nayo.
"Mhe. Waziri Mkuu katika mipango bora iliyopo ya kulifanya jiji la Arusha kuwa kitovu cha utalii na sasa katika usafiri wa anga kwa kipindi cha miaka mitano Arusha ingekuwa ni kitu kingine ni vile tu kuna uchaguzi na tumebakiza siku chache". Amesema Makonda.
"Nasema hivi ni uchaguzi tu naimani waziri Mkuu amenielewa na mimi nikutakie kila lenye kheri Ruangwa na mimi usiache kunitakia kheri ili baada ya uchaguzi utakapo malizika na tutakapo kutana tufurahie kwa pamoja kuwa tulitakiana kheri". Amesisitiza Makonda.
Naye naibu waziri wa Afya Dr Godwin Mollel alisema kuwa katika jimbo lake la SIHA amemaliza uchaguzi na kumtakia heri waziri Mkuu Majaliwa na kumuomba asiache kufika jimbo la Siha ili kuhakikisha kura zake zinaendelea kujaa.
"Mhe. Waziri Mkuu mimi ni kama M'bunge wa pili Ruangwa maana nimefika mara nyingi katika kuteleza majukumu katika sekta ya Afya nimejione kwamba umesha maliza na unasubilia kuongoza tena kwa miaka mitano na mimi pale Siha nimeshamaliza nasubilia kusheherekea na kuendelea kuchapa kazi". Amesema Mollel.
"Na kwa vile tunahitaji viongozi wanaochapa kazi na sio maneno nikutakie Mhe. Makonda kila la kheri pale ulipo panga kulitumikia taifa letu umefanya mengi katika uongozi wako kama Mkuu wa Mkoa na matunda yanaonekana". Ameongeza Mollel.
Kwa upande wake waziri Mkuu amewahamasisha wananchi kujitokeza kugombea nafasi yoyote ya uongozi kama haki yao ya msingi ya kila mwananchi.
Aliwataka wananchi kutafakari lugha za wagombea iwapo kama zinafaa kwa ushawishi .


Labels:
KITAIFA
June 18, 2025
Ametoa wito huo leo Jumatano (Juni 18, 2025) kwenye Kongamano la 13 la Kisayansi la Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) lililofanyika chuoni hapo kampasi ya Mloganzila, jijini Dar es Salaam.
“Tunataka kuona matokeo ya tafiti hizi yanatumika, msiweke tafiti hizi kwenye makabati tu, matokeo haya yanapaswa kuleta tija katika sekta ya afya, Ni matarajio yangu kuwa kongamano hili litatumika kutoa mapendekezo yatakayoimarisha mifumo, sera, na ushirikiano baina ya sekta ya umma na binafsi ili kuhakikisha Watanzania wananufaika kikamilifu na mapinduzi haya”
Kadhalika, Mheshimiwa Majaliwa amewataka wadau wa sekta binafsi na washirika wa maendeleo kuongeza uwekezaji katika vifaa tiba, na teknolojia mpya ili kuimarisha uwezo wa kukabiliana na magonjwa kwa wakati.
Amesema kuwa Serikali kwa upande wake itaendelea kuboresha sekta ya afya kwa kuwekeza zaidi katika miundombinu, rasilimali watu, tiba za kibingwa, na mifumo ya kukabiliana na milipuko ya magonjwa.
“Tutaendelea kushirikiana na wadau wote kuhakikisha kila Mtanzania anapata huduma bora, salama na rafiki bila kujali mahali alipo”.
Pia, Amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoomgozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inaendelea kuweka mazingira wezeshi ya kuvutia uwekezaji katika uzalishaji wa dawa, chanjo na vifaa tiba ndani ya nchi. “Tayari tumeanza kushuhudia hatua chanya katika maeneo haya, tukijivunia mchango wa wataalamu wetu wa ndani”.
“Serikali yetu imeendelea kuimarisha mazingira ya matumizi ya teknolojia katika sekta ya afya.
Leo hii, hospitali zetu zinatumia mifumo ya kidijitali kubaini magonjwa, kutoa tiba sahihi, na kufuatilia maendeleo ya wagonjwa.”
Akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Naibu Katibu Mkuu Sayansi, Teknolojia na Elimu ya Juu Prof. Daniel Mushi amesema kuwa Serikali imeweka vipaumbele kwenye elimu, sayasi na teknolojia.
“Tunajivunia mageuzi makubwa chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, uongozi wake umeleta mageuzi mapya katika kuimarisha taasisi za elimu nchini”.
Amesema kuwa maboresho yaliyopo chuoni hapo ni ushahidi mkubwa wa namna serikali inavyoweka mipango ya kuboresha mazingira ya Ujifunzaji na Kufundishia. Kwa upande wake, Makamu Mkuu wa Chuo hicho Profesa Appolinary Kamuhabwa
Ameipongeza Serikali kwa jitihada za dhati ambazo zimewezesha kuungwa mkono na wadau mbalimbali wa maendeleo na hivyo kufanikisha utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati inayoleta mageuzi makubwa katika mazingira ya elimu ya juu na afya nchini.
Prof. Appolinary amesema ujenzi wa Kituo cha Umahiri cha Magonjwa ya Moyo na Mishipa ya Damu cha Afrika Mashariki (yaani "East African Centre of Excellence for Cardiovascular Sciences") unaofadhiliwa na Serikali kupitia mkopo wa masharti nafuu wa Benki ya Maendeleo ya Afrika ni moja ya miradi itakayotekelezwa.
“Mradi huu unaingia katika awamu ya pili, baada ya kukamilisha awamu ya kwanza ya ujenzi wa kituo hiki muhimu hapa Mloganzila, Awamu ya kwanza iligharimu shilingi bilioni 21.62 na Awamu ya pili ya mradi huu ambayo imeanza rasmi mwezi Mei 2025, inalenga kujenga Hospitali ya Kisasa ya Kufundishia wataalamu bingwa na bobezi wa magonjwa ya Moyo na Mishipa ya damu”.
Alisema Prof. Appolinary Amesema kuwa Hospitali hiyo itakaongeza uwezo wa kutoa huduma za kibingwa, kufundisha wataalamu wa ndani na nje ya nchi, na kufanya tafiti zinazolenga kukabiliana na changamoto za magonjwa ya moyo na mishipa.
“Awamu hii itagharimu kiasi cha shilingi bilioni 221.57.”







