CPA MAKALLA: CCM ITAWALETEA WAGOMBEA WASIO NA MAKANDOKANDO

  Na Richard Mwaikenda, Mwanza   Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), CPA Amos Makalla akiwaahidi wananchi kwa...

Latest Post

CPA MAKALLA: CCM ITAWALETEA WAGOMBEA WASIO NA MAKANDOKANDO

Written By CCMdijitali on Tuesday, August 20, 2024 | August 20, 2024





 Na Richard Mwaikenda, Mwanza 

 Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), CPA Amos Makalla akiwaahidi wananchi kwamba ikifika wakati wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Novemba 27, mwaka huu na Uchaguzi Mkuu wa mwakani CCM itawapelekea wagombea wenye sifa, wasio na makandokando wenye malengo ya kuwaletea maendeleo.

 "Niseme, nisiseme, Niseme nisisemee? Mimi ndiye Katibu Mwenezi wa CCM, nataka niwahakikishie CCM itawaletea wagombea safi, wasio na makandokando ambao wako tayari kuwaletea wananchi maendeleo. Mko tayari, mko tayari?" Makalla aliwahakikishia wananchi hivyo kisha kuwahoji kama watakuwa tayari kuwapigia. 

 Ametoa ahadi hiyo alipokuwa akihutubia katika mkutano wa hadhara kwenye Uwanja wa Furahisha jijini Mwanza Agosti 15, 2024 ambao pia ulihutubiwa na Katibu Mkuu wa chama hicho, Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi. 

 Dk Nchimbi alihitimisha ziara hiyo yenye mafanikio makubwa aliyoifanya katika mikoa minne ya Kigoma, Kagera, Geita na Mwanza. 

Tangu ashike wadhifa huo, ameshafanya ziara katika mikoa mingine 13 ambayo ni; Katavi, Rukwa, Songwe, Mbeya, Njombe, Ruvuma, Singida, Manyara, Arusha, Kilimanjaro, Tanga, Lindi na Mtwara.


 Katibu Mkuu wa CCM huyo, katika ziara yake hiyo aliyoanzia Mkoa wa Kigoma Agosti 4, 2024, aliambatana na Wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Ndugu Issa Haji Usi Gavu, Katibu wa NEC - Oganaizesheni, Ndugu Amos Gabriel Makalla, Katibu wa NEC - Itikadi, Uenezi na Mafunzo na Ndugu Rabia Hamid Abdalla, Katibu wa NEC - Siasa na Uhusiano wa Kimataifa. 


 Malengo ya ziara hiyo ni; Kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka ‪2020-2025‬, kuhuisha uhai wa chama, kusikiliza na kutatua kero za wananchi pamoja na kuhamasisha wananchi kujitokeza kuhakiki taarifa zao na kujiandikisha katika Kitabu cha Kudumu cha Wapiga kura, kwa ajili ya maandalizi ya Uchaguzi wa serikali za mitaa Novemba mwaka huu.

MJUMBE WA KAMATI KUU YA CCM TAIFA APOKEA APOKEA TARIFA YA CHAMA NA SERIKALI MKOANI TANGA

Written By CCMdijitali on Friday, August 16, 2024 | August 16, 2024

Published from Blogger Prime Android App


Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa ambae pia ni Mlezi wa Mkoa wa Tanga Ndugu HEMED SULEIMAN ABDULLA amewataka wana CCM wa Mkoa wa Tanga kuhakikisha Chama cha Mapinduzi kinashinda kwa kishindo katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa inaotarajiwa kufanyika mwenzi November 2024.

 

Ameyasema hayo wakati akipokea tarifa ya Chama na Serikali mara baada ya kuwasili Mkoani humo katika Ukumbi wa Ofisi ya CCM Mkoa wa Tanga Mhe. Hemed amesema ushindi kwa Chama cha Mapinduzi katika uchaguzi wa Serikali za mitaa na Uchaguzi mkuu ujao  ni lazima kuanzia ngazi ya Mitaa ,Vijiji hadi Vitongoji kwa pande zote mbili za Jamuhuri Ya Muungano wa Tanzania.