FANYENI TAFITI ZENYE TIJA KWA WANANCHI-MAJALIWA
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa ametoa wito kwa watafiti na wapangaji wa Sera kuwekeza katika tafiti zenye tija kwa wananchi. Amesema kufanya hivyo, kutawezesha kuwa na matokeo ambayo yatatumika kutengeneza sera na mipango ya utekelezaji yenye kuleta mabadiliko halisi katika jamii.
- Ataka matokeo ya tafiti hizo yatumike badala ya kuyafungia
- Awataka wadau wa Sekta ya Afya kuongeza uwekezaji katika vifaa tiba na teknolojia mpya
Ametoa wito huo leo Jumatano (Juni 18, 2025) kwenye Kongamano la 13 la Kisayansi la Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) lililofanyika chuoni hapo kampasi ya Mloganzila, jijini Dar es Salaam.
“Tunataka kuona matokeo ya tafiti hizi yanatumika, msiweke tafiti hizi kwenye makabati tu, matokeo haya yanapaswa kuleta tija katika sekta ya afya, Ni matarajio yangu kuwa kongamano hili litatumika kutoa mapendekezo yatakayoimarisha mifumo, sera, na ushirikiano baina ya sekta ya umma na binafsi ili kuhakikisha Watanzania wananufaika kikamilifu na mapinduzi haya”
Kadhalika, Mheshimiwa Majaliwa amewataka wadau wa sekta binafsi na washirika wa maendeleo kuongeza uwekezaji katika vifaa tiba, na teknolojia mpya ili kuimarisha uwezo wa kukabiliana na magonjwa kwa wakati.
Amesema kuwa Serikali kwa upande wake itaendelea kuboresha sekta ya afya kwa kuwekeza zaidi katika miundombinu, rasilimali watu, tiba za kibingwa, na mifumo ya kukabiliana na milipuko ya magonjwa.
“Tutaendelea kushirikiana na wadau wote kuhakikisha kila Mtanzania anapata huduma bora, salama na rafiki bila kujali mahali alipo”.
Pia, Amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoomgozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inaendelea kuweka mazingira wezeshi ya kuvutia uwekezaji katika uzalishaji wa dawa, chanjo na vifaa tiba ndani ya nchi. “Tayari tumeanza kushuhudia hatua chanya katika maeneo haya, tukijivunia mchango wa wataalamu wetu wa ndani”.
“Serikali yetu imeendelea kuimarisha mazingira ya matumizi ya teknolojia katika sekta ya afya.
Leo hii, hospitali zetu zinatumia mifumo ya kidijitali kubaini magonjwa, kutoa tiba sahihi, na kufuatilia maendeleo ya wagonjwa.”
Akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Naibu Katibu Mkuu Sayansi, Teknolojia na Elimu ya Juu Prof. Daniel Mushi amesema kuwa Serikali imeweka vipaumbele kwenye elimu, sayasi na teknolojia.
“Tunajivunia mageuzi makubwa chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, uongozi wake umeleta mageuzi mapya katika kuimarisha taasisi za elimu nchini”.
Amesema kuwa maboresho yaliyopo chuoni hapo ni ushahidi mkubwa wa namna serikali inavyoweka mipango ya kuboresha mazingira ya Ujifunzaji na Kufundishia. Kwa upande wake, Makamu Mkuu wa Chuo hicho Profesa Appolinary Kamuhabwa
Ameipongeza Serikali kwa jitihada za dhati ambazo zimewezesha kuungwa mkono na wadau mbalimbali wa maendeleo na hivyo kufanikisha utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati inayoleta mageuzi makubwa katika mazingira ya elimu ya juu na afya nchini.
Prof. Appolinary amesema ujenzi wa Kituo cha Umahiri cha Magonjwa ya Moyo na Mishipa ya Damu cha Afrika Mashariki (yaani "East African Centre of Excellence for Cardiovascular Sciences") unaofadhiliwa na Serikali kupitia mkopo wa masharti nafuu wa Benki ya Maendeleo ya Afrika ni moja ya miradi itakayotekelezwa.
“Mradi huu unaingia katika awamu ya pili, baada ya kukamilisha awamu ya kwanza ya ujenzi wa kituo hiki muhimu hapa Mloganzila, Awamu ya kwanza iligharimu shilingi bilioni 21.62 na Awamu ya pili ya mradi huu ambayo imeanza rasmi mwezi Mei 2025, inalenga kujenga Hospitali ya Kisasa ya Kufundishia wataalamu bingwa na bobezi wa magonjwa ya Moyo na Mishipa ya damu”.
Alisema Prof. Appolinary Amesema kuwa Hospitali hiyo itakaongeza uwezo wa kutoa huduma za kibingwa, kufundisha wataalamu wa ndani na nje ya nchi, na kufanya tafiti zinazolenga kukabiliana na changamoto za magonjwa ya moyo na mishipa.
“Awamu hii itagharimu kiasi cha shilingi bilioni 221.57.”








Labels:
KITAIFA
June 18, 2025

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, Stephen Wasira amesema tangu kupata uhuru Tanzania imepata maendeleo makubwa na kwamba wanaosema hakuna kilichofanyika ni vema wakakaa kimya, wasiwe na tabia ya kasuku kukariri wasiyoyajua.
Wasira ameyasema hayo leo Juni 17, 2025 alipokuwa akizingumza katika mkutano wa hadhara Katoro, mkoani Geita akiwa katika ziara ya kukagua uhai wa Chama na kuzungumza na wananchi.
Akieleza kuhusu maendeleo yaliyofanyika nchini tangu kupatikana kwa uhuru alisema ni makubwa na wenye umri mkubwa wanajua vizuri nchi ilivyokuwa na wamekuwa wakishuhudia hatua mbalimbali zinazofanywa na serikali inayoundwa na CCM.
“Labda ninyi vijana hamwelewi lakini niwaambie wakoloni wa Kijerumani na wakoloni wa Kiingereza wamekaa Tanganyika miaka 75, Wajerumani wamekaa miaka 35, wamejenga reli kwa viboko bila malipo.
Waingereza wamekaa miaka 40 walitumwa na Umoja wa Mataifa (UN) watuendeleze tujitawalie, lakini miaka 40 ya Waingereza wametuacha na wahandisi wawili katika nchi isiyo na barabara.
“Wametuachia nchi hakuna daktari hata mmoja walikuwepo madaktari kutoka India na Pakistani nao walikuwa Dar es Salaam. Wakati tunapata uhuru akina mama walikuwa hawajifungui ila wanazaa maana hakukua na kliniki, hivyo walikuwa wanazaa kama ng’ombe anavyozaa ndama.
Ng’ombe umeona wapi ana kliniki (ya uzazi)? Hiyo ndio hali waliyotuacha nayo (wakoloni) wametuacha hatuna barabara.
“Leo anakuja mtu hajafikisha umri wa miaka 30 au miaka 40 anawaambia hakuna maendeleo. Wewe uliwahi kutembea kwa miguu, kuna maendeleo, hao wanaosema hakuna maendeleo ambayo yamefanyika akija muulizeni hivi kwako maendeleo ni kitu gani?.
Wasira amesema inawezakana wanaosema hakuna kilichofanyika anazungumza kama kasuku, maana kasuku huwa anakariri tu haelewi hata maana ya maneno anayosema na hao ndio wanasiasa wapya, sisi tumejitawala tulikuwa na msomi mmoja tu mwenye ‘Master’ (shahada ya uzamili) Julius Nyerere ndio alikuwa ameandaliwa na Wakoloni kwa miaka 75.
“Leo wala sio Tanganyika nilikuwa namuuliza Mkurugenzi wa Bukombe asubuhi anasema ana wahandisi 12, nikasema wewe ni tajiri kuliko Tanganyika ya mwaka 1970 maana kulikuwa na wahandisi wawili wewe unao 12. Namuuliza madaktari anasema wengi tu sisi hatukuwa na daktari.
“Hiyo ndio nchi tuliyorithi, leo unaweza kwenda mkoa wowote wa Tanzania kwa lami. Zamani wakati tunakabidhiwa nchi lami ilikuwa inatoka Dar es Salaam mpaka Morogoro kwa sababu kulikuwa na wazungu wanalima mkonge, ilikuwa inatoka Tanga mpaka Korogwe kwa sababu kulikuwa na wazungu wanalima mkonge.