 

Mjumbe huyo ambae pia ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Amesema akiwa Mlezi wa Mkoa wa Tanga atahakikisha kuwa  ndani ya Mkoa huo CCM inashinda nafasi zote za uongozi zitakazogombaniwa kama  ibara ya Tano ( 5)  ya katiba ya ccm inavyosema kuwa ushindi lazima.

 

 Sambamba na hayo malezi wa chama hicho Mkoa wa Tanga amewataka viongozi wa CCM kuhakikisha wanadumisha umoja, mshikamano na Upendo uliopo baina yao katika kukitumikia chama na Serikali ili kuhakikisha wanawasaidia viongozi wakuu wanchi kuwaletea maendeleo wananchi wake wakiwemo wana CCM.

 

Nae Mkuu wa Mkoa wa Tanga Dkt. BATILDA BURIAN amesema Mkoa wa Tanga unaendelea kuitekeleza vyema  Ilani ya CCM kwa kuekeza katika Miradi mbali mbali ya maendeleo ikiwemo miradi ya maji safi na salama ambapo changamoto ya uhaba wa upatikanaji wa maji ndani ya Tanga imeondoka  pamoja na zoezi la kusambaza nishati ya umeme atika vijiji vyote 779 limekamilika na kwa sasa wanajipanga kuvifikia vitongoji vyote ndani ya mkoa wa Tanga ili ifikapo 2025 kazi hio imekamilika kwa mafanikio.

 

Dkt. BATILDA amesema Sekta ya Elimu katika Mkoa wa Tanga imezidi kuimarika kuanzi shule za msingi hadi sekondari , ujenzi wa nyumba za walimu na mabweni ya wanafunzi pamoja ujenzi wa vyuo vya Veta unaendelea  katika Wilaya zote za Tanga sambamba na kuongezeka kwa ukusanyaji wa mapato katika Mkoa huo.

 

Mapema akisoma taarifa ya Chama Katibu wa CCM Mkoa wa Tanga Ndugu SULEIMAN SANKWA amesema CCM Mkoa wa Tanga imejipanga kusajili wanachama wapya zaidi ya laki moja hadi ifikapo Disemba 2024 ambapo zoezi hilo linaendelea vizuri.

 

SANKWA amesema Mkoa wa Tanga umedhamiria kushinda kwa kishindo katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa na uchaguzi Mkuu ujao wa mwaka 2025 na kumuhakikishia Mlezi wao kuwa Tanga itaendelea kufanya vizuri katika nyanja ya Siasa na Uchumi.

Published from Blogger Prime Android App

Published from Blogger Prime Android App

Published from Blogger Prime Android App

Published from Blogger Prime Android App

Published from Blogger Prime Android App

Published from Blogger Prime Android App

Published from Blogger Prime Android App

Published from Blogger Prime Android App

 Published from Blogger Prime Android App

Imetolewa na kitengo cha Habari ( OMPR)

LEO tarehe 16.08.2024

TANZANIA YASHIRIKI MKUTANO WA MAWAZIRI WA OACPS

Written By CCMdijitali on Friday, August 9, 2024 | August 09, 2024



Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayesimamia masuala ya Afrika Mashariki Balozi Stephen Mbundi, akichangia mjadala kwenye Mkutano wa Mawaziri wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Nchi za Afrika, Caribbean, na Pacific (OACPS) uliofanyika kwa njia ya mtandao tarehe 9 Agosti 2024

Mkutano wa Mawaziri wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Nchi za Afrika, Caribbean, na Pacific (OACPS) umefanyika leo tarehe 9 Agosti 2024, kwa njia ya mtandao, ukiwashirikisha mawaziri kutoka nchi 79 wanachama wa Jumuiya hiyo.

 

Tanzania iliwakilishwa na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, anayesimamia masuala ya Afrika Mashariki Balozi Stephen Mbundi, akimwakilisha Waziri wa Mambo ya Nje na Ushikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Mahmoud Thabit Kombo (Mb.).

 

Mkutano huo, ulioongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Angola, Mhe. TÉTE António, uliangazia masuala muhimu yanayohusu maendeleo ya Jumuiya, ikiwa ni pamoja na taarifa ya utekelezaji wa maamuzi ya mikutano iliyopita, maendeleo ya programu na miradi mbalimbali, hali ya kifedha ya Jumuiya, na maandalizi ya mkutano ujao wa Kilele wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa OACPS.

 

Katika hotuba ya ufunguzi, Mhe. António alisisitiza umuhimu wa mkutano huo katika kutatua changamoto mbalimbali, hususan za kifedha na kiutendaji, ili kuimarisha ufanisi wa Jumuiya.

 

Balozi Mbundi, akichangia katika mjadala, alisisitiza umuhimu wa matumizi bora ya rasilimali fedha na kuhimiza Sekretariati ya OACPS kuzingatia miongozo ya matumizi sahihi ya fedha ili kukabiliana na changamoto ya ufinyu wa bajeti. Pia aliungana na wajumbe wengine kuhimiza nchi wanachama kumalizia michango yao kwa Sekretariati na kupunguza matumizi yasiyo ya maendeleo kama njia ya kukabiliana na upungufu wa fedha.
 

Balozi Mbundi alieleza kuwa hatua hizo zitasaidia kuimarisha imani ya nchi wanachama na wadau wa maendeleo ambao wanachangia kwenye bajeti ya miradi na programu mbalimbali za Jumuiya hiyo.

 

Katika mkutano huo, ujumbe wa Tanzania ulijumuisha wawakilishi kutoka Wizara ya Fedha na Ofisi ya Makamu wa Rais, ukiongozwa na Balozi Stephen Mbundi.




Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na America (DEA) katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Swaiba Mndeme akifuatilia Mkutano OACPS uliokuwa ukiendelea kwa njia ya mtandao.







 

WAZIRI KOMBO APOKEA NAKALA ZA HATI ZA UTAMBULISHO KUTOKA KWA MABALOZI WATEULE WA ZIMBABWE, ITALIA NA RWANDA NCHINI

Written By CCMdijitali on Thursday, August 8, 2024 | August 08, 2024


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thatib Kombo (Mb.) akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Italia nchini, Mhe. Giuseppe Sean Coppola (Kushoto). Mapokezi hayo yamefanyika katika Ofisi Ndogo za Wizara jijini Dar es Salaaam tarehe 6 Agosti, 2024.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thatib Kombo (Mb.) amepokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Zimbabwe nchini, Mhe. Helen Bawange Ndingani, Balozi Mteule wa Italia nchini, Mhe. Giuseppe Sean Coppola na Balozi Mteule wa Rwanda nchini, Mhe. Jenerali Patrick Nyamvumba katika Ofisi Ndogo za Wizara jijini Dar es Salaaam tarehe 6 Agosti, 2024.

 

Akipokea nakala hizo Waziri Kombo amewapongeza mabalozi hao kwa uteuzi waliuopata na pia amewaahidi ushirikiano katika utekelezaji wa majukumu yao kwa kipindi watakachokuwa nchini kuziwakilisha nchi zao.

 

Aidha, ameeleza Mabalozi hao Wateule wanatarajiwa kuwasilisha Hati za Utambulisho kwa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 12 na 13 Agosti, 2024.

 

Akiongea na Balozi Mteule wa Zimbambwe nchini, Mhe. Ndingani, Waziri Kombo ameeleza kuwa Tanzania na Zimbabwe zimekuwa na ushirikiano wa kihistoria na kindugu ulioasisiwa na waasisi wa mataifa hayo mawili Hayati, Mwl. Julius Kambarage Nyerere wa Tanzania na Hayati, Robert Mugabe wa Zimbabwe.

 

Vilevile, akamkaribisha Mhe. Ndingani kutembelea Maktaba ya Hayati Mwl. Nyerere iliyopo Butiama, mkoani Mara ambayo imesheheni historia yake.