KAENI KIMYA KAMA HAMJUI NCHI ILIKOTOKA - WASIRA

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, Stephen Wasira amesema tangu kupata uhuru Tanzania imepata maendeleo makubwa na kwamba wanaosema hakuna kilichofanyika ni vema wakakaa kimya, wasiwe na tabia ya kasuku kukariri wasiyoyajua.
Wasira ameyasema hayo leo Juni 17, 2025 alipokuwa akizingumza katika mkutano wa hadhara Katoro, mkoani Geita akiwa katika ziara ya kukagua uhai wa Chama na kuzungumza na wananchi.
Akieleza kuhusu maendeleo yaliyofanyika nchini tangu kupatikana kwa uhuru alisema ni makubwa na wenye umri mkubwa wanajua vizuri nchi ilivyokuwa na wamekuwa wakishuhudia hatua mbalimbali zinazofanywa na serikali inayoundwa na CCM.
“Labda ninyi vijana hamwelewi lakini niwaambie wakoloni wa Kijerumani na wakoloni wa Kiingereza wamekaa Tanganyika miaka 75, Wajerumani wamekaa miaka 35, wamejenga reli kwa viboko bila malipo.
Waingereza wamekaa miaka 40 walitumwa na Umoja wa Mataifa (UN) watuendeleze tujitawalie, lakini miaka 40 ya Waingereza wametuacha na wahandisi wawili katika nchi isiyo na barabara.
“Wametuachia nchi hakuna daktari hata mmoja walikuwepo madaktari kutoka India na Pakistani nao walikuwa Dar es Salaam. Wakati tunapata uhuru akina mama walikuwa hawajifungui ila wanazaa maana hakukua na kliniki, hivyo walikuwa wanazaa kama ng’ombe anavyozaa ndama.
Ng’ombe umeona wapi ana kliniki (ya uzazi)? Hiyo ndio hali waliyotuacha nayo (wakoloni) wametuacha hatuna barabara.
“Leo anakuja mtu hajafikisha umri wa miaka 30 au miaka 40 anawaambia hakuna maendeleo. Wewe uliwahi kutembea kwa miguu, kuna maendeleo, hao wanaosema hakuna maendeleo ambayo yamefanyika akija muulizeni hivi kwako maendeleo ni kitu gani?.
Wasira amesema inawezakana wanaosema hakuna kilichofanyika anazungumza kama kasuku, maana kasuku huwa anakariri tu haelewi hata maana ya maneno anayosema na hao ndio wanasiasa wapya, sisi tumejitawala tulikuwa na msomi mmoja tu mwenye ‘Master’ (shahada ya uzamili) Julius Nyerere ndio alikuwa ameandaliwa na Wakoloni kwa miaka 75.
“Leo wala sio Tanganyika nilikuwa namuuliza Mkurugenzi wa Bukombe asubuhi anasema ana wahandisi 12, nikasema wewe ni tajiri kuliko Tanganyika ya mwaka 1970 maana kulikuwa na wahandisi wawili wewe unao 12. Namuuliza madaktari anasema wengi tu sisi hatukuwa na daktari.
“Hiyo ndio nchi tuliyorithi, leo unaweza kwenda mkoa wowote wa Tanzania kwa lami. Zamani wakati tunakabidhiwa nchi lami ilikuwa inatoka Dar es Salaam mpaka Morogoro kwa sababu kulikuwa na wazungu wanalima mkonge, ilikuwa inatoka Tanga mpaka Korogwe kwa sababu kulikuwa na wazungu wanalima mkonge.









Labels:
KITAIFA