 

Balozi Kombo pia, akaeleza umuhimu wa kuwekeza na kurithisha historia ya ukombozi kwa vijana ili waweze kufahamu kwa kina namna waasisi hao walivyojitoa kupigania uhuru wa Bara la Afrika hususan harakati za ukombozi wa nchi za Kusini mwa Afrika.

 

Viongozi hao pia jadili juu ya umuhimu wa kufanyika kwa Mkutano wa Tume ya Pamoja ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Zimbabwe ambapo ameeleza kuwa Tanzania inatarajia kuwa mwenyeji wa mkutano huo. Tanzania na Zimbabwe zinashirikiana katika masuala ya biashara, uwekezaji, usafirishaji, usalama wa chakula, mabadiliko ya tabia nchi, elimu, Sanaa na utamaduni, na sekta nyingine za kisiasa.

 

Akizungumza na Balozi Mteule wa Italia nchini, Mhe. Coppola, Mhe. Waziri Kombo amesisitiza kuwa Tanzania ina nia ya dhati ya kuendeleza ushirikiano na nchi hiyo ili kuwezesha utekelezaji wa miradi ya kimkakati kupitia mpango wa ushirikiano wa Italia na Afrika unaofahamika kama “Mattei Plan”. Tanzania na Italia zinashirikiana katika sekta za utalii, elimu, Maji, biashara na uwekezaji, kilimo, mifugo na uvuvi, na kuongeza thamani ya mazao yatokanayo na ngozi ili kukuza biashara yake kimataifa.

 

Tanzania na Italia zinatarajia kuwa na Kongamano la biashara litakalofanyika jijini Dar es Salaam mwezi Desemba, 2024 kwa lengo la kukuza sekta ya biashara na za kiuchumi kwa maslahi mapana ya pande zote mbili amabapo, pembezoni mwa kongamano hilo kutafanyika mashauriano ya kisiasa.

 

Vilevile, katika mazungumzo yake na Balozi wa Rwanda, Mhe. Jenerali, Patrick Nyamvumba, Mhe. Waziri Kombo ameeleza kuwa Tanzania itaendelea kushirikiana na Rwanda kupitia ujirani wa nchi hizo mbili sambamba na kusimamia makubaliano mbalimbali yaliyokubaliwa katika nyakati tofauti na majukwaa mbalimbali ambayo nchi hizo mbili zimekubaliana kuyatekeleza.

 

Tanzania na Rwanda zinashirikiana katika sekta za mawasiliano, biashara na uwekezaji, usafirishaji, elimu, utamaduni na michezo, miundombinu, kilimo na mifugo.

 

Jukumu hili la kupokea Nakala za Hati za Utambulisho limefanywa na Mhe. Waziri Kombo kwa mara ya kwanza tangu aapishwe na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kushika nafasi ya Waziri wa Mambo ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thatib Kombo (Mb.) akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Zimbabwe nchini, Mhe. Helen Bawange Ndingani (Kushoto). Mapokezi hayo yamefanyika katika Ofisi Ndogo za Wizara jijini Dar es Salaaam tarehe 6 Agosti, 2024.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thatib Kombo (Mb.) amepokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Rwanda nchini, Mhe. Jenerali Patrick Nyamvumba (kushoto). Mapokezi hayo yamefanyka katika Ofisi Ndogo za Wizara jijini Dar es Salaaam tarehe 5 Agosti, 2024.

TANZANIA YASHIRIKI MKUTANO WA 44 WA WAKUU WA NCHI NA SERIKALI WA SADC HARARE



Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu Mwamba akiongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa 44 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini wa Afrika (SADC) ulioanza leo tarehe 8 Agosti, 2024 Harare, Zimbabwe. Kushoto ni Balozi wa Tanzania nchini nchini Zimbabwe, Mhe. IGP (RTD) Simon Sirro.

Tanzania inashiriki mkutano wa 44 wa Wakuu wa Nchi na Serikali ulioanza leo tarehe 8 Agosti, 2024 katika ngazi ya Makatibu Wakuu jijini Harare, Zimbabwe, ambapo moja ya agenda itakayojadiliwa ni suala la gharama za kujumuisha Kiswahili kuwa lugha rasmi ya SADC.

Itakumbukwa kuwa, katika Mkutano wa 39 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC uliofanyika nchini Tanzania mwezi Agosti 2024 uliitambua Kiswahili kuwa moja ya lugha rasmi za Jumuiya hiyo. Lugha nyingine zinazotumika ni, kiingereza, kifaransa na kireno.

 

Mkutano huo unatarajiwa kufanya uteuzi wa Mwenyekiti wa SADC ambapo, Mhe. Emmerson Dambudzo Mnangagwa, Rais wa Jamhuri ya Zimbabwe ambaye kwa sasa ni Makamu Mwenyekiti wa SADC atateuliwa kushika nafasi hiyo kwa kipindi cha 2024/2025. Nafasi ya Makamu Mwenyekiti itajulikana kupitia Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali utakaofanyika tarehe 17 Agosti, 2024.

 

Aidha, hafla ya ufunguzi wa mkutano huo imewezesha makabidhiano ya nafasi ya unyekekiti katika ngazi ya mkutano wa Makatibu Wakuu ambapo Mwenyekiti anayemaliza muda wake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Angola, Balozi Nazaré José Salvador amekabidhi nafasi hiyo kwa mwenyekiti mpya, Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Biashara ya Kimataifa wa Jamhuri ya Zimbambwe, Balozi Albert Ranganai Chimbindi akisisitiza kumpa ushirikiano katika nafasi hiyo.

 

Naye Balozi Chimbindi amemshukuru Mwenyekiti aliyemaliza muda wake kwa kutekeleza majukumu yake kikamilifu. Pia ameahidi kuzingatia ushauri aliokuwa akiutoa kwa Sekretariet ya SADC na kufanya kazi pamoja ili kuyafikia malengo ya jumuiya hiyo kwa maslahi  jumuishi.

 

“Tumepiga hatu lakini bado tuna kila sababu ya kuweka bidii kwenye ujenzi wa miundombinu, usafiri na hatimaye tuweze kuifikia SADC tunayoitaka. Niwahakikishie kuwa Zimbabwe ipo tayari kufanya kazi pamoja nanyi kwa kufuata malengo, kanuni na mikataba ya SADC'', Balozi Chimbindi.

 

Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali utafanyika tarehe 17 na 18 Agosti, 2024 na utatanguliwa na mikutano ya awali kwa ajili ya maandalizi ambayo ni: Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Asasi ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama ya SADC (SADC Organ on Politics, Defence and Security) utakaofanyika tarehe 16 Agosti 2018 ambao utapitia na kujadili hali ya siasa, ulinzi na usalama katika kanda kwa kipindi cha Agosti 2023 hadi Agosti 2024. Mkutano huu utahusisha nchi tatu za SADC Organ TROIKA na wajumbe wake ambao ni Angola (Mwenyekiti wa sasa wa Asasi ya SADC ya Ushirikiano wa Siasa, Ulinzi na Usalama), Zambia (Makamu Mwenyekiti wa Organ) na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (Mwenyekiti wa Organ aliyemaliza muda wa uenyekiti wa Asasi).

 Mikutano mingine ni: Mkutano wa Mawaziri utakaofanyika kuanzia tarehe 13 hadi 14 Agosti 2024 pamoja; na Mkutano wa Makatibu Wakuu wa Jumuiya ya Maendeleo ya kusini mwa Afrika utakaofanyika kuanzia tarehe 8 hadi 11 Agosti, 2024. 


Mkurugenzi Idara ya Ushirikikiano wa Kikanda kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Talha Waziri akifatilia hafla ya ufunguzi katika mkutano huo ulioanza leo tarehe 8 Agosti, 2024 Harare, Zimbambwe.


Kushoto ni Afisa Sheria Mkuu kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Bi. Felister Lero na Afisa Mkuu kutoka Wizara ya Fedha, Bw. Joseph Haule wakifatilia mkutano.



Picha ya pamoja: Makatibu Wakuu wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) baada ya ufunguzi wa Mkutano wa 44 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC uliofanyika tarehe 8 Agosti, 2024 Harare, Zimbabwe.

SMZ IMEDHAMIRIA KUSIMAMIA UBORA WA BIDHAA-DKT.MWINYI

Written By CCMdijitali on Tuesday, August 6, 2024 | August 06, 2024


Published from Blogger Prime Android App
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dkt.Hussein Ali Mwinyi  amesema katika utekelezaji wa ilani ya CCM  ya mwaka 2020 hadi 2025 , Serikali imedhamiria kusimamia ubora wa bidhaa kwa kuziweshesha taasisi zinazosimamia ubora ikiwemo Taasisi ya viwango Zanzibar (ZBS) kwa kuwa na maabara za kisasa na wataalamu wenye uwezo kwa kazi upimaji na ukaguzi. 

Dkt.Mwinyi aliyasema hayo leo tarehe 6 Agosti 2024, alipofungua kituo cha ukaguzi wa vyombo vya moto, Maruhubi Mkoa wa Mjini Magharibi.

Aidha Rais Dkt.Mwinyi amesema Serikali imeendelea kuchukua hatua ya kuimarisha miundombinu ya ZBS kwa kujenga kituo cha ukaguzi wa vyombo vya moto ambacho amekifungua.

Kwa upande mwingine Rais Dkt.Mwinyi ameeleza kuwa Serikali itaendelea kufanya juhudi na  kuchukua hatua za kuhakikisha wananchi wanakuwa salama kwa kujenga miundombinu imara kuwezesha  shughuli za kusimamia ubora ziwe za kisasa kwa kuwapatia majengo ya maabara , vifaa vya kisasa na wataalamu.

Published from Blogger Prime Android App

Published from Blogger Prime Android App

Published from Blogger Prime Android App

Published from Blogger Prime Android App

Published from Blogger Prime Android App
Published from Blogger Prime Android App
Published from Blogger Prime Android App

Published from Blogger Prime Android App

WAZIRI KOMBO APOKEA NAKALA ZA HATI ZA UTAMBULISHO KUTOKA KWA MABALOZI WATEULE WA ZIMBABWE, ITALIA NA RWANDA NCHINI

Written By CCMdijitali on Monday, August 5, 2024 | August 05, 2024

https://drive.google.com/uc?export=view&id=1F88I7AJjHyK3-OA-DkVTlSXNuA5WSsce

ZA UTAMBULISHO KUTOKA KWA MABALOZI WATEULE WA ZIMBABWE, ITALIA NA RWANDA NCHINI


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thatib Kombo (Mb.) amepokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Zimbabwe nchini, Mhe. Helen Bawange Ndingani, Balozi Mteule wa Italia nchini, Mhe. Giuseppe Sean Coppola na Balozi Mteule wa Rwanda nchini, Mhe. Jenerali Patrick Nyamvumba katika Ofisi Ndogo za Wizara jijini Dar es Salaaam tarehe 6 Agosti, 2024.

 

Akipokea nakala hizo Waziri Kombo amewapongeza mabalozi hao kwa uteuzi waliuopata na pia amewaahidi ushirikiano katika utekelezaji wa majukumu yao kwa kipindi watakachokuwa nchini kuziwakilisha nchi zao.

 

Aidha, ameeleza Mabalozi hao Wateule wanatarajiwa kuwasilisha Hati za Utambulisho kwa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 12 na 13 Agosti, 2024.

 

Akiongea na Balozi Mteule wa Zimbambwe nchini, Mhe. Ndingani, Waziri Kombo ameeleza kuwa Tanzania na Zimbabwe zimekuwa na ushirikiano wa kihistoria na kindugu ulioasisiwa na waasisi wa mataifa hayo mawili Hayati, Mwl. Julius Kambarage Nyerere wa Tanzania na Hayati, Robert Mugabe wa Zimbabwe. 

 

Vilevile, akamkaribisha Mhe. Ndingani kutembelea Maktaba ya Hayati Mwl. Nyerere iliyopo Butiama, mkoani Mara ambayo imesheheni historia yake. 

 

Balozi Kombo pia, akaeleza umuhimu wa kuwekeza na kurithisha historia ya ukombozi kwa vijana ili waweze kufahamu kwa kina namna waasisi hao walivyojitoa kupigania uhuru wa Bara la Afrika hususan harakati za ukombozi wa nchi za Kusini mwa Afrika.

 

Viongozi hao pia jadili juu ya umuhimu wa kufanyika kwa Mkutano wa Tume ya Pamoja ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Zimbabwe ambapo ameeleza kuwa Tanzania inatarajia kuwa mwenyeji wa mkutano huo. Tanzania na Zimbabwe zinashirikiana katika masuala ya biashara, uwekezaji, usafirishaji, usalama wa chakula, mabadiliko ya tabia nchi, elimu, Sanaa na utamaduni, na sekta nyingine za kisiasa.

 

Akizungumza na Balozi Mteule wa Italia nchini, Mhe. Coppola, Mhe. Waziri Kombo amesisitiza kuwa Tanzania ina nia ya dhati ya kuendeleza ushirikiano na nchi hiyo ili kuwezesha utekelezaji wa miradi ya kimkakati kupitia mpango wa ushirikiano wa Italia na Afrika unaofahamika kama “Mattei Plan”. Tanzania na Italia zinashirikiana katika sekta za utalii, elimu, Maji, biashara na uwekezaji, kilimo, mifugo na uvuvi, na kuongeza thamani ya mazao yatokanayo na ngozi ili kukuza biashara yake kimataifa.

 

Tanzania na Italia zinatarajia kuwa na Kongamano la biashara litakalofanyika jijini Dar es Salaam mwezi Desemba, 2024 kwa lengo la kukuza sekta ya biashara na za kiuchumi kwa maslahi mapana ya pande zote mbili amabapo, pembezoni mwa kongamano hilo kutafanyika mashauriano ya kisiasa.

 

Vilevile, katika mazungumzo yake na Balozi wa Rwanda, Mhe. Jenerali, Patrick Nyamvumba, Mhe. Waziri Kombo ameeleza kuwa Tanzania itaendelea kushirikiana na Rwanda kupitia ujirani wa nchi hizo mbili sambamba na kusimamia makubaliano mbalimbali yaliyokubaliwa katika nyakati tofauti na majukwaa mbalimbali ambayo nchi hizo mbili zimekubaliana kuyatekeleza.

 

Tanzania na Rwanda zinashirikiana katika sekta za mawasiliano, biashara na uwekezaji, usafirishaji, elimu, utamaduni na michezo, miundombinu, kilimo na mifugo.

 

Jukumu hili la kupokea Nakala za Hati za Utambulisho limefanywa na Mhe. Waziri Kombo kwa mara ya kwanza tangu aapishwe na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kushika nafasi ya Waziri wa Mambo ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.https://drive.google.com/uc?export=view&id=1GiJ0B2rnEfTdT_dS9memp0cYwDzAamTAhttps://drive.google.com/uc?export=view&id=1-cpVH2etTLJnjw54VXM1Oibga5d73nq2


Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Hemed S. Abdulla afungua kongamano la Vijana Pemba

Written By CCMdijitali on Saturday, August 3, 2024 | August 03, 2024

Published from Blogger Prime Android App


Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Ndugu. Hemed Suleiman Abdulla amesema kufanyika kwa makongamano ya kitaaluma ndani ya chama ni uimarishaji wa chama na kuunga mkono jitihada za viongozi wa Chama na Serikali katika kutekeleza majukumu yao ya kuwaletea maendeleo wananchi wake.

 Ameyasema hayo wakati Akifungua Kongamano la Vijana la kuonesha mafanikio, fursa na maendeleo ndani ya miaka mitatu ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na Rais Dkt Hussen Ali Mwinyi lililofanyika katika Ukumbi wa Umoja ni Nguvu Mkoani Pemba.

 Mhe. Hemed amesema Jeshi la CCM ni Vijana ambao wanahitaji kupewa taaluma na kuelimishwa juu ya kazi mbali mbali zinazofanywa na Chama na Serikali ili nao wakawe mabalozi wazuri wa kuyatangaza mazuri yanayofanywa na viongozi wa nchi.

 Mhe. Hemed ambae pia ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amewataka Viongozi wa chama na Serikali kuungana na kufanya kazi ya kukitumikia chama cha Mapinduzi kwa pamoja, kutangaza fursa kwa vijana zinazopatikana ndani ya Chama na Serikalini jambo ambalo litaendelea kuipa heshima CCM ya kuongoza Nchi awamu kwa awamu.

 Sambamba na hayo Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa amekemea tabia ya baadhi wa wanachama kuanza kutangaza nia ya kugombea nafasi mbali mbali wakijua muda muafaka wa kugombea haujafika hivyo amewataka wanachama kushirikiana na viongozi waliopo madarakani katika kutekeleza majukumu yao ya kuwatumikia wananchi .

 Aidha Mhe Hemed amemuagiza mwenyekiti wa UVCCM Taifa kuwachukulia hatua za nidhamu wale wote ambao wanaenda kinyume na Katiba na sheria za chama jambo ambalo linakiletea sifa mbaya chama cha mapinduzi na jumuiya zake, pamoja na kusisitiza kuwa Serikali iko tayari kutoa kila aina ya msaada ili kuhakikisha malengo ya vijana yanatimia hasa katika kukipigania chama cha Mapinduzi.

 Nae Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Ndugu Mohammed Ali Kawaida amesema kufanyika kwa kongamano hilo kutatoa fursa kwa vijana wa Mikoa miwili ya Pemba ya kuona  fursa zilizomo ndani ya Chama Cha Mapinduzi na kutambua namna ya kuzifikia fursa hizo kwa maslahi yao binafsi na taifa kwa ujumla.

 Kawaida amesema Serikali zote mbili zimetenga fedha nyingi kwa ajili ya kuwawezesha vijana hasa wa CCM ili kuhakikisha wanawekeza katika shuhuli mbali mbali za kimaendelo zitakazowakwamua  kiuchumi.

 Mapema  Mbunge wa Vijana Mkoa wa kusini Pemba Mhe. Munira Mohammed Mustafa ambae pia ndie muandaaji wa Kongamano hilo amesema lengo la kuandaa kongamano hilo ni kuwaweka pamoja vijana wa CCM wa mikoa miwili ya Pemba ili kupatiwa mafunzo yatakayowasaidi kuzitambua fursa na namna ya kuzitumia fursa hizo zinazotolewa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

 Mhe. Munira amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imetenga zaidi ya Bilioni 16 kwa ajili ya vijana kujiendeleza kiuchumi, pamoja na kujenga vyuo vya mafunzo ya amali katika wilaya  za Zanzibar ambavyo vinatoa fursa  kwa vijana kujiendeleza kiufundi na kupata ujuzi utakaowasaidi kupiga hatua kimaendeleo.

Published from Blogger Prime Android App

Published from Blogger Prime Android App

Published from Blogger Prime Android App

 

Imetolewa na kitengo cha Habari ( OMPR)
03.08.2024.

Picha Uzinduzi wa Treni mpya ya kisasa SGR 2024 Tanzania 

Written By CCMdijitali on Friday, August 2, 2024 | August 02, 2024


Published from Blogger Prime Android App
Published from Blogger Prime Android App
Published from Blogger Prime Android App
Published from Blogger Prime Android App
Published from Blogger Prime Android App
Published from Blogger Prime Android App
Published from Blogger Prime Android App
Published from Blogger Prime Android App
Published from Blogger Prime Android App
















Published from Blogger Prime Android App
 
Support : #BegaKwaBegaNaMamaSamia | JAK | CCM Arusha
Copyright © 2011. CCM Dijitali - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Jasper K
Proudly powered by Blogger
Link